Simulizi: Malkia wa kuzimu-01

Simulizi: Malkia wa kuzimu-01

MALKIA WA KUZIMU..... 11
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0622 738 310




. ...............................................
SEHEMU YA KUMI NA MOJA.
( 11 )


ILIPOISHIA.....


"Mwanangu niliyekuzaa leo unanitupia nguo zangu! Unanitusi mwanangu, naumia sana nani atanizika mimi? wewe ndie mwanangu wa pekee uliyebakia" alizungumza kwa huzuni sana Mama Desmund.
"Utazikwa na wachawi wenzako" alidakia Desmund akasogea alipo mamake na kuanza kumvuta kumpeleka nje ya nyumba yake.
"Mwanangu unanivuta kama mwizi, mwili wangu umekufa ganzi, Eeh Baba wa mbinguni unauona moyo wangu ulivyopondwa pondwa na magumu ya Dunia. Hiki ndicho kilio changu cha mwisho, niokoe Baba moyo wangu unavuja damu! Iangalie roho iliyopondeka inayolia na kuhuzunika mbele yako."

ENDELEA NAYO.....

Mama Desmund kinywa kilikuwa kizito hakuweza kuzungumza tena, machozi njia mbili mbili aliyaachia yamwagike yakilowanisha mashavu yake na kudondoka kwenye kile kipande chake cha kanga alichokuwa amejifunika mabegani mwake.

Desmund alimvuta mamake akamfikisha mpaka nje ya geti, akamtupia begi lake chini kisha akafunga geti.

"Asante sana mwanangu, nashukuru kwa zawadi hii ya maumivu na aibu isiyokoma. Kama kukuzaa na kukulea ndio kosa langu naomba unisamehe, acha niondoke, moyo wangu umekauka sababu ya huzuni, nimeangukiwa na wingu kubwa la majonzi, njia ya maisha yangu imejaa miba mingi inayochoma, uzito wa mateso umenielemea nyakati hizi za uzee wangu, Baba wa mbinguni njoo hima unisaidie."

Baada ya Mama Desmund kuzungumza maneno hayo, aliinua Kichwa chake akaitazama nyumba ya mwanae akabeba begi lake kisha akaangua kilio kizito, kilio kisichokoma, kilio kisichopozeka, ila akajikaza akageuka zake na kuondoka ili akatafute usafiri arudi nyumbani kwake alipokuwa akiishi na mumewe kabla ya kufariki uko mkoani pwani.

Janeth alimrukia kwa nguvu mumewe huku akimwambia... "Asante sana mume wangu umefanya uamuzi wa busara sana, kumbe tulikuwa tunaishi na adui humu ndani ya nyumba"

"Yaani wewe acha tu mke wangu" alidakia Desmund kwa hasira sana.

"Nilivyokuwa nikimjali na kumthamini Mama! sikutegemea kama ipo siku angetaka kuutoa uhai wangu, kipi ambacho sikutimiza kwa Mama, kamuua kaka Deus kamuacha mkewe akiwa na watoto wachanga yaani najisikia vibaya sana"

Desmund alinyamaza akaenda ndani ya jokofu akachukua bia mbili akazibugia haraka haraka. Akiamini akili yake itatulia kitu ambacho hakina ukweli wowote ule.

Mama Desmund alikuwa na umri wa miaka sitini na tano, kichwa chake kilijawa na nywele nyeupe yaani mvi, alikuwa ni mweupe kiasi, kutokana na matatizo yake ya miguu kuvimba alikuwa anatembea kwa mwendo wa kunyata, Alilitumikia jeshi la wananchi Tanzania kwa miaka mingi anavyodai yeye ndio chanzo kikubwa cha mgongo wake kupinda kidogo. Alikuwa akisali kanisa katoriki na kwa pale mtaani kwake alikuwa ni mwenyekiti wa jumuiya ya mtakatifu Antoni wa Padua. Majirani walimpenda sababu ya ucheshi wake ulioambatana na hekima, mpaka watoto walimpenda sababu alikuwa akiwasimulia hadithi mbalimbali.

Mama Desmund alikuwa tayari amefika nyumbani kwake mkoani pwani. Usoni hakuwa na tabasamu lolote lile, simanzi na majonzi viliambatana nae kwa ukaribu sana. Alipikiwa chakula lakini alipojaribu kula alitapika chote, ndipo yule msichana wa kazi anayeishi nae akamkologea uji.

"Usiangaike tu mwanangu, sijisikii kunywa chochote kile, kinywa changu ni kichungu, Dunia imenibadirikia! sioni sababu ya kuendelea kuishi tena, kweli mtoto aliyenyonya kifuani kwangu ananitusi na kunitupia nguo zangu, acha nilie, niache nilie, uzee wangu umekuwa wa majonzi, nakufa kwa maumivu sana mimi"
Mama Desmund machozi yalizidi kumbubujika, aliamua ayaache yaendelee kumchuruzika walau yapoze moyo wake unaoteketea kwa moto.

Ilikuwa ni saa nne kamili za usiku, Mwili wa Mama Desmund ulikuwa umepoa na hauna nguvu kabisa, akaamua aende chumbani kwake kupumzika, alivyofika alijitahidi akapiga magoti sakafuni kwa uchungu sana sababu ya tatizo lake la miguu, akaikusanya mikono yake kwa pamoja kwaajili ya kusali.

"Ewe Baba wa mbinguni, macho yangu yametiwa uvuli kwa uchungu, tazama moyo wangu unasononeka kwa maumivu, najiona sina nafasi ya kuishi tena, ila bado naimani na wewe Mungu wangu, natambua unaimulika njia yangu yenye giza. Utazame moyo wangu unaoomboleza mbele yako, sipati tena tabasamu la thamani, njoo unisaidie Baba, nakuja kwako wewe ambaye kila mara wawahurumia wanaoteseka"

Mama Desmund akiwa katika maombi hayo ghafla machozi yalianza kumdondoka akasimama na kupanda kitandani, usingizi ulimsaliti kwa muda, kila alipojaribu kuyafumba macho yake ili apate usingizi picha ilimuijia jinsi Desmund alivyokuwa akimvuta na kumtoa ndani ya geti kama mwizi, ilikuwa ni kumbukumbu inayoumiza ambayo ilimkosesha usingizi.

Mama Desmund aliamshwa ghafla saa tisa za usiku na taa iliyowaka sebuleni,

"Nani kawasha taa usiku huu na hakuna mtu sebuleni hapo! " alijiuliza moyoni kwa mshango wa hali ya juu.

Pole pole alijitahidi akainuka kitandani na bila kuwasha taa ya chumba cha kulala, aliunyatia mlango akaufungua pole pole ila alishangazwa na kile alichokiona.

Sebuleni kulikuwa na kijana amesimama mezani, alipoangalia vizuri aligundua ni Deus mtoto wake, alikuwa amevaa nguo walizomzika nazo, ila hali yake kiafya ilionekana kuwa mbaya. Macho yake yalikuwa yameingia ndani alikuwa anatia huruma hata kumtazama
Deusi aliminina uji akaanza kunywa, akafunua masufuria akachukua ugali na kuanza kula bila hata mboga, alikuwa analia nyuma ya viganja vyake.

Nywele zilikuwa chafu na ndefu kama mwendawazimu. Alipomaliza kula alisimama akaelekea mpaka jikoni akanywa maji ndoo nzima, alivyomaliza alipotelea ukutani na taa ikazima ghafla.
Mama Desmund akiwa bado anatetemeka kwa hofu alisikia mishindo wa viatu vya mtoto wake akikimbia, pa! pa! pa! mlio huo ulimuumiza sana.

Mama Desmund alikuwa haoni tena, isipokuwa giza lililomgubika. Alijitahidi akapapasa akakaa kwenye sofa, "Deusi rudiiiiiiii" alipaza sauti lakini mtoto wake hakuitika, kitendo hicho kilimshtua sana, akaamini kumbe mwanaye hajafa ila kachukuliwa na watu wanaotegemea nguvu ya giza. Machozi yalianza kumbubujika upya yakalowanisha mashavu na kudondoka sakafuni.


************
 
MALKIA WA KUZIMU..... 12
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0622 738 310.

................................................................
SEHEMU YA KUMI NA MBILI.
( 12 )


ILIPOISHIA.....
Deus aliminina uji akaanza kunywa, akafunua masufuria akachukua ugali na kuanza kula bila hata mboga, alikuwa analia nyuma ya viganja vyake. Nywele zilikuwa chafu na ndefu kama mwendawazimu. Alipomaliza kula alisiamama akaelekea mpaka jikoni akanywa maji ndoo nzima, alivyomaliza alipotelea ukutani na taa ikazima ghafla.
Mama Desmund akiwa bado anatetemeka kwa hofu alisikia mishindo wa viatu vya mtoto wake akikimbia, pa! pa! pa! mlio huo ulimuumiza sana.
Mama Desmund alikuwa haoni tena, isipokuwa giza lililomgubika. Alijitahidi akapapasa akakaa kwenye sofa, "Deusi rudiiiiiiii" alipaza sauti lakini mtoto wake hakuitika, kitendo hicho kilimshtua sana, akaamini kumbe mwanaye hajafa ila kachukuliwa na watu wanaotegemea nguvu ya giza. Machozi yalianza kumbubujika upya yakalowanisha mashavu na kudondoka sakafuni.

ENDELEA NAYO...

Saa kumi na mbili za alfajiri Mama Desmund alikuwa amedamka tayari, kiubaridi kikawa kinapuliza kwa mbali, akafunga vimbuzi vyake vitatu pembezoni mwa nyumba yake, akashika ufagio na kuanza kukusanya uchafu uliokuwa umedondoshwa na miti ile ya matunda aliyokuwa ameipanda pale nyumbani kwake, pamoja na maradhi yake ya uzeeni hakupenda kukaa bila ya kufanya vikazi vya hapa na pale.

Alitandika mkeka wake, akaketi na kuinyoosha miguu yake, wakati akilisubir jua ambalo nalo lilikuwa likichomoza kwa maringo sana katikati ya mawingu ambayo yalikuwa yametanda katika anga. Akiwa bado ameketi pale mkekani, alimuita yule binti wake wa kazi kisha akaanza kumsimulia yote aliyoyasikia na kuyashuudia kwa macho yake japo yalikuwa yanaogofya usiku wa kuamkia siku hiyo.

Mdada uyo wa kazi alishangaa sana, hakuwahi kusikia kitu kama hicho kwamba mtu alizikwa lakini kaonekana tena akimimina mpaka uji na kunywa.

"Pole sana Bibi!" Mdada wa kazi alinena.
" Asante sana, Dunia ina mengi sana!" alijibu Mamake Desmund.
Mama Desmund alishangaa ghafla alipomuona mdada wa kazi machozi yakimdondonda,

"Umepatwa na nini tena?" Mama Desmund aliuliza kwa mshangao sana.

"Nimekumbuka mambo ambayo uwa yanauchoma na kuuralua moyo"
"Mambo gani hayo?" alihoji Mama Desmund.
Mdada wa kazi aliyafuta machozi yake kisha akaanza kusimulia.

"Nilikuwa na miaka kumi na miwili wakati vita vilipotokea pale kwetu Tarime mkoani mara. Baba yangu sikuwahi kumuona wala kumjua, sina uhakika kama nae aliuwawa katika mapigano hayo au laa..! Mama yangu alikuwa akifanya biashara ya kutembeza ndizi mbivu kichwani, jua na mvua vilikuwa vitu vya kawaida kwake. Nyumbani kwetu tulikuwa jumla ya watoto watano.

Kumbe ilikuwa ni vita ya makabira, koo kwa koo, hasa wafugaji na wakulima, sisi tulikuwa ni wakulima pamoja na ving'ombe kama vitano tu."

"Amani ilitoweka, mifugo ilikuwa ikiuliwa ovyo mashamba yakifyekwa bila ya huruma. Nakumbuka ilikuwa siku ya jumamosi jirani zetu walishambuliwa, nyumba zao zikachomwa moto, mali zao zikaporwa, watoto wakachinjwa, kiukweli ilikuwa vigumu kutembea, kula au kufanya jambo lolote lile." alisita kidogo kuendelea kusimulia, akajinyoosha na kuketi vizuri katika mkeka kisha akaendelea kuzungumza.
__________________________________________
KUPATA sehemu ya 13 mpaka MWISHO, lipia 2500 tu kwenda namba 0622 738 310. Jina lovi kijogoo. Sapoti kalamu ya mtunzi, azidi kuandika.
___________________________________________

"Baada ya majuma kama matatu kupita nyumba yetu ilishambuliwa, Mama aliuwawa katika vurugu hilo, nilisikia akilia kwa uchungu, "Mama ee! Msiniue! Nitafanya lolote mlitakalo!"

"Lakini haikuwa hivyo kilio chake hicho hakikuwagusa wala kuwaathiri ilikuwa kama dua ya kuku isiyompata mwewe. Mimi nilikuwa nimejificha upenuni na kujifunika kwa guo kubwa kuukuu ambalo mama alikuwa akianikia mihogo. Woga na hofu kubwa vilinifanya kujikunja mle kama nyoka."

"Ndugu zangu wote waliuwawa wakati huo, ni mimi tu niliyesalia, wauwaji hao waliondoka mara tu baada ya kuumaliza ukatili huo, niliondoka upenuni hapo nikatembea katika nyumba yetu iliyokuwa wazi, milango yote ilikuwa imevunjwa, niliweza kuiona miili ya ndugu zangu pamoja na ule wa mamangu mpendwa.Mama alikufa kwa uchungu mwingi, alikuwa ameuuma mdomo wa chini kwa meno! Macho yake yalimtoka kama ambaye alikuwa anagombana na ulimwengu uliompa mgongo!"

"Mwili mzima ulinizizima kutokana na hisia za kuiona mili ile, niliduwaa kwa muda, nililia Bibi! Nililiaaa Bibi, nikatamani kitokee kiumbe kitoweka nami, sikuwa na ndugu tena, kila nilipoyatazama mapanga yaliyowauwa ndugu zangu niliumia nililia kilio kisicho na mwisho, sina Baba, sina mama, wadogo zangu wote wameuawa, Bibi niliona Dunia imenibana."

Maumivu yalikuwa makali kuzungumza hakuweza tena, machozi njia mbili mbili aliyaachia yamwagike yakalowanisha mashavu yake na kudondoka kwenye mkeka.

"Pole sana! Usilie hayo ni mapito japo yanaumiza!" Mamake Desmund alijaribu kumtuliza binti yake wa kazi.

"Asante Bibi, baada ya ndugu zangu kuuwawa nikajipa moyo kwamba kwa vile mimi ni mtoto wa kike, ipo siku nitazaa watoto kisha nitawapa majina ya ndugu zangu ili ukoo uanze upya. Lakini Dunia haikupendezwa na wazo ilo, nilimpata kijana aitwae Marwa, akiniomba niwe na mahusiano naye nikakubali nilikuwa na miaka kumi na tano,"

"Baada ya muda alinipa ujauzito, akaanza sababu kwamba hajajipanga kimaisha, hayuko teyari kulea, mara nyumbani kwao hawajui kama anamahusiano na mtoto wa kike, akalazimisha nitoe mimba"

"Kwa vile nampenda nilimkubalia nikaenda kuitoa mimba, yaaani Bibi! Bibi!Bibi acha tu Bibi. Nilitokwa na damu nyingi sana, niliugua manusura nife, kijana yule alinikataa hakutaka kuniona tena, baada ya kusikia nimepoteza mfuko wa uzazi sikuwa napata hedhi tena kama mwanamke, mirija ya uzazi iliziba, Bibi nilipoenda hospitali niliambiwa nimekuwa tasa kwasababu ya kuziba mirija na kupoteza kizazi, nililia sana Bibi yangu, ndoto zangu za kuwa na familia zikaota mbawa ghafla, sitamsahau Marwa mpaka siku naingia kaburi, nilishamsamehe ila kumsahau nimeshindwa."

"Sikuwahi kukanyaga shule, hata darasa la kwanza sikuwahi kusoma, shule yangu ilikuwa ni shambani kwenda kulima basi, ningejuaje madhara ya utoaji mimba mimi?, nijibu Bibi ningejua vipi kwamba naweza kuchanika mdomo wa kizazi?, kutobolewa kizazi au majeraha ya kibofu cha mkojo na sehemu za haja kubwa!. Jamani niacheni nilie mimi, urembo wangu pasi kuwa na mtoto ni maumivu! sikujua kwamba najitafutia majuto yasiyokwisha na kukosekana kwa amani."

"Dada zangu, wadogo zangu au wanawake wenzangu kumbukeki kwamba, Maumbile tuliyonayo tumepewa na Mungu wetu, tuepuke kuyatumia maumbile yetu kwa njia imchukizayo Mungu, wapo wanawake na wanaume wengi wanaopita duniani bila kupata mtoto huku wakiutamani na kuulilia uzazi. Kama ninavyoulilia mimi hivi sasa! Lakini! nimechelewa."

Machozi yalizidi kumbubujika, ndipo Mama Desmund akamkumbatia na kumtuliza, Wingu la majonzi lilitanda nyumbani hapo, mvua ya maumivu ikazidi kucharaza! huku radi kali za mateso zikawa zinapiga na kuiunguza mioyo yao kwa simanzi. Mama Desmund alishindwa kulizuia chozi lake akaamua aliachie limdondoke aliguswa sana na maisha ya binti wake wa kazi.
FB_IMG_1622739579357.jpg
 
MALKIA WA KUZIMU..... 13
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0622 738 310

................................................................
SEHEMU YA KUMI NA TATU.
( 13 )


ILIPOISHIA.....
Machozi yalizidi kumbubujika, ndipo Mama Desmund akamkumbatia na kumtuliza, Wingu la majonzi lilitanda nyumbani hapo, mvua ya maumivu ikazidi kucharaza! huku radi kali za mateso zikawa zinapiga na kuiunguza mioyo yao kwa simanzi. Mama Desmund alishindwa kulizuia chozi lake akaamua aliachie limdondoke aliguswa sana na maisha ya binti wake wa kazi.

ENDELEA NAYO....
"Sasa Dada mimi natoka kidogo, naelekea kanisani kwenda kumuona Baba paroko, nikamueleze kila kitu, kuanzia mwanangu alivyonifukuza na kunituhumu mimi mchawi, sitamficha hata yale maajabu niliyoyashuudia usiku, kumuona mwanangu Deus akiwa na zile kuwa walizomzika nazo. Naamini kiongozi wa kiroho atanisaidia." alizungumza Mamake Desmund.

"Sawa Bibi ufike salama!" Dada wa kazi alijibu.

Baada ya dakika kama thelathini kupita Mamake Desmund alikuwa amefika kanisani tayari, akamkuta mlinzi getini.
"Samahani kijana wangu, na shida ya kumuona Baba paroko!" alinena Mamake Desmund.

"Pita ukamuone, yuko ofisini kwake!" alijibu mlinzi kwa sauti ya upole sana.
"Tumsifu Yesu Kristo Baba paroko!" alisalimia Mama Desmund.

"Milele Amina Mama yangu, sijakuona karibia majuma mawili yamepita sasa kulikoni?" aliitikia salamu Padri James ambae ndie paroko wa parokia hiyo, alishangaa sana kwa kutokumuona Mama Desmund hasa katika misa za asubuhi.

"Baba paroko ni shida sana, na ndio maana nimekuja kwako, Dunia imenishinda! Dunia inazidi kuniadhibu vikali sana pamoja na uzee wangu wote huu, kama kulia nimelia sana, nilifikia hatua ya kutamani kujiondoa uhai, nimetukanwa sana Baba paroko, nimeaibishwa vya kutosha."

Mama Desmund kinywa kilikuwa kizito maneno hayakusikika vizur bali machozi yalikuwa yakimdondoka.

"Usilie nieleze kwanini unailaumu Dunia kipi kimekupata!" alihoji Padri James kwa sauti ya unyenyekevu iliyojawa na imani ya kanisa katoriki la Mitume.

Mama Desmund alijikaza na kumueleza Padri kila kitu, alisimulia jinsi watoto wake walivyofariki ghafla, akaeleza alivyoambiwa ni mchawi akafukuzwa na kijana wake manusura amchinje kwa kisu, akaelezea jinsi alivyomuona mwanaye usiku alidhoofu sana macho yake yalikuwa yameingia ndani, alivalia nguo alizizozikwa nazo, kumbukumbu hiyo iliibua upya kilio cha Mama Desmund.

""Yaani Baba paroko, mtoto niliyebeba mimba yake miezi tisa, nikajifungua kwa njia ya upasuaji nikatia saini kufa au kupona, akanyonya kifuani kwangu mwaka mmoja na nusu eti leo anapata ujasiri wa kunishikia kisu na kutaka kunia! Acha nilie Baba, nimefika kikomo cha uvumilivu, moyo umeshindwa kuyapokea maumivu hayo ni mazito yanauchoma moyo wangu!"

Padri James alimtuliza na kumsihi asiendelee kulia kisha akamwambia.

"Zaburi 50: 15 imeandikwa "Ukaniite siku ya mateso nitakuokoa na wewe utanitukuza" Nakuomba ujipe moyo, muite Baba wa mbinguni siku ya mateso yako mwambie akuokoe nawe utamtukuza, unapokaribia kukata tamaa ndipo Mungu anajifunua kwako na kukusaidia. Yohana 14 : 14 "mkiomba neno lolote kwa jina langu nitalifanya" hivyo naamini Yesu Kristo atafanya yote utakayoomba sasa katika jina lake lenye thamani"

Padri alimbariki Mama Desmund kisha akampa kijitabu kidogo kwaajili ya sara za kupambana na nguvu za giza, akamuahidi ipo siku wataongozana nae nyumbani kwake akaibariki nyumba nzima.

Mama Desmund kabla hajaondoka alielekea kikanisa kidogo akapiga magoti na kuanza kusali,

"Katika jina la yesu kristo wa Nazareth ninakuja kinyume na nguvu zote za giza dhidi yangu zinazokuja ndotoni. Ninayafunga na kuyatupa mapepo yote yanayonishambulia kwa njia ya ndoto, ninakuja kinyume na ndoto zote za kipepo dhidi ya maisha yangu. Ninaamuru moto wa Roho Mtakatifu kuwateketeza wote popote pale mlipojificha, angani nchini na baharini ninatumia damu ya Yesu Kristo kujifunika ili msiweze kurudi tena kwangu katika jina la Yesu, Amen."

Mama Desmund alikuwa anapinda kwenye ujia unaotoka kanisani akiunganisha barabara kuu, akilini alikuwa akiyacheua mafundisho na ushauri wa Baba paroko alipokwenda kwaajili ya kupata ushauri na chakula cha kiroho.

Licha ya akili yake kuzongwa na mawazo ya kuwapoteza wanaye aliowapenda, alitembea kwa uangalifu sana hasa kwa mwendo wake ule wa taratibu, kama kawaida yake alitembea kando kando mwa barabara. Hatua kadhaa mbele yake kulikuwa na kundi kubwa la waumini wenzake waliomtangulia kutoka kanisani ila wao walikuwa kwenye kikao cha upadrisho, alishtukia anapigwa kwa nguvu na kuangukia kwenye kidimbwi cha maji machafu.

Maumivu makali yaliuchoma mwili wake wote, alijitahidi kuinua kichwa chake kujua ni nini hasa kilichompata lakini wimbi kubwa la maumivu lilimzoa na kumkwamiza kidimbwini, kapotewa na fahamu.
********* ITAENDELEA ***********
 
MALKIA WA KUZIMU..... 14
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0622 738 310.

................................................................
SEHEMU YA KUMI NA NNE. .
( 14 )


ILIPOISHIA.....

Mama Desmund alikuwa anapinda kwenye ujia unaotoka kanisani akiunganisha barabara kuu, akilini alikuwa akiyacheua mafundisho na ushauri wa Baba paroko alipokwenda kwaajili ya kupata ushauri na chakula cha kiroho.
Licha ya akili yake kuzongwa na mawazo ya kuwapoteza wanaye aliowapenda, alitembea kwa uangalifu sana hasa kwa mwendo wake ule wa taratibu, kama kawaida yake alitembea kando kando mwa barabara. Hatua kadhaa mbele yake kulikuwa na kundi kubwa la waumini wenzake waliomtangulia kutoka kanisani ila wao walikuwa kwenye kikao cha upadrisho, alishtukia anapigwa kwa nguvu na kuangukia kwenye kidimbwi cha maji machafu.
Maumivu makali yaliuchoma mwili wake wote, alijitahidi kuinua kichwa chake kujua ni nini hasa kilichompata lakini wimbi kubwa la maumivu lilimzoa na kumkwamiza kidimbwini, kapotewa na fahamu.

ENDELEA NAYO......

Wakati huu watu waliokuwa mbele walishageuka na kutambua kilichokuwa kimetendeka, Mama Desmund alikuwa amegongwa na gari aina ya Escudo, mwenye gari akiwa bado ameshika usukani alijitahidi kupata upenyu wa kutoweka lakini walimuwahi.

"Ni ajari gani hii ya maajabu, niliona mbwa barabarani mara ikageuka na kuwa binti mrembo mrefu mweupe, kisha nikaona tena fisi, kumbe nimegonga binadamu, hakika sijawahi kushuhudia mauzauza haya tangia nianze kumiliki na kuendesha gari" alinong'ona kwa sauti ya chini dereva aliyemgonga Mama Desmund.

Wale waumini wengine walisimama mbele ya gari, dereva akalazimika kulisimamisha gari lake, gari liliendelea kuunguruma pasipo kuondoka. Dereva alitoka garini pole pole huku akiogopa kuchafuliwa na maji machafu yaliyokuwa pale chini.

Mama Desmund alikuwa akitokwa na miguno ya maumivu, gauni lake lilikuwa limeraruliwa, walimbeba na kumuweka ndani ya gari, mwenye gari alichukia sana aliona wanamchafulia gari lake sababu ndie aliyegonga ilibidi awe mpole tu, aliuendea ule mlango wa mbele wa gari lake na kuufungua shingo upande huku uso ukijaa ndita.

Aliwasha gari lake na kumwangalia tena Mama Desmund aliyekuwa akiguna kwa maumivu, alitia gia na kuling'oa gari lake haraka na kuwaachia waliokuwa nyuma matope yakiwarukia usoni, wengine wakawa wanatema chini matope yaliyopenya vinywani mwao, Walielekea hospitali iliyopo jirani.

Hali ya Mama Deamund ilizidi kuwa mbaya, ndani ya juma moja alikuwa kwenye chumba cha uangalizi maalumu, Desmund alipata taarifa za kuugua kwa Mamake lakini alikataa kufika akidai Mama yake ni mchawi hataki kumuona.

Mdada wa kazi aliendelea kupeleka chakula asubuhi, mchana na jioni, lakini baada ya majuma mawili kupita hakuonekana kupeleka chakula tena, kitendo hicho kilimuumiza sana Mama Desmund akaona hata huyo binti nae kamchoka nyakati hizi ambazo alikuwa akihitaji msaada wake zaidi.

Padri James alitafuta mtu akawa anafata chakula kanisani na kumpelekea Mama Desmund hospitalini kila siku, mpaka pale atakaporuhusiwa kutoka na kurejea nyumbani.

Hali yake ilizidi kuwa mbaya, mguu mmoja ulikuwa kaburini na mwingine Dunia, hakuwa wa kula wala kunywa, nafsi yake ilikata tamaa ya kuishi tena, Padri James akamtembelea hospitalini na kumpa upako wa wagonjwa kama ilivyo kawaida kwa wakatoriki.

Baada ya huduma hiyo ya kiroho aliyoipokea kutoka kwa Baba paroko, iliibua tumaini jipya kwa Mama Desmund, alianza kuzungumza japo kwa sauti ya chini, ile harufu ya kifo ikatoweka kwa mwendo wa kunyata.

Hali yake iliendelea vizuri wakamruhusu kurejea nyumbani, Padri James na Baadhi ya ndugu waliokuwa pale hospitali walimshika Mama Desmund wakampandisha kwenye gari ya Padri, kisha safari ikaanza haukuwa umbali mrefu sana, walitumia kama dakika kumi na tano.

Walipofika tu nyumbani walipokelewa na hatufu mbaya sana, ni kama kulikuwa na mzoga mahali pale, harufu ile iliwazidi ujanja kila mtu akawa ameiziba pua yake.

"Dada! Dadaaaaaa!" alipaza sauti Padri James akiwa anamuita yule mdada wa kazi lakini hakuitika.

"Dadaaaaaaaaa!" alirudia kuita tena lakini ikawa kama mwanzo binti huyo wa kazi hakuitika na milango ilikuwa imefungwa kwa ndani.

"Kaenda wapi tena huyu!" alinong'onga kwa sauti ya chini sana Mama Desmund.

Padri alipigia mafundi wake akawaelekeza anapoishi Mama Desmund ili wafike wabomoe mlango, baada ya dakika kama kumi na tano kupita, mafundi waliwasili wakiwa na vitendea kazi, wakaubomoa mlango.

Harufu kali ilifyatuka kama risasi kutoka ndani ya nyumba, awamu hii harufu iliongezeka maradufu, walipoingia wakakuta mwili wa Dada wa kazi juu ya kochi hakuwa yeye tena, alikuwa amefariki, uso wake ulikuwa umejikunja, mikono yake alikuwa ameikusanya kwa pamoja, mwili ulikuwa umeanza kuharibika, kilichomuua ni ugonjwa wa kihoro, mawazo ya kutokuwa na ndugu, kushuhudia mama yake na ndugu zake wakiuwawa hakuweza kusahau jinsi mama yake alivyolia huku akiwasihi majambazi kwamba, Mama ee! Msiniue! Nitafanya lolote mlitakalo!"

Wingu la simanzi na uwoga uliokithiri lilitanda nyumbani hapo, Mama Desmund kulia alishindwa akabaki anautazama tu mwili wa Dada wa kazi, awamu hii hakujali tena harufu bali aliduwaa akikumbuka wema na heshima aliyokuwa nayo mdada huyo wa kazi, machozi njia mbili mbili aliyaachia yamwagike yakalowanisha mashavu yake na kudondoka chini.

Polisi walifiki na kuutazama mwili huo wakaruhusu azikwe, angezikwa wapi hakuna aliyejua kwao wala hata ndugu yake, Mama Desmund akaamuru wamzike pale nyumbani kwake, walimzika pasipo sara yeyote ile sababu hakuwa na Dini ila aliamini uwepo wa Mungu katika maisha yake.

Baada ya chakula cha jioni Desmund alifunga mlango kwa ufunguo akarudi mezani kuendelea kuzungumza na mkewe, lakini moyoni hali yake ilianza kubadirika. Hofu ilimwingia, Moyo wake ulianza kudunda. "Hivi naogopa nini?" alijiuliza mwenyewe. "Naogopa kulala? Hapana siwezi kuogopa kisa ndoto za ajabu!"

Nje hali ya hewa ilikuwa imeanza kubadirika. Upepo mkali ulianza kuvuma kutoka baharini. Ilipofika saa nane kamili za usiku mambo yakabadirika sauti za bundi juu ya paa na milio ya paka karibu na mlango ilisikika, kumbe ilikuwa ni ishara ya kumuamsha Janeth.

Upande aliokuwa amelala Janeth alitokea paka mmoja mnene, mwenye rangi nyeusi!, alijawa na manyoya mengi sana! kila alipokanyaga aliacha alama alikuwa na kishindo kizito mpaka nyumba ikawa inatikisika kila alipokuwa akipiga hatua moja kwenda mbele.

Paka yule alikuwa na ujumbe umeandikwa kwenye kiganja cha binadamu, " Damu ya huyo mumeo inahitajika kule kuzimu ili uongezewe nguvu na muda wa kuendelea kuwa malkia" Janeth alishusha pumzi taratibu baada ya kuusoma ujumbe huo, hakutaka kuupoteza umalkia wake mara moja alianza kazi. Aliinuka akakataa nywele za mumewe na kumpa yule paka kisha akatoweka, kitendo hicho kilimaanisha kwamba tayari Janeth kamkabidhi Mumewe katika utawala wa kuzimu.

Jua lilikuwa limekwisha chomoza, mionzi yake iliweza kupenyeza vyema mpaka chumbani mwa Desmund, Ndipo Janeth akakurupuka usingizini haraka na kuanza kumuamsha mumewe ili ajiandae kwenda kazini.

Desmund aligoma kuamka, "Naumwa, tazama ninavyochuruzikwa na jasho, mapigo ya moyo yanakwenda kasi sana," Desmund alizungumza kwa shida.
Janeth aliangaika huku na kule akitafuta dawa za kutuliza maumivu, Janeth alijua wazi kwamba mambo ya kumtoa kafara Desmund yamekwishaanza, hakutaka kuonekana kwamba anahusika.

"Mke wangu kichwa kinauma, tumbo linakata, nashindwa kupumua nipeleke hospitali, nakufa mimi hapa jamani!" alilalamika kwa maumivu makali sana Desmund.

"Hospitali hawatoi huduma nzuri, nakuletea dawa hapa hapa nyumbani" alijibu Janeth akiwa ameikunja sura yake kwa dharau.
 
MALKIA WA KUZIMU..... 15
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0713 417 189
0622 738 304.



................................................................
SEHEMU YA KUMI NA TANO. .
( 15 )


ILIPOISHIA.....

Janeth aliangaika huku na kule akitafuta dawa za kutuliza maumivu, Janeth alijua wazi kwamba mambo ya kumtoa kafara Desmund yamekwishaanza, hakutaka kuonekana kwamba anahusika.

"Mke wangu kichwa kinauma, tumbo linakata, nashindwa kupumua nipeleke hospitali, nakufa mimi hapa jamani!" alilalamika kwa maumivu makali sana Desmund.

"Hospitali hawatoi huduma nzuri, nakuletea dawa hapa hapa nyumbani" alijibu Janeth akiwa ameikunja sura yake kwa dharau.

ENDELEA NAYO.....

Janeth akiwa bado anazungumza alisikia mlango ukigongwa alipofungua anakuta ni Manumbu rafiki yake na Desmund.

"Aisee mbona hali ya rafiki yangu inatisha sana!" Manumbu alinena baada ya kumuona rafiki yake akiwa hawezi hata kuzungumza.

"Ugonjwa gani tena huu wa ghafla au Mamake anazidi kumuandama mpaka amuue kabisa" alijiuliza Manumbu pasipokupata majibu.

"Shemu naomba nimpeleke huyu mtu katika tiba za kienyeji huu sio ugonjwa wa kawaida." aliomba Manumbu.

"Usihangaike tu shemeji yangu tutamtibia hapa hapa nyumbani na atapona tu, sina amani katika moyo wangu, sili wala sinywi pindi nimuonapo kipenzi changu akiwa kitandani anaugulia maumivu makali" alizungumza Janeth huku akiwa anamfuta Desmund jasho ambazo zilikuwa zikimchuruzika kwa kasi kama bomba la maji.

Manumbu alionesha wazi kutokukubaliana na Janeth, alinyamaza kimya takribani dakika kumi kisha akafungua kinywa chake na kuanza kuzungumza,

"Shemeji kuna mganga nimemwambia afike hapa saizi aje amsaidie rafiki yangu, tukizubaa anapoteza uhai"

"Sawa shemeji, fanya hivyo" alijibu Janeth, alijiamini sana maana anajua hata aje mganga kutoka ulaya hawezi kumuokoa Desmund, kuzimu walikuwa wameishakamilisha kila kitu hivyo Desmund yupo katika mateso yake ya mwisho kabla ya kufariki katika Dunia ya kawaida na kuelekea katika ulimwengu wa kuzimu.
Mganga alikuwa tayari amefika, Janeth akamkaribisha mpaka ndani, aliachia tabasamu hafifu ili wasiweze kugundua kwamba kuna kitu kinachoendelea.

"Najua tu baada ya rafiki yangu kufanikiwa kimaisha, imesababisha walimwengu kumuonea kijicho yeye pamoja na mkewe. Wameamua kumfanyia hila kwa kumtesa na kumtupia gonjwa lisilojulikana" alinong'ona Manumbu kwa sauti ya chini kabisa.

Ndani ya siku tatu Desmund alikuwa amekonda kama sindano na kubaki mifupa tu, huku akiwa amenyonyoka nywele karibu zote kichwani, na zile zilizobaki kuwa kavu kama kamba za katani, alikuwa akiharisha.

Kwa hakika huu ulikuwa ugonjwa mmoja wa ajabu ambao mganga alikuwa hajaushuhudia kabla. Lakini kamwe asingeweza kukiri mbele ya mteja wake kwamba alikuwa mbumbumbu kuhusu ugonjwa huo. Hakuwa mgonjwa kiasi hicho ati!
Akaonesha juhudi kubwa katika kutumia tunguri na kibuyu kikubwa. Alichukua wembe akamchanja Desmund, kisha alianza kunuiza maneno ambayo hata yeye mwenyewe asingeyakumbuka, akamuwekea hirizi kichwani huku akiwa anamzunguka.

Hatimaye mganga alikuwa amemaliza uganga wake, alimfungashia mzigo mkubwa wa miti, majani, na mizizi ya kuchemsha, kufukiza na kupaka waliagana na Manumbu kisha mganga akaondoaka zake.

"Kichwa kinawaka moto, mwili mzima unachomachoma, hakika navuta pumzi za mwisho, uhai wangu u mashakani, naondoka, namuacha na nani mke wangu?, rafiki yangu Manumbu maumivu ni makali sana, oii! Kifua kinabana, mama kaniua, Mama kaniua, Aaah nakufa! Nakufa jamani" Desmund alizungunza kwa shida sana mwili mzima ukiwa unatetemeka hakuwa na nguvu hata ya kukiinua kichwa chake.

"Usilie rafiki yangu, piga moyo konde uyashinde majaribu ya Dunia, huyu mganga alieondoka hapa naamini kabisa dawa zake zitakutibu vyema. Kabisa" alinena Manumbu kwa sauti ya upole akiwa anaifunika miguu ya Desmund kwa shuka lililolowa kwa jasho.

""Usinipe moyo rafiki yangu Manumbu, usiku nimeota nikiwa nazikwa nilipiga kelele lakini haikusikika, nikasali lakini Baba wa Mbinguni akagoma kupokea maombi yangu, basi nikayafumba macho ili nikisubiri kifo changu, yaani aliyenizaa ndie anayeniua"

Ghafla Desmund kinywa kilikuwa kizito, damu nzito ikawa inamtoka mdomoni, ilivyokata alianza kutapika nywele za binadamu, kucha na kipande kidogo cha ngozi haikufahamika ni ya mnyama gani. Nguvu zikamuishia sababu ya kutapika mfululizo,

"Mungu wangu mbona umeaniacha!, kama umeridhia niondoke kwa maumivu haya, asante sana Baba," Desmund alipomaliza kuzungumza maneno hayo, alimuangalia mkewe kisha akayafumba macho yake, akatulia tuli hakutikisika tena.


ITAENDELEA.......
 
MALKIA WA KUZIMU..... 16
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0713 417189.
0622 738 310.
TANGA..

................................................................
SEHEMU YA KUMI NA SITA. .
( 16 )


ILIPOISHIA.....


""Usinipe moyo rafiki yangu Manumbu, usiku nimeota nikiwa nazikwa nilipiga kelele lakini haikusikika, nikasali lakini Baba wa Mbinguni akagoma kupokea maombi yangu, basi nikayafumba macho ili nikisubiri kifo changu, yaani aliyenizaa ndie anayeniua"
Ghafla Desmund kinywa kilikuwa kizito, damu nzito ikawa inamtoka mdomi, ilivyokata alianza kutapika nywele za binadamu, kucha na kipande kidogo cha ngozi haikufahamika ni ya mnyama gani. Nguvu zikamuishia sababu ya kutapika mfululizo,
"Mungu wangu mbona umeaniacha!, kama umeridhia niondoke kwa maumivu haya, asante sana Baba," Desmund alipomaliza kuzungumza maneno hayo, alimuangalia mkewe kisha akayafumba macho yake, akatulia tuli hakutikisika tena.


ENDELEA NAYO.....

Wingu la simanzi lilitanda ndani ya nyumba hiyo, upepo wa maumivu ukazidi kuvuma huku na kule, mvua ya majonzi ikashuka na radi za mfadhaiko ndani ya mioyo zikaendelea kupiga kwa kupokezana.
Hakuna mtu aliyekuwa tayari kuzungumza kwa wakati huo, Manumbu alisimama na kuanza kuzunguka ndani kama mtu aliyechanganyikiwa, alikiuma kidomo chake cha chini huku machozi yakimdondoka, macho ya hudhurungi ya Janeth yaliuangalia uso wa mume wake pasipo matumaini yeyote ya kuamka tena.

Manumbu alishika simu yake ya mkononi na kuanza kupekua namba zilizopo katika simu, lakini hakuona namba aliyokuwa akiitafuta, kijasho chembamba kilichokuwa kikimchuruzika kwapani kilisababisha shati lake kulowa makwapani. Alikuwa akizungumza mwenyewe maneno yasiyoeleweka.

Akamfunua Desmund shuka, akastaajabu kuona midomo imekuwa miekundu kama ini, hakika alikoswa jibu, akashika tena simu yake atafute dereva tax aje amchukue Desmund wamkimbize hospitali lakini Janeth aligoma.

"Unajisumbua shemeji yangu huoni kama huyo mtu itakuwa kafariki tayari, tufanye mpango wa kumpeleka mochwari" kauli hiyo kutoka kwa Janeth ilimshtua sana Manumbu, moyo ulimpapa na kumtweta, akapiga funda la mate machungu huku machozi yakimeremeta machoni kwake.

Manumbu alisogea pale alipolala mgonjwa akamshika kifuani ili ajue kama mapigo ya moyo yamesimama au laa..!
"desmuuuuuuuuuuuund" Manumbu alipaza sauti kwa uchungu sana.

Manumbu uchungu usioelezeka ulimshika, kwa kuamini kwamba rafiki yake ni mfu sasa, aliwaza jinsi walivyopendana na kucheza pamoja. Akakumbuka jinsi walivyoleteana njugu wakiwa shule ya msingi kibaha uko mkoani pwani.

Kumbukumbu ilizidi kumtesa, aliyafumba macho yake, akavuta picha siku ya Harusi yake, Desmund alijitolea, alinunua mchele, ng'ombe, soda na usafiri kwa ajili ya wageni waalikwa, alijitolea sana kwa rafiki yake.

Manumbu alizidi kulia, akajisemea kwa sauti ya chini, "Mateso ya rafiki yangu ni kama yale ya Mzee Ayubu wa kwenye Biblia!"

Walishangaa kuona Desmund akiamisha mkono wake na kuusogeza kifuni, kumbe alikuwa amepoteza fahamu, na wakati huo fahamu zilianza kurejea taratibu, na mapigo yake ya moyo yalikuwa chini kabisa. Aliyambufua macho yake yakiwa yamevimba.

"‘Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika mavumbi ya mauti” alizungumza Desmund kwa sauti ya chini sana uku machozi yakimdondoka, kumbe maneno hayo alikumbuka alipokuwa mtumiakiaji kanisani alipewa kusoma soma lililotoka katika kitabu cha Zab 22:15.

Maneno hayo aliyazungumza Yesu Kristo
kuonyesha kuwa alikaukiwa na maji mpaka mdomo wake ukawa mkavu kiasi cha ulimi wake kuganda kwenye taya zake.. Na ndio maana akasema nasikia kiu. Lakini pia sababu nyingine ya pili ambayo ni ya rohoni, ilikuwa ni kuonyesha kuwa sasa shughuli yote imekwisha, ni wakati sasa wa kunywa, maadui wamekwisha shindwa. Sikuzote kiu huwa kinakuja baada ya kufanya kazi Fulani ngumu ya kuchosha,au mazoezi "

Kitendo cha Desmund kufungua kichwa chake na kuzungumza japo ilikuwa ni kwa shida Janeth alichukia sana kwa sababu siku alizopewa kumuua Desmund zimekaribia kufika.
Janeth alisimama akaelekea bafuni akachukua nguo ya ndani ya mumewe, akailoweka kwenye kibuyu cha damu na kuanza kuikamua nguo ile.

" Ooooh! Nanyongwa shingo, nakufa mimi, shingo inauma! Manumbu rafiki yangu nanyongwa shingo mimi uwiiii" maumivu yalizidi Desmund akawa anajitahid kuishika shingo yake ili atoe kitu kinachomnyinga.

Kumbe Janeth alivyokuwa akikamua ile nguo ya ndani alikuwa anamnyonga mumewe ili ammalize mapema.
"Shemejiiiiiiiiii! " Manumbu aliita.
" Abeeeee..!!" aliitika Janeth akakurupuka kutoka bafuni akarejea upesi katika kile chumba alicholala mgonjwa.

Desmund alikuwa ameyatumbua macho yake kama kiumbe kilichofia kwenye matope. Manumbu alishindwa kuvumilia akainama kwenye kifua cha Desmund akiwa analia nakusema...

"Rafiki yangu amka nikusimulie maumivu ambayo sikuwahi kukwambia na ndio chanzo cha mimi kuanza mambo ya kwenda kwa waganga na kulisahau kanisa"
" Niliumia sana moyoni kiasi cha kutamani kufa, hasa pale nilipoingia chumbani usiku, nikaiona sura ya mwanamke katika kioo. Sikuweza kuutambua uso huo kwa haraka uliokuwa ukinitazama, lilikuwa jambo la ajabu."

"Nilipoiangalia sura ile vizuri niligundua ni marehemu mke wangu niliyemzika miaka mitatu iliyopita. Kisha akatoweka ghafla Anna wangu! Niliduwaa, nikapiga yowe la uchungu hakuna aliyenisikia, nikapanda kitandani nikiwa na majonzi zaidi kuliko siku zote za maisha yangu"

"Nilihisi kana kwamba sikustahili kuishi, sina faida! Yaani mimi Manumbu. Juhudi zote nilizofanya pamoja na kumtunza, vyote ni bure."

Manumbu alikuwa kama kapandwa na wazimu alipoona Desmund aonyeshi dalili zozote zile za kumsikiliza alimtikisa uku akimwambia..

"Nilijiuliza nitaendelea vipi kuishi bila Anna wangu, jibu sina. Hasira ilizidi kunipanda pindi niliposikia sauti ya mke wangu akiimba ule wimbo ambao alilkuwa akiniimbia ninapokuwa na huzuni."

"Nikamlaumu Baba wa Mbinguni kwa kuniweka katika hali ya kumfanya Anna kuwa kitu cha maana kuliko vyote Duniani. Nililia ili kutoa hasira yangu, mpaka leo mke wangu sijamuona tena, jaman,i sijui kama Anna alifariki kweli au laa? Ila Dunia, Wewe Dunia uliamua kunichukulia usingizi wangu, malkia wangu, kipenzi changu, moyo wangu. Wapi na lini nitaonana tena na Anna wangu, jibu sina."

Maumivu ya uchungu yalimzidia Manumbu akashindwa kuendelea kuzungumza, machozi njia mbili mbili aliyaachia yamwagike yakalowanisha mashavu yake na kudondoka kwenye kifua cha Desmund alichokuwa ameegesha kichwa chake, Manumbu akapoteza fahamu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom