Simulizi: Maisha Yangu Ya Uvuvi

Simulizi: Maisha Yangu Ya Uvuvi

SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA 21
ENDELEA.......
.......Mlango unafunguliwa na kuingia Vijana kama
watatu ambao sikuwa nawafahamu kwa sura, bali
kwa idadi kutokana na wao walikuwa wakinimulika
tochi usoni na kufanya nikose nuru.
"Eheee! Kwa hiyo bwana Paul hakuona vijana wa
kufanya nao kazi hatari kama hii na wakakutumia
wewe?".
Mmoja wao aliongea aliyeonekana kuwa kama
mkubwa kati ya wale watatu. Lile swali halikunifanya
nijibu kwa haraka kama vile ambavyo wao walihitaji
nijibu bali nilibaki kuwa kimya. Hii yote kutokana na
kichwa changu kupokea maumivu makali ambayo
yalisababishwa na purukushani za kutwa nzima hadi
nyakati zile.
"Kijana! Sisi hatuna shida na wewe kabisa,
tunachohitaji ni kujua unaeje huyu bwana Paul?"
"Mimi sijui chochote".
Nilimjibu.
Lakini ilionyesha wazi kuwa jibu langu hakulizika
nalo maana alisimama kisha akainama tena na
kuniangalia
"Unasemaje?"
Aliniuliza swali lilelile
"Mimi sijui chochote"
Alinizaba kibao cha maana, kilichonipeperusha
kama mzoga hadi ukutani na kujikuta napata
maumivu ya zaidi.
"Aiseee! Muite mzee mara moja nitamuua huyu".
Ndipo yule kijana mwingine kati ya wale wawili
waliobakia alitoka na kuelekea nje ya chumba
tofauti na pale.
"Kijana, nakuambia hivi huyu anaekuja ni mkatili
sana sasa mjibu upuuzi wako alafu utajua nini
atakufanya nyang'ao nyoooooooh!".
Dawa ya mjuaji au baunsa ni kukaa kimya tu wala
usijibujibu ovyo.
Punde tu wanaingia wawili. Taa iliwashwa na kunipa
mimi nafasi ya kuwaona wote wa mule ndani. Huyu
aliyeongezeka nadhani ndie alikuwa mkuu au mzee
wao ambao walikuwa wanamzungumzia.
Yule jamaa aliwaomba wale waondoke kwanza,
baada ya kuondoka ndipo akachuchumaa na
kunitazama kwa makini.
"Kijana unaitwa nani?"
"Naitwa Mnali"
Nilimjibu
"Ooooh! Wewe kijana sio mgeni kwa hilo jina lako,
bwana Paul ni mtu mdogo sana kwenye biashara,
sasa alinipa taarifa zako juu ya wewe kuwa
ukimsumbua sana".
"Lakini sio kesi, nahitaji unifanyie kazi yangu tofauti
na hapo nakuua"
Nilishtuka sana kiukweli,
"Kazi gani hiyo".
Alikuwa anacheka.
"Hahaaaah! Hahaaaa! Aaaaah"
Nilibaki kumtazama tu huku nikitafakari ile kauli
yake.
"Wewe ni mvuvi hodari si ndioo!"
"Ndio ndio kazi yangu hiyoo"
"Sawa! Kuanzia sasa acha kufanya kazi na Paul.
Mimi nina kazi yangu ya kuuza madawa ya kulevya,
sasa nitakutumia wewe kuuza".
"Hapana kiukweli siwezi kufanya hiyo kazi mimi, na
pia naomba uniachie tu maana mimi ni mtu duni
sana sina cha kukulipa au kukupa zaidi utanionea
bure".
"Hapana wewe ni muhimu kwetu na kama
utasumbua tunakuua".
Tulichukua kama dakika kama kumi tukizozana
ndipo mzee akapandwa na hasira akamuita kijana
mmoja aliyepo nje.
"Nataka huyu usiku huu.."
Akiwa anaangalia saa
"Saa! Saba...mpatieni Adhabu si hapa! Pelekeni
kokote kule piga mpaka afe! Pumbavu hatutaki
ushahidi..akiachwa huyu polisi watatusumbua
uaaaaa!".
Hilo ndilo lilikuwa tamko la huyu jamaa kuwa
niuliwe lakini si pale kwake.
Nikiwa nasubiri kinachoendelea, ghafla kwa nje
nilisikia gari likinguruma. Ndipo nikajua maandalizi
ya mimi kwenda kuuliwayalikuwa tayari.
Mlango ulifunguliwa na mimi nikachukuliwa
mkukumkuku hadi kwenye gari.
Vijana wapatao sita sasa walinizoa moja kwa moja
njia kuu kuelekea huko ambako walitaka kuelekea
kutimiza azma yao.
Njiani nikiwa naomba mungu anisaidie kikombe kile
kisinikute, nilijikuta nakumbuka mambo mengi ya
nyuma ambayo yalinipandisha hasira sana.
Nilishindwa kufanya chochote.
Walizidi kusonga mbele zaidi majira ya usiku, mimi
nikiwa nawasikiliza sina uwezo kwani hata nikipiga
kelele hakuna ambae anaweza sikia.
Kwa mbali sauti ya maji yakinguruma kutokana na
mawimbi ya bahari, ndipo nikajua kuwa napelekwa
baharini, baharini wakiniua kwao ni rahisi kunitupa
humo.
Nikakumbuka kifo cha Kibona alivyokufa, alifia mule
baharini tena kwa hila za hawa watu hasa za bwana
Paul. Bwana Paul anafanya kazi, anamiliki hotel
nyingi, lakini pia anafanya kazi za uuzaji wa madawa
ya kulevya, akishirikiana na huyu jamaa ambae
simfahamu kabisa.
Safari ilifika mwisho hadi kwenye ufukwe wa bahari
ambako kulikuwa kimya kabisa, kwa kuwa ni usiku
mnene. Walinitoa mkuku mkuku na kunitupa kwenye
mchanga.
"Moris!..."
"Naaam!"
"Tunafanya lipi, kupiga kwanza na kumtupa au
tunamtupa moja kwa moja".
Nilimsikia mmoja akiwa anaongea hivyo.
"Hapana! Hawezi kutupwa hivihivi, huyu ni mvuvi pia
anajua kuogelea! Tupige tuvunje nguvu kisha
tunamaliza kilain".
Nikiwa pale chini, nilihisi kama wale viumbe ambao
nilikutana nao kule kisiwani, wananiangalia kwa
huruma sana, pia niliona kama yule rafiki
niliyekutana nae kule kama namuona kwenye macho
yangu yenye kutoa chozi la hasira.
Kama unafahamu kuwa baharini kuna hali ambayo
inaonyesha harufu ya samaki. Ile harufu yake
nilipata kuivuta kwenye pua zangu na kuanza kuhisi
msisimko.
Wakati najikongoja kuondokana na ile hali ndipo
nashindiliwa teke, nikaanguka tena chini, akaja
mwingine akanipiga nondo ya mguuni
nikashtuka na mguu nikahisi umevunjika kwa
maumivu wakati wanavuta bangi zao na wengine
wakivuta kupitia viganja na pua zao, walianza
kunicheka kwa dharau..
"Haaaaa! Haaaaa! Lazima ukasalimie kuzimu
mbaaaaafu!"
Nilijaribu kuomba msamaha kwao ili wasiendelee
kunidhuru lakini majibu yao yalinikata maini.
"Jamanii mimi masikini, nisietaka shari na mtu,
nimetoka kwenye matatizo na mpaka leo hii
nahangaika nipate kumsomesha mwanangu naomba
mnisameheee"
"Haaaa! Una mtoto wewe! Ina maana una
mwanamke! Huyo mwanamke unampa
nini...anaitwa nani huyo demu maana wewe unakufa
yeye tunaenda kumhudumia sisi.."
"Jamani kuweni na huruma! Familia yangu inaishi
kwa mwingine..mwanangu anaitwa Asantee.."
"Oooh!!! Haijarishi kwetu hilo kukuua wewe sisi
tunapata pesa ndefu...."
Wakaanza kunivutavuta pale kama mpira wa kona.
Hapo sasa mwili unachachamaa kubadilika baada
ya kupata harufu ya nyama ile ya samaki. Nilijikuta
nikipiga keleleee.
"Kimbieniiiiiiii....msije karibu yanguuuu".
Walinicheka na hapo wakiwa na nia ya kuja
kunimaliza kabisa waondoke.
Aiseee! Nguvu na shauku ya kila kiungo cha mwili
wangu kufanya kazi ilikuja, sielewi hata ilikuwaje
maana nilikuja kujitambua Karibu alfajiri hivi kidogo
gari kwa mbali nilizisikia.
Niliamka na kuangalia pale chini yote mizoga na
wengine hawana viungo kama mkono pamoja na
uso hautamaniki.
Ghaaa! Nilistaajabu baada ya kuona lile tukio la
ghafla na hatari kwangu.
Gari naliona wale watu walikuwa sita. Pale chini
wako tano hata sikuwa naelewa kwa lile tukio kwa
kuwa sifahamu. Niliona vyema nijifiche kwanza,
niliiba mtumbwi wa karibu yangu kisha nikaingia
ndani ya maji na kukaa kwa mbali hivi nione nani
ambae alifanya lile tukio au ilikuwaje...
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI 22
ENDELEA......
.................Nilikaa kwa takribani dakika kadhaa,
jua likapambazuka na asubuhi ndio inaingia. Watu
walianza kuingia maeneo yale ya ufukwe ndipo
wakaanza kuzunguka lile eneo huku wengine
wakawa wanakimbia ovyo.
Akili yangu ilirejea sasa kwa kile kilichotokea kuwa
mimi ndio sababu kubwa.
Niliwaza baada ya kuwa na akili ya kawaida sasa ya
kibinaadamu na kujua kuwa yale niliyoyafanya si
mazuri kabisa. Ila tatizo nilishindwa kurudi pale
kuwa watanifikiria vipi. Nilisukuma lile jahazi langu
taratiibu kuelekea pale ufukweni.
Nikiwa na bukta yangu, nilikaribia fukwe ndipo watu
wakaanza kugeuka na kunitizama mimi pale.
Tukawa sasa tunashangaana. Lile eneo wengi
walikuwepo akiwa na yule mzee mashuhuri kwa
mambo ya uvuvi, yeye alikuwa ananifahamu fika
kutokana na kuujua mkasa wangu kidogo.
Mimi pia macho yangu yaligota kwenye viini vya
macho ya yule mzee na kufanya tutizamane kwa
sekunde kadhaa. Palepale lilisikika gari lenye mlio
wa king'ola kuhashiria ujio wa polisi ambao waliitwa
kushuhudia yaliyojiri pale.
Yule mzee nilimuona kama kapandwa na jazba
uliojawa na mshangao mkubwa, aliendelea kunikazia
macho na mimi nikaanza kurudi nyumanyuma baada
ya kuhisi jambo la hatari mbele yangu likikaribia
kupitia yule mzee. Ndipo alipoanza kusema na
kuwafanya wale wengine kushiriki kile akisemacho.
"Jamanii! Huyu mnamfahamu huyuu?"
Wengine walishindwa kuitikia kwa kuwa
hawakunifahamu ila wengi hasa akina mama
waliitikia.
"Ndio huyu si Mnalihuyu, alikuwa anatuuzia samaki".
"Sasa naomba mnisikilize! Huyu sio mtu kwa sasa"
"Sio mtuuuu...kivipi?"
"Hizi maiti huyu ndio mhusika na ndie alimuua
Kibona ndugu yetu hapaswi kumuacha hai".
Aliendelea kuongea huku akilazimisha kuendesha
hisia za watu na kuziteka kwa kuziamisha kuwa
mimi mbaya.
Ni kweli ila yeye alizidi kuliongea lile kwa hasira ya
kutaka kunimaliza. Palepale Polisi nao walifika mimi
nikiwa kwa mbali hivi nazidi kuyoyoma.
Huku ufukweni zilibaki kelele za kunipigia mimi
wakiwa hawafahamu kuwa wanampiga teke chura
kwenye maji.
"Huyooo muuaji huyoooo".
"Mkamateniiiiiii".
Nashangaa nilipata nguvu za kupiga kasia na
kukiondoa chombo pale. Punde kauli ya mapolisi
ambayo iliniamuru mimi kusimama ilisikika.
"Kijana kwa usalama wako simama kabla hata
hatujatuma vyombo kuja kukukamata kwa nguvu ya
sheria".
Nikiwa najisemea mwenyewe kuwa.
'Bora hata kwenda kuishi kule kisiwani kuliko
kunikamata nyinyi'.
Hapo ndipo kasi ilizidi kuongezeka zaidi ya kupiga
kasia. Niligeuka nyuma kwa mbali naona boti zenye
kutumia mashine zikipiga mwanga kuelekea
kwangu. Tayari kila mmoja ana uchungu na mimi na
ana hamu na mimi kukamatwa na kufanyiwa haki
ambayo ingepaswa kufanyiwa.
Kutokana na upepo kuvuma sana maji yakiwa
yanakupwa. Kutoka ufukweni kwenda mbali upepo
uliovuma kutoka nchi kavu kuingia baharini. Ulifanya
chombo changu kusonga haraka sana.
Sikuwa nafahamu wapi naelekea lakini niliwaza
kuwa lazima nifike kule kisiwani hata kwa nguvu
yeyote ile.
Kutokana na hofu kubwa niliyonayo, pamoja na
mashaka ya kukamatwa na mapolisi walioungana
na wavuvi kadhaa ilinifanya hali yangu kubadilika
sasa.
Mikono yangu ilikakamaa na kufanya misuli itune.
Hali hiyo ilipelekea damu nyingi sana kuelekea
kwenye mikono na hatimae kuwa na nguvu
maradufu.
Lakini damu ni ngumu kushindana na mashine, Wale
polisi walinikaribia na kunizingira huku wakitaka
nirejeshe chombo nyuma yaani nirudi nchi kavu.
Taratiibu hawa wanasogea kadhaa wakinionyeshea
bunduki, nilifikilia kuwa nikikamatwa nitakufa dhalili
mbele yao kwa sababu sitokubali kuteswa kwani
hata hali yangu tangu inianze haitajiki nisumbuliwe
hivyo nitasababisha madhara tu. Lakini pia
nikikamatwa nitafanywa kama jumba la
makumbusho kila mmoja kuja kunitizama
ninavyobadilika pia najua hata mke wangu na
mwanangu wakisikia hawatokuwa na amani.
Hili tatizo limetokea kisiwani kule inabidi nirudi
kulekule kutafuta tiba yake, siwezi kukubali
nikamatwe kizembe hapa.
Niliamua kujitupa kwenye maji na kuwaacha
wakizubaa kwenye vyombo vyao.
"Hakikisheni mnamkamata huyo".
Nilijaaliwa kuwa na uwezo wa kutopumua kwa
sekunde za kutosha ambazo pia nilizitumia kwa
umbali mrefu.
Niliibuka mbali na wao, waliponiona nikazama kwa
hiyo mchezo ukawa huo mpaka tulipopotezana.
Nguvu ziliniishia kabisa ndipo nikabaki nahemea juu
juu kama mwizi aliyepigwa na kusubiri hukumu ya
kifo tu.
Maji yalinipeleka nikiwa kwenye usingizi mzito
ambao ulitokana na kupoteza fahamu.
Nilishtuka baada ya kuanza kutema maji kwa wingi.
Kama mara sita hivi nilitapika maji tu, nilishtuka
nipo fukweni tofauti na pale ambapo napafahamu.
Niliinuka taratiibu huku nikipiga mahesabu kuwa
haya ni maeneo gani. Baada ya muda kadhaa jua
lilikuwa kali sana na mimi nikiwa ndani ya hiko
kisiwa nisichokifahamu.
Nilijichimbia ndani huku nikiwa makini nisije
kukutana na vile viumbe tena.
Lakini ghafla nilikutana nao kama watatu.
Nilishtuka, nikataka kurudi nyuma, nikapiga hatua
moja nyuma.
"Ng'raaaiiiii...iiiiiiieeeiii".
Sauti ya wale viumbe nyuma yangu ilikuwa
inasikika. Hapo ndipo nikajua maisha yangu
yamekuwa mwisho sasa.
Niligeuka kweli nilikutana nae mmoja na mbele
yangu wakiwa watatu sasa. Walinikaribia na kuanza
kuninusanusa mara kadhaa huku wakinizunguka.
Niliwaza nikimbie maana hofu ilinitanda mpaka
miguu ikaishiwa nguvu na haja ndogo ikigonga zipu.
Asikwambie mtu jasho lilitoka japo kulikuwa na
ubaridi wa aina yake. Sasa wote walikaa upande
mmoja yani wale watatu waliama mbele yangu na
kukaa kwa yule mmoja huku wakinirukiarukia kama
kunilazimisha kutembea.
Nililiwaza hilo nikapiga hatua moja na nyingine
wakawa wanafuata kwa nyuma. Ndipo nilipotembea
huku nikiwaangalia wale. Mmoja akasonga mbele
kwamba nimfuate. Nilitembea hivohivo hadi eneo
fulani hivi ambalo nilikuta mifupa mingi ya wanyama
na mafuvu ya wanadamu kadhaa.
Nilizidi kuchanganyikiwa pale, nilishindwa
kuwaelewa wale wanyama aina ya vibwengo vina nia
gani na mimi. Ndipo mmoja akawahi kwa mbele na
kupita kwenye kipango hivi, kazi huku nyuma hawa
wengine waliokuwa wakikoroma na minjino yao ya
ajabu. Sasa kila hatua niliyokuwa napiga pale
nakanyaga fupa au fuvu la kichwa cha mnyama au
binadamu.
'Daaah! Sasa kama hawa wameliwa mimi nitabaki
kweli au ndio naenda kuliwa'.
Nilizidi kuwaza zaidi huku nikiomba mungu japo
nilitaka mwenyewe kuja kisiwani.
Tulipofika pale kwenye lile pango mmoja akaingia
na kutoka huku wakikoroma kwa nyuma yangu
kama kunilazimisha na mimi niingie.
Niliinama na kujilazimisha kupita kwenye lile pango
hadi nilipofanikiwa kuingia ndani. Aisee huko ndani
hakusemeki kiza kinene, taa zilizokuwa zinaonekana
ni macho yao tu. Ghafla ule mlango wa kuingilia
ulifungwa "Mbaaa".
Mamaa yangu!.
Nilijisemea mwenyewe.
Nilitembea mule ndani hadi mahali fulani ambako
kuna ukuta hivi, ule ukuta katikati yake kulikuwa na
kama tundu ambalo lilikuwa linatoa mwanga mkali,
niliusogelea ule mwanga hadi karibu na kuangalia
lile tundu lipo la aina flani hivi limechongwa. Sikuwa
naelewa hata mara moja.
Nilipata wazo kurudi maana pumzi ziliniishia
kutokana na harufu kali ya mizoga. Kila
utakapokanyaga basi mwili wa mnyama uliooza.
Hatimae na mimi nikashindwa kuvumilia na
kudondoka palepale.
"...kijana! Unakumbuka mzigo gani ulikabidhiwa!..
jitahidi sana ile almasi nilikuambia itakusaidia
kwenye maisha yako nyakati zinyewe ndio hizi..na
hapo ndio mahali penyewe...ulipouona uo
mwanga...hao viumbe wamekulazimisha ufike hapo
kwa sababu hiyo..wameshindwa kukuua kwa
sababu una asili yao kutokana na kkuathiriwa baada
ya kung'atwa....fanya hima upate lile sanduku ndio
maisha yako...pia hao wanaamini kuwa wewe ndio
mwenye uwezo wa kuwasaidia..hao...hawawezi
kukuacha hapo...sasa fanya jitihada kuwatoka pia
fanya jitihada kurudi kwenu kuchukua lile sanduku
kwa maisha yako....".
Nilishtuka toka ndotoni. Maneno ambayo niliyapata
kutoka kwa mtu nisiyemfahamu sasa kibarua
kizito...
Je?...nini kitajiri
 
Simulizi nzuri sana.
SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU 23
ENDELEA........
.................
Watsapp:: 0766988172
.................
................
................Baada ya kuhakikisha kuwa nilikuwa
kwenye njozi nilikaa kitako lakini bado harufu kali
ilizidi kunibana puani mwangu.
Siku na hata la kufanya kwani mwanga ule wa
mwanzo sikuupata tena zaidi ya kiza kinene
kutanda.
Hata njia ile ya mwanzo niliyoingilia sikuweza
kuiona tena, hapo ndipo nilipojua kuwa sasa
nakwenda kuangamia. Nyakati hizo nilijishangaa ule
unyamaunyama ulishaniisha kabisa na nikabaki
kuwa wa kawaida sana. Nilisimama kisha nikaanza
kuchunguza mazingira ambayo ningeweza kutoka
mule pangoni.
Kwa kweli nilijiona nakwenda kufa kwani hewa yote
ya oxygen ilikuwa imepotea. Nilijipa moyo kwa
kutembea kwenye miili ya wanyama waliokufa.
Nilipata wakati mgumu kupitia ile ndoto kuwa lile
sanduku ndio maisha yangu na nahitajika nifanye
harakati zote kulipata, lakini hawa wasifahamu kuwa
natoka.
Niliendelea kuzunguka mpaka pale nilipoishiwa
nguvu za kutembea kutokana na harufu chafu ya
mizoga. Sikuwa nafahamu vyema ni aina gani ya
mizoga ilikuwemo humo japo ni ya wanyama lakini
wanyama wa aina gani, hii ilitokana na giza nene.
Nikiwa kwenye moja ya kona ndipo niliona kama
mstari hivi unajichora kumbe ni mwanga uliojitokeza
kutoka kule kwenye mlango wa kuingilia ndani.
Ule mwanga ulinipa mashaka kwa kiasi fulani, ndipo
moyo ukaanza kudunda ghafla ndege waliokurupuka
kutoka kule kwenye mwanga walikuja hadi lile eneo
ambalo mimi nipo. Ndege hao aina ya popo
walinipipa bishara kuwa mlango umefunguliwa
kwani walionekana kutokea nje.
Niliona ni wakati tosha sasa niweze kunyatia kupita
pale ili nitokee kule ufukweni. Kwa mshituko wa hali
ya juu nilishangaa baada ya kusikia sauti ya
mingurumo ya wanyama fulani ambao sikuweza
kuwafahamu vyema.
'Mh! Hili eneo ni hatari, hapa nikichelewa naweza
kuwa maiti muda si mrefu'.
Niliweza kutafakari mimi mwenyewe baada ya kuhisi
hatari kubwa mbele yangu.
Niliamua kuingia ndani zaidi ya pango kisha
nikafika mwisho wa safari yangu.
'Hakika mbio za sakafuni huishia ukingoni! Leo
yamenikuta'.
Tumbo langu lina njaa kali sana, lakini hakuna hata
chakula pale nilipo, hata kama kingekuwepo
nisingeweza kula kutokana na hali ya hofu
niliyonayo.
Kwa mbali nilisikia kama ukuta unapigwa na wimbi
la maji kutoka baharini,
'Khaaa! Ina maana nakaribia kutoka'.
Nilipata wazo niweze kubomoa sehemu ya ukuta ili
niweze kupita na kutokomea kabisa maeneo yale
yenye hatari. Nilifanikiwa kuvunja hadi nikaona tundu
kubwa limepatikana na ndipo nikalazimisha kichwa
kupita. Kama unavyofahamu sehemu yeyote kichwa
kikipita basi mwili nao utapita.
Nilipata nafasi hiyo na kutokeza hadi nje na mimi
kujiona mshindi wa lile shindano ambalo bado sijui
mwisho wake uko wapi . Sikuwa na jambo
lingine zaidi ni kuanza kutokomea pale. Ndipo
nashangaa kuona wanyama wale vibwengo wakipita
nao pale kwenye tundu na kushuka chini huku
wakionekana kuwa na hasira kubwa sana. Nilipatwa
na mshtuko mkubwa sana, nilikumbuka ile ndoto
kipindi nipo pangoni ikinisihi niondoke mule lakini
bila wale viumbe kuniona.
Itakuwa walikuwa wananitafuta mule pangoni na
hatimae wakafanikiwa kuniona. Niliwafahamu kuwa
hawa viumbe hawana uwezo wa kuingia ndani ya
maji kwa hiyo wataendelea kubaki palepale
wakitapatapa na ndimi zao ndefu kunitamani mimi.
Niliamua kuwakatisha tamaa baada ya kuingia ndani
ya bahari na kusogea eneo mpaka kule nilikokuwa
awamu ya kwanza.
Nakumbuka kipindi nipo na yule jamaa
aliyenisaidiaga kipindi kile baada ya kudhuriwa na
hawa viumbe kisha yeye akatokomea ndani ya maji
baada ya kunisaidia kupata sanduku.
Mitumbwi kwenye fukwe yeyote hata kisiwa huwa
haikosekani.
Niliupata mmoja kisha nikajipanga kurudi kuelekea
mjini kwa ajili ya kuchukua lile sanduku.
Safari yangu kama kawaida niliisubiri hadi usiku
ndipo nikaingia nchi kavu ya ule mji wangu
ninaoishi. Kama kawaida nilifika nyumbani sehemu
ambayo imekuwa kama gofu kwa sasa nikapata
shati na suruali nikabadili japo zilikuwa chafu sana.
Usiku uleule nilitimua mbio kuelekea kwa yule binti
anaejulikana kwa jina la Salha.
Sikufahamu yalikuwa majira gani lakini nilichojua ni
kufika tu kwenye ile nyumba basi. Hatimae nilitumia
muda mwingi kutokana na umbali wa lile eneo hivyo
nilichoka sana. Nilipofika getini sikutaka kuingia
kwa njia ya geti kutokana na shauku niliyonayo ya
kutaka lile sanduku.
Sikujali kama nitakutana na afande kolokoloni pale,
nilitafuta eneo zuri ambalo ninaweza kupitia.
Nilirukia ukutani na kwa jinsi nilivyouparamia
nadhani hata kama mlinzi alikuwa kalala basi
aliamka.
Nilijinyonga vyema kutokana na wepesi wangu wa
kupita maeneo kama yale. Sasa na mimi nilikuwa
kama kibwengo wa kule kisiwani maana mambo
yangu hata sikuwa nayaelewa. Nilipotua chini
nakutana na mlinzi ambae alishawasha taa na
kuukoki mgobole wake (Bunduki) ili akabiliane na
adui.
Nilimuangalia kisha nikataka kuwa mpole baada ya
kuhisi kuwa kaniona, lakini ajabu ananisogelea na
kunipita kana kwamba hanioni, nilipiga hatua mbele
napo hakustuka.
'Ina maana hanioni?, mimi ni nani safari hii'.
Nilijiuliza swali hilo huku nikimuona mlinzi huyo
akielekea eneo lake la kupumzika na kuupiga
usingizi.
Nilipata fununu kuwa labda mlinzi alikuwa na
mchoko wa usingizi ndio maana hakuweza
kunizingatia. Taratiibu naelekea hadi kwenye mlango
wa mbele ambao huwa wanaingilia. Nilishika kitasa
ghafla nikasikia kitchie!!!. Alafu mlango unajifungua.
Huwezi kuamini geti lilikuwa kama buwa kuligusa tu
napita. Nilijishangaa, lengo ni kupata boksi langu.
Nilitembea kidogokidogo kuelekea chumbani kwa
Salha ambako nilipafahamu mwanzo kabisa.
Nilifanikiwa kuingia hadi chumbani kwake ndipo
nilimkuta akiwa kalala kama alivyozaliwa. Tamaa ya
mwili kama mwanadamu ilinifanya nijikute
namuingilia binti yule bila hata yeye kujifahamu.
Nilikuwa kama shetani aliyekimbia kuzimu.
Lakini kwangu ndio lilikuwa kosa kubwa sana kwani
nilishtuka asubuhi baada ya kelele za Salha.
"Heeee! Nini"
"Wewe nani? Na umewezaje kuingia humu ndani".
Niliona ni muda wa kutumia nguvu sasa.
"Samahani ila, hata nikakuambia huwezi nielewa,
unanikumbuka mimi ni yule ambae ulinisaidia kile
kipindi nimekamatwa na polisi kupelekwa hadi
hospitali.. na wewe ukanisaidia hadi hapa".
"Sawa...nakumbuka umeingiaje humu....?"
Tulizozana sana hadi nilipotumia nguvu ya
kumkalisha kimya.
"Wewe mwanamke! Niambie sanduku langu
umeliweka wapi...?"
"Hapana mimi sifahamu tangu wazoa taka waje
hapa kuchukua ile siku nadhani walilibebelea..."
"Sikia lile sanduku ndio maisha yangu mimi mpaka
sasa.....nakutaka unipe taarifa kamili kuhusiana na
hao wazoa taka niwafahamu...boksi kama lile
likionekana lazima likamatwe hakuna anaeweza
kuliacha hivhivi.".
Salha alinielewa kwa kuwa hata mwanzo nilikuwa
pale.
Tulianza kupanga mishen nzima ili kupata lile
sanduku.
"Sasa...mnali unatakiwa kujificha humu
chumbani....utakuwa unatoka usiku tu huo ndio
msaada wangu uliobaki".
Nilikubaliana na yeye ila nilimuomba anipe taarifa
kuhusiana na hao watu wanaohusika na mambo ya
uchukuaji taka majumbani. Siku kama tatu nikawa
nimefanikiwa kuwajua hadi eneo ambalo wanaishi
wale wazoa taka na mimi nikajiandaa kwa ajili ya
kuelekea huko.
"Mnali... unajua sikuelewi siku ya pili hii unachokula
sikifahamu haya leo unakula nini?".
Nilishindwa kumueleza ukweli kuwa chakula cha
kawaida kwangu hakipandi zaidi ya nyama mbichi.
"Salha! Ngoja nikuhadithie historia yangu ili
unielewe..."
"Haya nakusikiliza..."
Nilimhadithia kila kitu.
"Daaah! Jamani sikudhani kamaa kuna watu
wanaishi hivyo kama wewe...kwa hiyo nyama
mbichi tu basi".
"Yani ndio hivyo ndio inanipa nguvu hata kufanya
vitu vingine ambavyo mwanadamu wa kawaida
hafanyi..."
"Mh! Kwa nini"
" teh teh"
Nilibaki kucheka tu.
"Unataka ufahamu?"
"Ndio..."
"Basi niletee nyama mbichi alafu kabla sijaenda
kuwafuata wale watu nitakuonyesha wewe kwanza
hapahapa chumbani...."
Salha alizidi kuchoka kwa kila hatua ninayomueleza.
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE 24
ENDELEA.....................
.................
...24.........
Salha alitulia kisha akaniuliza tena,
"Mnali, unajua sijakuelewa japo umenieleza kila kitu
kinachokuhusu, sasa inawezekana vipi usile chakula
cha kawaida alafu badala yake ukapenda nyama
mbichi?".
Swali lake lilikuwa lina maana kubwa sana kwangu
lakini sikuwa na namna zaidi ya kuwa muwazi
mbele yake.
"Salha! Nisikilize kwa makini tena kwa umakini
mkubwa sana"
"Ndio nakusikiliza".
Niliinuka kisha nikauelekea mlango nikautikisa ili
kujua kama umefungwa na kweli ulikuwa
umefungwa.
"Vipi! Hakuna mtu tofauti na mimi na yule mlinzi"
"Kwa nini uishi peke yako"
"Basi tu haya tuendeleee"
"Sawa Salha! Kama nilivyokuelekeza natafutwa na
makundi mawili mpaka sasa tena matatu..hapa
ninapokuambia polisi nao wananitafuta, maisha
yangu ni ya ajabu sana na yameibuka kutoka hivyo
na tatizo ni Uvuvi wangu".
"Uvuvi wako? Kivipi tena".
Aliuliza
"Maisha ya Uvuvi ndio chanzo cha haya yote. Kama
mke wangu asingekuwa analazimisha kutaka
maisha mazuri ya kifahari mimi nisingejiingiza
katika hali hii".
Tulitumia muda wa masaa kadhaa mimi na Salha
kuongelea maisha yangu kiujumla. Historia
iliyomuacha hoi na kumtoa chozi binti wa watu.
Wakati huo nina nia ya usiku kuwafuata wale
majamaa kufuatilia lile swala la Sanduku ambalo
ndio maisha yangu kwa sasa.
Ilikuwa majira ya Saa kumi na mbili jioni jua
kuzama nikiwa kwenye foronya moja wapo mule
ndani. Tangu niweze kuathirika na wale wanyama
sikuwa na akili zangu za kawaida kwanza nilikuwa
Mcheshi nisieogopa chochote kile, sikuwa muoga
tena wala mwenye aibu kama mara ya kwanza pia
ni historia yangu tu inayonihusu ndicho ambacho
nilikuwa nakikumbuka kichwani kwangu.
Salha alinyanyuka na kwenda kuandaa chakula huku
akiniacha peke yangu mule chumbani. Kama
nilivyokuambia sikuwa na hofu kabisa alafu nilikuja
kujiamini sana.
Wakati yeye Salha yuko Jikoni mimi nilijiegemea
kwenye kochi na kufumba macho kidogo huku
nikitafakari juu ya mustakabari wa maisha yangu
jinsi unavyokwenda.
...."Sikia! Usalama wako ni pale tu utakapofanikisha
kufikisha sanduku sehemu husika...".
Nilikuja kushtuka kumbe nilikuwa dotoni. Kuna kitu
kama kinanikumbusha wajibu wangu wa kufanya ila
bado sijatambua ni nani au anahusika vipi huyu na
maisha yangu mimi kiujumla.
Hapo ndipo Salha alikuja na Sahani mbili
zilizofunikwa.
"Haya! Ila bado siamini kuwa ukila nyma mbichi
unakuwa wa tofauti".
Kweli zililetwa Nyama kama vipande vitano hivi na
yeye akawa anakula chipsi yai pamoja na nyama za
kukaanga. Alianza kula na mimi nikaanza
kuzitazama zile nyama ndipo mwili ukaanza
kusisimka mate yakaanza kujaa pale ghafla napata
hamasa ya kuvamia vile vipande na kuvitafuna
dakika zisizozidi mbili tayari nilikwishamaliza na
kumuacha Salha akiwa anaduwaa.
"Mamaaaa yanguuuu weeeee!"
Salha hakuweza kuamini kama kweli naweza
kufanya vile.
"Salha! Unashangaa nini bado ngoja kama
unakumbuka awamu ya kwanza ulishangaa nyama
jikoni zinaisha hukuwa unafahamu alikuwa mimi
yule.."
Palepale mwili ulichangamka damu zilikwenda kwa
kasi ya ajabu mwilini. Mikono yangu ilikakamaa
nilitokwa na jasho jingi, Salha aliniogopa kwa kweli.
Binafsi sikuwa nafahamu nini nafanya kwa kuwa
hata akili iliruka. Kila nilichotaka kufanya niliona
sawa tu. Nilisimama ndipo nikamtia hofu zaidi
Salha aliyetaka kukimbia mule chumbani.
Muda wa mchache tayari nilishamkamata na
kujikuta tunaingiliana kimwili, katika hali
isiyofahamika Salha alilia kwa uchungu wa ukweli
kuwa anapata maumivu sana. Mpaka tunamaliza
hakuna ambae aliweza kumuangalia mwenzake.
Mimi tayari nguvu zote ziliniishia kwa kuwa
nilitumia hadi nguvu zangu za ziada. Nakuja
kushtuka saa nane usiku siwezi hata kuinuka
kitandani. Asubuhi na mapema najilaumu kwa nini
nilifanya lile tukio.
"Mnali sijawahi fikilia swala kama hili, kuanzia sasa
naomba niwe wako sitaki nikose mapenzi yako
kabisa".
"Hapana hata hivyo najilaumu kwa jambo kama hili
ila siwezi kuwa na wewe kwa sababu nina mke na
mtoto naamini mke wangu ananipenda bado sitaki
ijirudie tena".
Nilijikuta namlaumu sana Salha, amenifanya hata
kuchelewa katika lile dili langu.
"Khaaa! Unadhani ni mwanamke gani ambae
anaweza kuacha radha hii au ni mwanamke gani
anaweza kukuvulia nguo alafu umchezee umuache
eti nilikuwa sijielewi, sasa sikia ukisumbua hutotoka
humu ndani."
"Kwa nini Salha unifanyie hivyo"
"Au laaah! Utalikosa hilo sanduku."
"Hapana nakuomba uniache kwa sasa nikifanikiwa
nitarejea kwa ajili yako. Nakuahidi.."
"Mnali mimi sio mtoto mdogo unaelewa. Chagua
moja"
"Eeeeeh!"
"Husikiiii! Chagua moja kukosa Sanduku lako au
kuwa na mimi ili ulipate hilo Sanduku kwa muda
tutakaoishi kama wapenzi".
Hapo aliniacha nikiwa na mawazo mazito asubuhi
hiyo, mpaka nikajilaumu kwa nini nimefika hapa, pia
hali yangu.
Najua Salha niko mikononi mwake hadi sasa
inanibidi nikubaliane na lile alitakalo ili nifanikishe
azma yangu.
"Salha sawa nimekubali kuwa na wewe kama
unavyohitaji ili niweze kupata sanduku langu."
" "
Salha alicheka sana kwa kuwa anafahamu sina
ujanja mwingine zaidi wa pale. Salha aliendelea
kunipa maneno ya kimapenzi pale na ndipo
akanikamata sana kimawazo. Kila mmoja alienda
kuoga kwa muda wake. Wote tulikaa pale kitandani
huku mimi nikiwa nawaza vitu vyangu kabisa.
Siku hiyo ilipita kimawengemawenge, mpaka
ilipofika jioni ndipo nikajipanga vyema sasa
kuelekea katika kampuni moja ya uzoaji wa
takataka. Nilikuwa na Salha, tukiwa kwenye gari
Salha aliniomba nibaki kwenye gari alafu yeye
aelekee akaangalie humo ndani mkoje kisha atakuja
kuniambia.
Njia ambayo aliniambia kuwa ataingia kwa njia ya
kusema anaenda kulipia bili ya ukusanyaji wa
takataka tena. Hapo sikuwa na ubishi. Nikiwa
kwenye gari katika kuangalia angalia nilikutana na
Simu ya Salha, niliigundua baada ya kuwaka
mwanga.
Nilipoangalia niliona Meseji kutoka kwa mtu mmoja
anaitwa (Mr. Poooo).
Mh! Sikuweza kuangalia nini kimeandikwa kwa
sababu kulikuwa na pass word. Ila jina lilinitikisa
akili kidogo si kwamba nilijua ni yule mzee Paul ila
nilimkumbuka yule mzee. Ghafla Salha anarejea.
"Sasa! Sikia tayari nimeingia ndani nimeongea nao
kuwa kuna mzigo walikuja kuuchukua kule
nyumbani kimakosa...ila wanasema
hawaufahamu..."
"Daaah! Sasa inakuaje tena!"
"Mh! Ngoja kwanza naomba simu yangu hapo
kwenye kiti".
Niliichukua na kumpatia.
"Sawa nashukuru sana! Ngoja nakuja acha
nikaongee nao tena".
Basi nilitulia kwa kuwa sina Uhakika sanduku liko
wapi. Ghafla anakuja jamaa mmoja aliyeonekana
kama msimamizi hivi wa mule kwenye kampuni.
"Mambo vipi mheshimiwa"
Jamaa aliniuliza
"Poa kabisa"
"Ok! Vipi mwenye hili gari yuko wapi yani yule dada
ambae ulikuwa nae humu".
Kwa kuwa nilivaa jaketi lenye kofia hakuweza
kuniona vyema.
"Aaah! Huyu dada yuko humo ndani anafanya
mazungumzo na wahusika humo ndani".
Ajabu akanza kuniinamia kupitia pale dirishani, pia
na mimi nilifunika zaidi Sura yangu ili asinione.
"Sikia! Unamjua vyema huyu dada...."
"Mh! Kwa nini unauliza hivyo.."
Nilishangaa sana yeye kuniuliza swali lile. Lakini
alikuwa ananicheka sana kisha akasema
"Kijana Be care..".
Mh! Alinitisha sana sikujua anamaana gani kwa
sababu hii lugha siifahamu kabisa kiingeleza.
Ndipo Salha anakuja anapishana na yule jamaa.
"Mnali, ulikuwa unaongea nini na huyu!"
"Hapana alinishangaa tu kwa nn tupo hapa kwa
muda sana".
"Mnali, Be care".
Hapo nilishtuka sana "Salha! Hilo neno lina maana
gani?"
" maana yake Kuwa Makini na hawa
watu"
Ahaaaa na mimi nikajua kuwa yule jamaa aliniambia
niwe makini na Salhaaaa. Kwa nini niwe makini na
Salha, ana nini Salha.
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO 25
ENDELEA............
.................
................
Basi ndipo Salha akaingia ndani ya gari kisha
akafunga mlango wa gari yake na kuondoka yale
maeneo. Nikiwa nazidi kuwaza hali yangu ya
maisha niliyonayo ndipo nikagundua kuwa hata
matajiri hawana furaha kwa hali hii. Kama mimi
mwenye maisha magumu naishi kwa raha lakini
kwa hatua chache ya kushuhudia maish ya wale
walioendelea naona kabisa wanapata tabu.
Gari lilifika hadi kwenye nyumba yake na mlinzi
akafungua geti haraka sana na sisi tukapata kuingia.
Akili ya Salha ililala sana kwenye mapenzi tofauti na
mimi mawazo yangu aliniangalia kwa jicho la
mahaba lakini mimi nilimkata jicho tu. Sikutaka
kumuonyeshea moja kwa moja kuwa nimemkubalia
ndio maana nilikaza baadhi ya sehemu kama hizo
ambazo yeye alizifanya.
Alinishika mkono tukaelekea ndani baada ya
kufungua mlango wake. Nilifika nikatulia kwenye
kochi pale sebuleni kisha nikajishika kichwa changu
huku nikitazama jinsi Mzungu alivyotengeneza taa
na ikawa inatoa mwanga mzuri na ukatusaidia
kuangaza vitu vingi kwa sehemu mbalimbali.
Niliwaza maisha ya kule Kisiwani, nilijiuliza vipi
nirudi au niachane nayo. Kwa sababu nilijihisi kama
nimepona hivi. Ila nikaachana na hayo mawazo
ambayo yangenifanya niruke wazimu mule ndani
kwa kuumwa na kichwa. Ndipo namuona Salha
anarejea na chupa kimoja hivi, alikuja nacho hadi
pale mezani na kutoa glass mbili.
"Ehee! Beby unatumia hiki kinywaji?"
"Kinywaji gani?"
Nilimuuliza
"Heeee hujui kama hii ni pombee."
Nilishtuka Pombe na mimi wapi na wapi.
"Hapana situmii hiyo labda soda".
"Acha Ushamba baby ebuu onja kwanza".
Nilishindwa kumuelewa kwa mapema sana japo
wasiwasi uliniingia pale tu nilipoambiwa Be care
"Hapana Salha wee kunywa tu mimi sijawahi
kutumia kabisa na sihitaji kutumia".
Lakini alimimina ile pombe kwenye moja ya glass
pale mezani, kisha akaanza kuniangalia. Nilimkazia
uso ili kumuonyesha msisitizo kuwa situmii vitu
kama vile. Mwanamke alitumia uwezo wake kama
mwanamke akaanza kulegeza macho kama kameza
kungu manga. Aliigiza kulewa macho hata kabla
hajanywa bado aisee.
Nilipata tabu sana kuepukana na shetani yule wa
pombe lakini kwa bahati mbaya mfuasi wake
alikuwa na vigezo vyote vya kushinda. Alisimama
kisha ndipo akavua nguo zake zote na kubaki
mtupu. Binafsi moyo ulidunda akanijia hadi pale
nilipoketi, alizidi kuteka akili yangu na kumuacha
afanye kila kitu anachokitaka.
"Baby si nimekuambia kuwa nakupenda".
"Ndio"
"Shida yako nini?"
"Hakuna"
"Haya onja ili wote tuwe kwenye ulimwengu mmoja"
"Ila..."
"Nooo! Hakuna ila onja bhana".
"Haya".
Nilipiga glass moja mpaka macho nikahisi yanataka
kuchomoka.
"Hiyoo inaitwa Wisk honey"
"Oooh! Shalha hata mimi naiona hii".
.....Asubuhi na mapema nashtuka nikiwa kama
nilivyozaliwa tena nipo kitandani. Kichwa changu
kiliniuma sana.
Nilikumbuka kuwa ni zile pombe za jana lakini hali
yangu si nzuri siwezi hata kusimama. Mwili mchovu
kama nimepigwapigwa, mikono yangu iliishiwa
nguvu siwezi hata kuinua na kuipandisha.
Mdomo wangu pia mzito kusema kwa sauti kali
ambayo kama kuna mtu anaweza kunisikia.
Nilijishangaa kuona ile hali kuwa ni mbaya sana.
Nilijitahidi kuinua sauti na kumuita Salha lakini
hakuwa karibu, nilijitutumua na kufanikiwa kukaa.
Wakati natafakari lipi limetokea simu pale kitandani
inanguruma, nilitafuta nilipoipata ilikuwa ni ya Salha
aliiacha. Nilijiuliza Salha kaenda wapi basi atakuwa
hayuko mbali kwa kuwa simu kaacha.
Niliangalia ni meseji kutoka kwa bwana Pooo.
"Mh! Hivi hii namba si jana niliiona kwenye ile simu
kubwa leo ipo tena kwenye simu ndogo ngoja."
Nilifungua kwa kuwa haikuwa na pini yoyote.
Nakutana na ujumbe ulioandikwa kwa herufi kubwa
kuonyesha msisitizo. (SALHA! HAKIKISHA
UNAMALIZA KAZI ASUBUHI YA LEO.)
"Eboooo! Hakikisha unamaliza kazi asubuhi ya
leo?..ahaaa kazi gani ambayo kaambiwa
amalize..labda wafanya biashara hawa. Lakini yuko
wapi?".
Niliikariri ile namba harakaharaka kisha nikaacha
simu pale ilipokawepo mwanzo. Nililala tena huku
nikiugulia maumivu yangu. Nilijiuliza sawa kama
ndio mara yangu ya kwanza kunywa pombe lakini si
kwa maumivu haya, na kama wote wanaokunywa
pombe wanapitia haya maumivu wanakazi na ndio
maana kumbe pombe haramu.
Mengi niliongea lakini jambo la kizani niliekwenye
mwanga nitazidi kubashiri lakini hakuna uhalisia
kabisa. Muda unaenda lakini Salha haonekani ndipo
nilipojiondoa japo kwa kibishi hivyohivyo hadi
kusimama pale sakafuni.
Nilitafuta Nguo zangu sikifanikiwa kuziona kabisa.
Hapo ndipo nilizidi kuchanganyikiwa zaidi. "Huyu
kaenda wapi?".
Nilichukua taulo nikajifunga kisha nikataka kufungua
mlango ili nitoke Mngurumo wa simu ile ndogo
uliingia tena. Nikataka kudharau ila nikachukua
simu na kuangalia ilikuwa ni meseji. "TUNAKUJA
SASA HIVI HAPO KWAKO".
"Mh"
"Nilishtuka! Nikaona kumbee hili swala lawezekana
linanihusu...je? Yule jamaa kule kwenye kampuni ya
uzoaji taka aliniambia Be care yani niwe makini na
huyu mwanamke".
Pumbavu sina muda wa kupoteza nilienda hadi
bafuni huku nikichechemea kwa kuwa mguu wangu
sehemu za tako zinauma.
Sikuwa naangalia nini kinanisibu nilipofika bafuni
nikajisafisha vyema japo mwili unauma sana,
niliporejea ndipo nikaona beseni ambalo
limelowekwa Nguo zangu.
"Aisee! Kweli niwe makini na huyu mdada".
Nilikusanya zile nguo toka kwenye maji nikazivaa
kama zilivyo japo zimelowa, nikaingia chumbani na
kuchukua ile simu ya Salha. Nilikubali kufanya
uhalifu mule ndani kwa ajili nijisaidie ili nisije patwa
na madhara. Taratibu nikafungua baadhi ya vitu
mule ndani na moja ya sanduku nikakutana na
Kipande kimoja kidogo cha Almasi.
"Mh! Huyu mwanamke ni tajiri sana kumbe
anamiliki Almasi kama hii".
Niliachana nayo mpaka pale nilipopata kiasi cha
fedha ambazo zingenisaidia katika mihangaiko
yangu. Nikiwa nachechemea nilijiangalia na kuona
pale ambapo wale wanyama walinibana panatoa
funza yani wadudu kabisa hivi.
Nilizidi kuchanganyikiwa sijui lipi nifanye kutoka
mule ndani. Lakini nilifanikiwa kutoka nje hadi kwa
mlinzi ambae alisimama katikati ya geti na
kunitazama.
"Habari za asubuhi kiongozi".
"Salama mheshimiwa sema".
"Sawa naomba unifungulie geti mara moja kuna
mahali naeleke".
"Haaah! Hahaaaa! Hahaaaaa!"
Mlinzi aliangua cheko.
"Kwa nini unacheka"
Nilimuuliza
"Kwa sababu unanichekesha. Sijapewa ruksa ya
wewe kutoka humo ndani, ila nimepewa ruksa ya
kutokukuruhusu wewe kupita hapa getini".
"Daaah! Sasa kaka kama hukupewa ruksa ya mimi
kupita hapa getini limewekwa kwa ajili gani sasa
tutawezaje kuruka ukuta".
"Nisikie braza nipo kazini hutotoka nje nenda ndani
haraka".
Ndipo simu inaita.
Niliiweka sikioni na kuwasikiliza.
"Helloo! Salha hakikisha huyu kijana hatoki ndani,
pia mpige sindano nyingine tunakuja sasa hivi".
Sikujibu chochote.
Mwili ulipandwa na hasira lakini ni zile hasira zangu
za kawaida lakini maumivu yangu yalizidi maradufu
na wadudu nikiendelea kuhisi wanatoka na
kudondoka chini tako langu lilioza kabisa alafu
mlinzi ananipa kiwingu pale.
"Kaka! Mimi ni mwanaume mwenzako matatizo
niliyonayo mimi nahisi ungeyajua usingefanya hivo".
"Una matatizo gani wewe wakati unaishi na
wanawake wenye vyao kama hao mimi ndio nina
shida nalala nje kuwalinda nyinyi ndio nimekuambia
kuwa hapa hutoki mpaka Salha arudi".
"Poa Salha yuko wapi?"
"Sijui".
"Basi naomba dakika moja nikuonyeshe tatizo
nililonalo".
Nilivua ile suruali wakati inavuja maji nikageuka
nyuma na kumuonyesha jinsi funza wanavyopikitapi
kita na wengine kudondoka.
"Kaka unaponichelewesha, nazidi kuumia nataka
niende hospitali haraka kaka".
Ndipo nilipomuona kanywea kabisa pale.
"Daah! Kaka pole ilikuaje".
"Huu si muda wa kukuhadithia ila ni muda pekee wa
wewe kunifungulia na kutoka nje niende hospitali
nirudi kisha nakuhadithia kila kitu.".
Jamaa anafungua geti na haraka nachechemea kwa
kuruka mguu mmoja hadi nje nikashukuru sana.
Ghafla gari linakuja kwa kasi ya ajabu kuja pale
nilipo. Ndipo breki kali ikapigwa karibu na pale
nilipo kitendo kilichonifanya nidondoke chini na
kushikilia mikono yangu nyuma nikitafakari nani
ambae kaja na analengo gani na mimi.
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA 26
ENDELEA......
.................Ule uharaka wa lile gari ulinifanya
niweweseke na bila hata kutambua kinachoendelea.
Mlinzi ambae alikuwa kwenye nyumba ile ya salha
alishtuka kwa haraka sana akataka kufungua mlango
ajue nini kinaendelea.
Lakini alitokea jamaa mmoja ambae sikuweza
kumfahamu vyema kutoka kwenye lile gari lake na
kuninyanyua fasta kwa haraka sana hadi kwenye gari
na kufunga mlango na yeye kuingia upande wake.
Nikiwa mule ndani nilifungwa pingu mikononi hadi
miguuni pia jamaa yule maana walikuwa wawili
wakanifunga mdomo, safari ya gari lilikwenda huku
nikizidi kutapatapa maumivu ya mguu wangu, pia
sikuwa nafahamu wale akina nani, safari iliiva hadi
ufukweni kabisa wa bahari ndipo waliponishusha.
Nilikuwa nachechemea kutokana na mguu wangu
kuharibika sana. Yule dereva alifungua mask yake
usoni na nikapata kumuona sura yake ila kadri
nilivyojitahidi kuvuta taswira ilizidi kukataa kutokana
sikuwa namfahamu kabisa.
"Kijana samahani kwanza kwa hili tendo ambalo
tumekufanyia muda mfupi.."
Nilishangaa ananiomba msamaha.
"Sasa mnahitaji nini kwa mimi masikini". Akili yangu
ilizama kwenye ile simu ndogo ya salha yenye
jumbe mbili nilizozishuhudia kwa macho yangu
nikasoma hapo ndipo nikahisi kuwa hawa ndio wale
watu ambao walikuwa wanawasiliana na Salha.
"Sisi hatukuitaji wewe ila mimi ninahitaji roho yako
iendelee kuhema kama wengine."
"Mh! Nyinyi si wale watu mliokuwa mnawasiliana na
Salha kuwa mnamuambia ahakikishe namalizwa
mapema sana."
Niliona wakishangaa ndipo yule dereva akanijia na
kunishika bega.
"Kijana acha hizo fikra kabisa, unakumbuka neno hili
nikikuambia?.."
"Neno gani..?"
"Be care!"
Nilivuta taswira nikakumbuka kuwa neno hili
nilishaambiwaga na jamaa fulani. Wakati mimi na
Salha tunaelekea kule kampuni ya uzoaji
taka.nikaambiwa niwe makini na Salha.
"Wewe ni nani?"..........
"Hupaswi kuniuliza mimi nina?...bali ninachohitaji
kukusaidia na mimi unisaidie sawa..!"
Nia yao ilikuwa mimi kunisaidia japo sikufahamu ni
msaada gani ambao wanataka japo mimi tayari
wamenitoa kwenye kile kisanga cha hatari.
"Sasa nimefuatilia kwa makini kuwa lile sanduku
bado lipo tena kwenye ileile kampuni ambayo ile
usiku mlinikuta kama mlinzi...lakini kwa utafiti
ambao wameuchunguza kuwa lile sanfuku
halifunguki hata kwa njia gani, pia ni sanduku la
kale sana tunachohitaji mguu wako mguu wetu hadi
kwenye ile kampuni, tumeshafanya mchakato kuwa
wapi tunaifikia maana inaonekana wewe ndio
muhusika wa lile huo ndio msaada tunaohitaji."
Nilivuta pumzi ndefu yenye faraja la matumaini ila
hapa nikahitaji niwachezee akili kidogo.
"Jamani sikilizeni kwanza...nawashukuru sana kwa
kunifikisha hapa maana nilishakuwa marehemu..pia
nafurahi kupata ujumbe wa uwepo wa Sanduku
langu.."
"Wee Sanduku letu lako wapi yako maisha..."
Mh nilishtuka.
"Haya sanduku lenu.."
Lakini nina ombi mambo mawili. Hapo nilitulia na
nikawa nawaangalia kwanza muitikio wao.
"Yapi hayo..?"
"Jamani mimi siwafichi maisha yangu magumu hadi
sasa"
"Ongea muda unakwenda"
"Nina muda mrefu sana sijafanikiwa kumuona mtoto
wangu Asante pamoja na mke wangu pia mnisaidie
kuwaona hao viumbe pia mnipatie hilo sanduku
mimi ninawapeleka ambako hayo masanduku
yanapatikana kuna kama matatu makubwa sana
ambayo nilishindwa hata kusukuma na inasemeka
kuna vito vya thamani humo".
Waliangaliana wale wawili.
"Mh! Inaweza kuwa kweli haya tuambie hiyo famulia
iko wapi?"
"Familia yangu inaongozwa na rafiki wa bwana
Paul...."
"Paul huyu mfanya biashara za haramu hapo
mwanzo alikuwa ana hoteli nyingi sana"
Aliongea yule jamaa mwingine.
"Ndio yeye. Mke wangu aliniacha akaenda kwa
mwanume mwingine, nikajiingiza kwenye kazi ya
uvuvi ambayo nilikutana na huyu jamaa.......mpaka
sasa mnaniona upande wa huu mguu unaoza kama
hivi."
Niliwahadithia kila kitu mpaka wakakubali kabisa.
"Sasa tunakuletea familia yako hapa pamoja na
sanduku hilo, lakini kwa sharti moja tu hatutokupa
familia yako mpaka utupeleke huko Kisiwani."
Nilikubali kwa yale yote kutokana nahitaji kuwa huru
kabisa.
"Sawa fanyeni hivyo na mimi nitawafanikishia
kuwapeleka huko salama na mkachukua mtakacho".
Waliniacha pale wkiniahidi jioni yake wananijia pale
nilipo wakiwa na familia yangu pamoja na lile
sanduku ili mimi niwapeleke huko kisiwani.
Nikiwa nimebaki pale simu ilinguruma, hapo ndipo
nikakumbuka kuwa nilikuwa na simu ya Salha.
Niliipokea.
"Mnali...baby mbona haupo umeelekea wapi?"
Sauti yake ya kiunafiki Salha alidhani nitalegea na
kuwa bwege mtozeni".
"Sema shida yako katili mkubwa wewe mwanamke
uliyepoteza sifa ya uanamke wako..."
"Kwa nini unanituhumu hivyo mpenzi wangu..."
"Mshenzi weweeee mpenzi wako nani hapa na
ukome kabisa..."
"Sasa kama unakataa jamani mbona umelala na
mimi na mbona umeshika simu yangu unayo basi
lete...."
"Kulala na wewe ni kama kuingia kwenye dimbwi la
maji kwenye kiza...hunipati tena kumbe wewe
unashirikiana na shetani Paul kutaka kuniua mimi
ndio maana mmeniwekea sumu ile asubuhi eti
unaloweka na nguo zangu kwenye maji.."
Baada ya hapo salha aliona hawezi kunipata kabisa.
"Ahaaa...umejifanya mjanja zaidi ya sungura kula
mmea ambao mwanadamu akila anakufa.. sasa
nakuambiaje chagua moja kati ya haya..kupoteza
familia yako ambayo iko chini yangu sasa au wewe
kujisalimisha hapa mwenyewe."
Hapo akakata simu kabisa. Nilishtushwa na ile
habari maana kama hawa wanaenda kuchukua
familia yangu na wakati Salha anasema iko kwenye
himaya yake?. Mh nini hatma ya familia yangu au
nini hatma ya maisha yangu kule kisiwani?. Nilibaki
kusubiri nikiwa na maamuzi mawilimawili ya kubaki
kuwaamini wale waliokwenda au kwenda kujipeleka,
nilipatwa na hasira nikaitupia simu kwenye maji.
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA 27
ENDELEA.......
.
..
...
....
.....
......Baada ya kuhakikisha kuwa nimeitupa ile simu
hapo ndipo shughuli mpya ilipoanza. Mguu wangu
uliniuma sana mpaka kiuno kikawa kinanibana
kisawasawa. Ilifikia hali kuwa hata natamani yale
maeneo yakatwe nibaki na kidonda kipya ambacho
kinaweza kutibika kuliko hii hali.
Nilikaa takribani masaa kadhaa ambayo yalinifanya
niwaze kuwa wale watu hawawezi kurudi tena.
Kutokana na hilo nilijikokota na kusimama taratibu
ili niangaze kule ambako waliingilia. Nilihisi kuwa
ndio wamenitelekeza pale au vijana wa mjini
wanasema wameniacha mataa. jambo kubwa zaidi
ni wao kutowamini hali ya kutowafahamu. Muda
ulivyozidi kusonga ndipo hali yangu na mimi ilizidi
kuniwia ngumu sana. Lakini nilijikaza ili nifikie lengo
langu. Maisha yangu yamekuwa magumu pia yenye
kupitia misukosuko ya kila siku tangu nimeanza
hadi sasa, na sijui lini nitapata faraja ambayo
itanifanya nijihisi huru kama pale awali.
Kwa mbali ndipo nililiona gari likija yale maeneo
nilijikokota hadi pembezoni kabisa na kujificha ili
nipate uhakika wa kusema wale ni akina nani. Gari
lile lilisogea hadi maeneo yaleyale ambayo mwanzo
lilikuwepo la mwanzo.
Alishuka yule jamaa wa kwanza akiwa na yule
mwingine. Hapo ndipo niliponyanyuka na
kuwasogelea.
"Wee jamaa vipi?".
Waliniuliza.
"Safi tu nilikuwa pale kuwasubiri".
Mmoja wao akarudi ndani ya gari kisha yule
mwingine akanifuata.
"Sikia tumefanikisha jambo moja kati ya yale mawili
ambayo umetuomba kufanya."
Hadi pale kusikia ile kauli nikashukuru sana japo si
kwa ishara ila moyo wangu ulijawa na amani kubwa
tena ya kipekee sana.
"Jambo gani ambalo mmefanikisha?"
Niliwauliza.
"Tumepata lile sanduku tayari", kuhusu hiyo familia
yako tutaendelea kuifuatilia japo nasikia iko
mikononi mwa Salha yule mwanamke ambae
nilikuambia uwe nae makini".
Nilishtuka sana.
"Ina maana Salha alifanya kweli kuiteka familia
yangu?".
"Sas sikia lengo hapa sisi kufika huko ambako
umesema kuna mali nyingi....pia mbona hili
sanduku lako halifunguki ebu fungua tuone".
Walinikabidhi ili nipate kulifungua.
"Mh! Jamani siwafichi tangu hili niwe nalo sijawahi
kulifungua ila huko papo mahali sahihi pa kuweza
kufungua hili dude".
Waliniangalia kana kwamba hawaniamini, ila ukweli
sikuwahi kulifungua kabisa. Ilipita kama dakika
saba tukiwa tunazungumza. Waliniahidi kuwa
watanihakikishia familia yangu itarudi salama lakini
pindi tu nikiwapeleka kule kisiwani.
"Tunachohitaji hapa wewe kutupeleka huko kisiwani
na maswala ya familia yako tutahakikisha inakua
salama kwani huko pia tumemuacha mtu ambae
anashughulikia upatikanaji wa mtoto wako".
Waliniambia.
"Lakini mimi hali yangu sio nzuri maana nashindwa
hata kutembea".
"Kwa nn unashindwa kutembea?"
Nilisimama kisha nikafungua suruali yangu ili
niwaonyeshe.
"Unataka kufanya nini?"
"Ngojeni niwaonyeshe".
Nilifungua kisha niwaonyesha jinsi gani upande wa
tako langu lilivyoharibika.
"Oooh! Pole ilikuwaje nini tatizo.?"
Nilijifikiria sana nikiwaambia ukweli kuhusu kule
tunakotaka kwenda hawatoniamini au laa wataghaili
na leengo langu niwaonyeshe adabu hawa wapuuzi.
"Mambo ya maisha haya kuhangaika nikajikuta
nimekali kitu hatari sana ambacho kimenidhuru".
Niliamua kuwaongopea.
"Sasa tunachukua chakula kwenye gari kisha
tunakula baada ya kumaliza tunakodisha mtumbwi
sisi na wewe hadi huko kisiwani sawa?".
"Sawa..."
Kweli chakula kililetwa pale mboga ilikuwa nyama
ya ng'ombe ambayo wamenunua tokea mjini huko.
Kile chakula kilinishinda kabisa kula yani kwangu
kilikuwa kama shubiri. Ile nyama ilinifanya nijihisi
vibaya kisha niamshe hisia za mwili zilizolala.
Niliacha kula kabisa japo walinishangaa. Si kwamba
njaa sikuwa nayo hapana ila kutokana ile hali
ilinifanya nihisi kuwa kama nakula shubiri ambayo
hata nikibugia kilo ya sukari hakuna kinachofaa.
"Nimeshashiba tayari".
Baada ya kumaliza ndipo nikalala mule ndani ya gari
lao nikisubiri nini kinaendelea. Sasa inabidi tutafute
mvuvi yeyote kule mbali ambae atatusaidia
kutuvusha hadi huko tunakokwenda. Hapo ndipo
akatafutwa mvuvi. Kwangu ilikuwa rahisi sana
kuwajua vijana wa pale ambao wanajihusisha na
masuala ya uvuvi kwa kuwa nimeishi nao kwa muda
mrefu sana kipindi ambacho mimi mwenyewe
nilikuwa bingwa wa kuvua samaki.
Aliletwa kijana mmoja hivi wa makamo.
Wakaelewana nae kisha tukapanda katika chombo
chake kwa ajili ya kuanza safari. Niliwekwa nyuma
kabisa kule ambako nahodha wa chombo kile
alikuwa anakiongoza, pembeni walijipanga wale
jamaa wakiwa wamevaa makoti yao meusi.
Moyoni mwangu nilijua kuwa mambo yanayokwenda
kutokea huku ni mazito japo hawa jamaa hawajui
lakini lengo niwakomeshe tu. Lengo langu lingine ni
kutimiza kwenda kupeleka hili sanduku hadi kule
ambako panatakiwa.
Ninachokumbuka siku ile naanza kuingia ndani ya
kisiwa kile nilikutana na jamaa ambae alinipatia hili
sanduku na akaniambia kuwa ipo siku maisha
yangu yatakuwa magumu na hili likawa msaada
wangu mkubwa sana. Pia nilipata kuota ndoto
nyingine inayofanana na hii kuwa nijitahidi
kufanikisha lile ambalo wale vibwengo au viumbe
wa ajabu wanaamini kuwa naweza kuwasaidia na
hatimae leo nimepata lile sanduku nilupeleke
sehemu husika na mimi maisha yangu yarudi kama
awali.
Mwendo huo ulizidi kuyoyoma na kiza kilianza
kuingia. Ndani ya chombo wote tulikuwa kimya
kabisa kila mooja akifikiria kule aendako kutakuwa
salama au laa. Peke yangu ndio nilikuwa najua
ugumu, urahisi wa kufika huko na changamoto zote
ambazo tunaweza kukutananazo. Taa iliwashwa ili
mwanga upatikane kutokana na kiza ndani ya bahari
hiyo.
Yule kijana aliniuliza.
"Kaka nimepiga kasia mpaka mikono inaniuma hiko
kisiwa kiko wapi?..maana tangu nianze kazi ya uvuvi
sijawahi kusikia kama kuna kisiwa huku".
Aliniuliza swali gumu sana amblo hata mimi
nilishindwa kumjibu kwa wakati. Ndipo wale
wengine wakaingilia.
"Ina maana kijana huku hakuna kisiwa kabisa?"
"Ndio...hakuna huku".
"Oyaa Mnali unatuuza si ndio?"
Waliniangalia huku wakinitwanga maswali.
"Nyie sikieni huyu kijana ni mgeni kwenye hii bahari
mimi ndio nafahamu nimekutana....eheee tena
kileeeee mbele".
Nilifurahi baada ya kuona kisiwa kinaonekana. Kile
kisiwa ni cha maajabu sana muda kinaonekana ila
muda mwingine hakionekani. Basi wakaniamini na
muda si mrefu sana tulikaribia.
Upepo uliovuma sana ulifanya taa kuzima kabisa na
tukawa hatuoni. Tulipokaribia tulikanyaga maji
ambayo yalitufikia kwenye vifua vyetu ila yule kijana
akarudi hakutaka kubaki.
"Jamani mimi nawaacha huku siwezi kubaki maana
hakuna hata kisiwa nilichowahi kusikia kipo".
Ndipo akatuacha sisi tukimaliza yale maji hadi
ufukwe wa kile kisiwa.
Nilikumbuka kuwa wale viumbe wapo kila mahali na
dawa yao ni kuwa ndani ya maji kwani hawajawahi
gusa maji ndio kinga pekee. Sasa tukilala kwenye
mchanga lazima watulambe cha umuhimu kulala
ndani ya maji.
Nilijiuliza nikiwaambia watakubali au wataniamini?...
....
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE 28.
ENDELEA............
.................Ndipo pale nilipoamua kuwaambia
ukweli ili yasije kutokea mapema kabla hata
niliyokwenda nayo pale hayajitimia. "Jamani
naombeni mnisikilize, huku tunakoelekea si kuzuri
kabisa, kwa maana kuwa kuna viumbe vya ajabu
sana". Walinishangaa wakati yule mwingine
alishafika tayari nchi kavu na mimi nikiwa na yule
mwingine tupo ndani ya maji bado. "Kwa nini
unasema hivyo na viumbe gani hao wa ajabu ambao
wanaweza kututishia sisi maisha". Niliona vyema
kuwaeleza kwa kutumia busara kubwa ambayo
ingeweza kunifanikishia mimi yale malengo yangu
muhimu. "Huku kuna viumbe vya hatari sana,
viumbe ambavyo vinapenda kukaa nchi kavu pekee,
lakini ndani ya maji hawawezi kabisa kukanyaga".
"Kwa hiyo?". Aliuliza mmoja wao. "Inachobidi tulale
ndani ya maji mpaka asubuhi au laa tukae ndani ya
maji hadi asubuhi ndipo tutaanza kutoka na
kuwapeleka huko ambako mnataka." Walishtuka
lakini ndipo wakaanza kuongea wao wenyewe.
'Sasa, moris umesikia hayo mambo?" Ndio
nimesikia, lakini mimi sijawahi kutishika kabisa
acha mimi nikae hapa nchi kavu siwezi kulala
kwenye maji kama vipi laleni huko. Yule ambae
alikuwa anajulikana kwa jina la Moris alijifanya
ubishi basi akalala kwenye mchanga na sisi tukakaa
kwenye maji. Usingizi haukuja kabisa kutokana na
yale maji kuwa ya chumvi pia ni ya baridi. Mpaka
majira ya usiku sana maji yalizidi kujaa mpaka
tukashindwa kuvumilia ndipo tukakaa kwenye
mchanga karibu kidogo na yale maji lengo likitokea
la kutokea basi tunakimbilia kwenye maji kiurahisi.
Mpaamajira ya asubuhi yanatimia kila mmoja
alikuwa salama kwa kumuangalia tu kwa mbalimbali
japp hatukuwa na uhakika na kila mwenzake.
Niliwaingiza kwenye kijimsitu kile lengo nitokeze
kwenye lile pango. Aisee kabla hata hatujazama
mbali sana tayari harufu ya wale viumbe ilianza
kupatikana. Moris na mwenzake walianza
kushangaa sana ndipo wakaanza kujihami kwa
kuchukua bastola zao pamoja na visu. Hii ni baada
ya kuona mafuvu ya watu mule msituni. Oyaa ina
maana huku kuna watu ambao walifika na
wakashindwa kurudi?, waliniuliza. Ndio wapo wengi
sana na hawakuweza kurudi kwa sababu ya ubishi
wao kama wenu nyinyi. Walishangaa lakini
haikuwafanya waache zile silaha. Tulitembea kwa
uangalifu mkubwa sana. Mamaaaaaa!. Sauti
iliyosikika nyuma yetu ilitushtua na kutufanya
tugeuke wale tulioweza kugeuka laaaah! Moris
hayupo kwenye upeo wa macho yetu. Hofu ilianza
kutanda na mimi nilifahamu kuwa tayari wale
viumbe wameanza kazi zao. Lakini wale viumbe
hawana nguvu kubwa ya kuwanasa na kiwabeba
watu wakubwa kama sisi. Inakuwaje hili au ni
kiumbe gani huyo?. Yule jamaa alianza kuweuka
pale. Moriss, moriiiiiis. Niliamua kujikokota hadi
pale alipo. Ndugu moris yupo ila usitie kelele
utaleta matatizo makubwa sana tofauti hata na hilo
la kwanza. Ndipo tulitoka lakini akili ya yule jamaa
haikuwa pale kabisa. Safari yangu iliishia kwenye
lile pango ambalo ninatakiwa kuingia ndani yake.
Mnali!, umetuleta huku kuwa kuna masanduku ya
mali sasa yako wapi?, mbona nazidi kuona maajabu
tu mwanzo mwisho?, aliniuliza yule jamaa. Nilivuta
pumzi kisha nikamuangalia, nilijua kabisa ni uongo
na hakuna hizo mali wanazotaka bali tamaa zao tu.
Kaka mali ziko kwenye hili pango., sasa si tuingie
mara moja?....hapana kaka hapa panatakiwa mimi
niingie kwanza, nitengeneze mazingira ya humu
ndani kisha utaweza kuingia. Una maanisha nibaki
nje?, haswaaaaa. Weeeee nani kasema nimemuona
moris anachukuliwa hivihivi alafu mimi uniache huku
nje acha wewe. Wakati tunalumbana ndipo wale
viumbe wakaingia pale tulipo, tukiwashuhudia jinsi
walivyo na hawakuweza kuchelewa kabisa
walimfuata yule jamaa kwa hasira kali. Jambo
lililomfanya ashtuke na kuanza kukimbia ovyo mule
msituni. Ajabu mimi walikuwa wananipita kama
hawanijui. Hapohapo mlango wa lile pango
ukafunguka. Nikaingia na lile sanduku langu hadi
karibia lile eneo ambalo linapatikana kuwepo mahali
pa kutolea mwanga maalumu. Kwa kuwa nilikuwa
na haraka sana nikajikuta nafungua boksi kwa
urahisi hali liliwashinda watu wengi sana.
Nikakutana na kipande cha almasi kinachong'aa
sana. Kabla sijachukua ndipo mawazo ya upande wa
pili yananijia yaliyo kama ndoto hivi. "Fanya haraka
sana, kuweka hilo jiwe mahali husika kabla
hujazalisha milki yenye roho chafu." nilishangaa
kusikia ile kauli kuwa niwahi kuweka lile jiwe mahali
husika yani kabla hata sijazalisha milki yenye roho
chafu. roho chafu ipi hiyo ambayo ilikuwa
inaongelewa. nilifananisha yale maongezi na yale ya
kwanza kabisa ambayo siku nafika humu nilipata
kuyasikia. nilichukua lile jiwe kazi sasa ikawa
natafuta lile eneo mahali pake. lakini hofu kubwa
ilikuwa kutofahamu wapi ambapo wale wengine
wamekwenda. nilitembea taratibutaratibu sana kwa
hofu ya hali ya juu. mpaka pale ambapo niliona
kuwa kuna dalili ya mwanga kutoa kama ile awamu
ya kwanza kufika hapa. nilifurahi sana kwa kuhisi
kuwa tayari maisha yangu yatarudi kama mwanzo
na kuachana na mitihani hii ya kila siku. lakini chini
nilipokuwa nakanyaga kulikuwa na miili ya viumbe
vingi ambavyo vilikuwa vinatoa harufu nzito yenye
kunuka sana kiasi kwamba nikawa nashindwa hata
kupumua vyema kama awali nilipoingia. kadri muda
ulivyozidi kusonga ndipo harufu kali ilizidi kuenea
mule ndani. lakini nashukuru sana kutokana na
ujasiri nilionao na maisha magumu niliyonayo
nilijitahidi kuvumilia sana hadi kuifikia na kuanza
kulinganisha lile jiwe hadi yale maeneo.
nilipofanikiwa kuliweka nilisikia kama kitu
kinagonga masikioni mwangu yani ukelele mkubwa
sana. ukelele huo sikufahamu ulikuwa na maana
gani ndipo niliporudi kinyumenyume hadi pale
ambapo palikuwa na lile sanduku langu lakini kila
nikipapasa nashindwa kulifikia kutokana na
mitetemo niliyonayo kwenye mwili wangu. ghafla
bin vuuup! lile eneo lilitoa mwanga wa kila aina
kisha kama kitu kinajifunga hivi alafu makelele ya
makofi na vifijo vikirindima. hapo ndipo nikasikia
kama watu wanaongea huko nje ya pango. nikaanza
kutoka taratibu taratibu hadi nje lakino sikupata
kusikia zile kelele. jambo lingine la ajavu ni pale
nguvu nilipozikosa hata za kusimama maana
nilianza kulegea kama mlenda, viungo vyangu
havifanyi kazi kabisa na nikawa mbele sioni vizuri
mpaka pale nilipopatwa na usingizi mzito.
nakumbuka nilikuja kuzinduka toka usingizi baada
ya kutoka kwenye ndoto kali ambayo ilikuwa
inahusiana na kuonana na yule jamaa ambae
mwanzo alinichukuaga na kunitibia. aliniambia kuwa
hongera sana kwani umefanikisha lengo letu ndani
ya kisiwa hiki kufukuza hawa viumbe ambao
walikishikilia kwa muda mrefu sana. lakini tatizo ni
moja ambalo umezalisha. tatizo lenyewe kuwa bado
ndugu zako watapata tabu sana kwa.... " hapo
ndipo nikaamka toka kwenye njozi hiyo.
nikasimama niko kamili kabisa alafu nipo ufukweni
nani kanileta sifahamu. niliamua kuita mmoja
mmoja kati ya wale wawili ambao walipotea mbele
yangu kila mmoja. japo nia yangu ni kuwaonyesha
lakini huruma kama mwanadamu ilinijia. nilianza
kuwatafuta. kwa bahati nzuri kwa mbali namuona
morisi ambae alikuwa kasimama ananiangalia akiwa
kwa mbali. kila nilipojitahidi kumfuata alizidi kuingia
msituni. nilikaribia pale ghafla nilipigwa kofi takatifu
la nyuma ya kichwa mpaka nikazunguka kama mara
mbili hivi na kudondoka chini. nilishindwa
kujifahamu vyema maana netweki ilikata kabiasa.
mala ghafla niliona kitu kinanipita nyuma yangu kwa
kasi sana hata sikupata hata nafasi ya kujua ni kitu
gani. ndipo niliona mambo si mambo baada ya
kona mauzauza yanazidi nilikimbia hadi kwenye
maji lakini hapakuwa na hata mtumbwi wala mtu
ambae yupo karibu anaweza kunisaidia. kelele za
kutisha zilianza kwenye kile kisiwa mpaka miti
ikaanza kutikisika kama mtu anaitikisa. sauti zenye
kupishana zilizoambatana na mwangwi mzito sana.
hofu yangu ilitanda baada ya kuhisi kuwa kuna
mnyama au mtu anakuja karibu yangu lakini
haonekani ila hatua zake kwenye mchanga naziona
kama anatembea anakuja mbele yangu. sikujua ni
nini kwa kweli... hahaaaaa haaaaah! ziliendelea
kusikia huku zikizunguka karibu yangu alafu
mngurumo mkubwa sana. jasho lilinitoka huku
nikiomba mungu anisaidie kuushinda mtihani huu.
nikiwa kwenye maji pale kwenye mchanga naona
kabisa nyayo zinazunguka ila wenyewe
hawaonekani. nilijiangalia kwenye sehemu yangu
ambayo nilipata tatizo halikuwepo kabisa. ilipita
dakika kadhaa ukimya ulitawala kumbe kuna
mtumbwi kwa mbali unakuja. nilipiga kelele ili aje
kunisaidia nilishukuru kuwa alinisikia ndipo
nikafanikiwa kupanda na kumuomba afanye haraka
sana kutoka yale maeneo. lakini ajabu zaidi ni pale
tupo mbali na ufukwe wa kile kisiwa tukiwa ndani ya
mtumbwi ule sauti ilijitokeza ya mngurumo mkubwa
kama ule wa awali. nikajiuliza nausikia mimi tu au
wote. nilimuuliza na yeye alikuwa hafahamu wala
hata kusikia hakusikia. moyo wangu uliishiwa nguvu
baada ya kuhisi lile jambo. mpaka tunashuka
kwenye ufukwe ule ambao nilikuwa nautumia
zamani na akina manyota. sauti ilikuwa karibu na
mimi. watu walionifahamu walikuja karibu na
kunishangaa lakini ajabu pale mmoja wao alipotaka
kunishika kwa mshangao alio nao lakini alisukumwa
na kitu asichokijua na hata mimi nilikuwa
sikifahamu.
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA 29
ENDELEA...........
.................Baadhi ya wengi walionifahamu walitoa
chozi kwani walinihitaji kwa kipindi kirefu.
Haikutosha lakini pia hata wale watu ambao
nilikuwa nawauzia samaki walinipenda sana kwa
kunikumbuka. Ndipo mmoja wa vijana aliyejitokeza
mbele yangu akahitaji kunichukua na kunipeleka
nyumbani kwake kwa lengo la kunisitiri kwanza.
Nilimshukuru na tukaanza kusonga mbele kuelekea
kwake. Akili yangu ilijawa na wasiwasi mkubwa
sana ambao haukuwa na mfano wake. Kilichonijaza
wasiwasi ni kile ambacho nilikuwa nakisikia kila
muda niendako sauti mbaya, mbovu pia inanitisha
kujua nipo nayo kila ninakokwenda. Yule kijana
alinishangaa kuona nageuka mbele, nyuma na
pembeni. Kila aliyeniona alinishangaa na
kuninyooshea kidole kwa mshangao. Ni kweli
lazima wafanye hivyo kwa kuwa ni mambo
yasiyoweza kuwezekana kabisa. Wakati nafika
nyumbani kwa yule kijana ile sauti ilisikika kwa
mbali kama nimeiacha. Nilishukuru mungu kwa
kunisaidia kuachana na majanga kama yale.
Niliingia ndani na kisha kijana huyo aliyejulikana
kwa jina la Mshana, alipika ugali pamoja na nyama.
Nilijihisi vibaya sana kuona ile nyama maana
mafikirio yangu ni kutudia ile hali ya kupenda nyama
mbichi. Nilianza kula bila kuwa na mashaka yeyote
na hapakuwa na mabadiliko yeyote yale. Nilizidi
kufurahi moyoni mwangu. Masha nilimshukuru sana
kwani sikuwa na hata sehemu ambayo ningeweza
kujisitiri. Kijana nakushukuru sana..' nilimsemeza
Mshana, aliyeonekana kutabasamu. Hapana
usinishukuru hivyo maana hili ni kama jukumu langu
kukusaidia kwani nina jambo ninalihitaji kutoka
kwako...'alinishangaza kidogo. Eheee! Mshana
jambo gani tena...'usiwe na shaka nahitaji
unifundishe Uvuvi bwana nataka kujua hiyo
kazi..'nilimsikikitikia sana na nikamuambia ukweli
kuwa si kazi nzuri kwenye maisha yake bora atafute
vibarua vingine. Baada ya kumaliza nilihitajika
kwenda kuonana na kiongozi wa mtaa ambao
nilikuwa naishi maana nina kesi hiyo ambayo
natakiwa kwenda kujibu nilipotea kwa mazingara
gani. Kabla hata hatujatoka nje baada ya kumaliza
kula tulisikia sauti ya mtu akidondoka kama gunia
na sauti ya malalamiko. "...Mamaaa nakufaaa....Tii
iii". Mh! Kila mmoja mule ndani alishtuka sana
ndipo tukakurupuka ndipo tukamshuhudia mama
mmoja akitokwa na damu mdomoni. Tulishangaa
kiukweli kwani hakuna mtu anaefahamu kwa hili
lililotokea. Mnali kuna nini tena kimetokea?.
Unaniuliza mimi wakati wote tunashangaa. Mshana
alitoka hadi pale na kutaka kumnyanyua nikatoka
kwenda kumsaidia nakaribia pale walipo kwani
walikuwa mbali kidogo na mlango "..ngraaa!!
Khaaaahkhaaaa..ng'raaaa ng'raaaa.." nilishtuka
kuisikia ile sauti tena ikiwa yale maeneo. Mnaliiiii
njo tumsaidie huyu mamaaa atakufa hapa jamani
angalia damu zinamtoka kwa kasi..". Mshana
aliniita. Niliogopa hata kusogea kwani ile sauti
ilinijia hadi pale nilipo na ikaja karibu kabisa ila
sihisi kama mtu kanigusa hapana. Nilikimbilia hadi
pale na kujaribu kumshika miguu laaa haulaa!.
Nilipata kumuona Mshana akilalama kwa maumivu
ya mgongo na kulala chini huku akilia. Nilishindwa
nianze na yupi pale kumsaidia. Ndipo nikaomba
msaada Kwa majirani waliokaribu. Watu baadhi
walifika ndipo walipelekwa hospitali. Lakini kwa
muda ule mfupi tayari taarifa zangu zilishatambaa
kuwa nipo mzima kabisa. Nikiwa natafakari kipo
kipo nyuma ya pazia akili yangu ilichoka kutafuta
majibu ambayo hayapo kabisa. Ni kitu gani
ambacho kinafanya haya mambo kiasi nikawa
najiogopa hata mimi mwenyewe. Niliwakumbuka
vijana wenzangu ambao kipindi cha nyuma tuliweza
kuvua samaki kwa pamoja. Hapo ndipo wazo la
kuelekea maeneo ambako anapatikana kiongozi wa
mtaa. Ilipita miezi kama mitatu hivi jambo hili
likiniumiza kichwa. Siku moja nikiwa kwenye
mizunguko yangu nilifanikiwa kuona televisheni
ambayo ilikuwa inaonyesha kipindi cha watoto.
Nilisimama kidogo baada ya kusikia sauti ambayo
nilikuwa naifananisha na mwanangu Asante. Ama
kweli damu ni nzito kuliko hata maji mwanangu
Asante akiwa mbele ya umati anaongea lugha ya
kizungu, nilijisikia faraja jambo la kwanza kuona
kumbe mwanangu mzima na ninaweza kumpata.
Hapo nilikimbia safari ya kwenda nyumbani kwa
Mshana huku nikiwa na furaha tele, lakini kila hatua
ninayopiga nasikia kitu kama kina hema nacho
kinakimbia karibu na masikio yangu. Nikasimama
kusikiliza, ng'raaaaah!, ng'raaah. Nilipatwa na uwoga
nikakimbia hadi kwa Mshana ambae aliponiona
akataka kukimbia na yeye. Mshana...nimemuona
mwanangu nataka nikamfuate.nilimueleza mshana.
Khaaa basi habari nzuri hiyo ila mbona una kimbia?.
Daah! Weee acha tu tuingie ndani kwanza.
Tulipoingia ndani ile sauti sikuisikia tena. Mshana
mimi nina tatizo kubwa sana hadi sasa na sijui
nalitatuaje. Mh! Lipi tena hilo?. Mshana aliniuliza.
Ndugu yangu kuna kiumbe ambacho kipo karibu
yangu laiti ungewahi kukisikia maana si kukiona
kwani hata mm sijawahi naamini ungenielewa nini
namaanisha. Pole sana Mnali kwa maisha ya
misukosuko unayopitia..sasa unataka nikushauri
kitu gani. Mh! Nilipumua kidogo kisha
nikamuambia. Nishauri jambo lolote ambalo naweza
kuondokana na hili tatizo. Sawa mnali nakushauri
katafute fedha baharini yani fanya kazi ya uvuvi tena
ukipata ela njoo nikushauri nini cha kufanya.
Alinishangaza sana. Yani nipate ela alafu unishauri
ila haina shida kesho nitaenda mtungo mmoja tu
nazoa samaki wengi alafu napata ela utaniambia
nafanyaje. Basi tuliachana pale mimi nikabaki
mulemule ndani. Yani hiki kiumbe ndani hakiingi
nikitoka tu naongozana nacho na tatizo hakionekani
na kwa jinsi msauti wake ulivyokuwa mbaya
naamini angekuwepo yeye mwenyewe au kuonekana
nahisi ningezimia.
 
SEHEMU YA THELATHINI 30
ENDELEA.......
................Nakumbuka ilikuwa siku ambayo
nilipanga niende kuanza rasmi kazi ya uvuvi tena ili
niweze kupata kiasi ambacho kitanisaidia kutafuta
familia yangu. Lakini asubuhi hiyo wakati naelekea
pwani niliwaona watu wakikimbilia maeneo hayo.
Nilishikwa na mshangao ikabidi na mimi niwahi
kujua kuna jambo gani. Nilipata kumuuliza mmoja
wa wale wanaoelekea huko. Ndugu habari
yako..Salama vipi?, eti huko kuna jambo gani
mbona watu wengi wanakimbilia huko?. Haah!
Ndugu kuna watu watatu wamekufa wamekutwa nchi
kavi wamekufa ila kilichowauwa hakifahamiki. Mh
nilishtuka sana. Tulifuatana njianibkuelekea huko.
Ghafla ile sauti ya mngurumo karibu yangu ikanijia
naisikia sana inanguruma, ilinichukiza sana na hadi
ikanifanya safari yangu iwe nzito. Nilimuambia yule
jamaa basi atangulie tu. "Ndugu basi wewe tangulia
tu nitakukuta, vipi kuna shida, hapana ila nenda tu
basi. Nilimuacha aende ili yasije kutokea mengine
tena. Tulipofika kule kweli tuliwakuta polisi wakiwa
wamezunguka na kulinda mazingira yale.
Nilichoshukuru baadhi ya watu wengi walielewa
mustakabari wa maisha yangu hivyo wengi wao
hawakuwa wabishi sana kunielewa. Alitokea askari
mmoja na kutangaza kuwa kuanzia muda ule hakuna
shughuli yeyote ya uvuvi inayotakiwa kufanyika
mpaka pale watakapohakikisha usalama upo.
Baadhi ya watu kama sisi tunaotegemea maisha
yetu baharini tuliona kazi nzito kwani vipato vyetu
vinapatikana humo. Nikiwa naanda nyavu zangu na
mtumbwi wa kuazima kwa ajili ya kazi yangu ya
jioni. Nikiwa kwenye hatua ya kumalizia nashtushwa
na kicheko cha mtu akiwa mbele yangu. Hakuwa
mwingine bali ni bwana Manyota. ..haaahaa!..
aaaaaah! Aisee maisha kweli yanabadilika...wewe
hujafa mpaka sasa". Nilimuangalia na kujua kuwa
huyu alihitaji mimi nife. Kwa nini ulihitaji
nife?....kwa sababu kuwepo kwako kuna madhara
sana kwetu na hili nitalishughulikia mpaka unazama
chini ya ardhi kama nduguyo kibona...".
Nilimuangalia kwa jazba sana. Jamani nimewaacha
muishi mtakavyo ili nipate muda na nafasi ya kuja
kuishi na amani kama ya mwanzo, maisha magumu
niliyopitia leo hii sitaki niyakumbuke kupitia wewe.
Alicheka sana. Sawa mnali ila kumbuka kuwa huna
uwezo tena wa kuchukua samaki wengi kama
mwanzo na wakakusifia huna huo uwezo kabisa.
Nilimuitikia kwa kumuambia kuwa ndio sina ila pale
nafanya ili nipate hata ya mboga ingawa polisi
wamekataza kuvua samaki. Manyota alionyesha
kunipinga sana kwa kuwa maisha yake ni mazuri
sana tofauti na mimi. Niliona kubishana na huyu ni
tatizo niliondoka na kuhifadhi zile nyavu kwenye ule
mtumbwi na kuelekea mbali kidogo mala ghafla
askari wakauona ule mtumbwi na kuuvamia kutaka
kuuchima moto. Nilikimbilia hadi pale. Jambo
ambalo nilianza kupewa kipigo kwa kosa la kutaka
kuvua. Sisi tumekataza kuvua samaki kutokana na
haya matatizo wewe unajiandaa kwenda kuvua
pumbavu, nilimuambia askari kuwa kunipiga si ndio
kutanipatia shida yangu mimi niliyejia pale hapana
ila shida yangu ni kufanikisha kile ambacho
nakihitaji. Mpaka maijra fulani hivi waliniacha
nifanye kile ambacho nakitaka basi na mimi sikuwa
na ajizi
Baada ya kupata nafasi ile sikutaka kuchelewa
kabisa ndipo nilielekea kule ambako upo mtumbwi
wangu kisha nikauweka tayari kwa kazi husika. Kwa
kuwa ilikuwa ni jioni basi nilielekea sehemu zile
wanazouza samaki wa kuchomwa na mafuta
nilwakuta akina mama wengi ambao wananifaha
kuwa mimi ni mtabe kwenye mambo yale ya uvuvi.
Baadhi waliniuliza lini naanza kazi ya uvuvi. Niliona
ndio nafasi pekee ya mimi kukamata ela. Nilichukua
oda pamoja na kukusanya ela za kotosha nikiwa na
imani kuwa narudi na mzigo wa kutosha. Hapo
nilikamata kama laki na kitu nilielekea kwa Mshana
ambae nilimkabidhi kama kuhifadhi wakati mimi
naelekea ndani ya maji. majira ya usiku tayari
nilielekea na kuanza safari ya kuingia ndani ya maji.
Nilifurahi kuona napata kile ambacho nakitafuta
kwani mpaka narudi samaki walikuwa wengi ila
nikiwa ndani ya maji kufika ufukweni nahisi kama
kitu cha harufu ya samaki yani damu yake. Alafu
kama kuna kitu kinakula nyuma yangu. Nakuja
kutahamaki ile sauti iliyozidi kunguruma ikiwa na
mimi inatafuna samaki wangu wote. Nilishindwa
kuamini kama kweli naona damu zinatapakaa tu
hakuna hata samaki wale wakubwa niliowaamini
napata fedha za kutosha, hakika nilichukizwa sana.
Sikuwa na jinsi alfajiri wale wahusika niliwapa japo
hawakufurahia na kile ambacho walikiona ila
waliniheshimu tu. Na mimi nikaondoka hadi kwa
mshana nikamueleza kila kitu. "Mnali, inabidi tuende
kwa mganga ili ukatibiwe siku hilo dude likikosa
chakula litakukula wewe". Hakika maelezo yake
yalinijaza imani ya kuwa kweli inawezekana ikawa
vile asemavyo Mshana. Mchana huohuo taarifa
kuwa baharini wameonekana viumbe viwili vya ajabu
na wamesababisha mauaji kwa watu wawili kisha
wakatokomea. Sasa baharini kumechafuka hakuna
siku ambayo hakuna taarifa kama hizi. Tukiwa
tumepumzika sauti ya gari ilisikika ikipiga breki
tulichungulia mlangoni hatukuwafahamu watu ambao
walishuka na kuhitaji kuingia ndani. Tulitoka
nilishangaa kuwaona Salha na bwana paul wakiwa
na Manyota na musa. Nilimnong'oneza Mshana
kuwa aingie ndani haraka, alifanya hivyo. Walihitaji
wanibebe ila nilikataa jambo hilo liliwafanya
Manyota na musa kupata vipigo wasivyovitegemea
kutoka kwa mtu asiejulikana na kuwafanya wawe
hoi na kukimbizana na kuondoka. Mr Paul alibaki na
mshangao maana vipigo walivyopigwa si vya kitoto.
Damu ziliwadondoka, mimi pekee ndio nilikuwa
nafahamu nini kimewadhibu vile. Nilimuita Mshana
huku nikimuambia kwa sauti kuwa tuelekee kule
kwa mganga. Aise tulipigwa wote mimi na Mshana
na nusura yetu tulipoingia ndani daa! Nifanye nini
kuondokana na haya?.
 
SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA (XXXI) 31
Endelea.......
.............Tulibaki kushangaana mule ndani hali kila
mmoja ana maumivu yake. Kwa upande wa Mshana
alichukia sana kuhusu kile kitendo kwa kuwa
anafahamu nini kimefanyika.
Ghafla nje tunasikia watu wakikimbizana ovyo na
wengine wakiwa wanalia moja kwa moja tulijua
kuwa lile lijitu limeanza kuua watu. Kumbe haikuwa
kama vile ambavyo tumefikilia ilikuwa ni tofauti
kabisa.
Mimi na Mshana tulitoka taratiibu na kuelekea nje ili
tukaangalie nini kimetokea.
"Mshana.."
"Eeeh!"
"Unajua tufanye nini hapa.."
"Nakusikiliza Mnali"
"Inabidi tufute kwanza mawazo ya kwenda kwa
mganga kwanza tuwaze mengine kabisa alafu
baadae inawezekama tukawaza hilo na tukaenda
kabisa".
Alikubali wazo langu japo ni ngumu kuacha kuwaza
jambo ambalo lipo kichwani mwa mtu alafu
umuambie kuwa asijaribu kabisa kuwaza ni jambo
la ajabu. Tulipotoka nje tukawaona watu kadhaa
wanakimbia ndipo walipofika pale tulipo na kuanza
kuhema kwa harakaharaka sana. "Nini tatizo
niliwauliza".
"Jamanii baharini kuna matatizo"
"Matatizo gani tena".
"Mudaa huu huu watu watatu wamekufa kwenye
maji...alafu kama kuna viumbe wameonekana
wawili wakizama na kupotea kabisa".
Nilishika kichwa changu pale huku nikiwaza nini
tena hiki kinakuja kukumba sehemu muhimu ya
kuingiza kipato changu. "Sasa mmefanya nini
huko?".
"Watu wamejaa sana na sisi tunakimbia maana
polisi wanaingia sasa hivi".
Pale niliona kuwa kutokana na yale maisha nisije
kumpa tabu yule rafiki yangu bora hata nitafute
sehemu ya peke yangu nikae. Nikiwa nawaza hilo
nilirudi ndani baada ya kuhakikisha kuwa hata ile
sauti sijaisikia tena. Kipindi hiki nilikuwa nimepona
kabisa sina hata tatizo lolote mwilini kwangu, zaidi
ya hili janga jingine.
Usiku tukiwa tumelala. Niliota ndoto ya ajabu yenye
kunitishia maisha yangu. Niliota kuwa kuna watu
wawili wametoka kwenye kina kirefu cha bahari na
kuingia nchi kavu wakinitafuta mimi ili waje
kunimaliza na walikuwa na hasira sana pia
wakasema kuwa muda si mrefu wanakuja baada ya
kumaliza damu changa.
Ile ndoto ilinitisha kiukweli.
Ilikuwa majira ya usiku sikujua saa ngapi kwa kuwa
sikuwa na saa. Kelele za gari nilizisikia hapo nje
zikipitapita. Tulitulia kimya wote bila hata
kujinyoosha hata kama mbu walikuwa wanagonga
kwa kiasi gani. mpaka inafika asubuhi tulitoka huku
nikiwa na shaka kwa kuwa nilijua labda wale ambao
wananifuata sana. Nilimuambia Mshana kuwa hawa
watu walikuwa wananijia mimi hapa. Ikiqa mawazo
yangu ni kuondoka pale kwa bwana Mshana kwa
kuhofia majanga ambayo yatakayotokea mbeleni.
nilianza kusikiliza kama ile sauti ya yule kiumbe
kipp karibu nilihisi kuwa hayupo karibu yetu hapo
ndipo nikamsogelea Mshana.
"Mshana ndugu yangu"
"Ndio niambie mnali"
"Unajua kuwa hizi tairi ni za gari na pia zilikuwa
zinakuja kunifuatilia mimi hapa"
"Ni kweli naona si ndio lile lililokuwa linanguruma
majira ya asubuhi"
"Ndio kabisa na nahisi Kuwa kiumbe kinachonifuata
ndicho kinaua watu huko baharini.."
"Kwa nini unasema hivyo mnali? "
"Unakumbuka Kuwa ile siku nimeenda kuvua samaki
wale samaki waliliwa na lile jitu sasa nahisi
linapenda sana nyama mbichi ndio maana nasema
hivyo".
"duu! Mnali sasa tunafanyaje kuhusu hili?"
"Mawazo yangu mimi niache niondoke nikatafute
maisha yangu kule kijijini ambako Mke wa Kibona
anaishi kabla ya kwenda kwetu kama mtoto najua
ipo siku atanifuata tu".
Mshana alinishangaa sana kwa ile kauli ambayo
nilikuwa naiongea pale kisha akanishika mkono na
kunivuta.
"Unajua mnali tufanye jambo moja hivi kwamba...
ngoja nifunge mlango". Alienda kufunga mlango
huku nikimshangaa anataka kufanya nini. baada ya
kumaliza alinijia hadi pale nilipo kisha akaniangalia.
"Mnali unafikiri kuwa ni rahisi kuzungumza tu.
unamuachia nani familia yako badala ya kuifuatilia
na ujue wapi imeelekea au imehifadhiwa wapi eti
unataka kukimbia".
nilibaki kuduwaa tu pale kwa kuwa sikuwa na hata
ujanja wa kusema kwani ni kweli kabisa kwa kile
ambacho anakisema mshana. mimi kama baba wa
familia sina budi kupambana na kuhakikisha kuwa
familia yangu naiweka kwenye himaya yangu.
Alinishika mkono na kunivuta huku tukitoka pale
ambapo tulisimama. Nilimuomba tukae kidogo ili
tuweze kuongea kirefu kuhusiana na jinsi gank
naweza kuipata familia yangu. tulikaa kwenye
benchi lililopo karibu na pale tulipo.
"Mshana unajua kuwa kuna watu ndugu zangu na
marafiki zangu wa karibu sana wananifuatilia sana
mimi hadi hapa nilipo"
"Kwa nini na akina nani hao wanaokufuatilia wewe"
"Mshana wewe ni rafiki ambae unaonyesha moyo
wa kunisaidia lakini usije kuwa kama hawa wawili..
Manyota na Musa ambao wameamua kunisaliti na
kutaka kuniua kwa kuwa walitamani kuwa na mali
nyingi kutoka kwa mzee Paul ambae alinihitaji
kunitumia mimi kwa faida yake, pia nikajikuta kuwa
naingia kwa watu wabaya kama Salha pamoja na
kundi la wauzaji wa madawa ya kulevya wa bwana
Paul. hadi sasa nahisi kuwa baharini nina majanga
mengi nako ndiko natarajia kupata kipato changu,
pia mke wangu kachukuliwa na watu wenye ela. na
sijui mwanangu anaishi vipi, tena huko kisiwani
nimeishi kwa shida mpaka sasa unavyoona nafuu
yangu nilikuwa na ugonjwa mkubwa sana wa kuoza
tako hili ila mpaka nimepona mungu mwenyewe
anajua ndugu yangu. "
Machozi yalikuwa yananitoka na Mshana akawa
ananionea huruma sana ndipo akasimama na
akanishika mkono tena. Akawa ananivuta huku
akinilazimisha kuondoka bila hata kusema wapi
tunaelekea.
"Vipi unanipeleka wapi sasa"
"Mnali nifuate mimi najua familia yako iko utaipata
vipi na haya matatizo yako yataisha haraka sana".
Nilishangaa sana kusikia kwamba anataka
kuniambia anajua familia yangu naipata vipi.
tulikimbia kwa kuwa yeye muongozaji alikuwa
anakimbia na mimi nilimfuata.
tulifika mpaka maenwo fulani ya mapori kabisa
kama tunaelekea njia ya kwenda vijijini. nilisimama
na kumuaomba kitu. "Mshana tunaelekea wapi
lakini? ". "weee twende Mnali huku ndiko msaada
wako uliko fanya haraka kaza mguu". Akiwa
anasema hivyo ghafla na mimi nasikia sauti
ambayo peke yangu ndio naweza kuisikia na sauti
hiyo ya yule kiumbe akiwa anakimbia. alikuwa kwa
mbali sana akiwa anatukimbilia na kwa kujua
akitukuta hapa lazima tusage meno. nilimgeukia
Mshana "mshana yule kiumbe anakujaa
anatukimbilia huku tuliko namsikia.. "
"Mnaliiiiii unashangaa nini sasa tumefika
tukimbieeeew asitukute bwanaaaaa.... ". Daaaaa
tulikimbia kwa kasi kubwa sana mimi nikiwa sijui
wapi naelekea ila Mshana ndie anafahamu.
 
SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI 32
ENDELEA………………………
……………Mshana alinilazimisha nikimbie baada ya
kumueleza kuwa yule kiumbe anakuja kwa kasi ya
ajabu sana. Ndipo niliungana nay eye kumfuata kule
ambako anaelekea. Tulitumia nguvu nyingi sana
katika kuhakikisha kuwa yule kiumbe hatukuti.
Lakini cha ajabu Zaidi alikuwa ana hema karibu
yangu hata kila ninapojaribu kuongeza spidi ni kama
nakimbizana na chombo cha moto kama vile
pikipiki ama gari maana nilizidi kuchoka mimi tu.
Tulipofika mbele Zaidi kulikuwa na njia pacha
ambazo ziliweza kutuchanganya kwa kweli, ghafla
tulisimama pale tukihangaika huku hatufahamu wapi
tunaelekea, Mshana alinihoji kujua kama yule
kiumbe anakuja ama laa!.
“Mnali vipi anakuja huyo kiumbe unamsikiaaa?”
Aliniuliza Mshana.
“Hapana simsikii kabisa kwa sasa ehee wapi
tunaelekea?”
“Eheee huku hapa twende haraka”.
Tulisonga mbele lakini jambo ambalo lilinishangaa
ni kwa kutosikia sauti ya yule kiumbe tena.
Tuliendelea kukimbia hadi eneo Fulani lenye miti
mingi sana alafu kupo na kiza nene.
Maeneo hayo Mshana alisimama na kuniangalia
kisha akasema jambo Fulani kuhashiria kuwa
tumefika. Tulipunguza mwendo tukaanza kutembea
mwendo mdogomdogo sana.
“Mnali sikia kwanza”
Nilsimama kumsikiliza anataka kuniambia nini
“Unasikia tumefika unatakiwa kuvua viatu vyako
mpaka tunafika kule sehemu husika sawa fanya
hivyo sasa”.
Nilimshangaa kuwa nivue viatu na kwa kuwa sikuwa
na sauti pale nay eye ndie anapafahamu pale na
sikuweza kumtilia shaka kuwa atanifanyia unyama
ndani ya pori lile. Nilivua viatu kisha tukaanza
kutembea peku japo miba zilitusurubu sana.
“Mshana..huku wapi tena”.
“Tukifika ndipo utafahamu ni wapi wewe nifuate
mimi tu”.
Sikuwa na neno jingine Zaidi ya kuvumilia maumivu
ambayo nilikuwa nayapata kutokana na zile miba
kali, wasiwasi wangu pale ulikuwa kwa yule kiumbe
ambae alikuwa nyuma yangu japo sikuwa namsikia
lakini nilihofia sana endapo akiwa karibu yangu.
Tulitumia ndani ya dakika kama nne kutoka pale
tulipovua viatu hadi eneo Fulani kwenye kibanda
kimoja hivi hapo ndipo Mshana akaniambia kuwa
tmefika. Hapakuwa na mtu kabisa na pia eneo
lilikuwa linatishia sana kwa kukaa mtu.
“Mnali hapa sasa tumefika tayari”.
Aliniambia Mshana, kitu ambacho kilifanya
nimuulize swali
“Hapa wapi”
Huku nikimkodolea macho kama mtu aliyebanwa na
mlango.
“Sikia hapa ni kwa mganga tulipo..”
“Khaaa! Mshana kwa nini hukuniandaa kutoka kule
nyumbani uniambie huku eeeh!”
Nilimlaumu sana kwa kile kitendo ambacho alikuwa
amekifanya cha kunipeleka kwa mganga bila hata
mimi kunitaarifu kwanza.
“Mnali unajua kuwa mwanzo tuliliwaza swala la
kwenda kwa mganga yakatukuta yapi na tuliyapanga
yapi baada yay ale”.
“Hata kama lakini…….”
“Ahaaa! Kwa hiyo mnali leo nimejitolea japo na
mambo yote ya ajabu yanayotokea lakini leo
unanifanya kuwa mimi mjinga sana haya twende
turudi nyumbani”.
Mshana alikasirika na ninavyomjua rafiki huyu
hachelewagi kununa. Nilimkubalia na kumfanya
kama ulikuwa ni utani na namshukuru sana.
“Mnali acha utani tupo sehemu hatari hizi na wewe
mwenyewe ndio ulisema kuwa tufute mawazo ya
kwenda kwa mganga ili yule kiumbe kisijue na
kikatufanyia mabaya hapa”.
“sawa basi twende huko haraka”.
Tulisogea hadi pale kibandani ambapo
palitengenezwa kwa miti na udongo kwa chini kisha
pakafunikwa kwa kaniki zenye rangi nyekundu na
nyeusi. Eneo hilo lilikuwa linatishia sana.
Maana mambo mengi yalikuwa ya kutisha sana
tunguli nyingi pamoja na mafuvu ya wanyama
pamoja na ngozi za wanyama baadhi. Niliogopa
sana baada ya kuona yale mambo kwa kuwa
sikuwahi kuja kabisa haya maeneo.
“Mshana sasa mwenyewe yuko wapi sasa”.
“Ngoja atakuja sasa hivi…..”
Kabla hata hajamalizia sentensi ambayo alihitaji
kusema tulisikia sauti ambazo zilisambaa yale
maeneo. Sauti zenyewe zilikuwa za kicheko kikali
sana tulihangaika kutafuta mwenyewe yuko wapi
lakini hatukuweza kufanikiwa kumuona, ndipo ghafla
anaonekana mzee mmoja kwenye kile kibanda
akiwa amevalia nguo nyekundu pamoja na kilemba
chekundu.
“Hahaaaa! Vijanaaaa karibuni sanaaa…”
Tulikaa pale ambapo alisema kuwa tukae.
aliendelea kuongea lugha yake ya ajabu ambayo
sikuweza kuifahamu kisha akaniangalia na
kuendelea kucheka tena.
Tulibaki kuangaliana tu pale ndipo akachukua
Kibuyu kimoaja kisha akanipatia kwa kunielekezea
mimi ili nikichukue. Nilikuwa na wasiwasi kiukweli
lakini rafiki yangu Mshana alinisihi nisiogope.
Baada ya kukichukua na kukiweka mkononi ndipo
yule mzee akaanza kwa kuimba nyimbo zake huku
akiniangalia na kupiga chafya kali sana kama mtu
mgonjwa wa chafya.
“Kijanaa shika hiko kibuyu….”.
Nilikishika barabara.
“haya kinuse hiko kibuyu kisha pumulia mara tatu”.
Nilikinusa kisha nikapumulia kama alivyohitaji mara
tatu. Baada ya kumaliza ndipo akakichukua kisha
akakinusa nay eye akavutia hewa yake ndani kama
mara tatu.
“Kijanaaa…wewe ni shujaa si ndioo”.
Tulibaki kuangaliana tu pale kuwa mimi ni shujaa
tangu lini.
“Babuu hapana bwanaaa mimi si shujaa kabisa”.
“Unadhani nakutania!, je? Kama si shujaa
umewezaje kuingia kwenye kisiwa ambacho
hakijawahi kuingiliwa na mtu na akatoka salama?”.
Niliduwaa maana kitu ambacho amekiongelea
kimenigusa moja kwa moja mimi.
“Najua mmekuja hapa kuna kitu ambacho
kinawasumbua sana hasa wewe hapo…una matatizo
makubwa sana”.
“Ndio babu ni kweli nina matatizo makubwa
ambayo nahitaji unisaidie kuyaondoa”.
“Sikia kijanaaa!...siku umekwenda kupeleka kile kitu
kwenye sanduku uliambiwa nini kwenye ndoto yako
ya usikuu?”.
“Mzee umejuajeee lakinii” nilimuuliza
“Usihofu naona kila kitu hapaaa! Tatizo lako wewe
unapenda huruma san ahata sehemu ambayo
haihitaji huruma alafu pia Mnali wewe ni mzembe
sana wa mambo yanayokutokea unayadharau, najua
kuna kiumbe kinakusumbua sana kweli au si
kweli?”.
Mimi na mshana tuliangaliana.
“Kweli mzeee”.
“Haaa! Haa! Haaa! Haaa! Unaonaaa….nimewaambia
nafahamu kila kitu na tena kiumbe mwenyewe
hujawahi kumuona kabisaa machoni mwako je kweli
si kweli?”
“Kweli mzee”.
“Unaonaaa sasa na huyo kiumbee anakusaidia
hamna siku mlipanga kwenda kwa mganga na
mkakwamisha na huyo kiumbeee?”
Hapo ndipo tukakumbuka kuwa ile siku ilitokea na
tukapigwa Makonde kama wezi vile na tukashindwa
kabisa.
“Sawaaa! Mnali unakumbuka siku ambayo ulienda
Kisiwani na vijana wawili na wakapotea kwenye
mazingira yasiyojulikana je? Unaweza kuniambia
wapo wapi?”.
“Babuu! Kiukweli wale vijana sifahamu kwani
walikamatwa na viumbe vikali sana mbele yangu
kwa hiyo sijui kabisa”.
“Mnaliii unajidanganya sana. Jee? Mnapoishi karibu
na bahari hamsikii watu wanakufakufa kila taarifa
inapokuja wanakufa wawili kweli si kweli?”
“Kweli mzee”.
“Sasa wale vijana ambao uliwapoteza huko ndio
hao ambao wamegeuzwa viumbe hatari sana
wanamaliza na wataendelea kuwamaliza Zaidi watu
wenu, na huyu kiumbe anaekusaidia ni uongo mtupu
anashindwa kukumaliza kwa kuwa una kinga na
chembechembe za hao viumbe havijaisha sasa
nakuhitaji ufanye jambo ili nikusaidie”.
Nilibaki kung`aa sharubu pale mimi na Mshana ili
tujue nini ambacho mzee huyo ambae anafahamu
kila kitu kuhusu maisha yangu.”
“Vijana nahitaji muwe tayari kufanya jambo hili ili
mufanikiwe kupoteza haya mambo kabisaa, kazi hii
itafanyika baharini lakini naombeni utayari wenu”.
Tulibaki pale kusubiri nini ambacho mzee anataka
kutuambia.
JE NINI MZEE HUYO ATAWAAMBIA?
 
ENDELEA.......
Baada ya kumalizana na yule mganga alituruhusu
huku akitupatia masharti ya kawaida sana ambayo
kwa yeyote kati yetu angeweza kulitatua.
Mshana pamoja na mimi tulimhofia yule kiumbe
ambae kwa mujibu wa mganga kuwa tayari
kamkamata na hawezi kutoka tena mpaka pale
atakapommaliza kabisa na apotelee mbali. Safari
yetu ilikuwa yenye wasiwasi mkubwa sana lakini
tulijitahidi kufika nyumbani salama bila hata kuwa
na kipingamizi chochote. Mshana alizidi kunitia
moyo kuwa nisijali kutokana na yale ambayo
yanajitokeza.
Akili yangu ilibaki kuwaza familia yangu
inaendeleaje huko iliko, ghafla gari linaingia pale
tulipo na wanashuka Vijana wawili Manyota na
Musa ambao moja kwa moja walikuja kunikamata
bila hata kujua sababu ni nini zaidi. Walinilazimisha
kufika hadi kwenye lile gari ambalo alikuwemo
Mzee Paul pamoja na Salha.
Nilijua kuwa leo hii kazi ipo na lazima wanifanyie
kitu mbaya watu hawa. Walinibeba hadi kufika
kwenye nyumba ya moja ambayo sikuweza
kuitambua vyema. Walinisukumia ndani humo kisha
wakanza na kunihoji maswali ambayo kwangu
yalikuwa kama kitendawili.
"Mnali tumesikia kuwa wewe unamiliki kisiwa cha
majini kwenye ile bahari kweli ama si kweli".
Swali aliuliza Manyota. Nilimuangalia ila swali pia
nilimuuliza yeye tangu aanze pale kuvua samaki
alishamsiki nani kama kuna kisiwa cha majini pale?.
Swali hilo pia Manyota hakujibu ndipo walipoona
kuwa mimi ni kiburi wakaanza kunipiga kwa nguvu
sana sehemu za tumboni na kunipatia maumivu
makali.
"Unakataa unatakiwa kutueleza Sanduku lile wapi
umelipeleka, na pia vijana wawili ambao tunafanya
nao biashara umewapeleka wapi?". Kwa hakika
hakuna kati yao ambae anafahamu swala zima la
mimi kuwapeleka wale kule kisiwani japo wenyewe
ndio walitaka.
"Mimi siwajui na sijui hiko mnachozungumza".
"Mnali utakufa hapa tunahitaji kujua kuhusiana na
lile boksi pamoja na wale vijana waliopotea laa
sivyo hutatoka mzima".
"Nakuapia kuwa hiko kisiwa sikijui na wala hao
vijana siwajui kadhalika boksi sina na silitambui".
"Huyu jeuriii...."
Walimuita Salha alikuja mbele yangu na kunitizama
lakini mimi nilimkazia kama simjui kabisa.
"Unanijua mimi?"
"Hapana sikutambui kabisa"
"Mshenziiii! Umekaaa kwangu mwezi tena
unanifahamu nyuma na mbele shenzi wewe leo
utasema wale watu wako wapi na boksi
mmepelwka wapi".
Aliongea kwa msisitizo mkubwa sana kiasi kwamba
ana uhakika na kile anachokisema. "Sikieni nyinyi
wajinga...."
"Khaaaa! Anatukana huyu mpuuzi..."
"Ndio nyinyi ni wajinga kwanza mnalazimisha vitu
ambavyo haviwezekani, mmekamata familia yangu
alafu leo mnajifanya kunidhihaki kwa
lipi...hamtoweza kupata chochote kwangu kama
hamtoweza kuonyesha au kunipatia familia yangu".
Niliongea nao kwa jazba huku nikiwa na imani
tosha kuwa Mshana atafanya juhudi zozote zile ili
kunisaidia. Lakini mpaka masaa matatu yanafika
bado sioni dalili ya kuja mtu kunisaidia.
Kwa kweli walinipiga sana mpaka nikakosa nguvu
za kufanya mengine. Majira ya usiku wa saa tano
alifika Salha kwenye kile chumba, alipofika
aalinikaribia na kuanza kunishikashika bila
mpangilio alionekana ni mwanamke malaya sana
ambae anautumia mwili wake kupata anavyovitaka.
"Wewee mwanamke shetani unataka nini
kwangu....".
"Niko radhi nikupe mwili kwa mara nyingine ili
nifurahi kupata mambo mazuri".
"Nakuambiajeee hutofanikiwa na sina hisia yeyote ya
kimapenzi na wewe ila kama utaniahidi kunirejeshea
familia yangu nitawaonyesha wapi ambapo watu
wenu wanapatikana na hiko kisiwa kipo wapi".
"Kwa hiyo shida ni familia yako tu"
"Ndio"
"Unajua sisi tunashindwa kukuachia kwa sababu ni
kama kinga yetu ila ipo sehemu salama kabisa kwa
sasa usiwe na shaka. Kesho utatupeleka huko moja
kwa moja tukashuhudie."
Nikiwa bado nimetulia pale hali yangu haikuwa nzuri
sana kutokana a kipigo kutoka kwa Manyota. Ghafla
usiku huo baada ya Salha kutoka mule chumbani
ndipo sauti za ajabu ajabu zasikika zikisumbua
masikio yangu. Haraka sana nashtuka mlango
unafunguliwa na sauti ya mngurumo nausikia lakini
baada ya sauti ile kuingia nje pia nilipata kusikia
sauti za watu wakilalama.
Nilijua moja kwa moja yule kiumbe kafika pale
nilimuona Manyota anaingia akiwa na jazba kubwa
lakini hakuweza kunigusa hata kidogo maana
alipigwa na kuanguka mbali kwenye ukuta. Niliona
nafunguliwa na sauti ya mihemo nikiisikia karibu
yangu.
Bado nilizidi kuwaza kuwa ni kiumbe gani huyu
ambae ananisaidia na hali mganga alisema kuwa
kamfunga?. Niliondoka bila kikwazo chochote hadi
kwa rafiki yangu Mshana. Aliponiona alinikimbilia
lakini alishindwa kunikaribia baada ya kusukumwa
na yule kiumbeee.
"Duuuu! Karudiiiiii"
Nilipoingia ndani ndipo Mshana akafanikiwa
kunishika hakika niliumia sana kutokana na vipigo
vile.
"Mnali mbona wanakuandama sana hawa watu
jamani eeeeh! Umewafanyia nini..."
"Aaaah! Wanataka niwapeleke kule kisiwani sasa
mimi naogopa kuleta majanga mengine kama
yaliyonikuta".
"Nilienda kwa yule mtaalamu muda uleule
nikamueleza kuwa walikuja na wakakuteka akasema
msaada uliobaki ni kumuachia yule kiumbe aje
kukusaidia lakini anataka leoleo alfajiri tuelekee kwa
yule mganga kwa ajili ya ile kazi".
Nilimueleza nitashindwa kwa kuwa hata nguvu ya
kutembea sina kabisa, unaona nilivyopigwa?. Sawa
mnali ila unajua kuwa matatizo yatazidi kuwa
makubwa sana. Twendeeee.
Alinilazimisha huku akinibeba, akichoka ananishusha
natembea hivyohivyo, ilikuwa majira ya usiku sana
kama saa nane tunaingia kwa Mtaalamu yule
ambae alikuwa bado kulala akitusubiri.
Tulimsalimu kisha tukatulia tukimsikiliza.
"Mnaliiiii nimeona kila kitu, inatakiwa sadaka ya
damu haraka sana imwagwe baharini majira ya
asubuhi lazima ifanyike".
"Sasa tunapata wapi hiyo kafara?"
"Ipo tayariiii nenda wale ambao wanataka uwapeleke
huko kisiwani pia kumbuka nitakupa dawa ambayo
ukifika umbali wa kuiacha nchi kavu itupie ndani ya
maji alafu hakikisha unajitosa kwenye maji lakini
usafiri wenu uwe wa mtumbwi na sio boti"
"Mtaalamu vipi nitawezaje kufanya hivyo na hali s..."
"Ukishindwa amini kuanzia kesho mwezi unaandama
baharini na utashindwavkufanya kazi hiyo kwa
sababu nguvu ya mwezi itakinzana na dawa yangu
na kukufanya ufeli..kinachofuata wale wawili
watatoka baharini na kuanza kuuwa mmoja baada
ya mwingine wakikutafuta wewe".
Aiseee tuliishiwa nguvu kabisa. Inatubidi turudi kule
kwa Mzee paul nikawakubalie kwa haraka tuanze
safari.
Kweli tulielekea kule majira ya saa kumi tunafika
kwa mzee paul ambae alifurahi sana baada ya
kumueleza kuwa nipo tayari kuwapeleka ili wanipe
mwanangu. Mzee paul alifurahi sana akamuita yule
kijana wake Manyota pamoja na Salha wakajiandaa
kwa safari. "Tunasafiri kwa lile boti ili tuwahi
kufika". Nilimkumbuka mzee alisema kuwa usafiri
uwe wa mtumbwi na si boti.
"Hapana mzee ile sehemu haihitaji makelele
tutakwenda kwa mtumbwi tu".
Walishangaa lakini haikuwa na jinsi tuliongozana
kuelekea baharini. Bahari ilikuwa shwari kutokana na
matatizo kadhaa yaliyojitokeza siku chache
zilizopita.
Walimchukua kijana mmoja ambae namfahamu hata
mara ya kwanza tulipoelekea na wale wawili
alitupeleka. Kijana huyo aliponiona alishtuka kisha
akawashangaza kwa kusema.
"Haaaa wewe unawapeleka watu kule sehemu
mbaya aaaah! Sitaki kabisaaa siwapeleki
niliyojionea ile siku wakati narudi nayajua
mwenyewe..."
Manyota alinijia na kunieleza. Unataka kutumaliza
kwa njia zako za ajabu? Bosi hii safari haifai kabisa
inabidi tughailishe hii ni triki ya kutumaliza sisi
mkuu.
Niliumia sana maana muda unawadia sijui sasa
nifanyaje?.
 
Nilimuangalia kwa jicho la ukakasi yule kijana.
Hapo ndipo Mshana akanikonyeza kuashiria kuwa
muda umefika rasmi wa kuondoka pale na kwenda
nao.
Nilicheka kiunafiki kisha nikamuendea yule kijana.
"Najua una shida na ela sasa sema unataka kiasi
gani upewe ili utupeleke hadi huko tunakohitaji
sisi?" Nilimuuliza lakini malumbano yalikuwa kwa
hawa wakuu, wanang'ang'ana kuwa hawataki kwenda
na chombo kile ambacho usalama wake ni sifuri
kabisa.
"Mkuu! Huyu kijana mimi namfahamu vizuri sana
katika mambo ya bahari anayajua mpaka anakera
sasa tukimpa nafasi ya kutuongoza humo
atatumaliza mapema sana" alisema Manyota.
Yani Manyota kwa mambo anayonifanyia utadhani
kama hatuna ukaribu kipindi hiko wakati mimi
naanza maisha kwa bwana Kibona. Ila nilijifanya
sijui chochote na nikawa nawadharau.
Ndipo mkui wao alinijia na kuniuliza. "Mnali
nakufahamu vizuri umefanya kazi kwenye hoteli
yangu kwa muda mrefu wewe ni mvuvi hodari
unaonekana, maisha yako ni baharini ila nakutaka
unihakikishie kuwa tunafika salama huko tuendako?
Na tutafanikiwa kwa kile tukitakacho?"
Nikaona hapa ndio sehemu sahihi.
"Usijali mkui wangu tunafika salama kabisa tena
ingekuwa vizuri muda huu ambao maji yako mengi
kabla hata hayajakwenda mbali". Siku hiyo ilikuwa
mbaya kiukweli hasa uwepo wa Manyota ndio
uliharibu kila kitu. Alinijia na kunikazia uso ndipo
akanisukuma hadi kwenye maji ambayo yalikuwa
yanapiga mawimbi makubwa sana ilinifanya
niyumbe na hata nilichokuwa nakishikilia mkononi
ambacho ni ile dawa utoka kwa mzee yule kianguke
kwenye maji mule na kupotea.
Nilihaha huku na kule kujua wapi kimeelekea lakini
sikubahatika, nilihuszunika sana kwani kila kitu
nilihisi ndio mwisho wake pale.
"Sasa wewe mbona unamsukuma huyu jamaa".
Aliuliza Salha.
"Lazima nimsukume kwa sababu hana akili huyu
anataka kutuua huko tuendako, kama hataki hilo
mbona anakataa kwenda na boti na anataka
mtumbwi?".
Nilipaniki kisha nikamjia juu.
"Haya nyinyi ahida yenu ni nini? Si kwenda huko
kisiwani nimewaambia kule akuhitajiki kelele za
hayo maboti sasa kama wabishi twendeni."
Waliangaliana pale kisha wakatoka kidogo pembeni
wakatuacha mimi na manyota pale tulipo mimi
nikiwa nimelowa maji kutokana na kudondoshwa na
Mpumbavu Manyota yani nilimtamani sana.
"Mshana! Nimepoteza ile dawa siioni"
"Kivipi tena?"
"Wakati amenisukuma niliishika mkononi sasa sijui
tunafanyaje".
"Mh! Sasa hivi muda bado wa watu kuanza kuja
hapa ufukweni ngoja mimi nikimbie kwa yule mzee
nikamueleze na atusaidie tunafanyaje lakini wewe
nenda nao."
Wakati tunahojiana ndipo namuona yule mzee kwa
mbali akiwa anakuja upande wetu.
"Mshana angalia kuleeee yule mzee anakuja "
"Ni kweli sasa tufanyaje"
"Muendee haraka sana"
Mshana likimbia kwa kasi sana kuelekea kule. Huku
pia wakiwa wamemaliza maongezi yao ndipo
wakaja na kumuambia yule kijana kuwa wapo tayari
kwenda.
Tuliingia huku nikiwa nawaza Mshana anachelewa
kuja.
Kumbe alivyofika kule alimueleza yule mzee na
ndipo akamuambia kuwa yeye ujio wake pale
ufukweni muda ule ni baada ya kuona kuwa
tumepoteza ile kinga kwa hiyo yupo kuja kumaliza
kila kitu.
Mshana anaingia pale tulipo na kuungana. Tulikuwa
jumla ya watu sita na muongozaji ni wa saba.
Mtumbwi ulisogezwa taratiibu kuelekea kwenye kina
cha maji kukitafuta kile kisiwa.
Nilimsogelea Mshana na kumuuliza kipi ambacho
ameambiwa na yule mzee. Alininong'oneza kuwa
"Mzee kasema tuhakikishe tunafika hadi kisiwani
alafu pale ufukweni tutamkuta yeye ndipo anamaliza
kila kitu". Nilipatwa na wasiwasi mkubwa sana mara
ya kwanza ilikuwa kuwa dawa niitupe kwenye maji
alafu na mimi nijitupe japo sikujua kuwa baada ya
hapo nini ambacho kingeendelea, sasa hivi baada
ya dawa kudondoka kuwa tufike kisiwani alafu yeye
tutamkuta huko.
Wakati tunaendelea kuacha ufukwe kwa mbali ndipo
tunamshangaa nahodha wa mtumbwi akishtuka.
"Jamaniii angalieni kule mbele, kuna ukungu
mkubwa sana na siwezi hata kuendelea kwa kuwa
sitoweza kuona jamaniii".
Kila mmoja wetu alichungulia na kuona kweli kuna
ukungu mzito sana. Mh! Mbona hii hali hatukuwahi
kuiona, nilipomuangalia Musa na Manyota
walioshibiana kwa mazoezi wako tayari kumlinda
bwana Paul. Nilijisemea kuwa ngoja tudondoke
alafu niuone huo ubaunsa wako mshenzi wewe.
Manyota aliniangalia na kuniambia.
"Wewe jamaa nakutamani sana nikutafune hujui tu".
"Unajifanya baunsa, ngoja lidondoke alafu tuone
limwili lako hilo linafanyaje kazi, mana mimi,
mshana, pamoja na huyu nahodha tunajua kuogelea
nyinyi sasa mtakufa". Manyota alikasirika akataka
kutoka kunifuata pale nilipo ndipo yule kijana
akasema.
"Oyaaa kaka! Acha ujinga upo sehemu hatari kama
una nguvu njoo uongoze jahazi hili ngojeni
niwafikishe alafu mkapigane huko". Lakini kadri
tunavyzidi kwenda ndipo hali ya bahari inazidi
kuchafuka. Alafu sauti za ajabu zinasikika kila
upande wa eneo tulipo. Salha alikuwa muoga sana
kwa kuwa yeye pekee ndie mwanamke ukimya
ulitawala safari ya matumaini ikielekea kuwa tamu.
Nilijua kuwa sasa mauzauza yanaanza kuingia.
Wakati tunazidi kwenda ndipo alijitokeza kiumbe
kutoka kwenye maji na kumrukia kijana yule
aliyekuwa anaongoza jahazi na kutupiwa kwenye
maji.
Keleleee za kuomba msaada zilisikika na hatimae
kijana wa watu alizamishwa. Mule tumebaki sita
hakuna ambae anajua kuliendesha lile zaidi ya mimi
na mshana. Nilijisemea moyoni sasa mambo
yameivaa.
Mzee Paul pamoja na suti lake alishindwa kuamini
kutokana na tamaa zake za kijinga. Mimi na
Mshana tulibaki kama yatima tunawachora tu
wanataka kufanya nini maana kama kuruka
hawawezi na chombo kinaenda mrama.
"Mnali nitakuua endesha chombo turudi nyuma".
Alisema manyota.
"Manyota hivi wewe ndio mwenye uchungu sana
kuliko Musa au mzee mwenyewe maana unaongea
sana porojo, chombo hiko endesheni kama hamjui
acheni kitatupeleka chenyewe". Kweli Manyota
alishika na kuongoza huku akiniuliza kwa hasira.
Ghafla mtumbwi ule unaingiza maji, lakini ajabu
zaidi maji yenyewe rangi ya damu. Hofu kubwa
baina yao ilitanda hata manyota akaona kuwa leo
kumekucha. Wakati tunaendelea kupakua maji yale
Manyota anafurahi kuona kosiwa bila kujua kuwa
ndio sehemu husika.
"Jamanii tukatulie kwenye kile kisiwa alafu tutafute
msaada wa kurudi nyumbani sawa mkuu".
"Ndio hapa sina hamu tena inahitajika kurudi
kwanza alafu tujipange".
Nilicheka sana. Kwa kuona wale wabaya wangu
waliokuwa wananionea sana sasa wapo mikononi
mwangu.
 
.......Nilicheka kwa dharau kwani hawakufahamu
kama ile sehemu ndio sehemu husika kabisa.
Mshana hajawahi kufika huku ila kila kitu cha huku
anakifahamu kwa kuwa nilishamuambia
kinachoendelea, hivyo hakuwa na wasiwasi kabisa.
Taratiibu tulifika kwenye ule ufukwe wa Kisiwa,
mimi nilianza kuwa na wasiwasi sana maana
mambo ambayo yalinitokea mwanzo sikutamani
tena kurudi huku ila shida ndio ambayo ilinifanya
nirudi.
Ghafla ukimya ulitawala na kiza kilitanda tena
maana muda mrefu tuliutumia kukaa kwenye maji.
Manyota alikuwa wa kwanza kabisa kutoka mule
kwenye maji. Mimi nilikuwa muoga kidogo
walipoisha wote tulibaki wawili pamoja na Mshana
ndipo tukatoka na sisi. Manyota alikuwa na kisirani
sana na mimi aliniangalia kwa makini sana muda
wote ambao tulikuwa tunatembea. "Haya hapa
inabidi tupumzike" alisema Manyota.
Wote walikubaliana lakini mimi nilipinga, kitendo
hiko kilimnyanyua Manyota hadi kunisukuma na
kuniangusha chini kwenye mchanga. "Unapinga amri
yetu wewe bwege eeeh! Mjinga mkubwa wewe".
Nilibaki kucheka tu pale.
"Haya labda niwaambie kuwa sehemu yenyewe
tumeshafika tayari ndio hiki kisiwa chenyewe" ni
liwaambia huku wakiwa hawaamini kile
ninachowaeleza.
Mzee paul alisimama na kunifuata kwa ustaarabu
sana. "Kijana sema sasa wapi ule mzigo upo
nitakupa maisha mazuri utakayoyataka pamoja na
familia yako..lakini pia unafahamu mwanao sasa
yupo marekani anasoma huko mimi ndie
niliyempeleka". Nilipatwa na bumbuwazi na
kumuangalia
"Unasema kweli mzee sasa nitampata vipi Asante
wangu?"
"Utampata baada ya kutuonyesha mali ziko wapi".
Nilijua kuwa hapa hakuna ambae anaweza kwenda
kupona pindi tu wakija wale viumbe. Niliwakubalia
kuwaonyesha. Paul alichukua karatasi pamoja na
peni akanipatia, kidogo nilikuwa mjuzi wa
kuchorachora hata vibwengo kidogo hivyo haikunipa
shida.
Nilichora njia ambazo zitawapeleka kuzima mapema
sana lakini nikaweka na njia ya vibwengo ambavyo
vinaishi na mimi nikawaelekeza hapohapo.
Nilipomaliza nikawapatia. "Hii njia ya kushoto kuna
wanyama wakali piteni huku kulia alafu mtakata
kushoto te na kama mnawazunguka alafu mtakutana
na hili pango mtaingia ndani yake huko ndiko
ambako mtakutana na maboksi makubwa zaidi ya
lile".
Niliwaelekeza.
"Ina maana huku kote wewe ulipita?" Salha aliuliza.
"Ndio nilipita lakini huku hakufai mimi kurudi tena
maana milango hii ya pangoni ina kawaida ya
kushika sura za watu itagoma kufunguka kwa kweli"
Nilijiona naongopa bila hata aibu. Ndipo mzee paul
pamoja na timu yake wakatoka na kwenda pembeni
kisha wakaanza kuongea baadhi ya vitu.
Ajabu zaidi walipiga kelele za furaha sana walicheka
kiasi kwamba hata ndege walipo karibu na kisiwa
kile waliruka kwa pamoja. Zile sauti zao zilijirudia
mara kwa mara. Kitendo hiko kilianza
kuwaogopesha sana.
"Manyota sikia mbona kama kuna wengine
wanatusadifu kucheka?"
Musa alimuuliza Manyota.
"Mh! Nashangaa ebu piga kelele kidogo"
"Nyieeeew maipige keleleee acheni hiyo ni hatari"
Niliwaambia lakini Manyota ni mbishi kama mtu
anayejiharishia kusema lazima yatoke. "Musa
nimekuambia piga kelele tusikie kama kweli!".
Musa alijiandaa
"Tupooo hukuuuuuu". Baada ya kusema vile kwa
sauti kubwa wakasubiri majibu baada ya kuja pale
tulipo na tukawa wote tumekusanyika.
Assalaleeeee! Ile sauti baada ya kwisha ilijirudia
tena. "Tupooo hukuuuuuu". Kila mmoja wetu
alishtuka pale.
"Mnali huku kuna watu wanaishi?" Aliuliza Salha.
"Sikieni niliwaambia kuwa msipige kelele oneni sasa
matatizo mmeyaanzisha wenyewe. Huku hakuna
mwanadamu yeyote.
"Jamani tuyaache hayo tujipange jinsi ya kwenda
kuchukua mali basi". Uaiku unaingia zaidi watu
wamechoka njaa zatuuma. Nakumbuka kuwa yule
jamaa aliyenisaidiaga kipindi cha nyuma aliniambia
kuwa ili niishi vizuri haya maeneo basi nile nyama
mbichi.
Wazo hili lilikuja baada ya kuwaona wale yani Musa,
salha, Mzee paul na Mpumbavu Manyota
wanafungua mabegi yao watoe chakula. Mimi
nilimuambia Mshana rafiki yangu kuwa. "Oyaa!
Hapa hatuna chakula na lengo letu tuhakikishe hawa
wanapata adabu lakini kuna viumbe vile vibwengo ili
visikudhuru lazima ule nyama mbichi sawa"
"Kaka kwa nini iwe mbichi"
"Mshana mbona kama unafanya hujui nini
kinaendelea ebu ngoja kwanza wale wakila kile
chakula chao hakika wote watadhurika maana wale
viumbe watawafahamu kwa haraka sana."
"Hapana nenda uwaambie kuwa na wao watafute
nyama mbichi wale wasidhurike leo mpaka yule
mganga akija ndipo atajua anawafanya nini".
"Sawa nimekuelewa ebu ngoja niende".
Niliekea hadi pale maana walijitenge kidogo na sisi.
"Salha samahani nakuomba mara moja"
Nilimuita salha alipokuja ndipo nikamueleza kila
kitu japo alinikaidi sana lakini niliendelea
kumuambia kuwa wasijaribu kula chakula kile
walichobeba toka majumbani kwao tofauti na hapo
wale nyama mbichi".
Alienda kuwaeleza ndipo gumzo likazidi ghafla sauti
ilijitokeza.
"Tupooo hukuuuuuu".
Kila mmoja alikaa kimya na wakaanza
kunyoosheana vidole Manyota na Musa. Nilienda
kumueleza Mshana kuwa anisubiri mara moja
naelekea kwenye maji naweza kutoka na samaki
hata wawili. Hakuna aliyeamini kuwa ni kweli kuna
ulazima wa kula nyama hiyo kwa wakati ule.
Nilipiga mbizi baada ya muda kadhaa ni lifanikiwa
na kutoka na samaki wawili wakubwa ambao
niliwatupia nje ya bahari. Mshana alinishangaa kwa
umaridadi niliouonyesha alafu ni usiku. Mshana
alishindwa kula kwa kuwa hakuamini mwanzo, kwa
kuwa wale walikataa mimi nilionyesha mfano
nikatafuna robo ya yule samaki mmoja. Mshana na
yeye akamaliza robo nyingine akabaki nusu.
Walitucheka sana. Muda wa kulala tayari
niliwaambia kuwa hatutakiwi kulala haya maeneo
inatubidi tulale kwenye maji.
"Wee mshenzi njama zako tushazijua tayari sasa
hautupati unataka utulishe nyama mbichi, alafu
unataka utulaze kwenye maji ili tufe hujui kama maji
yanajaa eeeh mfano tunalalaje?...sasa njama zako
zimegonga mwamba asubuhi tukiamka tunachukua
mzigo tunasepa pumbavu wewe".
"Mnasepa etiii...haya laleni hapo Mshana tukae
kwenye maji kaka".
Mshana nilim buruza tu hata hakuwa anaelewa.
Tulikaa kwenye maji kwa mbali kidogo japo ubaridi
ni mkali na wale wakalala kwenye mchanga.
"Mnali ebu niambie kwa nini tupo kwenye maji".
"Mshana unajua kila ninalokuambia fahamu nalijua
fika sana mimi, hao vibwengo muda wao ni usiku
na asubuhi ila hawapendi maji kabisa. Yaani sisi
tuko salama zaidi kuliko wale"
"Ahaaa! Hapo imekuelewa".
Ghafla sauti ya mngurumo karibu yangu ikijitokeza.
"Aisiiii mshana yule kiumbe kafika tayari na sijui
hata kaja kwa usafiri gani yani". Basi pale tulikuwa
makini sana maana tunamfahamu huwa hapendi
ujingaujinga.
Tukiwa tumejisahau asubuhi inaingia tunaamshwa
na kelele za wale watu kuwa mwenzao katolewa
macho, na mkono pamoja na ulimi yani kafa
kabisa. Sasa walianaza kuhaha pale hakuwa
mwingine ni Musa. Kizaazaa tayari kimeanza
Manyota na ujanja wake wote kilimshuka mara
baada ya kuona vibwengo kama vitatu hivi watu si
watu wanyama si wanyama.
Mara wanaongezeka, sisi walitupita tu pale.
Walizongwa na si kuzongwa tu, Salha alianza
kushambuliwa mkono. Ndipo wale viumbe walianza
kukimbia baada ya kuona mmoja baada ya
mwingine anapigwa na kitu kisichojulikana hasa
walipojaribu kutukaribia sisi. "Mshana nahisi yule
kiumbe anatusaidia". Manyota baada ya kuona
mambo yamezidi alianza kutafuta wale samaki
wabichi na kuwasihi waingie kwenye maji.
Walifanikiwa na huku viumbe wengine wakija na
wengine wakiondoka. Manyota aliona yule samaki
mbichi ndio urithi tosha uliobaki kuwalinda
waligawana, lakini masikini Salha mkono wake
umejeruhiwa.
Tuliwasogelea. "Haya Manyota kidumee nenda
kapambane na vidume wenzako".
Alinikodolea macho tu.
"Vipi si mmesema kuwa asubuhi hii tunaenda
kuchukua mali twendeni".
Wote kimya.
Ghafla ile sauti ikajirudia
"Tupooo hukuuuuuu".
Kila mmoja alizidi kusogea kwenye kina baada ya
kuhisi ile sauti itawaletea tena wale viumbe.
 
SEHEMU YA THELATHINI NA SITA 36.
ENDELEA....
............
Kufikia muda ule kila mmoja sasa aliona ni bora
aokoe maisha yake hasa mzee Paul pamoja na
vijana wake. Mzee huyo aliona busara hapo
kunisogelea akiwa na wasiwasi mkubwa sana.
Sikujua nini ambacho anataka kuniambia. Ila kabla
hata hajaanza kusema nilidakia mimi na
kumuambia. Nawaombeni nyoote mtoke alafu
mnifuate mimi hapa. Walinitazama bila kufuata yale
maagizo, manyota alizidi kusogea mbali kidogo na
maji ili aweze kuwa salama zaidi. Salha na yeye
akiwa anaugulia mkono wake huku akiwa na
maumivu makali.
Mzee paul aliwaongoza kwa mkono kuwa watoke
kwenye yale maji kisha wanifuate. Walitoka mimi
nikawa nawaongoza sasa tunatembea kwenye fukwe
ile ya bahari pamoja na kisiwa.
Bila kujua mzew paul alitoa bastola na kupiga juu
paaah!!. Kila mmoja wetu alikaa chini kwa
kuchuchumaa hatimae wakatushika mimi na
mshana.
Manyota ndie alikuwa kiongozi wa kunishika mimi
maana nahisi alikuwa na hasira sana na mimi.
Ndipo mzee paul alitoa kauli ya kusema kuwa Salha
atafute haraka uwezekano wa kusafiri pale na
Manyota aendelee kutukamatia sisi pale wao
wakiwa wanatafuta hata mtumbwi waondoke.
Manyota alitukamata vyema tukashindwa hata
kutoka maana alitukamata na kamba ngumu
kukatika. Mnali, unadhani utacheza na akili zetu
wewe haya tuambie sasa hizo dhahabu ziko wapi na
hawa viumbe unawajua vipi mbona nyinyi
hamdhuriki?.
Aliuliza Manyota, manyota ebu fikilia mpaka leo kipi
umekipata kutoka kwa huyo mzew wenu mzungu?
Anawatumia vibaya kama hamjui kuna kitu
anakitafuta akipata atawaacha hamna kitu.
Nilimuambia Manyota aliyeonyesha kununa na
kunipiga kofi zito paah!!! Niliona Manyotanyota
mengi sana. Nilimgeukia Manyota unadhani hili ndio
suluhisho la nyinyi kufanikiwa hali hamjui mko eneo
baya sana kwa sasa. 'Keleleee mnali mpumbavu
wewe', umesababisha Musa kufa namuona kwa
macho yangu nakuambia tunawaacha humuhumu.
Haaaa! Haaa! Haaa! Nilimcheka kwa dharau sana.
'Manyota unajua kama unajidanganya, humu hakuna
atakaechomoka zaidi ya mimi na Mshana kama
huamini ngojeni sasa'.
Kumbe na Mshana hakufungwa vizuri ile kamba
ndipo alijichoropoa na kumvamia Manyota na
kumdondosha.
Kwa bahati mbaya Mshana hana mwili wa
kushindana na Manyota hivyo alidhibitiwa sekunde
kadhaa, lakini Manyota hakuwa na utani kwani
alichomoa bastola kiunoni na kumpiga nayo
kichwani, kwa macho yangu namuona Mshana rafiki
kipenzi anadondoka chini kama mzigo. Jambo hilo
liliniuma sana na kunifanya nikose nguvu ya kufanya
msaada wowote kutokana na kutaitiwa.
'Manyoooota haki ya nani hili ulilolifanya utakuja
kuulipa mjinga wewe'. ' Weeeewh! Usinitisheee tena
hata wewe inawezekana nisihitaji hizo mali
nikakumaliza na wewe mjinga wewe. Niliumia sana
pale, manyota hakuishia hapo aliniaogelea na
kunishika uso na kunitemea mate mazito usoni.
'Sikia, naelekea kum baka mkeo nikirudi mbele yako
shwaini wewe...pia kama hukuwa na taarifa umelala
na Salha yule binti Ameathirika zamani sana sasa ni
kukuzika tu.' Manyota alinieleza na kuniingiza
kwenye dimbwi la mawazo kuwa Mshana namuona
amekufa na damu zake zinachuruzika ina maana
sitomuona tena, nimelala na salha naambiwa ni
binti anaejiuza japo ni nesi lakini ana UKIMWI ina
maana namfuata na mimi Mshana huko aliko?.
Wakati nawaza hayo Manyota alitumia mwanya huo
na kunikita ngumi nzito kichwani iliyonisindikiza
kwenye usingizi mzito zaidi.
BAADA YA MASAA KUPITA.
Nakumbuka ilikuwa kiza kizito sana nashtuka
kwenye majani alafu harufu ya damu ikiwa inatawala
pale nilipo. Sikufahamu nini kinaendelea kwani
kichwa kizito sikumbuki chochote.
Nilikaa takribani dakika kadhaa pale kwenye majani
na kukumbuka kuwa niko kisiwani lakini pembeni
yangu nauona moto. Sikufahamu ni wapi nilipo na
nimekuja kufanya nini na nani kanileta. Kutokana na
maumivu ya kichwa nilijikuta nalala tena hadi
asubuhi.
Kwa mshangao mkubwa sana nilipoamka nakutana
na yule Jamaa w a mara ya kwanza kuingia ndani
ya kisiwa hiki cha maajabu. Nilibaki kuduwaa tu
pale. Alinisogelea na kuninyooshea mkono ili
niukamate. Nilifanya hivyo, ajabu zaidi alinionyesha
ile sehemu ambayo mara ya kwanza nilifika kuwa
ndipo anaishi.
'Nataka kurudi nyumbani'. Nilimuambia. Akanishika
kicwa kisha akatikisa na kunitaka kukaa chini karibu
na moto. Alinitizama sana wakati huo kwenye moto
kuna nyama inachomwa hapo ndipo ajabu ilinikuta
anatafuna nyama za kuchomwa. Sura ni ileile mpaka
matendo yake.
Alinipa kipande cha kutafuna lakini nilijikuta nakataa
tu sikufahamu kw a nini. 'Mnali, unataka kwenda
kwenu kulipiza kisasi?'. Aliniuliza 'ndio'.
Hapo ndipo akaanza kunieleza mambo kadhaa.
Alafu akanipa sanduku moja akaniambia nifike pale
kwenye fukwe kisha nifungue lile sanduku
nitakachokuta nikitupe kwenye maji alafu niondoke.
Na nitafika kw a nguvu za kiza. Sikutaka kuchukua
muda sana nilitembea sana maana hata njia
ilinitoka. Nikiwa na boksi langu nafika hadi kwenye
ule ufukwe nakuta mambo vululuvululu, ndipo
nakumbuka kuwa Mshana alifariki jana yake.
Ilibidi nifike mpaka pale ambapo nilihisi kuwa
atakuwepo lakini sikufanikiwa kumuona, bali nilikuta
msururu wa mtu kuburuzwa hivyo niliufuatilia ule
hadi karibu na kule ambako niliamka asubuhi.
Kwa macho yangu nakuta mwili wa Mshana kakatwa
vipande na katengenishwa kila kiungo. Niliumia
sana kimyakimya nikajua hapa hakuna usalama, na
kama ni wale akina Manyota ndio walifanya haya
nitafika na kurudisha kisasi hiki. Nilirudi
harakaharaka hadi pale kwenye maji na kuanza
kufungua lile boksi ili nipate kujua ndani kuna nini
na nitupe nisafiri hadi nyumbani kwa nguvu za giza
kama alivyodai yule jamaa. Nilitokea kumuamini
kwa kuwa namfahamu vyema.
Aaah! Niliifungua lile boksi ulifuka moshi mzito
ulioniingia machoni na mwilini mzima. Palepale
alikuja yule mganga sikufahamu wapi katokea akiwa
na sura ya yule jamaa aliyenipatia lile boksi.
Haaaa! Haaaa! Haaaa! Haaaa!. Pumbaaaaaavu
ushaingia tayari wewe..nilisikia neno hilo tu badala
ya hapo nilijikuta nipo kwenye eneo ambalo
silifahamu lakini sauti ya maji kupiga ukuta
niliyapata nikapata wazo kuwa hapo nilipo nibkaribu
na ule ufukwe. Ndipo mtu mmoja alikuja na kizinga
cha mti chenye kuwaka moto. Hakuwa mwingine
bali ni yule mganga.
Alianza kwa kucheka sana. "Haaaa! Haaa! Kicheko
chake ndicho kilinijulisha kuwa mule ndani siko
peke yangu kumbe zaidi ya watu wengi. Sikieni
nyooooote mko kwenye himaya yangu mimi sasa,
nataka kutengeneza ufalme wangu mimi mwenyewe
na nyinyi ndio ambao mtakuwa wafuasi wangu
sawaaaaa!.....alisema yule mganga.
"Ndioooooo......" tulijikuta tunaitikia wote bila hata
kupenda. Kwa nguvu niliyonayo ilinifanya nitambue
baadhi ya vitu maana akili bado haijabadilika kama
wengine. Nilijua kama watu wapo wengi kutokana
na sauti zao ila sikufahamu kuna nani na nani.'.
Ghafla alitoweka na mwanga ukapotea.
Nilipatwa na woga kwa kutojua hapa wapi pia
kumbe kwa yule mganga aliyenipeleka Marehemu
mshana ni mtu mbaya hivi. Usingizi haukupatikana
kabis kwa kuwa harufu mbaya pia misukosuko ya
watu ilikuwa ngumu kwangu.
Baada muda mrefu nikilia kutokana na yale
yanayonikumba mwanga ulianza kuingia ndipo
jambo la ajabu nakutana na Salha namuona na yeye
akiwa hovyo, ghafla Manyota na Paul. Aaaah! Hapo
nikaamini kumbe kweli tumepatikana.
Nililichukulia la kawaida lakini pindi nilipowaona
James na yule mwenzake ambae walitaka
kunisaidia kumrudisha mtoto wangu na mke wangu.
Nawaona wakipita karibu ya watu wengine. "Hawa si
walikufa hawa" hapo nilijiuliza nikiwa peke yangu.
Lakini nilijibiwa na sauti ambayo sikufahamu wapi
inatokea.
"Hapa hakuna mtu aliyekufa, ukifa unazaliwa upya!
Pia haya ni maisha yako baada ya Maisha ya uvuvi".
Nilishtuka sana nikaanza kuhaha kutafuta ni nani
huyo. Ndipo kwa mbali namuona yule mganga
ananiangalia kwa jicho kavu sana. Kisha akaja
"Weweeew ndio unataka kuniletea shida hapa
nisifanikishe ila dawa yako ipo".
Mh! Nilishangaa kuniambia kuwa mimi ndie
namfanya asifanikishe yale aliyoyapanga. Mala
ghafla watu wengine wanaletwa na wengine
wanasambaza chakula.
Hakika sikupanga kabisa kula chakula kile.
Nilipatwa na bumbuwazi kubwa kwa yule aliyekuja
kunipatia chakula kwenye kopo maalumu namjua
kabisa ni Kibona lakini hanijui amaaa maana
namuangalia ili nihakikishe kama ni yeye lakini wapi
aliendelea na kwa wale wengine. Nilivuta pumzi na
kusema. Mungu kanionyesha ndugu yangu sasa
nijue namsaidiaje. Mara nawaza hilo najibiwa
"Hakuna aliyeweza kutoroka au kumtorosha mtu
humu".
Niliishiwa pozi palepale.
 
Ilipoishia...
.....Mh! Nilishangaa kuniambia kuwa mimi ndie
namfanya asifanikishe yale aliyoyapanga. Mala
ghafla watu wengine wanaletwa na wengine
wanasambaza chakula.
Hakika sikupanga kabisa kula chakula kile.
Nilipatwa na bumbuwazi kubwa kwa yule aliyekuja
kunipatia chakula kwenye kopo maalumu namjua
kabisa ni Kibona lakini hanijui amaaa maana
namuangalia ili nihakikishe kama ni yeye lakini wapi
aliendelea na kwa wale wengine. Nilivuta pumzi na
kusema. Mungu kanionyesha ndugu yangu sasa
nijue namsaidiaje. Mara nawaza hilo najibiwa
"Hakuna aliyeweza kutoroka au kumtorosha mtu
humu".
Niliishiwa pozi palepale.
Endelea........
..........Hapo ndipo akili ilianza kunikaa. Nikiwa
nawaza nimefika vipi haya maeneo ghafla kila
aliepo pale alitulia. Nilijihisi kama pumzi zangu
zinakata alafu mbavu zinabana kana kwamba
zinataka kukutana.
Hali hii ilinitisha sana ndipo nikaanza kulala chini na
kutapatapa ili nipate kuwa sawa. Mabadiliko
nayaanza kuyaona baada kuhisi kuwa nabadilika
hata kimaumbile yangu. Niliendelea kuhaha pale
kutokana na kukosa pumzi. Ajabu zaidi wengine
walikuwa wametulia wananiangalia mimi jinsi
ninavyoteseka pale chini.
Nakiona kifo hiki hapa mwenyewe. Naanza
kukumbuka mambo mengi niliyoyafanya. Nilihisi
kama Tv iko mbele yangu nikiyashuhudia matendo
yangu yoote niliyowahi kuyafanya. Nikahisi sasa
mwisho wa maisha yangu ndio pale. Lakini baada
ya muda nilijikuta naweza kupumua baada ya mbavu
kuachia na hewa safi kuipata, chozi lilianza kunitoka
nguvu zikiwa zinaniishia, na njaa pia ikiwa inagonga
kisawasawa.
Alikuja yule mzee akiwa amevalia nguo za kiufalme
pembeni yake nakumbuka alikuwa amefuatana na
walinzi pamoja na wasaidizi wake. Huwezi kuamini
ufikaji wake tu wote tulijikuta tumetoka mule ndani
na kuwa nje kabisa ya pango lile na kuwa ufukweni
mwa kile kisiwa.
Pale nilipata nafasi ya kugundua mengi kidogo.
Alisimama yule mzee kisha akaanza kuongea lakini
macho yake makali yakinielekezea kwangu.
Niliogopa sana nilipatwa na hofu pia maana
alionekana mkatili mno. Akiwa anajiandaa kuongea
macho yangu yalikuwa kule ufukweni nijue tu jinsi ya
kuwakimbia pale. Alianza kukohoa kisha akasema.
"Sikieni! Nyinyi wafuasi wangu wa kisiwa hiki, nyinyi
ndio mtajenga milki hii ya ujinini sawaaaa!".
Alisema kwa nguvu. Nikajua Ahaaaa! Kumbe hiki
kisiwa ni cha majini ndio maana.
Hapo ndipo alisimama kisha akanisonta kidole
mimi pale nilipo. Nikajikuta nasimama bila hata ya
kutumia nguvu. Kwa kuwa tulikuwa wengi sana kwa
mbali namuona rafiki yangu Mshana akiwa tofauti
na vile alivyo. Tulikuja kuchukuliwa na watu wake
hadi mbele yao. Kisha akatamka. "Hawa hapa ndio
waliosaidia kwa namna moja ama nyingine kufufua
hiki kisiwa sasa wana zawadi yao. Wanatakiwa
kupewa zawadi nzuri kwa ajili yao." Hapo ndipo
nilipofurahi zaidi kuona narejeshwa nyumbani
kiurahisi.
Aliendelea kusema.
"Lakini watatakiwa kunywa damu ili wasije
kukumbuka chochote cha huku na kupasahau
kabisa. Nageuka nyuma yangu namuona Salha,
mzee paul, Musa na Manyota pamoja na wale
Michael na mwenzake na wao wanakuja pale tulipo.
Kufikia hapo nilikuwa na juhudi kumtafuta Kibona
kwani nilifanikiwa kumuona siku ya jana yake
akinipatia chakula. Ukungu machoni ulitanda na
ukanifanya nisimuone kabisa kibona.
Yule mzee alisimama na kuanza kusema kwa
msisitizo. "Nyinyi binadamu ni wa sumbufu sana
tena sana. Mnadiriki kufikia maeneo haya ambayo
si rahisi kufikika hasa wewe kijana Mnali hili lazima
ulilipe damu hii mtakayonyweshwa ninyi nyoote
yupo atakaendelea kuwa hai na mwingine atabaki
yule ambae atabaki basi yeye ndie atafanikiwa
kurudi kwake lakini atarudi kana kwamba kazaliwa
upya hatokumbuka chochote kile zaidi ya yale
atakayoyakuta huko". Tulisubiri kinachofuata kwa
sababu sikuwa na hata nguvu ya kusema lolote.
Kwa macho yangu namuona Kibona akija na kifaa
kilichojaa damu na yeye akiwa kama mzuka fulani
asiejielewa. Wengi wetu walifurahi sana lakini mimi
peke yangu ndie nilieonyesha wasiwasi mkubwa
dhidi ya yale yanayoendelea pale.
"Kibona kaka! Kibona kakaaa unanijua hapa wapi
hapa nini kilikukuta kaka". Nilimuita huku nikiwa
nimemshika na kumtikisa lakini hakuna alichosikia
zaidi ya kuendelea na kazi yake ya kuwanywesha
damu baadhi ya watu tuliokuwepo pale.
"Mnaliii! Huwezi kumrudisha mtu niliyemmiliki mimi
hakuna kabisa huo uwezo naandaa jeshi langubkwa
ajili ya kuangamiza binadamu sasa utakunywa damu
nina imani hutoki hapa na ukija kutoka basi amini
nitakutafuta pande zote za dunia na nitakurudisha."
Sikuelewa kabisa nini ambacho anakisema
aliendelea kusema.
"Mnali hawa wote hawa hawawezi kurudi kuwa
binadamu tena wewe una bahati kubwa kwa sababu
umelindwa na kiumbe alietusumbua kwa kipindi
kirefu akiwa anaishi hapa kisiwani na ndie yeye tu
alinifanya mimi nije kuishi kwa binaadamu kama
mganga nikiwa na lengo la kutafuta njia ya kurudi
hapa..." wakati anaendelwa kuropoka ndipo Kibona
ananifikia na kutaka kuninywesha ile damu mimi
niliipisha huku nikimuangalia kwa jazba yule mzee.
"Mnaliii hata uikatae lakini ndio njia sahihi ya wewe
kurudi kwako. Wewe ni mvuvi hodari ambae
unaweza mambo mengi sasa kumbuka kuna kiumbe
nilimuweka kwako baada ya kukugundua wewe una
uwezo wa kufika huku kisiwani kiumbe yule alikuwa
ananipa mimi taarifa zako na mipango yako hii ndio
maana mkiwaza kwenda kwa mganga sahihi lazima
awazuie mbona mlipowaza kuja kwangu hajawazuia
na mkafika...." hapo ndipo akaniacha hoi sana kwa
kweli.
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Ndipo alianza kunywa Salha ghafla akapotea kabisa,
nilishangaa sana akaja kunywa Mzee Paul ghafla na
yeye akapotea mpaka inafika kwa Mshana niligoma
kabisa kwa sababu nilijua na yeye atapotea alafu
nikamkosa rafiki kipenzi.
"Mnaliii unataka nini sema nikufanyie ili uwe chini
yangu na wewe uwe balozi wangu huko Kwa
binadamu ili nikitaka wafuasi basi unisaidie.."
Aliniuliza swali ambalo sikutaka kuchelewa kujibu
kabisa. "Naomba huyu asinywe kabisa nataka arudi
kama awali niondoke nae ukiweza kunifanyia hilo
nakuahidi leo nitakuwa balozi wako...lakini
niliahangaa kumuona Kibona anasikitika kwa mbali
baada ya mimi kukubali. Pale niliwaza itakuwa
nimekosea au ningemuomba niondoke na kibona
kisha nikamuacha Mshana?.
"Haaa! Haaaa! Haaaa! Mnaliii usije kutugeuka kwa
sababu sisi tunatunza kumbukumbu sana na
naomba utuahidi kuwa hii kazi utatufanyia. Mshana
ni marehemu hadi hapo huko duniani ataishi kwa
muda wa miaka 10 tu kisha atarejea kwetu
kuungana na sisi. Masharti hapana kujihusisha tena
na mambo ya bahari hata kukatisha huku kuja
huruhusiwi pia damu hii lazima uinywe".
Nilichukua ile birika kisha nikaipeleka mdomoni na
kuanza kunywa huku nikiwa nimefumba macho.
Ghafla najiona niko ufukwe mwingine huku
nimeshikilia birika yenye maji nikiwa nakunywa
maji. Niliibwaga chini kisha nikawa nashangaa
muda mchache nilikuwa kwenye hatari sasa hivi
nipo huku. Nilifurahi sana kwa kweli nikiwa na
furaha yangu pale ufukweni watu walikuwa wengi
sana ndipo nilipita palepale.
Tofauti na kuwashangaza watu kwa yale niliyokuwa
nayafanya kumbe pale kulikuwa na semina ambayo
ilikuwa inaendelea. Nilisimama na kusikiliza ghafla
taratiibu akili yangu ilisahau mengi sana ya zamani
na kuona kila jambo la pale kwangu ni geni. Mada
kuu ilikuwa kuhamasisha vijana kujiingiza kwenye
swala la uvuvi. Samaki ni wengi ila wavuvi hakuna
na bahari ni kubwa. Katika wachangiaji ndipo mama
mmoja.
Alisema yule mama kumuambia kiongozi yule.
"Mkuu! Hapa alikuwepo kijana mmoja anaitwa
Mnalii huyu ndie Mvuvi mzuri zaidi ya hawa wa
sasa..."
"Mama unaweza kutuambia huyo kijana anakaa
wapi?.." kiongozi alisema. Mimi nilikaa pale nikiwa
hata jina langu silijui maana wanamtaja mnali na
mimi namshangaa ni yupi. "Mkuu huyu alipatwa na
matatizo akapotea baharini ila inasemekana karejea
ila haijulikani wapi anaishi kwa sasa..."
Palepale kelele za watu walioniona wakapiga kelele
Mnalii huyi hapaaaa!... niliduwaa na mimi kugeuka
kumtafuta mnali yuko wapi bilabkujua kuwa ndie
mimi...."
 
SEHEMU YA THELATHINI NA NANE 38
ENDELEA.........
...Zile kelele zilinifanya nishtuke sana hasana
nikishangaa kuona wale wananitumbulia macho na
mmoja akisema. "Ni huyu hapa, tuliekuwa
tukimtafuta...". Ukimya ulitawala pindi pale
nilipowauliza nini ambacho wanakitafuta kwa
sababu sikuwa na hata kumbukumbu yeyote
kichwani mwangu.
Walizidi kunizonga pale ndipo yule kiongozi
akaomba nipelekwe mbele yake huku watu
wakinipigia makofi. Wakati huo sina shati nina
kikaptula ambacho kinatoa harufu mbaya sana kiasi
hata wale wa karibu yangu waliziba hata pua kwa
ajili ya usalama wao. "Sasa hatuna budi kumpigia
makofi ya ushindi kwa pamoja.." walinipigia makofi
ambayo kwangu yalikuwa kama mchanga
uliochanganywa na cement pamoja na kokoto na
kutia maji kisha kuchanganya kwa pamoja.
Nilijishtukia hata nguvu ya kutaka kusema jambo
nashindwa japo akili yangu kwa mbali nakumbuka
kama kweli nilishawahi kuwa mvuvi ila sijajua ni
kipindi gani. Ilipita muda kadhaa baada ya
maongezi yule kiongozi aliomba aondoke na mimi
baada ya yeye kutambua kuwa sina hifadhi yeyote
kwa ule muda.
Kila kitu kwangu niliona ni kigeni hasa yale maeneo
ambayo ndio yalikuwa maarufu kuyatembelea lakini
niliona kama kwenye ndoto kwangu. Safari hii
iliweza kunifikisha moja ya nyumba safi sana ya
kifahari zilizopakana kama nyumba tatu mstari
mmoja. Hapo akili yangu iliwaza kama nilishawahi
kupita haya maeneo lakini wapi inagoma kabisa.
Kila nikijitahidi wapi inagoma tu. Tuliingia ndani,
nikafikishwa sebuleni ambako nilikuta vitu vya
thamani vikizunguka kila pande ya ule ukumbi.
Nifika na kutaka kukaa kwenye kochi lakini
nilishikwa mkono na mmoja wa wafanya kazi huku
akinihitaji nielekee mahali. Yule mama mheshimiwa
alimueleza yule mfanya kazi wa kike kuwa
ahakikishe nimeoga na kunipatia nguo pamoja na
chakula. Ilipita majira ya masaa kadhaa ndipo kila
kitu niliweza kukifanya pale na ndipo nikatulia
kwenye kochi huku nikiangalia televisheni iliyopo
mbele yangu pale.
Masaa kadhaa chakula kililetwa na tayari kwa
kuliwa. Chakula kilikuwa kizuri lakini kwangu ilikuwa
kama ni adhabu kubwa sana kukila kwa kuwa kila
nikipitisha chakula kinagoma mpaka nikafikia hatua
natapika kabisa. Basi walijua kuwa nina homa ndipo
wakanibeba kwenye gari moja kwa moja hadi
hospitali moja maarufu ambayo nakumbuka mara
kwa mara niliwahi kwenda hapo. Nilichukuliwa
vipimo na mdada mmoja hivi ambae sikuweza
kumuangalia usoni kutokana na mazingira yaliyopo.
"Nesi hakikisha huyo mgonjwa anapaa matibabu
sahihi sawa...?", alisema yule mama kiongozi
akimueleza yule nesi aliyekuwa akinipa matibabu.
"Usijali mama huyu namtibia vyema kwa kuwa
namfahamu vizuri.", kauli yake ilinipa mshtuko
kidogo ndipo nikainua uso na kumuangalia lakini
simkumbuki. Kila nikitaka kumuuliza swali mwili na
nafsi vinakinzana nashindwa kabisa. Ndipo mama
yule akashtuka akamjia na kumshika bega.
"Nesi...umesema unamfahamu huyu eehee!
Mlionana wapi na unamjuaje..maana unaweza
kunisaidia jambo kupitia afya yake". "Hamna mama
utani tu lengo kukuondoa wasiwasi tu kuhusiana na
huduma ya mgonjwa wako..", "mh! Nesi haya basi
fanya hivyo mimi nakuja baada ya muda
kumuangalia".
Yule dada Nesi mambo aliyokuwa akiyafanya mengi
kama nayakumbuka alafu yananitoka. Alikuwa
kavalia jezi zake za kazi ajabu akavua lile jezi
akabaki na nguo za kawaida ambazo anaweza
kutoka nazo nje, kwenye mkono wake kuna alama
kama kitu cha duara kilichochomwa na moto au
rangi nyeusi ya moto ikaacha alama, kwa
muonekano ni nzuri sana ile alama, nikamuuliza
"dada hii alama yako ni nzuri sana nimeipenda
hongera.." akacheka sanaa "haaah! Haahaaa!
Hahaaa!... mnali unanichekesha". Akanitaja na jina
palepale. "Khaa! Nesi unacheka nini na
umenifahamu vipi".
"Khaaa! Wewe usifahamike, nakufahamu vizuri sana
pia mbona hata wewe hongera inakupasa maana hii
alama unayo kwenye huo mkono wako kwa chini".
Nilipindua mkono wangu nikaiona ile alama khaa!
Hapo nilipatwa na mshangao akili yangu iligubikwa
na vikwazo vya mawazo mazito sana juu ya
kutambua kipi kinachoendelea pale.
Nilimtazama kisha nikamuuliza swala la
harakaharaka. "Wewe ni nani.....?".
"Mnali... unataka kunijua mimi ni nani?"
"Ndio nataka kukufahamu na kwa nini hii alama iwe
kwako na kwangu sisi ni akina nani?". Yule Nesi
alisimama kisha akavaa ile jezi yake kisha
akasema. "Muda wangu wa kukaa hapa umekwisha
tutaonana kesho kwenye nyumba ya mheshimiwa
mkuu wa wilaya...ila mimi ni mtu wa kawaida tu
kwa heri.." akachukua vifaa akatoka ndani mule.
Aliniachia maswali kadhaa huyu ni nani na kwa
nini..niliangalia ile alama kweli ninayo na haifutiki
kabisa. Ghafla anaingia nesi mwengine tena. "Kaka!
Samahani...unaitwa". Alichukua daftari kisha
akasoma jina langu. "Mnalii...!" "Ndio.. ni mimi".
Akachukua vifaa vyake kisha akachukua tena lile
daftari na kuanza kuniambia.
"Kaka pole kwa kuumwa. Dokta kaniambia kuwa
unasumbuliwa na homa kali sana pia joto lako la
mwili haliko sawa na lile la kawaida unatakiwa
kufanyiwa matibabu ya ziada ili kuuweka mwili
wako sawa..ila hapa nitakufanyia baadhi ya vipimo
tu..!". Nilijiuliza vipimo vipi tena nifanyiwe hali ya
kuwa tayari nimefanyiwa?.
Baada ya masaa kadhaa yule mama alikuja na
kunichukua. Tukiwa kwenye gari alinihoji baadhi ya
maswali. "Kijana umesema unaitwa nani?.." aliuliza
"Naitwa Mnali". "Kwani maisha yako yakoje mpaka
uko na hali hii!.." "Sijui kwa kweli hata kitu kichwa
changu tu kinauma sana". "Haya una mke na
mtoto?" Hapo nilitulia kwa muda sana. Nikawa
nakumbuka sana nawaza na kuwazua kama kweli
maana kumbukumbu zote zilipotea.
"Nahisi kama nina mtoto....", kweli mnali unahitaji
upatiwe matibabu ya ziada sana. Nina kazi ya
kufanya na wewe ila nitajitahidi kukuhudumia ili
unifanyie kazi yangu. Tulipofika kwake tuliingia
ndani ndipo nakutana na watu wawili binti pamoja
na mdada wa makamo yangu. Yule binti alikimbia
na kuja kwangu huku akilia kwa furaha isiyo ya
kifani. "Dady!!....father I miss you...babaaaaa!"
Huyu ananiita baba ni nani alikuja kunikumbatia
pale huku nikimshangaa sana. Yule mama alimshika
mkono yule binti kisha akamuambia nendeni
mkapumzike kisha kesho njooni akituliza akili yake.
Tuliingia ndani kisha akaanza kunieleza mambo
mengi sana ambayo baadhi yalisababisha kujua vitu
kiuchache wake tu. Ilipita siku kama tatu hivi majira
ya usiku ndipo nilipata kuota ndoto ya mwanangu
akija kunikumbatia na mimi nikamkana. Ndoto
iliendelea hadi pale hospitalini nikimkumbuka yule
dada na ile alama. Ghafla nilisikia nikiitwa na mtu
na ndipo nikakatiza ile ndoto na kushtuka sana.
"Mnaliii....huu ni mwaka wa tano sasa. Hamna
ulichofanya chochote..mimi ni mjumbe kutoka
Kisiwani. Unatakiwa kufanya yale ambayo ulimuahidi
mkuu wetu bila hivyo jeshi litakuja kuingia duniani
na kusambaratisha watu wote wanaotembea
baharini. Na tutaifunga bahari isifanyike shughuli
yeyote...Pia epuka kumueleza yeyote kuhusu hili
kama ahadi yako ulivyoiweka mwenyewe"
"Mamaaaaaa!... palepale nikakumbuka kuwa mimi
ni nani na nilikuwa wapi...lakini niliambiwa nini
nifanye na je? Nini kuhusiana na Kisiwa hiko.
Kwangu ikabaki kama maswali tu ambayo
majawabu yake yalisubiriwa matukio ya baadae.
Usiku huo sikulala kwa kweli mpaka asubuhi na
mapema ndipo anakuja Yule mama huku
akinishangaa.
"Mnali.. umepata wazo lolote!.."
"Ndio..."
"Eheee nieleze.." alitaka nimuambie. Mimi
nilikumbuka kuwa nisimueleze chochote mtu
yeyote. Nilijiuliza nitamuambia nini ehee! Ndipo
nikakumbuka kuwa niluota kuhusiana na mwanangu.
"Mama! Nimekumbuka kuwa kuna mwanangu
alikuja kunikumbatia huku akiwa analia.."
"Mnali ewaaaaa! Sasa akili yako inarudi sawasawa.
Sasa yule ni mwanao na yule aliyekawa mkeo.
Wanaishi hapo nyumba ya mbele. Kwa hiyo sasa
unatakiwa uwe unakumbuka zaidi ili lengo hata
ninapotaka tufanye jambo muhimu ukiwa
unakumbuka ehee! Vipi yule Nesi unamfahamu vipi."
"Mimi simjui kwa kweli yule Nesi hata mimi nilikuja
kushangaa kuniambia ananijua". Wakati nachukua
glass ya maji tule mama aliiona ile alama yangu
kwenye mkono "Mnali heee! Ngoja kwanza hii
alama ni ya nini mbona kama..." niliificha kwa
haraka lakini ajabu zaidi alitoka kuelekea chumbani
kwake. "Ngoja nikachukue kitu.......".
Je? Nini anakwenda kuchukua.
 
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA 39.
ENDELEA..........
.......Yule mama alitoka pale nilipo kisha akaelekea
chumbani kwake na baada ya dakika chache tayari
alirufi akiwa na kitabu kimoja hivi. Kilionekana
kama ni cha zamani sana kile kitabu maana
kilikuwa na uchafuchafu. "Sasa mnali mimi nataka
nikusaidie jambo hapa ili hata uweze kuwa salama."
Alisema mama huyo. Mimi nilibaki kumkodolea
macho kwa yale ayasemayo.
Alifunua baadhi ya karatasi hadi sehemu moja
akanipatia. Kulikuwa na picha yenye alama kama ile
niliyonayo mimi, lakini pia kulikuwa na baadhi ya
picha ambazo zilionyesha sehemu za ajabuajabu ila
kama kuna mahali napakumbuka hivi. "Mnali!
Umegundua nini?" Aliniuliza "hapana sijagundua
chochote hapa" niliweza kumjibu. "Maana ya
kukuonyesha hii alama fahamu kuwa alama hizi ni
za hatari na zinapatikana sehemu za baharini na
wamiliki haswa ni majini, kwa historia hii ni milki ya
majini ambayo ipo pembezoni mwa bahari yani
kisiwa cha maajabu." Nilivuta pumzi kidogo kisha
nikamuacha aendelee " Ukibahatika kufika hapa
inasemekana kuwa mali nyingi utazipata"
nilimuangalia kwa makini "sasa mama unataka
nikusaidie nini labda". Ujasiri nilioupata kumuuliza ni
pale baada ya kuanza kupata taarifa kuu ya hii
alama "pia ina maana kila mwenye hii alama
inakuaje yani?". Nilimuuliza mama huyo. "Ina maana
kuwa wewe ni mmoja wa wafuasi wa hao kwa
namna moja ama nyingine hivyo basi Mnali
uniambie ilikuaje mpaka ukapata hii alama?".
Nilivuta taswira lakini nashindwa kukumbuka kabisa
"hapana sina kumbukumbu yeyote ile ambayo
ninayo". Basi tuliachana na hayo mada nyingine
ikaingia. "Sawa mwanao anakuja hapa sasa hivi sijui
kama unamfahamu." Kabla hajamaliza mlango
unagongwa Ngongo ngoo!! Ngo! Ngo! "Kuna mtu
anataka kuingia.". Alifunguliwa na hakuwa mwingine
ni yule binti na mama mmoja hivi. Baada ya muda
kusonga maongezi yetu yalifika tamati na hawa watu
na kuja kutambua kuwa mimi ni baba wa huyu
mtoto. "Mnali! Unajifanya umesahau mimi niliekawa
mkeo na huyu mtoto wako, je? Ile siku nilikumwagia
maji ya ukoko wa ugali umesahau.." Alisema yule
mwanamke kwa kweli kumbukumbu imepotea
kabisa. "Mama usimlaumu huyu ana tatizo la
kumbukumbu kwa kuwa matatizo aliyoyapata
nadhani hamyajui ndio maana ila taratiibu ataelewa
kwa msaada wenu utatusaidia kurudisha
kumbukumbu zake na akawa sawa kama mwanzo"
alisema yule mama. "Baba mimi mwanao
Asante...." nilishtuka sana baada ya kulisikia jina hili
yani vyote vimepotea kwenye kumbukumbu lakini si
hili jina la mwanangu. "Eeeeeh! Asante mwanangu!
Utanisamehe bure nimepoteza kumbukumbu sijui
nini kinaendelea ila kamwe mwanangu siwezi
kukusahau." Tulikumbatiana na mwanangu Asante
ambae kwa sasa ni binti mkubwa kabisa. Ilipita
masaa kadhaa yule mwanamke ambae alikuwa mke
wangu aliondoka kwa kuwa kaolewa na mwanaume
mwengine mwenye mali na akaniacha mimi na
mwanangu tukiongea mengi. "Baba kwani Baba
Kibona yupo kulekule?". Alisema Asante akiwa
ananiuliza "Kibonaa!!!..." niling'ata kidole. "Ndio yule
ambae alikuwa anakufundisha Uvuvi alafu mama
akawa anakukataza!". Nilivuta picha wapi sikumbuki
"mwanangu tuyaache hayo kwanza habari ya miaka
mingi" tulizidi kuongea wakati huo yule Mama
aliyenichukua akiwa anaendelea na shughuli zake.
BAADA YA MWAKA KUPITA
....Siku moja ilikuwa Juma tatu ambapo ni siku
maalumu kwa Mheshimiwa kama yule kwenda
kazini. Mama huyo aliyejulikana kwa jina la Mama
Penina aliniaga kuwa anaelekea kazini aliniacha
nikiwa peke yangu. Kwa kawaida nilishazoea kuwa
mwanangu huja kunisalimu pale mchana hadi jioni
kisha anaondoka. Maisha niliyoishi yalinifanya
nisahau shida kabisa. Kutokana na upweke nilionao
ulinifanya nielekee sebuleni wakati huo mfanya kazi
yupo jikoni huko. Nikiwa pale sebuleni ghafla
nilihisi kama tetemeko linasumbua kwa kasi ya
ajabu mara ghafla masikio yangu yanapata kusikia
sauti kali inayonizibua kabisa masikio na kufanya
ngoma za masikio kupata hitlafu ya muda.
Haikuishia hapo ndipo mwili ulianza kulegea kama
kambare ashikwapo toka matopeni. Mdomo wangu
ulikuwa kama nimebeba zege sinyanyui hata kidogo.
Ikawa sasa sisikii sisemi sichezi nikawa
nimeparalaizi kwa muda. Ndipo mingurumo na
misauti niliyokuwa naisikia vilikata punde tu, na
ndipo kukabaki shwari lakini sikuweza kufanya
jambo lolote. Nilisikia vishindo vya mtu kuingia
ndani. "Mnaliiii!!!. Nimekuziba masikio unisikilize
mimi, nimekuziba mdomo ili usipate kunijibu
chochote nimepata kudhoofisha mwili wako ili
usilete upuuzi wowote...Nadhani Salfa alikujia
mwaka uliopita ukiwa hospitalini na akakujuza
jambo sasa tekeleza vile tunahitaji". Baada ya neno
hilo aliondoka na mimi ndipo hali yangu ikawa
inarejea tena. Nilivuta pumzi jasho likinitoka nibaki
kujiuliza ni kazi gani nilipewa mpaka wananifuata
hawa watu. Majira ya jioni alirudi yule mama kisha
akaomba akae na mimi pamoja ili apate kujua
mengi. "Ehee! Nini kinaendelea au nipe habari
kuhusiana na Kisiwa ambacho kipo mbali na hapa".
Alivyoeleza ndipo nikakumbuka na lile jina la Salha
basi pale nikaanza kurejesha kumbukumbu zangu.
"Naomba uniache nitulie kesho nitakupa jibu kamili".
Nilimuacha nikaenda kulala maana nilikuwa
nimechoka sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom