Simulizi: Malkia wa kuzimu-01

Simulizi: Malkia wa kuzimu-01

RIWAYA : Usilie Rehema.... 01
MTUNZI : Lovi Pius Kijogoo
. 0757238304, ( whatsap )
0713 417 189
0622 738 310
Tanga.

_ SEHEMU YA KWANZA _
( 01 )

Issa akiwa ameikunja sura yake iliyogubikwa na hasira alimuita mkewe...

" Rehema"

" Abee Issa mume wangu!"

" Hivi wewe Rehema ni mwanamke wa aina gani? au una moyo wa chuma! pamoja na mateso yote haya nayokufanyia lakini bado unavumilia. kwanini hutaki kurudi kwenu! sasa nakwambia lazima nikurudishe kijijini kwenu Buseresere. Mwanamke mpuuzi sana" alifoka Isaa.

"Mimi nimekuchoka, umezeeka hufai kuwa na kijana kama mimi. Muone kwanza kifua chake kimesinyaa kama nyasi msimu wa kiangazi. Nakwambiaje usipoondoka kwangu nitakuuwa. Alafu tuone utanishitaki wapi masikini mkubwa wewe usiye na haya."

Rehema alikuwa kimya, asiamini kwamba maneno yale ya kejeli yanatoka kinywani kwa Issa ambaye ndiye mumewe. Uvumilivu ulimshinda akaamua amjibu mumewe...

"Issa mume wangu, kwanini unatoa maneno makali kiasi hicho! nami nina moyo wa nyama, maumivu nayasikia. Leo unasema nimezeeka! asante sana. Nani aliyenizeesha kama sio wewe? unaniona mimi kinyago, tahira nisiye na faida kwako. Kumbuka ni wapi uliponitoa! umesahau ni mambo mangapi nimekusaidia mpaka hapo ulipofika."

"Issa mume wangu, ukitaka salama ya Dunia chunga ulimi wako, hata kama umenichoka sio kwa manyanyaso haya. Tazama nina mtoto mdogo ndio kwanza ana miezi mitatu na ulimuita jina la mama yako ambalo ni Rabia. Lakini leo unanifukuza mimi pamoja na mwanao."

Rehema alimbeba mwanaye akamuweka kifuani kwake, huku machozi yakiwa yanamdondoka, hakuwa na lakufanya zaidi ya kusubiri aone mume wake atafanya nini.

Issa alivimba kwa hasira kama puto, hakutaka kabisa kumuona Rehema mbele ya macho yake. Akamsogelea karibu kisha akamshika mkono huku akimwambia...

"Wewe mwanamke, una matatizo ya masikio eeeeh! nimekwambia kwamba sitaki kukuona katika nyumba yangu. Niondolee mkosi shetani mkubwa wewe. Nimekufadhili vya kutosha, kwanini unaniganda kama kupe?. Narudia tena siwezi kukaa na takataka kama wewe, kama kukutumia nimekutumia sana ila kwa sasa umeisha muda wako, ondoka hapa uende ukatafute wazee wenzako"

Issa alipoona kwamba amezungumza maneno mengi yenye vitisho ndani yake, lakini Rehema alikuwa ametulia tuli. Kitendo hicho kiliuponda sana moyo wa Issa, akamzaba Rehema kibao kizito katika shavu lake. Hakuishia hapo alimzoa ngwala, Rehema akadondoka chini mzima mzima yeye pamoja na mwanaye.
Rehema aliumia sana kichwani damu zikaanza kumchuruzika, kwa bahati nzuri alimkumbatia mwanaye. Issa alimvuta na kumchukua yule mtoto kisha akamning'iniza juu huku akisema...

"Huyu mtoto naitoa roho yake leo, atakuwa sio mwanangu, mwanaharamu mkubwa huyu. Damu yangu haiwezi kutoa sura ya hivyi! hapa kwangu umechemsha nenda ukatafute Baba wa huyu Mtoto. Kuanzia leo mimi nimemkana mnataka kuniletea ushetani katika nyumba yangu? sitaki kusikia tena huyu mtoto akiitwa jina la mama yangu yaani Rabia, ikiwezekana huyu mtoto nitachukua panga nimkate vipande vipande kisha nimpikie mbwa wangu, washenzi wakubwa ninyi."

Issa alimuinua yule mtoto juu kabisa kisha akamuachia ili ajipige chini afariki papo hapo. Rehema alijitosa na kumdaka mwanaye huku akipiga kelele ..

"Jamani Issa unauwa mwanangu! niachie Rabia wangu, amekosa nini malaika wa Mungu huyu mpaka unamtupa chini! muogope Mungu wako, na kila siku unaswali wewe! Leo unaikana damu yako! unamkataa Rabia tazama mpaka mbingu na ardhi vinakushangaa. Sikuwahi kufanya mapenzi na mwanaume yeyote zaidi yako! ni wewe uliyeitoa bikra yangu nikiwa kidato cha nne mwanzoni, ni wewe pia uliyenilaghai niingie katika mahusiano na wewe, nilimaliza kidato cha nne huku nikipata daraja la tatu nilifaulu vizuri masomo ya sayansi nikaona mwanzo wa kutimiza ndoto zangu za kuwa Daktari zimeanza vizuri."

"Wewe Rehema nakuomba ufunge mdomo wako mchafu huo." alipaza sauti Issa.

"Hapana siwezi kunyamaza mume wangu, ni wewe uliyenitorosha nyumbani nikashindwa kuendelea na masomo yangu. Nilikusaidia vitu vingi sana, lakini leo unaniona mimi mpuuzi. Nilikutolea damu ulipougua, hakuna hata ndugu yako aliyekuja kukuona nikakuuguza mpaka ukapona. Unaniona sifai naiachia Dunia ikuhukumu. Ni mimi niliyekutafutia kazi katika kampuni hiyo ya kusafirisha mizigo nchi za nje, nimegeuka takataka kwako! Unaniita Malaya."

"Rehema nimekwambia ufunge huo mdomo nitakukata makofi Mshenzi mkubwa Wewe!"
"Wewe nipigie tu Issa!. Wazazi wangu walinitafuta kwa muda mrefu pasipo mafanikio na, siku walipofariki kwa ajari ya basi ulinizuia nisiende msibani, ama kweli uliamua kunitesa na kunitenganisha kabisa na ndugu zangu! saizi ni yatima mimi sijui nitaenda wapi na kijijini kabaki bibi mwenywe nasema ubarikiwe sana Issa."
Rehema alishindwa kupambana na hisia za moyo wake, hata kuzungumza hakuweza tena, akabaki analia. Lakini mumewe alikoswa hata chembe ya huruma, akaamua kumshika Rehema mkono na kuanza kumvuta mpaka nje ya geti kisha akamsukuma akadondoka chini Pamoja na mtoto wake,

_ ITAENDELEA _

OFA... OFA... OFA ....OFA

Usikose vitabu vyangu ( nakala laini ) unatumiwa kwa njia ya email au whatsap Navyo ni:- ________________====_________

Narudi Songea... 5,000/= tu!
Yolanda.....4,000/= tu!
Malkia wa kuzimu... 4,000/= tu!
Hadithi ya Suzi..... 2,500/=
Usilie Rehema.... 5,000/= tu!
________________====_________
PIA NAFUNDISHA MASOMO YA JIONI KWA WALE AMBAO WANARUDIA MITIHANI YA KIDATO CHA NNE. KIDATO CHA TANO NA SITA KWA MICHEPUO YA, HKL NA HGL.

KAMA UNAHITAJI KUANDIKIWA KITABU CHA HISTORIA YA MAISHA YAKO UNAKARIBISHWA...

NAPATIKANA TANGA MJINI,....
0622 738 310.
0713 417 189.
( 0757 238 304, whatsap )

MWL, LOVI PIUS KIJOGOO.
FB_IMG_1629011556998.jpg
 
NARUDI SONGEA

Safari ikiwa inaendelea Eva machozi yalikuwa yakimbubujika muda wote. Amani ya moyo wake ilizidi kutoweka. Alipoteza matumaini ya kuishi. Hakujua kwa nini dunia iliamua kumcharaza vile. Hakujua alimkosea wapi Mungu. Hakujua kabisa. Maumivu ya moyo wake yalipita ya msumari moto kwenye kidonda.

Kwa simanzi, alikiinamisha kichwa chake na kuanza kulia huku akiwaza. Alikumbuka jinsi alivyokuwa mrembo. Naam, mrembo wa kupigiwa mfano na kushinda tuzo zote duniani bila ushindani mkuu. Alikumbuka macho yake mazuri. Macho ya kikombe yaliyikaa lahiki kwenye vishimo vyake. Alikumbuka nywele zake za singa zilizokolea weusi wa kizimwili kabla ya yote kumfika. Alikumbuka mashavu yake yalivyotutumka kutokana na lishe. Alikumbuka alivyokuwa akila vinono. Masiko yake ya mpunga yalivyokuwa yamekita vyema kwenye kichwa na kumpa tambo la kupendeza.

Shingo yake ya upanga ilijikita na kukibeba kichwa chake kizuri hakuisahau. Hakusahau midomo yake ya miteko ambayo iliwapa wengi hanjamu. Alikumbuka mazima. Alikumbuka jinsi meno yake meupe mithili ya theluji yalivyokuwa yamejipanga kwa magigimo kinywani kama lulu katika chaza. Hakusahau kukumbuka kifua chake. Naam, kifua chake kilichobeba dodo zilizokuwa zimesimama kabla ya kulaliwa na janadume lile aliloliita mumewe. Alikumbuka tumbo lake la mlazo. Alikumbuka kiuno chake cha nyigu na miguu yake ya cherehani iliyoviringwa kwa ustadi na Mungu. Alhasili, alikumbuka jumla ya vitu vyote vilivyomfanya awe mrembo. Tofauti na sasa.

Alikuwa amenyauka kama mche uliokosa maji. Midomo yake ilikaukiana. Ikakonda. Mashavu yake yalikondeana. Kichwa kilikonda kutokana na njaa. Mabega yake yalimpanda. Akatisha kama shetani. Tumbo lake lilijitokeza, sio kwa kushiba chakula bali njaa. Mikono yake ya mbinu za Mungu, ilikondeana. Ikawa kama mikwiro ya kucharazia ngoma. Alhasili, jisimu lake liliumbuka. Akawa kama kimbaumbau mwiko wa pilau. Parafujo za mwili wake zikamlegea. Akawa zaidi ya utumbo wa samaki. Mtuo mmoja tu wa nzi, popote pale kwenye kiwiliwili chake, usingembakisha tisti. Ungembwaga kwa kishindo. Alitia huruma mtoto wa watu.
FB_IMG_1617644945820.jpg
 
Sauti hii naipaza kutoka katika pango la maumivu. Si tu maumivu, machozi yaliyokaukiana katika mashavu yangu. Ni ishara tosha dhidi ya kupata nisichostahili.
Ubinadamu wetu usitufanye tukalemaa. Usiwe chanzo cha kulimwaga chozi la mtu. Siku hiyo yaja, siku ngumu, siku ya majuto, tutalia na kuomba turudishwe Duniani tutubu.

Ukiamua kusimulia mabaya yangu, wakumbushe na lile jema moja nililotenda. Waweke bayana, Majuto si mjukuu tena, watu hawaoni yajayo. Piga goti, omba dua. Lipa wema kwa ubaya, Nitazidi kuandika hata wakinikata vidole, nitaandika kwa ishara.

Amka sasa, simama upya. Usiwe sehemu ya kuharibu furaha ya mtu. Fanya kile unachokiamini kwamba upo sahihi. Baba wa mbinguni anatupenda sana, alituma manabii wa kutosha kutufikishia ujumbe. Sisi tukaamua kumshabikia Tito yule nabii wa Gezaulole.

Samaki wanasema mkunje angali mbichi vile vile, wanasema upatilize udongo ungali maji. Walakini wanadamu wamekuwa si wanadamu tena. Hata hayawani hawawezi kumithilishwa nao. Wamekuwa kama vivuli vya mapepo na majini, kutujia na kututia unyamavu wa milele. Nafsi zetu zinaisha, matumaini nayo yanatapakaa kama maji ya mvua.

Natamani kuamba mengi, lakini mlisema wa kuambiwa ni gamba la kuamba hawakosi. Vichwa vimebimba. Wamejitia ukiburi wakakaza kama ngozi ya mamba. Tazama sasa jua limezama, lakini mwangaza ungali. Tazama jua linachomoza, lakini kiza kimekolea. Ni vipi hali itatengenea?
220px-Coq_Belle-Ile.jpg
 
NARUDI SONGEA.....01
Lovi pius kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )
0622 738 310.

SEHEMU YA KWANZA.
SURA
YA
1






BAADA YA MIAKA MITANO ( 5 ) KUPITA

JIJINI DAR - ES - SALAAM


Ilikuwa ni majira ya saa kumi na moja kamili. Alfajiri. kijibaridi kilikuwa kikipuliza. Wingu zito la mavunde lilitandama kote. Malumbano ya radi ilisikika. Mimweso mikali ilipita angani kwa kasi ya ajabu. Uso wa mandhari ulifinga. Ukungu nao ulianza kunyemelea halahala.

Kwa mbali alionekana Eva Mapunda! Alikuwa katika Kituo cha mabasi yaendayo mikoani pale ubongo Jijini Dar - es - salaam! Alikuwa amejifunika kipande kimoja cha kanga! Hivyo, kijibaridi kile cha asubuhi, kilichokuwa kimeshika usukani, kilipata upenyenye kwenye kiwiliwili chake. Naam, baridi ile ilipenya vyema na kumwingia mtoto wa watu. Hata hivyo, hakuwa na jinsi. Waliokuwa pale, walikuwa yabisi. Waliamini kila mja na msalaba wake. Hawakujali siha ya yule binti ambaye kwa mwonekano wake tu, aliashiria madhila kama sio makuruhu. Alijikonganya pamoja kama kuku aliyenyenyewa. Lengo likiwa kulitafuta joto ambalo halikuridhia kamwe kumbusu. Maskini Eva.

Macho yake yalivimba na kukolea wekundu wa damu. Ishara kuwa alikuwa akilia sana. Aidha, kutokana na baridi iliyomkumbatia, hakuwacha kutetemeka. Ala!
Michirizi ya machozi ilikaukiana kwenye mashavu yake, alishiba njaa na kudondokea kinywani. Alitia huruma.
Eva alikuwa ni binti mdogo ambaye alizeeshwa na makuruhu ya ulimwengu. Alikuwa kadiri wa kimo. Ngozi yake yenye weusi uliokoza, ilipauka kutokana na matatizo yaliyomsibu. Urembo wake aliokuwa nao angali bado hajaingia kwenye kinamasi cha matatizo, ulimtoroka. Japo alionekana mdogo, moyo wake uliyabeba mazito ambayo mtoto wa umri kama wake, asingeweza kamwe kuyasweka na kuyafichama moyoni. Yangelimuua kama sio kumbwaga. Makosa.

Mkononi, alibeba mkoba. Mkoba uliokuwa umesakini chote alichokiita chake. Rangi yake ilibambuka na kuashiria uchakavu. Ilishabihiana na madhila yaliyokuwa yamemfurika furifuri moyoni.

Moyo wake ulibeba siri nzito. Nzito mithili ya nanga. Siri ambayo kama kimelea, ilimfyonza isimbakishe. Siri iliyouchoma moyo wake kwa maumivu makali. Maumivu ambayo yalitangua mpangilio wa nafsi yake. Yakavifungua vikawa vya macho na hatimaye kupisha vua la machozi kunya.

Watu walipomuona walikisia labda kawa wazimu. Taswira hii ilijengwa na mwonekano wake. Afya yake iliyodhoofu, nywele zake zilizotumka ovyo na kujisokota kwa kukosa kudiriwa, mavazi chakavu yaliyoshiba viraka vya kila nui, miguu yake iliyojaa magombo na kuparara mithili ya nyong’inyo ya mganga, vilikuwa ishara tosha kwa wenye fikra hasi kukata kauli kwamba Eva karukwa. Usilolijua wanasema siku zote ni kama usiku wa kiza.

Maumivu aliyopitia Eva, yalituama katika moyo wake. Moyo wake ulikuwa kata ya kujua siri ya mtungi. Maumivu yale kama maji yalipojaa pomoni, yalifurika. Moyo nao ulichoka kuvumilia. Neva zilipitisha ujumbe akilini. Akili nayo ilirusha waraka kwenye milizamu ya macho. Kekevu na shake. Machozi njia nnenne hayakuwacha kumbubujika kivoloya. Alikinai furaha, akajazwa huzuni ya milele. Hayo ndiyo yalikuwa majaaliwa ya Eva binti mdogo aliyepigwa na maisha.
.
***

Alielekea kwenye ofisi ya mabasi yaendayo Songea. Aliushika upande wa kanga na kuyafuta machozi ambayo yalizuumu kabisa kumlemaza. Alitoa pesa aliyokuwa ameifunga upande mmoja wa kanga na kukata tiketi.

Saa kumi na mbili na robo, basi lilitekenywa. Nalo kutokana na hisia, lilikubali mtekenyo. Lilicheka huku likipumua moshi mweupe. Labda kuashiria linatunzwa au kumsuta Eva. Sijui. Kila abiria aliyekuwa akielekea Songea, hakupoteza wakati. Baada ya dakika tatu, gari lilishiba watu. Nao watu kutokana na itikadi za kidini, wakaamua kupiga dua maana barabara ile ya kuelekea Songea kutoka Dar, ilikuwa imewatafuna na kunyonya damu ya wengi kupitia ajali. Dua ilipoisha, barabara basi ilijikita kwenye barabara ya lami na kuanza masafa ya kuelekea ilikostahiki.

Kwasababu njia ya kutoka Dar - es - salaam kwenda Songea imekuwa na ajari nyingi sana!. Ambazo mpaka leo zimewacha simanzi tele kwa baadhi ya familia, ambazo ziliwapoteza wapendwa wao wa karibu, waliotangulia katika makao yao ya milele. Lakini kwa nyakati hizi barabara zimeboreshwa na kuwa bora zaidi.

Safari ikiwa inaendelea Eva machozi yalikuwa yakimbubujika muda wote. Amani ya moyo wake ilizidi kutoweka. Alipoteza matumaini ya kuishi. Hakujua kwa nini dunia iliamua kumcharaza vile. Hakujua alimkosea wapi Mungu. Hakujua kabisa. Maumivu ya moyo wake yalipita ya msumari moto kwenye kidonda. Kwa simanzi, alikiinamisha kichwa chake na kuanza kulia huku akiwaza. Alikumbuka jinsi alivyokuwa mrembo. Naam, mrembo wa kupigiwa mfano na kushinda tuzo zote duniani bila ushindani mkuu.

Alikumbuka macho yake mazuri. Macho ya kikombe yaliyikaa lahiki kwenye vishimo vyake. Alikumbuka nywele zake za singa zilizokolea weusi wa kizimwili kabla ya yote kumfika. Alikumbuka mashavu yake yalivyotutumka kutokana na lishe. Alikumbuka alivyokuwa akila vinono. Masiko yake ya mpunga yalivyokuwa yamekita vyema kwenye kichwa na kumpa tambo la kupendeza. Shingo yake ya upanga ilijikita na kukibeba kichwa chake kizuri hakuisahau.

Hakusahau midomo yake ya miteko ambayo iliwapa wengi hanjamu. Alikumbuka mazima. Alikumbuka jinsi meno yake meupe mithili ya theluji yalivyokuwa yamejipanga kwa magigimo kinywani kama lulu katika chaza. Hakusahau kukumbuka kifua chake. Naam, kifua chake kilichobeba dodo zilizokuwa zimesimama kabla ya kulaliwa na janadume lile aliloliita mumewe.

Alikumbuka tumbo lake la mlazo. Alikumbuka kiuno chake cha nyigu na miguu yake ya cherehani iliyoviringwa kwa ustadi na Mungu. Alhasili, alikumbuka jumla ya vitu vyote vilivyomfanya awe mrembo. Tofauti na sasa. Alikuwa amenyauka kama mche uliokosa maji. Midomo yake ilikaukiana. Ikakonda. Mashavu yake yalikondeana. Kichwa kilikonda kutokana na njaa. Mabega yake yalimpanda. Akatisha kama shetani.

Tumbo lake lilijitokeza, sio kwa kushiba chakula bali njaa. Mikono yake ya mbinu za Mungu, ilikondeana. Ikawa kama mikwiro ya kucharazia ngoma. Alhasili, jisimu lake liliumbuka. Akawa kama kimbaumbau mwiko wa pilau. Parafujo za mwili wake zikamlegea. Akawa zaidi ya utumbo wa samaki. Mtuo mmoja tu wa nzi, popote pale kwenye kiwiliwili chake, usingembakisha tisti. Ungembwaga kwa kishindo. Alitia huruma mtoto wa watu.

** ITAENDELEA***
FB_IMG_1617644945820.jpg
 
NARUDI SONGEA.....02
Lovi pius kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )
0622 738 310.

SEHEMU YA PILI.
SURA
YA
1


ILIPOISHIA....
Mashavu yake yalikondeana. Kichwa kilikonda kutokana na njaa. Mabega yake yalimpanda. Akatisha kama shetani. Tumbo lake lilijitokeza, sio kwa kushiba chakula bali njaa. Mikono yake ya mbinu za Mungu, ilikondeana. Ikawa kama mikwiro ya kucharazia ngoma. Alhasili, jisimu lake liliumbuka. Akawa kama kimbaumbau mwiko wa pilau. Parafujo za mwili wake zikamlegea. Akawa zaidi ya utumbo wa samaki. Mtuo mmoja tu wa nzi, popote pale kwenye kiwiliwili chake, usingembakisha tisti. Ungembwaga kwa kishindo. Alitia huruma mtoto wa watu.

ENDELEA NAYO....
Basi kwa magigimo lilizidi kumenyana na lami. Mara lipumue kwa shida, mara lipumue kama mwenye afya nzuri. Almradi lilitenda hayo kudhihirisha ubora wa injini yake. Watu nao walizidi kupiga soga hapa na pale. Sauti zao zilihanikiza. Wengine walisikika wakiimba nyimbo za kuongoaongoa. Wengine walitia vidude masikioni kusikiza Profes wa Fasihi nchini Kenya almaarufu Timothy Sumba na shemejiye Paskali. Wengine walifakamia njugu nyasa. Hawa walikuwa mabinti na vijana masmuma wa kiume. Wengine walionekana wenye mawazo. Mara kadha, walijishika tama. Walisirima mazima. Mara watunge macho kwenye dari la gari. Mara wasonye. Mara wabadili mkao. Walionyesha kutoridhika mtimani. Kilichokuwa kikiongea usoni mwao, kilikuwa bayana kilichokuwa ndani ya mioyo yao. Usumbufu.

Moja wapo wa hawa waliokiwa wakitabangwa nafsini, hakukosa Eva. Naam, binti ambaye aliamua kuchukua hatua nyingine ya maisha. Hatua ya kuondea jiji la Dar, ambalo alilina moto wa chuma kwenye kidonda. Dar, wakati wa kwanza, aliliona jiji imara na lenye kutaanisi. Aliamini kuwa, lingempokea kwa mlahaka na kumwonjesha tamu ya maisha. Kumbe alikosea. Hakujua uzuri wa jiji lile la Dar, ulikuwa kiinimacho cha ukatili wake wa ndani. Jiji ambalo aliamini lingempa kitulizo, ndilo jiji lililompa maumivu na makovu ya moyoni ambayo yaliungama na kujenga kasri la banguzi. Jiji lilimtema kama mfereji wa maji taka utemavyo maji ynyewe. Halikumwonea huruma. Lilimsaliti.

Alikinyanyua kichwa chake. Macho yake hayakuisha wekundu wa damu. Yaliiva kama nyanya mbivu. Baya zaidi, alisawijika. Miayo nayo haikumwwacha. Ilimkumbatia kila sekunde. Aliiona dunia kama panya. Naam, panya anayuma akivuvia. Hakuamania kabisa kupatana na yaliyomsibu.

Akiwa mchanga, alitamani kuwa mkubwa. Sasa ukubwa wenyewe aliuona maji mafu ambayo yalimmeza bila huruma. Aliamani kurudi utotoni mwake. Naam, awe mtoto wa mama yake. Acheze mwajificho. Achezee mvua. Achezee matope na alie atakapo. Haya yote yalikuwa laiti tu. Yalikuwa yamemfik kichwani. Alitamani hata bora yangemfika kooni. Angeweza kupapatika na kujinasua. Ila kwa wakati huo, laiti, haikumsaidia. Kila kitu kiliingia mchanga. Maji yalizidi unga na yalikuwa yamemwaika. Kuzoleka je? Muhali wanasema.

Siti jirani, alisakini mwanamke mwenye jirim la kifaru. Huyu alikuwa kala kashiba. Shibe ilimtapika. Ilimjenga kama sio kumkarafati. Alikuwa tipwatipwa. Alijaa sikupigi mafamba. Kichwani alivaa kofia aina ya tarbushi ya kike. Alivalia na miwani. Miwani ya jua. Kama ujuavyo usasa. Naam, wengi wamemezwa na usasa leo. Wanauita udijitali. Eti huo ndio unaomtambulisha mwanamke. Eti ndio urembo. Tuache hayo. Midomo yake ilikolea lipstiki nyekundu. Uso wake nao ulipigwa msasa wa vipodozi. Rangi yake isingejulikana kirahisi. Miaka nayo?

Miguuni alivalia viatu vya sports vyeupe. Alivalia na njuga ya rangi ya dhahabu kwenye mguu wake wa kuukeni. Kupanda, alivalia kaptura aina ya three quater iliyombana kisawasawa. Blauzi yake, haikumfika nyongani. Kitovu kilitapikwa nje. Mgongo je, sikwambia alivalia mgongo wazi.

Naam, mwanamke huyu ndiye aliyestaajabishwa na kadhia za Eva Mapunda. Kila mara, jicho halikutoka kwake. Alitamani sana kujua siri iliyokuwa ikimla. Aligeuka kata kujua siri ya mtungi. Je, atadokezwa siri yenyewe ambayo Eva alipania kutoinena hata kwa Mungu aliyemuumba?

Uvumilivu ulimshinda. Akamua kuchovya ndani ya buyu lenye shubiri. Akaanza.

"Vipi binti una shida gani mbona tangu tumeanza safari wewe unalia tu?"

Eva alimtazama yule mama. Chozi la simanzi likamdondoka. Akalifuta. Alitamni kuongea ila alishindwa. Alikifungua kinywa chake, lakini maneno yalikataa katakata kumtoka. Akatamauka.

“Kwanini huongei mwanangu. Kipi kinachokuumiza?” alisaili yule mama.

“Mama, hatimaye Eva alipata nguvu, “Sio kupenda kwangu kuwa hivi. Zaidi. Uhawinde. Uhawinde mama.”

“Uhawinde. Uhawinde umefanya nini mwanangu?”

“Mama, ni makubwa yaliyonikumba. Hili lililonikumba, limechangiwa na ufukara uliotupiga na kutukonganya pamoja kama kuku aliyenyeshewa. Umaskini umetuguguna. Ukasababisha wengine kutemwa kwa kuozwa mapema. Huko tulikokwenda tukifikiri tutapata kitulizo, kumbe ndiko jehanamu yenyewe. Niliyatamani maisha mazuri. Maisha yenye baraka tele ya kupendeza. Maisha mazuri ya kupigiwa mfano. Lakini yoye, yalikuwa mawazo ambayo takdiri haikuridhia. Nilipanga hivi, Mungu akapanga hivi. Akaamua niteseke, kwa kuonjeshwa shubiri ya ndoa yenye doa, alimeza mate Eva, kisha akaendelea,

“maumivu niliyo nayo mimi, ni makubwa ukilinganisha na ukubwa wa bahari. Maumivu yasiyokadirika. Uchungu wa maisha nimeuonja na kuumeza. Uchungu huu ndio sababu kuu ya kuondoka Dar, naelekea kwetu Songea maeneo ya Mkuzo. Narudi kwa mama. Naam, narudi kwa mama anipe angalau kitulizo kwa siku kadhaa, kabla maisha yangu sijayatupa baharini au kuyatia kitanzi, nife nizikwe hata nikienda jehanamu, sawa. Mabaya nimeyaonja. Hadhi gani niliyo nayo mie ya kufika peponi? Kama Mungu amenisusa hivi, je, huko ndiko ataridhia uwepo wangu?,"

Alitulia Eva. Akavuta kanga yake na kuyapangusa machozi yaliyokuwa yakimtoka. Akavuta kekevu kuu na kuendelea, “machozi niliyomwaga, yanaweza kujaza bahari. Aliyonitendea yule mwanamume, anayejua ni mimi tu. Ila, sidhani kama nitayamwaga wala kuyaavya kwa yeyote. Nataka nife nayo ili walimwengu waweze kunisahau kabisa na pasiweko yeyote ambaye atayafanya maisha yangu kuwa kama sinema. Sitaki kukumbukwa. Hata hivyo, naweza kumpasulia mama yangu mbarika. Nione kama ataridhia kunipa furaha!”
Alipojaribu kuendelea, kinywa chake kilitetemeka. Alishindwa kabisa kuendelea na zoezi la kusimulia kitendawili cha makuruhu yakiyompata. Sio kwamba alishindwa kutokana na msukumo, bali kutokana na shibe ya njaa iliyomzunguka. Tumbo lake lilianza kulumbana. Mlumbano ambao ulisababisha kiwiliwili chake kukosa nguvu. Kama kiwambo, kikaanza kucheza. Masikini Eva.

BONYEZA HIYO LINK TUKUTANE WHATSAP


**ITAENDELEA


FB_IMG_1617644945820.jpg
 
PILI....... 01
Na, Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )
Tanga.

SEHEMU YA KWANZA.

Barabara ya 16, Tanga mjini. Naam! maeneo ya kujidai ya binti aliyefahamika kwa jina la Pili, alipozaliwa tu, na kukulia katika mtaa huo. Alilelewa katika raha, neno taabu na shida kaja kulisikia ukubwani. Kwa yeyote aliyemsema na hata kumgusa kidogo tu, basi ugomvi huo ulikuwa ni wa familia nzima.

Mama Pili alimlea mwanaye kushinda hata yai, kwamba likianguka, limepasuka!. Wapo waliokunja sura, wengine wakadiriki kumshushia maneno ya dhihaka kwamba anamdekeza mwanaye, yote akayapokea na kuyaona hayana nafasi, katika maisha yake.

Dunia haigandi, kadili inavyojizungusha katika muhimili wake na hata kulizunguka jua. Ndivyo siku zinavyozidi kwenda kasi. Eeh!
Pili alifikisha miaka ishirini na moja, mamake kimoyomoyo akakiri, "Sasa nimekuza" sio Pili yule wa utotoni, aliyechezea matope na kujimwagia michanga ka mwendawazimu. Japo uzuri wake ulianza kujifunua angali akiwa shule ya msingi. Lakini pili huyo wa sasa akisimama na malaika utapata wakati mgumu kuwatofautisha, utakataa na ilo kama hujabahatika kumuona.

Pili alikuwa ni mrefu wa wastani, kichwa chake chembamba chenye umbo la mvirigo, kilichozibeba nywele ndefu na laini ka za kiarabu. Paji la uso pana kiasi ukishuka kwa chini unapokelewa na macho yaliyolegea ka yataka kudondoka, macho hayo yalichagizwa na nyusi nyeusi tii ka mkaa, kadiri jicho lilipokuwa likicheza basi kope ndefu zilizochanua ka mkia wa tausi zilikuwa zikipanda na kushuka kufuata mapigo ya mkonyezo wa macho.

Pua ilikuwa si kubwa si ndogo, si ndefu si fupi, ilikuwa ya wastani tu. Shingo yake nene ya kuvalia mkufu ilijawa na pingili ka nne wee!, muacheni Pili aitwe pili, huo muondoko wake sasa, unaweza ukadhani kasimama juu ya ardhi iliyopitiwa na tetemeko, maana sio kwa mtikisiko huo uliokuwa ukitimua vumbi huko nyuma kwa vijana wenye tamaa kama fisi.

Huyo ndo alikuwa Pili binti Ramadhani, mitaa ilimtambua hivyo, na ikakubali hadharani tena kwa mikono miwili kwamba binti aliumbwa nae akaumbika.

"Jamani sio kwamba najisifia, huo ndio ulikuwa muonekano wangu, kabla jinamizi la ulimwengu alijanivaa" alizungumza Pili, machozi yakiwa yanameremeta machoni pake.

"Mbona unalia?" nilimuuliza.
"Hapana kaka, najitahidi kulizuia chozi, lakini napata wakati mgumu, kufanikisha ilo."

"Kwani kuna kipi kinachoumiza moyo wako, eeh!, binti mrembo ka wewe?" nilimuuliza swali huku nikimtazama kwa jicho la kiudadisi zaidi.

"Sijawahi kusimulia mkasa wa maisha yangu mpaka mwisho, popote pale. Naishia njiani na kuyaachia machozi yachukue nafasi yake.

"Pole sana dada Pili!" nilitamka neno ilo pasi kujua ni kipi kilichompata. Nilitaka ajue nami nimeguswa na maneno hayo aliyotamka hapo awali. Alichukua kitambaa chake cha mkononi akayafuta machozi yake, akaibana miguu yake vyema, huku akirekebisha juba lake, akanitazama usoni kisha akazungumza.

"Kaka Lovi, kabla sijafikwa na mfiko huo, nilikuwa mfatiliaji mzuri sana wa simulizi zako. Na nilipoona umeandika ujumbe kwamba upo Tanga, nikajihapiza ni lazima nikuone. Nikusimulie mkasa huu huenda ukapata cha kuandika"

"Ni kweli kabisa Da Pili" nilidakia kwa haraka, kitendo hicho kikafanya pili atabasamu kwa mara ya kwanza. Mungu wangu! na hapo ndipo nilipofanikiwa kuyaona meno meupe kama theluji, yalijipanga vyema kama batani za kinanda.

"Basi kaka yangu, nikiwa nakaribia kufikisha miaka ishirini na mbili, ulisalia mwezi mmoja tu. Hapo nikaanza kuhisi mabadiliko katika mwili wangu. Nilimchukia kila mtu, nikawa najitenga muda wote. Wazazi wangu walifedheheka sana. Mama akaniita na kunisihi nimwambie kinachonisibu, alihisi labda ni mahusiano yananitatiza. Mama alilia sana! kuona kashindwa kuupata ukweli aliotegemea"

Pili alivyomaliza kutamka kauli hiyo ya mwisho, nae aliangua kilio kizito. Nikajiuliza kimoyomoyo, "Huyu binti kaamua kunionesha kwa vitendo kilio alichoangua mamake siku hiyo"

"Pumbavu" nilijitukana mwenyewe, kwa kuona nawaza ujinga, wakati moyo wa pili ukiteketea kwa maumivu.

*********** ITAENDELEA*********
received_1028400684310942.jpg
 
PILI....... 02
Na, Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )
Tanga.

SEHEMU YA PILI.

Sehemu ya kwanza iliishia hapa......
"Basi kaka yangu, nikiwa nakaribia kufikisha miaka ishirini na mbili, ulisalia mwezi mmoja tu. Hapo nikaanza kuhisi mabadiliko katika mwili wangu. Nilimchukia kila mtu, nikawa najitenga muda wote. Wazazi wangu walifedheheka sana. Mama akaniita na kunisihi nimwambie kinachonisibu, alihisi labda ni mahusiano yananitatiza. Mama yangu alilia sana! kuona kashindwa kuupata ukweli aliotegemea"

Pili alivyomaliza kutamka kauli hiyo ya mwisho, nae aliangua kilio kizito. Nikajiuliza kimoyomoyo, "Huyu binti kaamua kunionesha kwa vitendo kilio alichoangua mamake siku hiyo"

"Pumbavu" nilijitukana mwenyewe, kwa kuona nawaza ujinga, wakati moyo wa pili ukiteketea kwa maumivu.

ENDELEA NAYO...........

"Pole sana dada! kila jambo lina makusudio yake" nilitamka kauli hiyo, nikiwa nayatazama macho yake yalivowiva na kuwa mekundu ka nyanya mbivu. "Nashukuru kaka!" alijibu pili kwa sauti hafifu ilifunikwa na blanketi la huzuni.

"Kichwa kilianza kunigonga, isivyo kawaida. Vyakula vya nyumbani nikaviona kama taka kuvipitisha kinywani mwangu. Nikawa naongea na kucheka peke yangu, hata nikiwa natembea barabarani."

"Makubwa! watu walikufikiliaje?" nilimkatisha huku nikimtwanga swali.
"Nilikuwa siwafatilizi, ila nilikuwa nikisikia sauti zao kwa mbali, wakisema nimezidisha maringo, sababu tu ya uzuri wangu" alijibu Pili, huku akiponyokwa na tabasamu lililopoa kabisa.
"Mmh! usilolijua ni sawa na usiku wa giza" aliguna kidogo pili, kisha akamalizia kwa maneno hayo.

"Hali ilizidi kuwa mbaya, kuoga nikagoma, nikaanza kuokota makopo na kubeba vitambaa chakavu kichwani pangu. Sikuogopa mtu! nikawa napita karibia barabara zote za namba. Na kwenda kupumzikia pale 12 stendi ya zamani"

"Watu walinishangaa, pasi kupata majibu. Mama akawa anatuma vijana wananishika, na kunifunga kamba, nikaogeshwa na kupelekwa hospitali ya Bombo. Kwa Daktari bingwa wa magonjwa ya akili.Walidhani ni malaria, wakanipima kila kipimo hawakuona kitu, na sikuwa hata na tatizo la akili. Mama alizidi kuchanganyikiwa, presha ikawa inapanda na kushuka."

"Aisee! ulifikia hatua hiyo?" nilimkatisha kidogo, kwa kumuuliza swali baada ya kuona, si muda ataachia masika ya machozi machoni pake.

"Nafuu hapo, wee acha tu!" alijibu pili huku akiinamisha kichwa chake chini.
"Ikawaje tena baada ya hapo?" awamu hii nilimuuliza kwa utulivu, nami sura yangu nikiwa nimeiweka katika umbo la huzuni. Nikiwa bado nasubiri jibu kutoka kwa Pili, nikasikia simu yangu ikiita kuangalia nakuta ni kaka yangu, aliyenipokea Tanga ndo anapiga, nikapokea.

"Hallo! naam kaka, habari za wakati huu?
"Nzuri, wee Lovi uko wapi? na unajua hapa Tanga wewe ni mgeni bado!" swali ilo lilinifanya niyakodoe macho kwa mshangao, kama chizi aliyechomewa makopo yake. sikujua pale tulipokaa na Pili ni wapi, hivyo nikasogeza simu mbali kidogo kisha nikauliza kwa sauti ya chini kaka asiweze kusikia,

"Samahani pili, hapa tulipokaa ni wapi?"
"Forodhoni!" pili nae alijibu kwa sauti ile ile ya kunong'ona kama jinsi nilivyouliza.
"Mmh! yes, nimekaa forodhani hapa kaka!"
"Whaaaat!"
"Nasema nimekaa forodhani hapa nikipunga kiupepo cha bahari, siunajua kwetu musoma hakuna bahari" nilimjibu kaka nakuchombeza utani kidogo, kumbe kaka alikasirika.

"Ondoka hapo tafuta eneo lingine la kukaa, ukishindwa chukua pikipiki rudi nyumbani" alifoka kaka, kisha akakata simu. Nilitulia kama sekunde kumi na tano, nikamtazama Pili kwa jicho la kuibia nikihisi labda ananifatilia mazungumzo yangu. Laa asha! masikini ya Mungu, yeye alikuwa amejiinamia chini machozi yakimdondoka huku akipambana kuzizuia kamasi, zilizokuwa zikilazimisha kuchuruzika.

"Pili!" nilimuita.

"Naam kaka mtunzi wa hadithi, nipo" aliitika huku akikurupuka kama mtu aliyestushwa na ndoto mbaya katikakati ya usingizi mzito. Hapa nilicheka kidogo.

"Hahahahahaha!! naona sasa umeweka kibwagizo kwamba, kaka mtunzi wa hadithi, hahahahah..!! unavituko wewe" kauli hiyo ikamfanya pili atabasamu kidogo tu.
"Ok! sorry eti hapa forodhani kuna nini! baada ya kumwambia kaka nipo hapa, naona kachukia kasema niondoke nitafute mahali pengine nitulie"

"Mmh! " aliguna Pili.

"Mbona waguna nieleze!" nilizidi kusisitiza.
"Kaka tuachane na hayo, siku ukipata muda pita hapa usiku, ndipo utajua kwanini kaka amechukia" alizungumza pili kisha akaking'ata kidomo chake cha chini kilichokaukiana kwa maumivu.

"Sawa nitafanya hivyo!" nilitoa jibu ili kuokoa muda. Kisha nikamtazama pili usoni na kumwambia, "baada ya kuanza kuokota makopo na kutembea na furushi la vitambaa chakavu kama muuza mtumba ikawaje?"

Ilo neno nililomalizia kwamba kama muuza mitumba, likamfanya pili agune na kutikisa kichwa. Haraka haraka nikagundua hajapendezwa nalo. Nikatulia tuli nikisubiri nisikie atazungumza nini.

Katika simu yangu nilikuwa nikiandika, matukio muhimu yalipompata pili, pasi yeye kugundua ilo. Nilitumia ustadi wa hali ya juu.

****** ITAENDELEA*******
 
NARUDI SONGEA.....03
Lovi pius kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )
0713 417 189.

SEHEMU YA TATU.
SURA
YA
1


ILIPOISHIA....
Alipojaribu kuendelea, kinywa chake kilitetemeka. Alishindwa kabisa kuendelea na zoezi la kusimulia kitendawili cha makuruhu yakiyompata. Sio kwamba alishindwa kutokana na msukumo, bali kutokana na shibe ya njaa iliyomzunguka. Tumbo lake lilianza kulumbana. Mlumbano ambao ulisababisha kiwiliwili chake kukosa nguvu. Kama kiwambo, kikaanza kucheza. Masikini Eva.

ENDELEA NAYO.....

Abiria yeyote yule anaejisikia vibaya kuna rambo laini hapa, tunawapenda sana na kuwathamini wateja wetu!. Kuweni huru kusema chochote mnachohitaji asanteni sana tuendelee kumuomba Mwenyezi Mungu ili tufike salama Songea.”

Makanga wa basi alinena. Eva hakusita. Aliomba rambo. Maskini mtoto wa watu alikuwa akihisi kichefuchefu. Alipopokea kile kijirambo, alianza kutapika. Ajabu ni kuwa, alitapika maji tu. Kisa na maana? Tumbo lake halikupata chakula kwa siku tatu mfululizo.

“Ewe Dunia nitese tu!
Ewe Dunia niangamize tu!
Ewe Dunia nisulubu tu!
Ewe Dunia ninyanyase utakavyo niko tayari kukuaga nikapumzike!
Kwanini umeruhusu maumivu haya yadumu nami?,
Nionee huruma nami natamani kutabasamu, Sio kwa manyanyaso haya, nimevumilia sana pasipo kuona tumaini la safari mpya iliyojawa na furaha isiyo na kifani."
Alinong'ona kimoyomoyo baada ya kutapika.

Ukimya ulishika usukani baada ya Eva kuemewa kuzungumza. Njaa aliyokuwa nayo, ilimlemaza asiweze hata kukonyeza. Hata machozi yalimkauka kutokana na ile njaa. Mama mtu, alimtazama Eva.

Akamwonea imani. Naye kwa sababu ya uchungu alioupata kwenye maneno ya Eva, alishindwa kabisa kulizuia chozi. Lilimtoka. Alitwaa hachifu yake. Akajipanguza kisha akautwaa mfuko wake. Alitoa soda chupa moja na keki tatu. Alimkabidhi Eva ambaye aliviparamia na kuanza kuvishambulia kama shumdwaa aliyenyimwa chakula wiki tatu. Kwa bahati mbaya, tumbo ilivikataa vyakula vile. Navyo kwa ghadhabu, vikamtokea na puani.

Njaa ni mbaya. Njaa inaua ndugu yangu. Juzi tu jamaa yangu Kafiri Rafiki, katiwa ndani kwa tuhuma kuwa kaiba kuku wa jirani. Kortini alijitetea kwa kusema njaa ilimsukuma kufanya vile. Hata hivyo, hakuskizwa. Sauti yake ilikuwa changa. Huyo… gerezani miaka kumi. Nakumbuka pia rafiki yangu wa kitambo. Huyu aliitwa Mkono Wazi.

Mkono wazi alifia kazini. Kazi ya mjengo. Alikuwa kwenye sekta ya kubeba mawe kupandisha ghorofani. Alipatikana kalala sakafuni, huku mawe aliyokuwa kayabeba, yakiwa kando yake. Uchunguzi ulifanyika. Habari kuhusu kifo chake zilitufikia. Eti alikufa kutokana na njaa. Ndugu yangu mwengine kwa jina la Maozi Kazungu. Huyu aliachwa na mke wake kwa madai kuwa, hakuweza kazi ya kukwea mnazi kutokana na njaa. Njaa ni hatari sana. Njaa si ya kuchezewa. Tuyaache hayo.

Hata na chakula, kilimsusia Eva. Hakikumpemda. Kutokana na kukosa chakula kwa muda mwingi, vidonda vya tumbo vilianza kumnyemelea. Nyemelea hiyo ilipata upenyenye. Naam, upenyenye kwenye utumbo wake. Mwisho wa yote, ikulu ikajengeka kwenye chango zake. Vidonda vya tumbo vikawa vimepata hifadhi rasmi ya kustakiri. Ah, maisha haya.

Mama mtu alishindwa kabisa kuelewa kilichomfika binti Eva. Mawazo yake hayakuwacha kumtekenya na kumchokonoa. Alitamani sana kujua kilichomfika Eva ila hakuwa na mwao. Eva naye alizungumza ila hakuwacha wazi mafumbo yaliyompata. Kila kitu kilikuwa fumbo kwa yule mwana mama.

Alivyoongea Eva, kweli iliashiria makuu. Lakini kilichosababisha maumivu haya yote, mbali na umaskini, hakutaka kusema kabisa. Ala!
"Hivi kikubwa kipi alichofanya binti huyu jamani! Mbona mateso anayopitia ni makali! kwanini lakini? Kama kulia amelia sana tazama sasa anavyoungukia, huku akilalamika kwamba maumivu yalioko ndani ya moyo wake ni sawa na moto mkali unaoyeyusha chuma. Eti anahisi kana moyo wake unateketea. Natamani sana nimsaidie binti huyu ila bado hajawa tayari kuniambia kilichomsibu katika maisha yake. Inaonekana anatembea na salau pana sana ya maisha yake, ambayo akiamua kuiweka bayana lazima ulimwengu mzima udondoshe chozi la huzuni." Aliwaza kimyakimya yule mama.

"Mbona maumivu yameamua kudumu nami? Ni kipi hicho kikubwa nilichokosea hapa Duniani?, Enyi Malaika wa mbinguni nielezeni, kama kuna baya nililotenda niweze kuomba msamaha!."

"Hata kama nimekosea, kwa mateso haya niliyokutana nayo kwa mume wangu ni adhabu tosha. Ni lini tena Eva mimi nitatabasamu kama zamani! Ni heri walioko kaburini kwani wametulia! Heri hata ndege wa angani wanao uhuru wao. Heri hata vipepeo. Waliolala kaburini, ni zaidi yangu. Hata walio jehanamu, ni zaidi yangu. wameondokana na shida za ulimwengu!." "Fimbo ya mnyonge hulipwa na Mungu"

"Kama ni kusali nimesali sana jamani!, Nimelia usiku na mchana, uko wapi mtetezi wangu uje uniokoe na kunifuta haya machozi? kwanini Mwenyezi Mungu hasikilizi maombi yangu? Au kaamua kuniwacha peke yangu dunia iniadhibu kadri itakavyo? Nimefika kikomo cha uvumilivu naelekea kukata tamaa ya tumaini zima la kuokolewa!."

"Nasubiri kufukiwa chini ya ardhi. Nadhani huko ndiko nitapumzika, japo wadudu wenye hila kama mchwa nao watashangilia kwa kuushambulia mwili wangu uliopoteza tumaini tangia nikiwa hai."
"Nazungumza maneno haya nikiwa na bubujikwa na machozi yasiokoma. Natamani nifike nyumbani mapema, nimueleze Mama yaliyonikuta nikiwa huko Dar."
"Siamini kama mpaka muda huu niko hai! Na kama nitafika salama Songea ni Mungu pekee ndiye anajua."


********* ITAENDELEA********
 
PILI....... 03
Na, Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )


SEHEMU YA TATU.

Sehemu ya pili iliishia hapa......
Katika simu yangu nilikuwa nikiandika, matukio muhimu yalipompata pili, pasi yeye kugundua ilo. Nilitumia ustadi wa hali ya juu.
ENDELEA NAYO.......
Eeeh! nakusikiliza pili, maana muda nao sio rafiki!" nilijiongelesha hivyo kwa lengo la pili aendelee kusimulia, naam! mtego wangu ulifanikiwa kumnasa, nikaona anatazama huku na kule kama kuna watu wanasikiliza, kisha akendelea,
"Kaka nilizidi kupagawa sikutaka tena chakula cha nyumbani, mashimo ya taka ya baarabara ya saba ( 7 ) kwa wasomali na waarabu ndipo pakawa mahali pa mimi kushibisha tumbo langu, aisee..!! acha, acha nilie tu, yaaani! yaani mimi ni wakula kwenye mataka, Dah! Eeh Dunia, kwanini hukutaka kusimama upande wangu.
Mapaka hapo pili alishindwa kuzungumza, akaangua kilio ambacho siwezi kukielezea hapa, ukapata kunielewa, ningelipata kikombe na kuyakinga yale machozi aliyoyabubujisha hakika kingelijaa. Bahati nzuri tulipokuwa tumeketi tulifichwa na mti mkubwa, wale wa upande wa pili, ilikuwa ni vigumu kutambua kinachoendelea.
Jukumu la kumtuliza tena pili, awamu hii likanihusu. Nikamsihi kwa sauti ya upole, kwamba matatizo tumeumbiwa binadamu na si ndege wala wanyama. Takribani dakika tatu ziliteketea kwa kufanikisha jambo ilo. Pili alitulia lakini sauti za jazba na uchungu zilitoka kinywani mwake, akajitahidi kuizibiti kasi ya kamasi, zilizokuwa zikichungulia katika tundu mbili za pua.
"Nilianza kuvua mpaka nguo kaka, ukichaa ulikolea, nikawa natembea nimejifunga kipande kimoja tu cha kanga, aisee. Vibaka wa usiku, walinzi, watoto wamitihani wasio na makazi walinisulubu sana kaka, ukizingatia na ili umbo langu lilivyokubwa niliteseka sana mimi."
"Usilie pili, please! stop!" nilimtuliza pili, huku akili yangu ikiwa imeenda mbali sana. Nikamtaza pili alivyo na shepu pana iliyotuna kwa nyuma, vijana wa sasa wanaitwa msambwanda. Ilikuwaje sasa akiwa kwenye hiyo kanga moko ka wasemavyo wacheza baikoko. Mimi mwenyewe ka mwanaume kamili mwili wote ulisisimu nikajawa na matamanio ila nikajikaza.
"Kwa hiyo usiku ulikuwa ukilala wapi?" nilimuuliza swali la kizushi, ili asigundue ujinga uliokatiza kichwani mwangu kuhusu hiyo kanga moja.
"Nililala kwenye maduka nje, na kuna siku mama alikuwa akifanikiwa kunikamata na kunipeleka nyumbani. Sitaisahau siku hiyo nilikuwa nimeokota kisu, mama aliponishika nilipeleka kile kisu kumchoma ila alikwepa kingempata kifuani ningemuuwa kabisa. Aaah! kaka! kaka! kichwa kinaniuma, hivyi kweli mimi ni wakutaka kumuuwa mamangu, aliyebeba mimba miezi tisa, akanizaa kwa uchungu kwa hospitali ya ngamiani. Naumia pili mimi, ni bora ningelikufa mapema kuliko kuishi maisha haya yenye kumbukumbu chafu isiyofaa kusimuliwa kwa vizazi vijavyo. Jambo nilikuwa nimechanganyikiwa, matukio mengine nayakumbuka."
"Hapana dada pili, hukuwa wewe kichwani. Usiumie sana, pole, majonzi, shida, na misukosuko yote ndio ukamilisha maisha yetu ya kila siku." nilimsihi kwa maneno hayo ya faraja.
"Miguu yangu ilipasuka, vidonda vikaipamba mikono yangu, sababu ya kutembea peku. Kaka niliyaishi maisha haya ya ukichaa yaliyotawaliwa na machungu, machozi, na mateso takribani miaka mitano." alieleza pili akiwa anaangalia muda katika simu yake.
"Niliposimuliwa kwamba, kipindi mimi ukichaa unakolea, ndipo Baba yangu akawa anazidi kununua majumba ya kifahari. Nasikia watu walishangaa, wakiulizana shughuli ya baharini kuvua ndio imempa pesa ya kununua majumba hayo!. Kaka nilikuwa na hasira na Baba, niliona msamaha wangu ni kuondoa uhai wake tu, ila nikaona nitakuwa nimejichimbia kaburi langu mwenyewe. Mzee Ramadhanj ni kama alikubali bintiye nizidi kuteseka na kulala katika mashimo ya taka alikuwa akibadili magari kila kukicha."
"Nasikia ndugu zangu wakakaa kikao, wakakubaliana wanipeleke kwenye kisomo. Baba aligoma akawa mkali ka mbogo. Akamshikia mpaka panga Dadake, ambaye ni shangazi yangu mie. Wakaamua wawape vijana pesa kimyakimya, wakanitafuta na kunikuta barabara ya 12 nikiwa nimepumzika chini ya mti na mizigo yangu. Wanavyosema wao walinikwapua mithili ya mwewe akwapuapo kifaranga cha kuku. Wakaniweka nyuma ya gari na kunifunga kamba kama ng'ombe."
"Ndio maana nakwambia kaka, mimi sifahi tena kuendelea kuwa hai, Dunia itanitazama vipi!, achilia mbali Dunia, hata hapa tanga hizo barabara za namba zenyewe zina waja wanamidomo michafu, pamoja na kuvaa nikabu bado wananitambua ni mimi, sababu ya miondoko yangu."
"Ooooh! basi nyamaza pili, jikaze usilie mamiii, muda umekwenda. Vumilia yatakwisha, yote yatabaki ka historia ambayo haitasimuliwa katu." nilijaribu kumtuliza baada ya kuona kashikwa na kigugumizi maneno yakawa hayatoki, isipokuwa machozi njia nnenne, yaliyombubujika na kutapakaa katika mashavu yake.
"Kwa hiyo pili, baada ya kupelekwa kwenye kisomo ikawaje?"
"Nilipelekwa kwa Ustadhi Juma kule pangani, baada ya dua takribani dakika arobaini. Mwili wangu ulianza kusisimka, nikahisi kitu kama moshi mchafu ukitoka kupitia vinyweleo vyangu. Mwili ukawa mwepesi. Nikabaki nimeduwaa, ni kama mtu aliyefariki miaka mingi iliyopita kisha afufuke ni lazima ataushangaa ulimwengu ulivyobadirika. Ndivyo ilivyokuwa kwangu. Nikaanza kuona aibu sikuweza hata kuwatazama ndugu zangu usoni."
"Hukuhisi mabadiliko katika mwili wako?" nilimkatisha pili kwa kumtwanga swali. Akanyamza kidogo, akachukia maji yake akabugia mafunda mawili ya nguvu kulainisha koo lake, lililokaukiana sababu ya kulia sana. Akatazama pembeni huku akizungumza,
"Kaka Lovi, we acha tu, kama huu mwili ungeweza kuzungumza, basi ungeeleza mengi uliyotendewa. Kiukweli mimi nashindwa kuyaweka bayana ulivyonyanyaswa mwili kipindi nikiwa nashinda vichochoroni, huku dampo la usagara ndipo pakiwa supamaketi kwangu pakupata mahitaji kama nguo chafu za kujifunga, na hata chakula."
"Ni miaka mitano, lakini uliteseka sana Dada yangu!" nilizungumza kauli hiyo kwa lengo la kumpa sekunde kadhaa pili apumzike. Nilifanikiwa ilo, akaendelea zungumza,"
"Nilimshukuru Ustadhi Juma kwa kunisaidia. Ndugu wakampa chochote kitu kama shukrani. Walinikumbatia sana, wakasema nimezaliwa upya. Wakanieleza kidogo nilivyokuwa awali, nilimwaga mvua ya machozi mbele yao."
"Kwani mama mmemuacha wapi?" niliwauliza swali hili ndugu zangu. Baada ya kuangaza huku na kule bila mafanikio. Mwanzo nikajua labda katoka kidogo atarejea, haikuwa hivyo kama nilivyodhani."
"Swali hilo liliwashtua, hawakutegemea kama ningewauliza." "mmh! eeh! ma.. maa" ma mkubwa alishikwa na kigugumizi ghafla akiwa ananijibu, akatulia kama sekunde tatu, kisha akaendelea kuzungumza, "Siunajua tena mamako anapresha tungekuja nae huku labda yangekuwa mengine"
"Jamani mamangu, yaani presha inamtesa sana!" nilimjibu ma mkubwa, huku huzuni ikikatiza kwa kasi ndani ya moyo wangu. Ikapelekea nipigwe na kiubaridi mwili mzima.
 
PILI....... 04
Na, Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )


SEHEMU YA NNE

Sehemu ya tatu iliishia hapa......
"Jamani mamangu, yaani presha inamtesa sana!" nilimjibu ma mkubwa, huku huzuni ikikatiza kwa kasi ndani ya moyo wangu. Ikapelekea nipigwe na kiubaridi mwili mzima.

ENDELEA NAYO.......
"Baada ya hapo ndio mlikwenda nyumbani?" nilimuhoji pili, kutaka kujua kilichoendelea kwa haraka.

"Ndio, ila tulipofika tu nikawa na shauku kubwa ya kumuona mama. Kisha nimuone Baba anieleze kilitokea nini! Niweze kuzishuhudia hizo nyumba alizozinunua. Fikra hizo zikiwa zinapita kwa kasi kichwani kwangu, ndipo nikakumbuka niliambiwa kwamba, nilipojitambua tu nyumba hizo zilikuwa zikiwaka moto moja baada ya nyingine. Kumbukumbu hiyo iliniumiza saana kaka lovi"

"Usilie jikaze pili, yote yana mwisho, hakuna binadamu aliyeumbiwa matatizo mpaka kufa kwake. Mungu wetu ni mwenye huruma sana, kwa sisi waja wake." Nilimsihi sana pili pale nilipoona nguvu ya kuyazuia machozi hanayo tena.
"Vipo vya kujikaza mtu usilie lakini, sio kwa mambo haya nayopitia!" alidakia pili huku matone ya machozi kutoka machoni pake yakiisindikiza kauli hiyo, ya kukata tamaa.

"Mama ulimuona?" nilimtwanga swali pili.
"Nilipoingia chumbani kwake, nilistuka ghafla kaka, nilimsahau mama, mwili ulidhoofu, ngozi ikakunjamana. Sio yule niliyemuacha nililia mbele ya kitanda chake nisijue ni nini cha kuzungumza kwa wakati huo."

"Umepatwa na nini mama?" nilimuuliza huku midomo ikiwa inanicheza kwa uchungu, mama hakunijibu kitu, alinitazama tu huku machozi nae yakimdondoka, kaka nililia sana" Awamu hii nilishindwa kumzuia pili asiangue kilio, mpaka watu waliokuwa kwa mbali kidogo wakasikia, walipuuza wakijua ni mtu na mpenzi wake.

Kichwa cha pili nikakiweka katika kifua changu na kuanza kumbembelea kama mtoto. Machozi yaliilowesha tisheti yangu ikaweka alama ya ramani isiyoeleweka. "Urembo alionao huyu Dada na maisha anayoyapitia mbona haviendani, au kuna malaika huko mbinguni kazi yao ni kutesa warembo tu" nilijisemea kimoyomoyo huku nikimshuhudia pili akizivuta kamasi zake kwa mkupuo.

"Jikaze Dada angu!"

"Najitahidi lakini nami na moyo wa nyama!"

"Natambua ilo, piga moyo konde, usonge mbele."

"Sijioni kama ni binadamu ninaestahili kusonga mbele na maisha mapya."

"No! usiseme hivyo pili!, huwezijua Mungu anakusudi lipi katika maisha yako. Hata dhahabu lazima ipitishwe kwenye moto kwanza."

"Hapana kaka Lovi, imetosha. Duniani nimeteseka hivi je huko nitapoelekea baada ya maisha ya hapa Duniani, nitapokelewa katika hali gani! acha tu kaka, liwalo na liwe"

Baada ya kuona bado pili akubaliani na ushauri wangu, nikamkatisha kwa kumuuliza swali ili niendelee kunukuu mapito ya maisha yake, na muda ulizidi kukimbia kasi ka kibaka aliyekwapua mkoba kituo cha mabasi.

"Kwa hiyo pili mamako alifungua kinywa na kuzungumza nawe au?"
"Nilipomuuliza kwa mara ya pili, kwa shida saana mama alifungua kinywa chake kikiwa kimejaa mate nikampa kopo akatema, nikampangusa kwa kutumia kiganja changu cha mkono wa kulia. Mwanangu tangia umeondoka hapa nyumbani ni kama uliikwapua roho yangu na kutoweka nayo, hapa nazipigania pumzi zangu za mwisho."

"Uchungu nilioupata siku ya kukuzaa u katika nyonga zangu, nilikupenda hata wewe wajua. Mwanangu ukawa unakula kwenye mashimo ya taka. Kwamba ulikuwa mwendawazimu. Kitendo hicho kilifanya kila chakula kinachoingia kinywani mwangu nikitapike, sikuwa napata usingizi hata kidogo, naanzaje kulala angali mwanangu akipigwa na baridi huko nje. Babako alikuwa bize na mambo yake. Sijui ulipatwa na nini? Wewe ndio tegemeo langu pindi nitakaposhindwa kujihudumia mwenyewe lakini nikashuhudia unanikana na kutaka kunichoma kisu najua haukuwa wewe mwanangu" mama alipozungumza kauli hiyo ya mimi kutaka kumchoma kisu, alilia sana kaka, nami nikajikuta nalia huku nikijitupa chini kama furushi la nguo. Nyumba ilizingilwa na vilio visivyopozeka."

"Pole sana dada Pili!" japo nami roho iliniuma, ila nikajikaza kuitoa pole hiyo. Pili alionesha wazi kwamba hawezi kuendelea kunisimulia tena. Nami nikamuelewa, akarekebisha juba lake vizuri, akayafuta machozi na michirizi iliyokuwa imetapakaa katika mashavu yake. Tukapanga kukutana tena siku nyingine.

Nilisimama nikaita boda na kuondoka zangu. Nilipofika nyumbani nikamkuta kaka tukasalimia ikawa imetoka hiyo. Nilipomaliza kula chakula cha usiku niliingia chumbani kwangu, nikatulia tuli na kuanza kuyacheua masimulizi kutoka kwa pili, maswali mengi yalikiangaisha kichwa changu kwa wakati huo. "Kwa muonekano wa nje alionao pili kuna mwanaume anaekataa kumuoa!.

Kavaa ijabu pana na refu lakini kilichomo ndani kinaonekana. Pamoja na kulia sana ila bado akikutazama usoni nikama anakuita. Muondoko wake wa kunyata huku akiangusha moja moja ni mwanaume gani na yupi anayeweza kustahimili na asigeuke kutazama nyuma, hapana! hajazaliwa bado.

Au historia mbaya na chafu iliyomvaa pili imeondoa tena hamu ya kuitwa mama katika ulimwengu tuliomo. Kama nitaonana nae nitamuuliza pia.
Kusubiri mpaka kupambazuke ndio nimpigie pili, niliona nitaipunja nafsi yangu. Nilitamani walau nisikie sauti yake tu, labda kuna vitu vingine angelinieleza kwa usiku huu. Nikapiga simu ikaita mpaka ikakata, nikapiga tena awamu hii ikapokelewa ila nilisikia sauti ya pili akiwa analia, hakuzungumza chochote kile nikakata simu, sikuweza kupata usingizi kwa wakati huo, niliwaza ni kipi kilichompata pili usiku huu, ila sikupata majibu mpaka pale usingizi uliponisomba tena.


****** ITAENDELEA*******
 
PILI....... 05
Na, Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )

SEHEMU YA TANO.
Sehemu ya nne iliishia hapa......
Kusubiri mpaka kupambazuke ndio nimpigie pili, niliona nitaipunja nafsi yangu. Nilitamani walau nisikie sauti yake tu, labda kuna vitu vingine angelinieleza kwa usiku huu. Nikapiga simu ikaita mpaka ikakata, nikapiga tena awamu hii ikapokelewa ila nilisikia sauti ya pili akiwa analia, hakuzungumza chochote kile nikakata simu, sikuweza kupata usingizi kwa wakati huo, niliwaza ni kipi kilichompata pili usiku huu, ila sikupata majibu mpaka pale usingizi uliponisomba tena.

ENDELEA NAYO.....
Kulivyopambazuka asubuhi, nikafanya usafi wa mazingira hapo nyumbani. Nikaweka kila kitu sawa, nikapata chai ya moto na kachori huku ukwaju ukinishinda kutumia, "hahaha..!!" nilijicheka mwenyewe nikidai ushamba wa bara wanisumbua, kwetu musoma vitu kama hivyo hatutumii, unadamka asubuhi unakutana na ugali wa mtama nyama choma na kichuli, wee unakula mpaka unahisi roho inataka kutoka. Sambamba na yote mawazo yangu yalikuwa yapo kwa binti pili. Shauku yakutaka kujua kile kilio cha usiku sababu ilikuwa nini, ilizidi kufukuta ndani ya mtima wangu. Nikashika simu na kumpigia awamu hii akapokea,
"Habari za asubuhi pili?"
"Nzuri kiasi!"
"Kwanini unasema nzuri kiasi?"
"Hakuna kitu, basi tu" jibu kutoka kwa pili lilinitafakarisha kidogo ikabidi nimuulize kitu,
"Jana usiku nilikupigia simu, ukapokea ila hatukuelewana!"
"Sikuwa hata na uwezo wa kuzungumza zaidi ya kulia tu, nilikumbuka mbali sana, wenzangu wote niliocheza nao utotoni wengi wameolewa na kuoa, ila.! ila.!" Pili alishikwa na kigugumizi akaanza kulia.
"Ila nini pili, please! usilie!"
"Hapana mbona silii kaka!"
"Haya niambie Dada angu, kwanini unajutia hivyo?"
"Naumia kuelezea haya kaka, mimi peke ndio sijaolewa, na nani wa kunioa angali walinishuhudia nikilala kwenye mashimo ya taka?" ghafla simu ilikata, nikaangalia salio kumbe lilikuwa limeniishia.

Nikitazama ratiba yangu nimebakiza siku moja tu, niweze kuondoka jijini Tanga, lakini bado kuna mengi sijayapata kutoka kwa pili. Kaka yangu alikuwa bado hajaoa, hakuwa muumini sana wa kuchangamkia suala ilo. Nikaenda hapo soko la mgandini nikanunua samaki aliyekaangwa na fungu moja la mchicha. Ndani ya dakika kumi na tano nilikuwa nafuta meza ni ishara kwamba matonge ya ugali yashajipanga sawa bin sawia ndani ya tumbo la mvuja jasho.

Nikachukua simu yangu, nikatafuta namba ya pili, nikamtumia ujumbe mfupi wa maandishi kwamba leo tuonane. Lakini ujumbe huo haukujibiwa. Nikatuma tena vipi utapata nafasi tumalizie maongezi yetu maana nimebakiwa na siku moja tu ambayo ni kesho. Dakika ishirini na tano zilikatika bila jumbe hizo kujibiwa, wingu la kukata tamaa taratibu likaanza kunifunika. Nikaona kama mkasa huu wa pili unaenda kuishia njiani. Nikawaza ni njia ipi itanifikisha kwao pili, ukizingatia barabara za namba ni ngeni kwangu, "hahahahah..." nilijichekea mwenyewe ka chizi, sasa haya mambo ya barabara kupewa namba waliyatoa wapi ila watu wa pwani nao wamezidi uswahili.

Muda ulizidi kuyoyoma ilikuwa ni saa tisa na robo za mchana. Nikajilaza kidogo sofani, nikiufungulia mziki kwa mbali uweze kunisindikiza katika safari ya kutafakari namna ya kuonana tena na pili.
"Samahani kaka mtunzi, nilikuwa mbali na simu, sioni umuhimu tena wa kuwa nayo kila muda. Inanikumbusha mengi, na kama tusipoonana leo basi utakuja kuona kaburi langu, kama itatokea umepata taarifa za kujipiga kwangu kitanzi." "What! ulinistusha ujumbe huo mfupi wa maandishi kutoka kwa pili. Nikaishika simu yangu vizuri na kuanza kuusoma upya huenda nilikuwa naota.

"Samahani kaka mtunzi, nilikuwa mbali na simu, sioni umuhimu tena wa kuwa nayo kila muda. Inanikumbusha mengi, na kama tusipoonana leo basi utakuja kuona kaburi langu, kama itatokea umepata taarifa za kujipiga kwangu kitanzi." Ujumbe ulisomeka vivyo hivyo hakuna kilichobadirika hata kidogo. Nikakurupuka upesi pale sofani nikakaa vyema.

"Inamaana pili anataka kujinyonga!" nilijiuliza pasi kupata majibu, nikaona bado jukumu la kumuokoa pili lingali mikononi mwangu. Nikamtumia kaka meseji kwamba natoka kidogo, hakuwa na neno alinikubalia. Hata sikuoga, nikachukua shati langu lenye maua kama bustani nikatupia na ile kadeti yangu ya kijivu aliyonipa kakaangu wa songea, chini nikatupia raba zangu nyeusi nilizonunua 2500 pale tangamano. Kwaaliye niona alijua labda nimeingia jana kutoka Dubai, nilipendeza haswa sikuchosha kutazamwa. Niliita boda nikamwambia nipeleke mjini sehemu ambayo naweza pata upepo na hata maji.

"Haina shaka kaa twende!" ilikua ni sauti ya bodaboda mwenye asili ya kiarabu. Nami nikakaa upesi safari ikaanza, takribani dakika kumi tulifika. "Mwambia upo hii bichi ya kulipia, ka ni mwenyeji atapajua maeneo ya raskazoni" alihitimisha maelezo yake dereva boda huyo. Nikatikisa kichwa kuashiria nimemuelewa nikampa pesa akaondoka.

Tayari bila kupoteza muda nikampigia pili nikamuelekeza nilipo, akasema, "naja ila sina nauli!" sasa naja ndo nini watanga bwana, nilicheka kidogo kisha nikamwambia akifika nitamlipia nauli. Nikaingia hapo bichi watu walikuwa si wengi saana, nikatafuta sehemu yenye uficho na utulivu kidogo nikaketi hapo. Nilipouliza vinywaji nikaambiwa pale ndani hawauzi ila kuna duka lipo nje, nikaenda nikanunua maji chupa mbili, maana pili nae ni mdau mkubwa wa maji kuliko soda.
Nikiwa naangaza huku na kule ujumbe mfupi wa maandishi ukaingia katika simu yangu, "kaka umekalia kwa wapi, mbona sikuoni" naam! ulikuwa ni ujumbe toka kwa pili, nikasimama kwenye uwazi nikamuona na kumpungia mkono akaniona na kuanza kuzipiga hatua kuja nilipokuwa. Nikamlipa boda, Kama kawaida yake alivalia ijabu kubwa na refu jeusi kichwani akiwa na remba jeupe alipendeza haswa, huo muondoko wake sikuweza kuuzoea kila alipoinua mguu mapigo yangu ya moyo yalipiga na kuachia sauti kwamba, "Sijui nikwambie, sijui utanichukia, shetani niache!" nikajikuta nacheka kwa sauti, kumbe pili nae kasimama mbele yangu akashangaa. "Mmmh! mbona wanicheka" alihoji pili. "Hapana nacheka wale watoto hawawezi hata kuogelea!" "Mmmh! we nidanganye tu" aliguna pili.

"Karibu sana dada pili pole kwa safari fupi!"
"Mmh! asante sasa hii nayo utasema safari, kutoka hapo 16 tu!"
"Ndio ni safari maana ajali za bodaboda zimekuwa ni nyingi sana." Baada ya kujibu hivyo, nikaona nisipoteze muda nikaiweka simu yangu sawa kwaajili ya kurekodi maongezi yetu. Nilimueleza pili anieleze, kauli ya kusema kwamba tusipoonana leo nitakuja kuliona kaburi lake alimaanisha nini? Pili alinitazama usoni takribani sekunde tano, mdomo ulikuwa mzito kila alipotaka kunieleza, alikuwa kama anasita, "Usinifiche pili nieleze huenda naweza kukusaida. "Utakachoweza nisaidia ni kuja siku ya mazishi yangu, usaidiane na vijana wenzio kuchimba kaburi na kunihifadhi ndani basi" alizungumza pili huku machozi yakiwa yanamlenga machoni pake.

"Usiseme hivyo pili unakosea!" nilidakia baada ya kutatizwa na kauli hiyo kutoka kinywani mwa pili, nahisi kipindi anaitoa hata yeye ilimuunguza. "Nakuomba usithubutu kujiua!" nilizidi kumsisitiza asifanye hivyo. Pili aliyafungua maji yake akabugia mafunda ka mawili ya maji kisha akafunga, ni wazi alikaukiana kooni. Alinitazama tena akaanza kulia huku akizungumza kwa chungu uliokithiri,
"Kaka Lovi kuna kijana alijitokeza, akanipenda sana. Ni mzaliwa wa Tanga ila amekulia nchini Oman aliitwa Farid.

Alikuwa ni shombeshombe, pua yake ya kuchongoka na ndefu, nikisema nadhani unanielewa, alibarikiwa nywele yule mkaka. Makadirio ya urefu wake ni futi tano na inchi mbili kakuzidi kidogo tu urefu, yule kaka nami nikatokea kumpenda, ndugu zake wakaja nyumbani wakaongea na wazazi japo mama alikuwa bado u mgonjwa. Baba yeye alikuwa aeleweki kabisa kuna wakati nae alikuwa akizungumza mwenyewe huku akisema, "nisamehe mwanangu! nisamehe mwanangu!" kila tulipomuuliza anamaanisha nini kuhusu kauli hiyo hakueleza chochote kile." nilimkatisha kidogo pili asiendelee kuzungumza maana simu yangu ya mkononi ilikuwa ikiita, kutazama vizuri nikaona ni namba ngeni, "aaah! hawa watakuwa ni wasomaji wa simulizi zangu fesibuku, ukiweka namba za simu tu kosa, bora wapige wakihitaji simulizi ila wao ukipokea tu wakasikia sauti yangu ya kiume wanakata simu sijui jina lovi linawachanganya, "hahahha..!!" nilicheka kidogo nikamuona pili nae akiachia tabasamu hafifu kabisa.
 
PILI....... 06
Na, Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )

SEHEMU YA SITA.
Sehemu ya tano iliishia hapa......
"Kaka Lovi kuna kijana alijitokeza, akanipenda sana. Ni mzaliwa wa Tanga ila amekulia nchini Oman aliitwa Farid. Alikuwa ni shombeshombe, pua yake ya kuchongoka na ndefu, nikisema nadhani unanielewa, alibarikiwa nywele yule mkaka. Makadirio ya urefu wake ni futi tano na inchi mbili kakuzidi kidogo tu urefu, yule kaka nami nikatokea kumpenda, ndugu zake wakaja nyumbani wakaongea na wazazi japo mama alikuwa bado u mgonjwa. Baba yeye alikuwa aeleweki kabisa kuna wakati nae alikuwa akizungumza mwenyewe huku akisema, "nisamehe mwanangu! nisamehe mwanangu!" kila tulipomuuliza anamaanisha nini kuhusu kauli hiyo hakueleza chochote kile." nilimkatisha kidogo pili asiendelee kuzungumza maana simu yangu ya mkononi ilikuwa ikiita, kutazama vizuri nikaona ni namba ngeni, "aaah! hawa watakuwa ni wasomaji wa simulizi zangu fesibuku, ukiweka namba za simu tu kosa, bora wapige wakihitaji simulizi ila wao ukipokea tu wakasikia sauti yangu ya kiume wanakata simu sijui jina lovi linawachanganya, "hahahha..!!" nilicheka kidogo nikamuona pili nae akiachia tabasamu hafifu kabisa.

ENDELEA NAYO.....

"Pole hao ndio binadamu hawana jema!" nikaitikia, "asante dada pili" ebu tuendelee kwa hiyo wazazi walivyokubali ndoa ikafungwa au?, "si bora hata hiyo ndoa ingefungwa kisha ikavunjika ningekuwa nimetoa mkosi" alijibu pili akionekana ametonesha kidonda kilichokuwa kimeanza kupona. "Unamaanisha nini?" nilimuuliza pili, nikiwa nimekodoa macho yangu kwa mshangao nikitaka kujua ilikuaje.

"Ndoa haikufungwa!"
"kwanini tena wakati tayari kijana alishakubaliwa na wazazi wako?" swali lilikuwa mwiba mchungu kwa pili hakuweza kujibu akachukua kitambaa chake na kuufunika uso nisiweze kuyashuhudia machozi yanavyombubujika ila miguno aliyokuwa anaitoa niligundua fika kwamba pili analia.

Awamu hii nilimuacha alie bila kumtuliza ili tu aweze kuupoza moyo wake unaoteketea kwa moto mkali usiozimwa kwa maji wala mchanga. Nilipoona pili ameanza kutulia, nikampa pole nyingi zisizokuwa hata na idadi, sikuchoka kufanya hivyo. Maana huenda mimi kumuuliza kwangu ni kama naurudisha nyuma msiba ambao tayari ulikuwa umekwisha kumalizika.

"Nakuomba usilie tena pili! punguza mawazo utadhoofu na kubaki flemu ya mtu" "hapana kaka hapa duniani siwezi kupumzika tena labda mbinguni tu," alijibu pili katika hali ya huzuni. "samahani pili, nimalizie kuhusu hiyo ndoa yako" nilimsisitiza anisimulie ili nipate kujua, pili aliinamisha kichwa chini, hakutaka kunitazama usoni.

"Kaka uwa sipendi kusimulia kabisa kilichotokea, ilibaki siku moja tu ndoa ifungwe. Nakumbuka ilikuwa ni Alhamisi kama saa kumi na moja za jioni, nilishachorwa na inna aisee nilipendeza saana. Kumbe kipindi kile nilivyokuwa kichaa nilikuwa mpaka navua nguo zote na kubaki mtupu ka nilivyotoka ndani ya tumbo la mamangu, anhaa! kaka! kaka! we acha tu, uzito wa mateso ulinielemea" "jikaze pili usilie" nilimsihi tena kwa mara nyingine baada ya kuona dalili zote katika uso wake kwamba si punde angeangusha mvua ya machozi.

"Basi kumbe kipindi nikiwa katika hali hiyo, kuna watu walifurahi wakawa wananipiga picha huku wengine wakinirekodi nikicheza uchi katika mashimo ya taka. Inaniuma sana pamoja na hali ile ya ukichaa bado watu hawakunionea huruma, unaniambia nisilie, acha nilie tu kaka!, yule mume wangu mtarajiwa ambaye kesho yake tungefunga ndoa, alitumiwa picha hizo pamoja na video nikiwa mtupu!. Dah! alikasirika, hakutaka kusikiliza ndugu yangu yeyote yule, pesa alizoandaa sherehe zikateketea na ndoa ikateketea.

Nilipoziona hizo picha sikuamini kama ni mimi, nilipiga yowe moja kwa uchungu nikapoteza fahamu papo hapo. Baada ya dakika ishirini fahamu zilirejea nakuta ndugu wamenizunguka wakijaribu kunituliza, nilichukua kisu na kutaka kujichoma asingekuwa shangazi Rehema kunifatilia nyuma saizi nisingekuwa na wewe hapa, lakini bado duniani sina nafasi ya kuishi kwa furaha tena. Muda wowote utasikia habari zangu katika vyombo vya habari, wewe ndie wanichelewesha"

Nilimkatisha asiendelee kuzungumza huku nikimwambia "Haa! we pili mara ngapi nimekusihi usitoe kauli hiyo. Siku yako ikifika utakufa, lakini si kwa kufanya hivyo kwa mikono yako mwenyewe, adhabu itakuwa ni kubwa sana uko uelekeapo." "sidhani kama hiyo adhabu itashinda hii niliyopata hapa duniani hivyo siogopi tena kaka" alidakia pili, kauli hiyo iliniongezea kitu katika akili yangu kwamba pili kafika kipimo cha mwisho kabisa cha uvumilivu, kama ni mshale wa mzani umegota mwisho hauwezi songa mbele tena.

Ulikuwa ni wakati wangu wakumshukuru pili kwa ushirikiano wake. Kwa yale tuliyozungumza yaliibua kitu kipya katika maisha, nikafarijika kuona nimekutana na msomaji au mfatiliaji wa simulizi zangu katika mitandao ya kijamii. Nilijikuta napata nguvu na shauku ya kuzidi kuandika zaidi, huenda nikakutana na watu waliopitia maumivu zaidi ya pili. "Pili kesho mimi nasafiri, narudi zetu musoma!" "asante kaka Mungu akusaidie ufike salama" alizungumza kauli hiyo huku machozi nayo yakimdondoka. Akajikaza na kunitazama usoni kisha akazungumza,

"ukaribu uliouonesha kwangu ni Mwenyezi pekee ndo mwenye kujua, umeutumia muda wako mwingi kunisikiliza, asante sana. Kikubwa uendelee kunikumbuka katika maisha yako yote, na usiache kuandika watu wazidi kujifunza. Kama nilivyokueleza miaka niliyoishi kwa mateso imetosha liwake jua inyeshe mvua lazima niwaachie dunia yenu. Utakapoandika simulizi kuhusu maisha yangu naomba usiniandike kwa ubaya, ieleze dunia bila kuficha jambo kuhusu matatizo yote yaliyonizonga angali nikiwa binti mbichi kiasi hiki, nakupenda sana kaka lovi, mtunzi bora wa simulizi kwangu" kauli hiyo ya mwisho kutoka kinywani mwa pili ilikuwa ni nzito kwangu kidume mzima nikalimwaga chozi hadharani, nikakiinamisha kichwa changu chini kwa aibu pili asiweze kugundua kwamba chozi nimelimwaga.

******** ITAENDELEA ******
 
RIWAYA : PILI ....... 07
MTUNZI : Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )

SEHEMU YA SABA.

Sehemu ya sita iliishia hapa......
Utakapoandika simulizi kuhusu maisha yangu naomba usiniandike kwa ubaya, ieleze dunia bila kuficha jambo kuhusu matatizo yote yaliyonizonga angali nikiwa binti mbichi kiasi hiki, nakupenda sana kaka lovi, mtunzi bora wa simulizi kwangu" kauli hiyo ya mwisho kutoka kinywani mwa pili ilikuwa ni nzito kwangu kidume mzima nikalimwaga chozi hadharani, nikakiinamisha kichwa changu chini kwa aibu pili asiweze kugundua kwamba chozi nimelimwaga.

ENDELEA NAYO......

"Dada pili nimekuelewa vyema kabisa. Nitatembea na yale uliyonisihi, katu sitayaacha njiani. Nitakuwa shuhuda mzuri wa yote uliyonisimulia, maisha yako, manyanyaso yako, vitaishi nami daima katika mtima wangu. Kumbukumbu hii haitafutika kamwe." nilimjibu pili kwa sauti iliyotawaliwa na simanzi. Pili hakuwa na muda wa kunitazama alikuwa amejiinamia kichwa chini. Lakini najua alinisikia sababu masikio hayachagui vya kusikia. Nilimtazama kisha nikamuita,

"Pili!"
"Abee kaka!"
"Naona upo nami kimwili tu! lakini akili yako iko mbali sana"

"Hapana nipo pamoja nawe, nakusikia vizuri kabisa!" Nilipotazama saa yangu ya mkononi niligundua muda si rafiki tena, masaa yanakimbia ka mwanariadha Bolt. Nikiwa bado natafakari namna ya kumuaga pili nilistushwa na sauti yake nyororo ikiniambia, "kaka geuka niangalie" maana nilikuwa nimekaza macho yangu kutazama baharini huku nikiishangaa ile miti ya mikoko, "hii miti imeweza vipi kuota ndani ya bahari itabidi nifatilie jambo ili kwa kina kabisa!" wakati sauti ya pili ikinisihi nigeuke mimi nilikuwa nikitafakari jambo ilo la mikoko.

"Nishageuka tayari!" nilijibu huku nikiwa najiweka sawa, nikachukua chupa yangu ya maji nikabugia kwa haraka mafunda kama manne, nikaiweka chini na kumtazama pili usoni.

Nilijawa nashauku ya kutaka kujua ni kipi anataka kunieleza huku tukiwa tunatazamana. Mapigo ya moyo yalinienda mbio kama mwanambuzi anayekimbizwa na mbwa mwitu. Pili akashika ule mkoba wake mdogo ulikuwa na rangi ya ugolo kwenye zipu ya mbele paliwekwa kimdoli cha mtoto wa kike. Nilikuwa nikimtazama kwa makini alifungua zipu ya kwanza akafunga ila nilibahatika kuiona kamba mpya ya katani, sikutaka kuhoji kitu kwa wakati huo. Akafungua zipu ya pili akatoa picha akaibusu ka mara nne kisha akanikabidhi mikononi mwangu nikaipokea.

"Niwewe huyu!?" Nilimuuliza pili nikiwa nimeyatumbua macho yangu kwa mshangao! Nafuu hata chura aliyebanwa na mlango, na vile nina jicho kubwa.

"Ni mimi ndio!" baada ya jibu ilo kutoka kwa pili, nikaitazama tena picha ile, ni kweli alikuwa ni yeye. Sikuzoea kumuona katika yale mavazi, alivalia taiti nyeusi, juu akaweka blauzi ndefu nyeupe, akastili kichwa chake kwa lemba jeusi, viatu vya wazi viliipamba miguu yake huku unyayo ukifichwa kwa soksi nyeupe. Nilisisimka ghafla kama mwanaume, hisia zikaenda mbali nikajilaumu kwanini nisingelimwambia pili mapema kwamba! kwamba.. nikifika hapo tu ulimi unakuwa mzito. Nikaitazama ile picha kwa mara ya mwisho kisha nikamtazama tena pili juu mpaka chini, nikiwa nafikiri cha kuongea pili aliniwahi.

"Vivyo ndivyo nilivyokuwa! Kabla dunia haijanitandika viboko!"

"Aiseee Pili!" Nilisita kidogo kuzungumza, nikaachia tabasamu huku nikijifanya naitazama simu yangu, hakuna ujumbe wowote uliokuwa umeingia ila nilijifanya tu, niweke koo langu sawa kwa kujikohoza kidogo, nikanywa tena maji.

Nikamueleza bila kumficha kwamba, asijione kazeeka, yeye bado ni mrembo kuanzia hapo awali na mpaka sasa. Nikamuapia kwamba ipo siku isiyo na jina, tarehe wala mwaka Mungu atamfuta machozi, atazaliwa upya na kuisahau historia chafu ya maisha yake, mlango wa baraka utafunguliwa, atajazwa furaha na tabasamu lisilokoma.

Waliomdhihaki na kumpiga picha za utupu watarudi kwake na kumpigia magoti wakihitaji msaada wake. Mwisho nikamwambia, hii ndio dunia na lazima maisha yaendelee!. Huyu analia yule anacheka, huyu anazaliwa leba, yule anakata roho na kupelekwa mochwari kwenda kuhifadhiwa. Maneno yangu hayo yalimchoma sana pili, akayafumba macho yake asinitazame ila machozi yalipenya vivyo hivyo njia nne nne akayaachia yachuruzike.

"Nashukuru sana pili, kwa zawadi hii ya picha, ni kubwa na sikutegemea kama utanitunuku upendo huu wa dhati kutoka chini kabisa ya uvungu wa moyo wako uliopondeka kwa maumivu!. Nitaitunza, nitailinda, nitaithamini picha hii. Katika maisha yangu tukio ili litaacha alama ya moto isiyofutika katika moyo wangu." Wakati nikizungumza maneno hayo, pili alikuwa ametulia tuli kama mtu anayetazama tamthilia isyokuwa na mikasa ya kutisha hata kidogo.

"Hiyo ndio zawadi nimeona itakufaa wakati ambao sitakuwepo!" alizungumza pili kisha akanyamaza takribani sekunde kama nane, ndipo akaendelea kuzungumza tena, "Katika mitandao yangu ya kijamii nimefuta picha zote, na kujiondoa kabisa. Isipokuwa fesibuku tu, nimeacha picha moja ya njiwa mweupe akiwa na ua jekundu mdomoni. Unaweza usinielewe ni kwanini nimefanya hivyo ila utakuja kunielewa siku za mbeleni."
"Unamaanisha nini?" nilimkatisha pili, aliniacha njia panda.

"Tulia kakangu bado naendelea, kwa hiyo nimeamua nikupe hiyo picha ili siku ukipata taarifa zangu usiwe na wakati mgumu wa kupata picha yangu. Hivyo utaipiga picha hiyo picha nilokupa kwa kutumia simu yako kisha utaiweka kama ni fesibuku au laah..!! Utachagua maneno ya kuandika kama ni, Gone too soon! Rest in peace my friend pili, Umeumaliza mwendo umepigana vita vilivyovyema hapa duniani. Kwa kuwa wewe ni mtunzi huwezi kosa cha kuandika." Maneno hayo kutoka kwa pili yalinihuzunisha sana, ndipo nikaelewa ni kwanini anakamba mpya ndani ya mkoba wake, kuna wazo liliniijia nikatoe taarifa polisi ila sina uhakika hiyo kamba ni ya kazi gani, nikahofia nami nitajumuishwa na safari yangu isiwepo tena.

Pili nisikilize kwa makini kabla sijaondoka, "kila leo huwa na jana, juzi ikawa zamani. Hivyo maisha ni sawa na safari ndefu. Shida haina hodi, shida haziishi. Usipokubali taabu, hutaonja raha. Wanja sio dawa ya kengeza. Chura akitupwa majini hafi, usikate tamaa bado unayo nafasi nyingine ya kuishi. Kunyolewa kipara si mwisho wa kumea nywele. Mtu hukimbia wingu, hakimbii mvua. Tayari umeshanyeshewa Da pili huna sababu ya kuikimbia tena mvua."

"Nakuomba usilie pili nisikilize!"

"Hapana kaka silii!" alijibu pili huku akijizuia asilie, lakini haikuwa vyepesi kama alivyodhani. Nilimuonea imani, nikiwa kama binadamu nilijihisi vibaya sana, nikasimama huku nikisubiri pili nae asimame tuweze kuondoka, "Naomba unishike mkono na kuniinua sina nguvu tena!" alilalamika pili. Nikamshika na kumuinua.

"Sitaacha kukupenda kaka!" alizungumza pili kwa sauti iliyopooza. Nami nikatikisa kichwa kuonesha nimekubaliana na kile alichosema.
"Leo najua upendo ni nini! Ni kwasababu yake mamangu, lakini napozungumza wakati huu, mama yupo kitandani, hajiwezi! Yaani si marehemu, si mzima, taabani, hajui wala hajitambui. Jamani mama yangu.!!" pili aliangua kilio, tena kilio haswa! tukiwa tunaingia ndani ya bajaji.





ITAENDELEA
 
PILI....... 08
Na, Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )

SEHEMU YA NANE.
Sehemu ya saba iliishia hapa......
"Leo najua upendo ni nini! Ni kwasababu yake mamangu, lakini napozungumza wakati huu, mama yupo kitandani, hajiwezi! Yaani si marehemu, si mzima, taabani, hajui wala hajitambui. Jamani mama yangu.!!" pili aliangua kilio, tena kilio haswa! tukiwa tunaingia ndani ya bajaji.

ENDELEA NAYO.........
Dereva wa bajaji alikuwa na mashaka, nikajua kinachomsumbua ni umbea tu. Aliuliza kulikoni sikumjibu kitu nikafanya kama sijamsikia wakati akiuliza. Akafungulia mziki ukasikika ule wimbo wa dini kwamba dunia haina huruma, kabla haujaisha akapeleka mbele ukaja wimbo wa zamani kidogo wa mzee mapangala, Dunia tunapita kila kitu kitabaki.

Nilimuangalia dereva wa bajaji nikajisemea mwenyewe, "Mpuuzi kweli huyu, kwahiyo hizo nyimbo anamuwekea nani! Katuona kwamba sisi tumekata tamaa na maisha si ndio!" Nikamtazama Pili kuona kama alikuwa akizifatilia nyimbo hizo, nikagundua yupo mbali sana kimawazo.

Alikuwa amejiinamia kichwa kama mwanakondoo aliyenyeshewa na mvua.
"Kwa hiyo Pili unashukia wapi?" Hakunijibu kitu, nikaamua kumuuliza tena.
"Naongea na wewe mpendwa washukia wapi?"
"Oooh! Kumbe waongea na mimi!" Alikurupuka pili kana kwamba alikuwa usingizini, akili yake ilisafiri na kuelea mbali kabisa kimawazo.

"Itapendeza kama utaniachia nyumbani kabisa, kisha wewe uendelee na safari yako" Alijibu pili, akainamisha tena kichwa chake kama alivyokuwa awali. Sikupenda kumuona Pili akiwa katika muonekano huo lakini machungu anayoyapitia ni siri ya moyo wake. Dunia imegeuka kuwa jehanamu kwake, kashindwa kufurahia maisha katika ujana wake. Dereva alisema kwamba tayari tumeishafika barabara ya 16, asimame wapi. Pili aliinua kichwa kisha akasema nyumba ile pale mbele yenye rangi nyeupe.

Tulivuka kama nyumba tano tukawa tumefika tayari. Dereva akashuka na kuja kufungua mlango wa nyuma, maana alikuwa ameuchomelea sana, kwa mtu mgeni si rahisi kuufungua. Pili alishuka akaniita nami nikashuka alinikumbatia kwa sekunde kadhaa kama ishara ya kuniaga.

"Ubarikiwe sana kakangu, tumeonana kwa muda mfupi, ila tuliyozungumza ni mengi. Nakusihi tena kwa mara ya pili, usinisahau katika maisha yako, usiniandike kwa ubaya kama itatokea umeandika simulizi juu ya maisha yangu, kila wakati nimekuwa nikikukumbusha juu ya ilo. Nakupenda sana kaka mtunzi wa hadithi nzuri." alizungumza maneno hayo pili huku akiwa amenikumbatia, hakuogopa hata watu waliokuwa wakipita, nilishuhudia akilia kwa hisia kali, huku akipambana kuizuia sauti isitoke. "Pole sana pili, huenda ipo siku tutaonana tena!" Nilijaribu kumtuliza kwa kauli hiyo lakini bado haikuwa na msaada wowote ule. Pili alitoa kitambaa chake akayafuta machozi tayari kwaajili ya kuingia ndani.

"Naomba twende ukamuone mamangu hata sekunde moja!"
"Naingia vipi ndani kwenu pili!"

"Wewe nifuate mimi nyuma!" nilipata wakati mgumu kwakweli, nikajiuliza naingia vipi kwao na mtu ambaye hakuna hata nduguye mmoja anaenifahamu. Kama nikikataa basi pili anaweza nung'unika maisha yake yote. Nikajikaza huku nikimuambia yule dereva bajaji aondoke zake nitachelewa kutoka, nikamlipa pesa yake akaondoka. Watu walikuwa ni wengi pale uwani, nilitambua fika kwamba wapo kwaajili ya kumjulia mgonjwa hali. Wale wakubwa niliwapa heshima yao bila kupepesa macho, baadhi ya kinamama walinikazia macho na wengine kukonyezana.

Pili aliniongoza mpaka ndani alipo mgonjwa. Nilipoingia tu ndani ya chumba hicho nilipokelewa na chupa za maji zilizokuwa juu ya meza, pembeni kulikuwa na matunda kama ndizi na maembe. Nilipoyatupa macho yangu juu nikashuhudia dripu la maji ambalo lilikuwa likishuka taratibu na kuzama mwilini kwa mamake pili angalau kumpunguzia makali ya maumivu.

Nilijawa na uwoga, huruma ikanivaa ghafla nikajisemea kimoyomoyo kama mtu unaamka ukiwa salama unakula bila mpira wala kupumua pasi ya kutumia msaada wa mashine unapaswa kumshukuru Mungu kila baada ya sekunde moja. Je ni wangapi wanafanya hivyo? Nikiwemo mimi namkumbuka Mwenyezi Mungu pindi niwapo na shida ila leo nimejifunza kitu katika maisha nitakuwa nikisema neno asante kila iitwapo asubuhi, mchana na hata usiku. Wagonjwa wote mliopo vitandani mkiupigani uhai wenu, nitashiriki nanyi katika dua, ipo siku mtasimama kutoka vitandani na kuendelea na majukumu yenu ya ujenzi wa taifa la Mungu.

"Kaka huyo unaemuona hapo kitandani ndiye mamangu!" aliniambia pili, huku nikiona wazi machozi yanamlenga. Alinionesha mamake baada ya kuniona nikiwa nimezama katika tafakuri nzito sana. Nikamtazama yule mama pale kitandani, alikuwa amemezwa na shuka, unaweza usijue kama kuna mtu kalala pale, mwili wake ulikuwa umeisha. Baadhi ya ndugu kila walipomtazama waliishia kuangusha chozi wakijua pale wanahesabu siku tu. Pamoja na ugonjwa wake bado mdomo ulikuwa imara, akiwa anaongea ukimsikia kwa nje unaweza fikiri ni mzima kabisa.

Pili alisogea akaketi pembeni ya kitanda kisha akamfunua mgonjwa kichwa. "Mama vipi hali?" Pili aliuliza akiwa anamtazama mama usoni. "Kila kunapokucha nafuu ya jana, sina maisha tena mwanangu!" Jibu ilo kutoka kwa mamake lilimuumiza sana pili, kulia alishindwa akabaki anamtazama usoni, bila ya kujua afanye nini.

"Mama kuna rafiki yangu anataka akusalimie!" Alinena pili. "Yuko wapi mbona simuoni!" Alijibu kwa tabu sana ma pili, ndipo nikasimama na kusogea pembezoni mwa kitanda ili aweze kuniona, nikiwa najianda kuzungumza nikasikia sauti ikitoka nje kwamba,"Msimuongeleshe sana mgonjwa muacheni apumzike" Lakini pili akanisihi, "Achana nao wanafiki hao!" Nikajiuliza nianzie wapi kuzungumza, nikaona salamu itakuwa ni muhimu kabla ya mengine, ili niwahi kuondoka nikajiandae na safari yangu.
"Mama shikamoo!"

"Marahaba mwanangu!" Aliitikia mama pili, huku akitokwa na kikohozi kizito mfululizo. Nikatulia kama sekunde tano hivyi apate kutulia, nilimuonea huruma alikuwa akizivuta pumzi zake kwa kasi na kuzitoa nje taratibu, nikagundua ni maumivu kiasi gani yalikuwa yakipita kwa kasi katika mwili wake kwa wakati huo. Alivyotulia nikaendelea kuzungumza, pili alikuwa akinitazama kwa makini ajue ni nini nitazungumza. "Pole sana kwa maumivu unayopitia mama, siku si nyingi naamini utasimama na kukiacha hicho kitanda. Jipe moyo hakuna aliyeteseka milele, wakati wako wa kutabasamu nauona u karibu!" Nilivyoongea kauli hiyo mama pili aliguna.

"Mmh! Mimi kupona si rahisi mwanangu, hapa nilipo mguu moja u duniani na mwingine kaburi, sasa ninakinukia kifo!" Alidakia mama pili kabla hata sijamaliza kuzungumza, lakini hayo maneno yake aliyatamka akiwa ameikunja sura kwa uchungu, akaomba msaada tumgeuzie upande mwingine, alichoka kulalia ubavu tangu asubuhi. Tayari alikuwa ameanza kutokwa na vidonda mgongoni sababu ya kulala muda mrefu. Mama pili alimuongelesha mwanaye kwa kilugha sikuweza kuelewa ndipo akanidokeza, "Mama ananiambia kwamba au wewe ndiye mchumba mpya nimekuleta ujitambulishe kabla hajafa!" Niliwaza mengi pamoja na hali ya ugonjwa aliyonayo bado anatamani ashuhudie ndoa ya bintiye angali akiwa hai.

"Hapana mama ni rafiki yangu tu!" Pili alijibu kwa kiswahili ili nami nipate kuelewa kinachozungumzwa. Furaha ilimuishia ghafla nikajua tayari pili kakumbuka vitu vinavyomuumiza, nikamuona anainamisha kichwa chake chini, akamshika mamake katika paji la uso na kumwambia, "Mama kwa ule uchafu wa zile picha na video ni mwanaume yupi atakayekuwa tayari kunioa! Maisha yangu yameoza yanatoa harufu." Si pili si mama pili walilia kwa pamoja, machozi yao yalituumiza wote tuliokuwa mule ndani, ndugu wakajaribu kuwatuliza nami nikamshika pili kwa lengo la kumuaga ila nikaona bado nina deni kwake.

"Pili usilie, unapolia unazidi kumuumiza mama aliyepo kitandani. Anahitaji faraja kutoka kwako katika nyakati hizi ngumu kuliko nyakati zote za maisha yake. Usiwaze kuhusu hizo video na picha ukiwa unacheza uchi tena kwenye mashimo ya taka. Kumbuka hukuwa wewe yule! Ulichanganyikiwa tambua ilo, hakuna wa kukuhukumu!"

"Wee unasema tu kaka!, unadhani ni wote watakaoelewa hali niliyokuwa nayo wakati huo, wengi wanaishia kuushangaa utupu na maumbile yangu, nakusema huyu mdada kauimbika ila kajiaibisha. Naumia sana,"
"Pole dada ndio maisha, wapo waliojirekodi video za utupu, tena wakiwa na tabasamu tele, na niwasomi kabisa. Zilivyosambaa hawakujiuwa zaidi ya kuonesha kujutia tu tena katika mitandao ya kijamii. Sembuse wewe waliyekurekodi ukiwa umechanganyikiwa bado unayo nafasi ya kuitwa mama bora umri wako bado, sa yule aliyetumia kifungashio cha kinywaji baridi kuzimaliza haja zake tena ameridhika kabisa, aisee pili we acha tu." Nilipomaliza kuzungumza maneno hayo niliaga pili akasema hatoweza kunisindikiza anataka ambadili mama nguo, ila alininong'oneza sikioni kwamba, "Nasikitika sana kaka, kuonana nawe kwa mara ya mwisho, kwaheri ya kuonana. Ukipata taarifa kuhusu mimi usilie sana, bali tumia kalamu yako kama mwandishi kunililia."
 
RIWAYA : PILI....... 09
MTUNZI : Lovi Pius Kijogoo.
0757 238 304. ( Whatsap )

SEHEMU YA TISA.

Sehemu ya nane iliishia hapa......
"Pole dada ndio maisha, wapo waliojirekodi video za utupu, tena wakiwa na tabasamu tele, na niwasomi kabisa. Zilivyosambaa hawakujiuwa zaidi ya kuonesha kujutia tu tena katika mitandao ya kijamii. Sembuse wewe waliyekurekodi ukiwa umechanganyikiwa bado unayo nafasi ya kuitwa mama bora umri wako bado, sa yule aliyetumia kifungashio cha kinywaji baridi kuzimaliza haja zake tena ameridhika kabisa, aisee pili we acha tu." Nilipomaliza kuzungumza maneno hayo niliaga pili akasema hatoweza kunisindikiza anataka ambadili mama nguo, ila alininong'oneza sikioni kwamba, "Nasikitika sana kaka, kuonana nawe kwa mara ya mwisho, kwaheri ya kuonana. Ukipata taarifa kuhusu mimi usilie sana, bali tumia kalamu yako kama mwandishi kunililia."

ENDELEA NAYO....

"Nitumie kalamu yangu kukulia!" Niliwaza kauli hiyo kutoka kwa pili nikiwa naelekea nje ya geti. Sikuwa na lakufanya tena, maana kama nikumshauri nimefanya hivyo sana. Nimekubali mpaka kuingia nyumbani kwao ili tu apate kufarijika. Nilichukua pikipiki nikaelekea zangu nyumbani, sikuwa hata na muda wa kupoteza nilianza kupanga nguo zangu. Ilipofika saa mbili kamili za usiku kaka alikuwa ndio anarejea nyumbani, alikuja na nyama ya kuchoma na ndizi, nilivishambulia kwa fujo ni siku nyingi sikuitia kinywani nyama ya kuchoma. Kabla sijaelekea chumbani kwenda kulala kaka alinipa tiketi yangu. Ilikuwa ni safari ndefu ilinipa mawazo nikifikiria nitaingia jijini mwanza saa nane za usiku, itanibidi nikalale ili niwahi kudamka.

"Kwaheri ufike salama mdogo wangu!"
"Asante sana kaka Mungu atasaidia!" Ilikuwa ni saa kumi na moja za alfajiri tukiwa tunaagana na kaka, alinisindikiza mpaka kituo cha mabasi kule kange, nilipopanda ndani ya basi nae akaondoka huku akiwa ananipungia mkono wa kwaheri. Safari ilianza dereva akaliondoa gari kwa fujo, tairi zikaishika barabara vyema ikawa ni zaidi ya vunta n'kuvute. Kila abira alikuwa ametulia, wengine walikuwa wakibofya simu zao na kuachia tabasamu. Bila kusahau wale wa kutapika safarini walikuwa wamezikunja sura zao wakijitahidi kulamba ndimu. Mimi pia nilikuwa nikipitisha macho na kusoma maoni ya wafuatiliaji wa simulizi zangu huko fesibuku, lengo niweze kusogeza masaa niukwepe uchovu wa safari ila ghafla usingizi ulinichota nikasinzia.

Niliamshwa na mlio wa simu ikiita, kuishika tu ikakata, "Nani tena huyu anabipu!" nilijisemea nikiwa nimeuvuta mdomo kwa hasira, nilikuwa naota niko nchi za mbali huko. Kutazama nakuta ni namba ya Pili, mimi mwenyewe sikuwa na salio la kupiga simu, wakati nikiwa nawaza nikope nikaona ujumbe mfupi wa maandishi ukiingia katika simu yangu, naam! Ulitoka kwa pili. Kabla sijaufungua nilinyoosha miguu yangu sababu niliikunja kwa muda mref, nikachukua kitambaa na kujifuta jasho, kisha nikaanza kusoma ujumbe huo.

"Kaka Lovi pole na uchovu wa safari, nimeona nikujuze mapema, nikikwambia muda wowote kwamba mama kaipa dunia kisogo usishangae. Mpaka nilivyochukua jukumu la kukuandikia ujumbe huu, yaani mama haongei, kila anachokula anatapika. Nimechoka kuanzia mwili mpaka roho, hata nikilia machozi hayatoki tena, sauti imenikauka kakaangu, nitahabika na dunia hii mimi!" Nilipomaliza kusoma nilizivuta pumzi kwa fujo kisha nikazitoa nje taratibu huku nikichungulia dirishani, jinsi wakinamama walivyosimama pembezoni mwa barabara wakiwa wameinua bidhaa zao juu.

Gari lilikuwa limesimama nikafungua kioo nakumuita binti mdogo aliyekuwa akiuza mahindi ya kuchoma. Nikamuuliza bei akasema ni shilingi mia tatu, nikatoa miatano nikampa, nikaona akihangaika kuomba chenji wenzake, ila walimnyima. Nikamuita nikamwambia abaki na hiyo pesa huku nikitoa shilingi elfu mbili na kumpatia. Sikuwa na hamu na muhindi hata kidogo, ila macho yangu yalivyotua tu kwa huyo binti mdogo alivaa shati jeupe lililotapakaa madoa ya uchafu na viraka kila kona. Midomo yake ilikaukiana kwa dhiki. Nywele zilimfumuka ovyo alijaribu kuzifunga kwa kitambaa chakavu. Hiyo sketi yake ilinihuzunisha sana ilichanika pembeni mpaka nguo ya ndani iliweza kuonekana japo alijitahidi kufunga na pini iliyojawa kutu huenda aliikota.

Miguu yake iliyopauka sijui mara ya mwisho alipaka mafuta lini! Masikini binti wa watu huyo hakuwa na viatu wala kandambili unyayo wake ulikuwa ukipekua chini, kuchomwa na miiba na chupa vilikuwa ni kawaida kwake, alikuwa akichechemea, kisigino cha mguu wa kushoto hakutaka kiguse chini, hivyo alikanyagia vidole vya mbele. Nilimuonea imani sana, nikatamani ningepata hata dakika tano niijue historia ya maisha yake ila dereva aliondoa gari na safari ikaendelea. Nilitikisa kichwa kwa mshangao huku nikijisemea mwenyewe ka chizi, kwamba Afrika bado tunasafari ndefu ya kujikwamua katika umasikini, ila kwa viongozi wanaojali matumbo yao tutaendelea kuuishi umasikini mpaka mwisho wa dunia.

Kiukweli nilizama katika tafakari nzito na ya kuumiza, ndipo nikajikuta nimepata wazo la kuandika simulizi itakayoitwa, "KWAHERI AFRIKA" Nikakumbuka kuna ujumbe kutoka kwa Pili bado sijaujibu, nikausoma tena upya, "Kaka Lovi pole na uchovu wa safari, nimeona nikujuze mapema, nikikwambia muda wowote kwamba mama kaipa dunia kisogo usishangae. Mpaka nilivyochukua jukumu la kukuandikia ujumbe huu, yaani mama haongei, kila anachokula anatapika. Nimechoka kuanzia mwili mpaka roho, hata nikilia machozi hayatoki tena, sauti imenikauka kakaangu, nitahabika na dunia hii mimi!" Niliguna kidogo baada ya kuusoma tena ujumbe huo kwa mara ya pili, "Nimjibu kitu gani pili! Maana yote nilimshamueleza!" Nilijihoji mwenyewe na kujipatia majibu mepesi ambayo yasingelimfaa pili katika kipindi kigumu anachokumbana nacho katika maisha yake.

Nikaingia katika uwanja wa meseji na kuanza kumjibu pili. "Pole sana rafiki yangu pili, neno langu litabaki kuwa lile lile katika maisha yako. Mateso yakizidi tambua faraja u mlangoni, si wakati wa kukata tamaa angali ukiwa hai. Ukishindwa kutembea jaribu kutambaa lakini kamwe usithubutu kusimama huwezi fika pale unapotamani. Zidisha dua kwa Mwenyezi Mungu, mshirikishe maumivu yako yeye ni mwenye huruma, atakuvusha katika bonde ilo la uvuli wa mauti." Nilivyomaliza kuandika nikautuma ujumbe huo. Dakika zilizidi kuyoyoma pasi kupokea majibu kutoka kwa pili, nikajua atakuwa amebanwa na majukumu ya kumuhudumia mgonjwa, nikaiweka simu yangu pembeni usingizi ukanichukua tena.

"Pata maji baridi, biskuti za maziwa, soda za kopo, wahi zimebaki chache, vipi kaka hapo nikupe nini? Kuna karanga mbichi hapa!" Kelele hizo zilifanya niamke kuchungulia dirishani naona tumeingia kituo cha mabasi musoma kilichopo maeneo ya bweri. Nikachukua mizigo yangu, kuangalia simu siioni nikaangaza huku na kule, nikainama mpaka chini ya siti, nikaambulia kuona maganda ya pipi tu!. Mwili ulipigwa na ubaridi ghafla nikawa kama mjinga, nikamfata konda na kumueleza tukasaidiana kutafuta lakini wapi. "Hiyo ndio imekwenda hivyo!" Kauli hiyo kutoka kwa konda ilinichefua sana, taratibu nikashuka zangu ndani ya ilo basi, nikaenda zinapopaki bajaji nikapanda na kuelekea mjini.

Dakika kama 15 nilifika nyumbani wakanipokea kwa furaha, wakadai wamenipigia simu ikawa inaita tu, mpaka pale walipojaribu kupiga tena wakaambiwa haipatikani. Nikapewa simu ndogo nitumie kwa muda, nikaomba waniazime na laini, mimi sikuwa na namba ya kitambulisho cha taifa kwa wakati huo. Nikawaza nitaipata wapi namba ya pili, nilikoswa majibu. Ni mwaka mzima sasa ulipita bila ya mimi kuwa na smatfoni, nilimuwazia sana pili, mawazo yangu yakaegemea upande ule kwamba atakuwa tayari ameisha jinyonga.

_ITAENDELEA
_______________________________'_____________
Ni mwaka mmoja sasa umepita bila ya mimi kuwasiliana na Pili, maswali ni mengi sana je pili bado u hai au laa.!



"PUNGUZO LA BEI."

Lipia 3000/= nikutumie simulizi ya YASINTA WANILIZA, kwa njia ya sauti. Nione whatsap kwa namba hizi 0757 238 304, nikuonjeshe hata vipande viwili.

OFA... OFA... OFA ....OFA
Usikose vitabu vyangu ( nakala laini ) unatumiwa kwa njia ya email au whatsap Navyo ni:- ________________====_________
Narudi Songea... 5,000/= tu!
Yolanda.....4,000/= tu!
Malkia wa kuzimu... 4,000/= tu!
Hadithi ya Suzi..... 2,500/=
Usilie Rehema.... 5,000/= tu!
________________====_________

KAMA UNAHITAJI KUANDIKIWA KITABU CHA HISTORIA YA MAISHA YAKO UNAKARIBISHWA...

NAPATIKANA TANGA MJINI,....
0622 738 310.
0713 417 189.
( 0757 238 304, whatsap )
LOVI PIUS KIJOGOO.
 
EMMY........01
Lovi Pius kijogoo
0757 238 304.



Miale ya jua ilikuwa ni mikali, wenye kujipepea kwa kutumia viganja vyao walifanya hivyo. Jasho zikawachuruzika kila kona ya miili yao. Wapo waliosonya na kugomba kimoyomoyo sababu ya michirizi ya jasho iliyochafua nguo zao. Ndivyo hali iliyokuwepo mitaa hiyo ya sahare kwa baba ubaya Tanga mjini.
Kwa mbali alionekana kijana mmoja mrefu, mweusi wastani, umbo lake ni jembamba. Nywele aliziachia zilikuwa nyingi, unaweza sema anazikuza aweze kusokota dredi, mmh! maana vijana wa sasa wanatengeneza kitu waweze kupata warembo. Ukiachilia mbali urefu wake, alikuwa amevalia jinzi ya bluu, na shati jeupe. Katika mkono wake wa kuume alishika kibegi cheusi. Wengi waliomtazama walifikiri kwamba ni mwana sheria. La asha! Jambo usilolijua ni sawa na usiku wa kiza.
Jicho lake likatua kwa binti mfupi wa kimo. Nywele zilimwagika mgongoni, sura yake ilijichonga vyema kabisa. Akitembea ni kama ana udugu na ardhi kila hatua aliinua unyayo kwa kunyata. Weupe wake ni wa asili hajatumia nguvu na makemikali kama wale mabinti wa kileo. Ukimtazama usoni, kafunikwa na taswira ya aibu, sekunde mbili nyingi anakiinamisha kichwa chake chini akiachia tabasamu dogo ka kitoto kichanga. Peter akaingia mzima mzima.

"Dada samahani!"
"Nina haraka sana!!"
"Naomba hata dakika moja tu!"
Alifyatuka kwa kasi, akielekea aliposimama binti huyo. Hofu na jasho vikimsindikiza kadri alivyozidi kuzipiga hatua.
"Naitwa Peter!"
"Unanipotezea muda, unajitambulisha upo mkutanoni hapa!"
Alibwatuka kwa sauti, boda waliokuwa wamepaki hapo waligeuza shingo zao, huku wengine wakiangua vicheko.
"Ok! mimi nilitamani sana nipate muda,"
"Kumbe! sasa hivi ni saa tano na nusu za asubuhi"

Alidakia binti huyo kabla hata Peter hajafika kikomo kwa kile alichokizungumza.
"Hapana, namaana kwamba nipate muda wa kuongea nawe zaidi!"
"Nyooooo!!"
Alisonya na uso akiukunja kama kalamba ndimu. Lakini Peter hakujali, akaendelea na kile alichokusudia.

"Basi dada nisaidie namba ya simu!"
"Hujui kama mimi mke wa mtu?"
"Nipe, amini sitokusumbua"
"Ole wako, ok chukua!"
"Umesahau kuniambia jina"
"Naitwa Emmy"

Baada ya kutamka jina lake alimuacha Peter akiwa ameduwaa. Hakuamini kama angeweza kuzipata namba za Emmy. Hakuna mkate mgumu mbele ya chai, ni msemo uliponyoka kinywani mwa Peter na kumfanya atabasamu.
"Lakini! japo kanipa namba, sio kwamba karidhia kila kitu, ok any way ngoja tuone"

Aliamua kuendelea na safari, ni katika harakati zake za kukusanya madeni yake. Ujasiriamali ni kitu kilichomtoa kigoma na kuangukia Tanga maeneo ya barabara za namba. Kikubwa alikuwa akikopesha vitu mbalimbali kama vile, vyombo, viatu, hereni na redio ndogo. Kazi ikamfanya jua liwe lake na hata mvua pia. Mwanaume atakula kwa jasho, basi kauli hiyo ilienda sambamba na maisha ya Peter.

Jua liliondoka zake kwa manung'uniko kama limelazimishwa, uwanja ukabaki wazi. Mwezi ukajitosa dimbani na kusakata lumba lililotoa mwanga mzuri, uliokitupilia mbali kiza. Masaa yalizidi kuyoyoma ilikuwa ni saa mbili kamili za usiku.
Peter akiwa amejilaza kitandani, alitazama chini, akasonya.
"Yaani hawa mafundi wa barabara ya 15, walichonifanyia, sasa ni kitanda gani hiki. Kinaliwa na wadudu kila baada ya dakika tano ninafuta vumbi chini ya kitanda, kama nimelalia mashine ya kusaga na kukoboa."

Alicheka kidogo huku akitazama kwa umakini pale panapoliwa, akashuhudia vitundu vingi na vidogovidogo.

"Ila mimi nae nimezidi kulalamika, kitanda cha laki na nusu nilitaka kiweje sasa, shiiiit. Acha nitafute pesa kuna vitanda bana, ukilala unahisi uko paradiso lakini hiki changu ni chitanda, na si kitanda, kinapiga kelele kila ukijigeuza, kwa uzito gani nilonao mpaka kilalamike kiasi iko ."
Kicheko kilimtoka tena, baada ya kuona kwamba kile kitanda kinaendana na pesa yake.

"Huu ni muda muafaka sasa wa kumtafuta yule binti niliyekutana nae sahare"
Alitulia kidogo, kuna kitu kilikatiza akilini mwake wakati akiendelea kupekua jina la binti huyo katika simu yake.

"Lakini nakumbuka aliniambia ni mke wa mtu, muda huu hautakuwa hatari kwangu kweli?"
Alijiuliza bila ya kupata majibu.

"Mimi ni mwanaume ngoja nijaribu, liwalo na liwe, alaaaaaa! potelea pwete"
Alijikaza, akiwa anaiweke simu sikioni akingoja ipokelewe.

"My God! inaita, mambo si hayo"
Alikuwa ka chizi akijikuna kichwani, ila uwoga ulimvaa kwa kiasi kikubwa. Alipiga zaidi ya mara tano simu haipokelewi, tumaini lake taratibu likaanza kufifia kama mtungi ulioisha gesi.

"Huyu manzi vipi, mbona hapokei simu!"
Alifoka mwenyewe, kisha akapiga ngumi pembezoni wa kitanda chake.

"Sasa napiga tena kwa mara ya mwisho"
Aliweka raudi spika, hakutaka kuisogeza simu sikioni akijua haipokelewi.
"Waoooo! kapokea" aliinua mkono mmoja juu na kuanza kushangilia kimya kimya.
"Eeh! hallo.. hallo.. mbona huongei, ni mimi peter"

Hakupata jibu lolote kutoka upande wa pili, zaidi ya kusikia sauti za kike zikicheka kwa dharau.
"Inamaana kapokea simu pasipo kujua au kakusudia kukaa kimya"
Peter akaiweka tena simu sikioni kwake ikawa inaita bila kupokelewa, akakata simu na kuiweka pembeni.

Katika chumba kidogo, kilichopambwa kwa mikoba na viatu vya kila aina, ukutani walining'iniza nguo zao za ndani. Meza ilijaa manukato na chanuo kubwa na dogo. Redio na runinga kubwa kiasi viliongeza umaridadi wa chumba hicho kilichomilikiwa na Emmy katika mtaa wa Sahare. Usiku huo alikuwa ametembelewa na rafiki yake aliyeitwa Mage, walipiga umbea unaofaa na usiofaa, vicheko vikawa ni sehemu ya mazungimzo yao.
"Mmh! Shoga angu, mbona wamfanyia hivyo huyo apigaye simu! ni nani eti?"
Aliuza Mage wakati huo akiwa anaendelea kuibofya simu yake.

"Ni mpuuzi mmoja tu, nimekutana nae barabarani, sasa kaniganda kama ruba"
"Wachezea bahati wewe, kumbuka haiji mara mbili, shauri yako!"
"Hata kama shoga angu, kila anisimamishaye njiani nimkubalie, mbona nitatembea na Tanga nzima"
Walijikuta wote wakiangua kicheko baada ya jibu ilo kutoka kwa Emmy.

"Kama hana mbambamba au ushe ushe, we ruka nae tu shogale!"
"Unaijua sahare vizuri wewe, hasa hapa ba ubaya?" Emmy aliuza.
"Unakwama wapi yaani, bado upo dunia ya kufanya mambo kwa kuhofia watu watasema nini? pole sana shoga angu"
"Simaanishi hivyo!,"
"Wamaanisha nini ?" alidakia Mage.
"We nawe kwa umbea, tulia nikupe michapo. kuna wanaume hapa sahare ni waongo, kushinda hata wanawake. Wanaweza nitangaza mpaka kwanjeka wakajua. Ni hizo tu tarumbeta gharama zipo juu, ningekuwa nishaenda wasuta nazo. Mara ooh! Emmy anadanga, kila mtaa ana bwana nyooo...!! inahuuuu!, wanachonga ka walishaninunulia hata kipande cha sabuni." Hakuna aliyevumilia na kuzuia kicheko chake, waliyaachia meno nje wakicheka na kugonga mikono yao kwa pamoja. Mage aliaga na kuondoka zake.

Usiku ulizidi kuwa mchungu kwa Peter, kila alipojigeuza vicheko kutoka kwa wadada wale vilizidi kujirudia masikioni mwake. Ni adhabu inayopenya na kuacha maumivu mtimani.

"Dunia ikiamua kukuelemea inafanya hivyo kweli, sasa hadi usingizi pia unaniletea jeuri, nashindwa kuupata. Na kumeshakuchwa sasa!"
Peter alilalamika akiwa analitupilia mbali lile shuka lake jekundu, ikiwa ni zawadi kutoka kwa Babu yake huko Kigoma.

********************* ITAENDELEA **********
emmy%20promo_101248.jpg
 
EMMY.....02
Lovi Pius Kijogoo
0757 238 304.





SEHEMU YA PILI.

ILIPOISHIA.........


Usiku ulizidi kuwa mchungu kwa Peter, kila alipojigeuza vicheko kutoka kwa wadada wale vilizidi kujirudia masikioni mwake. Ni adhabu inayopenya na kuacha maumivu mtimani.
"Dunia ikiamua kukuelemea inafanya hivyo kweli, sasa hadi usingizi pia unaniletea jeuri, nashindwa kuupata. Na kumeshakuchwa sasa!"
Peter alilalamika akiwa analitupilia mbali lile shuka lake jekundu, ikiwa ni zawadi kutoka kwa Babu yake huko Kigoma.


ENDELEA NAYO........

"Acha nijiandae nikatafute pesa, hiyo ni sifa pekee ya kuitwa mwanaume, iliyosalia hapa duniani"
Alijitapa Peter, akachungulia dirishani na kutabasamu mwenyewe.

"Nina hamu na supu, ila pakuipata sasa!"
Alijiuliza Emmy, wakati huo akiendelea kutazama majina katika simu yake.

"Sio kwamba sijui wanapouza, la asha! tatizo mane yaani pesa"
Awamu hii alikuwa ameifikia namba ya peter kumbe aliisevu, akabofya kitufe cha kupiga simu, Kisha akaweka raudi spika.

"Huyu boya atashangaa sana kuona leo nimempigia, wajinga ndio waliwao, tulia uone"
Hatimaye simu ilipokelewa baada ya kuita kwa muda mrefu.

"Hello! Darling, Emmy hapa naongea"

"Eeeh, mmh! ndio, na na na nakupa.. ta"

Peter kigugumizi cha ghafla kilimva, huenda hakutegemea kama ipo siku angepigiwa simu na binti huyo. Lakini kilichompagawisha sana ni kuitwa Darling.

"Natamani supu ya mbuzi kipenzi changu!"
"Kwani inauzwa wapi?"
"Waooh, hata si mbali, hapo tu Amazon"
"Sawa tutakutana hapo"
Peter, moyo ulijawa na furaha, akaona Mungu kajibu maombi yake. Alikuwa hajafika mbali.

Alirudi mpaka pale anapoishi akachukua shilingi elfu kumi tu.

Hizo pedeli za baiskeli zilivyonyongwa, ni kama inatumia umeme. Shati lilipeperuka kwa nyuma, upepo ukijaa ndani yake, ni kama kitambaa cha mashineni. Jasho likiufunika uso, kifua kikawa kinapanda na kushuka, akihema juu juu.

"Karibu, tukuhudumie nini kaka?"

"Aaah! Aah! sawa ntakwambia!" alijibu Peter, akiwa anakodoa macho kila kona, akimtafuta Emmy. Ghafla alistushwa na mkono uliomgusa katika bega lake.

"Nimechelewa eeh"

"Hata hujachelewa, isingekuwa baiskeli nami ningekuwa sijafika"

"Baby! nimekuja na rafiki yangu anaitwa Mage" aliongea maneno hayo Emmy, na kuachia tabasamu la kitapeli kwa waliosoma nchini Cuba wataelewa hapa.

"Ooh! sawa haina neno!" Peter alijibu lakini neno baby lilizidi kusumbua masikio yake, lilikuwa likijirudia. Alisali kimoyomoyo akijua kazi imemalIzika.

"We msichana mbona umeleta supu mbili tu!" aliuliza Emmy.

"Nafata maelekezo ya huyo mkaka!" alisisitiza mhudumu.

"Nyie kunyweni mimi niko vizuri tumboni!"
Alitabasamu Peter baada ya kutoa kauli hiyo.

Alitamani sana supu, lakini pesa ilikuwa haitoshi. Akajikaza kisabuni, mambo yasiharibike.

"Huyo mtoto leo simuachi, amekula vya mbwa na hana mbio!"
Bado mawazo ya Peter yalikuwa kwa Emmy, alimtazama kila alipokuwa akipeleka kipande cha nyama mdomoni. Akatamani wangelikuwa wawili chumbani basi angemlisha kwa kutumia kinywa chake.

"Asante sana mpenzi, sisi tunaondoka!"
"Mbona mapema sana, nilitaka tuongee hata mawili matatu"

"Ok! ntaku call kwenye simu"

Emmy alisimama, akamshika mwenziye mkono wakaondoka zao. Peter akabaki anawasindikiza kwa macho. Nafsi inatamani kuwafuata, ila mwili unakuwa mzito. Akatikisa kukubali kwamba kafeli akasimama na kuiendea baiskeli yake kinyonge sana. Akaingia mtaani kuendelea na majukumu yake

"Simu inaita au ni yule binti ananipigia nini? Aah! kumbe si yeye. Sasa huyu jamaa kunidai shilingi elfu tano tu, anapiga simu kila wakati ebu atulie kwanza"

Aliongea pekeake Peter, alijua ni simu kutoka kwa Emmy, la asha! ilikuwa tofauti. Akairudisha mfukoni kwa hasira huku akisonya.

"Shoga tushashiba supu, tuunge zetu bando, tukatazame umbea instagramu" Emmy huyo akijitapa.

"Umeona eeh, wajinga ndo waliwao" Mage alidakia, wakacheka kwa sauti kuuubwaaa.

"Emmy, simu yako inaita!'

"Niangalizie ni nani anapiga!"

"Ni namba ngeni"

"Ok niletee hapa"

"Hallo, mambo mpenzi?" ilikuwa ni sauti kutoka upande wa pili. Emmy akasita kuitikia.

"Kwani wewe nani, maana namba ngeni?" Emmy aliuliza.

"Ni mimi John mpenzi wako"

"Malaya mkubwa wewe!"

Aligomba Emmy, akakata simu na kuirusha kitandani. Baada ya dakika tano simu iliita tena, Emmy hakupokea.

"Mbona umemjibu kwa ukali na kumkatia simu ni nani huyo" Mage ilibidi aulize.

"Ni stori ndefu shogaangu ila ntakusimulia kwa ufupi tu"

Emmy alivuta pumzi na kuitoa nje taratibu. Alionekana wazi amekumbushwa yaliyomuumiza katika historia ya maisha yake.

"Huyo John, nilikuwa natoka nae, lakini anakupostia demu wake status. Hakuwa hata na chembe ya hofu mbwa huyo."

Emmy alisita kidogo kuendelea, ni uchungu ulianza kumnyemelea. Akajikaza tu ili aendelee kuzungumza.

"Hapo mwanzo mapenzi yalikuwa matamu sana, yaani simu muda wote.. tena ukilala bila kuongea nae kwenye simu, anakununia. Acha tu rafiki yangu Mage. Asubuhi ukiamka unafanya kazi ya kubembeleza maisha yanaendelea"

"Ulipitia magumu shoga angu" Mage alikatisha mazungumzo.

"Mage sijamaliza mpenzi, nisikilize!"

"Nakumbuka ilikuwa ni siku ya Ijumaa, saa kumi jioni, John akanikaribisha kwao hapo tu barabara ya 7. Nikaenda nilikuta wanamaisha magumu, ila sikuangalia ilo. Mapenzi upofu tena kuna muda nilikuwa nampa pesa ya kula kenge yule...

**************** ITAENDELEA ***********************
emmy%20promo.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom