Simulizi: Malkia wa kuzimu-01

Simulizi: Malkia wa kuzimu-01

MALKIA WA KUZIMU..... 17
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0622 738 310.
0713 417 189.
TANGA.

Janeth hakushtuka wala kujali kwa kile kilichotokea bali aliendelea na shughuli zake, wakati huo Desmund akiwa amekata tamaa pale Kitandani akisubiri roho yake kutengana na mwili muda wowote ule.

Mama Desmund alikuwa katika hali ya upweke ndani ya jumba kubwa lililotazamana na Barabara. Aliamua achukue kitabu cha picha akaanza kufunua akakutana na picha yake ya ndoa, alitikisa kichwa, akaitazama pete yake ya ndoa katika picha ile, ambayo pete hiyo akumbuki ilipotea katika mazingira gani.

Alipofunua tu ukarasa uliofuata mwili wake ulianza kuwa wa baridi. Aliogopa kutazama picha iliyokuwa mbele yake. Akiwa bado anatazama picha hiyo alisikia mdada mpya wa kazi akimuita kwamba chakula tayari, Mama Desmund alifata chakula kile kisha akarejea kuketi alipokuwa mwanzo.

Aliporudi picha ile ilikuwa bado ikimkodolea macho kwa huruma.Ilikuwa picha ya mtoto wake aliyeitwa Deus alikuwa na tabia ya kuwapa watoto wake majina ya ukoo na ubatizo pia.

Mtoto huyu alifariki miezi kadhaa iliyopita, kifo chake kilikuwa ni cha ghafla sana, hakupata hata muda wa kuzungumza na Mamake kabla ya kufikwa na umauti, alizima ghafla na kuiacha familia yake ikilia kilio kikuu,kilio kisicho na mwisho.

Mama Desmund hakutaka kuitazama tena ile picha ilimsikitisha sana. Alifunika upesi buku lile la picha. Akaamua achukue kitabu kimoja kilichoandikwa na mwanasaikolojia wa Nchini Marekani "Wiley and sons 1960" akafunua ukurasa wa mia moja tisini na moja na kuanza kusoma.

"Sikumbuki mama yangu alinibusu mara ya mwisho lini. Yawezekana jambo hilo lilifanyika nilipokuwa mtoto mchanga, kwani hakika alinibusu mara nyingi nilipokuwa ninakua. Wakati sikumbuki busu lake la kwanza, nakumbuka busu lake la mwisho."

"Miaka inapita kwa kasi, na kila uhusiano wa binadamu huleta misongo na kero. Hili si jambo la kutisha au kufedhehesha bali ni la kawaida. Lakini tukiwa na kanuni ya heshima pekee ya utii mioyoni mwetu, upendo utatawala. Kisha, kadiri misongo inavyotutisha, pengine kutusababishia maumivu na hata uchungu, tungekumbusha lile busu la mwisho maana hakika litakuja.Unataka ukumbuke nini unapowaaga wazazi wako mara ya mwisho?"

"Rafiki yangu alinisimulia kwamba baba yake alipozeeka, si wakati wote akili yake ilikuwa ikifanya kazi vyema. Hata hivyo, siku yake ya kuzaliwa ilipokaribia, rafiki yangu aliamua kumpigia simu. Alimwambia, "Heri ya siku ya kuzaliwa ( Happy Birthday, Day )" "na Mungu akubariki."

"Siku hiyo akili ya Baba ilimrudia kwani alijibu mara, "Hapana, mwanangu. Mibaraka ni yako. Mungu akubariki kwasababu siku zote umekuwa ukiniheshimu." Miezi miwili baadaye rafiki yangu alimzika baba yake. Ilikuwa faraja ya kiasi gani kwake, kuyakumbuka maneno ya marehemu baba yake!"

"Nimehudhuria mazishi machache ya kusikitisha, lakini kamwe sijashuhudia machungu zaidi na kilio kuliko wakati majuto yalipofanya huzuni ya kutengana kuwa chungu zaidi."

"Tafakari suala hili wakati bado unayo fursa, wakati bado unaweza kufanya kitu au kusema kitu kinachoweza kuleta tofauti. Tafakari busu la mwisho kwasababu litakuja. Waheshimu baba yako na mama yako na siku zako duniani hazitakuwa nyingi tu ila zitakuwa za kuridhisha zaidi zilizojaa amani, furaha na ufanisi." ( New York: Wiley and Sons 1960 ), p. 191.

Mama Desmund alizivuta pumzi zake kwa fujo kisha akazitoa nje taratibu sana.
"Nilitamani mwanangu apate kitabu hiki akisome hasa ukurusa huu kwamba " Waheshimu baba yako na mama yako na siku zako duniani hazitakuwa nyingi tu ila zitakuwa za kuridhisha zaidi zilizojaa amani, furaha na ufanisi."

"Ni kweli nimekubali kuwa mbali na mwanangu! Damu yangu, hapana, nafsi yangu inaniuma, Desmund ni mwanangu, alinyonya kifuani kwangu, leo niwe adui yake, mwanangu ananiuma sana, kama yeye haoni umuhimu wangu ila mimi bado nahitaji kuwa karibu na mwanangu" alizungumza mama Desmund huku akiwa anatazama jarada la kile kitabu, mkono wa kushoto akiwa ameuweka shavuni, na kujitahidi kulizuia chozi lisimdondoke tena.

"Furaha yangu imekanwa na ulimwengu, moyo wangu umelainika sababu ya maumivu, siamini kama kumlea Desmund ilikuwa ni sawa na muda kupoteza, nguvu nyingi kutupa. Nimesikia mwanangu anaumwa lazima niende, mimi ndie mama yake, maamuzi yangu sitakuja kuyajutia kamwe, akiamua kuniua ni sawa, ulimwengu umenichosha." Mama Desmund alizidi kunong'ona mwenyewe kwa sauti ya chini yenye kuongozwa na machungu, machozi na uzito wa moyo.

ITAENDELEA....
 
NARUDI SONGEA
MTUNZI ; LOVI KIJOGOO.
0622 738 310.
0713 417 189.

SURA
YA
1






BAADA YA MIAKA MITANO ( 5 ) KUPITA

JIJINI DAR - ES - SALAAM


Ilikuwa ni majira ya saa kumi na moja kamili za alfajiri, kiubaridi kilikuwa kikipuliza kwa mbali sana huku wingu zito likiwa limetanda jijini Dar - es - salaam, kuashiria kwamba ni muda wowote ule mvua inaweza kutimiza wajibu wake!.

Kwa mbali alionekana binti mmoja aliyefahamika kwa jina la Eva Mapunda! Akiwa katika Kituo cha mabasi yaendayo mikoani pale ubongo Jijini Dar - es - salaam! Alikuwa amejifunika kipande kimoja tu cha kanga! Hivyo ubaridi ulifanikiwa kupenya vyema katika mwili wake. Na kumfanya aikusanye mikono yake kwa pamoja, akitegemea anaweza kupata joto walau kidogo.

Alionekana macho yake yakiwa yamevimba, yakimaanisha kwamba amelia muda mrefu. Pia macho yalikuwa ni mekundu sana!. alikuwa akitetemeka mwili mzima.

Na michirizi ya machozi ikiwa bado inaonekana katika mashavu yake!, kiukweli kama una moyo mwepesi usingeweza kumtazama mara mbili.

Ni mtu ambaye moyo wake umebeba siri nzito! yenye maumivu ndani yake!, ndio maana siri hiyo inauchoma moyo wake na kuyaruhusu machozi yachuruzike angalau moyo upumzike.

Eva alikuwa amebeba begi dogo, ambalo alikuwa ameweka nguo zake, ila begi ilo lilikuwa limejaa vumbi liliupoteza mvuto wake.

Watu walipomuona walitambua kwamba labda ni mwendawazimu!. "Jambo usilolijuwa ni sawa na usiku wa giza!" "moyo wa mtu kichaka" maumivu pamoja na mateso aliyopitia yalikuwa ndani ya moyo wake!, ni moyo pekee tu ndio hujua uchungu wa nafsi yake.

Maumivu yanapokuwa makali, moyo ukichoka kuyavumilia, ndipo uruhusu pumzi ile ya uhai iondoke zake na kurejea kwa Muumba. Ndipo mtu anapopewa jina lisilozoeleka wala kuvumilika yaani marehemu.

Afya ya Eva ilikuwa imedhoofu sana!, rangi yake ilipoteza mvuto. Tabasamu lake lilikuwa ni hafifu!. Ngozi yake ilibadilika rangi na kuonekana kama njano vile, kiukweli alikuwa katika mapito ambayo yeye mwenyewe alishindwa kuelewa, kwamba ni kwanini yote hayo yametokea kwake.

Kuanzia sura, nafsi, na hata moyo vilionesha wazi kabisa kwamba Eva binti wa mzee Mapunda, alipoteza furaha yake na kupokea huzuni pamoja na simanzi ya milele.

Hatimaye alielekea kwenye ofisi ya mabasi ambayo ufanya safari zake kutoka Dar- es - salaam kwenda mpaka Songea, ila kabla hajaingia ndani ya ofisi ile alishika kipande chake Kile cha kanga kisha akayafuta machozi yake.

Hakutaka watu wajue kwamba alikuwa akilia!, alitoa pesa ambayo alikuwa ameweka kama akiba. Basi akakata tiketi kisha akapanda ndani ya gari kwa ajili ya safari!.

Saa kumi na mbili na robo za alfajiri dereva aliondoa Gari kituo cha mabasi ubungo safari ikawa imeanza, kila abiria alianza kumuomba Mungu wake ili awasaidie waweze kufika salama katika safari yao.

Kwasababu njia ya kutoka Dar - es - salaam kwenda Songea imekuwa na ajari nyingi sana!. Ambazo mpaka leo zimeacha simanzi tele kwa baadhi ya familia, zilizowapoteza wapendwa wao wa karibu, waliotangulia katika makao ya milele. Lakini kwa nyakati hizi barabara zimeboreshwa na kuwa bora zaidi.

Safari ikiwa inaendelea Eva machozi yalikuwa yakimbubujika muda wote. Amani ya moyo wake ilizidi kutoweka. Na kuelekea katika msitu mnene wenye wanyama wakali, mpaka akapoteza tumaini la kuendelea kuwa hai katika Dunia hii iliyoamua kumuadhibu vikali.

Aliamua ainamishe kichwa chake chini, hakutaka kutazamana na mtu yeyote yule kwa wakati ule, akayafumba macho yake..

"Jamani Eva mimi mtoto wa mzee Mapunda! Jinsi nilivyokuwa mrembo kabla sijaolewa na mwanaume huyu katili!, tazama leo ninavyoonekana nimepoteza amani ya moyo!"

"Nimepoteza tumaini langu pamoja na ndoto zangu za kuwa mama bora wa familia. Najuta sana, kwa nyakati hizi nilizozama katika Dimbwi la maumivu, kila nikitafakari nakoswa jibu lililo sahihi kwangu."

"Mbona wanawake wengine wamekuwa na furaha muda wote! Ila kwangu jasho la maumivu na manyanyaso ndio lanidondoka kila siku."

"Jamani ebu nitazameni kwa jicho la huruma, mwili pamoja na sura yangu vimenisaliti na kunipa muonekano usioendana na umri wangu kabisa!. Kweli ndio mimi Eva Mapunda leo ninanukia kifo!. Asante Dunia!, kama uliamua nije katika ulimwengu huu niteseke nasema asante!."

"Nasubiri mwisho univike taji la maumivu, litakalo nisindikiza vyema mpaka kaburini!. Ambako nitafunikwa na udongo mzuri, utakaoweza kuzifukia na ndoto zangu zote nilizokuwa nazo hapa Duniani!. Naona wazi hii ndio safari yangu ya mwisho nikiwa hai, viungo vyangu vimechoka kuvumilia havina budi kwenda kupumzika mbinguni kwa Baba."

NB, simulizi hii inapatika yote kwa njia ya soft copy ( nakala laini ) kwa gharama ya 5000/= namba ya mawasiliano ni 0622 738 310.

Lakini simulizi ya "Malkia wa kuzimu na Ntagambi zitaendelea hapa hapa katika uzihuu mpaka mwisho.
tapatalk_1589302053245.jpg
 
NARUDI SONGEA
MTUNZI ; LOVI KIJOGOO.
0622 738 310.
0713 417 189.

SURA
YA
1






BAADA YA MIAKA MITANO ( 5 ) KUPITA

JIJINI DAR - ES - SALAAM


Ilikuwa ni majira ya saa kumi na moja kamili za alfajiri, kiubaridi kilikuwa kikipuliza kwa mbali sana huku wingu zito likiwa limetanda jijini Dar - es - salaam, kuashiria kwamba ni muda wowote ule mvua inaweza kutimiza wajibu wake!.

Kwa mbali alionekana binti mmoja aliyefahamika kwa jina la Eva Mapunda! Akiwa katika Kituo cha mabasi yaendayo mikoani pale ubongo Jijini Dar - es - salaam! Alikuwa amejifunika kipande kimoja tu cha kanga! Hivyo ubaridi ulifanikiwa kupenya vyema katika mwili wake. Na kumfanya aikusanye mikono yake kwa pamoja, akitegemea anaweza kupata joto walau kidogo.

Alionekana macho yake yakiwa yamevimba, yakimaanisha kwamba amelia muda mrefu. Pia macho yalikuwa ni mekundu sana!. alikuwa akitetemeka mwili mzima.

Na michirizi ya machozi ikiwa bado inaonekana katika mashavu yake!, kiukweli kama una moyo mwepesi usingeweza kumtazama mara mbili.

Ni mtu ambaye moyo wake umebeba siri nzito! yenye maumivu ndani yake!, ndio maana siri hiyo inauchoma moyo wake na kuyaruhusu machozi yachuruzike angalau moyo upumzike.

Eva alikuwa amebeba begi dogo, ambalo alikuwa ameweka nguo zake, ila begi ilo lilikuwa limejaa vumbi liliupoteza mvuto wake.

Watu walipomuona walitambua kwamba labda ni mwendawazimu!. "Jambo usilolijuwa ni sawa na usiku wa giza!" "moyo wa mtu kichaka" maumivu pamoja na mateso aliyopitia yalikuwa ndani ya moyo wake!, ni moyo pekee tu ndio hujua uchungu wa nafsi yake.

Maumivu yanapokuwa makali, moyo ukichoka kuyavumilia, ndipo uruhusu pumzi ile ya uhai iondoke zake na kurejea kwa Muumba. Ndipo mtu anapopewa jina lisilozoeleka wala kuvumilika yaani marehemu.

Afya ya Eva ilikuwa imedhoofu sana!, rangi yake ilipoteza mvuto. Tabasamu lake lilikuwa ni hafifu!. Ngozi yake ilibadilika rangi na kuonekana kama njano vile, kiukweli alikuwa katika mapito ambayo yeye mwenyewe alishindwa kuelewa, kwamba ni kwanini yote hayo yametokea kwake.

Kuanzia sura, nafsi, na hata moyo vilionesha wazi kabisa kwamba Eva binti wa mzee Mapunda, alipoteza furaha yake na kupokea huzuni pamoja na simanzi ya milele.

Hatimaye alielekea kwenye ofisi ya mabasi ambayo ufanya safari zake kutoka Dar- es - salaam kwenda mpaka Songea, ila kabla hajaingia ndani ya ofisi ile alishika kipande chake Kile cha kanga kisha akayafuta machozi yake.

Hakutaka watu wajue kwamba alikuwa akilia!, alitoa pesa ambayo alikuwa ameweka kama akiba. Basi akakata tiketi kisha akapanda ndani ya gari kwa ajili ya safari!.

Saa kumi na mbili na robo za alfajiri dereva aliondoa Gari kituo cha mabasi ubungo safari ikawa imeanza, kila abiria alianza kumuomba Mungu wake ili awasaidie waweze kufika salama katika safari yao.

Kwasababu njia ya kutoka Dar - es - salaam kwenda Songea imekuwa na ajari nyingi sana!. Ambazo mpaka leo zimeacha simanzi tele kwa baadhi ya familia, zilizowapoteza wapendwa wao wa karibu, waliotangulia katika makao ya milele. Lakini kwa nyakati hizi barabara zimeboreshwa na kuwa bora zaidi.

Safari ikiwa inaendelea Eva machozi yalikuwa yakimbubujika muda wote. Amani ya moyo wake ilizidi kutoweka. Na kuelekea katika msitu mnene wenye wanyama wakali, mpaka akapoteza tumaini la kuendelea kuwa hai katika Dunia hii iliyoamua kumuadhibu vikali.

Aliamua ainamishe kichwa chake chini, hakutaka kutazamana na mtu yeyote yule kwa wakati ule, akayafumba macho yake..

"Jamani Eva mimi mtoto wa mzee Mapunda! Jinsi nilivyokuwa mrembo kabla sijaolewa na mwanaume huyu katili!, tazama leo ninavyoonekana nimepoteza amani ya moyo!"

"Nimepoteza tumaini langu pamoja na ndoto zangu za kuwa mama bora wa familia. Najuta sana, kwa nyakati hizi nilizozama katika Dimbwi la maumivu, kila nikitafakari nakoswa jibu lililo sahihi kwangu."

"Mbona wanawake wengine wamekuwa na furaha muda wote! Ila kwangu jasho la maumivu na manyanyaso ndio lanidondoka kila siku."

"Jamani ebu nitazameni kwa jicho la huruma, mwili pamoja na sura yangu vimenisaliti na kunipa muonekano usioendana na umri wangu kabisa!. Kweli ndio mimi Eva Mapunda leo ninanukia kifo!. Asante Dunia!, kama uliamua nije katika ulimwengu huu niteseke nasema asante!."

"Nasubiri mwisho univike taji la maumivu, litakalo nisindikiza vyema mpaka kaburini!. Ambako nitafunikwa na udongo mzuri, utakaoweza kuzifukia na ndoto zangu zote nilizokuwa nazo hapa Duniani!. Naona wazi hii ndio safari yangu ya mwisho nikiwa hai, viungo vyangu vimechoka kuvumilia havina budi kwenda kupumzika mbinguni kwa Baba."


NB, simulizi hii inapatika yote kwa njia ya soft copy ( nakala laini ) kwa gharama ya 5000/= namba ya mawasiliano ni 0622 738 310.

Lakini simulizi ya "Malkia wa kuzimu na Ntagambi zitaendelea hapa hapa katika uzihuu mpaka mwisho.View attachment 1892470
"Karibuni saana, tuburudike kupitia fasihi andishi."
 
MALKIA WA KUZIMU..... 18
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0713 417 189.
0622 738 310
TANGA.


ILIPOISHIA.......

Ni kweli nimekubali kuwa mbali na mwanangu! Damu yangu, hapana, nafsi yangu inaniuma, Desmund ni mwanangu, alinyonya kifuani kwangu, leo niwe adui yake, mwanangu ananiuma sana, kama yeye haoni umuhimu wangu ila mimi bado nahitaji kuwa karibu na mwanangu" alizungumza mama Desmund huku akiwa anatazama jarada la kile kitabu, mkono wa kushoto akiwa ameuweka shavuni, na kujitahidi kulizuia chozi lisimdondoke tena.
"Furaha yangu imekanwa na ulimwengu, moyo wangu umelainika sababu ya maumivu, siamini kama kumlea Desmund ilikuwa ni sawa na muda kupoteza, nguvu nyingi kutupa. Nimesikia mwanangu anaumwa lazima niende, mimi ndie mama yake, maamuzi yangu sitakuja kuyajutia kamwe, akiamua kuniua ni sawa, ulimwengu umenichosha." Mama Desmund alizidi kunong'ona mwenyewe kwa sauti ya chini yenye kuongozwa na machungu, machozi na uzito wa moyo.




ENDELEA NAYO.....

Hatimaye Manumbu fahamu zilikuwa zimerejea takribani dakika ishirini na tano kupita.

"kulikoni tena hapa, rafiki yangu bado amegoma kuamka"! alinena Manumbu akiwa anayaangaza macho yake huku na kule kana kwamba amechanganyikiwa, Janeth alikuwa jikoni akikaanga nyama ya kuku, chumba kizima kilitapakaa harufu nzuri kutokana na mapishi hayo ya Janeth.

"Mwanamke huyu kapata wapi nguvu na ujasiri wa kukaangiza chakula chenye kunukia kwa wingi wa viungo, angali mumewe akiwa hoi kitandani, kweli haya ni maajabu ya karne" alinong'ona manumbu kwa sauti ya chini kabisa. Kila alipotaka kuaga ili arejee nyumbani kwake hali ya Desmund ilikuwa inabadirika na kuwa mbaya kabisa.

Mapovu yalianza kumtoka mdoni, damu nazo zikawa zinachuruzika taratibu masikioni na mapuani, haja kubwa na ndogo zilikuwa zikitoka bila idhini ya Desmund, alichoka, alichoka alichoka, hakika aliutazamwa ulimwengu kama gereza lenye mateso makali na machungu hata kwa waliokufa tayari.

"Baba nichukue mapema, kwanini unaniacha hai mpaka sasa ili niendelee kuteseka! adhabu uliyonipa inatosha, sio mimi tena bali ni mfu ninayevuta pumzi ya mwisho, ningelijua kama ipo siku mwili na moyo wangu vitateseka hivi nisingelikubali kutoka katika tumbo la mama yangu" ilikuwa ni sauti ya Desmund akizungumza kwa shida, mapovu nayo yakiongeza kasi ya kumtoka kinywani mwake.

Jua nalo lilikuwa likizama kwa kasi ya ajabu, mwanga ukatoweka kwa huzuni na kulipisha giza kwa mwendo wa kunyata ilikuwa ni saa moja kasorobo za usiku.

"Rafiki yangu kwa heri naona giza limeingia sasa, ugua pole, kesho alfajiri nitakuwa hapa" Manumbu alikuwa akiaga, lakini Desmund hakujibu neno lolote lile alikuwa ameyafumba macho na kuyang'ata meno yake, kitendo hicho kiliashiria kwamba ni machungu na maumivu mazito yalikuwa yakipita katika mwili wake.

Baada ya Manumbu kuondoka, Janeth alisogea pale alipolala mumewe akamsogezea mto vizuri katika kichwa chake.
"Vipi nikuletee chakula kipenzi changu?" aliuliza Janeth. Lakini Desmund hakuwa na nguvu za kuzungumza bali alijitahidi kumtazama mkewe huku machozi yakiwa yanameremeta machoni kwake.

Usiku wa manane Janeth aliamshwa na sauti iliyokuwa ikimuita, aliamka akaketi kitandani, mwanga mkali ukatanda chumba kizima, ndani ya mwanga huo akatokea binadamu aliyejawa na mifupa mwili mzima anatoa harufu mbaya, ana macho makubwa na mawili, urefu wake haukuwa na mwisho, alikuwa amebeba maiti ya binadamu katika mgongo wake, kiumbe hicho kilisogea na kuketi karibu na Janeth.

"zimebaki siku tatu" kilizungumza kiumbe hicho kwa sauti nzito na ya kukoroma huku wadudu wadogo wadogo aina ya funza wakitoka ndani ya mdomo wake. Janeth ghafla akabadirika na kufanana na kiumbe hicho.

"Mimi ndiye malkia, huyu nishammaliza" alijibu Janeth. Wakiwa katika muonekano huo walitoa ndimi zao na kuanza kumlamba Desmund karibia kila kona ya mwili wake, kisha wakambana kwa nguvu kifuani.

"Oooh! Oooh! Oooh! Baba wa mbinguni nihurumie mwanao" alilalamika Desmund akijua yuko katika ndoto lakini maumivu aliyasikia. Sauti kutoka kuzimu ilimuamuru Janeth afanye tendo la ndoa na Desmund kwa mara ya mwisho kama ishara ya kuridhia kumtoa kafara.

Sehemu za siri za Desmund hazikuweza kuhimili tendo ilo zilijawa na maumivu mazito, wakati Janeth akijiandaa kufanya kitendo hicho kile kiumbe kingine kilitoweka na kuacha moshi ukitanda chumba kizima. Janeth akajibadirisha na kuwa bibi kizee, kinywani hakuwa na jino hata moja, akashika kibuyu kikubwa kikiwa na mafuta ya maiti za watoto wachanga, akampaka Desmund katika sehemu zake za siri ndipo zikawa imara, janeth akaanza kufanya kile alichokusudia, lakini Desmund yeye alikuwa katika usingizi mzito.

Barabara ilikuwa imenyooka, watu wakawa wanapishana kwa utulivu, kila mtu alikuwa akielekea katika shughuli zake. Mama Desmund nae alikuwa akitembea kwa tahadhari kubwa sana, mwendo wake ulikuwa ni ule ule wa taratibu kutokana na matatizo yake ya miguu. Alikuwa akielekea kanisani kwenda kuonana na Padri James ambaye ni Baba Paroko.

"Oooh! Karibu sana Mama Desmund"

"Asante sana tumsifu Yesu Kristo Baba paroko" alisalimia Mama Desmund.

"Milele amina mama yangu" aliitikia padri james huku akiachia tabasamu pana, mikononi mwake alikuwa ameishika Rozari.

"Leo nimerudi tena, lakini nimerudi moyo wangu ukiwa umefunikwa na mbawa za maumivu, nahitaji msaada wako Baba paroko, kama nitaendelea kuwa mbali na mwanangu basi ugonjwa wa moyo utaondoka na uhai wangu, kila pumzi nayovuta inauchoma moyo wangu. Nasikia mwanangu Desmund anaumwa sana, wamesisitiza kwamba nikichelewa nitakuta sio yeye tena bali nitapokelewa na mwili uliopoa na kutulia tuli mithili ya maji ndani ya mtungi."

Mama Desmund macho yalishindwa kuvumilia yakaamua yaachie machozi yabubujike ili yaupoze moyo ambao ulikuwa unateketea kwa simanzi na kilio kisicho na mwisho.

"Usilie mama, nyamaza , Baba wa mbinguni hajawahi kumuacha yule amtegemeaye, na mwenye kuzishika amri zake aendelee kuteseka, katika majonzi na simanzi ya milele" alizungumza Padri James kwa unyenyekevu, mikono yake akiwa ameikusanya kwa pamoja kana kwamba yuko ibadani.

ITAENDELEA.......
 
MALKIA WA KUZIMU..... 20
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0622 738 310
0713 417 189



ILIPOISHIA......
Mama Desmund alishindwa kuzungumza akaangua kilio kizito, akahisi moyo wake unavuja damu. Manumbu ambaye ni rafiki yake mkubwa na Desmund alikuwa ameketi pembeni huku machozi yakimdondoka kutoka na yale maneno ya uchungu aliyokuwa akiyanena Mamake Desmund. Janeth alikuwa ameketi pembeni ya kitanda muda wote alikuwa ameinamisha kichwa chake chini kama ishara ya masikitiko kwa maumivu anayopitia mumewe.
Desmund alijitahidi akayafumbua macho anashangaa kumuona mama yake, "Umekuja kunimalizia, asante mama yangu niue, niue tu mama, nilikupenda nilikuheshimu ila unaamua kuniuwa kwa uchungu kiasi hiki, asante sana" baada ya kuzungumza maneno hayo Desmund alinyamaza akaikunja sura yake kuashiria kwamba mwili wake ulikuwa unakabiliwa na maumivu makali kwa wakati huo.

ENDELEA NAYO....
Janeth alisimama akaelekea chumbani walipokuwa wakilala na mumewe kabla ya ugonjwa, akafunga mlango, akainua mikono yake miwili juu, akapokea kibuyu cha damu, viganja viwili vya binadamu, nguo ya ndani ya desmund pamoja na sanamu lenye sura ya binadamu, wakati wa kuitoa roho ya Desmund ulikuwa umewadia.

Alichukua nguo ya ndani pamoja na picha akaviweka nda ya kibuyu cha damu, kisha akaanza kuzungumza maneno yasiyoeleweka, akashika kiganja kimoja na kukoroga ile damu ndani ya kibuyu, akachukua kale kasanamu na kuanza kukakaba katika shingo, kumbe sanamu linasimama badala ya Desmund.

* "Hao wamefika, mnaniumiza shingo siwezi kupumua, kwa heri ya kuonana mke wangu, siamini kama nakuacha peke yako, mama yangu sijui kipi nilichokukosea"* alitamka maneno hayo Desmund. Mapovu mazito yakawa yanamtoka mdomoni hakika alijigeuza huku na kule akiwa anaipigania roho yake iliyokuwa mbioni kutoka.
Maneno hayo ya Desmund yalimfanya Padri James achukue maji ya baraka aliyoyabeba katika kichupa kidogo akaanza kuyanyunyuzia katika chumba hicho, kisha akaanza kusali huku Mama Desmund akiwa anaitikia.

"Ninazikemea nazifunga na kuziharibu falme na mamlaka ya wakuu wa giza hili, majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho, nanena bila uficho wala kumuhofia shetani, nakemea kwa ujasiri. Ninaamuru moto wa roho Mtakatifu kuwateketeza wote katika jina la Yesu"

Ghafla Padri James alipigwa na kitu kizito kifuani kwake akadondoka chini huku jasho zikiwa zinamchuruzika, alijitahidi kukiinua kichwa chake kujua hasa ni nini kilichompata lakini wimbi kubwa la maumivu lilimzoa akabaki amejilaza chini.

"Wapuuzi hawa wanataka kuniharibia! sasa ngoja niwaoneshe kwamba mimi ndiye malkia wa kuzimu, na huyo anayejifanya kwamba ni padri anamjua sana Mungu, na ilo ni kombora dogo tu sasa ngoja nitume la mwisho niwamalize kabisa" Janeth alizungumza mwenyewe akiwa ndani ya kile chumba alichojifungia, akachukua damu iliyokuwa na sura ya Desmund ndani yake akainywa huku akiwa anafanya ishara ya kumchinja Desmund.
Manumbu alishangaa baada ya kumuona Padri James akiwa ametupwa chini na kitu kisichoonekana, lakini kwa pembeni mama Desmund nae alidondoka kwa mshtuko akapata jeraha kichwani damu zikawa zinamchuruzika.

*"Kwaherini wote kwaherini wapenzi wangu, Ninakwenda kwetu kwenye makao ya milele sitarudi tena,
Kwaheri Baba paroko kwaheri Mwanangu mpendwa uliyeniumiza kwa maumivu, Mungu akipenda, kwake tukutane tena mwanangu."* yalikuwa ni maneno ya Mama Desmund akiwa amelala pale chini, taratibu alianza kuyafumba macho yake.

Padri James alipoyasikia maneno ya Mama Desmund alishtuka ghafla na kujikuta amepata nguvu za ajabu, akainua kichwa na kutazama juu akiwa ameikusanya mikono yake kwa pamoja akasali kwa sauti ya unyenyekevu,

"Ninawafunga wachawi wote, majini, mizimu, majini bahari wakati wa giza, roho wa udhaifu na roho chafu zote zilizopo ndani ya familia hii, ninayaharibu maficho yako na kila mbinu unayoitumia wewe shetani. Ninaamuru moto wa roho mtakatifu kuwateketeza wote katika jina la Yesu kristo. Nataka ukweli juu ya maovu yaliyofanyika hapa, nawatupa wote kuzimu, nisikilize shetani mimi ni kiongozi wa jeshi la Bwana, nakuteketeza leo kwa moto mkali usiokoma."

"Uwiiiii, mniache naunguaaa, naunguaaa mimi" Alipaza sauti Janeth kutoka katika kile chumba alichokuwa amejifungia. Padri James alipokuwa akizidi kuomba basi Janeth nae alizidi kulia kwa sauti kali yenye maumivu ndani yake.

Janeth alikuja akiwa anajivuta kwa kutumia tumbo kama nyoka, mwili ulivimba akawa anaunguruma kama simba, manumbu na mama Desmund walishangaa sana, lakini Padri James kuna kitu alikuwa amegundua hivyo akazidisha maombi.
"Mnaniumiza naungua, moto ni mkali jamani" alipaza sauti tena janeth huku akiwa amejilaza karibia na miguu ya Padri James.

"Ninaamuru moto wa roho mtakatifu uzidi kukuteketeza, nashusha moto, nashusha moto" alizidi kuomba Padri James.
Janeth alianza kutapika damu nyeusi, kucha za binadamu, vidole na kiganja cha mtoto, alihema kwa fujo kana kwamba roho inauaga mwili, mwisho alitapika maji yenye harufu mbaya sana yakiambatana na picha ya marehemu Baraka mdogo wake na Desmund aliyefariki miaka kadhaa iliyopita.

Padri James alimshika Janeth kichwani na kuanza kusali, na hapo ndipo Janeth alianza kuzungumza huku akiwa analia....
"Niache mikono yako inanichoma, nisamehe Baba ni mimi, ni mimi nayefanya haya yote, nachapwa mimi jamani, uwiiiii nachapwa nisaidieni" Janeth alizidi kulalamika kwamba anachapwa na hapo ndipo ilipodhihirika kwamba fimbo ya Mungu haina mlio.

"Sema yote vinginevyo nitaendelea kuamuru roho mtakatifu akuadhibu" alifoka kidogo Padri James.

"Eeeh! Bhabhaaaa nasema, ila nitauwawa nikisema, mimi ndie malkia nilikubali kuwa niko tayari kufa kwaajili ya kuilinda siri ya ulimwengu wa kuzimu, jamani namwagiwa maji ya moto mimi uwiiiiiiiii" alizungumza Janeth huku akiwa analia, alijigaragaza chini akiwa anajikuna huku na kule akiamini anaweza kupunguza ukali wa maumivu.
ITAENDELEA.......
 
MALKIA WA KUZIMU..... 21
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0713 417 189
0622 738 310


ILIPOISHIA....
Padri James alimshika Janeth kichwani na kuanza kusali, na hapo ndipo Janeth alianza kuzungumza huku akiwa analia....
"Niache mikono yako inanichoma, nisamehe Baba ni mimi, ni mimi nayefanya haya yote, nachapwa mimi jamani, uwiiiii nachapwa nisaidieni" Janeth alizidi kulalamika kwamba anachapwa na hapo ndipo ilipodhihirika kwamba fimbo ya Mungu haina mlio.
"Sema yote vinginevyo nitaendelea kuamuru roho mtakatifu akuadhibu" alifoka kidogo Padri James.
"Eeeh! Bhabhaaaa nasema, ila nitauwawa nikisema, mimi ndie malkia nilikubali kuwa niko tayari kufa kwaajili ya kuilinda siri ya ulimwengu wa kuzimu, jamani namwagiwa maji ya moto mimi uwiiiiiiiii" alizungumza Janeth huku akiwa analia, alijigaragaza chini akiwa anajikuna huku na kule akiamini anaweza kupunguza ukali wa maumivu.


INDELEA NAYO....

wewe sema hakuna wakukuuwa, Nimeshazikemea nikazifunga na kuziharibu falme na mamlaka ya wakuu wa giza, hivyo usiogope palipo na nguvu za Mungu shetani hawezi sogeza pua yake" alitamka Padri James kwa kujiamini zaidi akiwa ameishika misale ya waumini katika mkono wake wa kushoto.

"Siku ya kwanza nilikutana na Desmund baharini, alikuwa ameketi peke yake, nilimtokea kwa nyuma lakini hakujiuliza mimi ni kiumbe wa aina gani. Nikajipa umbo zuri tamaa zake zikaangukia kwangu akanitongoza nami nikamkubalia, lengo langu ni kupata damu ya kuwa napeleka kuzimu, nimeua watu wengi, nimemwaga damu zisizo na hatia, watoto wachanga nimeziua ndoto zao kwa kuwauwa pindi tu walipotoka kwenye matumbo ya mama zao, nilisababisha vilio, majonzi na machozi yasiyokoma. Bibi yangu kizaa mama ndiye aliyenirithisha utawala huu wa kuzimu, nikaua Baba yangu mzazi, nikaua wadogo zangu wote, naumia sana mama yangu mzazi alifariki bila kuujua ukweli huu" Janeth akasita kuendelea kuzungumza akawa anaunguruma mithili ya simba dume.

Desmund kifua chake kilikuwa kinapanda na kushuka kama maadhi ya ngoma ya dogori, kumbe roho ilikuwa inauaga mwili, Janeth aligundua ilo akajivuta na kwenda kuingiza vidole katika kinywa cha Desmund akatoa kipande cha nyama chini ya ulimi, angalau Desmund akaanza kupumua vizuri.

Vile viumbe kutoka kuzimu vilichukia sana kwani vilikuwa vimefika kwaajili ya kuitoa roho ya Desmund, chumba hicho kiligeuka uwanja wa vita dhidi ya adui asiyeonekana.

"Wananiua mnisaidie, naumia! Wanaitoboa shingo yangu wanywe damu, niokoe Padri" alipaza sauti Janeth. Padri James na Mama Desmund walizidisha maombi, Janeth akaendelea kuzungumza huku akiwa analia.

"Ili Desmund aweze kupona kuna kitu natakiwa nikichome lakini! mnaweza mkafa wote, kule kuzimu sasa kuna watu wananguvu zaidi yangu baada ya mimi kuwasaliti kwa kuwaeleza ukweli" Janeth alisema.

"Wewe sema hakuna nguvu ya giza itakayopenyenza ndani yetu" alijibu Mamake Desmund huku akiwa anaendelea kusali Rozari ya huruma ya Mungu.

Janeth alijivuta mapaka uvunguni akavuta kipande cha ngozi ikiwa imeoza vibaya sana ilijawa na funza wadogo wadogo, lakini ngozi ile inasemekana ina miaka mia mbili na haijulikani ni ya mnyama gani.

"Hatima ya maisha ya Desmund iko katika ngozi hii endapo itateketezwa" alinong'ona Janeth kwa sauti ya chini yenye maumivu ndani.

Padri James aliagiza kiberiti na mafuta akaichoma ngozi ile pale pale ndani, ghafla Desmund alianza kubadirika yale madonda yakapotea, harufu ikatoweka, akarudi katika hali yake ya kawaida. Manumbu alikuwa ameketi pembeni akitazama kana kwamba anaangalia mchezo wa kuigiza kwenye runinga akajaribu kuyafikicha macho yake asiamini kile anachokiona, alihisi yuko ndotoni. Mamake Desmund aliiweka mikono yake katika kichwa kwa mshangao baada ya kumuona mwanae karejea katika afya njema ghafla.

Desmund aliinuka kisha akaketi kitandani asiamini kile kilichotokea, akatazama mbavu zake zilizokuwa zimejawa na madonda lakini hakuona hata kovu moja, alistaajabu sana.

Ngozi ile ilipoteketea yote, Janeth alianza kutapika damu na mapande ya nyama, kumbe ilikuwa ni ile damu ya binadamu na nyama aliyokuwa akiila kule kuzimu. Alipomaliza kutapika alikuwa sawa kabisa akajivuta kwa kutumia magoti yake mpaka pale alipokuwa ameketi Desmund akamuangukia katika miguu na kuanza kulia kwa majuto yasiyokoma.

"Nisamehe mume wangu, japo damu za watu zimenililia vibaya, sidhani kama nastaili kusamehewa ila uonee imani moyo wangu. Mama yako hakuwahi kuwa mchawi ila ni mimi niliyeingia katika nafsi ya yule mganga wa sumbawanga kisha nikaanza kuzungumza kwamba mama yako anataka kukuondoa uhai, nahapa mbele ya Maulana ni mimi niliyetaka nikuue ili nizidi kuwa malkia wa kuzimu, nimekusumbua sana usiku, nilikuweka ndani ya jeneza, nikakulaza juu ya makaburini nimekulisha nyama za watu, hakika nilikuchosha mume wangu, leo najuta! Najua, chozi la damu lanidondoka, Nalia kilio kikuu, kinachoniunguza mwili na hata nafsi"

Ghafla Janeth alisita kuendelea kuzungumza baada ya kumuona Desmund akiwa anatetemeka kwa hasira machozi njia mbili mbili aliyaachia yamwagike yakalowanisha mashavu yake na kudondoka sakafuni.

"Janeeeeeeeeeeeeeeeeth" alipaza sauti Desmund akiwa ameyatumbua macho yake.

"Moyo wangu unavuja damu! unasononeka kwa uchungu, nitamwambia nini mama yangu! nilimsukuma akadondoka chini! nilimtolea maneno machafu nikijua ni mchawi. Uchungu alioupata leba bado nikamuongezea tena uchungu katika nyakati zake hizi za uzee, chozi alilonililia Mama linaniadhibu ndani ya moyo wangu, limeacha jeraha kubwa sijui ni nyuzi ngapi zitaweza kushona, Nitaueleza nini ulimwengu!?, nitasali sara gani ili nisamehewe, niliyoyafanya matokeo yake ni machozi, maumivu na uzito wa moyo. Tenda wema huende zako, mema yote niliyokutendea ndio malipo yake haya Janeth"

Desmund akiwa bado anazungumza alimrukia Janeth na kumkaba shingoni, akawa anamzungusha huku na kule kwa lengo la kumnyonga mpaka afe. Manumbu pamoja na Padri James walimzuia kisha wakamvuta Janeth na kumuweka pembeni.
ITAENDELEA....
 
MALKIA WA KUZIMU..... 22
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
MUSOMA


ILIPOISHIA....
Ghafla Janeth alisita kuendelea kuzungumza baada ya kumuona Desmund akiwa anatetemeka kwa hasira machozi njia mbili mbili aliyaachia yamwagike yakalowanisha mashavu yake na kudondoka sakafuni.
"Janeeeeeeeeeeeeeeeeth" alipaza sauti Desmund akiwa ameyatumbua macho yake.
"Moyo wangu unavuja damu! unasononeka kwa uchungu, nitamwambia nini mama yangu! nilimsukuma akadondoka chini! nilimtolea maneno machafu nikijua ni mchawi. Uchungu alioupata leba bado nikamuongezea tena uchungu katika nyakati zake hizi za uzee, chozi alilonililia Mama linaniadhibu ndani ya moyo wangu, limeacha jeraha kubwa sijui ni nyuzi ngapi zitaweza kushona, Nitaueleza nini ulimwengu!?, nitasali sara gani ili nisamehewe, niliyoyafanya matokeo yake ni machozi, maumivu na uzito wa moyo. Tenda wema huende zako, mema yote niliyokutendea ndio malipo yake haya Janeth"
Desmund akiwa bado anazungumza alimrukia Janeth na kumkaba shingoni, akawa anamzungusha huku na kule kwa lengo la kumnyonga mpaka afe. Manumbu pamoja na Padri James walimzuia kisha wakamvuta Janeth na kumuweka pembeni.

ENDELEA NAYO...
Janeth mwili mzima ulilowa machozi na jasho za maumivu, akasimama na kupiga magoti mbele ya Mamake Desmund ambaye alikuwa amejiinamia chini machozi yakimchuruzika na kudondoka katika miguu yake.

"Nimepiga magoti mbele yako Mama yangu mpendwa, niwie radhi, nimeutesa moyo wako, nimekusababishia ulemavu kwasababu ni Mimi niliyetengeneza ile ajari na nilitaka nikuondoe uhai, nazungumza haya nikiwa mtupu ndani ya moyo wangu hakuna nililoficha, umelimwaga chozi lako na kuchuruzikwa na damu kwaajili yangu, nimeuondoa Upendo, usheshi, busara dhidi ya mwanao Desmund, Hakika nilikuwa zaidi ya shetani niliyafurahia maisha Yale pasipokujua ni machungu na yanaumiza, sina ndugu Mimi katika ulimwengu huu, sina Baba, mama, kaka, Dada wala shangazi, baadhi yao nilikunywa damu zao na kuwauwa kabisa, waliondoka Duniani kwa maumivu makali ila Mimi sikujali, leo! Leo moyo wangu umelainika nahitaji msamaha najiona sifai Tena kuwa hai"

Janeth aliangukiwa na kilio kizito akaikumbatia miguu ya Mamake Desmund, kifua chake kilikuwa kinapanda na kushuka akawa anazivuta kamasi, machozi yalimuishiya na sauti kumkwama.

"Usilie mwanangu" alizungumza Mamake Desmund akiwa anajaribu kumtuliza Desmund.

"Siwezi kulizuia chozi ili mama, ni unyama nilioufanya ndio unautoboa moyo wangu nakuruhusu damu na maji kunichuruzika, Mume wangu alitamani sana mtoto lakini hakulitambua ili kwamba kila nilikuwa nikipata ujauzito nilikuwa naelekea kuzimu nalipasua tumbo langu na kutoa katoto kisha natumia mafuta yake kupakwa ili nizidi kuwa Malkia wa kuzimu, Mama no mimba takribani tank nilifanya hivo, najuta muda mwingi nimepoteza katika mambo ya kishetani. Hiyo haitoshi mama nilimuua mke wa rafiki yake na Desmund yaani nilimuua mke wa Manumbu kwa sababu shemeji Manumbu ndiye alikuwa akimpeleka Mume wangu kwa waganga ili wajue nani anaemsumbua nilijua nitaumbuka nikawa naua kila aliyetaka kuujua ukweli."

Kabla Janeth hajamaliza kuzungumza Manumbu alichukua kisu juu ya meza akamrukia Janeth, kwa Bahati mbaya kisu kile kilimchubua kidogo damu zikaacha kumchuruzika Janeth.

"Kumbe in wewe uliyenizawadia simanzi,majonzi na maumivu ya milele" alifoka kwa sauti ya juu Manumbu.

"Alipofariki mke wangu nilikuwa na majonzi zaidi kuliko Sikh zote za maisha yangu, nilihisi kana kwamba sikustahili kuishi tena" alizungumza Manumbu huku machozi yakimwagika na kulowanisha mashavu yake.

"Weka kisu chini, kumbuka auwae kwa Upanga nae atakufa kwa Upanga, usilipize baya kwa baya" alikemea Padri James.

"Hapana padri, muache aniue! Nastahili kwa Yale niliyotenda, shemeji Manumbu njooo nakuita shemeji yangu, hiki ndicho kilio changu cha mwisho, chukua kisu nichinje kama wachinjavyo ng'ombe ili mioyo yenu ipate nafuu, ni Mimi huyu niliyemuua Deus na Baraka nikanywa damu ikiwa ya moto hivyo nami nikateni kichwa ooooh! Oooh niueni niwapishe muendelee na maisha yaliyo bora, Desmund usilie Mume wangu muda mwingi ulipoteza na nguvu nyingi ulitupa kwaajili yangu, ukijua umepata mke, nami mwanzo sikuyapenda maisha yale" Janeth alipomaliza kutamka maneno hayo alijilaza chini akaiinyosha shingo yake.

"Shemeji Niko tayari kufa njoo unichinje Sasa! Nimelala chini kama afanyavyo ngamia" alipotamka maneno hayo Janeth aliyafumba macho yake ili asiweze kushuhudia jinsi atakavyochinjwa..

Mama Desmund, Padri James, Manumbu na Desmund walijikuta chozi likiwadondoka baada ya maneno hayo ya mwisho aliyotamka Janeth, yalikuwa in maneno yenye majuto ndani yake ndipo Desmund akasimama akaenda akamuinua Janeth na kumkumbatia kwa nguvu sana huku machozi yakimbubujika mithili ya bomba la mvua.

"Janeth wangu mimi sina mamlaka ya kukuhukumu wewe, umetubu, umeungama makosa yako,, chozi ulilolidondosha limeusafisha moyo wako, hakika umezaliwa upya. Namshukuru Mungu aliyejifunua kwetu na kumuumbua shetani mchana kweupe, nakupokea upya kipenzi changu, nimekusamehe, umejuta na kukiri uwepo wa Baba yetu wa Mbinguni" Desmund hakusikika tena anachokiongea bali kilio cha kwikwi kilitawala kwa wakati ule.

"Desmund, upokee moyo wangu, machungu na machozi yanayokububujika ni sababu yangu, niliyaishi maisha ambayo katu sihitaji kuyakumbuka, pole mume wangu nauona mwili wako umekufa ganzi, msamaha wako utaifufua upya furaha yangu, nitalienzi lako penzi yaani Daima na hata milele" alitamka Janeth akiwa amemkumbatia Desmund.

Kimya kilitawala kwa sekunde kadhaa, kila mtu alikuwa akitafakari kwa namna yake jinsi Mungu alivyotenda maajabu katika familia hiyo. Shetani kaondoka kwa aibu sana, kaondoka bila kuaga kama ifanyavyo njaa.

"Ee Mungu Mwenyezi na wa milele, kwa wema na huruma yako ya ajabu umetaka watu wako waokoke, watubu na kujutia makosa yao, utukinge na adui zetu wasitusumbue saa ya kufa kwetu, bali tuongozwe naye kwenye utukufu wako mkuu. Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristu"

"Amina" waliitikia wote kwa pamoja baada ya Padri James kuongoza sara hiyo fupi. Desmund pamoja na Mamake walitazama usoni wakaachia tabasamu pana lenye furaha tele usoni. Mvua ya furaha iliyojawa na tumaini jipya ilinyesha hapo ndani wakashikana mikono kwa pamoja kama ishara ya upendo uliotukuka.

"Asante Baba wa Mbinguni kwa kuiunganisha tena familia hii na kuirejeshea amani na upendo uliotoweka hapo awali, umeniokoa kutoka Malkia wa kuzimu na kuwa malkia wa familia bora yenye hofu ya Mungu. Asante sana Baba, nitalishika neno lako nakuhubiri injili mpaka ukamilifu wa Dahari. Mungu awabariki nyooote wenye kumtii na kumuheshimu yeye aliyeziumba Mbingu na Nchi" alizungumza Janeth kwa unyeyekevu wa hali ya juu huku magoti yake yakiwa sakafuni.

*NA HUU NDIO MWISHO WA SIMULIZI HII YA "MALKIA WA KUZIMU" NAWASHUKURU SANA KWA KUWA PAMOJA NAMI, MWANZO MPAKA MWISHO.
NIWAKUMBUSHE KWAMBA NIMETOA T-SHIRTS MPYA KARBU UNIUNGE MKONO,
PIA KAMA UNATAKA SIMULIZI ZANGU, NAUZA SOFT COPY, KARIBU UBURUDIKE.*

MAWASILIANO.

0713 417 189.

0622 738 310.

( WHATSAP, 0757 238 304. )
 
Simulizi : SHOLA WA DIGITALI
Kalamu ya : LOVI PIUS KIJOGOO
0713 417 189.
0622 738 310.
SEHEMU YA KWANZA
( 01 )
*"Sikuamini kama nilikuwa ni mimi nikitendwa vile. Nilivutwa huku na kule, walinitandika viboko visivyohesabika, mwili wangu ukagoma kuvumilia."

"Moyo ukapasuka, viungo vyote vya mwili vikasinyaa kutokana na uonevu huo. Nilikunjwa mithili ya nondo, nilibanwa kooni sauti haikuweza kupenya. Nilijua nakufa, Nilijua nakufa ndugu zangu."

"Nilishikwa shikwa kila kona ya mwili wangu. Lakini sikupata hisia zozote zile zaidi ya jasho la maumivu kunichuruzika."

"Hakika Shola mimi, nilitumika, nilitumika na vijana hao ambao sikujua lengo lao ni nini kwangu."

"Walinivua nguo zangu zote, nikabaki mtupu, mimi mwenyewe sikuweza kujitazama nikiwa katika msitu wa aibu hiyo. Kila nilipojaribu kupiga kelele, niliambulia kupigwa ngumi za mdomo, huku chuchu zangu zikivutwa. Yaani zilivuta kana kwamba niligeuka mipira ya manati."

"Nililia sana jamani, walizivuta nywele zangu, manusura waondoke na kichwa. Tumbo langu liligeuka godoro la kuegesha vichwa vyao, mdomo wangu ukawa kama pipi kwao, waliunyosha bila huruma mpaka ukavimba. Sidhani kama nafaa tena kuitwa mwanamke, kipi vijana hao hawakukiona katika mwili wangu."

"Wakanishika na kunipanua miguu na mikono yangu, kana kwamba wanataka kuniwamba msalabani. Niliyafumba macho yangu nikijua naenda kuuwawa."

"Waliaanza kuniingilia kimwili huku wakipokezana, Unaweza fikiri kwamba ulikuwa ni mchezo wa kuigiza. Viungo vyangu vya mwili hawakuvithamini kabisa."

"Niliugulia maumivu makali. Nilikuwa kama nimemwagiwa maji ya moto.Wakawa wananitandika makofi mgongoni wakidai kwamba siwalizishi, Nikaitwa Gogo, msukule kiuno kigumu. Hakika jamani kulia nilichoka nikawaomba vijana hao waniue tu kama wanaweza."

"Hawakutosheka!, kuna baadhi ya vijana wakaanza kuniingilia kinyume na maumbile yangu. Aibu hii sitaisahau mpaka siku naingia kaburini. Aibu hii itanifanya niwe mnyama nisiye na huruma. Nasema aibu hii itamwaga Damu nyingi sana zisizokuwa na hatia."

"Niliuchukia mwili wangu, Nikazichukia siku zangu za kuishi zilizobaki hapa Duniani, Nikawachukia wanaume wote wenye vitendo vya kikatili."

"Tangu siku hiyo nilivyofanyiwa vitendo hivyo vya kinyama, Niliyaanza maisha mapya, Nilijibatiza kwa damu nyeusi yenye sumu kali., Nilijivisha ngozi ya Chui, Niliagana na aibu, huku huruma nikiipa kisogo. Nikawa na roho mbaya sana kwa viongozi wanyanyasaji, wenye kuamini ushirikina, kwasababu ni wao walituma vijana wanifanyie ukatili huo."

"Upepo ulibadirika Ghafla, Sauti za vilio zikatawala. Sura zilizoipoteza furaha zikaongezeka. Taharuki nzito ikaibuka katika Mkoa ambao Umepakana na Geita upande wa magharibi, Shinyanga na Simiu upande wa kusini na Mara upande wa mashariki."

Ziwa la Viktoria Nyanza kaskazini, ambalo ndilo ziwa kubwa kuliko yote barani Afrika na la pili kwa ukubwa duniani. Maji ya ziwa Nyanza (Victoria) ni baridi yasiyo kuwa na magadi. Vile vile mji unaopatikana kutoka usawa wa bahari mita 1,140. una mandhari nzuri yenye kupendeza kama vile majabali ya mawe na vilima vyake vya hapana pale, yaani panaitwa Jiji la mwanza.

Miili ya wanaume ilikutwa ikiwa imeuwawa katika nyumba za kulala wageni, Jiji lilipoa Ghafla. Familia nyingi zilikumbwa na lindi la huzuni.

"Kila mwili wa mwanaume aliyekutwa ameuwawa, ulikuwa umechorwa na maandishi ya Damu yake kifuani, maandishi yaliyosomeka kwamba.. "Mapenzi yakifa yazike na usiweke maua juu ya kaburi, mlichonifanyia nikiwa mdogo leo nalipiza kisasi. Na wale mliowaua wazazi wangu mjiandae."

Serikali ilikuwa katika wakati mgumu sana, kutambua muuaji ni nani. Na hapo ndipo Inspekta Majuto na timu yake wanaingia kazini kumtafuta muuaji huyo.



☆☆☆☆☆☆☆☆☆

FB_IMG_1612615859908.jpg
 
Wewe jamaa ni muuaji
'akamrukia Janeth, kwa Bahati mbaya kisu kile kilimchubua kidogo damu zikaacha kumchuruzika Janeth'
Kwa bahati nzuri alitakiwa afe Janeth?
Hongera kwa utunzi wako. Unatumia software gani kutengeneza picha ya kitabu?
"Vipi niachie kigongo kipya kwenye uzi huu"View attachment 1899951
 
MALKIA WA KUZIMU..... 22
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
MUSOMA


ILIPOISHIA....
Ghafla Janeth alisita kuendelea kuzungumza baada ya kumuona Desmund akiwa anatetemeka kwa hasira machozi njia mbili mbili aliyaachia yamwagike yakalowanisha mashavu yake na kudondoka sakafuni.
"Janeeeeeeeeeeeeeeeeth" alipaza sauti Desmund akiwa ameyatumbua macho yake.
"Moyo wangu unavuja damu! unasononeka kwa uchungu, nitamwambia nini mama yangu! nilimsukuma akadondoka chini! nilimtolea maneno machafu nikijua ni mchawi. Uchungu alioupata leba bado nikamuongezea tena uchungu katika nyakati zake hizi za uzee, chozi alilonililia Mama linaniadhibu ndani ya moyo wangu, limeacha jeraha kubwa sijui ni nyuzi ngapi zitaweza kushona, Nitaueleza nini ulimwengu!?, nitasali sara gani ili nisamehewe, niliyoyafanya matokeo yake ni machozi, maumivu na uzito wa moyo. Tenda wema huende zako, mema yote niliyokutendea ndio malipo yake haya Janeth"
Desmund akiwa bado anazungumza alimrukia Janeth na kumkaba shingoni, akawa anamzungusha huku na kule kwa lengo la kumnyonga mpaka afe. Manumbu pamoja na Padri James walimzuia kisha wakamvuta Janeth na kumuweka pembeni.

ENDELEA NAYO...
Janeth mwili mzima ulilowa machozi na jasho za maumivu, akasimama na kupiga magoti mbele ya Mamake Desmund ambaye alikuwa amejiinamia chini machozi yakimchuruzika na kudondoka katika miguu yake.

"Nimepiga magoti mbele yako Mama yangu mpendwa, niwie radhi, nimeutesa moyo wako, nimekusababishia ulemavu kwasababu ni Mimi niliyetengeneza ile ajari na nilitaka nikuondoe uhai, nazungumza haya nikiwa mtupu ndani ya moyo wangu hakuna nililoficha, umelimwaga chozi lako na kuchuruzikwa na damu kwaajili yangu, nimeuondoa Upendo, usheshi, busara dhidi ya mwanao Desmund, Hakika nilikuwa zaidi ya shetani niliyafurahia maisha Yale pasipokujua ni machungu na yanaumiza, sina ndugu Mimi katika ulimwengu huu, sina Baba, mama, kaka, Dada wala shangazi, baadhi yao nilikunywa damu zao na kuwauwa kabisa, waliondoka Duniani kwa maumivu makali ila Mimi sikujali, leo! Leo moyo wangu umelainika nahitaji msamaha najiona sifai Tena kuwa hai"

Janeth aliangukiwa na kilio kizito akaikumbatia miguu ya Mamake Desmund, kifua chake kilikuwa kinapanda na kushuka akawa anazivuta kamasi, machozi yalimuishiya na sauti kumkwama.

"Usilie mwanangu" alizungumza Mamake Desmund akiwa anajaribu kumtuliza Desmund.

"Siwezi kulizuia chozi ili mama, ni unyama nilioufanya ndio unautoboa moyo wangu nakuruhusu damu na maji kunichuruzika, Mume wangu alitamani sana mtoto lakini hakulitambua ili kwamba kila nilikuwa nikipata ujauzito nilikuwa naelekea kuzimu nalipasua tumbo langu na kutoa katoto kisha natumia mafuta yake kupakwa ili nizidi kuwa Malkia wa kuzimu, Mama no mimba takribani tank nilifanya hivo, najuta muda mwingi nimepoteza katika mambo ya kishetani. Hiyo haitoshi mama nilimuua mke wa rafiki yake na Desmund yaani nilimuua mke wa Manumbu kwa sababu shemeji Manumbu ndiye alikuwa akimpeleka Mume wangu kwa waganga ili wajue nani anaemsumbua nilijua nitaumbuka nikawa naua kila aliyetaka kuujua ukweli."

Kabla Janeth hajamaliza kuzungumza Manumbu alichukua kisu juu ya meza akamrukia Janeth, kwa Bahati mbaya kisu kile kilimchubua kidogo damu zikaacha kumchuruzika Janeth.

"Kumbe in wewe uliyenizawadia simanzi,majonzi na maumivu ya milele" alifoka kwa sauti ya juu Manumbu.

"Alipofariki mke wangu nilikuwa na majonzi zaidi kuliko Sikh zote za maisha yangu, nilihisi kana kwamba sikustahili kuishi tena" alizungumza Manumbu huku machozi yakimwagika na kulowanisha mashavu yake.

"Weka kisu chini, kumbuka auwae kwa Upanga nae atakufa kwa Upanga, usilipize baya kwa baya" alikemea Padri James.

"Hapana padri, muache aniue! Nastahili kwa Yale niliyotenda, shemeji Manumbu njooo nakuita shemeji yangu, hiki ndicho kilio changu cha mwisho, chukua kisu nichinje kama wachinjavyo ng'ombe ili mioyo yenu ipate nafuu, ni Mimi huyu niliyemuua Deus na Baraka nikanywa damu ikiwa ya moto hivyo nami nikateni kichwa ooooh! Oooh niueni niwapishe muendelee na maisha yaliyo bora, Desmund usilie Mume wangu muda mwingi ulipoteza na nguvu nyingi ulitupa kwaajili yangu, ukijua umepata mke, nami mwanzo sikuyapenda maisha yale" Janeth alipomaliza kutamka maneno hayo alijilaza chini akaiinyosha shingo yake.

"Shemeji Niko tayari kufa njoo unichinje Sasa! Nimelala chini kama afanyavyo ngamia" alipotamka maneno hayo Janeth aliyafumba macho yake ili asiweze kushuhudia jinsi atakavyochinjwa..

Mama Desmund, Padri James, Manumbu na Desmund walijikuta chozi likiwadondoka baada ya maneno hayo ya mwisho aliyotamka Janeth, yalikuwa in maneno yenye majuto ndani yake ndipo Desmund akasimama akaenda akamuinua Janeth na kumkumbatia kwa nguvu sana huku machozi yakimbubujika mithili ya bomba la mvua.

"Janeth wangu mimi sina mamlaka ya kukuhukumu wewe, umetubu, umeungama makosa yako,, chozi ulilolidondosha limeusafisha moyo wako, hakika umezaliwa upya. Namshukuru Mungu aliyejifunua kwetu na kumuumbua shetani mchana kweupe, nakupokea upya kipenzi changu, nimekusamehe, umejuta na kukiri uwepo wa Baba yetu wa Mbinguni" Desmund hakusikika tena anachokiongea bali kilio cha kwikwi kilitawala kwa wakati ule.

"Desmund, upokee moyo wangu, machungu na machozi yanayokububujika ni sababu yangu, niliyaishi maisha ambayo katu sihitaji kuyakumbuka, pole mume wangu nauona mwili wako umekufa ganzi, msamaha wako utaifufua upya furaha yangu, nitalienzi lako penzi yaani Daima na hata milele" alitamka Janeth akiwa amemkumbatia Desmund.

Kimya kilitawala kwa sekunde kadhaa, kila mtu alikuwa akitafakari kwa namna yake jinsi Mungu alivyotenda maajabu katika familia hiyo. Shetani kaondoka kwa aibu sana, kaondoka bila kuaga kama ifanyavyo njaa.

"Ee Mungu Mwenyezi na wa milele, kwa wema na huruma yako ya ajabu umetaka watu wako waokoke, watubu na kujutia makosa yao, utukinge na adui zetu wasitusumbue saa ya kufa kwetu, bali tuongozwe naye kwenye utukufu wako mkuu. Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristu"

"Amina" waliitikia wote kwa pamoja baada ya Padri James kuongoza sara hiyo fupi. Desmund pamoja na Mamake walitazama usoni wakaachia tabasamu pana lenye furaha tele usoni. Mvua ya furaha iliyojawa na tumaini jipya ilinyesha hapo ndani wakashikana mikono kwa pamoja kama ishara ya upendo uliotukuka.

"Asante Baba wa Mbinguni kwa kuiunganisha tena familia hii na kuirejeshea amani na upendo uliotoweka hapo awali, umeniokoa kutoka Malkia wa kuzimu na kuwa malkia wa familia bora yenye hofu ya Mungu. Asante sana Baba, nitalishika neno lako nakuhubiri injili mpaka ukamilifu wa Dahari. Mungu awabariki nyooote wenye kumtii na kumuheshimu yeye aliyeziumba Mbingu na Nchi" alizungumza Janeth kwa unyeyekevu wa hali ya juu huku magoti yake yakiwa sakafuni.

*NA HUU NDIO MWISHO WA SIMULIZI HII YA "MALKIA WA KUZIMU" NAWASHUKURU SANA KWA KUWA PAMOJA NAMI, MWANZO MPAKA MWISHO.
NIWAKUMBUSHE KWAMBA NIMETOA T-SHIRTS MPYA KARBU UNIUNGE MKONO,
PIA KAMA UNATAKA SIMULIZI ZANGU, NAUZA SOFT COPY, KARIBU UBURUDIKE.*

MAWASILIANO.

0713 417 189.

0622 738 310.

( WHATSAP, 0757 238 304. )

Safi sana... Story nzuri sana...

Chapter Closed...
 
Wewe jamaa ni muuaji
'akamrukia Janeth, kwa Bahati mbaya kisu kile kilimchubua kidogo damu zikaacha kumchuruzika Janeth'
Kwa bahati nzuri alitakiwa afe Janeth?
Hongera kwa utunzi wako. Unatumia software gani kutengeneza picha ya kitabu?
Shukrani Sana, picha ya kitabu kuna mtaalamu ananifanyia kazi hyo.
 
"Kusoma kimya kimya na tozo, naona maumivu yake yanalingana."
 
OFA... OFA... OFA ....OFA

Usikose vitabu vyangu ( nakala laini ) unatumiwa kwa njia ya email au whatsap Navyo ni:- ________________====_________

Narudi Songea... 5,000/= tu!
Yolanda.....4,000/= tu!
Malkia wa kuzimu... 4,000/= tu!
Hadithi ya Suzi..... 2,500/=
Usilie Rehema.... 5,000/= tu!
________________====_________
PIA NAFUNDISHA MASOMO YA JIONI KWA WALE AMBAO WANARUDIA MITIHANI YA KIDATO CHA NNE. KIDATO CHA TANO NA SITA KWA MICHEPUO YA, HKL NA HGL.

KAMA UNAHITAJI KUANDIKIWA KITABU CHA HISTORIA YA MAISHA YAKO UNAKARIBISHWA...

NAPATIKANA TANGA MJINI,....
0622 738 310.
0713 417 189.
( 0757 238 304, whatsap )

MWL, LOVI PIUS KIJOGOO.
FB_IMG_1617644945820.jpg
 
Simulizi fupi

Mtunzi : LOVI PIUS KIJOGOO
( 0757 238 304 Whatsap )
0713 417189.
0622 738 310.

NISAMEHE MWANANGU SIKUJUA NIANZIE WAPI KUKWAMBIA UKWELI.

Naomba Dunia unihukumu mimi na sio mwanangu, Duniani nitandike viboko vingi visivyo kuwa na idadi ila mpunguzie mwanangu adhabu ya kaburi.

Jaman!i leo niko katika kaburi la mwanangu Aisha, nitaeleza vipi mimi Dunia inielewe?, nitasali sala gani mimi Baba wa mbinguni apate kumpokea mwanangu?.

Mwanangu Aisha nipo katika makao yako ya milele sio ghorofa wala ile nyumba yetu ya nyasi tuliyokuwa tukiishi, ila leo umepumzishwa katika nyumba ya ajabu isiyokuwa hata na upenyo wa kupitisha hewa.
Mwanangu Aisha nisamehe, najua umeondoka katika sayari hii ukiwa na hasira sana juu yangu, kumbuka mimi ni mama yako nilikupenda sana, ndio maana sikutaka kukwambia Siri hii ambayo imefanikiwa kukusindikiza vyema katika makazi ya wote.

Jamani ndugu zangu nisikilizeni kwa makini, niwaeleze sababu kubwa iliyopelekea mimi kuwa hapa katika kaburi la binti yangu Aisha.

Ila naomba msinihukumu jamani, ilikuwa hivyi mwanangu tangia nilipomzaa alipofikisha miezi kadhaa kuna dawa nilikuwa nampa, kumbukeni alikuwa mdogo sana hakuweza kuuliza kitu chochote kile, basi alifika mpaka kidato cha cha tatu, kila siku nampa vidonge anameza huku nikimwambia ni vya malaria tu, mwanangu alinielewa na kuendelea kubugia vidonge hivyo.

Hali ilibadirika pale binti yangu alipofika kidato cha nne, nakumbuka ilikuwa ni siku ya jumatano jioni, mwanangu aliniita chumbani kwake na kuanza kuniambia..

"Mama yangu nisamehe kama nitakuwa nimekukosea heshima, mpaka leo hii hujawahi nionesha baba yangu lakini suala ilo nimelifumbia macho tu lipite, lakini la mimi kumeza vidonge tangu nikiwa darasa la kwanza mpaka leo kidato cha nne! Kisha unasema nasumbuliwa na Malaria, jamani mama ni malaria gani hii Mama yangu.

Kiukweli maneno hayo kutoka kwa mwanangu yalinifanya nichanganyikiwe
, Ghafla kijasho chembamba kikaanza kunichuruzika kwapani, mapigo ya moyo yakawa yanaenda kasi sana, kila nilipotaka kumficha mwanangu nikaona anazidi kuwa mkali, ikabidi nianze kumueleza kwa utulivu kwamba..

"Binti yangu nisamehe kwa maneno haya nitakayokueleza, umekuwa ukinywa vidonge kila siku mpaka leo umefikia hapo, ila mama yako vidonge hivyo nimevinywa saaana mwanangu. Najua unajiuliza wapi Baba yako alipo ila yeye ndiye chanzo cha sisi kubugia vidonge hivyi katika maisha yetu yote mwanangu"

"Mwanangu! Baba yako alifariki wewe ukiwa na mwaka mmoja, aliugua sana ila akawa anaficha tatizo ni nini ila alivyozidiwa sana tulibaini ugonjwa wake, nisikilize kwa makini mwanangu hizo dawa ulizokuwa unakunya ni za kupunguza makali ya virusi vya ukimwi."

Jamani hamuwezi kuamini mwanangu alivyogundua kwamba anaishi na virusi hivyo alipoteza fahamu takribani nusu saa, ila fahamu ziliporejea nilimbembeleza akatulia na kwenda kulala.

Sitaisahau asubuhi hii katika maisha yangu yote ya hapa Duniani, niliamka nakuta mwanangu akiwa amejinyonga katika mti wa muembe pale nyumbani, aliniachia kipande cha karatasi kikiwa na ujumbe uliosomeka kwamba...

"Mama umeninywesha vidonge vya kutosha, kiukweli umenikosea sana, kuna baadhi ya wanafunzi nilikuwa na mahusiano nao ya kimapenzi, nitawaeleza nini wakiugundua ukweli kuhusu afya yangu, Eeh jamani mama yangu! mimi nakuachia Dunia yako na vidonge vyako, acha nielekee alipo Baba akanieleze kwanini alisababisha yote haya, jamani rafiki zangu tuliokuwa wote kidato cha nne nitunzieni mtihani wangu labda ipo siku nitarudi nakuufanya upya nikiwa mwenyewe na sanda yangu."

Huo ndio ulikuwa mwisho wa ujumbe mfupi aliouacha mwanangu, nielezeni kosa langu nini au kumficha miaka yote hiyo nilikosea.. acheni nilie mimi Dunia imenielemea.

MWANANGU MAMA YAKO NIKO KATIKA KABURI LAKO NAOMBA UNISAMEHE KAMA NILIKUKOSEA.

__ mwisho_


OFA... OFA... OFA ....OFA

Usikose vitabu vyangu ( nakala laini ) unatumiwa kwa njia ya email au whatsap Navyo ni:- ________________====_________

Narudi Songea... 5,000/= tu!
Yolanda.....4,000/= tu!
Malkia wa kuzimu... 4,000/= tu!
Hadithi ya Suzi..... 2,500/=
Usilie Rehema.... 5,000/= tu!
________________====_________
PIA NAFUNDISHA MASOMO YA JIONI KWA WALE AMBAO WANARUDIA MITIHANI YA KIDATO CHA NNE. KIDATO CHA TANO NA SITA KWA MICHEPUO YA, HKL NA HGL.

KAMA UNAHITAJI KUANDIKIWA KITABU CHA HISTORIA YA MAISHA YAKO UNAKARIBISHWA...

NAPATIKANA TANGA MJINI,....
0622 738 310.
0713 417 189.
( 0757 238 304, whatsap )

MWL, LOVI PIUS KIJOGOO.
FB_IMG_1632038286819.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom