Simulizi: Maisha Yangu Ya Uvuvi

Simulizi: Maisha Yangu Ya Uvuvi

SEHEMU YA AROBAINI 40
ENDELEA.........
Nikiwa nipo kitandani mawazo yanaanza kunijia
lakini niliamua kulala ndoto ya ajabu ilinijia. Sura ya
bwana Kibona inakuja machoni mwangu
ikinikumbusha mambo mengi sana ambayo
yalifanya kurudisha kumbukumbu zangu ndipo
nikaamka. sasa nikakumbuka kule nyumbani
ambako nilikuwa ninaishi kwa mara ya kwanza
kabla ya haya matatizo. Nikakumbuka pia kuwa
nina familia yangu ambayo nilikuwa nayo miaka
kadhaa, pia nikakumbuka kuwa kuna familia ya
kibona ambayo nilijiahidi kuwa mimi pekee ndie
nitaitunza. Ndoto ilikuwa na maana tosha kwangu
kutimiza ile ahadi yangu lakini mawazo makuu
kuhusu ile alama niliyonayo kwa mkono wangu wa
kuume. Nilipata kuangalia sana ile alama kisha
nikaamua kulala. Lakini nilipanga nikiamka asubuhi
nianze kwenda kule nyumbani pamoja na familia
yangu ili nikazidi kurudisha kumbukumbu zangu
labda naweza kujua chochote.
Asubuhi na Mapema sana niliamka na kuvaa nguo
ambazo yule mama Penina alikuwa kaninunulia.
Mama Penina ni Mkuu katika moja ya ofisi za
serikali mtoto wake aliondoka na kwenda kusoma
nje za nje kabisa, hivyo sikupata kumfahamu
mapema. Baada ya kuvaa kwa kweli sikukumbuka
hata kusafisha mdomo na uso kwani kwangu
ilikuwa ni kawaida sana vitu kama hivyo kutofanya.
Nilitoka na kuikanyaga sebule kubwa nika angaza
huku na kule ili kuona kama kuna mtu ananiona
nilitoka na kushika kitasa cha mlango lakini nyuma
yangu ulisikika mlango ukifunguliwa na sauti ya
salamu ikitawala sebule. "Mnali umeamkaje?.."
niligeuka nyuma uso kwa uso na mama mwenye
nyumba. "Salama mama sijui za kwako". Nilimjibu
jambo ambalo lilimshangaza kidogo. "Ebu!..njoo
tukae hapa kwenye kochi kwanza..." niliuachia
mlango kisha nikafika pale kwenye kochi.
"Unaelekea wapi asubuhi yote hii saa kumi na mbili
kasoro haya na hii si kawaida yako..". Nilibaki
kuduwaa tu. "Nimbie kuna kipi ambacho unataka
kukifanya?". "Mama..kuna kitu nimekumbuka nataka
nirudi kwanza kule nyumbani kwangu kwa mara ya
kwanza". Yule mama alisimama kwanza
"Khaaa!..ina maana unaanza kurudisha
kumbukumbu zako?...basi ngoja nimueleze dereva
akuchukue hadi huko". Nilimkubalia na baada ya
hapo maandalizi yakaanza. Tuliianza safari mnamo
majir av y saa tatu asubuhi taratiibu tukielekea
nyumbani. Nilimuomba kwanza anipitishe kule
baharini ili kuna vitu nikapate kuona. Mwendo wa
dakika kadhaa nilifika ufukweni na yule dereva.
Baada ya kushuka nikamuomba aendelee na safari
yake na ikiwezekana arudi kabisa kwani mimi
nitarejea mwenyewe huko nyumbani. Nikiwa
nazunguka pale. ndipo nikagundua jambo ambalo
lilinifanya hata nighaili kuendelea na kazi
niliyoiendea. Nilirudi nyuma kisha na kuongoza njia
ambayo ilinifikisha kwenye nyumba ya mshana.
Kumbukumbu ilinifanya nijue kuwa rafiki yangu
nilimuacha kwenye wakati mgumu sana. Hapo
ndipo hasira zilinishika na laiti wangekuwa karibu
basi ningefanya hata mauaji dhidi yao. Niliamua
kurudi ufukweni. Kwa kweli hali ya ufukwe uko
kwenye hatari sana maana watu hawakai kutokana
na matatizo yanayoendelea kutokea. Ukimya
ulioendelea kutokea pale ndipo na mimi nikaanza
kutafuta ukweli hata nije kukumbuka kitu. Maji
yaliyokuwa yanapiga pale ufukweni nilijihisi mpweke
sana kutokana na ile hali. Mwendo wa dakika
kadhaa nilifika hadi maeneo ya nyumbani lakini
sikupata kupaelewa vyema kutokana na ile sehemu
kuvunjwa na kujengwa jumba la kifahari. Ajabu zaidi
nilifika hadi kwa mjumbe ambae anaishi karibu
yangu pale lakini hakuweza kunipa msaada thabiti
ambao ungeweza kunipa matumaini kwangu.
Alinifukuza kama mnyama na akitaka nisionekane
kabisa yale maeneo. Nilirudi kinyumenyume kisha
nikaelekea kwenye nyumba ya mke wa marehemu
Kibona ambako nilifanikiwa kumkuta akiwa na
watoto wake wawili. Hali yao kwa kweli hairidhishi
kwa muonekano wa kawaida maana umasikini ndio
sababu ya kuwa dhoofu. Alivyoniona hakuweza
kuamini kama ni mimi pia mimi sikuweza kuamini
kama nitamkuta huyu mama. Kwa sababu siku ya
mwisho kuonana basi yeye aliondoka kijijini kwenye
familia ya mumewe ili akapate hifadhi. "Shemeji
habari ya miaka mingi.." uchungu ukiwa umemshika
machozi ya huruma yakimtoka, mwili wake ukiwa
mwembamba kutokana na ukosefu wa chakula
bora. Pia akiwa na mtoto mdogo mchanga sana
aliyekuwa akimnyonyesha jambo ambalo lilinipa
shaka kidogo. Kibona tangu afariki miaka takribani
sita mpaka saba sasa huyu mtoto mchanga
imekuaje sikutaka kuuliza sana maana nilijua sasa
anaishi na mume mwingine. "Salama
shemeji..angu.." tukiwa tunaangaliana pale
tukajikuta wote tunadondosha chozi. "Mnali...kwa
nini huniulizi kuhusu huyu mtoto?." Kwa kweli
nilijisikia aibu sana na uchungu mkubwa hasa
nikiangalia ile familia. "..mnali uliniahidi kuwa
utanitunza lakini ona sasa nimebakwa na ndugu wa
kibona huko kijijini na wakanifukuza kwa kuniita
mimi kaaba..Mnaliii hali yangu mbaya
sana..njamaniiiii" nilipatwa na uchungu mkubwa
sana pale ndipo nikapata wazo la haraka haraka
sana. "Shemeji! Kweli ila ukweli ninao mimi pekee
kwa nini nilishindwa kuwa karibu na wewe labda
niseme mpaka kuwa hapa ni mapenzi ya mungu
maana niliyoyapitia yanadhihirisha uwepo wa mungu
kwangu...sasa nimekuja kukuchukua tukakae kule
ambako mimi naishi sawa hapo itakuwa na
usalama wa wewe kukupa huduma kwa urahisi
sana". Shemeji kwa kweli alikuwa mgumu kukubali
kuondoka pale nyumbani kwake lakini nilimforce
sana hadi alipokubaliana na mimi japo sikuwa na
uhakika wapi nampeleka huyu mtu pamoja na
familia yake. Lakini nilipata wazo kwenda kwenye
nyumba ile ya Mshana ambayo zamani tulikuwa
tunaishi. Muda ulipotimu wa saa tisa jioni ndipo
tunaingia hadi ndani mulikuwa shaghala baghala.
Ndani ya dakika kadhaa tayari tulishamaliza usafi.
***********************
Majira ya jioni nikiwa na shemeji pale kwenye ile
nyumba ndipo gari linaingia na hawakuwa wengine
bali ni yule dereva akiwa na yule mama kiongozi.
Walishuka na kutukuta mimi na shemeji yangu
tukikoka moto kutokana na baridi kali. Walishuka
ndipo wakajumuika na sisi pale. "Mnali naomba
kuongea na wewe tafadhali..." nilitoka pembeni
kisha tukaanza kuongea "..mnali unajua unajiweka
kwenye hatari kubwa sana...unafahamu wewe kwa
sasa ni mtu wa thamani sana kwenye hili
eneo?...shida ni nini na huyu mama ni nani.."
Nilivuta pumzi kidogo " huyu ni mke wa Marehemu
rafiki yangu anaitwa Kibona nakumbuka katika hali
halisi ambayo naikumbuka nikiwa kwenye kile
kisiwa nakumbuka nilikutana nae. Ila nilimuahidi
huyu mama kumuhudumia ndio maana safari yangu
ilifika kwake na kumchukua mama huyu." Ndipo
maamuzi ya mwisho yalikuwa ni kuwaacha pale ili
kesho t utajua tunawasaidia vipi. Tuliwafanyia
utaratibu wa chakula usiku huo kisha sisi
tukaondoka hadi kule kwa yule mama. Usiku nikiwa
nimelala ilinijia sauti ya ukumbusho kutoka kwa mtu
nisie mfahamu ikisema. # CHAKULA_CHA_MWE
NDAWAZIMU_HUPIKWA_NA_WENYE_KUS
AZA_CHAKULA . Hii kauli ilinitia mashaka sana
ilijirudia sana kichwani mwangu mara kwa mara.
Nikajaribu kupotezea ndipo ikaja kauli nyingine
ambayo kama roho fulani ikiniambia
# Tulilolifanya_ni_funzo_kwako . Naamka asubuhi
akili yangi hainipi kabisa kutokana na ile kauli mbili
za usiku. Niliwaomba wanipeleke kwa mke wa
marehemu kibona. Sikutaka hata kusubiria chai na
nini niliwataka mara moja kwenda kuwaangalia.
Kweli tulipanda gari mara moja hadi kule kwa
Mshana. Aaaaah! Sikuweza kuamini kabisa
nilichokuwa nakiona. Maiti tatu zikiwa kitandani
pale mke wa kibona na watoto wake wamefariki
iliniuma sana tena sana. Sikuendelea kuchunguza
chochote pale. Baada ya siku tatu kupita mazishi
yaliisha huku nikitafakari kwa yale yanayonikuta
mara kwa mara. Tulikutana nyumbani kwa yule
mama Penina pamoja na mwanangu Asante baada
ya kutoka masomoni kwake. Mama Penina
alinipasha habari pale. "Mnali! Kuna mambo hapa
nataka kukujuza" niligeuka na kumsikiliza. "Ile siku
ya msiba pale nilipata barua iliyoandikwa kwa damu
hii hapa.." alinipa ile barua kisha nikaanza kuisoma.
Ilisomeka hivi. """Sasa ahadi umeshindwa kuitimiza
sasa tuna siku chache kuja kuikamata dunia"""".
" haya niambie ahadi gani hiyo na akina nani
wamemuua yule mama wa watu kule kwenye
nyumba?". Nilishindwa kumjibu kwa ufasaha
kutokana na kichwa changu kuuma sana. Wakati
huo yule mke wangu ambae tayari kaolewa na
mwanaume mwengine alikuja juu kwa kunituhumu
mimi huku akizidi kumpandikiza chuki mwanangu.
"Mama Penina kwa kweli huyu mwanaume ni muuaji
kabisa hafai kukaribiwa na huyu mwanangu acha
akae na mimi hutokuja kumuona anakuja hapa
tena.." maneno makali ambayo nilikuwa
nashambuliwa pale huku nikizidi kubanwa zaidi kwa
maneno ya shombo. Japo mama penina aliniombea
msamaha lakini haukuweza kusaidia. Mwisho wa
muda waliondoka kabisa mule ndani na kutuacha
sisi. "Ebu nambie ukweli mnali kuhusiana na hii
barua..". Nilitulia kisha nikaanza kumueleza kila kitu
ambacho nilikuwa nakikumbuka. "Ukweli ni
kwamba....ndio hivo niliyafanya hayo nika ahidi
kuwafanyia hayo ili nipate kuwasaidia ndugu zangu
ambao walipotelea huko..". "Pole sana hapo naweza
kukusaidia kabisa inatakiwa tuelekee kwa mtaalamu
mmoja hivi ambae yeye anaweza kutusaidia
kurudisha mwili wako wa halali na tukaanza kazi
ambayo nilitaka unifanyie." Siku ya pili mimi, mama
penina pamoja na dereva tulielekea mkoa wa jirani
kwa mganga mmoja maarufu tulipofika tulimueleza
kila kitu ambacho kinanisibu. Alianza kwa kucheka
sana na kunisikitikia kwa majonzi sana huku
akiniambia "kijana wangu upo na wakati mgumu
sana..una alama ambayo inawafanya wao wakuone
na wakufuate mara kwa mara popote ulipo. Na
ahadi uliyoiweka ya kuwasaidia wao wapate wafuasi
ndio itakugharimu sana maishani mwako". Daah!
Kila mmoja wetu alisikitika sana. "Sasa
unatusaidiaje baba". Alisema yule mama Penina.
"Mimi sitowatoza hata senti ila niwaombe nyinyi
mtanisaidiaje mimi ili nipate njia ya kuwasaidia."
Tuliangaliana pale "sema babu tupo tayari". "Sawa
dawa yake ni ndogo sana nenda baharini wewe
mwenyewe usiku a saa sita, kisha chukua maji
kwenye chupa, ukifika nyumbani andaa udi 12 alafu
sita ichome alafu sita ivunjevunje alafu itie kwenye
maji ya bahari ukimaliza hapo paka kama mafuta
kwa siku tatu tu utaona mabadiliko. Mabadiliko
yake ni kuondoa hiyo alama na kukurudishia
kumbukumbu wewe". Tulielewana kuwa baada ya
kufanikiwa ndipo nitakuja kumuona pale kwake kwa
ajili ya kumshukuru....
 
SEHEMU YA AROBAINI NA MOJA 41
ENDELEA…….
Baada ya kutoka kwa yule fundi ndipo mimi, mama
Penina pamoja na dereva ambae alikuwa
anatupeleka mahala popote pale. Ilichukua muda
kama masaa sita na dakika zake kufika hadi kule
ambako mama Penina anaishi. Tukiwa tunakaribia
ndipo mama penina alinidokeza jambo moja, hii
ilitokana kwa kuwa sote tulikaa viti vya nyuma hivyo
ilikuwa rahisi sana kuongea. “mnali kuna jambo
muhimu hapa nataka kukuambia” alisema mama
penina na kufanya nimuangalie kwa makini sana
mpaka anamalizia ile kauli yake ya mwisho. “Ndio
nakusikiliza kwa makini sana”. Nilimjibu ili kumpa
hamasa juu ya lile jambo ambalo anataka kulisema.
“Sawa naomba tukifika nyumbani tutatenga muda ili
nipate kukuambia”. Nilikubaliana na yeye.
Muda ulipowadia tulifika na ndipo geti kubwa
lililopambwa kwa rangi nyekundu na nyeusi
lilifunguliwa na mlinzi anaeishi hapo. Gari liliingia
na dereva akasimamisha baada ya kufika sehemu
maalumu ya kuegesha gari hilo. Nilishuka huku
nikiwa makini sana nay ale maagizo kutoka kwa
yule mganga. Tuliingia ndani sote na kumkuta dada
wa ndani akiwa tayari kaanda chakula kwa ajili yetu,
tulikaa mezani na kuanza kula kwa pamoja. Tukiwa
tunaendelea kula taratibu ndipo mama penina
akaanzisha maongezi ambayo yalinishtua kidogo.
“Mnali unajua kuwa humu ndani tunaishi mimi na
wewe pekee, alafu isitoshe mwanangu anarejea
mwezi ujao kutoka masomoni huko marekani, sasa
nilikuwa nataka kazi hii tuifanye mimi na wewe tu
na mwingine asijue kabisa”. Niliduwaa na kusubiri
sasa jambo gani ambalo anataka kuniambia baada
ya hayo.
Alipoona kuwa nimefadhaika akaanza kucheka
kidogo “hahaaa! Haaa! Haaahaaa!... najua una
wasiwasi sana juu ya kauli yangu lakini utanielewa
tu na ukija kunifanyia jambo hilo basi familia yako
kiujumla itapata amani sana nikiwa na maana mtoto
wako nitamtoa kwa nguvu yangu na kumuweka
hapa karibu yako na akatoka kabisa kuishi kule
aliko.”. “Mama jambo gani hilo tena mbona
hulisemi?” nilimuuliza. “usiwe na shaka juu ya hilo
nitakuambia muda ukifika”. Tulipomaliza ndipo
nilimuomba kwenda kupumzika lakini huku
akinisisitiza nisiwe na shaka juu ya lile swala.
Nikiwa kitandani usingizi unanijia na mawazo tele
hasa kuhusiana na mwanangu na mustakabali wa
Maisha yangu kiujumla jinsi unavyokwenda.
Ghafla ndoto ya mchana kabisa kweupe na nikiwa
bado sijalala inanijia. Nilihisi kama utani kumbe ni
kweli sauti za watu wakinijia pale nilipo kitandani na
kuhisi kabisa mtu anakaa kitandani kwangu, nilianza
kuweweseka kila nikijaribu kupiga ukulele
nashindwa kabisa, pia hata kutoka pale nilishindwa
hivyo nikabaki kutetemeka. “mnali mara ngapi
tulikukanya usijihusishe na mambo ya kipuuzi!
Utakuja kugharimu Maisha yako ya baadae kama
hukutekeleza ile amri! Amri! Amri! Ni kauli ya
mwisho ambayo ilijirudia sana ndani ya masikio
yang una kufanya kuogopa Zaidi. “nyinyi ni akina
nani?” baada ya kuuliza lile swali ndipo nakutana
uso kwa uso na kiumbe wa ajabu ambae sijapata
kumuona akiwa mwenye umbo la kutisha
lisiloelezeka hata kidogo.
Baada ya muda akabadilika na kuwa n asura ya
mwanamke salha. “naitwa salha nadhani sio mgeni
machoni mwako….nimetumwa na mkuu wa kile
kisiwa kuja kukuchunguza kwa yale yote ambayo
unayafanya, unakumbuka vyema ahadi ambayo
uliiweka kwa mkuu wetu ili upate kuwanusuru Rafiki
zako pamoja na dunia nzima?” aliuliza kiumbe yule
aliyejitambulisha kwa jina la Salha japo kweli
anafanana na salha ila sikuweza kumuamini kwa
asilimia zote. “Sasa! Nataka unifanyie kitu kimoja tu
ukifanya hiko mimi nitakusaidia na hawatokuja
kukufuatilia kabisa wewe”. “sawa jambo gani
hilo!,,,,,” baada ya mimi kukubali ndipo alipoanza
kucheka sana na kusema “Usiku wa leo saa nane
nakuja hapa kitandani kwako kuja kufanya maoenzi
na wewe hivyo tukishamaliza tu mimi sitokufuatilia
kabisa na nitakusaidia kwa mambo yote
yatakayotokea. Je umekubali?”.
Mh! Nilishindwa kumkatalia kwa sababu ya woga
nilionao na jinsi nilivyoweza kumuona pale mwanzo.
Aliondoka na kuniacha nikipumua kwa nguvu zangu
zote huku nikiwa siamini. Baada ya muda mchache
tu ndipo mlango unagongwa nilishtuka nikahisi
labda yule jinni anakuja tena. “pita mlango uko
wazi…..” hakuwa mwingine bali ni mama Penina.
Kwa mara ya kwanza mama huyo kuingia ndani ya
chumba changu tangu anikaribishe kwenye nyumba
yake. Nilimuheshimu sana kama mama tu wa
nyumba ila ki umri kama tunafanana au tumezidiana
kidogo sana. “Mnali ehee! Umejipanga vipi
kuhusiana na kwenda baharini usiku wa leo?”
aliuliza swali. “mh! Lazoma niende kwa kweli haina
jinsi hata”. “sawa basi ngoja niende dukani kisha
nikanunue ule udi kisha nakuja nakukuta leo ndipo
nitakuambia nini nataka unifanyie kwa hiyo ngoja
nikauchukue”. Mama huyo alinyanyuka ndipo
nikamkatiza. “hapana mama usijali acha nikanunue
mimi wewe pumzika tu nitarudi muda si mrefu na
kisha uje unieleze hilo jambo”. Tulikubaliana na
ndipo mimi nikaelekea dukani.
Nikiwa njiani nawaza Zaidi kuhusiana na kile
kiumbe ambacho kilinitokea mchana kuwa kinakuja
saa nane usiku akihitaji kufanya mapenzi na mimi
na wakati muda huohuo nahitajika kwenda kufanya
dawa ili niwafukuze kabisa hawa mashetani wa
kisiwa cha maajabu. Ndipo kwa nyuma naitwa
“Mnaliiiiiii…….!” Nilipogeuka hakuna mtu yeyote
aliyekuwa karibu yangu. Mala ghafla sauti kama tatu
tofauti na pande zote nne zinatoa sauti ya mimi
kuitwa nilipatwa na mshituko mpaka nikaona ni
bora hata yule mama angekuja kuchukua vitu
vyenyewe. Alijitokeza yule mwanamke akiwa mbele
yangu huku kakasirika sana. “Mnalii! Unataka
kuchezea akili zetu si ndio” alisema “mh!” mimi
niliguna tu “Sasa wewe kama mwanaume kweli
fanya mapenzi na huyo mama alafu utaona
nitakachokuja kukufanyia…” kisha akaondoka
nilijiuliza kuwa kufanya mapenzi na mama yupi na
kama mama penina mbona hata hatujawaza hilo
jambo kabla.?” Nilipotezea kisha huyo nikafika
dukani nikanunua udi kama ile idadi pamoja na
ubani kisha nikageuza kurudi.
Nakaribia nyumbani nakutana nae tena salha! “sasa
nakuambiaje ukidiriki kufanya nae basi elewa kuwa
nitakachokuja kufanya hutokuja kusahau na
nakuhakikishia kuwa utapata kidonda cha moyo
hutokuja kusahau…..” akaondoka kimiujiza. Wakati
huo mlinzi alikuwa karibu kidogo na mimi nilipo
“vipi mbona ulikuwa umesimama alafu unashangaa
kuna jambo gani?” alipouliza hivo nikajua kuwa
hakuna jambo ambalo analijua baina yangu na lile
shetani. Nikafungua geti nikafunga ghafla namuona
tena kasimama mlango wa kuingilia ndani. “sikia
sihitaji harufu yeyote ya manukato chumbani kwako
pindi muda ukifika usije kujilaumu…kingine hiyo
alama yako sisi ndio wenye uwezo wa kuitoa kwa
hiyo hata huko ulikokwenda kakuongopea haiwezi
kutoka wewe ni nusu mfu ndio maana unayo hiyo na
umeletwa hapa kwa ajili ya kutomiza yale ambayo
umeagizwa na si jingine tofauti na hayo ungekuwa
miongoni mwetu….”. nilibaki kuchoka pale mlangoni
bai tu matatizo kila siku hakuna siku ya furaha.
Nilifungua mlango na kutaka kuingia chumbani
kwangu lakini nikakumbuka kuwa mama penina
kuna jambo anataka kuniambia. Nilivihifadhi vile vitu
kwenye begi langu kisha nikaenda kumgongea
mlango kwake.
Hakuwa na desturi ya kunikaribisha ndani lakini kwa
siku hiyo alinikaribisha ndani kwake. “karibu sana
uketi hapo ehee! Vipi umefanikisha ulichokiendea?”
aliniuliza “ndio japo misukosuko ya hapa na pale
inazidi kunisumbua”. “ya kawaida hayo lakini si
unakumbuka nini yule mganga alikuambia ufanye?”
alinikumbushia vyema yote ambayo alisema
mtaalamu “nashukuru sana sasa nasubiri usiku
niende tu baharini kuchukua yale maji”. Baada ya
muda kidogo alichukua simu na kumpigia mtu
ambae sikuwa namfahamu. “sawa yupo hapa ndio
alikwenda kununua vile vifaa”. Alikuwa anaongea na
mt una kwa hakika kuwa mada inanihusu sana.
“mnali haya chukua simu uongee na mganga yule
anasema kuna maelekezo anataka kukupa wewe”.
Nilichukua simu na kuweka sikioni.
Sauti yake niliweza kuifahamu na ikaniaminisha
kuwa kweli ni yeye. “kijana” alisema mganga “ndio
mkuu”. Nilimjibu “tangu umefika hapo nyumbani
hakuna viumbe vya ajabu majini wamekufuata au
kuona mbwembwe zao?...” aliuliza swali kama
alikuwa anawaona vile wananisumbua “ndio mkuu
yupo ananisumbua sana”. “haya huyo
anaekusumbua anakudai nini?” sasa niliona ni aibu
kusema anataka kufanya mapenzi na mimi wakati
nipo kwa mama penina “kijana sema nisikie n ahata
huyo mama yako akisikia haina tabu lengo
kukusaidia wewe”. Ubaya sasa aliweka loud speaker
“alikuja na akadai kuwa anataka kuja kufanya
mapenzi na mimi majira ya usiku wa saa nane, alafu
aliniambia kuwa nikikataa basi nitazikwa…” mganga
alicheka sana. “sawa kijana huyo alijua mtego
wangu uko wapi ndio maana anataka
kukuchanganya akili kabisa ukikubali kufanya nae
maana yake muda huo wewe hutokwenda kuchukua
na dawa itakuwa imeharibika sasa kuzuia hilo fanya
mapenzi na yeyote kati ya wanawake uwapendao
wewe ili uzuie nguvu yake na hatokuja kukufuata
kwa hilo na ikifika muda huo wewe uelekee
baharini… atapaniki na kukutisha tu ila hana
madhara kabisa huyo kiumbe”.
Simu ilikata pale, mama penina nilimuona akifurahi
nikamuuliza kulikoni anafurahi vile alishindwa
kunijibu vizuri. “mnali nimesikia kila kitu hapo
mlichokuwa mnaongea. Sasa hakuna jinsi ni mimi
na wewe kufanya hilo jambo ili usiku uende huko..”
khaaa! Alikuwa anaongea bila kuwa na wasiwasi
kabisa “mama hilo haliwezekani kutokea kwako
nakuheshimu sana siwezi fanya hilo…” “huwezi sasa
unadhani nani ambae utaenda kufanya nae, eeeh!
Kuwa na akili ya kujiongeza pindi unaposaidiwa
bwana…” wakati huo mama penina ananisogelea na
kuanza kunifanyia mambo ya wale watu wa
magharibi hali ya kuwa sikuwa nahitaji kutokana na
hofu ya mama huyo. Nilijikuta nakubali kutokana na
hali halisi iliyojitokeza. Baada ya kumaliza
tunajikuta tupo kitandani tukiangaliana na woga
ukiwa umetoka kabisa. “mnali hakuna siku
nimefurahia kama leo! Mimi na mume wangu
sikuwahi kufurahi nay eye kwa sasa…sijajua lini
anarejea”
Alijikuta ananihadithia kila kitu. Majira ya saa saba
na nusu nilichomoka mimi na dereva moja kwa
moja hadi baharini kule nilikuta ukimya mkubwa
sana kiasi kulianza kuniogopesha, cha ajabu Zaidi
kama kuna watu walikuwa wanaoga kwa mbali
lakini nilipiga moyo konde ndipo nikachota maji
kirahisi na kurudi kwenye gari na kuanza kurudi.
Inatakiwa mahira ya saa nane na dakika kadhaa
kabla ya saa tisa niwe nimeshamaliza matumizi ya
maji hayo lakini njiani gari linapata pancha tairi
mbili…majira hayo sasa ni usiku na mbali kidogo
kufika nyumbani kwetu…dereva aliniomba mimi
nikimbie kwenda nyumban yeye atalala kwenye gari
mpaka asubuhi akisubiri msaada ili arudi na gari
yake. Sikuweza kumbishia ndipo nilichomoka na
kuanza mkukumkuku kukimbia kuelekea nyumbani.
Gari aina ya taxi likiwa linanifuata na kunipiga
mwanga mkali wa taa ulinifanya nisimame na kwa
bahati nzuri alinipatia rift baada ya kuonekana na
yeye anaelekea mitaa ambayo mimi nakwenda.
Nikiwa nyuma ya gari nimeyashikilia yale maji
kwenye chupa ghafla nikahisi mabadiliko wa dereva
wa lile gari japo ni usiku lakini muda namuona ana
nywele nyingi ndefu kama wanawake wa kiindi
baada ya muda namuona umbo la mwanaume
nywele chache, nikabaki hoi sifahamu nini nifanye
na gari lipo kwenye mwendo mkali. Tulifika sehemu
moja mataa magari yamezuiliwahapo ndipo
nilipokuja kumfahamu kuwa si binadamu wa
kawaida baada ya kugeuka na kuniangalia kwa uso
wake wa kutisha akiwa kakasirika….
Niliomba mungu nikafungua mlango japo magari
yalianza kuruhusiwa nikachomoka mule ndani kisha
nikaanza kukimbia, kwabahati nzuri kulikuwa na
magari ya abiria kwa wale ambao walikuwa
wamechelewa kutoka kazini hasa wale wa shifti
nilijikuta naparamia japo lilitaka kuondoka mkononi
nikiwa na maji yangu. Gari liliendelea na mwendo
wak, lakini kwenye ile siti niliyokaa pembeni yangu
alikuwa mwanaume niimpa salamu akaitikia lakini
karibia na sehemu ya kushuka yule jamaa
akabadilika na kuwa sura ya salha aisee nilisimama
na kumlazimisha konda anishushe haraka sana.
Lakini nachungulia nje nawakuta akina salha kama
watatu hivi nikarudi ndani ya gari humohumo, watu
walinicheka na kunibeza kwa kuniita mshamba hali
hawajui nini kinanisibu.. sasa wale wote ndani
nikawa nawahisi kama salha tu usoni kwao. Mpaka
pale niliposhuka nikakimbia sana hadi getini kwenye
ile nyumba na kuomba kufunguliwa. Mlinzi alifungua
geti akiwa anashangaa akajua ni majambazi hivyo
akafunga haraka sana. Nilipoingia ndani moja kwa
moja chumbani kwangu nakuta kufuli limewekwa.
Nikaelekea kwa mma Penina kule namkuta akiwa
kalala tayari. “mama penina kuna hatari kubwa
inakuja mbele yetu sasa” nilimshtua toka usingizini
“hatari,,,,ipi tena”. “tufanye haraka sana maji haya
kafungue mlango nichukue zile dawa haraka sana”.
Alinishangaa ninavyotweta “kufungua mlango gani
tena na wewe?” “mlango wangu umefungwa kule na
ndiko dawa nilikoweka”. “Khaaa! Mimi sijafunga”
“hujafungaaaaa?” alitoka kitandani na kwenda
kuangalia mlango wang una kukuta umefungwa na
muda ndio huo unaisha na dawa zipo chumbani
kwangu maji yapo.”daaah! eheee! Dereva yuko
wapi?” aliuliza “yeye gari limepata pancha hivyo
kaamua kulala kwenye gari mpaka
utakapompelekea usaidizi”. Tulichanganyikiwa huku
tukijaribu kuvunja mlango huo bila mafanikio…………
 
SEHEMU YA AROBAINI NA MBILI 42.
ENDELEA………….
Mama penina alizidi kunishangaa wakati mimi
nikiendelea kumtumbulia macho. Mama penina
hakuwa na aibu yeyote ile kwa wakati huo aliinuka
akiwa kama alivyozaliwa ndipo mimi nikageuka
nyuma nikitaka kujificha, “khaa! Wewe vipi unajificha
kwani cha ajabu kitu gani hapa kama kuona
umeshaona nitokee mimi hapa”. Alipomaliza
kujitanda “Mama mimi nimejaribu sana kuufungua
lakini nimeshindwa sijui hata nani ambae kaufunga”
nilimuambia mama penina aliyekuwa tayari kavaa
taulo lake.
“sasa wewe mwanaume unashindwa kufungua
mlango je? Mimi nitaweza kweli”tulirudi tena kwa
mara ya pili kuusukuma ule mlango lakini hakuna
kitu tuylichoambulia jambo la mwisho ni kuvunja ule
mlango ndipo nilielekea jikoni ili kuchukua nyundo
ambayo huwa wanaitumia sana kupasulia mkaa na
nazi wakati wa kupika. Muda huo jasho linaendelea
kunitoka kwa hofu kwa sababu muda umekaribia.
Nilifika pale nikiwa na nyundo yangu lakini
sikumkuta mama penina, “mh! Huyu mama tena
kaenda wapi nah ii nyumba ya watu kuvunja
unaweza kugeukiwa tena kulipa” nilijisemea
mwenyewe baada ya kuona mama huyo katoka
ghafla. Ndipo mlango unafunguliwa wan je aliingia
mlinzi na mama penina kumbe alienda kumuita yule
mlinzi.
Mlinzi alikabidhiwaa ile nyundo akaanza kupiga kwa
nguvu lakini ilishindikana kwa kweli ilionekana
jambo la ajabu kufuli dogo kama lile kushindwa
kuvunjika, wote tulichemka kabisa kufungua ndipo
mlinzi aliondoka kuelekea sehemu yake. Tulibaki
kuangaliana maana hakuna jinsi tena, “Mnali
tunafanyaje sasa hapa maana kama dawa iko huku
na mlango ndio hivyo haufunguki lakini hay ani
maajabu kabisa maana sio rahisi kuamini kabisa”
alisema mama Penina. “ndio hivyo mama…” “weee
komaaa mama yako nani kwa nini usiniite tu my
eeh!” aligomba mama huyo na kunifanya nikae
kimya “ sawa ila labda ungejaribu kumpigia kwanza
yule mganga japo ni usiku labda anaweza kuamka
na ukamuuliza anatusaidiaje”.
Nilitoa wazo la mama penina ampigie yule mganga
baada ya kushindwa kufungua mlango. “mh! Sasa
hivi ni usiku tutakuwa tunamsumbua…ila mnali
kweli hukufunga mlango wewe ulivyotoka”. “Mh!
Sikumbuki vyema ila sikufunga”. Mama penina
akanyanyua simu kisha akampigia yule dereva.
“halooo!...Moris mama penina hapa”. “ndio bosi
habari yako…” “salama ehee! Unaendeleaje na hali
sasa”. “mama usihofu naendelea vyema vipi mnali
kafika salama hapo nyumbani?” “ndio kafika hapa
ila kuna shida kubwa sana huku nyumbani…” “mama
shida gani tena hiyo?” “mlango wa mnali haufunguki
hata kwa kuvunja kufuli yake..” “mama! Mbona
mnali alisahu funguo kwenye gari hapa alivyotoka?”.
“unasema….” “ndio funguo ninayo hapa alale tu
kesho asubuhi maana niko porini”.
Maneno yale niliyasikia vyema sana lakini akili
yangu haikuweza kupambanua kama kweli nilifunga
mlango na kuacha kule kwenye gari. “haya ulijifanya
ukaidi sasa kikowapi mbona umeacha kwenye gari
funguo…” akiwa ananiongelesha mimi aliendelea
kushika simu yake na wakati huo ni saa nane na
dakika hamsini na dawa ipatikane kabla ya saa
kumi alfajiri. Aliinua sim una kuiweka sikioni tena
kisha akawa anaisikiliza. “haloo babu! Habari tuna
matatizo hapa”. Kumbe alikuwa anampigia yule
mganga nilifurahi sana maana niliona kumpigia
dereva wake kama anapoteza muda tu. “ndio! Yapi
hayo…”.
Mganga aliuliza kwa sauti ya chini sana alionekana
alikuwa tayari kwenye usingizi. “Mnali alitoka hapa
akiwa kafunga mlango wake na kuelekea huko
baharini akiwa na dereva wetu yule, ajabu sasa gari
limeharibika karibu tu na hapa nyumbani lakini
dereva kabaki hakutaka kuliacha lenyewe, mnali
anarudi nyumbani akiwa na yale maji sasa kila
tukifungua mlango haufunguki ni mgumu…”. Mganga
alicheka sana baada ya kumueleza yale mambo
“mama unasikia..” “ndio nakusikiliza mkuu”. “Hao
watawachanganya sana mnadhani kuwa hapo kuna
kufuli, laaah! Hakuna kufuli hapo kuna kitu tofauti
kimewekwa mimi nakiona hapa…mpatie simu huyo
kijana”. Nilipewa simu niliipokea na kuiweka
sikioni. “Kijanaaa!....” “ndio babu”.
Alichokiongea kilinivunja nguvu sana hadi nikaiacha
simu pale kwenye kochi. Nilijitupia kwenye kochi
nikiwa nawaza lile jambo ambalo mganga
amenieleza nilifanye. Mama penina alikuwa anazidi
kunihoji sana maana alitamani kujua yale ambayo
tulikuwa tukizungumza na mtaalamu. Alipozidi
kuongea Zaidi nilisimama na kumuangalia kwanza
“mama samahani ngoja nikirudi bafuni nakuja
kukuambia alichoniambia mganga kwanza yale maji
yako wapi”. Nilichukua chupa ya maji ya bahari
kisha nikanawa mikononi kisha na usoni baada yah
apo nilielekea bafuni.
Mganga aliniambia pale mlangoni kuna kitu tofauti
na ile kufuli tunayoiona na ili kuweza kufungua pale
au kile kitu kitoke basi inabidi niwe na uwezo wa
kuona kilicho pale, sasa kitu hiko nakiona vipi?,
ndipo akaniambia lazima nitoe mbegu zangu za
uzazi kisha nichanganye na maji ya bahari kisha
nipakae usoni mara tatu kisha nielekee pale
mlangoni. kwangu ulikuwa kama mtihani mkubwa
sana kufanya vile, kwa kuwa muda ulizidi kusonga
niliamua kuelekea bafuni na kuanza kujichua jambo
ambalo mama penina alilisikia na kunifuata. “khaaa!
Wewe mnali ina maana mimi sijakuridhisha mpaka
ufikie hatua hii mbona unanifanya nijione
sijakamilika mwenzio eeeh!”.
Aliongea mengi sana kwa kuwa hafahamu
nilimuacha tu na mimi nikamaliza kisha nikapakaza
mikononi mwangu kisha nikanawa kulekule bafuni
kisha nikatoka. Safari ilienda hadi pale mlangoni
sikuamini kabisa jitu lamkutisha lililokuwa limezuia
ule mlango pale. Aliondoka baada ya kugundua
nimemuona. Akili ya ujasiri ilinijia haraka haraka
sana na kushika ile kufuli na kuigonga mara moja
na kufungua kirahisi sana. Kila mmoja hakuamini
hasa mama penina maana alizidi kuniuliza maswali
mengimengi nimefanikiwa vipi mpaka kufungua.
Niliingia ndani kutokana na muda nilifanikiwa
kuchukua zile udi kumi na mbili pamoja na ubani
kisha nikaelekea kule chumbani kwa mama penina
ndipo nikachukua maji na kufanya kama
nilivyoagizwa kule.
Mara moja nikanawa na nikamaliza kila
kilichotakiwa na muda saa kumi ndio hiyo ikaingia.
Mwanzo kila muda kichwa kilikuwa na maluelue ya
kila aina lakini baada ya kupaka ile dawa na
kuinywa pamoja na kufukiza udi na marashi ndani
kote kichwa change kilitulia sana. Baada ya
kumaliza ndipo mimi na mama penina tulitulia
pamoja kwenye kochi tukifikilia yaliyopita na
kumfikilia yule dereva. “unajua mnali hatujalala
kabisa maana leo tumekesha kabisa”, “ndio kwa
sababu ya hali iliyotokea ila mimi niseme
nikushukuru sana mama ya…” mama penina alikata
ulimi kwa kusema “mara ngapi nikuambie jambo
hilohilo..” “sawa nikuitaje sasa maana mimi
nimezoea”.
Mama huyo kama kawaida alienda kufunga mlango
na kunihakikishia kuwa chumbani kwake sitoki
kabisa. basi tulilala mpaka asubuhi majira ya saa
nne ndipo usingizi unaisha kutokana na purukushani
za dawa na zile za ziada za mama penina. Ikawa
sasa mimi na mama huyo kama mt una mumewe.
Asubuhi hiyo alipigiwa simu kuwa anahitajika ofisini
mara moja ndipo akaniaga huku akiahidi kuwa
atampitia mapema sana yule dereva wake. Niliamini
sasa Maisha yangu yanaanza kurudi kama mwanzo
baada ya kupata uzima ule wa kutokukumbuka hata
nyama mbichi na mambo ya maajabu ajabu. Nikiwa
nawaza sana niliona vyema nifungue televisheni
kupata habari za hapa na pale huku nikimsubiri
dereva. Niliendelea kuangalia ghafla usingizi ulinijia
ndipo ghafla ndoto ilinionyesha mambo kadhaa ya
mbele.
Niliota njozi kuwa kuna siku moja jamaa mmoja
ambae sikumfahamu anaitwa nani tulikutana
bandarini mimi nikiwa nafanya kazi za ubebaji
mizigo kutoka kwenye meli za mizigo. Ndipo mzee
mmoja wa makamo anashuka kwenye meli ya abiria
na ndipo kwa bahati mbaya sana tukakumbana pale
ana kwa ana akadondoka chini na kufanya achafue
suti yake. Yule mzee aliniongelea maneno mabaya
sana huku akitoa kauli za ajabu mbele yangu. Kila
nikimuomba msamaha lakini anazidi kuongelea
mambo mabaya Zaidi, alijitapa sana kuwa yeye ana
hela nyingi sana anaweza kunifunga ama kuniua
muda mfupi tu. Sikujali kutokana nay ale niliamini
ndivyo watu walivyo kila siku. Niliendelea na
shughuli zangu za ubebaji wa mizigo hadi jioni na
kupokea ujira wangu kulingana na ukubwa wa kazi
niliyoifanya.
Ndipo nikaanza kutafuta njia ya kwenda nyumbani ili
nikapumzike. Ghafla nikiwa barabarani gari lilikuwa
linapiga honi kubwa sana lakini nikawa siisikii
niliendelea kutembea. Ghafla gari lile lilikuja
kunigonga kichwani”….. Nilishtuka kutoka usingizini
baada ya kujua kuwa ndoto nilikuwa naiota.
Namuona moris yule dereva akiwa nyuma yangu
kanishika kichwa “aiseee nimepiga honii nyingi huko
nje mlinzi sijui alikuwa wapi nakuja hapa wewe
nawe umelala…” Mh! Nilishtuka na kushangaa sana
“kaka unajua hata sielewi hapa nilipo kabisa”.
“kivipi tena”. Yani nimeota ndoto na haya mazingira
unayoyasema yananipa wakati mgumu sana
kuitafsiri ndoto hiyo”. Nilimueleza, “ndoto gani hiyo
unaweza kunieleza kidogo”. “Nimeota nikiwa
barabarani alafu gari linapiga honi kwa nguvu alafu
mimi siisikii kabisa kumbe ni wewe huko nje! Alafu
baada ya kutoisikia ndipo likaja kunigonga kichwani
lile gari kumbe ndio wewe hapo umekuja kunishika
kichwani kumbe ndio wewe hapo.” Basi pale
tulibaki tukicheka sana, maongezi yaliendelea na
ndipo akanisimulia alivyotoka kule na mimi pia
nikamsimulia kila kitu kuhusiana na kumaliza ile
dawa na sasa hakuna kiumbe ambacho kinaweza
kunisumbua tena.
Tulipungiana mkono kwa furaha Zaidi. Majira ya
jioni ndipo mama penina anaingia akiwa kachoka
mno, haikujulikana kwa nini kakosa furaha kiasi kile.
Tulimuuliza ndipo aliniomba nimfuate. Nilinyanyuka
tukaelekea hadi chumbani kwake haikuchukua muda
mrefu nilitoka na kufika pale sebuleni. Yule dereva
aliniangalia sana huku akitoa wasiwasi na mimi
nililigundua hilo mapema sana. Mama penina alikuja
pale sebuleni na kuanza kusema jambo ambalo
mimi pamoja na moris tulishtuka sana…
 
SEHEMU YA AROBAINI NA TATU 43
ENDELEA……….
Mama Penina alikuja pale sebuleni akiwa kachoka
kweli hata sisi alizidi kutushtua maana si kawaida
yake. Mimi pamoja na yule dereva tulimuangalia tu
na tusijue nini cha kufanya maana tulibaki
kumtazama tu. “Mama Penina nini kimekukuta
mbona uko kwenye hali hiyo?” Nilimuuliza huku
nikiwa kwenye hali ya mshangao. “Mh! Kuna tatizo
ambalo lipo hapa ila achene tu tuendelee na
mambo mengine kwanza” alisema mama huyo na
kutufanya sisi wote tukae kimya kabisa. Moris
ambae ni dereva wa gari mule ndani alisimama na
kutoka nje kisha akatuacha tukiwa ndani wawili.
Hapo sasa nilipata muda wa kutaka kujua kile
ambacho kinamsumbua maana nilijua kuwa alikuwa
anamuogopa Moris. “haya sasa Moris katoka
tumebaki wawili ebu nieleze kipi ambacho
kinakusumbua”. Mama penina aliniangalia kisha
akaanza kwa kusema.
“Mnali mwanangu Penina kalazwa huko ambako
anasoma, sasa natakiwa nikamuangalie hali yake na
natakiwa kesho nisafiri hapa nielekee marekani”.
Nilishtushwa na ile taarifa lakini kwa sababu
sikuwahi kumuona mtoto wake na kasema
anaumwa sikuwa na upinzani kwa sababu mimi pale
ni kama mkimbizi tu basi, nilimpa pole na kumtakia
safari njema huko aelekeako.
“Ila kabla hujatoka nataka nikufanyie mambo matatu
muhimu maishani mwako kwanza”. Nilimuangalia
kwa mshtuko “mambo gani tena hayo?”
“Baada ya kukusaidia kukutibia kutokana na ile hali
yako basi mambo matatu hayo kwanza nitakupatia
fedha ya kuendesha Maisha yako, pili nitakununulia
nyumba kule ambako ulikuwa unaishi na jambo la
tatu nitakupatanisha wewe pamoja na mkeo na
mtoto wako nikiwa na maana mimi na wewe sasa
Maisha yetu yatakuwa ndio mwisho”.
Nilishikwa na bumbuwazi la ghafla kwanza
“Ina maana mama penina mimi na wewe ndio basi
kivipi yani au ndio kwa sababu mwanao
anaumwa?”. Aliinamisha kichwa chake chini huku
kama akitaka kutoa chozi
“Aaaah! Hapana sina maana hiyo ila usijali ngoja
nifanye mpango wa haya niliyokuambia kwanza.”
Ilipita siku mbili ili nilipata nyumba yangu nzuri, kwa
kweli nilifarijika sana baada ya kuona mimi pamoja
na familia yangu tukiwa pamoja. Hadi hapo mimi
na mama Penina tuliachana baada yaye kuniahidi na
kuniambia kuwa yeye anaelekea marekani kwa ajili
ya mwanae ambae ni mgonjwa huko aliko. Mimi
nikiwa na familia yangu pamoja hasa nilichokapenda
ni kumuona mwanangu akiwa mbele yangu.
Niliacha kazi za uvuvi na kuanza kazi za uuzaji wa
nguo kwa sababu fedha za mtaji nilikuwa nazo.
Watu kadhaa ambao walikuwa karibu na mimi kwa
kile kipindi ambacho nilikuwa na matatizo makubwa
yale walizidi kunichanganya kwa kuendelea
kuniogopa kwa kudhani kuwa mimi bado nipo nay
ale mambo n ahata kama nikiwaeleza kwa kina
kuwa nimepona lakini ilikuwa ngumu sana wao
kunielewa. Usiku mmoja nakumbuka niliota ndoto
mbaya sana ambayo inafanana moja kwa moja na
ile ambayo niliipata nikiwa kwa mama Penina.
Niliamua kumueleza mke wangu ukweli kuhusiana
na ile ndoto lakini sasa ikaja kuleta mtafaruku baina
ya mimi na mke wangu juu ya mama penina. “Ehee!
Ndio maana mimi nikawa nashangaa mama penina
yule akununulie gari kwa msaada gani kama
hukuwahi lala nae eeeh! Nimabie ukweli la sivyo
hapa hapataeleweka”.
Mke wangu aling`aka sana kuhusiana na lile swala
la mimi na mama penina.
“Sasa mke wangu shida iko wapi….”
“huoni shida si ndio…kama hukuniambia ukweli
ulikuwa nae kivipi yule mama utanieleza leo hii la
sivyo mimi na wewe kila mmoja agawane chake
aondoke moja kwa moja siwezi kuishi na
mwanaume mzinzi”.
Nilimuangalia kisha nikaanza kucheka kwa
kumdharau sana mama Asante.
“Wewe mwanamke unasema jambo gani mbele
yangu sasa hivi…”
“Hujanielewa nini kila mmoja afe na chake”
“Mpumbavu wewe yani huna hata adabu kukusitiri
kote kwenye hii nyumba lakini bado unaleta kiburi
nyumba yangu mimi nakuruhusu nenda kama
umechoka unajua jinsi gani mimi nimehangaika na
Maisha haya mpaka sasa nimefikia unajua mangapi
nimepitia?”
Tuliendelea kulumbana hadi nilipoamua kumfukuza
yeye aondoke kabisa pale.
“Naondoka na mwanangu unadhani nitashindwa
kumlea eeh! Nenda zako huko mwanaume gani
unalelewa na mwanamke”.
“Sawa huyo ni damu yangu na hapo anaelewa nini
ambacho anakisikia na kama atakuwa na akili ya
kumjali baba yake basi atakuja hap ani kwake na
hizi ndio mali zake hakuna mwingine zaidi”.
Waliondoka na kuniacaha mimi peke yangu, zilifika
siku tatu bila hata ya kumuona Asante wala mama
yake ila nilishukuru baada ya kujua kuwa Maisha
yangu yatakuwa mazuri kwa sasa. Ilikuwa siku ya
tatu ndipo nikaelekea kwenye mihangaiko yangu ya
kawaida. Nilikutana na baadhi ya vijana ambao
tunafanya kazi ya kuchagua nguo ili kuendelea
kufanya biashara zetu. Nikiwa kwenye mihangaiko
na huyo jamaa tulifanikiwa kupata zile nguo na
tukakaa kwenye moja ya kijiwe maarufu hivi
tukipiga stori za hapa na pale.
“Mnali hivi unayaonaje haya Maisha kwa upande
wako? Maana mimi siyaelewi hata kidogo yani”.
Aliongea yule mwenzangu huku akisubiria majawabu
toka kwangu
“Ni kweli Sudi najua Maisha ni magumu ila naamini
tunatofautiana Maisha yetu inawezekana wewe
ukawa na Maisha mazuri kidogo lakini mimi
niliyopitia ikawa Zaidi ya ugumu”
“Haaaa! Haaaaa! Mnali unanichekesha kwa kweli
nadhani mimi ndie mwenye Maisha magumu Zaidi
ya wote hapa unajua kwa nini?....”
“Eheee! Nipe habari”>
Alianza kunihadithia huku tukiendelea kuziweka zile
nguo vizuri.
“Mnali mimi nimepitia Maisha magumu sana,
nilikuwa naishi kwa ndugu zangu lakini baba na
mama walipofariki ndugu zangu walinikataa na
kunifukuza kule kijijini, ndipo nikakimbilia huku mjini
na nimefika hapa nikawa naishi kwenye vijiwe na
majumba mabovu mpaka pale nilipoanza kazi za
kubeba mizigo Napata ela ya kula ndipo Napata
kuishi lakini ukweli nilipata tabu maana mvua, jua
vyote vyangu hadi sasa unaniona namshukuru
mungu sana”.
Nilimuangalia sana huku nikisikitika kwa yale
ambayo amepitia kama kijana wa kiume lakini bado
niliona hana mfano kabisa na mimi.
“Ehee! Na wewe Rafiki yangu maana ulisema kuwa
nikikuhadithia na wewe utanihadithia”
Nilianza kwa kukohoa kidogo kisha nikaanza
kumueleza moja baada ya mwingine.
“Sudi Rafiki yangu, unajua Maisha yangu yamepitia
sehemu nyingi sana nimeanzia baharini, nikakutana
na vimbwanga vingi vya ajabu, mizimu na wafu
waliokufa na mambo mengi sana,….hivyo mpaka
sasa nimepitia sana Maisha hayo ya kupishana na
majini na mizimu tulipitia mpaka kwa waganga,
unajua ukifikia hatua ya kuishi sehemu kama hizi
Zaidi ya miaka tano nyuma imepita. Mambo
hayakuishia hapo mke wangu aliniacha kutokana na
Maisha yangu kuwa magumu sana na hatimae
akamchukua mwanangu na hadi sasa nina muda
mrefu sijamuona”.
“Mnali kwa kweli pole sana ama kweli nimeamini
kuna watu wanapitia Maisha magumu sana sikuwahi
kuwaza kitu kama hiki kwa kweli pole sana tena
sana”.
Wakati tunaendelea kuongea pale ghafla gari lilifika
karibu yetu ila lilionekana kuwa na hitilafu maana
hata mwendo wake ulikuwa wa tofauti kidogo. Gari
hilo lilikuja hadi karibu na pale kisha lilionekana
kuzimika na kila kadri alivyozidi kulishtua
lilishindikana kabisa kila kadri alivyoliwasha liliishia
kulia na kuzimika, ndipo mzee mmoja wa makamo
alishuka na kutuelekea hadi pale tulipo.
“Sudi unaona watu wenye Maisha yao hao sasa sijui
anakuja kutuambia nini huyu mzee”
“Ngoja tuone”.
Mzee huyo alikuwa amevalia nguo aina ya kitambaa
fulani hivi juu na chini vikifanana rangi zake alikuja
hadi pale kisha akatusalimia.
“Hamjambo vijana”.
“Hatujambo mzee shikamoo”.
“Marhabaa sasa nina shida kidogo gari langu
limeharibika sijui mnaweza kunieleza wapi ambako
gereji inapatikana?”.
Tuliangaliana pale lakini kwa ujuzi wangu
nakumbuka nilishawahi kuchezea haya mambo
kidogo ndipo niliposimama na kumuomba mzee
tukaliangalie gari lake
“Daaah! Pole sana ebu ngoja niliangalie labda
inaweza kuwa tatizo dogo tu ukaenda liwa na wazee
huo”.
Tulifuatana hadi pale kwenye gari kisha nikafungua
mbele kwenye injini lilikuwa ni aina ya Taxi
nilimuombaawashe ili niweze kutambua tatizo
alipowasha nikagundua shida iko wapi. Nilimuomba
spana kama alikuwa nazo kwa bahati nzuri alikuwa
nazo nilikaza baadhi ya pipe kadhaa ambazo
zilikuwa zinatoa presha nje na kufanya gari
lishindwe kuondoka. Hadi kwenye system ya
umeme pia yani Betri lilikuwa linasumbua zile nyaya
moja ulichomoka nilipoipachika akawasha mambo
yakawa vyema kabisa.
‘Mzee tayari hapo unaweza kuondoka sasa”.
“Aaaaah! Nashukuru sana sasa shikeni hiki kiasi
kitawasaidia jamani”.
alitoa kiasi cha shilingi elfu thelathini mimi
niliikataa ile ela.
“Mzee hapana nimekusaidia tu bwana maana kwa
kweli binadamu tunasaidiana hii sio kazi yangu
ingekuwa kazi yangu ningekukubalia”
“Mzee nipatie mimi hiyo hela kama yeye
anaikataaa”
Alikuwa Sudi, nilimshangaa kwa kweli aliichukua na
palepale akaondoka zake akasahau kama tulikuwa
pamoja sote pale.
“Basi kijana kama hutojali nikusindikize hadi karibu
hivi alafu nikuache mbele huko”.
“Nashukuru sana mzee wangu”
Tuliondoka moja kwa moja hadi kwenye mtaa
mmoja ambao nilikuwa naufahamu nilimuuliza kama
yeye ndio anaishi kule akanijibu ndio ila alikuwa nje
ya chi kwa muda ki kazi hivi ndio maana hakuwepo
hapo kwa muda huo.
“Sawa mzee wangu basi mimi acha niishie hapa
nadhani siku nyingine tutaonana”. Alinipatia namba
yake kisha mimi nikaendelea na matembezi yangu.
Siku iliyofuata nilikuwa natoka kwenye moja ya njia
kuelekea mtaa wa pili huku nikiwa nawaza juu ya
Maisha niliyonayo kwa zile nyakati kwa bahati
mbaya gari lilinivamia na kuniangusha nhadi chini na
kukosa fahamu kabisa. Nakuja kushtuka nipo
kitandani alafu ni usiku na nimewekewa dripu
nyingi, nilishtuka baada ya kujua niko hospitali pale.
Nilishindwa kutoa sauti kutokana na hali niliyonayo.
Asubuhi na mapema Manesi wanaingia na kuanza
kunihudumia mimi nikiwa sitambui nini kinanisibu
ndipo kwa mshangao mkubwa ndipo anaingia mtu
ambae sikudhani kama atakuja pale………
 
SEHEMU YA AROBAINI NA NNE 44
IMEDHAMINIWA NA: Mudhihili Media
ENDELEA………….
Ghafla uso kwa uso nakutana na yule mzee ambae
nilimsaidia kumtengenezea gari lake baada ya
kuharibika. Moyo wangu ulijawa na mshangao kwa
kuhisi ni yeye ambae alinigonga au ni jambo gani
liliweza kutokea siku ile. Baada ya manesi kumaliza
kunihudumia ndipo mzee yule alikaa kwenye kitanda
kisha na kuniangalia kwa makini sana mpaka
nikawa nina hofu.
“Kijana pole sana kwa ajali iliyokutokea, ila
natumaini utaendelea vizuri bila shaka”. Hapo ndipo
nikagundua kuwa nilikuwa nimepata ajali ya
kugongwa na gari.
“Ahsante ila sijajua ajali imetokeaje maana
sikumbuki chochote sasa hivi”. Nilimueleza
“Ni kweli huwezi kukumbuka jambo lolote sasa
maana nadhani kutokana na kupoteza kumbukumbu
kidogo hiyo ndio sababu ila baada ya matibabu
kukamilika utakuwa sawa kabisa usijali”.
“sawa mzee nashukuru ila kama nakukumbuka
mzee si ndie ambae nilikutengenezeaga gari jana
au”
“Aaaaah! Ni kweli ndie mimi ila haikuwa jana
ilikuwa majuzi una siku tatu tangu uletwe hapa”.
Maongezi yaliendelea mimi pamoja na mzee huyo
ilitokea kufurahi sana.
“Lakini sababu ya mimi kupata ajali ilikuwa nini n
ani nani ambae alisababisha?”
Nilimuuliza tena swali baada ya muda kidogo kupita
“Mimi nilikukuta tu umedondoka maana ulikuwa hali
mbaya kwa kweli”.
Ilichukua siku mbili baada ya yeye mzee kufika pale
na alikuwa anajitahidi kila siku kunijulia hali. Siku ya
tatu alikuja na kutaka kunichukua baada ya
matibabu yangu kuwa tayari yamekamilika na hali
yangu kuwa nzuri sasa.
Alichukua jukumu la kunihudumia kwa kunipeleka
nyumbani kwake ili kuendelea kupata huduma zote
zinazostahiki alikuwa kama baba yangu sasa maana
kwa upendo aliokuwa ananionyesha. Tulipanda
kwenye gari lake na moja kwa moja safari ilianza
kuelekea nyumbani kwake.
“Kijana samahani sikuwahi kukuuliza jina lako
unaitwa nani?”
Aliniuliza
“Mimi naitwa Mnali”
“Sawa jina zuri mimi naitwa bwana Moka, sasa
tunaelekea nyumbani kwangu mpaka pale
utakapopata nafuu kabisa wewe sawa na ndugu
yangu kwa sasa”. Alinieleza hayo maneno na
kunifanya nijione mwenye bahati sasa baada ya
kufanyiwa huduma kubwa kutoka kwa mganga
kupitia msaada wa mama Penina.
Safari ilinishangaza sana baada ya kuona geti la
mama penina na gari likawa linasimama kwenye
geti lile na kupiga honi kwa ajili ya kufunguliwa geti
lile.
“Mzee Moka samahani ina maana hii ndio nyumba
yako wewe au tunapitia tu”
Mzee alicheka sana huku akiniangalia na kunishika
bega
“Ndugu yangu hapa ndipo nyumbani kwangu nah ii
ni nyumba yangu ambayo tutaishi mimi na wewe
sawa au unapajua hapa?”
Aliniuliza swali gumu ambalo lilinifanya niwe na
hofu kwani mlinzi akiniona tu itakuwa kesi kwa
sababu kama ni nyumba yake basi mama penina
atakuwa mkewe.
“Hapana yani nilikuwa nashangaa jinsi nyumba
ilivyokuwa kubwa sana ndio maana”.
Ghafla geti lilifunguliwa na gari likapata kuingia
ndani. Wakati natoka moyo wangu uliendelea
kutokuwa na amani kabisa ila cha ajabu mlinzi
hakuwa yule ambae nilikuwa namfahamu kwa wiki
kadhaa zilizopita. Tuliingia ndani wote kwa pamoja
huku nikiwa na mabendeji kichwani na mkononi.
Mzee Moka alionekana haswa kuwa ile ni nyumba
yake na mimi nimeingia kwenye himaya hatari
kabisa.
“Mke wangu mama Peninaaaa haya nimerudi kutoka
hospitali na mgonjwa wetu nimekuja nae kwa hiyo
fanya haraka sana uandae chakula kisha apumzike”.
Ilikuwa ni kauli iliyomuamuru Mama Penina afanye
yale ambayo aliyakiwa kuyafanya na Mumewe, kwa
hamu nilikuwa ninamsubiri huyo mama Penina ni
yuleyule au yupi maana ninaemfahamu mimi
aliniaga kuwa anakwenda Marekani kwa ajili ya
mwanae penina.
Sikuamini macho yangu ninapoweza kuonana na
yule mama macho yake na yangu yalikutana na
kutumbuliana kana kwamba mmoja wetu kaona
mzimu.
“Vipi mama penina unamuangalia hivyo kuna shida”.
“Hapana….” “sasa mbona unamtazama hivyo”
“Nilikuwa sijamuona kama kaumia hivi ndio maana
namuonea huruma sana kijana wa watu”.
Basi tulikaa tukapata kula chakula hadi pale
tulipomaliza. Vimbwanga vya hapa na pale
viliendelea baada ya mumewe kwenda kazini huku
nyuma mama penina hakutaka kuniacha salama.
Alihitaji kabisa niondoke pale maana siku akija
kufahamu mumewe basi atakuwa kwenye hali
mbaya sana.
Ilikuwa usiku mmoja nikiwa nimelala ndipo nasikia
mume na mke wakigombana huko chumbani kwao
kipindi hiko hali yangu ikiwanzuri na nilikuwa
nimepona kabisa.
sababu ya ugomvi wao sikuifahamu kabisa maana
nilikuwa chumbani kwangu nikiwa nimelala. “Mh!
Watakuwa wanagombana jambo gani usiku huu isije
kuwa sababu ni mimi” nilijiuliza sana maswali
mengi ambayo sikuwa Napata majibu yake Zaidi ya
kubaki yakielea tu kichwani mwangu”. Mpaka
asubuhi na mapema ninaamka lakini nikiwa na
mawazo ya kuondoka mule ndani. Mzee Moka
alikaa sebuleni na kutuita kuanzia mimi mkewe
mtoto wake Penina pamoja na wafanya kazi na
hatimae nikafanikiwa kumuona na Derick yule
dereva wa gari.
Nilijua leo kuna kazi kubwa ambayo inakuja
kutokea.
“Mke wangu nilikuacha humu ndani Zaidi ya mwaka
mmoja nikiwa na maana nilienda safarini kikazi,
nilikuacha humu ndani ukiwa wewe na hawa
wafanyakazi huyu pamoja na Derick, kweli ama si
kweli?”
Mzee Moka alimuuliza mkewe
“Ndio kweli mume wangu”.
“Ehee! Kijana ebu eleza ukweli ambao ulinieleza
jana” alimuita yule kijana mfungua geti “Baba mimi
kweli nilikueleza ila yule mwenzangu ndie ambae
anafahamu kila kitu”
“Sawa ebu nenda kamuite hapo kibandani mwambie
geti afunge na kufuli kabisa kisha aje humu ndani”.
Kufikia hapo nikagundua pamenuka na ule ulikuwa
kama mtego kwangu.
“Mnali ebu nikueleze ukweli mwanzo nilikuwa
nakutafuta sana labda jambo ambalo ulikuwa hulijui,
ile siku nakuja pale upo wewe na Rafiki yako
nikajifanya gari bovu sana hapana kila kitu
nilikilegeza mwenyewe ili nipate kukupata wewe
vizuri, Maisha yako nimeyafuatilia sana baada ya
kugundua wewe umetembea na mke wangu huyu,
na isitoshe wewe ukadiliki kufanya nae mapenzi na
ukaishi hum una siku ambayo unapata ajali ile
nilisababisha mimi….”
Nilishtuka ghafla hofu ikinitanda pale
“Unashtuka nini….nilifanya vile kukuua kabisa
mpumbavu mkubwa wewe na isitoshe nikaona
umeshindikana kukuua nikakuchukua na kukuleta
hapa nyumbani uje kujua kwa sababu gani nataka
kukuua nakueleza haya maana naona huyo
anachelewa kuja, Derick ebu eleza ukweli kuhusiana
na huyu kijana…”
Derick aliniangalia kwa aibu kubwa ila hakuwa na
jinsi maana bosi wake ndie kamueleza afanye hivyo.
Wakati Derick anaeleza dhambi zangu tulizozifanya
mimi na Mama Penina ndipo Mlango unafunguliwa
anaingia yule mlinzi pamoja na Mama Asante
ambae ni mke wangu akiwa amefura kwa hasira
sana. Nikajua leo ni leo asemae kesho ni muongo
jasho zito lilinijaa maana sin ahata hali ya kufanya
lolote pale, ndipo nikakumbuka enzi zile ambazo
nilikuwa na uwezo wa kugeuka hata kiumbe la ajabu
hapa ingekuwa msaada wangu tosha lakini sasa
nimepona.
“Mnali huyu ni mke wako msikilize anachosema
kisha mbishie”.
“Bwana Osward sikiliza! Huyu hatakiwi kuishi hapa
duniani maana kwa aliyokufanyia si muungwana
kabisa hawezi kuishi na mkeo hali anajua ana mtoto
wake hapa, hajui anasoma nini anaishi wapi na kwa
bahati mbaya sasa mkeo kamnunulia nyumba huyu
mpuuzi pamoja na kumpa ela ya mtaji”. Mama
Penina alikuwa analia tu hajui afanye nini.
Mama Penina alinifanya nikumbuke mengi sana
ambayo niliyapitia na kuona kuwa bado safari ya
Maisha yangu yapo kama Mvuvi haya ndio
(MAISHA YANGU YA UVUVI Mvuvi anaetegemea
samaki kuwa ndio sababu ya kuishi kwake bila
kujua kuwa samaki wenyewe wanataka kujikwamua
kuendelea kuishi huku akitamani Chambo wa mvuvi,
Maisha yangu sasa ni kama Mvuvi ambae anakaa
asubuhi kutwa hana kazi anasubiri jioni aelekee
baharini kwa ajili ya kuvua samaki, siku bahari
ikichafuka maana yake hali ya Maisha yake yanazidi
kuwa magumu sana, siku bahari imetulia basi furaha
kwake lakini anapata manufaa kwenye chombo
hatari).
Kufikia hapo nilipiga magoti na kutaka kusema
jambo, lakini sikupewa nafasi ya kuongea chochote
pale. “Mama Penina wewe ni mke wangu najua
huyu alikushawishi na alichukua nafasi ya mimi
kutowepo muda mrefu kuja kukuteka mimi nadili na
huyu wewe nenda chumbani Walinzi mchukueni huyu
muwekeni kule chemba”.
Alimaliza kwa kusema hivyo na mimi nikaswekwa
chemba huku nikiumia sana na kujua wakati wangu
umefika. Usiku uliingia baada ya kuona giza tu
likitanda kwenye ile chemba nikisubiri wakati wangu
wa kwenda kuonana na marafiki zangu akina
Kibona. Majira ya usiku sana ukimya uliposhika
nafasi ndipo kwa mbali nasikia sauti ya vicheko
vikiendelea na maneno ya kashfa juu yangu.
“Haaaa! Tulikuambia wewe kuwa na sisi ona sasa
umeishiwa mimi ni salha kwa sasa sina uwezo wa
kukusaidia Zaidi ya kukusubiri ufe uje kuungana na
sisi huku ili upate kulipiza kisasi chako…” Maneno
yale yalipenya kwenye masikio yangu na kunifanya
niumie sana wapi niende nani atanisaidia. Siku tatu
niliwekwa nikiwa na njaa kali sana nguvu zimeniishia
ndipo naona mlango unafunguliwa na nikatolewa.
Nilibebwa hadi kwenye gari na kupelekwa hadi
kwenye bahari huko ndipo walianza kunipiga.
Kutokana na homa niliyonayo ya ajali kichwa
kilibangua na kurudisha tena yale maumivu makali
niliyonayo, ukimya niliokuwa nimekaa walijua fika
kuwa nimekufa hivyo walinitupia baharini na
kunifanya nizimie nisijue kitu kilichokuwa
kinaendelea.
Najikuta kwenye ufukwe wenye michanga mingi
sana yenye kung`aa, hayo maeneo yalinivutia
palikuwa kama kisiwa cha kuvutia kwa akili yangu
sikutambua ni mazingira gani hivyo nilibaki
kuangalia kwa kuwa sikuwa na nguvu yeyote ile.
Walitokea viumbe kama wale wa awali mbele yangu
huku kama wakinionea huruma hivi wengine
wakitaka kunidhuru ndipo kwa mbali naona watu
kadhaa nisiowafahamu wakija pale nilipo. Alikuwa
Kibona namuona kwa macho yangu. Nikajiuliza ina
maana huku nimerudi kuzimu au ndani ya kile
kisiwa nikiwa nawaza hilo ndipo kibona akaongea
“Mnali unapata tabu sana lakini huu ndio mwisho
wa hizo tabu zote nitakuweka sehemu salama na
utarudi ukiwa mtu wa tofauti Alikuja mmoja wa
viumbe wale wakening`ata mkononi na mimi
kushtuka nilikuwa kwenye ndoto kali. Najiona nipo
kwenye mtumbwi mbovu wa zamani ukiwa
umenisaidia sikujua nani kaniweka wakati
nakumbuka nilitupwa humo. Sauti kuu ilisikika
ikiniamuru jambo.
 
SEHEMU YA AROBAINI NA TANO 45
SEHEMU YA MWISHO.
CONTACT:: 0652667153
ENDELEA...
Sauti ile iliniambia kuwa nisiwe na wasiwasi
wowote kuhusu yale yote ambayo walinifanyia. Ni
wakati wangu sasa wa kufurahi na kurudisha
machungu yote ya awali. Nilipata mfadhaiko
mkubwa kwani nilihisi kuchoka sana ikichanganywa
na njaa kali ambayo ilinifanya nikose nguvu hata za
kutembea. Nakumbuka ilikuwa ni majira ya jioni
kiza kikiingia nilitambaa kutoka pale nilipo hadi
karibu na mti mkubwa ambapo nilipata kupumzika.
Ilipita dakika kadhaa hadi pale Niliposikia harufu
fulani hivi kama kuna watu wanakula nyama
iliyochomwa. Nilipata nguvu kisha nikaanza
kuifuatilia ile hadi nilipofika eneo moja kutokana na
mwanga wa moto. Nilifarijika baada ya kuhisi kuwa
pale kuna watu ambao wanaweza kunisaidia mimi.
Nilifika na kweli nikawaona watu wakiuzungula ule
moto huku wakizungumza lugha ambazo wao
wenyewe wanazitambua. Kwa kuwa nilikuwa nina
njaa sana niliomba msaada wa chakula ili nipate
kutia chochote kile. Lakini jambo la kushangaza
walinitaja mpaka na jina langu huku wakicheka kwa
furaha na kuniudumia bila wasiwasi wowote.
Nilikula ile nyama mpaka pale tumbo langu
liliposhukuru na kutoa gesi kwa kuwa nilijaza sana.
Hatimae napatwa na usingizi mzito palepale na
kama ningekuwa na saa ningekadiria au kujua kuwa
ni saa mbili sasa usiku ndipo napata chakula na
kulala sehemu ambayo siifahamu. Ghafla nashituka
nakutana na Kibona macho kwa macho akiwa mbali
na mimi huku akininyooshea kidole kuwa njia sahihi
ya kupita. "Kibona kaka! Na..." ghafla ububu
uliniingia bila hata kupenda na sikuweza kusema
lolote pale. Ghafla upeo wa macho yangu ulizidi
kutoweka kila nimuangaliapo Kibona.
Sikujua kwa nini jambo lile linatokea, hadi pale
Kibona alipopotea mbele ya macho yangu lakini
nilipata kujua kuna mahali alinionyesha njia nikiwa
naendelea kuwaza sauti ya kuniamrisha kuwahi ile
sehemu iliendelea "Mnali fanya haraka muda
mchache Kisiwa kinaondoka..." khaaah! Kisiwa
kinaondoka kinaenda wapi sasa. Hapo kila Swali
nililokuwa najiuliza basi niliyapata majibu yake
kuwa kama kuna mtu ananinong'oneza jambo.
"Kisiwa huwa kina muda wa kukaa juu ya maji na
kutokomea ndio maana unakaa na kutokiona kabisa
sasa fanya haraka kupita hiyo njia ili ufanikiwe".
Sikuwa na ubishi na jambo hilo alafu nilijikuta
napata furaha sana kila baada na kila hatua.
Nilisimama na kuongoza ile njia ambayo
nilielekezwa. Kidogo kidogo niliona njia
inafuinafunga Alafu kama maji ya bahari yanaingia.
Nilipata kuona kuna Sanduku. Sanduku nililikumbuka
baada ya kumkubuka Salha ndie ambae alinifuatilia
sana mpaka ikamsababishia kifo chake.
Niliinama kisha nikakinyanyua hadi juu ya kifua
changu. Lwa mbali hivi nikamuona Kibona akiwa
kwenye mtumbwi akiniita. Sauti yake niliisikia kwa
mara ya kwanza ikiniambia Njoo Rafiki yangu haraka
muda umefika wa hiko Kisiwa kuondoka. Niliingia
kwenye maji pamoja na Kile kisanduku. Nilijitahidi
kuogelea hadi pale kwenye Mtumbwi na kukaa
nyuma mimi mbele Kibona huku tukiangaliana. Ni
yuleyule Kibona ambae mimi namfahamu. "Kibona
twende nyumbani Mkeo anapata tabu sana, tangu
mimi nipate matatizo kwa kweli sina amani na ule
mji hata nyumbani sikai" Nilimuona akiwa
anahuzunika sana huku akionekana kama mtu
memwenye wasiwasi na mtumbwi muda huo
umesimama hautembei. "Hapana Mnali sina maisha
kama uliyonayo wewe, nadhani utakuwa
unakumbuka vyema sana nini ambacho kinaendelea
baina yangu na Uhai wangu' mimi si binadamu tena
bali ni laika. Nafasi hii uliyoniona hutowea nioma
tena na nimekukabidhi zawadi hiyo ukamtunze mke
wangu kutokana na hali yake fanya juu chini"
aliongea mpaka mimi nikaanza kulia pale ndani ya
Mtumbwi.
"Kibona siamini kama kweli nakuona. Sawa
nitafanya hivyo ila nawezaje kumtunza hali maisha
yangu yamegeuka juu chini na sina nguvu za
kuyanyanyua na kuyarejesha tena najua nafika eneo
ambalo watu walitaka kuniua kabisa nisiwepo
duniani." Niliongea " Usijali mimi ndie niliekuokoa.
Kuhusu hao hawataweza tena kukudhuru ila
nakuomba kitu kimoja kama ahadi unifanyie kwani
ukifanya hivyo nitafurahi mno".
Nilionyesha mshangao kwanza na tabasamu "haya
jambo gani rafiki yangu" Sasa ikawa tunaongea
kama wote ni binadamu sawa.
"Nataka Umuoe mke wangu..."
Mwili wangu ulisisimka sana baada ya kusikia ile
kauli. Kwa kweli nilipata mtihani na nilishindwa
kumjibu kuwa sawa kwani siwezi kabisa kumuoa
mke wake.
"Nakuambia hivi Mnali Maisha yako kuwa mazuri
Muoe mke wangu najua utamtunza vizuri zaidi
kuliko ukiwa mbali nae pia mwambie mke wangu
mimi ndie niliekuambia kuwa umuoe. Naona mke
wangu anateseka sana fanya hivyo....Naona muda
wangu umetimia nataka kuondoka Mnali".
Nilishangaa anatoa machozi na kulia. Ila kila
nikijaribu kumgusa ni kama hewa tu kumbe ni nafsi
tu ndio ambayo nilikuwa naongea nayo pale. Ndipo
naona kivuli cha Kibona kinapotea mbele yangu na
kujua sasa ndio mwisho wa Kuonana na Kibona ila
mtihani mkubwa anaoniachia wa kwenda kumuoa
mke wake ambae mimi ni shemeji yangu.
Sikutaka kujua ndani ya boksi kuna kitu gani kwa
kuwa majonzi moyoni mwangu ndio yalizidi.
Taratiibu nilisogeza mtumbwi kutoka pale kisiwani
lakini jambo la ajabu niliona Kisiwa chote kinazama
na nikausikia ukelele mkubwa sana wa malalamiko.
Kila nilichokiona pale mbele yangu ni kama ndoto
kumbe ni kweli kabisa. Sehemu ambayo kisiwa
kilikuwepo basi maji tupu na hapakuwa na dalili
yeyote ile ambayo ilionyesha kuwa palikuwa na kitu.
Taratiibu hadi katikati ya bahari na siku ya pili
Asubuhi yake mapema ndio naingia. Baada ya
kufika nchi kavu nilijiuliza nianze kwenda wapi ndipo
nikaenda hadi kwa mke wa kibona karibu na ile
nyumba ambayo mama Penina alinipatia kama
zawadi yake kwangu. Nilipokaribia kwenye ile
nyumba nikaona watu wakiwa wanatoka na kuingia
ikiwa na maana kuwa wanaishi humo. Nilinyoosha
moja kwa moja hadi nyumbani kwa mke wa kibona
huku nikiwaza nimuanze vipi kumshawishi ila
sikutaka kumuambia kuwa kibona ameniambia
hapana bora nitumia maneno yangu tu.
Baada ya kufika mke wa kibona sikumuona pale
kwake. Nilimuuliza jirani yake. "Mh! Huyu mama
ana muda sana anakaa kule barabarani
anaombaomba kila siku anarudi usiku sana na
watoto wake na kuondoka asubuhi sana." Niliumia
baada ya kusikia kuwa Mke wa Kibona ni
Ombaomba. "Ahsante nashukuru ngoja nimfuate
kwanza". Nilimueleza yule mama. " Samahani kaka
hivi huyu ni ndugu yako?". "Ndio ni ndugu yangu".
Alicheka sana "Khaaa! Ndio maana mmefanana....".
Nilimuangalia lakini sikujua kwa nini anasema
tumefanana. "Sasa kaka hauoni wote ombaomba
nyinyi mmetoka huko kwenu na kwa taarifa yako hili
eneo analokaa huyu limeuzwa wajanja
wameshachukua ela akija anashusha bonge la
mjengo hapo". Maneno mengi sana aliyasema hadi
akafikia hatua ya kusema kuwa Lile sanduku
nililolibeba ni kwa ajili ya kuombeaombea. Iliniuma
sana hadi nikatamani nimrukie au nirudi kwenye zile
enzi zangu ili nimdhuru. Nilielekea hadi kule
barabarani kweli nilimkuta akiombaomba nilifanya
kumshika mkono pamoja na wale watoto
akawashika tukaongozana taratibu huku akiwa analia
sana na hawezi kutembea vizuri.
Mabaya mengi amefanyiwa mama wa watu.
Tuliingia ndani kwake yule jirani akiwa anacheka.
Baada ya maongezi na kumriwaza nikamuomba
anisaidie kulifungua lile Sanduku dogo. Tulisaidiana
kama mke na mume vile hadi lilipofunguka. Haki ya
mungu hatukuweza kuamini baada ya kukuta
madonge ya Almasi pamoja na dhahabu. Macho
yangu hayakuweza kuamini kwa kile ambacho
ninakiona. Nilimuomba atulie niende kuuza kwani
najua hatuna hata kiasi chochote cha kula. Mara
moja nikafika Smaeneo ambayo sonara zinapatikana
kwani hayo maeneo kulikuwa na jamaa nilielekezwa.
Niliuweka ule mzigo kisha yule Bosi akaniuliza.
"Una akaunti ya Benki...?" Aliuliza.
"Hapana Sina..." Alijiandaa kisha akaniambia kuwa
tufuatane.
"Huwezi kuamini siku kuanzia Asubuhi hiyo mpaka
jioni tuliangaikia kufuatilia swala la kutengeneza
akaunti mpaka ikatimia. Baada ya hapo aliniingizia
kiasi cha pesa kingi sana mpaka nikawa nashindwa
kukihesabu ila ni zile milioni mia kadhaa ambazo
nilizipata. Baada ya hapo akawa rafiki yangu
akaniuliza swali. "Oya! Unaenda kuishi wapi sasa
maana nina taka kufanya kazi na wewe".
Baada ya wiki mbili nilipata Nyumba yangu kubwa
yenye mabanda na fensi kubwa maeneo ambayo
alijenga bwana Osward mume wa Mama Penina.
Kila nilichokuwa nakifanya Mke wa Kibona hakuwa
ana amini kabisa. Baada ya hapo maisha yangu
yalikuwa vizuri sana kwa kweli na sikua naamini.
Nilifanya kila njia ya kumchukua mtoto wangu
Asante hadi nilipofanikisha kuwa nae ndani ya
mjengo wangu. Baada ya mwaka ndoto kali zenye
vitisho vikiniandama kila nikilala. Nilisahau kabisa
kama Kibona alinipa mali hizi ili nipate kuishi na
mkewe kama alivyohitaji yani nimuoe. Mtaa mzima
mimi nilijulikana lakini sikuwa na raha kabisa kwa
sababu ndoto mbaya zilinikosesha amani. Ndipo
siku hiyo napata kuwaza kuwa na mke lakini kila
nikijaribu wazo linatoka na kubaki kumfikiria yule
mwanamke. Ndipo niliamua kumuambia ukweli japo
hakuamini kama ni mimi naweza kumuambia
utumbo ule kama yeye alivyouita. Lakini sikuwa na
jinsi nilimlazimisha mpaka akakubali na tukafunga
ndoa na kuwa mke na mume.
Nakumbuka bwana Osward alituma watu kuja
kunivamia lakini walishindwa na hata waliponiona
waliniogopa sana. Yule mke wangu ambae ni mama
Asante alijuta kwelikweli kwa maana hakuamini kwa
kile alichokiona.
Baada ya wiki Bwana osward pamoja na kundi lake
walikuja kwa wema na kuniomba niwaonyeshe
utajiri niliupata wapi. Hata yule Bosi wa madini
alinijia na kutaka kuniomba nimuonyeshe ila mimi
nikamueleza ukweli kuwa asitasithubutu Kwenda
kama anavyotaka kwenda huko kisiwani. Lakini yule
Bwana Osward na vijana wake niliwaelekeza waende
watakikuta na Almasi zipo zikiwasubiri. Japo
walipanga kwenda ila sikujua kama walifika na
kama walikwenda sikujua kama walipona.
Nilinshukuru mungu sana kwa kila hatua ile na
ndipo nikapata kusoma baadhi ya wandishi ndipo
nikakutana na Mwandishi mmoja aliyejulikana kwa
jina la Mudhihili Mnali (Author Mudhihili ).
Nilimsimulia kisa hiki cha kweli mwanzo hadi
mwisho na yeye akaifanyia kazi maneno yangu na
akatengeneza kitabu kupitia yale niliyomsimulia
akakipa kwa jina la MAISHA YANGU YA UVUVI.
MWISHO
 
SEHEMU YA AROBAINI NA TANO 45
SEHEMU YA MWISHO.
CONTACT:: 0652667153
ENDELEA...
Sauti ile iliniambia kuwa nisiwe na wasiwasi
wowote kuhusu yale yote ambayo walinifanyia. Ni
wakati wangu sasa wa kufurahi na kurudisha
machungu yote ya awali. Nilipata mfadhaiko
mkubwa kwani nilihisi kuchoka sana ikichanganywa
na njaa kali ambayo ilinifanya nikose nguvu hata za
kutembea. Nakumbuka ilikuwa ni majira ya jioni
kiza kikiingia nilitambaa kutoka pale nilipo hadi
karibu na mti mkubwa ambapo nilipata kupumzika.
Ilipita dakika kadhaa hadi pale Niliposikia harufu
fulani hivi kama kuna watu wanakula nyama
iliyochomwa. Nilipata nguvu kisha nikaanza
kuifuatilia ile hadi nilipofika eneo moja kutokana na
mwanga wa moto. Nilifarijika baada ya kuhisi kuwa
pale kuna watu ambao wanaweza kunisaidia mimi.
Nilifika na kweli nikawaona watu wakiuzungula ule
moto huku wakizungumza lugha ambazo wao
wenyewe wanazitambua. Kwa kuwa nilikuwa nina
njaa sana niliomba msaada wa chakula ili nipate
kutia chochote kile. Lakini jambo la kushangaza
walinitaja mpaka na jina langu huku wakicheka kwa
furaha na kuniudumia bila wasiwasi wowote.
Nilikula ile nyama mpaka pale tumbo langu
liliposhukuru na kutoa gesi kwa kuwa nilijaza sana.
Hatimae napatwa na usingizi mzito palepale na
kama ningekuwa na saa ningekadiria au kujua kuwa
ni saa mbili sasa usiku ndipo napata chakula na
kulala sehemu ambayo siifahamu. Ghafla nashituka
nakutana na Kibona macho kwa macho akiwa mbali
na mimi huku akininyooshea kidole kuwa njia sahihi
ya kupita. "Kibona kaka! Na..." ghafla ububu
uliniingia bila hata kupenda na sikuweza kusema
lolote pale. Ghafla upeo wa macho yangu ulizidi
kutoweka kila nimuangaliapo Kibona.
Sikujua kwa nini jambo lile linatokea, hadi pale
Kibona alipopotea mbele ya macho yangu lakini
nilipata kujua kuna mahali alinionyesha njia nikiwa
naendelea kuwaza sauti ya kuniamrisha kuwahi ile
sehemu iliendelea "Mnali fanya haraka muda
mchache Kisiwa kinaondoka..." khaaah! Kisiwa
kinaondoka kinaenda wapi sasa. Hapo kila Swali
nililokuwa najiuliza basi niliyapata majibu yake
kuwa kama kuna mtu ananinong'oneza jambo.
"Kisiwa huwa kina muda wa kukaa juu ya maji na
kutokomea ndio maana unakaa na kutokiona kabisa
sasa fanya haraka kupita hiyo njia ili ufanikiwe".
Sikuwa na ubishi na jambo hilo alafu nilijikuta
napata furaha sana kila baada na kila hatua.
Nilisimama na kuongoza ile njia ambayo
nilielekezwa. Kidogo kidogo niliona njia
inafuinafunga Alafu kama maji ya bahari yanaingia.
Nilipata kuona kuna Sanduku. Sanduku nililikumbuka
baada ya kumkubuka Salha ndie ambae alinifuatilia
sana mpaka ikamsababishia kifo chake.
Niliinama kisha nikakinyanyua hadi juu ya kifua
changu. Lwa mbali hivi nikamuona Kibona akiwa
kwenye mtumbwi akiniita. Sauti yake niliisikia kwa
mara ya kwanza ikiniambia Njoo Rafiki yangu haraka
muda umefika wa hiko Kisiwa kuondoka. Niliingia
kwenye maji pamoja na Kile kisanduku. Nilijitahidi
kuogelea hadi pale kwenye Mtumbwi na kukaa
nyuma mimi mbele Kibona huku tukiangaliana. Ni
yuleyule Kibona ambae mimi namfahamu. "Kibona
twende nyumbani Mkeo anapata tabu sana, tangu
mimi nipate matatizo kwa kweli sina amani na ule
mji hata nyumbani sikai" Nilimuona akiwa
anahuzunika sana huku akionekana kama mtu
memwenye wasiwasi na mtumbwi muda huo
umesimama hautembei. "Hapana Mnali sina maisha
kama uliyonayo wewe, nadhani utakuwa
unakumbuka vyema sana nini ambacho kinaendelea
baina yangu na Uhai wangu' mimi si binadamu tena
bali ni laika. Nafasi hii uliyoniona hutowea nioma
tena na nimekukabidhi zawadi hiyo ukamtunze mke
wangu kutokana na hali yake fanya juu chini"
aliongea mpaka mimi nikaanza kulia pale ndani ya
Mtumbwi.
"Kibona siamini kama kweli nakuona. Sawa
nitafanya hivyo ila nawezaje kumtunza hali maisha
yangu yamegeuka juu chini na sina nguvu za
kuyanyanyua na kuyarejesha tena najua nafika eneo
ambalo watu walitaka kuniua kabisa nisiwepo
duniani." Niliongea " Usijali mimi ndie niliekuokoa.
Kuhusu hao hawataweza tena kukudhuru ila
nakuomba kitu kimoja kama ahadi unifanyie kwani
ukifanya hivyo nitafurahi mno".
Nilionyesha mshangao kwanza na tabasamu "haya
jambo gani rafiki yangu" Sasa ikawa tunaongea
kama wote ni binadamu sawa.
"Nataka Umuoe mke wangu..."
Mwili wangu ulisisimka sana baada ya kusikia ile
kauli. Kwa kweli nilipata mtihani na nilishindwa
kumjibu kuwa sawa kwani siwezi kabisa kumuoa
mke wake.
"Nakuambia hivi Mnali Maisha yako kuwa mazuri
Muoe mke wangu najua utamtunza vizuri zaidi
kuliko ukiwa mbali nae pia mwambie mke wangu
mimi ndie niliekuambia kuwa umuoe. Naona mke
wangu anateseka sana fanya hivyo....Naona muda
wangu umetimia nataka kuondoka Mnali".
Nilishangaa anatoa machozi na kulia. Ila kila
nikijaribu kumgusa ni kama hewa tu kumbe ni nafsi
tu ndio ambayo nilikuwa naongea nayo pale. Ndipo
naona kivuli cha Kibona kinapotea mbele yangu na
kujua sasa ndio mwisho wa Kuonana na Kibona ila
mtihani mkubwa anaoniachia wa kwenda kumuoa
mke wake ambae mimi ni shemeji yangu.
Sikutaka kujua ndani ya boksi kuna kitu gani kwa
kuwa majonzi moyoni mwangu ndio yalizidi.
Taratiibu nilisogeza mtumbwi kutoka pale kisiwani
lakini jambo la ajabu niliona Kisiwa chote kinazama
na nikausikia ukelele mkubwa sana wa malalamiko.
Kila nilichokiona pale mbele yangu ni kama ndoto
kumbe ni kweli kabisa. Sehemu ambayo kisiwa
kilikuwepo basi maji tupu na hapakuwa na dalili
yeyote ile ambayo ilionyesha kuwa palikuwa na kitu.
Taratiibu hadi katikati ya bahari na siku ya pili
Asubuhi yake mapema ndio naingia. Baada ya
kufika nchi kavu nilijiuliza nianze kwenda wapi ndipo
nikaenda hadi kwa mke wa kibona karibu na ile
nyumba ambayo mama Penina alinipatia kama
zawadi yake kwangu. Nilipokaribia kwenye ile
nyumba nikaona watu wakiwa wanatoka na kuingia
ikiwa na maana kuwa wanaishi humo. Nilinyoosha
moja kwa moja hadi nyumbani kwa mke wa kibona
huku nikiwaza nimuanze vipi kumshawishi ila
sikutaka kumuambia kuwa kibona ameniambia
hapana bora nitumia maneno yangu tu.
Baada ya kufika mke wa kibona sikumuona pale
kwake. Nilimuuliza jirani yake. "Mh! Huyu mama
ana muda sana anakaa kule barabarani
anaombaomba kila siku anarudi usiku sana na
watoto wake na kuondoka asubuhi sana." Niliumia
baada ya kusikia kuwa Mke wa Kibona ni
Ombaomba. "Ahsante nashukuru ngoja nimfuate
kwanza". Nilimueleza yule mama. " Samahani kaka
hivi huyu ni ndugu yako?". "Ndio ni ndugu yangu".
Alicheka sana "Khaaa! Ndio maana mmefanana....".
Nilimuangalia lakini sikujua kwa nini anasema
tumefanana. "Sasa kaka hauoni wote ombaomba
nyinyi mmetoka huko kwenu na kwa taarifa yako hili
eneo analokaa huyu limeuzwa wajanja
wameshachukua ela akija anashusha bonge la
mjengo hapo". Maneno mengi sana aliyasema hadi
akafikia hatua ya kusema kuwa Lile sanduku
nililolibeba ni kwa ajili ya kuombeaombea. Iliniuma
sana hadi nikatamani nimrukie au nirudi kwenye zile
enzi zangu ili nimdhuru. Nilielekea hadi kule
barabarani kweli nilimkuta akiombaomba nilifanya
kumshika mkono pamoja na wale watoto
akawashika tukaongozana taratibu huku akiwa analia
sana na hawezi kutembea vizuri.
Mabaya mengi amefanyiwa mama wa watu.
Tuliingia ndani kwake yule jirani akiwa anacheka.
Baada ya maongezi na kumriwaza nikamuomba
anisaidie kulifungua lile Sanduku dogo. Tulisaidiana
kama mke na mume vile hadi lilipofunguka. Haki ya
mungu hatukuweza kuamini baada ya kukuta
madonge ya Almasi pamoja na dhahabu. Macho
yangu hayakuweza kuamini kwa kile ambacho
ninakiona. Nilimuomba atulie niende kuuza kwani
najua hatuna hata kiasi chochote cha kula. Mara
moja nikafika Smaeneo ambayo sonara zinapatikana
kwani hayo maeneo kulikuwa na jamaa nilielekezwa.
Niliuweka ule mzigo kisha yule Bosi akaniuliza.
"Una akaunti ya Benki...?" Aliuliza.
"Hapana Sina..." Alijiandaa kisha akaniambia kuwa
tufuatane.
"Huwezi kuamini siku kuanzia Asubuhi hiyo mpaka
jioni tuliangaikia kufuatilia swala la kutengeneza
akaunti mpaka ikatimia. Baada ya hapo aliniingizia
kiasi cha pesa kingi sana mpaka nikawa nashindwa
kukihesabu ila ni zile milioni mia kadhaa ambazo
nilizipata. Baada ya hapo akawa rafiki yangu
akaniuliza swali. "Oya! Unaenda kuishi wapi sasa
maana nina taka kufanya kazi na wewe".
Baada ya wiki mbili nilipata Nyumba yangu kubwa
yenye mabanda na fensi kubwa maeneo ambayo
alijenga bwana Osward mume wa Mama Penina.
Kila nilichokuwa nakifanya Mke wa Kibona hakuwa
ana amini kabisa. Baada ya hapo maisha yangu
yalikuwa vizuri sana kwa kweli na sikua naamini.
Nilifanya kila njia ya kumchukua mtoto wangu
Asante hadi nilipofanikisha kuwa nae ndani ya
mjengo wangu. Baada ya mwaka ndoto kali zenye
vitisho vikiniandama kila nikilala. Nilisahau kabisa
kama Kibona alinipa mali hizi ili nipate kuishi na
mkewe kama alivyohitaji yani nimuoe. Mtaa mzima
mimi nilijulikana lakini sikuwa na raha kabisa kwa
sababu ndoto mbaya zilinikosesha amani. Ndipo
siku hiyo napata kuwaza kuwa na mke lakini kila
nikijaribu wazo linatoka na kubaki kumfikiria yule
mwanamke. Ndipo niliamua kumuambia ukweli japo
hakuamini kama ni mimi naweza kumuambia
utumbo ule kama yeye alivyouita. Lakini sikuwa na
jinsi nilimlazimisha mpaka akakubali na tukafunga
ndoa na kuwa mke na mume.
Nakumbuka bwana Osward alituma watu kuja
kunivamia lakini walishindwa na hata waliponiona
waliniogopa sana. Yule mke wangu ambae ni mama
Asante alijuta kwelikweli kwa maana hakuamini kwa
kile alichokiona.
Baada ya wiki Bwana osward pamoja na kundi lake
walikuja kwa wema na kuniomba niwaonyeshe
utajiri niliupata wapi. Hata yule Bosi wa madini
alinijia na kutaka kuniomba nimuonyeshe ila mimi
nikamueleza ukweli kuwa asitasithubutu Kwenda
kama anavyotaka kwenda huko kisiwani. Lakini yule
Bwana Osward na vijana wake niliwaelekeza waende
watakikuta na Almasi zipo zikiwasubiri. Japo
walipanga kwenda ila sikujua kama walifika na
kama walikwenda sikujua kama walipona.
Nilinshukuru mungu sana kwa kila hatua ile na
ndipo nikapata kusoma baadhi ya wandishi ndipo
nikakutana na Mwandishi mmoja aliyejulikana kwa
jina la Mudhihili Mnali (Author Mudhihili ).
Nilimsimulia kisa hiki cha kweli mwanzo hadi
mwisho na yeye akaifanyia kazi maneno yangu na
akatengeneza kitabu kupitia yale niliyomsimulia
akakipa kwa jina la MAISHA YANGU YA UVUVI.
MWISHO

Safi sana... Story nzuri sana...

Chapter Closed....



Cc: mahondaw
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni http://www.equatorstory.com/
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom