Simulizi: Malkia wa kuzimu-01

Simulizi: Malkia wa kuzimu-01

0713417189

Senior Member
Joined
May 12, 2021
Posts
115
Reaction score
201
MALKIA WA KUZIMU..... 01
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0622 738 310.
TANGA.

SEHEMU YA KWANZA

Baada ya miaka mingi kupita, bado alizidi kuikumbuka historia Mbaya na Chungu, Katika Maisha yake. Achia mbali alivyosumbuliwa na maradhi ya ajabu akiwa shule ya msingi.

Akavuta Picha Jinsi wazazi wake walivyopambana kuhakikisha anapata mahitaji yake. Alitabasamu Kidogo, alivyowakumbuka wale mabinti waliomkataa kipindi kile akiwa anasoma chuo kikuu cha Dar -es- Salaam.

Ni kijana mtanashati, mwenye kujua kupangilia mavazi yake. Mwenye urefu wa futi sita na nchi moja, mweusi kiasi ndio sifa yake kubwa, kifua chake kipana kutokana na mazoezi ya kuinua vyuma vizito. Alifahamika kwa jina la Desmund.

Kwa wafanyabiashara wakubwa wa Jijini Dar - es - Salaam, jina ilo sio geni katika masikio yao au wakazi wa mtaa wa masaki.

Kumbukumbu hiyo ya kuumiza ilipenya katika kichwa cha Desmund, akiwa ameketi sebuleni akitazama runinga.

"Mmh! Unawaza nini kipenzi changu? " aliuliza Janeth ambaye ni mkewe Desmund.

"Mmh" aliguna kidogo kisha akazungumza, "Unajua sisi wanaume tuna mambo mengi, hakika maandiko hayakukosea kwamba tutakula kwa jasho, na kuna wakati Dunia inatuelemea, pia zipo nyakati tunakata tamaa kabisa ya kuendelea kuwa hai. "

"Sasa mume wangu! Jumba lote ili bado unayawaza maisha kweli? " alidakia Janeth ila Desmund hakujibu neno lolote lile, bali aliachia tabasamu uku akitikisa kichwa.

Janeth nae aliponyokwa na tabasamu pana lisilo kifani. Akambusu mumewe katika paji la uso, akaelekea jikoni kuendelea na majukumu yake.

"Hakika nilipata mwanamke, siishiwi hamu ya kumtazama, kila siku anazidi kuwa binti mdogo, tazama hata kifua chake kilivyo chanua, kimepambwa na titi changa. Aisee ndio maana wivu hauniishi" alinon'gona Desmund kwa sauti ya chini, akacheka mwenyewe kana kwamba alikuwa akizungumza na mtu.

Ukiachilia mbali uzuri wa sura yake nyembamba, urefu wa sentimita 160, rangi yake nyeupe inamtambulisha vyema Janeth kwamba ni toto la kinyatulu kutoka mkoani singida. Ukiitazama pua yake ndogo imejichonga vizuri kama kito cha dhahabu, akikutazama usoni ni kama anakukonyeza, ilo ni jicho lake la hudhurungi, kubwa kiasi na la mviringo, lenye mng'aro wa aina yake ukifananisha na golori utakuwa hujamtendea haki Janeth.

Kwa wacheza pulutebo mnajua ulaini wa kitambaa kile basi ndivyo ilivyo ngozi yake, yaani ni nyororo, maji yanatereza tu kana kwamba yanatoka kilimani. Makalio yake sio madogo wala makubwa, ila mtikisiko wake nafuu ya tetemeko la ardhi, kwa uzuri huo wa Janeth ni haki Desmund awe na wivu kwa mkewe.

"Janeth!"

"Abee mume wangu! "

"Naona kiubaridi kinapuliza sana leo? "
"Siunaona huu ni msimu wa mvua.! "

"Kweli mke wangu joto lilizidi. "
Janeth alitabasamu kidogo kisha akasema..

"Sasa jamani joto kwa hapa Dar -es- salaam ni kawaida kabisa. "

"Ndio natambua ilo lakini ili lilizidi mpaka nikadhani uko juu angani kuna watu wanachochea kuni aisee. "

Jibu ilo kutoka kwa Desmund lilimfanya Janeth aangue kicheko mpaka akajikuta amekaa chini.

"Sasa mke wangu andaa chakula nile nilale."
"Usijali una njaa sana eeh? "

"Sio sana, ila chakula chako kitamu. "

"Hahahahahahah!!," alicheka sana Janeth kisha akazungumza ..

"Mwanamke mapishi, nisipopika vizuri ukapikiwa uko nje unaweza ukaniacha."

" Wee! Siwezi kukuacha Malkia wangu wa pekee, jinsi wanaume wengi wanavyokutamani, mimi ni wako yaani Daima na hata Milele. "

Janeth alianza kuzipiga hatua kuelekea jikoni, alipofika aligeuka nyuma ili aone mumewe anafanya nini. Akaona Desmund kainamisha kichwa chake akisoma gazeti la habari za michezo, basi Janeth alisimama katikati kisha macho yake yakabadirika ghafla na kutoa mwanga mweupe, ndipo wakatokea wasichana wanne wenye sura kama ya Janeth. Wakaanza kumsaidia kazi ya kupika, mmoja alikaanga samaki, mwingine akapeta na kuosha mchele, lakini mmoja alisimama mlangoni na kutazama kule alipokuwa ameketi Desmund.

Baada ya dakika ishirini chakula kilikuwa tayari, wale wasichana wengine wakasogea pembezoni mwa ukuta kisha wakatoweka, akabaki Janeth mwenyewe anabeba vile vyakula vilivyopikwa na kupeleka katika meza ya chakula.

"Aisee ndio maana nakuaminia!," alizungumza Desmund.
"Kwanini mume wangu? "

"Unakwenda na muda sana kana kwamba umefungwa mashine katika mikono yako."

"Hahahahahahah..!!!!" alicheka sana Janeth kisha akajibu " Natambua wajibu wangu kama mwanamke," "Hapo sibishi mahabuba wangu." alidakia Desmund.

"Mmh! mbona chakula cha leo kitamu hivi?," aliuliza Desmund. "Na kati ya siku ambazo sijapika vizuri ni leo." alijibu Janeth uku akitabasamu.

"Una mbwembwe mke wangu, chakula kitamu hivi kisha unasema hujapika vizuri" alizungumza Desmund uku akiwa anabugia kipande cha samaki aliyekaangwa.

Desmund hakuelewa nini kinachoendelea, wingu zito lilikuwa limetanda katika mboni za macho yake. Penzi la Janeth lilimlevya, alikuwa asikii wala haoni.

Hatimaye Desmund alikuwa amemaliza kula chakula, akaelekea bafuni akaoga kisha akajitupa kitandani, ni sababu ya uchovu wa siku nzima. Janeth nae alielekea kitandani kwaajili ya kwenda kupumzika.

Wakiwa kitandani walizungumza uku wakicheka, Janeth akatumia muda huo kumpapasa Desmund hasa katika kile kifua kikubwa na kipana, akakilaza kichwa chake juu ya kifua hicho, hakika mahaba moto moto yalitawala juu ya kitanda.

Janeth aliinua kichwa chake akampuliza Desmund usoni, na hapo ndipo usingizi mzito ulimpitia akaanza kukoroma. Janeth alianza kubadirika taratibu mpaka akawa joka kubwa lenye rangi nyeusi. Joka ilo likaanza kujikunja katika mwili wa Desmund.

------------- ITAENDELEA ---------------///
FB_IMG_1622739579357.jpg
 
MALKIA WA KUZIMU..... 02
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0622 738 304.
TANGA.



SEHEMU YA PILI
( 02 )

ILIPOISHIA.....

Wakiwa kitandani walizungumza uku wakicheka, Janeth akatumia muda huo kumpapasa Desmund hasa katika kile kifua kikubwa na kipana, akakilaza kichwa chake juu ya kifua hicho, hakika mahaba moto moto yalitawala juu ya kitanda.

Janeth aliinua kichwa chake akampuliza Desmund usoni, na hapo ndipo usingizi mzito ulimpitia akaanza kukoroma. Janeth alianza kubadirika taratibu mpaka akawa joka kubwa lenye rangi nyeusi. Joka ilo likaanza kujikunja katika mwili wa Desmund.

ENDELEA NAYO....

Nataka kuwa jambo la maana sana kwako Janeth wangu, hakika wewe ni Dunia yangu. Kila mahali nikiangalia ninakumbushwa upendo wako."

"Amini kwamba mimi ni wako, joto lako pengine siwezi lipata, peke yangu bila wewe sina maisha mwenzio. Upendo ni kama upepo, huwezi kuuona lakini unaweza kuhisi hivyo. Leo najua upendo ni nini ni kwasababu yako Janeth. Ewe kipenzi changu, asante daima kwa kuwa upinde wangu baada ya dhoruba ya mapenzi. Nakupenda saaaana mpenzi wangu wa daima na hata milelele."

Maneno hayo alikuwa akiyazungumza Desmund katika ndoto nzito, alihisi kwamba kakumbatiwa na mkewe kumbe ni joka kubwa likiwa limejizungusha katika mwili wake.

Wakati mauzauza hayo yakiendelea wasichana wawili walijitokeza mbele ya kitanda alicholala Desmund. Walikuwa na nywele ndefu zinagusa mpaka chini, jicho moja kubwa likiwa kwenye paji la uso, ila walikuwa na meno mawili marefu yaliyojaa damu, urefu wao hauwezi kuelezeka kwamba ni mita ngapi, hakika viumbe hivyo vilikuwa vinastajabisha.

Wasichana hao walikuwa wamebeba jeneza lililopambwa kwa dhahabu tupu. Janeth alibadirika tena kutoka katika umbo la nyoka na kufanana na wale mabinti wawili, wakati Janeth anabadirika nyumba nzima ilijaa mwanga mkali uliotoka ndani ya jeneza lile la dhahabu.

Desmund akiwa kitandani alianza kujigeuza huku na kule, lakini hakuweza kuamka kwa wakati ule kutokana na upepo ambao alipuliziwa na mkewe. Basi mabinti wale wawili walimvuta Desmund kutoka kitandani, kisha wakamlaza ndani ya jeneza. Wakati wakifanya hivyo Janeth aliangua kicheko kizito nyumba ilitikisika, radi kali ikapiga wakati hakukuwa na dalili yeyote ile ya mvua kunyesha uko nje.

Mabinti hao pamoja na Janeth walipiga magoti kuzunguka jeneza ilo wakaanza kunywa damu iliyokuwa ndani ya kibuyu. Iliyobaki wakamwaga ndani ya jeneza, walianza kuimba nyimbo zisizoeleweka, ghafla zikasikika sauti za watoto wachanga wakilia ndani ya jeneza ilo. Kitendo cha kumfanyia vile Desmund ni kwamba walikuwa wanamuweka katika himaya ya kichawi, kila neno atakalolisema Janeth basi lisiwepo pingamizi la aina yeyote ile.

Janeth alisogea katika lile jeneza akalinyooshea kidole wale mabinti wakatoweka pamoja na lile jeneza ila Desmund akarejeshwa kitandani.

"Mke wangu leo nimeamka mwili unauma sana!"

"Ooh pole sana mume wangu itakuwa ulilala vibaya" alijibu Janeth.

"Mmh!" aliguna Desmund kisha akaendelea kuzungumza, "mbona kila siku hii ndio staili yangu ya kulala."

"Basi itakuwa ni uchovu tu mahabuba wangu, uwe unafanya mazoezi." alikazia Janeth.

"Mazoezi mbona nafanya lakini nimeota ndoto za ajabu sana!" alizidi kusisitiza Desmund.

" Usiamini katika ndoto hazina ukweli wowote ule."

Janeth alimshika mkono mumewe akamsindikiza mpaka bafuni, mabusu ya mahaba yakitawala kwa wakati huo. Baada ya Desmund kumaliza kujiandaa alimuita mkewe aliyekuwa jikoni ili aweze kumuaga ndipo aelekee kazini.

"Mimi naenda mke wangu ila mbavu zinauma sana, kama nilikuwa nabanwa na kitu."

"pole sana utapona eti? "

" Sawa kipenzi acha niende kazini."

"Mwaaaaah nakupenda Desmund wangu."

Hakika mwili wa Desmund ulitawaliwa na maumivu, sababu ya heka heka zile alizofanyiwa usiku. Kwa jicho la kawaida hakuweza kugundua kinachoendelea baina yake na mkewe.
Desmumd akiwa kazini alisikia simu yake ya kiganjani ikiita alipotazama akakuta ni mamake ndie anapiga.

"Hallo! "

" Shikamoo Mama,"

"Marahaba mwanangu, habari za uko mjini?"

"Huku tu wazima ila nina mafua yananisumbua,"

" Pole sana mama yangu,"

"Asante sana mwanangu! Nimekupigia simu ili nikwambie kwamba mdogo wako Baraka amehitimu kidato cha nne, kila siku ananisumbua kwamba nimlete hapo katikati ya jiji la Dar - es - salaam, sasa leo mimi namtuma kwenye gari sawa mwanangu? "

"Kwa ilo usijali mama yangu! angalau pale nyumbani patachangamka, tulikuwa tunashinda wapweke hasa siku ambazo siendi kazini."

Mamake Desmund alitabasamu baada ya jibu ilo kisha akasema.. "Ubarikiwe saaaaana mwanangu, naona kasalio nako kameniishia" kabla mamake hajamaliza kutamka neno la mwisho simu yake ilikuwa imekata tayari. Lakini mambo ya msingi walikuwa wamekwisha yazungumza hapo awali.

"piiiiiii..!! Pipipiiiiiiii...!! " ulikuwa ni mlio wa gari uliosikika nje ya geti.

"ooh! Karibu mume wangu," alizungumza Janeth.
"Nimepiga oni muda mrefu ulikuwa wapi? "

"Nilikuwa jikoni jamani."

Desmund alishuka ndani ya gari akiwa na mdogoye aliyefahamika kwa jina la Baraka. Janeth alifurahi sana, akampokea mgeni, wakaingia mpaka ndani. Akaoneshwa chumba chake atakachokitumia kwa wakati wote atakapokuwa hapo kwa kakake.

Baada ya wiki tatu kupita Baraka alikuwa ameishayazoea mazingira, majirani walimpenda hasa kwa ile rangi yake nyeusi tiiii!, wakampachika jina la cheusi mangara, alikuwa akitabasamu tu.

Watu hao watatu walifurahi sana, furushi la tabasamu lilisheheni katika nyumba hiyo. Walicheka pamoja ikawa silaha pekee ya kutokomeza chuki, kiburi, hasira na kila lililobaya.

"Mamaaaaa! Mamaaa! Nakufa! "

"Mama hiki nini? " alipaza sauti Baraka kwa uchungu, wakati huo upepo mkali ulikuwa ukivuma ndani ya chumba chake, madirisha yakifunguka yenyewe na kujibamiza kwa kishindo kisicho cha kawaida!, sauti za bundi nazo zilisikika pembezoni mwa chumba hicho. Kumbe alikuwa ni Janeth akiwa katika sura ya tofauti, meno mawili marefu yaliyochongoka!. Alisogea mpaka pale alipolala Baraka akaishika shingo akaing'ata na kuanza kunywa damu. Maumivu yalimzidia akazidi kupiga kelele.

"kaka! - Kaka! - Kaka! naumia!"

Desmund alikurupuka kutoka usingizini baada ya kusikia kelele za maumivu alizokuwa akipiga mdogo wake.

"Baraka! Baraka! umekuaje?"

" wewe Baraka!"

Baraka alikuwa ameyatumbua macho yake, jasho likimchuruzika, hakuweza kuzungumza bali alikuwa akimtazama tu kakake usoni, Desmund moyo ulimpapa na kumtweta.



-------- ITAENDELEA----------
FB_IMG_1622739579357.jpg
 
MALKIA WA KUZIMU..... 03
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0622 738 310.
0713 417 189.
TANGA.

................................................................
SEHEMU YA TATU
( 03 )


ILIPOISHIA.....
kaka! - Kaka! - Kaka! naumia!"
Desmund alikurupuka kutoka usingizini baada ya kusikia kelele za maumivu alizokuwa akipiga mdogo wake.
"Baraka! Baraka! umekuaje?"
" wewe Baraka!"
Baraka alikuwa ameyatumbua macho yake, jasho likimchuruzika, hakuweza kuzungumza bali alikuwa akimtazama tu kakake usoni, Desmund moyo ulimpapa na kumtweta.

ENDELEA NAYO.......

"Janeth! Janeth! amka tumkimbize huyu hospitali."
"mimi nina usingizi wewe nenda." alitamka Janeth.

Gari iliwashwa haraka, Baraka akapakizwa kisha safari ikaanza kuelekea kituo cha afya cha temeke. Baada ya dakika thelathini kupita walikuwa wamefika, wakapokelewa vyema na wauguzi waliokuwa zamu, na uchunguzi ukaanza.
"Huyu mbona kaishafariki tayari!" alisema Daktari.

"what! unasema? " aliduwaa Desmund.
"inamaana kafia njiani? "

"Ndio alikuwa hana damu hata kidogo,"
alizungumza Daktari kisha mwili wa marehemu ukapelekwa mochwari. Desmund alikiuma kidomo chake cha chini huku machozi yakimdondoka.

"Nimekukosea nini mdogo wangu? mpaka uondoke ghafla kiasi hiki! umeuchoma moyo wangu! huzuni kubwa imenigubika, nitamueleza nini mama? Nitatumia lugha gani? nitaanzaje masikini ya Mungu, hapana mdogo wangu usinifanyie hivyo."
Desmund alishindwa kuendelea kuzungumza, machozi yalizidi kumbubujika bila simile, kilio kisicho na mwisho, kilio kisichopozeka kilisikika kutoka kwake.

Majirani walijitokeza kwa wingi nyumbani kwa Desmund kwa lengo la kutoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lililohifadhiwa mwili wa marehemu, kisha safari ielekee pwani kwaajili ya mazishi. Kila mtu alikuwa anazungumza lake juu ya kifo cha Baraka.
"huyu kijana kamtoa kafara mdogo wake" alisema jirani wa kwanza.
"kisa tu utajiri wao uzidi kuimalika huo ni ushetani." alifoka jirani wa pili.
"mnauhakika au mnaropoka tu" alidakia jirani wa tatu, alikuwa ameketi pembeni yao akiwasikiliza. Kimya kilitawala hakuna aliyetoa jibu, wale majirani mawili waliibetua midomo yao kwa dharau kisha wakasimama na kwenda kukaa mahali pengine.

"Mbona Dunia chungu hivi! walimwengu kipi mnataka mpewe ili mtumie ndimi zenu vizuri kunena yale mlio na uhakika nayo. Nimuue mtu nimpendaye kweli!?, oneeni huruma chozi linalonidondoka nami ni binadamu kifo kinauma jamani." alijisemea mwenyewe Desmund kwa sauti ya chini kabisa uku akiwa anapita mbele ya jeneza kutoa heshima ya mwisho kabla ya safari kuanza. Uvumilivu haukuwa upande wake aliangua kilio kizito kilichowatoa machozi majirani.

Hatimaye msafara uliokuwa unasafirisha mwili wa marehemu ulikuwa umefika pwani nyumbani kwao na Desmund.
"mmemfanya nini mwanangu?" alihoji mamake machozi yakimdondoka.
"Dunia kwanini umeamua kuniumiza kiasi hiki? nilimsindikiza mwanangu akiwa mzima, eti leo mnanirejeshea akiwa mfu." alizungumza mamake Desmund kwa majuto na uchungu mkubwa akiwa kama mzazi.

"Desmund.. Desmund.. " ilikuwa ni sauti ya mamake ikimuita.
"naam mama." aliitika kwa sauti hafifu sana. "umemfanyaje mdogo wako - mwanangu? ni bora angeugua ningemuuguza pasi kuchoka, eti leo mnaniletea mwanangu macho yake yamefumba! amewekwa pamba katika masikio yake, hatikisiki wala kusimama tena, aaah! Dunia - umenichoma sindano ya sumu, umenilowesha na mvua ya maumivu." Mama Desmund kinywa kilishindwa kuhimili maumivu hayo, hakuweza kuzungumza tena bali machozi, jasho na kamasi vilizidi kumchuruzika kwa kasi sana.

"Aliishiwa damu, nilipojaribu kumkimbiza hospitali kwa lengo la kuyaokoa maisha yake ndipo madaktari waligundua alikuwa amekwisha fariki tayari" alijibu Desmund macho yake yakiwa yamefunikwa na bahari ya machozi, kiza kinene kilitanda katika mboni zake.

Ni miezi mitano na majuma mawili yalikuwa yamepita, msiba ulikuwa umemalizika, watu wakatawanyika kuendelea na majukumu yao ya kila siku.
"sasa utawaza mpaka lini?" aliuliza Janeth baada ya kumuona Desmund akiwa ameweka mkono wake shavuni - haikuitaji akili kubwa ili kugundua kwamba Desmund alikuwa amesafiri mbali kabisa kimawazo, alikuwa mwili tu pale ndani.

Desmund hakujibu neno lolote lile, alitikisa kichwa akasimama akaelekea chumbani kwenda kupumzika ilikuwa ni saa nne kamili za usiku.
"upepo mkali ulivuma katika chumba hicho, vitu vikawa vinaruka huku na kule! milango inafunguka na kujibamiza kwa nguvu, radi na ngurumo kali zikawa zinasikika! sauti za ndege wa ajabu zikatawala ndani ya chumba. Zilisikika nyayo za mtu akiwa anatembea."
Purukushani hizo zilimfanya Desmund ashtuke kutoka usingizini, akashusha mkono wake akaishika silaha yake.
"kuna nini tena uko sebuleni? nani anafungua mlango na kubamiza! na uyo bundi analilia wapi? " alijiuliza maswali pasipo kupata majibu akahisi kijasho chembamba kikimchuruzika kwapani na mgongoni pote pakalowa.

"Nimevamiwa hapa!" alinong'ona Desmund, wakati huo alisikia meza ikivutwa, watu wakiwa wanaimba sebuleni kwake, alipotega sikio kwa makini ni lugha gani waliyokuwa wakiitumia watu hao hakuweza kuelewa.
Desmund alijikaza kiume, akasimama taratibu akawasha taa na kuanza kunyata, alipofika sebuleni aliduwaa, palikuwa pametulia meza iko pale pale ilipo siku zote.

"sasa mbona milango imefunga vizuri kabisa! nilisikia vyombo vinamwagika - lakini mbona viko sawa." alijisemea mwenyewe Desmund akiwa anatetemeka mwili mzima sababu ya sintofahamu hiyo anayokumbana nayo.
Alipogundua kwamba hakuna kitu kibaya, wala jambazi yeyote aliyeingia pale ndani, alizima taa ya sebuleni kisha akaelekea chumbani kuendelea na usingizi wake.

Usiku wa manane Desmund aliamshwa na mlio wa kitu kilichokuwa kinagonga mlango kama mtu anapiga ngoma. Alitazama kwa uangalifu mlangoni hakuamini macho yake, mlango ulianza kufunguka pole pole! alishika panga lake akawa tayari kukata uso wowote ambao ungejitokeza katika mlango huo.

Desmund alisikia sauti inamuita kwa upole "kaka! kaka! kaka! nahisi njaa!" Desmund alisisimuka, mwili mzima ukafa ganzi mithili ya mtu aliyepigwa na shoti ya umeme. Panga lililokuwa mkononi mwake lilidondoka sakafuni.

"kaka! kaka! kaka! nahisi njaa," sauti ilirudi tena, sauti ilijieleza ilikuwa ni ya mdogo wake aliyefariki miezi mitano iliyopita.

"Baraka! Baraka! Baraka!" Desmund alijikaza na kuita jina la mdogo wake ambaye ni marehemu. Kimya kilitawala sauti ile haikusikika tena. Aliwasha taa ya sebuleni akaufungua mlango akaita kwa sauti ya juu sana "Barakaaaaaaa!" ilikuwa kama mwanzo, hakuitika wala kuonekana.

MALKIA WA KUZIMU..... 04
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0713 317 189.
0622 738 310.
TANGA

................................................................
SEHEMU YA NNE.
( 04 )


ILIPOISHIA.....
Desmund alisikia sauti inamuita kwa upole "kaka! kaka! kaka! nahisi njaa!" Desmund alisisimuka, mwili mzima ukafa ganzi mithili ya mtu aliyepigwa na shoti ya umeme. Panga lililokuwa mkononi mwake lilidondoka sakafuni.
"kaka! kaka! kaka! nahisi njaa," sauti ilirudi tena, sauti ilijieleza ilikuwa ni ya mdogo wake aliyefariki miezi mitano iliyopita.
"Baraka! Baraka! Baraka!" Desmund alijikaza na kuita jina la mdogo wake ambaye ni marehemu. Kimya kilitawala sauti ile haikusikika tena. Aliwasha taa ya sebuleni akaufungua mlango akaita kwa sauti ya juu sana "Barakaaaaaaa!" ilikuwa kama mwanzo, hakuitika wala kuonekana.
..................................................................................
ENDELEA NAYO......

Desmund akiwa katika taharuki hiyo ya kushangaza, aliufunga mlango akaelekea chumbani kulala. Akamkuta Janeth kalala usingizi mzito anakoroma tu! hakutaka kumuamsha ili kumueleza yaliyojiri kuepuka kumuharibia usingizi wake.

Usingizi ulimsaliti na kumpiga teke Desmund, hakuweza kupata usingizi tena - mawazo na maswali mengi yalikuwa yakikatiza katika kichwa chake. Akahisi amefungwa katika gereza la mateso akisubiri kunyongwa. Alianza kujiuliza kama kweli mdogo wake alifariki au alifanyiwa mazingaombwe. Japo ilikuwa ni usiku lakini jasho zilikuwa zikimchuruzika kutoka katika paji la uso na kusambaa karibia kila kona ya mwili wake.

Akapiga funda la mate machungu, kisha akaendelea na tafakuri yake, akawatilia mashaka wazee wote waliohudhuria mazishi ya mdogo wake na pia wale waliokuja kumpa pole nyumbani, lakini hakumtilia shaka yeyote ile mke wake. Ghafla usingizi mzito ulimpitia.

Mwanga hafifu ulipenyeza kwenye madirisha ukafanikiwa kuingia ndani kwa utulivu kabisa. Ndege wa angani walitoa milio tofauti iliyosindikizwa na kuku waliowika kwa kishindo kizito! Ilikuwa ni asubuhi, jua nalo likiomba ridhaa ya kuweza kuchomoza.

Mwanga huo uliweza kumkurupua Desmund kutoka usingizini, akadamka na kuanza kujiandaa.

"karibu chai mume wangu! " alisema Janeth.

"kuna mayai, chapati na tunda kidogo." alikazia Janeth akiwa anamtazama Desmund usoni.
"Hahahahahah..!!!" alicheka kidogo Desmund, kisha akajikohoza kabla ya kuanza kula.

"Umeandaa chakula bora kabisa," alimwaga sifa kedekede kana kwamba hajawahi kula chakula kama kile maishani mwake.

Baada ya sekunde kadhaa Desmund alikuwa amemaliza kunywa chai, akamkumbatia mpenzi wake kama ishara ya upendo na kuagana pia. Akaingia ndani ya gari na kuelekea kariakoo lilipo Duka lake kubwa la nguo za jumla.

"huyoooooo..!! anapotelea sasa." alitamka Janeth akiwa anachungulia nje ya geti akihakikisha kwamba mumewe ameondoka. Janeth alivyorudi ndani akajifungia chumbani, akavua nguo zote na kubaki mtupu! akasimama wima pembeni ya chumba, ghafla alianza kubadirika uso uliumuka kama maandazi yaliyozidishwa amila, meno yalichongoka kama mkuki, macho yalikuwa makubwa ajabu yakawa yanatoa matone ya damu, ulimi ulikuwa mrefu yani futi tano na nchi moja.

"Ngruuuuuuh! Ngruuuuuh!" aliunguruma Janeth kama simba jike mwenye njaa, akiwa bado anaunguruma alitokea mtoto mdogo chini ya uvungu wa kitanda chao. Hali yake kiafya ilionekana kuwa mbaya, alivaa matambara machafu yaliyochanika, macho yake yalikuwa yameingia ndani, alikuwa anatia huruma sana mtoto huyo.

Janeth alimvuta kwa hasira mtoto huyo, akamng'ata tumboni na yale meno yake marefu, utumbo wote ulitoka nje! alianza kula utumbo akiwa anaunguruma. Akatoboa shingo na kuanza kunywa damu, mtoto huyo hakulia bali alikiuma kidomo chake cha chini huku machozi yakimdondoka! uso wake na macho vilionyesha wazi alikuwa amekata tamaa kutokana na mateso aliyokumbana nayo huko. Na ndio maana alitulia tuli akiwa anatazama utumbo wake unavyoliwa kwa huzuni isiyoelezeka.

Janeth alivyotosheka alipaza sauti kubwa na kali, "Malkia wa kuzimuuuuuuuuuu!" sauti hiyo ilifanya upepo mkali utokee pale ndani, nyumba ilitikisika! likatokea joka kubwa likaumeza mwili wa mtoto huyo na kisha kutoweka. Janeth alishika titi lake la kushoto akalibonyeza kwa nguvu - papo hapo akarejea katika hali yake ya kawaida.
"piipiiiiiiiii! piiiiiiiii....!!!" ilikuwa ni oni ya gari.

"Nakuja"
"Mmh! Mbona leo mapema sana!" alihoji Janeth, kumbe ni mumewe alikuwa anarejea majira ya saa tisa za mchana.
"Nimekuja ili twende kwa Daktari kama nilivyokwambia" alitabasamu Desmund.
"Nilishasahau ila niko tayari!"
"Hatuna muda wa kupoteza ingia kwenye gari tuondoke" alizungumza Desmund akiwa anafungua mlango wa gari. Janeth aliingia na safari ikaanza kuelekea hospitali ya Muhimbili.

Desmund pamoja na mkewe Janeth, ni miaka sita sasa ilikuwa imepita tangia waingie katiaka ndoa, lakini hawakubahatika kupata mtoto ndani ya miaka yote hiyo sita. Uvumilivu ukawashinda wakaamua wampigie simu Daktari bingwa wa magonjwa ya uzazi pale hospitali ya Muhimbili, alifahamika kwa jina la Dokta Etimba Makukumulo, aliwasikiliza kwa makini kisha akawapangia siku ya kwenda kumuona.
"Oooh! karibuni mmefika? naona mnapendeza sana," alitamka Daktari Makukumulo.

"Asante sana tunashukuru Daktari," Janeth na mumewe waliitikia kwa pamoja. Daktari aliwaelekeza katika chumba maalumu kwaajili ya uchunguzi na vipimo zaidi. Baada ya dakika kama thelathini na tano kupita mambo yote yalikuwa yamekamilika.

"Eeeh!" alisita kidogo Daktari, kisha akaendelea kuzungumza, " Kwa mujibu wa vipimo mnaonekana nyote mko sawa, hakuna aliye na tatizo. Niwasihi muwe na subira mtapata mtoto," aliishia hapo kuzungumza Daktari.

Janeth alitoa tabasamu hafifu akasema, "Tunashukuru sana, pia tunakutakia kazi njema," Desmund yeye aliachia tabasamu pana, kwani alitaraji kwamba mkewe angegundulika na tatizo la kutopata ujauzito, kutokana na kasumba iliyozagaa mtaani kwamba wanandoa wowote wale wakiishi kwa muda mrefu bila kupata mtoto, basi madhaifu yote utupiwa mwanamke.

Baada ya kutoka katika maeneo ya hospitali, walielekea katika mgahawa maarufu sana wa nyama choma pale jijini Dar - es - salaam.

"Ooh! Waooh! nilimisi sana nyama choma ya hapa kipenzi changu" alitamka Janeth akiwa anashuka ndani ya gari na kuanza kupiga hatua kuelekea katika mgahawa huo wa kisasa.

"Nakujali, nakuthamini, lazima nihakikishe unakula vilivyobora" Desmund alijibu.
"Wewe ni kama yai kwangu nakulinda usipasuke, najiona nimeshika puto nikiangaza uku na kule asitokee mtu mwenye sindano na kulitoboa puto langu" Desmund alizidi kusisitiza.

"Hahahahah...!!!! " alicheka kwa sauti ya juu sana Janeth, baada ya kusikia mifano hiyo aliyoitoa Desmund, mara sijui yai au puto.
Kimya kilitawala, kilichokuwa kikisikika kwa wakati huo ni jinsi walivyokuwa wakitafuna nyama hizo kwa utulivu. Janeth alikuwa akishika nyama mwishoni kabisa mwa vidole vyake utadhani inataka kudondoka. Aliipeleka kinywani taratibu akiufungua mdomo wake mdogo na kubugia kipande cha nyama. Jicho nalo lilikuwa likimeremeta kwa ukali wa chachandu iliyowekwa ndani ya nyama ile.

Vijana waliokuwa wameketi pembeni ya meza ya kina Janeth, mate yalikuwa yakiwadondoka! sio kwa utamu wa nyama waliyoiona ila ni jinsi Janeth alivyokuwa amelegeza jicho lake, alivutia kwa urembo wake. Vijana hao walijaribu kumkonyeza lakini Janeth akawa anatabasamu tu kana kwamba hawaoni. Wengine wakajaribu kuandika namba zao hewani kwa ishara, Janeth aliishiia kucheka tu! hakika uzuri wake uliwanasa wengi.

Giza nalo lilianza kuuvamia mji, taratibu mwanga ukimezwa, mwezi ukijaribu kutokeza na kuonesha umahiri wake wa kumulika nyakati za usiku. Hatimaye Janeth na mumewe walikuwa wamemaliza kula nyama choma, wakanawa mikono yao wakaingia ndani ya gari na kuanza safari ya kurejea nyumbani.

Baada ya dakika kama ishirini hivi kupita walikuwa wamefika. Siku hiyo hakukuwa na foleni kubwa sana njiani kama ilivyozoeleka kwa Jiji ilo la Dar - es - salaam.

"Nenda kaoge kila kitu nimeishaandaa bafuni! " Janeth alinena akiwa amejifunga kipande kimoja tu cha kanga, akamshika mumewe mkono na kuanza kumsindikiza mpaka bafuni.

"Eeh! kumbe tayari! nikaoge nipumzike maana tumezunguka sana leo, tumeenda hospitali, tukapita mjini kwenye nyama choma duh! leo nitalala kama mzigo nitashtuka kumekucha tu" Desmund alijibu.

Binti mrembo akiwa amevishwa mavazi kama malkia, alikuwa amelala juu ya kaburi lililojaa nyasi na chakavu sana. Alizungukwa na mabinti watatu waliokuwa wamevalia mavazi meupe yasiyokuwa na doa. Mabinti hao walikuwa wakizunguka kaburi ilo wakiwa wanasujudu na kutoa heshima kwa binti yule aliyekuwa amelala juu ya kaburi ilo.

Lakini kaburi la pembeni alikuwa amelazwa kijana mwenye urefu wa futi tano na nchi moja, mweusi si mweusi _ mweupe si mweupe, tunaweza sema ni maji ya kunde. Binti yule mrembo aliyekuwa amelala juu ya kaburi alinyoosha mkono wake akauingiza ndani ya lile kaburi akatoka na viungo vya binadamu kama moyo, figo na viganja vya mtoto mchanga. Kisha akasogea na kutaka kumlisha yule kijana aliyelazwa kwenye kaburi la pembeni. Lakini kijana huyo alikuwa akigoma kuachama mdomo ili alishwe kipande cha nyama ya moyo wa binadamu.

"Mama yanguuuuuu..! " alipaza sauti kwa hofu Desmund akikurupuka kutoka usingizini.
"Ni ndoto gani hii! mbona inatisha kiasi hiki eeh!" Desmund alinena akiwa anamuamsha mkewe.

"Tazama maajabu haya nimeota ndoto ya kutisha sana, kwamba wewe mke wangu ukiwa juu ya kaburi nami nikiwa kwenye kaburi la pembeni yako, kisha wewe ulisimama na kutaka kunilisha mimi kipande cha nyama ya binadamu. Lakini wewe ulivalia mavazi ya kung'ara sana! ukiwa umezungukwa na mabinti waliovalia mavazi meupe wakiwa kama wanakusujudia wewe" alimalizia kuzungumza Desmund, kijasho chembamba kikawa kinamchuruzika kwapani kutokana na hofu kubwa aliyokuwa nayo dhidi ya ndoto ile.

"Yaani unaukatisha usingizi wangu sababu ya ndoto! kwanini unapenda sana kuteseka na ndoto zisizokuwa na hata chembe ya ukweli ndani yake?" aliongea Janeth akiwa ameikunja sura yake iliyofunikwa na usingizi mzito.
FB_IMG_1594922887276.jpg
 
MALKIA WA KUZIMU..... 05
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0622 738 310.

................................................................
SEHEMU YA TANO.
( 05 )


ILIPOISHIA.....

Ni ndoto gani hii! mbona inatisha kiasi hiki eeh!" Desmund alinena akiwa anamuamsha mkewe.

"Tazama maajabu haya nimeota ndoto ya kutisha sana, kwamba wewe mke wangu ukiwa juu ya kaburi nami nikiwa kwenye kaburi la pembeni yako, kisha wewe ulisimama na kutaka kunilisha mimi kipande cha nyama ya binadamu. Lakini wewe ulivalia mavazi ya kung'ara sana! ukiwa umezungukwa na mabinti waliovalia mavazi meupe wakiwa kama wanakusujudia wewe" alimalizia kuzungumza Desmund, kijasho chembamba kikawa kinamchuruzika kwapani kutokana na hofu kubwa aliyokuwa nayo dhidi ya ndoto ile.

"Yaani unaukatisha usingizi wangu sababu ya ndoto! kwanini unapenda sana kuteseka na ndoto zisizokuwa na hata chembe ya ukweli ndani yake?" aliongea Janeth akiwa ameikunja sura yake iliyofunikwa na usingizi mzito.
.........................................................................

ENDELEA NAYO.....

Desmund aligoma kulala tena, mwili wote ulikuwa umetawaliwa na maumivu, alisimama akawasha taa alipoitazama mikono yake aliona alama za viboko.

"Nani kanichapa nikiwa nimelala!" alinong'ona kwa sauti ya chini ila hakuweza kupata majibu. "Nikisema nimsimulie mama juu ya mauza uza haya naweza nikampoteza pia, kwasababu presha inamsumbua, pindi nitakapomwambia kwamba nilisikia sauti ya mdogo wangu Baraka akiniita usiku wa manane, nahisi nitakuwa nimemchimbia mama yangu kaburi. Ipo siku kifua changu kitachoka kuhifadhi siri hizi nzito zinazochoma moyo wangu" wakati Desmund akiyazungumza maneno hayo alikuwa ameyafumba macho yake kana kwamba anasali au yuko usingizini.

Jua nalo lilikuwa tayari limejitahidi na kufanikiwa kupenyeza, likawa tayari limeyashinda mawingu yaliyokuwa yamelificha, ilikuwa ni asubuhi nyingine na ya kupendeza pia.

"Kuna misukosuko nayopitia nyakati za usiku rafiki yangu Manumbu" Desmund alishusha pumzi ya kukata tamaa, akapiga funda la mate machungu kisha akaendelea kuzungumza, "Rafiki yangu Manumbu nimekuita hapa Dukani kwangu nikueleze kitu kimoja, huwezi amini nilisikia sauti ya mdogo wangu aliyefariki miezi mitano iliyopita akiwa ananiita usiku wa manane! milango na madirisha ikifunguka yenyewe, michirizi ya viboko katika mwili wangu."

Desmund alisita kidogo kuzungumza akatoa kitambaa akafuta jasho zilizokuwa zikimchuruzika kwa fujo kisha akaendelea kuzungumza, "Kibaya zaidi ni ndoto niliyoota nikiwa juu ya kaburi na mke wangu akiwa anataka kunilisha kipande cha nyama ya binadamu. Nilichukia sana na kuilaani ndoto hiyo kumbe na mke wangu nae anakumbana na magumu, sijui ni nani anayetundea hivyo!"
Desmund alielezea kwa masikitiko makubwa sana akiwa anatikisa kichwa chake kwa mshangao.

"Pole sana rafiki yangu," alidakia Manumbu. "Dunia ina mengi nashindwa kuelewa ni kitu gani kizito hicho kinachokuandama," Manumbu aliachia tabasamu hafifu uku akikodoa macho yake katika hali ya mshangao.

"Heri adui mwerevu kuliko rafiki mpumbavu" alinyamaza kidogo Manumbu kama sekunde kumi, kisha akaendelea kuzungumza, "Hivyo nami sitakubali kuwa rafiki mpumbavu kwako, nitakusaidia kwa hali na mali"

Desmund alitikisa kichwa kuashiria kwamba anakubaliana na kile anachokizungumza Manumbu. "Heri kuzuia kuliko kuuguza" "Kuna watu watakuwa wanakufanyia mchezo mchafu na ni kutokana na utajiri ulionao. Binadamu hawafadhiriki hawa ndugu yangu" alisisitiza Manumbu.

"Kwa hiyo unataka kusema kuna ushirikina juu ya haya yanayonitokea" aliuliza kwa mshangao Desmund. "Kabisa rafiki yangu" alidakia Manumbu. "Afadhali kuvumilia joto kuliko msiba, sasa ukiendelea kuzubaa utazidi kuzika ndugu zako bila sababu ya msingi, siunajua jinsi kifo kinavyouma? " alieleza Manumbu.

Desmund akatikisa kichwa kuashiria anajua uchungu wa kifo na hata kufiwa pia, ndipo Manumbu akaendelea kuzungumza, "Msafara wa maisha hauna kurudi nyuma, ukiendelea kuzembea ili suala katu muda hautakusubili, ni aibu kujikwaa kwenye jiwe moja mara mbili, ukitaka kubugia unga uwe na mate ya kutosha. Unaingia katika vita ngumu rafiki yangu! jiandae vya kutosha. Sasa mimi nitakupeleka kwa mganga bingwa akusaidie, vinginevyo utaangamia angali bado kijana mdogo" alimaliza kuzungumza Manumbu.

"Mganga!" alistuka Desmund.
"Ndio mganga" Manumbu alijibu kwa sauti ya utulivu.

"Imani yangu hairuhusu masuala ya uganga" alinena Desmund.
"Nisikilize rafiki yangu hata simba akizidiwa uwa anakula nyasi" aliachia tabasamu pana Manumbu akiwa anautikisa mguu wake wa kushoto.

"Naogopa sana mambo ya waganga" alizidi kusisitiza Desmund. uku akipunguza sauti ili yule kijana anayemuuzia Duka asiweze kusikia maongezi yale kwani wao walikaa chumba cha kuhifadhia bidhaa za hapo dukani ( stoo ).

"Ndimu mpaka uikamue, ndipo utaona maji yake, hata mambo ya waganga pia mpaka uingie kwanza ndio utaona utamu wake" alizungumza Manumbu.

"Basi rafiki yangu kwa vile nina shida usiku silali kabisa, nipeleke kwa uyo mganga tu! maana nikisinzia ndoto za kutisha zinaanza, naumia sana"

"Bahari haivukwi kwa kuogelea!" alitania kidogo Manumbu wote wakajikuta wanaangua kicheko na kugonga mikono yao kwa pamoja.

"Inabidi twende ili tuwahi kurudi, kwasababu Mama yupo nyumbani alikuwa anaumwa kidogo" Desmund alinena. "Basi amka tuelekee kwa uyo mganga" alijibu Manumbu.

Safari ilikuwa ndefu kidogo, mganga aliishi pembezoni mwa jiji la Dar - es - salaam, Desmund pamoja na rafiki yake walipokelewa na kijumba kidogo kilichoezekwa kwa nyasi. Pembeni kulikuwa na zizi la mifugo bata, kuku walikuwa wakizunguka kwa nje, palikuwa na mbwa wawili. Mzee Matiku alikuwa amejitenga na makazi ya watu, kando na kijumba hicho cha kutibia wagonjwa alikuwa na nyumba nzuri ya kuishi yeye na familia yake.

"Ooh! karibuni sana" alizungumza mzee Matiku kwa sauti ya kukoroma kutokana na uzee wake, japo alianza shughuli za uganga akiwa bado kijana mdogo sana mwenye umri wa miaka kumi na tano, alipewa mikoba na marehemu Bibi yake kizaa Baba mwaka 1945 uko mkoani Mara wilaya ya Musoma vijijini, kabla hawajaamia pembezoni mwa Jiji la Dar - es - salaam 1975.

"Asante sana mzee Matiku, nimemleta rafiki yangu ana matatizo makubwa sana, anasumbuliwa usiku yaani halali kwa amani" Manumbu alizungumza.

Kabla mganga hajazungumza neno lolote lile zaidi ya kuitikia salamu. Alitoa jamvi lake lililozeeka akatandika pembezoni mwa kibanda chake maalumu kwaajili ya kutibia wagonjwa.

"Ingieni ndani" ilikuwa ni sauti ya mganga. Akatoa vibuyu na vyungu kadhaa akaviweka juu ya jamvi lile chakavu, akatoa pia hirizi kubwa mbili moja ina rangi nyekundu na ya pili ina rangi nyeusi. Akachukua mahindi kidogo na ulezi akaweka ndani ya pembe ya ng'ombe.

Mganga alitoa ngozi ya fisi iliyokaushwa akamwambia Desmund akae juu ya ngozi hiyo. Desmund alitetemeka mwili mzima kwa uoga uliokithiri, akajikuta anajamba kwa sauti kubwa hakuna aliyecheka kimya kilitawala, jasho likawa linamchuruzika mgongoni, moyo unakwenda mapigo mia mbili na hamsini kwa dakika. Alijikaza kiume akakaa juu ya ngozi ya fisi, akapewa kibuyu kimoja akishike katika mkono wake wa kulia.

Mganga akaanza kazi ya kumuagua Desmund, alimzunguka Desmund kutoka kushoto kwenda kulia na kutoka kulia kwenda kushoto, uku akiwa anaimba nyimbo zisizoeleweka, akamuwekea hirizi mbili katika paji la uso kisha akazitoa.

Ghafla mzee Matiku ambaye ndie mganga aliona mwanga mkali pembezoni mwa kale kajumba alikokuwa anamtibia Desmund, ila Desmund na rafiki yake wao hawakuweza kuona kinachoendelea isipokuwa mganga tu.

Katika mwanga ule akatokea binti mweupe na mrembo sana, anakadiliwa kuwa na urefu wa futi tano na nchi moja, macho ya kuvutia yenye rangi ya hudhurungi. Binti uyo alikuwa amekasirika sana! akamnyooshea kidole mganga huku akimwambia...
FB_IMG_1594922887276.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom