MALKIA WA KUZIMU..... 06
MTUNZI: LOVI PIUS KIJOGOO
WHATSAP: 0757 238 304.
0622 738 310.
................................................................
SEHEMU YA SITA. .
( 06 )
ILIPOISHIA.....
Ghafla mzee Matiku ambaye ndie mganga aliona mwanga mkali pembezoni mwa kale kajumba alikokuwa anamtibia Desmund, ila Desmund na rafiki yake wao hawakuweza kuona kinachoendelea isipokuwa mganga tu.
Katika mwanga ule akatokea binti mweupe na mrembo sana, anakadiliwa kuwa na urefu wa futi tano na nchi moja, macho ya kuvutia yenye rangi ya hudhurungi. Binti uyo alikuwa amekasirika sana! akamnyooshea kidole mganga huku akimwambia...
ENDELEA NAYO......
Nakusihi acha mara moja kufatilia maisha ya watu, ukiendelea nitakupoteza nitainywa damu yako kabla haijapoa, mimi ndie Janeth Malkia wa Kuzimu." Binti uyo alitoweka ghafla.
"Aanh! Anhaa! sasa saa" Mganga alishikwa na kigugumizi cha ghafla. "Naomba mrudi kesho kutwa, leo mizimu imegoma." ilikuwa ni sauti ya mganga akizungumza, aliogopa vitisho alivyopewa na kiumbe kile cha ajabu kilichotokea pembezoni mwa kile kijumba chake anachotibia wagonjwa.
"Sawa mzee nimekuelewa" alijibu Desmund uku akiwa anasimama kutoka kwenye ile ngozi ya fisi. Hakujua kilichoendelea pale ndani mpaka mganga kusitisha huduma.
"Umesikia rafiki yangu uyu ni mganga bingwa siunaona alivyo na madawa mengi? sasa kesho kutwa nitakuleta pia" alitamka Manumbu wakati wakiwa wanaingia ndani ya gari na kuianza safari yao kurejea katikati ya Jiji la Dar - es - salaam. Desmund alimshusha rafiki yake kisha yeye akaelekea nyumbani kwake Masaki.
"Habari ya hapa nyumbani mama? "
"Nzuri mwanangu za miangaiko? " alijibu mamake Deamund.
"Ni nzuri vipi hali yako? "
"Kwa kweli leo na kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu niko vizuri kabisa Mungu ni mwema kila wakati mwanangu!"
"Amina" aliitikia Desmund uku akimpa koti mkewe ampokee.
"Waoooh! karibu mume wangu! " ilikuwa ni sauti ya Janeth.
"Pole na majukumu! nakupenda sana kipenzi changu, kutokuwa nawe kwa masaa yote hayo uwa nahisi kuchanganyikiwa kabisa, najihisi mwenye furaha sana wakati nikiwa nawe, ni wewe pekee uliyenitoa katika dhoruba ya mapenzi," baada ya Janeth kuzungumza maneno hayo alimkumbatia Desmund kwa nguvu akambusu shavuni, akamshika mkono na kumsindikiza mpaka chumbani. Mamake Desmund alipoona mahaba hayo alisimama kwa aibu na kuelekea chumbani uku akijisemea mwenyewe kwa sauti ya chini, "Mmh! wazungu hawa wametuletea balaaa!, sisi enzi zetu hatukuwa na mambo kama hayo."
"Lakini leo mume wangu umechelewa ulikuwa wapi? " Janeth aliuliza.
"Mmh! Mmh! leo! " alisita kidogo Deamund akajikohoza kuweka koo sawa kisha akaendelea kuzungumza, "Nilikuwa kwa rafiki yangu tukipanga mipango ya biashara!." "Eti eeeh! sawa endelea kupanga hiyo mipango ya biashara!" Janeth alijibu kwa dharau, akaelekea sebuleni kwenda kuandaa chakula. Baada ya dakika kama thelathini walikuwa wamemaliza kula chakula wakaelekea chumbani kupumzika, Desmund na mkewe wakamtakia mama usiku mwema kama ilivyo utamaduni wetu watanzania, na hata nchi za Afrika kwa ujumla.
Ilikuwa ni Ijumaa siku ambayo Desmund aliamini ilishiba matumaini na inao upya wa maisha yake. Akaamini ni siku ambayo anakwenda kufunguliwa minyororo ya mateso, ndoto mbaya za usiku. Hakika moyo wake ulijawa na imani ya ushindi dhidi ya siku hiyo ya Ijumaa ambayo alitakiwa arudi kwa mganga.
Jua lilikuwa ndio kwanza linajitahidi kutokeza nyuma ya yale mawingu mazito yaliyotanda angani. Mvua nyepesi iliyonyesha jana usiku ilifanikiwa kuacha vidimbwi vya maji machafu hapa na pale kando ya barabara za jiji la Dar - es - salaam.
Desmund alijiandaa haraka, alivaa ile suti yake maridhawa ya hudhurungi, akaweka na tai nyeusi yenye madoa meupe, akazama ndani ya kabati akatoa manukato na kujipulizia, kisha akaenda kumjulia hali Mamake, akamkumbatia mkewe tayari kwa kuondoka.
"Mmh! mume wangu mbona leo mapema sana? " Janeth aliuliza.
"Kuna mzigo naenda kufata!"
"Subiri basi nikuandalia hata chai"
"Nitachelewa ngoja niwahi sawa mke wangu? "
"Sawa Baba nenda ufike salama,"
Wakati Desmund akipiga hatua kuelekea ndani ya gari, Janeth alijisemea mwenyewe kwa sauti ya chini, "Hivi uyu anadhani sijui kinachoendelea sasa ngoja." Janeth alielekea nyuma ya nyumba akafukua chini na kutoa kibuyu chenye damu ya moto ya binadamu ilikuwa ikichemka kana kwamba inatoka jikoni, akanywa kisha nyingine akajimwagia usoni na kuutoa ulimi nje uku akisema..
"Nani anataka kunijaribu mimi! nitamaliza wote," akaanza kuunguruma. "Ngruuuuuh! Ngruuuuuuh! mimi ndie malkia wa kuzimu nataka damu mbichi saa hii!! Ngruuuuuuh!" Janeth akazidi kuunguruma.
"Njoo! Njoo! Njoo! aje mmoja hapa" Baada ya Janeth kutamka neno njoo mara tatu, ghafla alitokea binti mrembo aliyefanana kama Janeth kuanzia unyayo mpaka utosi, usingeweza kuwatofautisha. Janeth akamuacha yule binti pale nyumbani kisha yeye akatoweka ulionekana moshi ukipaa juu angani kwenda kumfatilia Desmund.
"Mama karibu chai tayari!"
" Asante mwanangu nakuja!" alijibu Mama Desmund.
"Mmh! chai ya leo tamu, naona chapati laini zinatafunika kwa raha utanifundisha na mimi kupika mwanangu. Maana hata sisi wazee tunatakiwa tule vitu vizuri," alizungumza Mama Desmund uku akiachia tabasamu.
"Usijari Mama nitakufundisha,"
" Sawa mwanangu,"
Mama Desmund yeye alijua anazungumza na Janeth mkamwana wake, la ashaa!!... Jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Yule hakuwa Janeth bali ni mzimu uliovikwa sura ya Janeth, na hata kile chakula alichokula hakikuwa cha kawaida kabisa.
"Ooh! rafiki yangu karibu sana naona umewahi, unakwenda na muda kweli wewe msomi," alipaza sauti Manumbu akiwa anamkaribisha Desmund nyumbani kwake.
"Asante sana lazima nizingatie muda sababu nina shida ndugu yangu," alijibu Desmund kwa sauti ya upole kabisa. Safari ilianza kuelekea kwa mzee Matiku ambaye ndie mganga, kutokana na kujitenga kwake na makazi ya watu aliishi pembezoni sana, walitumia takribani masaa sita kufika sababu ya msongamano wa foleni za magari ya watu waliokuwa wakienda makazini kwao.
Umati wa watu ulikuwa umekusanyika vilio na simanzi vilitawala. Nyuso za huzuni ambazo machozi yalimelemeta machoni kwao zilidhihilisha wazi kuna msiba umetokea.
"Kuna nini tena hapa!?" aliduwaa Matiku.
"Mbona kama watu wanalia!" alidakia Desmund. "Ebu ngoja tuulize kwanza," alizungumza Matiku kwa sauti ya chini sana.
"Binti habari za kwako! Kuna nini hapa?" Manumbu aliuliza. "Nzuri tu shikamoo!" "Marahaba binti ebu nieleze kwa marefu na mapana sasa!"
" Mimi ni mjukuu wa Mzee Matiku ambaye alikuwa ni mganga hapa. Dakika kumi zilizopita historia ya mji huu ilibadirika ghafla! ikawa ni historia mbaya na chungu kuisimulia,"
"Babu alilalamika kwamba kichwa kinamuuma sana! tukampa dawa aliyoitengeneza mwenyewe, tukasahau kwamba mganga hajigangi, baada ya kunywa dawa hiyo Babu alilala usingizi, usingizi wa milele, aliipa Dunia kisogo, alisafiri njia ya wote yaani alikuwa tayari amefariki Dunia."
Binti uyo aliangua kilio cha kwikwi, akakumbuka ucheshi aliokuwa nao Babu yake, akakumbuka zawadi na hata pesa alizovuna, hakika kumbukumbu hiyo ilizidi kuuponda moyo wake.
Desmund na rafiki yake walibaki vinywa wazi kana kwamba walitaka kupiga chafya lakini chafya ikagoma kutoka, taharuki kubwa iliwazonga ndani ya mioyo yao.