Simulizi: Maisha Yangu Ya Uvuvi

bioto

JF-Expert Member
Oct 1, 2017
1,261
2,095
RIWAYA:: MAISHA YANGU YA UVUVI
MTUNZI:: Author Mudhihili
SIMU:: 0652667153
LINDI-RUANGWA
SEHEMU YA KWANZA 01
ENDELEA..............
.................Niliweza kuishi Maisha ya tabu baada
ya kufukuzwa kazi ambayo niliamini kuwa ndio
kitegemea uchumi wangu. Maisha yangu kiukweli
nilishindwa kuendelea kwa kuwa Nilishindwa
kumudu familia niliyonayo. Nilibahatika kuwa na
watoto wawili nikiwa na mke wangu.
Baada ya kukaa kwa muda mrefu sana ndipo siku
moja mke wangu aliniita. Nilienda kumsikiliza pale
alikoniita.
"Mume wangu nina jambo nataka kukushauri".
Moyo wangu uliahtuka baada ya kuona jambo la
ajabu sana kwa mke wangu. Kwani sikubahatika
kupata neno kama hilo kutoka kwa mke wangu.
"Ehee! Nakusikiliza mke wangu nambie".
Nilimuelea huku nikikaa vyema ili nipate nipate
kunsikiliza vizuri.
"Unajua kuwa mpaka sasa tuna maisha magumu
sana pia, mtoto wetu hapa anahitaji ada ya
shule...unaonaje ukatafuta kazi".
Mke wangu aliniambia.
"Kiukweli, Mke wangu jambo ambalo unaliongea
limeniingia akilini kabisa, ila sasa nilikuwa nawaza
kazi gani ambayo itaniwezesha kupata Fedha kwa
muda mfupi ili nifanikiwe na kujikwamua na maisha
haya?"
Nilibaki nikiduwaa baada ya kumueleza jambo lile.
"Sawa ila kumbuka kuwa Mtafutaji hachoki na
akichoka basi kapata, sitaki nikuvunje moyo tafuta
kazi yeyote halali pia mafanikio hayaji kwa wepesi
kama unavyofikilia jitihada zako ndizo zitafanikisha
kupata yale uyatakayo, kikubwa sisi tutakuombea
mungu na utafanikiwa kabisa".
Maneno ya Mke wangu, yalinifanya nijione kuwa ni
mtu wa kipekee kabisa.
Nilijiona sasa mwenye nguvu na kuamini kama
kweli nina mke ambae anapenda sana mafanikio
yetu.
Nilimpa moyo kuwa nipo tayari kufanya kazi yeyote
halali ambayo inaweza kunipatia kipato cha halali.
"Mke wangu hakika nakushukuru, wewe ni mke
ambae unajua majukumu yako ndani ya familia hii
nakuahidi kuwa naelekea sasa hivi kwa bwana
Kibona nadhani nikirudia nitakuwa na akili mpya".
Nilimuacha Mke wangu akiwa anaendelea
kunisindikiza kwa macho yake yaliyojaa mapenzi na
huruma. Safari yangu ilifika hadi kwa bwana Kibona.
Nilimfika hadi kwa bwana Kibona, nilimkuta
akitengeneza Mtumbwi wake vizuri. Kwa maisha ya
Pangani ambayo niliyazoea kama huna elimu basi
utaishia kuvua samaki mtoni au baharini.
"Bwana kibona, habari yako ndugu naona hapo
mambo yamepamba moto".
Nilimsalimu.
"Eeeh! Ni kweli ndugu bwana karibu sana nilikuwa
namalizia hapa kutengeneza huu mtumbwi kisha
nifungefunge nyavu yangu hapa kisha baadae
nielekee kazini".
Nilitamani sana ile kazi japo nilikuwa na uwoga
nayo mwanzo. Kitu ambacho nilikuwa nina hofu
kubwa kutokana na maji ya bahari aikupenda kua
karibu nayo kwa kuwa sikujua hata kuogelea.
Bwana Kibona alinikaribisha kwa bashasha sana
ndipo nilipomsogelea na kuketi karibu na yeye.
"Ndugu yangu kama unavyofahamu kuwa tangu
niache kazi yangu kule nina muda sasa, na halo
yangu kama unavyoifahamu sina hili wala lile
nilikuwa naomba sasa unishauri au hata kunipa
kibarua katika kazi zako hizi ili niweze kupata
chochote kitu."
"Mh! Teh teh teh! Teh......bwana unanishangaza
sana.."
Alikuwa anacheka baada ya kauli yangu kumueleza
kuwa nipate hata kibarua kupitia kazi yake ya Uvuvi.
"Sasa unacheka jambo gani?" Nilimuuliza
"Unajua, bwana Mnali ukisema kuwa nikupe kibarua
unanishangaza sana kwa kazi gani hapa...sema
tuungane tuifanye kazi hii kwa pamoja na si eti
nikupe kibarua..."
Nilimshukuru sana maana niliona sasa matumaini
yangu ya kuendelea kuishi vyema mimi na familia
yangu ilionekana. Niliondoka pale na kunyoosha njia
ya nyumbani huku nikiwa na Imani kubwa sana ya
kupata kazi kupitia kwa bwana Kibona.
Nilipofika nyumbani nilimuita Mke wangu kisha
nikamueleza kwa kila kitu ambacho kiliendelea
mimi na Kibona.
"Mke wangu ndio kama hivyo nimeongea nae na
kazi yenyewe ni Uvuvi........"
Nilishangaa kumuona mke wangu akikasirika baada
ya kumueleza kuwa kazi ya uvuvi. Ilinibidi nitumie
nguvu ya ziada kuendelea kumuuliza na kumtuliza.
"Sasa...wewe umenishauri nitafute kazi lakini mbona
sasa umebadili na uso?"
"Ndio ile kazi mbaya bwana Mtu mwenyewe hujui
hata kuogelea kabisaaa ukidondoka humo ndani ya
maji nani atakuokoa...tafuta nyingine".
Maneno yake yalionyesha hali ya ukakasi kwangu
lakini sikuwa na jinsi ilibidi nilazimishe lakini bila
hata yeye kujua, niliamua kufanya kazi ile mpaka
pale nitakapohisi nina uhitaji wa kutafuta nyngine.
"Sawa mke wangu ila itakubidi uvumilie mpaka
niikpata........"
Majira ya jioni bwana Kibona aliniambia kuwa nifike
kule kwake. Nilielekea na nilimkuta akiwa
anamalizia kupanga shughuli zake. Baada ya
kumaliza alinijia na kunikamatisha vifaa kadhaa
ikiwemo Magunia yaliyowekwa kwenye ndoo.
Nilibeba zile ndoo huku akili yangu ikiwaza
nyumbani kwa mke wangu pindi atakapojua kuwa
nipo baharini.
Yote niliyaacha na nikafanya kile ambacho kipo
mbele yangu. Tulifuatana hadi baharini muda
ulikuwa jioni sana na kiza kilianza kuingia zaidi.
Tulipofika sehemu hiyo bahari ilikuwa shwari kabisa
mawimbi hayakuwa makubwa sana yalikuwa
madogomadogo. Tulikaa kusubiri muda ufike usiku
hapo ndipo aliponielekeza mambo kadhaa.
"Ndugu yangu umekubali kufanya kazi hii lakini
fahamu kuwa inahitaji uvumilivu sana,juhudi pamoja
na ushujaa......kuna kukosa na kupata".
Baada ya hayo maneno ndipo tukaelekea kwenye
mtumbwi.
Safari ilianza kufika kwenye kina kirefu cha bahari.
Niliwasha chemli ndipo tukatundika nyavu kisha
tukatulia. Kibona alikuwa mzoefu mimi nilikuwa
muoga sana hata kusimama pale kwenye mtumbwi.
"Ukijifanya muoga haki ya nani utaishia humuhumu
ndani ya Maji kuwa makini". Kibona hakuwa mzito
alinieleza ukweli kabisa uliotokana na uoga wangu.
Baada ya muda tukaanza kuvuta nyavu na hatimae
samaki wakubwa wakubwa tuliwakamata.
Tulifika ufukweni na kutupa nyavu iliyokawa nzito
sana.
"Eeeeeeh!, hakika leo ni maajabu sana sijawahi
kupata samaki wengi kama hawa tangu nianze kazi
hii tena wakubwa sana...."
Alinishangaza kiasi kwamba nikajihisi kuwa mimi ni
mtu mwenye bahati sana. Muda ulikuwa umekwenda
ndipo Kibona aliniruhusu nifike nyumbani kisha
adubuhi na mapema niweze kurudi kwa ajili ya
kuangalia Mapato.
Kwa kawaida baada ya kuwapata samaki basi
wanunuzi wengi sana wanajitokeza pamoja na zile
biashara za kuagiza ambazo ndio nyingi sana.
Niliondoka majira yale japo yalikuwa magumu sana
yani muda mbaya. Nilimuodikia Mke wangu. Kumbe
alikuwa hajalala alikuwa ananisubiria mimi.
Alifungua mlango, niliingia nilimsalimu lakini hata
hakuitikia. Nilichofanya nikaelekea chooni haraka
nilioga kisha nikarudi kitandani. Mke wangu alinijua
kuwa natoka baharini kutokana na harufu ya samaki.
Asubuhi na mapema bado alikuwa kanuna japo
nilijua kipi kimemfanya anune.
"Mke wangu nitarejea muda si mrefu"
Japo nilimuambia lakini hata hakujibu. Nililazimisha
kuondoka asubuhi hiyo kuelekea kwa bwana kibona.
Nilimkuta tayari kashafanya biashara na akanipatia
kiasi cha pesa na ndipo nikarejea nyumbani.
 
SEHEMU YA PILI 02
ENDELEA.................
................Nikiwa na furaha ya kupata kipato kizuri
kama kile ambacho sikutarajia kabisa. Nilitembea
njiani nikiwa na faraja moyoni mwangu pia nikiwa
na shauku kuwa mke wangu atafurahi mimi kupata
ile pesa yenye kutosheleza mahitaji yangu.
Lakini ilikuwa ni tofauti kabisa na vile nilivyotarajia
kwa mke wangu kwani pindi aliponiona tu ndipo
alizidi kukasirika. Nilifika pale nyumbani kisha
nikachukua kiti na kuketi karibu pale alipo mke
wangu, lakini yeye aliondoka pale alipokaa na
kuingia ndani. Kiukweli aliniumiza akili sana kuwaza
mke wangu anahitaji jambo gani zaidi na kibaya
kipi nilichofanya.
Nilinyanyuka na kuelekea kule chumbani ndipo
nilimkuta akiwa kajilaza kitandani hana hata hamu
ya kuonana na mimi. Nilijiuliza mwanamke wa aina
gani ambae hataki hata kunielewa, wanaume wengi
huwa tunapata tabu sana kwa wake zetu pindi hali
inapokuwa ngumu ya kimaisha inafikia hatua
mwanamke anafanya vituko vya ajabu ili umzingue
kama kumpiga apate sababu ya kuondokea kwako.
"We!..weweee!" Nilimshtua kwa kumshika mgongo
wake ili apate kunisikiliza japo alikuwa kimya kama
kobe aliyeonewa.
"Mke wangu....ebu! Kaa tuongee...!"
Niliendelea kumuamsha.
"....Aaah! Sitakiiiii wewe si kiburi sana siku hizi
endelea...". Aliwaka kama kifuu na ikawa ngumu
kumzima. Niliona ushenzi kabisa kama huu
siupendelei kabisa.
Niliujua udhaifu wa mke wangu, pindi akinuna najua
nini nimfanyie.
Nilinyanyuka ndipo nikaamua kumuita mtoto wangu
mmoja aliyejulikana kwa jina la Asante. Mtoto huyu
ni wa kwanza kabisa kuzaliwa na niliamua kumpatia
jina hili kutokana na matatizo kadhaa ambayo
yaliyotokea ndipo nikabahatika kwa kumpata mtoto
huyo na ndipo niliona nimpatie jina la Asante.
Nikimaanisha nikimshukuru mungu.
Nilimpa kiasi cha fedha kisha nikamuagiza
akanunue mboga pamoja na mchele wa kutosha,
kutokana na maisha ambayo tulikuwa tunaishi
kununua kiasi kama kile cha mchele kiliweza
kumshangaza sana Mama Asante.
Baada ya Muda alirejea kisha nikampatia mke
wangu.
"Mama Asante, haya pika kwanza kisha tuongee
vizuri hali tumeshashiba."
Alipokea japo kwa shingo upande akayafanya
maandalizi tosha kwa ajili ya mapishi. Alipomaliza
tulikula wote hapo ndipo niliona furaha ya mke
wangu ikijitokeza mbele yangu. Nilimshika mkono
na kumpeleka kitandani kisha nikamuangalia kama
mara tatu.
Baada ya kumtazama ndipo nilipombusu na kumpa
maneno mazuuri ya mapenzi. Hakika hakuna ambae
nilikuwa nampenda kama mke wangu kwani
tulikuwa tunapendana na kuhurumiana.
"Mke wangu, nakuomba uvumilie kazi ya Uvuvi
nahisi ndio chaguo langu kutokana na uhaba wa
elimu na uwezo tulio nao nakuomba ubariki kazi
yangi hii ambayo inatupatia kila kitu.
Baada ya hapo ndipo tulikubaliana kuwa mimi
niendelee kufanya kazi na yeye akawa ananibariki.
Siku hiyo mapema nilitoka nikiwa na furaha sana
baada ya Mke wangu kukubali mimi kufanya kazi.
Niliondoka hadi kwa bwana Kibona, bwana kibona
nilimkuta anaandaa nyavu kwa ajili ya kazi.
Nilimsaidia kufanya maandalizi hayo ili iwe rahisi
kumaliza jioni tuondoke kwa ajili ya kazi.
Nilikuwa na furaha, nilifanya kazi huku nikitabasamu,
nilifanya kwa morali mpaka bwana Kibona
akanishangaa.
"Mnali kipi kinakufurahisha hivyo"
Aliniuliza swali.
"Mimi nafurahi kwa kuwa naenda kufanya kazi"
Niliweza kumjibu kwa kujiamini kabisa.
"Haya ila furaha yako iwe ya kheri japo kule
hakutabiriki...ulishawahi kusikia stori au hadithi za
bahari pamoja na huu mto pangani?"
Swali lake lilikuwa gumu kwa kiasi chake kwani
eneo la pangani kwangu lilikuwa ni geni sana hivyo
kauli yake ilinishitua kwa kiasi chake.
"Mh! Bwana kibona unajua kuwa wewe ndie
mwenyeji mimi tangu niamie hapa nina muda wa
mwaka mmoja tu! Sasa kuhusiana na mto huu
pamoja na bahari hii hapana sifahamu kabisa."
Nilimueleza ukweli kwamba sifahamu chochote
kuhusiana na yale maeneo.
"Haya! Ina sifa nyingi sana kwa miaka ya babu
yangu akiwa anafanya kazi hizi aliweza kunihadithia
kipindi ananifundisha njia za uvuvi, kuna ule wa
kupata samaki wengi na kuna ule wa kupata samaki
wachache".
Aliongea bwana Kibona.
"Mh! Natamani kujua hizo aina mbili za uvuvi na je?
Sisi tunafanya uvuvi wa aina gani?"
Niliweza kumuuliza.
"Aaaaah! Ahsante kwa swali zuri sana, uvuvi wa
kupata samaki wengi tunatumia nyavu zenye
matundu madogo na kutumia mabaruti kwenda
kupiga chini ya bahari kwenye mazalia ya samaki
kisha tunawakusanya huku juu, hapa tunapata kila
aina ya samaki wadogo kwa wakubwa. Pia wa
kupata samaki wachache basi tunatumia nyavu
kama hii tunapata samaki wakubwa tu kama
unavyowaona wale wa jana".
Maelezo yake yalinishangaza sana. Jioni ilifika
ndipo tukaingia ndani ya maji tukatega nyavu zetu
kisha tukasubiria kuna wale ambao tuliwapata kwa
Ndoano japo wachache sana, muda ulipowadia
tulivuta nyavu mpaka ukingoni mwa bahari
tulichambua lakini tulibahatika kupata samaki sita tu
tofauti na siku zote. Tulifanya kazi ngumu yenye
ujira mchache.
Kibona alinieleza mengi sana kuhusiana na ile hali
kuwa niivumilie tu.
Ilipita kama Miezi mitatu sasa. Siku moja ya mwezi
Nilikuwa Naumwa sana Kibona alikuja kuniangalia
nahukuru. Ndipo alipotaka kuondoka kwenda mtoni.
"Sasa...nimesikia leo bahari imechafuka sana lakini
nyumbani hakuna mboga wala fedha ya kula".
Aliniambia hayo huku akiwa ananishika mkono.
"Daaah! Bwana Kibona ni bora ukae nyumbani kama
bahari imechafuka sio vyema kwenda huko kabisa".
Rafiki yangu aliniambia huku akinisisitiza kuwa
lazima aende huko ili akapate chochote cha kula.
Mimi sikuweza kumkataza kwa sababu yeye mzoefu
pia ni maarufu.
Tuliachana pale mimi nikiwa kitandani. Nakumbuka
siku hiyo ilikuwa ya Majonzi bwana Kibona
kutomuona tena. Habari iliyosikika ni kuwa Kibona
Kapotea Baharini hakika iliniuma sana......
 
SEHEMU YA TATU 03
ENDELEA........
..................Ilikuwa ni pigo kubwa sana baada ya
kupata taarifa ya Kibona kupotea Ndani ya Bahari.
Sikuwa na raha kutokana na hali ya mwili wangu
haukuwa vyema kabisa. Baada ya miezi kadhaa
nilipata nafuu lakini matatizo mengi pale nyumbani.
Nilianza kutafuta sasa jinsi gani naweza kujitatua na
matatizo yangu niliyonayo. Kutokana na hali ya
kukosa pesa ya kuihudumia familia yangu ndipo
chokochoko kwa mke wangu.
Hapo ndipo alipoanza kubadilika, sikudhani kama
anaweza kubadilika kwa kiasi kama hiki, kwanza
maongezi yalianza kukata kati ya mimi na mke
wangu, alianza kugoma sana hata kuongea na mimi
hapendi kabisa.
Nikitoka nyumbani basi na yeye anatoka kurudi
alianza kurudi usiku lakini anarudi akiwa na mboga
pamoja na Mchele. Nilikuwa sina nguvu ya kufanya
kazi ngumu ambazo zingeniwezesha kupata kipato
cha kuhifadhi familia yangu.
Nilizidi kuumia sana zaidi ya maelezo majibu ya
mke wangu yalinionyesha dhahiri kuwa sasa
kanichoka kabisa. Hata nikihitaji haki ya ndoa lakini
nilinyimwa huku akisema kuwa kachoka sana.
Nilijaribu kupata hata ushauri wa Marafiki zangu
nipate hata ushauri. Mwili wangu ulikosa nguvu
kutokana na maradhi niliyokapata. Niliamua
kumfuata Dada mmoja alikuwa rafiki wa Mke wangu
Mama Asante.
"Monika, samahani nahitaji kujua kwa nini mke
wangu anakuwa vile?, siku hizi kabadilika kabisa
nakuomba hata umueleze kama kuna jambo
nimemkosea basi aweze kuniambia labda naweza
kujirekebisha".
Nilimuambia kila kitu ili niweze kupata msaada.
Monika alinionyesha hali ya kutaka kunisaidia baada
ya kunionea huruma kutokana na hali niliyonayo.
Niliondoka na kwenda nyumbani huku nikiwa hoi
kabisa, homa au ugonjwa nilionao sikuufahamu
kabisa kwa sababu sikuwa na pesa baada ya bwana
Kibona kupotelea baharini. Ilipita siku kama mbili
mke wangu hajarudi kabisa nyumbani wanangu
walikuwa wananiuliza sana kuhusiana na mama yao
kutoonekana.
Siku ambayo alirudi alikuwa na hasira sana na kiburi
kikubwa sana baada ya kuona kuwa namtegemea
yeye.
"Mke wangu, haya kulikoni huko utokako siku ya
tatu hii hujarudi watoto wanakuulizia"
Niliweza kumuuliza lakini hakunijibu kitu.
Nilimfuata hadi chumbani ndipo nikamshuhudia
akipanga nguo zake kwenye begi.
"Mke wangu bado hujanieleza kulikoni".
Sikuamini kama Mama Asante atanisukuma na
kuangukia sufuria yenye maji machafu ikafanya
suruali yangu kuchafuka lakini sikuwa na nguvu ya
kusimama kutokana na mwili kutetemeka.
Nilibaki kuumia moyoni huku nikiwa nimechutama
pale chini. Nilijikongoja kidogo kisha nikainuka na
kumsogelea mke wangu. Sikuadhania kabisa kwani
alinikunja shati langu shingoni huku akinisukuma
hadi ukutani nilijigonga na kichwa Tiii!, kama mti
ulioanguka chini, chozi lilinidondoka nashindwa
kumzuia nguvu sikuwa nazo.
"Nakuomba unielewe wewe mwanaume
usiejitambua, siwezi kukulisha hapa kila siku.
Nataka utambue kuwa, nimempata mwanaume
ambae anaweza kunihudumia! Pia usinisumbue na
sasa nakutaka uniandikie Taraka haraka sana laaa!
Sivyooo! Nitakuharibu sasa hivi."
Alipoanza kuongea hadi anapomaliza, sikuwa
naamini kama kweli anaweza kunifanyia haya
anayonifanyia.
"Mke wangu nikuache kwa sababu gani maalumu
ambayo inasababisha wewe kutamka hivo mke
wangu".
Alinipiga kama mtoto vile mpaka nikaanguka chini.
Nilipandwa na jazba nikajikakamua kuinuka kisha
nikataka hata kupambana nae lakini niliishia
kufinywa kipigo alichonipiga hakika sikufahamu
maana maumivu yalinizidi hadi nikatamani kulia.
"Mke wangu Unaniuaaaaaaaah!"
Nililalamika sana. Lakini hakutaka kunielewa ndipo
alipochukua karatasi na penina kunijia pale nilipo.
Alinilazimisha nimuandikie Taraka ili nimuache.
"Andika nitakunyonga...pumbavu wewe".
Basi niliandika Taraka tatu si mke wangu lengo ili
nilinde maisha yangu.
Aliwachukua watoto kisha akaondoka nao.
Sikufahamu wapi kaelekea mimi nilibaki kulala pale
kitandani. Nilizidi kuugulia kutokana na hali
niliyonayo, rafiki yangu Kibona sitomuona tena,
maisha yangu nilitarajia Uvuvi sasa hakuna chochote
ambacho naweza kujitetea ili kupata fedha yeyote
ile. Basi niliamua kukalisha hata uji ili nipate nguvu,
niliyafanya hivyo ili nipate nafasi ya kwenda kutafuta
chochote.
 
SEHEMU YA NNE 04
ENDELEA..................
................Baada ya Miezi kadhaa kupita hali
yangu iliweza kutulia kabisa na kuwa na unafuu,
nilijikuta nikiwa peke yangu ndani ya nyumba yangu
japo nilizoea kuonana na wanangu pamoja na mke
wangu. Siku hiyo nilitoka zangu nikaelekea
nyumbani kwa bwana Kibona ambako nilifanikiwa
kumkuta mkewe ambae yupo akiwa kwenye hali ya
majonzi kama mjane. Nilijitahidi kumtuliza na
kumueleza kuwa ni mapito tu ambayo kila mmoja
anatakiwa kuyapitia.
Ili kumpa matumaini zaidi nilimueleza jinsi mke
wangu alivyonikimbia kutokana na hali ya maisha
yangu. Kadai taraka na niandike kuwa taraka tatu si
mke wangu tena. Hapo ndipo alianza kujishangaa
yeye na akaacha kulia. Mipango tuliyoipanga ni
kuwa nitajitahidi kuishikilia ile familia na
kuihudumia kama alivyokuwa akihudumia
marehemu kibona. Hapo ndipo alinipatia kila kitu
ambacho bwana kibona alikuwa anatumia katika
harakati zake za uvuvi.
Nilijipa moyo kuwa nitafanikiwa na kupata samaki
wengi tena wakubwa sana nilichukua zile nyavu tena
zingine zilikuwa ni mpya kabisa hivo sikupata tabu
ya kutaka kununua nyavu zingine hali ya kuwa mpya
zipo pale. Sikuwa mzoefu sana katika harakati za
uvuvi japo nilikuwa na uelewa nao kidogo nilioupata
kwa muda mfupi ambao tulikaa na bwana kibona.
Maisha yangu sasa yalibaki kuwa ya uvuvi kwani
hakuna jambo ambalo nilikuwa nalitegemea tofauti
na swala hilo.
Siku iliyofuata nilidamka asubuhi kwanza kisha
nikatembelea baharini, lengo kuu lilikuwa ni
kuangalia mazingira ya pale baharini. Ilikuwa kama
majira ya asubuhi sana na kipindi kile ambacho
mvua zimeacha kunyesha karibuni. Kipindi hiko
kilikuwa cha Bamvua la kushitukiza yaani kipindi
cha Majikujaa ambayo yalikuwa yanashitukiza.
Sikuwa nafahamu nilichoelewa ni kuwa maji yatulie.
Kwa mbali nilishuhudia samaki mkubwa akiruka juu
na kuingia tena ndani ya maji. Nilishtuka na nikajua
kitu tofauti na samaki kimemdhuru kumbe ilikuwa ni
kawaida pale aliporejea ule mchezo kama mara
mbili hivi.
Vijana wengine nilipata kuwasikia kuwa ni Papa
lakini mimi sikuwa namfahamu anafananaje huyo
papa. Kidogo majonzi yalipungua lakini nilifahamu
kuwa bado mke wangu ataendelea kuwa kichwani
mwangu lakini ndio basi siwezi kuishi nae tena kwa
kuwa yeye si mke wangu kabisa. Nilikuja kushtuka
muda umekwenda mfukoni nina senti chache
nahitajika hata ninunue samaki kwa ajili ya familia
ya Kibona pamoja na mimi mwenyewe. Kiasi cha
pesa nilichonacho hakiwezi kununua mahitaji ya
pande mbili yani hata kwangu mwenyewe
hazitoshelezi. Ndipo nilipomuendea jamaa mmoja
alikuwa anauza samaki pembezoni mwa beach.
"Habari yako...samaki hawa naweza pata kiasi
gani?". Niliweza kumuuliza ili ninunue. "Hao wote
elfu mbili" Fedha niliyonayo shilingi miatano "basi
naomba unisaidie Samaki hawa nina shida ya
mboga kesho nitakupitishia hapa mimi pia ni mvuvi
nitakupatia pesa yako kesho asubuhi kwa sasa nina
kiasi hiki cha miatano". Nilimshangaa akiwa
ananicheka sana huku akinisikitikia. "Weee mvuvi
wa wapi wewe acha kuingilia kazi za watu sema una
shida usaidiwe lakini usijitie mvuvi....".
Japo na zile dharau aliweza kunipatia wale samaki
ndipo nikaenda kumpatia mke wa marehemu Kibona
na mimi nikawachukua wachache nikarejea
nyumbani. Nikiwa nawaanda nilimkumbuka mama
Asante, mpaka napika nilikuwa namkumbuka yeye,
hakika alinikaa kweli akilini.
Majira ya jioni nilifika baharini nikaelekea pale
ambapo mtumbwi wangu ulikuwa unakaa kutokana
na Kibona alipapenda. Niliuchunguza ndipo
nikaingia na kuanza kupiga kasia zangu kuelekea
kwenye kina kirefu cha bahari ili nitundike nyavu
humo.
Uoga ulinitoka kwa kuwa mimi pekee ndie
nategemewa na familia ya Kibona. Nilifika katikati,
nikafanikiwa kuiweka Nyavu ile kisha nikawa
nimetulia kusoma mazingira na muda wa kuitoa.
Chemli yangu ilikuwa na mafutaa mengi ya kutosha
ghafla nilihisi kama kichwa kinaniuma hivi, kwa
mbali niliona taa za wavuvi wenzangu wakiwa
wansogea karibu kwa kuwa ni kawaida. Nilijikuta
nalala ndani ya mtumbwi wangu usingizi mzito
kweli. Ghafla pumzi nahisi kama zinaniishia ndipo
najikuta mtumbwi maji yamejaa unataka kuzama.
Nilipata hofu isiyo na mchezo. Nilipata ujasiri
nikayatoa kwa kutumia kikombe kilichopo ndani
yake.
Ajabu zaidi pale nilipojikuta niko peke yangu bahari
nzima. Niliyapakua mpaka kuchoka huku nikipiga
kasia kurejea nchi kavu bila kujua kama wavu upo
au laa! Nilipofika karibu na nchi kavu nikasikia
kicheko kama mtu ananicheka mimi. Nilipaniki sana
ndipo nikajikuta najitupa ndani ya maji na kuanza
kutapatapa mpaka nje, nilikunywa maji ya kutosha
ambayo yalinisumbua sana mwilini nilichojua ni
kuutoa mtumbwi wakati huo chemli imedondokea
ndani ya maji.
Sikutamani hata kujua chochote kile tu
kiliniogopesha. Nilirejea nyumbani kabisa usiku huo
huku nikiwa nakumbuka maneno ya Kibona kuwa
baharini kuna mambo mengi kikubwa vumilia.
Nilifika nyumbani nikalala bila kujua ni saa ngapi.
Nilijikuta naingia kwenye ndoto kubwa inayonielezea
mazingira ya bahari na ile net niliyoiacha nikiwaona
samaki wakubwa sana wakiwa wanaingia ndani
yake. Nilizidi kushangaa mpaka pale nilipowaona
wamejaa mpaka net inataka kuchanika na
wanashindwa kutoka. Nilishtuka toka kwenye ndoto
hiyo na kujikuta niko Asubuhi na kichwa kinaniuma
kutokana na yale maji chumvi.........
 
SEHEMU YA TANO 05
ENDELEA.....................
................Baada ya kuamka nilijihisi kama
kaufuraha fulani hivi kwa kuwa ile hali ya kuona
nyavu yangu imejaa samaki wengi nikaona kweli
unaweza kuota ndoto kuwa umejenga ghorofa
kubwa sana lakini ikawa ni tofauti kabisa na
uhalisia.
Niliamka toka pale kitandani, kisha baada ya hapo
nikajiuliza nifanye nini ambacho kitaniwezesha na
maisha yale magumu. Nilinyanyuka nikaelekea kwa
Familia ya bwana Kibona niliwakuta wakila chakula
na mimi nikaungana nao mpaka pale nilipohakikisha
maua ya sahani yanaonekana. Nilipata wazo kuwa
nitembelee ufukweni tena. Nilipofika nikaona bahari
asubuhi ile mapema imechafuka kweli hata kuingia
na mtumbwi kama unajitakia matatizo. Nilijishangaa
napatwa na hamu ya kuchukua mtumbwi na kutaka
kuingia hata hivyo walikuwepo vijana ambao
walikuwa wananishangaa na wengine wakawa
wananisihi kuwa nisijaribu kwenda kwani ni hatari.
"Kijanaaah!. Acha kabisa hayo mambo unaona maji
mengi hayoo...!"
Mzee mmoja aliongea huku akinikaribia, lakini hata
hivyo moyo wangu pia ulinisukuma kuingia ndipo
nikausukuma ule mtumbwi hadi karibu na maji
mengi nikaingia ndani yake na kuanza kupiga kasia
ili kufika katikati. Nikiwa naelekea kule huku nchi
kavu watu wananishangilia na wengine
wakinisikitikia sana lakini hata mimi mwenyewe
nilijishtukia lakini ikawa kama kuna nguvu
inanisukuma hivi, na ikinipa hamasa ya kuendelea.
Nilijikuta niko mbali kidogo na nchi kavu moyo
ukanituma nitoa nyavu mpya ambayo ilikuwemo
mule na kuitupa.
Baada ya kuitupa nikawa naangalia, ndipo kwa
mbali kidogo nikaona maji kama yanapanda alafu
yanashuka..yanapanda kisha yanashuka..yanapanda
kisha yanashuka mithlo ya mawimbi makubwa
lakini ilikuwa kama kitu ambacho kimejikusanya
alafu kikawa kinakuja upande wangu kwa mwendo
mdogomdogo. Nilijipa moyo kwa kusema mungu
yupo. Hatimae mtumbwi wangu ulianza kusumbua
nilianza kupata hofu kwani maji mengi alafu
hayajatulia nikajisemea moyoni 'kipi kimenileta na
sikusikiliza ya watu?'.
Kwenye ile sehemu niliona kama nyavu ambayo
inaonekana. Niliifuata kisha nikaahuhudia kuwa ni
ile nyavu yangu ya jana. Nilichukua fimbo ambazo
tunatumia kuvutia Nyavu nikaikamatia vyema kisha
nikaiweka kwenye moja ya tundu ya ile nyavu kisha
nikaanza kuivuta.
Aaah! Hakika ilikuwa ni nzito sana. Niliiweka
hivohivo nikafunga nyuma ya mtumbwi ndipo
nikaanza kupiga kasia baada ya kuitoa ile ambayo
niliiweka muda mchache. Nilipiga kasia kwa nguvu
zote baada ya kuhisi labda ile ndoto itakuwa
inafanana kweli na jinsi nilivyoiona net yangu.
Mawimbi yalinipiga sana lakini nilijikaza niliona nchi
kavu watu wakiwa wamejipanga kuniangalia nadhani
watu walijua nitapotea na nitakufa hukohuko kama
ndugu yangu Kibona.
Niliona watu wakifurahi mimi nikiwa sijui kipi
wanakishangilia.
"Eeeh! Jamaniii wengiiii alafu wakubwa
kweli...eeeeh ndioooo!".
Nilishangaa kusikia wanasema vile ndipo
nikaangalia nyuma na kushuhudia lundo la samaki
wakubwa hakika furaha ya ajabu sana ikinijia
nilishuka wachche walinisaidia kuwatoa kuna
samaki ambao walikaa ndoo kubwa akiwa peke
yake.
Watu palepale walijaa wakiulizia bei. Ndani ya
masaa kadhaa pesa nyingi nilipata kwa makdilio
mauzo yalikuwa ela nyingi. Japo wengi waliniibia
kwa kuwa nilishikwa na bumbuwazi kuona maajabu
kama yale. Ilifika majira ya saa saba mifuko ilituna
ndipo nikaondoka nyumbani huku nyuma nikiwa
nimewaachia mshangao mkubwa sana.
Baada ya kufika nyumbani ndipo nikajifungia ndani
na kuanza kuhesabu mapato yangu ya maajabu.
Kweli mnyonge riziki yake bado ipo muda na saa
yeyote ile kikubwa ni uvumilivu wake tu. Nilipanga
kiasi cha laki moja na nusu nikaenda kumpatia Mke
wa Kibona kwani bila yeye nisingepata mavuno
haya. Furaha yake naamini kuwa itaniwezesha mimi
kupata vikubwa zaidi ya hivi.
Baada ya wiki nilifanikiwa kununua mashine za
kusukumia mtumbwi. Niliona maisha yangu sasa
yakiwa mazuri ndipo nikaamua kumtafuta mtoto
wangu Asante, maana mtoto mwingine alikuwa wa
kumkuta alizaa na mwanaume mwingine. Malengo
yangu ni kutaka kulea damu yangu. Nilipata bahati
ya kujua wapi anaishi yule mwanamke ambae kwa
sasa si mke wangu tena. Nilifanya juhudi zote na
kufika hadi mahali ambapo anaishi kiukweli ni
pazuri sana. Niliamua kuachana na kazi ya uvuvi
mpaka pale nitakapohakikisha mwanangu anakiwa
kwenye himaya yangu. Nyumba kubwa ya kifahari
iliyopo mbele yangu geti likiwa limefunguliwa na
gari nzuri sana inatoka.
Kwa kuwa nilikuwa na uhakika kuwa ndio pale
anapoishi Asante na mama yake niliwahi haraka na
kulifikia lile gari.
Uzuri lilisimama na kufungua kioo!. Daah! Sikuamini
macho yangu.....
 
SEHEMU YA SITA 06
KAMA UMEIPENDA LIKE,COMENT,SHARE.
ENDELEA............
..................Nilishtuka baada ya kumuona Mama
Asante akiwa ndani ya gari hiyo tena yeye
mwenyewe akiwa ana drive. Kiti cha pembeni alikaa
mwanaume mwenye suti safi sana aliyekuwa
akifungua kioo huku akiniangalia kwa mshangao
sana.
Tena nashukuru alisimamisha yeye mwanaume pale
aliponiona na kumuambia kuwa asimamishe ndipo
akasimamisha na mimi nikasogelea karibu yao.
Hatua zangu zilikuwa ndogondogo nikiwa na
uangalifu mkubwa sana juu yao kwa kuwa sifahamu
wapoje au walinichukuliaje. Nilizunguka gari kisha
nikafika hadi kule ambako aliko Mama Asante.
"Mama Asante..habari yako". Nilipatwa na
mshangao huku nikigusagusa lile gari. " Hey!! Beby
huyo kapuku ni nani hapo na anakujuaje?" Sikujali
maneno ya yule jamaa ambae alikuwa anaongea
kwa kujibeza. "Mwanangu yuko wapi Asante eeeh!
Nataka nimuone". Kipindi naongea hivyo yule jamaa
aligungua mlango ndipo na mimi nilishtuka sana.
"Mpenzi wangu, usijali huyu ni yule jamaa ambae
nilikuhadithiaga kuwa Mvuvi alikuwa na shida zake
ambazo nilishazitatua kwa hiyo muache tu","hapana
sasa kaja kufanya nini hapa hii takataka sitaki
kuiona hapa ngoja..Nelson..Nelsoooooon kuja
hapa!". Alimuita mfunga na mfungua geti aliyekuja
kwa haraka sana "Naaam bosi ndio nimefika",
"Pumbavu unaitwa unang'ang'ana tu huko eeeh!, toa
takataka hii shenzi sana sitaki kuiona hapa".
Nilimshika Mke wangu wa zamani huku chozi
likinitoka.
"Mama Asante, naomba niambie mwanangu yuko
wapi eeeh yuko wapi mwanangu". "Eeeeeeeeh! Acha
uchuro Mnali sitaki hata kukusikia nobe kukuona
niondolee kelele hapa tena naomba unisikie
hivi..huyu ndie mume wangu kwa sasa na hapa
usithubutu kuja". Sikuumia maneno yake bali
nilichokaumia zaidi ni kutojua mwanangu asante
yupo wapi. Lakni nikiwa pale chini napata maneno
mengine yaliyonizidisha uchungu zaidi.
"Nakuambiaje wewe mfupi kama kifutu, sina mtoto
kwani siwezi kulea mtoto wa laana kama wewe
a...me...ku...fa."
Laaah! Sifahamu nguvu nilizitoa wapi nilinyanyuka
na kwenda kumkamata Yule mwanamke
nikamtikisa..nikamtikisa mpaka cheni yake ya
shingoni ikamdondoka chini daah! Nilishtuka
napigwa kitu kizito kwa nyuma yangu palepale
nilidondoka chini. Fahamu zilianza kupotea kabisa.
Pale chini nilianza kuhisi kuwa ndio mwisho wa
maisha yangu kutokana na maumivu makali
yaliyosababisha na kudai damu yangu mwenyewe.
Nuru ilianza kupotea machoni, giza likianza kutanda
machoni, sauti ilijirejea ya Mama Asante kuwa
Asante kafa.
Sikutaka kuamini kwa mbali masikio yalishindwa
kunasa sauti za wale watu lakini nakumbuka sauti
ya mwisho ilikuwa ya gari kama lilikuwa linaondoka,
nilihisu msukumo mkubwa kwenye mbavu zangu
kama mtu ananipiga. Nilipoteza fahamu moja kwa
moja sikufahamu nini kiliendelea baada ya hapo.
Sikujua masaa mangapi nililala pale. Nilihisi ubaridi
mkali ukiniingia mwilini na ndio ulinifanya niamke.
Kijana mlinzi aliyechuchumaa mbele yangu
akiniangalia kwa huzuni. Sikumlaumu sana kwani
ndio kazi yake na ndipo anapopata riziki yake kwa
kufuata ya bosi wake. "Daaah! Kaka pole sana
kwani huyu ni mke wako?" Aliniuliza "Alikuwa mke
wangu...lakini tuliachana mazingira ya utata na
tulizaa mtoto mmoja anaitwa Asante". "Pole sana
sasa chukua hiki kiasi kikusaidie njiani mimi
natumikishwa tu kaka ila usije kumuamini mtu hasa
baadhi ya wanawake kama huyu kaja hapa muda
mfupi lakini lakini aliyoyafanya makubwa".
Nilijikongoja kuinuka pale huku nikichechemea,
niliambulia kipigo cha mbwa koko hakika nilipata
tabu sana. Nilifika nyumbani hoi, nilimeza panadol
za kenya kutuliza maumivu na kweli zilinisaidia.
Baada ya muda jioni hii sikutoka kokote bali
nilimuagiza dogo anichukulie miogo ya kuchomwa
ndio ambayo nilikula kutwa nzima. Majira ya usiku
nikiwa nalia peke yangu nikiwaza mengi pamoja na
mustakabali wa maisha yangu sijui wapi naelekea.
Nililala nikiwaza kesho yake niende baharini kuvua
samaki maana muda mrefu umepita sikwenda
kabisa. Lakini usingizini Mungu kama aliniletea laika
kuja kuniambia kuwa siku hiyo nisijaribu kwenda
kwani bahari chafu zaidi ya maelezo. Kweli asubuhi
hata nafsi yangu ilishindwa kwenda kabisa.
Nilifika ufukweni nikipita kukaguakagua pale.
Nilibahatika kukutana na mzee mmoja ambae pia ni
maarufu maeneo yale ya pwani. "Mnali, leo
hauingii?", "Ndio! Na ikiwezekana hata wewe
usiende". "Lakini kuna bosi kajitokeza hapa anataka
wavuvi awajiri kaanzisha hoteli yake sasa moja ya
mboga ni samaki anataka wavuvi watakaompelekea
samaki wa kutosha sijui unaonaje".
Nilifurahi kusikia maneno matamu ya ela kama hayo
"Baba mimi natafuta ela akitaka hata kesho." "Sasa
leo mchana anakuja kwa hiyo tumsubiri tuongee nae
maana wewe ni wa tatu kukupata kwa hili dili
nadhani ndio mwisho kwako". Nilisubiri kweli
mpaka mchana pale ndipo likaingia Prado moja zuri
sana wakatoka watu wawili. Walifika hadi kwa yule
mzee.....
 
SEHEMU YA SABA 07
LIKE , SHARE NA COMENT USISAHAU KUSAMBAZA
CHAPISHO HILI
ENDELEA.....
................Nilibaki kucheki mchezo unaendeleaje
kati ya wale wawili na yule mzee ambae alikuja
kunipa lile dili. Niliwaona wakiongea kwa mbali hivi
ndipo nikamuona yule mzee akinionyeshea mkono
kama anawaonyeshea mimi pale nilipo. Nikaona
mambo sasa yanaenda mwake mungu anaanza
kunionyesha njia.
Ndipo aliponiita na mimi sikufanya ajizi maana haya
mambo ni kuwahi ukicheza tu kuna vijana wengi
sana ambao wapo pale wanatafuta hata nafasi
ndogo ya kupata miambili. Nilitembea haraka hadi
pale walipo.
"Ehe! Sasa huyu kijana anaitwa Mnali, ndie kati ya
wale vijana ambao wataifanya ile kazi". Nilimeza
mate kwanza kujiweka safi koo langu ili nipate
kujibu kama nitapata swali.
"Sawa nimemuona sasa mbona kama mdhoofu sana
ataiweza kweli". Alinitazama yule mzee kisha
akaniminyia jicho.
"Hapana yani huyu kijana hapa ufukweni anajulikana
kama unakumbuka juzi nilikuambia kuwa kashika
samaki wengi sana tena wakubwa ndio maana
nikakuletea". "Haya twende ndani ya gari alafuuuu
wale wengine nitakuja kesho kuwaona acha huyu
nikaongee nae". "Sawa bosi wangu ila kuwa makini
mtunze kijana wangu huyo". Niliombwa kuingia
kwenye lile prado, niliingia kisha tukaondoka pale
hadi kwenye hoteli moja hivi kubwa tena nzuri ya
kifahari. Nilikuwa mshamba sana ndani ya gari
kwani sikuwahi kupanda gari hilo maana maisha
yangu baiskeli mpaka tunafika kwenye hoteli
siamini kabisa.
Nikiwa pale hotelini nilishindwa hata kukaa maana
vitu vilivyomo mule ni adimu sana tofauti na
nilivyozoea mimi mwenyewe. Nguo zangu hazikuwa
na hadhi ya kukalia kochi safi za bei kama zile
niliona nachafua.
Yule Jamaa alikuwa mnene sana alinikaribisha
mezani ili tuanze mazungumzo. "Hapana bosi nguo
zangu chafu ona nitachafua hapa samahani sana
nitasimama". "Haaa! Haahaaaa!" Alicheka sana "
kijana usinifurahishe ni kawaida kabisa wewe kaa
tuongee mambo hayo wahusika wapo,". Nilikaa
kisha nikawa namsikiliza. "Kijana nahitaji kufanya
kazi na wewe naitwa Mr. Paul hii ni hoteli yangu
ndio ambapo hao samaki wanahitajika, sasa je?
Unataka nikulipe kwa kiasi gani na kwa muda
gani?". Daah! Ilikuwa mtihani sana kwangu kutaja
bei mpaka alinigundua kuwa nashindwa kutaja bei
ambayo itakuwa nafuu kwangu. "Ok! Usijali
nitakulipa kwa mwezi laki tatu pamoja na kila siku
elfu kumi na nitakulipa kubwa zaidi ukiniletea mzigo
mzuri na mkubwa sawa". Nilimshukuru sana mpaka
nikamsogelea pale kutaka kuzidi kushukuru.
"Hapana kijana fanya kazi nione kwa sasa utashika
hii laki moja utaenda kutumia ila kesho njoo
nimeagiza boti toka nje likija nitakukabidhi uanze
kazi haraka sana." " nakushukur pia nakuahidi kuwa
nitaifanya kazi yako vizuri sana bila hata uwoga
wowote.". Hakika alifurahi sana. Basi nilirejea hadi
kule ufukweni nikiwa na amani tele maana mfuko
umetuna japo nilitoka kula vipigo kwa Mama
Asante.
Baada ya kufika ufukweni nilijitahidi kumtafuta yule
mzee kwanza nilifanikiwa kumpata ndipo nilianza
kumueleza kile ambacho nilikipata kutoka kwa Mr
Paul. "Babu kwanza nashukuru sana maana
niliyoyapata kule ni makubwa na ambayo sikutarajia
kabisa kuyapata", "yapi hayo?" Aliniuliza. "Mh!
Kwanza nimefika tu tukapandisha juu ghorofani mule
ndani mnanukia sijui harufu gani ile nimeipenda
sana kama ni mafuta basi mazuri zaidi ya maelezo,
Kingine nilipewa kinywaji kizuri sana pia niliwaona
wazungu pale". Wakati naendelea kuongea ndipo
akanisimamisha kwanza "Ebu eleza mliongea nini
maana unazunguka sana mpaka nashindwa
kukuelewa".
"Daaah! Babu kanipa kazi kuwa kwa mwezi atanipa
laki tatu alafu kila siku elfu kumi na nikimpelekea
samaki wengi ataniongezea hela na pia kesho boti
la kutumia mashine linakuja atanikabidhi na kazi
kuanza". Nilimuona mzee kama kasizi hivi kisha
akanipa mkono akataka kuondoka, ndipo nikaingia
mfukoni nikachukua elfu thelathini na kumpatia
nilivunja mzizi wa fitina kabisa pale.
Ile siku niliimaliza na furaha ndipo nikaelekea
nyumbani kwa mke wa Kibona na kumuangali.
Napo niliwaachia kiasi cha fedha na mimi kuelekea
nyumbani. Usiku wa manane nakumbuka niliota
ndoto mbaya sana nilipoamka nikajishangaa mwili
wangu unatokwa na jasho jingi ambalo ni tofauti
kwangu likanifanya nitoke kwenda kuoga huku
nikiwaza kipi kinajiri. Wakati huo nafahamu niamke
nielekee kwa yule mzee kukabidhiwa kazi rasmi.
Kama kawaida yangu asubuhi lazima nipitie kwa
Mke wa Kibona ndipo nielekee ufukweni kuangalia
mazongira halisi. Nilipofika ufukweni sikuamini pale
nilipokuta Nyavu zangu pamoja na mtumbwi wangu
umechomwa moto nilihuzunika sana, kila mtu
niliekuwa namuuliza hakunijibu sawasawa ilionekana
kama ni dili la wale vijana kuniharibia. Yule mzee
alitukutanisha vijana watatu ambao tunahitajika na
yule tajiri. Tulikaa mimi nikiwa nafikilia nani kafanya
ule ushenzi wenzangu wanafurahia tu.
Ndipo lile gari likaja na wote tukaingia kwenye lile
gari hadi sehemu ya kazi ambayo tunatakiwa kufika.
Walipewa mikataba wale wengine ndipo na mimi
nikapewa sehemu ya kuthibitisha kuwa pindi
ninapopoteza maisha mrithi wa pesa zangu ni nani
nilimuandika Asante pamoja na ndugu yangu
mmoja. Sikuwa na uhakika kama kweli Asante kafa.
"Sasa, vijana Hoteli yangu kuna wageni wengi
wanakuja sasa leteni mzigo mkubwa pia mkifanya
vyema zaidi naweza kuwagawa kuna tajiri mwingine
na yeye anatafuta vijana kama nyinyi sawa".
Tuliitikia kwa pamoja. Ndipo tukatolewa kuelekea
bandarini huko tuliikuta Boti moja Kubwa ambayo
tutaweza kuitumia. Hapohapo tuliingia na dereva wa
lile alielekezwa maeneo gani ambayo akaiweke,
tulifika hadi kule na tukakaa kupata maelekezo zaidi
ya kazi.
 
SEHEMU YA NANE 08
ENDELEA........
................Tuliendelea kutulia pale mpaka mida
ambao dereva aliona kuwa unafaa ndipo akatugeukia
sisi watatu sote. Kwanza mimi nilihisi kama ndoto
kuwa kwenye yale mazingira kwani nikikumbuka
umbali wa maisha nilioanzia nilitaka kukata tamaa
kabisa lakini juhudi zangu niliamini kama
zinanifanya kufika hadi maeneo niliyopo kwa sasa
na maombi kwa Mwenyezimungu.
"Haya vijana mko watatu, Nani anataka kuwa dereva
wa hili boti nimfundishe ili kazi yake iwe hiyo tu!"
Kila mmoja alikaa kimya kwa uwoga japo nafsi
zinatusuta kwa kutaka kujua kile kisemwacho.
"Nauliza nani afunfishwe ili muanze kazi au kama
hamtaki nimpigie simu Mr Paul". Hapo ndipo
Jamaa mmoja aliyejulikana kwa jina la Manyota
alinyoosha mkono huku akisema
"Mimi hapa nitakuwa dereva".
Akamuangalia kwa makini kisha akauliza "kwa hiyo
nyinyi vipi hamtaki?".
"Hapana ila naamini akiwa huyo dereva sisi
tutafanya kazi zingine" maneno hayo aliongea
Jamaa aliyejulikana kwa jina la Musa. Mimi nilikaa
kimya tu.
"Haya nyinyi wawili kaeni nyuma kisha wewe
Manyota njoo karibu hapa uniangalie kisha nisikilize
kipi nazungumza sawa?" Kila mmoja alielekea kule
ambako aliambiwa mimi na Musa tulikaa nyuma na
Yule Dereva pamoja na Manyota wakakaa mbele.
Waliyokuwa wanafundishana huko waliyafahamu
wenyewe ila tuligundua tu jinsi chombo kilivyokuwa
kinapelekwa Mrama tunaamini kuwa Mwanafunzi
kashikilia mtambo na kikienda sawa basi mwalimu
kashikilia usukani. Tulitumia masaa kama Manne
kuzunguka fukwe yote na jmbali kidogo kutoka pale
nchi kavu.
Muda ulipotimia ndipo tukarudishwa pale hotelini
tuliwakuta wazungu wakipata chakula, jamani mimi
sifichi elimu sikuwa nayo hivyo nilipita mbali na
watu wale kwanza hata kukaa nao karibu sikupendi
kikubwa zaidi lugha yao tu ilikuwa shida kwangu
maana nilishazoea lugha ya mtaani pamoja na
kiswahili.
Tulipelekwa juu lakini kila tulipokuwa tunakatiza
walituangalia sana alafu walikuwa wanacheka hiko
ndicho kilizidi niwachukie wazungu niliona kama
dharau sijui walikuwa wanatuchukulia kama
wachoma Mkaa sikuelewa kabisa.
Tulifika kwenye meza moja hivi ndipo ilikaa muda
kidogo akaja muhudumu hapo ndipo kimbembe
kilianza.
Wahenga wanasema kama hujui hujui tu na ni bora
watu wajue kama hujui ila usijifanye unajua hali hujui
na ukawafanya watu wewe kukuona unajua nasema
utapata tabu sana. Hii ilitokea hapo. Muhudumu
kafika akiwa na ile Menu ya chakula kabla ya
kutupatia akauliza
"Samahani, nyinyi ndio vijana wa Mr Paul?"
Tukaangaliana ndipo tukaitikia kwa kichwa kuashiria
kuwa Ndio.
"Ok! Karibuni Menu ya chakula ni hii mtachagua
chakula mkipendacho kisha nitawaletea". Kha!
Nilijiuliza kitu ina maana hiko chakula
tutakachoagiza analipa nani? Niliichungulia ile Menu
Looh! Nikaona hainifai chakula kuanzia 5000/= Mh!
Hiyo ndio bei ya chini nikawaachia wale Musa na
Manyota wahangaike nayo niligundua kwa kuangalia
bei ya vyakula japo sikufahamu ile lugha. Wakati
wale wameshika ile Menu mimi nikamuita yule dada
"Dada samahani! Kwani kuna vyakula gani hapa
vinapatikana?" Nilimuuliza
"Kaka unanishangaza Menu iliyotolewa pale ina
idadi zote za vyakula ila kiufupi kila chakula
unachokitaka kinapatikana". Nilijihisi aibu sana
mbele ya yule dada maana kama nilizalilika
"samahani mimi sijasoma kile kiingereza
mlichoandika pale sijui mimi kama mfanyakazi
mpya ambae nimeletwa hapa kuja kuanza kazi
kama nyinyi".
"Ahaa! Basi subiri nichukue huduma kwa hawa
wenzako alafu nitakuletea Menu yenye lugha ya
kiswahili". Nilirudi nikitulia huku nikiwashangaa
Musa na Manyota pindi wakiniambia mimi
mshamba.
"Mnali unatuangusha sana unashindwa hata kujua
kama hiki chakula gani, aaah! Ona mimi lile boti
nimefundishwa sekunde kadhaa nimelielewa". Ndipo
yule dada alipokuja na wenzake wawili wakileta
chakula na yeye akanipatia ile Menyu ndipo
nikachagua Wali nyama. Nilitamani Kucheka sana
pindi majamaa hasa Manyota alipoletewa Mchuzi
wenye nyama kama supu.
Baada ya kumaliza alikuja dada kisha Manyota
akauliza "dada kwani supu ya nini ile maana ni tamu
sana". Yule dada akatabasamu. "Hapa tuna supu
aina nyingi kuanzia ya Mbuzi, Ng'ombe, Samaki,
Nyoka na Chura". Tuliangaliana "Ehee na ile
uliyoniletea?" Manyota akauliza "usiseme
niliyokuletea sema niliyoagiza".
"Sawa ile niliyoagiza?"
"Ile pale ni vyakula vya watu wa kichina kama
unavyoona hapa Chinese Food. Na yule ni Chura".
Jamaa ilibidi azuge tu. "Daaah! Kumbe hata chula
mtamu mamaa nimekula Chula". Dada aliondoka
huku tukibaki na kicheko cha ajabu. Ghafla alikuja
Meneja wa ile Hotel ndipo akatuchukua na gari
kutupeleka mahali fulani. Tulienda kukamilisha
baadhi ya vitu ndipo tukakabidhiwa Rasmi usiku huo
kuanza kuvua Samaki wakati huo Bosi akiandaa Boti
mbili zije tugawane majukumu zaidi.
Tulilala palepale Mpaka majira ya saa sita usiku
tukachomoka kuelekea Kwenye fukwe ili kuanza
kazi.
Tulihakikisha Nyavu ziko sawa ndipo tukawasha taa
ili kuwavutia samaki, tukatundika vyema ile Nyavu
kisha tukaanza kusubiria huku tukitembea, ilifika
Majira ya saa kumi Samaki hatukupata wengi
walikuwa wanahesabika. "Jamani, mnaona sasa
hakuna samaki na bosi anatarajia kuwa leo
tumfurahishe inakuaje hapa?" Mimi niliwauliza swali.
"Aaaah! Na yeye pia binadamu anajua kuwa kuna
kupata na kukosa leo sio bahati yetu kwa hiyo
turudi maana najisikia uvivu hata kuendesha
nimechoka".
Manyota kachoka alafu yeye ndie dereva sasa
inakuaje Musa pia alikubaliana na Manyota. Ndipo
tuliyoyoma taratibu tukiwa na samaki wetu kadhaa
ambao ni kama aibu kabisa kuonyesha.
Kikubwa kilichonifanya niogope ni gharama
alizotumia bwana Paul kwa kutuhudumia sisi na
kutuahidi fedha nyingi sana. Tulipofika ufukweni Saa
Kumi na Moja watu wanaokuja kununua samaki
wanaanza kuingia pia nilijua kuwa Muda mfupi tu
wale mabosi watakuja kuchukua mzigo.
Niliwageukia wale wenzangu na kuwambia jambo.
"Oyaa! Sikieni tunatumia boti lenye Sauti kubwa kule
linasababisha kelele mnaonaje tuchukue Mtumbwi
hata dakika kadhaa tuongezee hawa?"
Kila mmoja alinicheka na alikuwa tayari kachoka
kalala ndani ya hilo boti. Nilitoka kisha nikachukua
Mtumbwi sikujua wa nani nikachukua wavu nikapiga
kasia kuingia tena Majini.
Kilichotokea huko nyuma sifahamu. Nilitega kisha
nikazubaa mpaka usingizi ulinikamata ghafla
yalinichukua masaa mawili mpaka nashtuka
mtumbwi unaelemewa, nashtuka naona nyavu
imekamata Samaki nikajitahidi kuwavuta lakini
nilishindwa. Mtoto wa Masikini furaha yangu kuona
nafanikiwa mbona sasa napata shida?.
Nilijisemea mwenyewe mara upepo ulianza kuvuma
ukawa unanisogeza taratibu nchi kavu huku
nimeikusanya Neti na nikiwa makini kutoiachia
mpaka nchi kavu nakuta gari likiwa lipo pale.
Walikuja kunisaidia hadi kuvusha nao daah!
Nilimshukuru sana mungu kiasi cha samaki
niliowapata niliona wanaridhisha kuliko wale
wengine. Niliona ajabu naingizwa ndani ya gari na
kuambiwa nibadilishe nguo nawakuta Musa na
Manyota wakiwa wameninunia huku Manyota
akisema tunaharibiana siku.......
 
SEHEMU YA TISA 09
ENDELEA.......
.................Kauli ya bwana Manyota ilinishtua
kiukweli eti Tunaharibiana siku kivipi labda. Basi
nilibadilisha zile nguo ambazo zilikuwa zimelowa
tayari kisha nikavaa nguo nyingine ambazo
tuliletewa.
Lakini kitu ambacho kilikuwa kinanishangaza ni
pindi tu nilipomuona dereva na jamaa mwengine
mwenye Miraba Minne wakiwa wamekasirika sana.
Aliangalia nyuma akatuona wote tumekaa ndipo
akawasha gari na kuliondoa pale ufukweni. Safari hii
tulifika hadi kule hotelini lakini ofisini kwa Mzee
Paul. Tulishushwa nje huku tukisubiria nini
kinaendelea.
Mimi kwa Wasiwasi Nilimfuata Manyota. " Oyaa!
Leo vipi kwani?".
Walonichunia haya Musa na yeye akawa ananichunia
nikaona isiwe kesi kubwa zaidi nikatulia pembeni.
Niliona sasa kazi inaanza kama kuota nyasi
mapema sana. Walikuja vijana kadhaa ndipo
wakafungua lile gari nyuma wakachukua wale
samaki. Mmoja wao alihamaki kwa kuona wingi wa
wale samaki huku akisifia kuwa ni wengi sana
kuliko kawaida ambayo wao walikuwa wamezoea.
Ndipo kwanza akaitwa Musa Ofisini. Wengine
tulibaki tukaona leo mambo yameiva. Wakati
tunaendelea kusubiria Manyota akanigeukia "Mnali
umetuuza sana leo". Nilikunja uso kwa mshangao
mkubwa
"Nimewauza! Sijakuelewa bado"
"Ndio walipofika walifurahi na wale samaki
tuliowapata ila walikuulizia tukasema umekwenda
kuwachukua wengine ila daaah!.." hapo ndipo Jina
la Manyota lilivyoitwa na Musa akatoka nje.
Muonekano wa Musa kweli ulionyesha ndani si
pema mimi nilihisi patanishinda mapema tu. Muda
mchache nikaitwa Mimi nikahisi kabisa kuwa haja
zinataka kunitoka miguu yangu ilitetemeka ndipo
nikavuta pumzi kwa nguvu kisha nikashusha pumzi
kisha nikaingia ndani. Niliwakuta watu wanne mule
ndani niliowafahamu ni yule dereva, yule jamaa
mwenye Miraba minne pamoja na Mzee paul
wakiwa wananisubiri.
Nilijihami kwa chochote kile ambacho kinataka
kutokea kwangu. "Haya keti kwenye hiko kiti".
Nilikaa kisha nikawatumbulia macho kuwasikiliza
nini hicho walichoniitia pale na kama kunifukuza
walinitaka wenyewe mimi sina shida kabisa
nitaondoka.
"Unaitwa Mnali?"
"Ndio".
"Sawa ebu tueleze historia yako ya elimu kidogo ili
tujie tunachotaka kukipata kutoka kwako".
Duu! Niliona sasa ubaguzi wa kielimu umeanza
sasa.
"Mimi niliishia elimu ya msingi na sikupata cheti ila
nilibahatika kupata kazi ya mikono yangu na
nilipoachishwa hiyo kazi kwa kuwa sina elimu basi
nikajiingiza kwenye mambo ya uvuvi hapo ndipo
mliponiona".
Niliona dereva na baadhi wanacheka sana. "Daaah!
Nilijua labda unacheti chochote sasa hapa sijui
tunakusaidiaje ok! Utafanya kazi mwezi huu kisha
mkataba wako tutaufikilia sawa?"
"Aaah! Sasa nitafanyaje ila mngeniuliza tangu nipo
kulekule lakini si leo kuja kunidhalilisha hapa haina
shida sijaanza kula ela yenu naomba bora niache
nikapigane na maisha yangu mwenyewe".
"Kijana tulitaka kukusitili tu. Nimepata habari yako
kuwa ni mvivu sana huko baharini unawaachia
Manyota na Musa sasa utafika hapo mbele kwenye
ule mlango mpatie hii karatasi kisha utaondoka
kabisa hatukuitaji".
Huwezi kuamini kuwa nililia sana pale nilipokakaa.
Kwa hasira sikutaka kuchukua hata ile karatasi
wakati nanyanyuka ndipo waliitwa wale wengine
yaani Musa na Manyota. Walipoingia niliwaona
kama wanacheka hivi.
Nilisimama huku nikitetemeka na kutoka kwenye
kiti.
"Kijana chukua hii karatasi umpelekee yule dada
atakupatia ela ya kuendelea na maisha yako na ya
pole kwa usumbufu maana sisi tunataka vijana
kama hawa wachapa kazi na si ndezi kama wewe."
Maneno ya bwana Paul yalikuwa yanauma sana
moyoni mwangu
"Usijali Baba sina shida na iyo ela yako, kikubwa
nina uzima nitaenda kupambana na hali yangu sisi
tusiokuwa na elimu basi acha tukaishie huko".
Nilitoka mule mfukoni nikiwa na kama elfu ishirini
tu.
Nilitafuta gari likanipeleka hadi nyumbani, nililala
kupunguza mawazo nikijiuliza kwa madhambi yapi
ninayoyafanya mpaka nakosa maisha hata ya kujidai
kama wengine. Niliwaza kuwa uvuvi nao niuache.
Lakini niliwaza jambo moja kuwa nitafute kwa
nguvu zangu. Niliona vyema niende kwa Mama mke
wa Marehemu Kibona ili nikaongee nae jambo.
Nilikwenda kweli nikamkuta akiwa amejiinamia hana
hili wala lile.
Tuliongea mengi sana na mke wa Kibona jambo
ambalo niliona ni la umuhimu kuongea nae ni
kuhusina na mimi kutaka kuanzisha sehemu ya
kuuzia samaki pale nyumbani.
"Sasa Shemeji nakuomba huyu mwanao Mihayo
niende nae baharini anisaidie kisha wewe uwe
unauza samaki ambao tutakuwa tunawapata".
"Shem kweli vipi huko ambako mlikuwa mnafanya
kazi"
"Aaah! Achana nae huko bhana maana nahisi kama
unanichoma moto vile sasa hivi ila Mwambie
Mihayo jioni aje nyumbani pale natengeneza
sehemu ya kuuzia hivyo mwambie aje".
"Haya kila la heri shemeji ila hata leo hatuna hata
cha kula mpaka natamani nirudi kijijini maisha ya
hapa yananishinda kabisa".
"Hapana Shemeji mimi niliahidi pale baharini kuwa
kama Rafiki yangu Kibona Kafia mule basi
nitahakikisha kuwa familia yake nailinda mimi
mpaka mungu atakapotuchukua mmoja kati yetu."
Niliondoka kuelekea nyumbani kisha nikaanza
kutengeneza kibanda kikubwa hivi cha kuwekea
samaki wabichi ambao niliamini kuwa watu watajaa
na watakuja kununua kabisa. Jioni kweli Mihayo
alikuja nikamuelekeza na tukaanza kazi hadi pale
tulipomaliza.
Majira ya usiku nilikwenda nae baharini tulifanya
kazi kwelikweli mpaka tunafika majira yale
kuondoka tuna samaki wa kutosha na asubuhi na
mapema tunawakusanya ili kuondoka nao.
Akina mama wengi wakitaka kugombaniana hadi
kutaka kupigana kabisa kwa kuhitaji wale samaki.
"Jamani kama mnawataka hawa samaki njooni
nyumbani ndiko sasa ninakouzia". Walitufuata hadi
nyumbani nikamkuta Mama Mihayo akisubiria
mzigo tuliwapanga mpaka sehemu ikajaa na
haikutosha.
Tuliwauza wakabaki kiasi ambacho baadhi tuligawa
na wengine tukabaki nao kwa matumizi. Walikuja
kununua kwangu kwa kuwa nilikuwa nauza bei nafuu
tofauti na sehemu zingine.
Jioni yake Mzee yule ambae aliniunganisha na
bwana paul alikuja nyumbani. Alinikuta nikifanya
baadhi ya mahesabu na mipango ili nijue natoka vipi
kutokana na wale samaki. "Sasa kijana umetoka
kule kwa bosi kwa sababu gani?"
"Mzee nimeamua kutulia mwenyewe sasa hivi
sihitaji usumbufu kabisa maisha yangu nataka
kujitegemea mwenyewe, wale wasiotutaka sisi
tusiosoma basi waendelee na hao wasomi". Mzee
basi aliondoka.
Ndipo waliingia akina mama kuja kutaka oda ya
samaki kwamba wakija tu basi wao wawe wa
kwanza.
Nilijihisi kama Bosi masikini maana si kwa hali ile.
Asubuhi na mapema kama kawaida nilikwenda
kuangalia mazingira na kuandaa vifaa hukohuko
baharini.
Kila mmoja aliniangalia sana huku wakinionyeshea
vidole. Wakati narudi sasa akaja rafiki yangu mmoja
na yeye Mvuvi. "Ndugu unajua wewe rafiki yangu
sikufichi hata neno moja"
"Najua hilo"
"Wamepanga kukuua ndugu yangu siku hizi za
karibuni maana wewe ni mgeni kwenye Uvuvi baada
ya Kibona kukufundisha kwa muda mfupi sasa hivi
umewapita wote kila mteja anakuja kwako
wamekasirika ndio maana nikaona nikuambie
wanataka kukuulia ndani ya bahari kama kibona".
Nilishtuka baada ya kusikia wataniua kama kibona.
"Ina maana Kibona Aliuliwa, je na ni nani huyo
anaepanga hizo hatua?"
Nilimuuliza
"Mnali! Usijali tukutane leo jioni kabla ya kuja
kufanya kazi pitia nyumbani".
Niliondoka pale nikiwa na wasiwasi...
 
SEHEMU YA KUMI 10
ENDELEA......
.................Nilipatwa na Mshangao sana maana si
kwa hali ile. Kumbe kuna watu wananiandama
hivihivi. Ila nilijipa Moyo kuwa nitashinda katika vita
ya wanafiki na wale wasiopenda mafanikio ya
wengine. Nilifika mapema nyumbani siku hiyo
nikitafakari huku nikijitahidi kufikiri katika swala lile
nyeti. Siku hiyo hata sikutaka kuandaa chochote kile
kinachohusiana na mambo ya uvuvi nilisubiri jioni
ifike niende kwa rafiki yangu akanieleze kisa na
mkasa.
Kabla ya jioni nilifika kwa yule jamaa baada ya
kwenda kutoa taarifa kwa Mke wa Kibona kuwa leo
sitokwenda kabisa Baharini maana kuna jambo
kama lile linanitatiza. Safari yangu iliendesha na
hulka ya Moyo kupiga kwa kasi mapigo yake
pamoja na nafsi kutamani kumjua na kujua mpango
mzima wa hao watu wanaotaka kuniua.
"Haya, Mnali unafahamu kama hili swala ninalotaka
kukuambia ni hatari sana japo linahusu kuhatarisha
maisha yako?" Aliniuliza swali huyo rafiki.
"Aaah! Unajua ni kweli hatari ila naona hatari zaidi
kwa mimi ninaetakiwa kudhuriwa". Nilimjibu huku
nikimuangalia usoni.
"Ndio ila basi tuseme kuwa sisi sote ni hatari kwa
wewe unaepangiwa kuuliwa pamoja na mimi".
"Mh! Kivipi yani".
Nilimuuliza
"Unajua kuwa mpango wa wewe kukuua ulianza
muda sana kipindi upo na Kibona siku ambayo
mulitakiwa kuuwawa wewe hukuwepo akawepo
Kibona pekee. Nikisema ni hatari kwako ndio
maana nakuambia ili ujihadhari kwa kuwa ni rafiki
yangu na hatari kwangu kwa kuwa mimi ndio mtoa
taarifa kwako ya haya mambo pindi wakifahamu
nimetoboa siri hii".
Nilisikitika sana ila nilijikaza kiume nipate ukweli
zaidi wa lile swala.
"Sasa kifo cha Kibona Kilikuwaje ".
"Daaah! Mnali kifo cha Kibona kiukweli kinasikitisha
sana Mpango huo mimi nilishilikishwa kiulazima
kwa kuwa niliwakuta wakiongea kuwa Kibona
anapata samaki wengi sana kuliko kawaida,
nilipowashtukia walinikamata na kutaka kuniua ila
waliniomba kuwa niwe katika hilo kundi siku hiyo
ilikuwa hivi..
Akiwa ana hadithia.
..Kibona alikuwa anasukasuka Nyavu yake huku
akiwa anatumbuiza na nyimbo kadhaa. Ndipo
akaingia Mzee Mmoja makamo ya Kibona kisha
akakaa.
Waliongea machache ndipo yule mzee akamuuliza
maswali kadhaa.
Kibona unajua siku hizi hali ni ngumu sana, ndio ni
ngumu lakini hatuna jinsi ya kusema zaidi ya
kujitahidi kupiga kazi kila siku., ndio ila kwa nini
kwa upande wako baada ya kumpata kijana yule
Mnali Mnapata Mavuno mengi sana kuliko sisi,
khaa! Yani huwezi amini kabisa maana ananisaidia
kila hatua, unajua kama huyu atakuja kukubadilikia,
mh! Haiwezekani kabisa afanye hivyo namuamini.
Ndipo yule mzee akasimama na kuondoka.
Mzee Kibona hakusita kabisa kuhusu yule Jamaa
kuondoka kwa kutoridhika yale aliyojibiwa.
Muna roho mbaya sana nyinyi kama si binadamu
maana kila siku nyinyi kuwangalia watu tu
wanafanya nini.
Jioni yeye Kibona aliingia kazini huku akiwaangalia
wengine hakuona watu kabisa. Naona leo watu
wamechoka kabisa hakuna watu haya ngoja niingie,
Kibona akiwa na Imani tosha anaingia ndani ya
mtumbwi ndipo Mimi nikajitokeza nikiwa na hamu
ya kutaka kumuambia kuwa anakokwenda siko
kuzuri kwani wale vijana kadhaa wamejitega baadhi
ya sehemu kule mbele.
Lakini nilimuacha aende maana niliogopa kabisa
kuongea ili nisije kuuliwa na wale watu. Wakati
Kibona akiwa anaelekea ndani kabisa baharini mimi
nilirudi nyuma ambako baadhi ya vijana ambao
walibaki kule nchi kavu.
Baada ya hapo ndipo muda baadae vijana walikuja
ndipo wakaanza kuhadithia kuwa tayari
wameshammaliza na wakamtumbukiza kwenye
maji. Hapo ndipo habari ya Kibona iliishia na yote
haya yalisababishwa na yule mzee ambae
kakufanyia mpango wa kwenda kwa bwana Paul.
Alimaliza Kuhadithia.
Nilipatwa na kigugumizi huku chozi likinitoka baada
ya kuhadithiwa kisa cha Kibona. Nilijikuta naondoka
pale kisha nikapata na hasira kubwa sana baada ya
kukipata kile kisa cha kuhudhunisha na sikutaka
hata kumhadithia Mkewe.
Ilipita kama wiki hali yangu ilikuwa nzuri ya
kimaisha nilifanya mpango wa kuanza kutengeneza
nyumba mpya. Nilisimama kwa muda swala la
uvuvi kwa kuogopa lile jambo na nilianza kuwa na
hofu kubwa juu yao. Nikiwa usingizini niliota ndoto
kuwa Kibona anakuja usiku na kuniambia maneno
ambayo yalinifanya nishituke toka usingizini. "Mnali,
usije kuogopa kuvua samaki kwa kuwahofia hao
hapana wakijaribu kukufanyia chochote hakika kila
mmoja lazima alipize". Nilishtuka kutoka usingizini
majira kama saa nane.
Ile ndoto kwangu ilikuwa na maana gani na ilikuwa
inanieleza jambo gani.
Sikupata hata lepe la usingizi nilikaa mpaka
asubuhi.
Nilijihisi kama mtu mwenye hamu ya kwenda kuvua
samaki. Nilifanya hivyo kwa kuwa nilikuwa na
Mitumbwi kama sita mingine niliiweka ya kukodisha
na mmoja nilitumia mwenyewe.
Mauzo ya samaki kwa upande wangu niliona kabisa
yanafaida kubwa sana. Nikiwa baharini napita
kuzunguka nione wapi naweza kutega kwani
niliamua kubadili mazingira. Ndipo nikaliona boti
likija kwa kasi kubwa pale nilipo niliogopa nikihisi
labda majangili hawa wanakuja kunivamia.
Uwezo wa kuwakimbia sikuwa bao kwani mashine
ya mtumbwi wangu haikuwa na uwezo mkibwa
kama lile boti la kutengenezwa kutoka kiwandani.
Ndipo liliponikaribia na nikamuona Manyota na
Musa wakipita na Nyavu zao, walisimama.
"Mnalii aaah! Afadhali sana tumekuona ndugu yetu"
Aliongea Musa.
"Unajua tangu utoke hatupati samaki wakubwa
kama wale wa ile siku".
"Poleni"
"Ahsante sasa unaonaje tuvue na wewe alafu
tunakulipa"
"Hapana mimi siku hizi nina wateja wangu ambao
nawapelekea mizigo".
Nilishangaa wakiondoka kwa haraka huku wakisema
Achana nae huyo atakufa masikini.
Narudi na samaki kadhaa ambao niliona wanafaa
kwa siku hiyo maana bahari kidogo ilichafuka
haikuwezekana kuwapata wengi.
Nilirudi hadi Nchi kavu na kuliona gari la kifahari
likiwa limesimama na watu wengi hasa akina mama
ambao walikuwa wanasubiri mzigo.
Niliwapatia kile ambacho walikuwa wakikisubiria
lakini nilihisi kama mtu ananifuatilia kimyakimya
pale nilipo. Nilipatwa na woga sasa. Baada ya
kumaliza nilitaka kuondoka ndipo akanigusa begani
yule niliyekuwa namhisi.
"Kijana Unahitajitajika na tajiri kwenye lile gari".
Nilishangaa maana nilidhani kibaka au wale
waliopanga kuniua.
"Tajiri nani?"
Nilimuuliza
"Kijana unapata bahati unachezea twende
utamuona".
Nilihisi kuwa hakuna salama unajua ndugu msomaji
Nilifanyaje?.....
 
SEHEMU YA KUMI NA MOJA 11
ENDELEA.....
................Niliona wanalazimisha ikawa sio kesi
acha mimi niende nikawasikilize. Nilitrmbea
mdogomdogo kama wimbo ule wa Msanii wa
Tanzania Diamond Platnum hadi pale kwenye gari
nikiongozana na yule jamaa.
Niliishia nje ya gari sikutaka kuingia kwa kuwa
nanuka shombo ya samaki pili sikuwa na uhakika
na wale majamaa wanaojiita matajiri.
"Ndugu yangu, nimekufuatilia sana tangu kipindi
kirefu ila nahitaji msaada wako"
Nilimshangaa kuniambia anahitaji msaada wangu
yani mimi leo niwe mtu wa kumsaidia mwenzangu.
"Khaaa! Msaada gani ambao unahitaji kutoka kwa
mtu kama mimi?"
Walicheka sana kisha wakatulia
"Kwa nini unajidharau sana"
"Lazima niwe nashangaa kwa sababu watu kama
nyinyi wakubwa ndio wa kuwasaidia wengine kama
sisi tena sisi tuwasaidie nyinyi hivyo vichekesho".
"Hapana haya tuongee biashara sasa"
"Biashara?"
"Ndio"
"Biashara ipi tena".
Ghafla niliona wakinizunguka kwa haraka vijana
kadhaa kama watatu hivi.
Walinishika na kunisweka ndani ya gari, gari lile
liliwashwa haraka na kuanza kuacha sehemu za
bahari na kuelekea barabara kuu ya kuelekea mjini.
"Nyinyi vipi sasa mnanikamata?"
"Utajua huko mbele si hutaki kuelewa unaleta kiburi
ngoja tufike mahali utuelewe vizuri zaidi tena kwa
haraka".
"Ila kwa nini sisi mnatuonea hivi "
Hawakutaka kunisikia tulitembea umbali kidogo
hadi kwenye shule moja ya watu binafsi kisha
likasimama.
"Sikiliza, tumekuleta huku kwa maana. Mr Paul
anahitaji mzigo mkubwa sana Hoteli yake inataka
kufa kutokana hakuna upatikanaji wa samaki wa
kutosha, vijana waliokuwepo hawawezi kukidhi
mahitaji ya pale. Sasa tunataka wewe urudi tena
pale".
Kila neno alilokuwa analiongea liliniingia masikioni
vizuri sana na kunipandisha hasira.
"Yani kunitisha kote huko mnilazimishe kufanya kazi
zenu?"
"Ndio utafanya au hufanyi"
"Sasa..."
Kauli yangu ilisitishwa na mlio wa gari uliokuja pale
watu kadhaa wakatoka waliovalia suti ndipo
namuona bwana Paul anaingia kwenye lile gari
nililopo mimi akakaa mbele yangu huku nje baadhi
ya vijana wakirandaranda.
"Mnali habari za siku"
"Safi"
"Karibu tena"
"Wapi?"
"Teh teh teh! Unanichekesha, ok! Manyota na Musa
nataka niwafukuze hawafanyi kazi yeyote ile na
kilichonifanya hivyo ni baada ya kuona kuwa una
mchango mkubwa sana na sitoangalia kigezo cha
elimu wala nini kama elimu nitajitahidi utajua
kingerez kuongea na wageni pamoja na hilo
naongeza mshahara wako mara mbili ya pale".
Nafsi ilinisuta kutokana na umasikini nilionao.
"Daaah! Ila hapana nipe nijifikilie".
Aliingia upande wa dereva kisha akatoka na boksi
sikufahamu ni aina gani ya simu. Aliifungua na
kuitoa simu nzuri sana hizi sijui wanaziita Smat poni
sijui smatphone. Alinikabidhi.
"Hii ni simu chukua itakusaidia kufanya mawasiliano
na mimi imesetiwa kila kitu".
Niliishika na kisha nikawa naiangalia sijui hata
wanaitumiaje.
"Aaah! Mimi sijui hata jinsi ya kutumia". Walicheka
kidogo.
"Hapana usijali wanafanya hivi..nimeitengeneza hii
Whatsapp nitakuwa nakupigia huku tunaonana".
Alitumia kama nusu saa kunielekeza ile simu hadi
nilipoikubali kuona dunia ilivyo. Walinisindikiza hadi
karibu na nyumbani kisha wakaondoka kusubiri
majibu yangu kama nimekubaliana nao.
Nilikaa sana pale kufikilia lile jambo kama kwenda
kuwafanyia kazi au nitulie na shughuli zangu
mwenyewe.
Nilipata majibu kuwa bora nifanye shughuli zangu
binafsi sitaki kuwa chini yao kuwa mtumwa kila
muda.
Nilipanga kabisa kuwa sitaki kwenda tena kule.
Ilipita siku kama mbili nikawa nafanya shughuli
zangu mwenyewe ndipo Mke wa Kibona alishindwa
kuishi pale na ndipo akaondoka kabisa kwenda
kijijini.
Nilibaki peke yangu huku nikiwa makini kila hatua
ambayo naipitia. Siku moja nikiwa narudi nyumbani
niliona nyayo za tairi la gari likikunjia pale nyumbani
na kuondoka. Sikutaka kufikiria mengi sana.
Ile naingia ndani tu na gari hili linaingia, walishuka
haraka sana vijana kama wawili. Waliniachia barua
kisha wakaondoka zao. Nikiwa naendelea kuishika
ile barua na sijui ni akina nani anakuja Manyota pale
nyumbani. Manyota alionekana kuwa ana jazba sana
kuliko kawaida.
"Mnali umeridhika si ndio"
Nilipigwa na butwa
"Umeridhika nilijua tu kuwa wewe ndio kila kitu na
ni chanzo cha haya yote"
Alionekana ana hasira ndipo niliingia ndani kwanza
nikachukua maji na kuja kumpatia anywe ili
apunguze zile hasira.
Lakini kile kikombe alikitupilia mbali
"Manyota unaonekana hauko sawa tatizo nini
lakini?"
Nilimuuliza
"Unajifanya hujui sasa hivi sisi tumefukuzwa kazi
kule kwa bwana Paul"
"Mh! Mmefukuzwa kaziiiii!!!"
"Unajifanya kushangaaa sasa hivi wakati naliona gari
la Mr paul hapa kwako kama mara ya pili inakuja
na kuondoka na hapo umepewa ela nyingi na sisi
tumetolewa ili wewe ukae pale sasa tunakuambiaje
sisi ndio wazawa wa bahari tutakuharibia mulemule
yani"
Aliondoka huku akiniacha na mkanganyiko wa
mawazo.
Niliingia ndani kisha nikakaa kitandani na kuifunua
ile barua ili nipate kuisoma. Nilipoifungua
nikakutana na picha moja ya mwanafunzi
nilipomuangalia vizuri alikuwa mwanangu Asante.
Niliifungua ile barua na kukuta maelezo kadhaa
kuhusu ile picha.
""Mnali kama kweli damu ni nzito kuliko maji basi
tunataka kuona jeuri yako. Mtoto wako muda
wowote tunaweza kumchukua na kumpoteza ila
angalia mwanao ana akili sana kumpoteza kiumbe
kama hiki. Tunachotaka sasa ni amri tuletee mizigo
kumi ya maana ya samaki laa sivyo nahakikisha
anaangamia mwanao.
Fungua watsapp"".
Jasho jembamba lilinitoka pale huku mikono
ikinitetemeka sijui hata nifanye nini.
Nilichukua simu kisha nikaangalia nakutana na
video ambayo walikuwa wanaongea na mwanangu
Asante.
"Unaitwa Nani?"
Naitwa Asante
"Ahaa baba yako unamuambia nini"
Baba Nampenda sana na nasoma vizuli na mtihani
nimefaulu
Video ilikatwa hakika nililia sana sikujua kwa nini
nafanyiwa hivi mpaka kwenye familia yangu
inaingiliwa kwa kazi yangu ya kipuuzi ya Uvuvi
daaah!.
 
SEHEMU YA KUMI NA MBILI 12
ENDELEA...............
..................Nilikaa nikawa najiuliza maswali mengi
sana ambayo hayana majibu. Swali kubwa ni kujua
wapi naelekea?. Siku ya mwisho ni pale nilipoona
sitaki kwenda kwa hao jamaa yani kumfanyia kazi
tena bwana Paul nitapambana mimi mwenyewe ili
nimlinde mwanangu. Niliona haina haja sana ya
kujiuliza nilichomoka pale na kwenda sasa muda
muafaka wa kwenda kuanza kazi kwa nguvu zangu
zote.
Niliandaa kila kitu huku nikiwa sina habari yeyote
ile, hakika siku hiyo bahari ilikuwa shwari sana yani
tulivu zaidi ya maelezo. Niliweka mashine ya
kusukumia mtumbwi wangu kisha nikaelekea mbali
sana ya bahari nikipita kuangalia sasa maeneo
mengine ya kuwapata samaki. Nilichokuwa
nakifanya ni kumwaga matunda fulani ambayo huwa
wanayapenda sana samaki kula.
Nilimwaga nyingi kiasi kwamba wale samaki pale
wazoee. Nilipohakikisha kuwa tayari ndipo
nikasonga mbele zaidi kama unavyojua bahari ni
kubwa sana. Niliendelea mpaka nikahisi kama
napotea.
Niligeuza Boti kwa ajii ya kurudi nyumbani sasa.
Wakati nageuza ndipo nikakiona kisiwa kwa mbali,
nilijiuliza kuwa yale maeneo sikuwahi kwenda kabla
ila leo nimepaona sasa ngoja siku nyingine nitafika
kule.
Nilitembea taratiibu kurudi huku nikisikiliza nyimbo
za wasanii wetu wa bongo hapa. Nilikuwa napenda
sana kusikiliza ngoma za bongo kwa kuwa ndizo
zilikuwa zinanifanya nijisikie nafuu sana.
Simu yangu iliita kuashiria kuwa kuna mtu ana piga
hakuwa mwingine alikuwa bwana Paul.
Nilimpotezea kabisa. Alipiga tena ndipo nikapokea
simu yake.
"Mnali!!"
"Ndio mimi unasemaje?"
"Mnali, unaongea na mimi hivyo!!"
"Kwani nini unanifuatilia sana jamanii tafuteni watu
wengine wenye digilii zao za uvuvi mimi sitaki"
"Sawa basi fungua watsapp sasa hivi kuna ujumbe
mfupi naamini utakufurahisha sana.."
"Usinitisheee nakuambia usiniti....shee"
Bwana Paul akakata simu.
Nilitamani ile simu kuitupia ndani ya maji lakini
niliona vyema kwanza niangalie ule ujumbe ambao
kaniambia.
Pale nilipo mtandao ulikuwa unasumbua sana hivyo
sikuwa na papara sana kwanza alishanichanganya.
Nilitembea lakini kwa mbali nikahisi kama mlio wa
boti ukinifuata kwa kasi mbele yangu. Ilinibidi
nisimame kwanza ndipo nijue kuna jambo gani
kabla hata haujachukua hatua yeyote. Nililiona kweli
linakuja kwa kasi zote nilichuchumaa kisha
nikageuza kuelekea upande mwingine japo
haikuwazuia wao kutonifuata.
Hatimae walinikaribia pale nilipo wakiwa na ile
spika ya kutangazia matangazo.
Wakiwa kwa mbali walisema kwa sauti iliyonifanya
mimi kusikia
"Mnalii, umekataa agizo la tajiri yetu na kumfanya
apoteze wateja wengi kwa ajili yako...sasa tunakupa
dakika tatu za kusali ili tukupoteze kabisa".
Walinisogelea hadi pale nilipo na ndipo wakawa
wananitisha sana. Sikuweza kuona sura zao.
Nilipatwa na wasiwasi sana baada ya ile kauli
ambayo wameitoa mbele yangu. Nikawa najiuliza
wametumwa kuniua kwa lipi?. Hata sikuweza
kusema ndipo nilishtukia tu kitu kimekita kwenye
Boti yangu alafu ikatoboa sikujua kitu gani
nilichoshangaa ni sauti pamoja na mtumbwi
kupitisha maji tu.
Maji yalizidi kuingia ndipo wale watu waliondoka
nilisimama na kuinua mikono juu ili hata wanione
lakini haikusaidia.
Nilibaki kupakua yale maji ili yatoke maji yalikuwa
yanaingia kwa kasi sana
Kila yalipokuwa yanazidi kuingia ndani na mimi
ndipo niilipokuwa nachanganyikiwa zaidi na kama
kama kuogelea ndio lakini siwezi kwa ule umbali
wote ambao nilikuwa kutoka nchi kavu. Mtoto wa
kiume hofu iliingia zaidi ya maelezo japo na ukubwa
wangu lakini chozi lilianza kujitokeza bila hata
kulitaka.
Nilifanya kazi ya kupakua lakini nguvu ziliniishia .
Ajabu zaidi mvua ilionekana kuanza hatimae mvua
kubwa ikaanza kupiga pale, sikuwa na hata la
kufanya zaidi ya kusubiria kifo ndicho ambacho
kilibakia. Nakumbuka kauli yangu ya mwisho pale ni
kuwa Kama nimewafanyia dhulma basi naomba
msamaha ili nikifa niwe huru.
Hii yote kutokana na kutapatapa tu bila hata
mpango kwa kuwa kifo kipo mbele yangu.
Mawimbi makubwa yalizidi kunipeleka tofauti na
mimi ninakotaka kwenda.
Yalinisukuma upande ule ambako nilitoka. Hofu
ilitanda sikujua nifanye jambo gani ili kujinasua na
lile swala ambalo linaendelea pale. Hatimae wimbi
likanipiga na kujaza maji mule nilimo, daah!.
Mengine yalikuwa yanaingia mvua inazidi na
mawimbi pia yalizidi kuniyumbisha hatimae nauona
kabisa unazama nikajiokoa kwa kuruka na kuanza
kupiga mbizi ambazo hazikuleta matumaini kabisa
kwani, nilichoka kwa haraka sana.
Ma ya bahari ni tofauti kabisa na ya mto na
mengine. Maji ya bahari ni yenye chumvi sana kwa
wale wasioyajua.Yaliingia mdomoni puani
nikashindwa kuhema.
Kilichoendelea pale sikuwa nafahamu kabisa kwani
nilizimia yani.
Muda nashituka toka usingizi wa kifo ni usiku.
Nilihisi tumbo kujaa, kifua nacho kujaa niliinuka
nashindwa nguvu zimeniishia. Sikujua ni mahali gani
pale nilipo kabisa kwa kuwa mazingira ni ya usiku
ila kilichonijulisha kuwa sipo kwenye maji ni
mchanga ambao nilikuwa nimeushika mikononi
mwangu huku nikiwa nimelala chali.
Nilikohoa ndipo nikatapika maji kwa wingi sana,
niliendelea kutapika hivyohivyo mpaka pale
nilipopata nguvu ya kuinuka.
Usiku mkubwa sana na mazingira yalinitisha kwani
sikufahamu. Nilisimama huku nikiwa
nayumbayumba tu. Mbele niliwaona kama watu
wawili wamesimama.
Nilijitahidi kutoa sauti nikashindwa kbisa kutoa.
Nilivuta kumbukumbu hakika sikuwa nakumbuka
kitu nikawa kama nimezaliwa upya kabisa.
Kwa kuwa nilikuwa tofauti kabisa pale. Nilishindwa
kuwafuata wale watu ndipo nikaanguka chini na
kushindwa kabisa kufanya jambo lolote lile pale.
Asubuhi na mapema sana jua likiwa limechanua na
kuwa ng'avu niliinuka. Mbele yangu nilipoangalia
naona nyayo za simba mnyama ambae hana mzaha
kabisa, lakini si nyayo za simba tu ila pia na za
binadamu zipo pale, nikajishtukia baada ya akili
yangu kurudi kuwa nilipo sio pale ambapo
nastahiki. Nikajua labda nimekuja na mtumbwi
wangu kumbe hapana sijui hata nimefikaje pale.
Nikakimbia kuelekea karibu na maji nashangaa
nimefikaje lile eneo. Nikavuta picha ndipo
nikagundua kuwa ni pale kisiwani ambapo nilipaona
jana yake.
"Eeeeeh! Mama yangu hapa ni sehemu gani, na
nimefikaje sasa, aaah! Mh! Mbona haya majaribu
sasa je? Hizi nyayo za watu nibwatu wa aina gani
wanaishi huku je? Na wao ni wavuvi kama mimi au
je? Wanafanya kazi gani."
Nilibaki kujiuliza huku nikiwa nimeshika kichwa
changu na mikono kama mtu ambae kafiwa na
wazazi wake wote.
Nilijipa moyo baada ya kuona zile nyayo nikajitahidi
kwenda kuanza kuzunguka kile kisiwa nijue kuna
jambo gani hasa lipo mule. Niliingia zaidi
kuzunguka kile kisiwa sikuona hata pakuanzia
kuingia ndani.
Wakati nazidi kuangalia ndipo nikawashuhudia watu
kama watatu wakiwa wanakula nyama ya mnyama
daah! Kilichonishangaza ni maumbile ya wale watu.
Vichwa vyao ni vidogo sana kiasi kama ngumi mbili
zilizounganishwa. Hawakuniona kabisa. Niliendelea
kuwaangalia ndipo nikatikisa mguu wangu kutokana
na kutokuwa na nguvu maana ulikuwa umechoka
sana. Waligeuka nyuma wakapiga kelele.
""Nyaaaaaaa nyaaaaaa""".
Wakanisogelea kha! Japo nguvu sikuwa nazo
nilikimbia huku wakinifuata kwa nyuma
niliposhindwa nikajirusha kwenye maji baada ya
kuhisi kuwa na udogo wao hawatoweza kuingia.
Niliwashangaa wanarudi huku wakirukaruka yale
maji na upiga kelele.
Walikaa pembezoni kabisa na mahali panapoishia
maji wakinisubiri ndio ikawa afueni yangu pale.
 
SEHEMU YA KUMI NA TATU 13
ENDELEA...............
.......Ilinibidi nikae mule kwenye maji kwanza huku
nikitafakari nimefika vipi mule na wale viumbe
nawakwepa vipi.
Ilikuwa ni kasheshe sana pindi vile viumbe vya
ajabu nilivyoviona kama vibwengo hivi vinanisubiria
muda wote vikiwa vinatembea pembezoni mwa
ukingo wa bahari.
Ilikuwa ni asubuhi hiyo maana jua lake lilikuwa tamu
sana kwenye mwili wangu. Nilipiga hesabu nyingi
sana lakini ziligoma. Ndipo nilipoamua kutafuta
msaada kwa kuangalia kama kuna mtu yeyote
ambae anaweza kujitokeza na kunisaidia. Baada ya
muda kupita vile viumbe viliondoka mbali kabisa na
pale nilipo ndipo na mimi nikaanza kujitoa
kidogokidogo sasa kuelekea tena kule kwa
mwanzo.
Mwendo wangu ulikuwa makini kwa kujua pindi
likifumuka mimi nakimbilia kwenye maji, hatua ya
kwanza, ya pili na ya tatu nikawa nimefika eneo
husika la Kisiwa kutoka baharini.
Nilichungulia kwa umakini wote nikaanza kuingia
sasa kutoa miti ambayo inanizuia mbele yangu.
Jambo la kwanza nashukuru sikukutana tena na vile
vibwengo mpaka nafika ndani ya kisiwa.
Mule ndani hakika ni pabaya sana. Miti imeshonana
na kuweka kiza kizito. Sauti za ndege na wadudu
pekee ndizo zilikuwa zinatawala pale. Wakati
nashangaa kuangalia juu ndipo nikajikwaa na
kudondoka chini, pale chini nilikutana na mizoga ya
watu pamoja na wanyama kadhaa.
Mara yangu ya kwanza kumuona mtu aliyekufa
ilikuwa siku hiyo, nilitetemeka sana kiasi kwamba
nguvu pia ziliniishia nikashindwa hata nifanye nini.
Nilijiziba mdomo baada ya kumuona kiumbe mmoja
akikatisha mbali na pale.
Niliogopa sana na kujua sasa maisha yangu
yamefikia mwisho kabisa na vile nilivyokuwa
natarajia kabisa. Nilinyanyuka ili nitafute hata
sehemu ya kujihifadhi na wakati huo tumbo langu
sasa linadai chakula. Siku ya balaa ni balaa tu na
siku ya bahati ni bahati tu ndivyo hivyo ilivyo.
Wakati natoka kwenye zile maiti nilikutana na
mtumbwi upande mwingine wa kisiwa, daaah!
Nilifurahi nikajikuta napiga yowee kubwaaa.
"Yerewiiiiiiiiiiiiiiiiii"
Nakuja kushtuka kumbe zile kelele zilisababisha
mambo mengine baada ya ndege juu kuruka kwa
wingi na sauti za wale viumbe nikivisikia kwa mbali
kama wanakuja pale nilipo.
Nilipiga hatua kama za wanajeshi hivi wakipiga
gwaride lile la guz-match kama hatua tatu nakutana
na ule mtumbwi lakini.
Niliduwaa baada ya kuona ndani yake kuna mwili wa
mtu.
"Daaah!!! Hawa viumbe washenzi wanaua watu hivi
jamani yalaaa sasa nafanyaje".
Niliongea peke yangu mule msituni, mwanaume
siku zote penye shida ndipo anajua anafanya nini.
Niliukokota japo ulikuwa mzito nilijitahidi nikaona
bado nafanya kazi ya bure.
Nilichukua miti kadhaa jambo la harakaharaka huku
nikiwa na ujasiri wa hali ya juu sana niliipanga kwa
chini yake kisha nikaisukuma na likatambaa juu ya
miti ile ikawa kama kiterezeshi.
Nilifanikiwa kulitoa hadi nje na kuona bahari ilipo.
Nilifurahi sana na nikajua sasa nyumbani napaona
japo sijajua nyumbani ni upande gani. Nikaipanga
tena nikatumia nguvu zangu zote likatereza hadi
sehemu ya maji yalipoanzia.
Wakati nafika kwenye maji wale viumbe wanaingia
maeneo ya ufukwe yale kutoka ndani ya kisiwa.
"Ooooh!! Jamanii mtumbwiii haraka kwendaaa!!"
Niliufosi mtumbwi kusonga kwenye maji kwa
maneno nikiamini ndio njia ya pekee kwangu ya
kuondoka pale.
Ndani ya mtumbwi au Dau lile bado ile maiti
ilikuwepo iliendelea kutoa harufu kali lakini sikujali
bola ya hayo kuliko mimi kubaki pale na kuuliwa na
wale viumbe.
Nilishukuru kuufikisha kwenye maji, kwa sababu
najua ujanja wa wale viumbe huwa hawawezi
kugusa maji kabisa.
"Shenziiii!!! Mnadhani mtanipata marabuuku mimi
ndio Mnali baba yake Asante sasa nyinyi viumbe
mtakula kwa macho".
Nilijitapa sana pale kwa madaha bila hata kujua
jambo la mbele baada ya kumtukana mamba kabla
ya kuvuka mto.
Jamani haya mambo yaacheni nahadithia kama
mazuri ya kufurahisha ila inahuzunisha kwani,
nilitembea kama hatua tatu za mguu ndipo nikaona
kwanza niondoe ile maiti imezidi kunitia woga, ile
naondoa kumbe ndio ambayo ilisaidia kuzuia maji
kupenya. Kutokana na ule mwili kukaa kwa muda
mrefu uliozesha mpaka mtumbwi kwa chini lakini
maji mwanzo hayakupita kwa kuwa ulikamatana na
ule mwili.
Baada ya kuuondoa ndipo maji yakaanza kuingia
kwa kasi, niliduwaa sana kama kifaranga asiekuwa
na mama vile.
Ndipo ikanijia kumbukumbu kuwa nimefika pale
baada ya watu wa Paul kutoboa Boti langu na
kupitisha maji kama vile.
Chozi lilianza kunitoka moyo wangu
ulipwita kwa hofu kubwa sana hivyo nikajua sasa
sina jinsi inabidi nitoke kwenye mtumbwi na
kuuacha ukizidi kujaa maji na kuzama taratiiibu.
Hiyo ndio inaitwa Usitukane mamba na mto
hujavuka. Njaa ilinigonga sana kiasi hata nguvu
zilinishia. Nilikaa kwenye maji yale huku
nikiwaangalia vile viumbe vya ajabu.
Ningejua ningewakubalia wale jamaa kuwafanyia
kazi zao naamini haya leo yasingetokea, lakini kwa
nini wanionyeshe roho ya kutu kama hii lengo lao
kuniua sasa jamani daaah!!! Uvuvi wangu mdogo tu
unanipa shida kama hizi leo nakutana na viumbe
hata siwajui je wangapi wanawafahamu hawa.
Ilipita kama majira kadhaa jua likiwa katikati,
lilinifanya nioene mwili unachemka kwa joto kali
sana.
Hatimae sijifahamu kabisa baada ya kuona
naanguka kwenye yale maji kwa kukosa nguvu,
macho yangu yalipoteza nuru na kiza kikitanda.
Sauti za wale viumbe zilitawala masikioni mwangu
sikujua kama wanakuja kunichukua au nini. Ndipo
nikapoteza fahamu na sikufahamu kipi kilifuata.
Nakuja kushtuka ni baada ya kujiona nipo kwenye
moja ya kajumba fulani cha miti nikiwa nimelazwa.
Nilikurupuka na kukutana uso kwa uso na binadamu
ambae kajichanjachanja kama wale wamakonde
wenyewe wale.
Alininyooshea mkono usoni kwangu kama trafiki
anaposimamisha gari kwa kuonyesha kiganja
chake. Nilibaki kuduwaa nikiikodolea ile mikono.
Basi nilirejea kuegemea lile tawi ambalo
limejengewa kama nyumba fulani hivi.
Yani huwezi kuamini niliapa mimi mwenyewe huku
chozi likiwa linanitoka "yani nikifanikiwa kutoka
huku bwana Paulo atanieleza".
Ajabu zaidi ni pale nilipohisi maumivu makali sana
maeneo ya tako langu la kushoto. Jamaa akanivua
suruali nikagoma khaa!! Huyu vipi anivue suruali
mimi mwanaume pumbavuuu unataka uni nini mimi
nyooo!.
Nilimuangalia kwa jicho la kumtamani kumtafuna ila
sikuwa na jinsi nipo kwenye himaya yake,
alilazimisha kunivua suruali nikagoma daaah!!!
Nilipokea kofi la shavu nikatulia tuliii,
Akanivua akanigeuza, nilipeleka mkono wangu na
kupapasa pale nilipohisi maumivu kumbe kuna
kidonda kama shimo hivi.
Akaniweka dawa gani aiseee nilipiga kelelee
akanitwanga vidole vya shingo sehemu za mshipa
uliokuwepo karibu na sikio nikakata moto.
Nakuja kushtuka maumivu yanazidi kuwa makali
nilijigeuza na kuona kweli kulikuwa na jeraha ila
sikufahamu limetokana na nini?.
Kingine huyu jamaa haongei kabisa na hapo ilikuwa
kama saa za jioni.
Nilimuona mbali kidogo akifanya shughuli zake. "Ina
maana huku wanaishi watu kweli?, au huyu jamaa
ndio walewale maana ila kawa msaada wangu
tosha". Ilipofika majira ya usiku ndipo naisikia sauti
ya huyu jamaa.
"U..u..unaitwa..na..ni?"
Nilishangaa kuwa umbe anaongea ila kama
kigugumizi hivi
"Khaaa! Unasemaje?"
Nilizidi kumuuliza mpaka akachukia sana na
kumuona kakasirika.
"Oooh! Samahani mimi naitwa Mnali"
Alitikisa kichwa
"U..u...k..u...umel..etwa na.. nani?"
Daaah! Aisee hiki kisanga ilibidi nilazimishe
kumuelewa hivyohivyo anavyotaka.
"Mimi sijui nani kanileta, nilipata ajali kule ng'ambo
nikazama majini nikajikuta natokezea huku alafu
nawakuta watu wapo huku wadogoooo wanakula
nyama mbichii..."
Nilikuwa namuelekeza na huku najitahidi vitendo
kumuambia.
"Po...le..nak..wenda...kula"
Aliposema hivyo kuwa pole alafu anakwenda kula
aliruka kutoka pale juu ya mti hadi chini
akatokomea. Daah!!! Sasa anaenda kula mimi
nakula wapi na nitakula nini?.
Aliporejea alikuja na nyama mbichi pale.
Akanikabidhi. kwa kuwa nilianza kumjua tatizo lake
la kuongea nikamuuliza.
"Moto uko wapi tuchome ili tutafune?"
Nilimuuliza kama mara tatu hakunijibu ndipo
alinionyesha kwa vitendo tu.
Akachukua kipande chake akaanza kutafuna jamaniii
"Tobaaaaaaaaa!!"
Yani na mimi nile nyama mbichi....
 
SEHEMU YA KUMI NA NE 14
ENDELEA......
........Nilimkodolea Macho huku akiifakamia ile
nyama, Aiseee nilishindwa hata kuila nikaiacha chini
ndipo ilipodondoka chini.
Jamaa alinyamaza hata kuongea kabisa hakutaka
hata kusema neno lolote. Kwa kuwa nilikuwa
naumwa sana na sikujua nini kimeniumiza kwenye
moja ya kalio langu.
Bwana nikajilaza pale huku nikiwa simuamini kabisa
pia natafakari juu ya maisha ya yule jamaa. Ilikuwa
usiku sana niliposhtuka baada ya kusikia vile
vibwengo vikiwa vinapiga kelele pale chini. Nyumba
au kibanda cha huyu jamaa ilikuwa juu ya mti
mkubwa sana ambao ulikuwa na matawi mengi
sana. Jinsi alivyokuwa ameijenga alifahamu
mwenyewe, basi wale viumbe walizidi kupiga kelele
za ajabu, nilichungulia chini na kuwaona wakiwa na
macho yenye rangi nyekundu yalikuwa yanang'aa
sana, hakika niliogopa kiukweli.
Nilianza kuhaha pale lakini nilichoshangaa yule
jamaa alikuwa kimya hana hata dalili ya kulala
alikuwa anawasikiliza tu. Mpaka asubuhi naamka
pale kidogo nilijihisi vizuri kiukweli maana maumivu
yalipungua kiasi hata kusimamisha mguu niliweza
kwa kweli. Nilipata kujiuliza maana akili yangu
tayari ilishanijia kutaka kuondoka pale.
Sikumbuki kule kisiwani nilikaa kwa muda wa wiki
au masiku mangapi ila nilichukua muda mrefu
nilichojua ni jua kuzama na kutokeza giza kutoka na
kuingia yani wengine wanasema ukawa usiku ukawa
mchana. Katika hayo masiku ambayo niliweza
kukaa mule msituni hadi pale nilipozoeana na yule
jamaa. Historia fupi ya yule kijana iliweza
kunisisimua mpaka nikaanza kunitoa machozi.
Ila mpaka anafika hatua ya kuhadithia kwanza
nilifanya kazi kubwa ya kumfundisha lugha ya
vitendo, kwa kuwa hakuweza hata kuongea kwa
muda mrefu zaidi ya hapo hasira itamshika na
kukaa kimya tu.
Aliniambia na yeye alikuwa anafanya biashara zake
za kawaida kipindi cha zamani sana kwa upande
mwingine tofauti na ule ambao mimi nilitokea,
katika shughuli zake alijikuta anaingia kwenye hatari
kubwa sana baada ya kushawishiwa na wakongwe
wa mji yani vile vibosile kuwa kuna mali mahali
fulani kwenye bahari.
Walimuomba huyo jamaa sana kwa kuwa kidogo
ana ujuzi wa kuogelea waweze kwenda nae kisha
wakifika eneo ambalo walisema kuna mali basi yeye
aingie chini ya maji kisha achukue wagawane kwa
pamoja. Ndipo siku ya siku ikafika na watu
wakajiandaa ili kwenda kuchukua mzigo ndani ya
bahari. Huyo jamaa alibebwa japo ni mara yake ya
kwanza kufanya kazi na tajiri huyo ila aliona jambo
la kheri kwake kufanya nae ili aweze kupata
chochote kitu.
Safari ya boti ilianza pale hadi maeneo fulani hivi
ndipo boti likasimamishwa kwa ajili ya kuifanya kazi
yao. Jamaa huyu aliingia ndani ya maji hadi pale
alipoelekezwa na kweli alikuta sanduku kuukuu la
zamani sana lakini kulibeba alishindwa kutokana na
uzito na kukamatiana na udongo wa chini pale.
Aliibuka na kuwapa taarifa kuwa ameliona ila hana
nguvu ya kulichukua, ndipo ilibidi itumike njia
mbadala ambayo ni kuchukua ndoano kubwa kama
nanga na yeye kwenda kuivalisha kisha wao kuivuta
hadi juu.
Mafanikio yao yalizaa matunda sasa jambo la ajabu
sana pale tu yule tajiri anavyobadilika kama
kinyonga kwa kumbadilikia jamaa huyu huku
akimuambia kuwa pale hana chake, alijitetea kwa
kusema yeye ndie kaingia je? Angewapa taarifa
kuwa halipo au angekataa kuja.
Japo kauli hiyo haikuwafanya wao kuacha kumcheka
na kumtisha huku wakitaka kumdhuru. Jazba na
hasira za kudharauliwa ilimfanya kutaka kulishika lile
sanduku ili kulitupia mulemule, lakini walimshikilia
huku wakimtundika makonde ya nguvu, jamaa
hakutaka kuachia mpaka pale damu zinamvuja kwa
wingi lakini alilishikilia kwa nguvu zake zote na
kulisukuma mule ndani ya maji. Baadhi ya wale
matajiri waliogopa kwa woga hawajui kuogelea pia
kupoteza lile sanduku walioamini kuna mali, moja
wa tajiri ambae alipigana sana kumpiga jamaa ni
mzungu aliyefanya utaratibu wa kugundua kama yale
maeneo yana mali zilizoachwa kwa kipindi kirefu
sana. Lakini mpaka jamaa anapigwa ngumi ya koo
alilegea kisha akadondoka na lile sanduku ndani ya
maji, lakini pia alijitahidi kwa zile nguvu alizonazo
mpaka kulifikisha mahali pengine kabisa na
kuliachia.
Liliingia ndani chini kabisa ya bahari, na yeye
akapoteza fahamu. Mpaka siku anajiona yuko hai
yuko pembezoni mwa kisiwa wakati huo kang'atwa
na wale viumbe ambao mimi wamenibana.
Anashangaa lakini ilimbidi kuendana na masiha yale
aliyonayo.
Kila siku anabadilika na kupenda kula nyama mbichi
mpaka pale alipofikia.
Daah! Alikuwa ananihadithia lakini mimi pale chozi
lilianza kunitoka kwa wingi.
Nilijua kuwa mwenye matatizo ni mimi Mnali peke
yangu kumbe kuna watu wana matatizo zaidi yangu
daah! Ama kweli Mtazame aliye chini yako ili
umshukuru mungu kwa kichache ulicho nacho, ila
usimtazame aliyejuu yako usije kumkufuru mungu
kwa nini hajanipa.
Hapo ndipo nikapata nguvu sasa ya kujua naishi vipi
pale. Ila nilimuuliza jambo moja.
"Ina maana baada ya wale viumbe kukung'ata ndio
wamefanya sasa uwe unatafuna nyama mbichi?".
"Ndio..baada ya kuning'ata ndio nilianza kuzipenda
sana nyama mbichi".
Daah! Nilijishtukia sana.
"Ehee! Kwa hiyo mimi hili jeraha nimelipata kwa
kung'atwa au?"
"Ndio.."
"Tobaaaaaa!!, kwa hiyo na mimi nitaanza kutafuna
nyama mbichi"
"Ndio..ila dawa niliyokupa itakuzuia kidogo
hutotafuna kwa kiasi kikubwa kama mimi"
Jamanii ina maana nimeathilika na hali ya wale
wanyama kweli.
"Sasa unaweza kunisaidia mimi kurudi nyumbani
kwetu?"
"Ndio utarudi ila unisaidie kitu kimoja"
"Kitu gani?"
Nilimuuliza
"Nataka tukachukue lile sanduku, kisha ufike
nyumbani baada ya kukupa maelekezo ndipo ukirudi
utakwenda kwenu".
"Sasa kwa nini niende peke yangu? Bora twende
sote".
Lakini mwisho wa muda tulikubaliana kuwa
tukatafute lile sanduku kisha mimi nirejee nyumbani
ndipo nipange safari ya kurudi hadi upande wa pili
wa bahari kwao kufanya kile alichoniambia.
Ghafla anapita swala karibu yetu ndipo akaniziba
mdomo, alitembea taratibu sana hadi akamrukia na
kumkamata pale. Muda mchache alimrarua vibaya
mno na kuanza kunyonya damu yake kisha akamleta
pale kwangu.
Ukiangalia nina kiu ya maji haswaa na yeye ndio
anasema kuwa damu ya wanyama ndio maji yake
kule hakuna kitu chochote zaidi ya vile afanyavyo.
Niliinama na mimi nikajikuta nina hamu ya ile damu
maana kama nimeathirika hivi, mate yalinitoka huku
nikitamani ile nyama.
Niliinama na kuanza kuchukua mnofu na kuuweka
mdomoni daaah! Nilitafuna ila kumeza nilishindwa
nilificha tu mdomoni na kutema. Nilipata wazo
kuwa nitafute mwanzi mkavu mkubwa, nilipoupata
nikauvunja kati kwa kati kisha nikaulaza chini,
nikakata kijiti cha mwanzi uleule kisha nikanza
kusugulia pale kwenye mwanzi mkubwa penye
uwazi mkubwa uliopo.
Wakati huo nyasi nimezisogeza, jamaa alikuwa
ananiangalia sana kile ninachokifanya. Hadi moto
unatokea anashangaa kwani hakuwahi kufikilia kitu
kama hiko ndipo wahenga wakasema "Ukijua hili,
mwenzako anajua lile".
Niliweka kuni pale moto ukawa mkubwa ndipo ule
mwanzi nikaufanya kama kisu maana nao unajitahidi
kwa makali.
Nilikatakata nyma ambazo ziliwezekana, kisha
nikazibanika sehemu kwenye mjiti mkubwa kisha
nikawa naongeza kuni. Sikujua ilichukua masaa
mangapi, zilikuwa tayari ndipo nikampa atafune
kwanza.daah! Alifurahi sana ndio ikawa chanzo cha
jamaa kuacha nyama mbichi.
Sikujua ni siku ngapi zilipita tena mpaka ile siku
majira ya usiku ananipeleka sehemu ambayo
kulikuwa na boti nzuri kidogo hivi ambayo
iliwezekana kunitoa pale. Niliweza kutumia nguvu tu
kuisukuma ile mashine maana hata mafuta haikuwa
nayo.
Safari sasa ilianza mimi na jamaa kuelekea yale
maeneo husika. Tulipofika ndipo akaniomba nitulie
kwanza aliniambia kuwa anaenda na kamba
akiifunga basi ataitikisa kisha mimi niivute tu.
Kweli muda tu aliingia humo kisha baada ya muda
kidogo akaitikisa kuhashiria kuwa niivute sasa.
Niliivuta ilikua ni nzito sana kupindukia. Nilivuta
hadi inafika juu kweli ni sanduku dogo hivi la
zamani. Nilibaki kumsubiri atokee lakini kimya.
Nilisikitika sana baada ya kupita masaa mengi
jamaa hajatokea, nikajua kuwa kajitoa maisha yake
kwa ajili yangu pia nilimshukuru sana.
Nilitoka pale mdogomdogo kutafuta eneo ambalo
nilitokea. Safari yangu ilikuwa ndefu sana mpaka
njaa ikanikuta. Hali ya mwili wangu ilibadilika sana
pale nilipokuwa natamani sana nyama mbichi,
nilijilazimsha kukataa yale mazingira lakini yalinizidi,
hadi sasa nikafanya mpango hata kuwakamata kwa
kuwachoma na mjiti wale samaki waliokuwa
wanafuata nyuma kama wanacheza.
Nilibahatisha mmoja na kuanza kumtafuna vilevile.
Ilitulia kidogo. Mabadiliko ya mwili wangu sikujua
yanaenda kufikia wapi. Nilitembea usiku na mchana
hadi siku nabahatisha kuona ufukwe kwa mbali sana
watu wakiwa wamefurika.
Sikufahamu nini kilikuwa kinaendelea pale,
nilichohitaji mimi kufika nyumbani kwangu kwanza.
Nilihisi kama nitajulikana kwani nilifahamu kuwa
watu wengi wanajua kuwa nimekufa ndani ya maji
kama Kibona. Nilisubiri ifike usiku ndipo niweze
kuingia mjini kwangu.
Itaendelea........
 
SEHEMU YA KUMI NA TANO 15
ENDELEA.....
.......Nilibaki kuhemea ndani ya chombo changu
huku nikisubiri muda wa kutoka pale, nilipanga
kusubiri mpaka pale usiku utakapoingia ndipo na
mimi niweze kuondoka zangu.
Kila dakika zilivyokuwa zinazidi kwenda na mimi
hamu ya kula nyama mbichi ilizidi japo kuwa
nilishakula kabla na sikutamani kabisa kula tena
maana nilihisi na mimi tayari nitakuwa mmoja wa
wale vibwengo kule kisiwani.
Pia nilipata kujiuliza maswali mengi ikiwemo na lile
la kula nyama mbichi itakuwaje kule ambako
naelekea kuishi na watu ambao mambo hayo ni
tofauti kabisa. Pia swali hilo lilitoweka baada ya
kujiuliza kuhusu lile sanduku lina nini ndani yake?.
Majira hayaongopi yalitembea na kufikisha majira
husika yale ambayo niliyataka. Usiku ulipoingia
ndipp nikaanza taratiibu kutoka, zile kelele ambazo
nilikuwa naendelea kizisikia ziliendelea kuzidi na si
kitu kingine ni Mziki.
Nilikwepesha kidogo na yale maeneo ambayo wao
wapo pale, nilipofika karibu na ufukwe ndipo
nikatoka ndani ya mtumbwi na kuanza kutembea
taratiibu. Mwendo wangu ulikuwa mpole na wenye
wasiwasi sana. Mwili wangu uliendelea kutetemeka
meno yangu yalizidi kugonganagongana huku mate
ya uchu wa nyama yakivuja.
Nilipofika sehemu zile zenye mchanga nilishangaa
kuwaona wanawake na wanaume wengi sana,
mambo yalikuwa tofauti na yale ambayo mwanzo
niliyaacha. Kwanza nilikuta kama vijimba
vimejengwajengwa hivi, na kama miamvuli mikubwa
ipo na watu wa kila aina pale walikuwepo.
Nilitoka sasa nikaitafuta njia ya kwenda nyumbani
kwa kuwa kumbukumbu nilikuwa nazo hapo awali.
Nilifika hadi nyumbani nikakuta nyumba yangu ipo
na kufuli mbili kubwa wakati huwa sina hata tabia
ya kugunga kufuli kubwa tena mbili. Nilifanya
jitihada hata kuvunja mlango lakini nilishindwa ndipo
nikapitia dirishani.
Nafika hadi ndani hakika sikupaelewa kabisa kwani
pamebadilika sana, vitu vilikuwa vimekaa
shaghalabaghala. Nikiwa bado nimeathirika na ile
hali ya uhitaji wa nyama sana nilijikuta najifosi
kutafuta kokote kule iliko japo nilishindwa na
kulala. Nilishtuka asubuhi baada ya kupatwa na
usingizi wa ghafla.
Nje nilipata kusikia sauti za miziki ikiwa inaendelea
kulia tena karibu na nyumbani kwangu pale nilipo,
nilitoka taratiibu na kufungua mlango kwa kuugonga
na nyundo ambayo ilikuwemo ndani humo.
Nilifanikiwa kuvunja na kutoka nje.
Mtu wa kwanza kumuona machoni mwangu alikuwa
mama mmoja ambae namfahamu vyema alikuwa
mteja wangu sana wa samaki. Alivyoniona hakika
alishtuka sana kwani sijajua kuwa alinifikilia kama
mtu wa aina gani pale.
Ila mawazo yangu ya kwanza nilijishika kichwa
nikihisi kuwa labda na mimi nimebadilika na kuwa
kama wale viumbe ambao walikuwepo kule
kisiwani, walikuwa na vichwa vidogo kweli hivyo
nilijishika kuhakikisha kama na mimi nina kichwa
kama chao ndio maana ananikimbia kumbe ni
tofauti kabisa na mafikilio yangu.
"Jamaniiiii njooni! Njooni mumuone Mnali
karudiiiiiii"
Alikuwa anaongea maneno mengi, nilibaki
kushangaa kwa nini alafu alikuwa ananikimbia sasa.
Nilivyoona kuwa wale watu wote wa pale kwenye
sherehe walitoka kuja nyumbani kwangu ndipo
nilipoingia ndani na kufunga mlango.
Nilipatwa na wasiwasi nikijiuliza mimi nimepatwa
na nini mpaka wananishangaa?, sikuwa na majibu
zaidi ya kubaki na kuwasikiliza wao wanaongea nini.
Nilibaki kuwasikiliza kwa nje wakiwa wanaongea.
"Hivi, mnamjua yule Mvuvi mzuri aliyekuwa analeta
samaki wengiii!!" Mtu mmoja aliuliza mwenye sauti
ya kike.
"Ndio tunamjua"
"Ehee"
"Ndio hivo nimemuona kwa macho yangu haya
mawili kwenye nyumba yake hii".
"Acha uongo Mnali umuone wewe si utani huu,
tusimuone sisi ambae tumezunguka bahari umuone
kwenye nyumba hii".
Mpaka pale nikajua kuwa kuna watu walikuwa
wanafanya jitihada za mimi kunitafuta. Nikiwa bado
nipo ndani ndipo nasikia kauli ambayo ilinivunja
moyo kabisa.
"Lakini jamani si ilisemekana kuwa Mnali kafa huko
baharini iweje leo museme mumemuona inakuaje
tena hapo?"
"Ndio ebu lakini kama yumo ndani tufungue kwanza
ili tujue kama ndie yeye au laah!"
Nikiwa ndani humo najisikia hali mbaya ya mwili
natamani kutapika kutokana na kichefuchefu
nilichonacho.
Muda mfupi niliona mlango ukisukumwa taratiibu na
mwanga wa jua ukiingia mule ndani. Nilibaki
kuduwaa pale ulipokuwa wazi na kuwaona watu
wakinishangaa sana.
Nilinyanyuka ndipo watu wakaanza kunikimbia pale,
nilipatwa mfadhaiko mkubwa lakini nilipata fahamu
kuwa wengi wao wanajua kuwa mimi nimekufa
baharini ndio sababu tosha kuwa wananikimbia.
Haikupita dakika hata kumi na tatu gari la polisi
linaingia palepale wanashuka na kuanza kuniangalia
kwa umakini.
Nilimuendea askari mmoja lengo nipate kumuuliza
kulikoni?, lakini na yeye alirudi nyuma na
kunionyeshea silaha aina ya SMG kama mhalifu vile.
"Usinyanyue mguu wako kusogea mbele yangu
nitakumwaga ubongo"
Aliongea yule askari
"Afande mbona sielewi mimi nimefanya nini?" Baada
ya kusema hivyo ndipo wengi wao walishangaa
"Eeeeh!! Anaongea kumbe"
Ghaa! Walijua kuwa mimi bubu. Walinichukua na
kuniweka ndani ya gari. Mimi nikiwa na lile sanduku
langu dogo. Safari hadi kituo cha polisi. Nilipifika
kule wakaniweka chumba changu peke yangu.
Niliendelea kuishi kule kwa masaa kadhaa
niliyoyaona kama mwaka mzima.
Ndipo nikatolewa na kupelekwa hadi hospitali moja
hivi maarufu sana. Walinipima huku nikiwa na ulinzi
mkali.
"Haya, mgonjwa wetu anasumbuliwa na nini pia ni
binadamu au mzuka huyu"
Askari mmoja aliuliza
"Kwa nini awe mzuka?"
Dakatari alihoji
"Ilisemekana kuwa alipotelea baharini kwa kipindi
cha miezi minne na ilisemekana kuwa kafariki,
alivyorejea tukapigiwa simu ndio maana
tunakamleta kwanza tujue afya yake".
Hayo yote walikuwa wanaongea nayasikia maana
nilijifanya kama nimelala.
"Msijali kabisa, ni binaadamu ila kaathirika hapa"
"Daaah!!! Pole yake sasa tunashukuru daktari ngoja
tumpeleke nyumbani akapatiwe uangalifu zaidi."
"Mimi ningewaomba muacheni kwanza ili apate
pumzi kidogo kisha nitawaruhusu afande tumuache
apumzike kwanza".
Askari wote walitoka nje tukabaki wawili tu pale
mimi mgonjwa mtuhumiwa na yule Dakatari.
Ndipo yule daktari wa kike alinifunua shuka yangu
na kuniamsha kwanza, nilimuangalia kwanza ndipo
nikaamka na kumsikiliza.
"Kaka, kwanza pole sana kwa yaliyokukuta ulifanya
kosa gani huko mtaani".
"Dada ni stori ndefu sana ambayo hata hapa
nashindwa kukuelezea nianze wapi maana we acha
tu" nilikuwa natoa chozi kwa uchungu kutokana na
watu wale wanavyonifikilia kuwa mimi nilikuwa
nimekufa japo nia yao ndio ilikuwa mimi nife kabisa
nisionekane.
Yule dada alinionea huruma akachukua leso kisha
akaanza kunifuta chozi langu ambalo hata mama na
baba yangu marehemu wangeliona wasingevumilia
mtoto wao nateseka vile.
Japo mimi mwenyewe nina damu yangu lakini
mpaka pale sijui yuko wapi mtoto wangu, sijui yuko
wapi mwanangu na anaendeleaje.
"Kaka usilie nitakusaidia, ngoja kwanza nakuja ila
lala wakija polisi usionyeshe dalili ya kuamka"
"Sawa dada"
Alitoka nje baada ya muda ndipo akaingia tena.
Akaniamsha kwa kunigusagusa lakini sikuamka
maana nilijua kuwa ni wale askari.
"Mimi hapa bwana amka kwanza"
Niliposikia sauti yake ndipo nikaamka.
"Nimewaambia kuwa kutokana na maradhi yako
mimi nitakaa na wewe kukulinda mpaka unakuwa
salama na wameondoka kabisa".
Nilipumua pumzi kubwa kisha nikamshukuru. Ilipita
siku ile nikiwa mule hospitalini ndipo nikatoroshwa
na yule daktari hadi nyumbani kwake. Ndipo siku
moja nikamuambia ukweli wangu na yale yote
yanayonisibu kuanzia mwanzo hadi mwisho jambo
ambalo lilimuacha hoi yule dada na kumtoa chozi
kabisa.
"Pole sana Mnali yani sikudhani kama kweli kuna
watu wanapata shida kama zako, imeniuma sana ila
kuna swala nataka kujua"
Aliposema hivyo nikashtuka kwanza.
"Kitu gani"?
"Usishtuke tulia tu kwanza...wakati nakupima
kwenye mwili wako nikakuta kidogo damu yako ina
utofauti yani umeathirika"
"Imeathirika..sijajua una maana gani dada yangu"
"Usiniite dada bwana naitwa Salha"
"Sawa Nifafanulie salha"
"Yaani damu yako kuna vidudu vimeingia tofauti na
binadamu anavyotakiwa kuwa navyo si UKIMWI
hapana huo hauna ila una vinasaba tofauti na vya
kibinadamu wa kawaida".
Nilishangaa nini hiki vinasaba maana kwa kutoelewa
au kwa kutosoma huku ni shida.
"Salha, Vinasaba ndio nini?"
"Haaah! Haaah! Haaaaah!"
Alikuwa ananicheka sana nikajua ndio dharau ile ya
kunidharau mimi nisiejua hata kusoma hakika
sipendi na nilikasirika kwelikweli,"basi naomba
usinune sina maana nakucheka mnali ila nafurahi tu
kusikia sauti yako kama hivi ninachomaanisha kuwa
tayari kuna vimelea ambavyo vimeingia ndani ya
damu yako ambayo vinaendesha mwili tofauti na
wewe je? Kuna jambo gani limekupata?"
Niliamua kumficha japo nilijua ipo siku ambayo
atafahamu tu. Ilipita siku kama mbili ndipo
waandishi wa habari wanakuja kwa daktari pale
mimi nikiwa ndani nimelala.
Niliamshwa na wakaanza kunihoji maswali kadhaa
ambayo niliwajibu vyema.
"Bwana mnali, ilikuwaje maana ilisemekana kuwa
ulipotea kabisa kwenye uso wa dunia jambo gani
lilikukuta?"
Aliuliza mmoja wa waandishi wa habari. "Ilo swala
siwezi kulijibu kwa sasa mpaka pale nitakapojua
ilikuwaje kwa sasa hakuna ninachofahamu".
"Sawa vipi kuhusu maisha ya huko uliko hadi hapa
kurudi"
"Hata hilo mkuu sifahamu"
"Tumesikia kuwa umeathirika je? uliuapata kwa njia
gani?"
"Niliapata kwa sababu nina vimelea tofauti na mimi
kama binadamu vilivyoingia ndani ya mwili". Wakati
wanaendelea kuniuliza Salha akaja kisha akanitoa
maana nilikuwa naropokaropoka tu pale. Siku
iliyofuata nasikia kwenye Televisheni na si kusikia
tu na najiona kabisa wakisema mimi ni mmoja wa
wale ambao wamejitokeza kujitangaza kuwa
mwathirika wa UKIMWI daaah!! Walimwengu acha
tu...
 
SEHEMU YA KUMI NA SITA 16
ENDELEA......
.......Nilishtuka mno baada ya kuona zile taarifa za
kuonyesha kuwa mimi nina ugonjwa wa UKIMWI. Si
peke yangu bali hata Salha ile taarifa iliweza kumpa
mashaka sana kilichoweza kuendelea ni mshangao
tu ndio ambao ulitawala kati yetu kujiuliza kwa nini
hawa watu wameweza kunizushia vitu vya hatari.
Ilipita kama wiki hivi mimi nikiwa ndani ya nyumba
ya Salha Daktari mzuri sana, ukweli sikuwa
nafahamu baadhi ya vitu vingi kwani akili yangu
nilishapoteza kabisa kumbukumbu.
Siku moja nikiwa mezani nyakati za usiku mimi na
Salha tunasubiri chakula kiweze kuiva ili tupate kula,
chakula hiko kiliandaliwa na mfanya kazi wa ndani
humo. Salha alikuwa ananitazama sana kiasi mpaka
mimi nilishindwa hata kumuelewa kwa nini
ananitazama kiasi kile.
"Mnali, samahani kama nitakuudhi nahitaji kukuuliza
swali". Nilimkodolea macho wakati huo nimeacha
kwa kile nilichokuwa nakifanya nimsikilize yeye, ila
kwa muonekano nilimuona kuwa hakunielewa kwa
kile alichosema ikambidi aweze kurejea ile kauli
yake."Mnali, naongea na wewe mbona unanikodolea
macho! Naweza kukuuliza swali?".
Hapo nilikohoa kisha nikaongea "Ukimya wangu una
maanisha kuwa ongea nipate kukujibu" alicheka
kwanza "Mh! Yani wewe una vituko sana, eti
tukiachana na maswala ya matatizo uliyonayo je
kwa upande wa maisha yako ya kawaida wewe ni
nani zaidi". Nilivuta pumzi kwani swali ambalo
alikuwa anauliza nililiona ni jepesi sana.
"Mimi hapa ni Mvuvi" niliweza kumjibu kwa
kujiamini kuwa kazi yangu ni ya uvuvi. "Haya
unafaidika na nini kupitia kazi hiyo unayoifanya?".
Aliuliza kwa mara nyingine.
"Mh! Faida ninayoiona ni kuwa napata samaki pia
naendesha maisha yangu kwa njia ya Uvuvi".
Alifurahi sana kusikia hivyo. Muda mchache chakula
kilikua tayari na sisi maongezi yalikuwa yameishia
pale. Ghafla mwili wangu ulianza kuweweseka
baada ya kuona nyama zilizopikwa zipo pale
mezani, mate yalianza kunitoka mithli ya mbwa
koko anaetamani mnofu lakini kupata hawezi.
Salha najua alinishangaa sana kutokana na ile hali
na mimi nilijitahidi kuweza kuficha udhaifu wangu
au matatizo yangu ili nisije gundulika mapema
mbele za wale wenye kunipa msaada japo
sikufahamu ile kauli ya wahenga kuwa ( Mficha Uchi
Hazai ). Baridi lilianza kunishika kwa kasi sana alafu
misuli yangu ya miguu ilianza kunishika sana huku
ikivuta kwa kasi ya ajabu kama tu aliyekamatwa na
ugonjwa wa Ngili. Mambo yalianza kubadilika pale
mezani. Harufu ya ule wali ulianza kunichefua kisha
nikatapika kabisa pale sakafuni.
Salha na yule dada mfanya kazi walihaha huku na
kule ili kunisaidia binadamu mwenzao, Salha
nilimsikia akiwa analia sana huku akilalamika kuwa
nini kimenikuta, ndipo ghafla sikusikia sauti yake
tena pale sebuleni zaidi ya yule mwenzake, punde
Salha namuona akitokea chumba cha karibu na
sebule akaja pale nilipo.
Nilisikia kitu kikiingia mkononi mwangu kichungu
sana kumbe ni sindano. Nilipoteza kabisa nguvu na
kulala palepale, kwa mbali nahisi kama nabebwa
hivi alafu naachwa mahali kumbe nilikuwa
napelekwa kitandani.
Majira ya usiku nilinyanyuka ilikuwa kiza totoro,
nilipapasa kitandani nikahisi kama kuna mtu yupo,
nilinyanyuka polepole kwa kuwa niko kawaida
kabisa.
Nilinyanyuka kisha nikatua miguu yangu juu bila
hata kumgusa yule aliyepo kitandani kwa kuwa
sikuwa namfahamu hapo mwanzo. Nilipapasa ukuta
ambao nilijua kuwa swichi niliyoelekezwa kuwa
ndipo pa kuwashia nilibonyeza lakini umeme
haukuwaka kabisa.
Hakika nilichoka sana nikabaki nimeduwaa pale
natafakari 'hivi hii hali yangu wapi inaelekea ina
maana kuwa nitabadilika moja kwa moja kama wale
viumbe?, lakini tofauti na hilo kwa nini yule jamaa
kule kisiwani aliniambia nisije kumueleza yeyote
kuwa kile kisiwa kipo kule na kuna wale viumbe?
Je? Nimueleze huyu dokta apate kunisaidia au nikae
hivihivi nikiuficha ukweli wangu?'.
Wakati naendelea kutafakari ndipo umeme ukawa
umerejea. Macho yangu ya kwanza ni kupeleka kule
ambako yupo yule mtu pale kitandani. Ndipo naiona
sura ya Salha.
Nilishtuka nikajiuliza kwa nini yeye alikuja kulala
pale kitandani kwangu. Wakati huo akili yangu
ilikuwa kama imepumbazwa hivi na yale matukio ya
kila mara kwenye mwili wangu. Tumbo lilianza
kudai chakula na wakati tangu usiku sikula
kutokana na yale majanga niliyoyapata. Niliamua
kuufungua mlango kwa upole sana. Nikazipiga
hatua kadhaa kisha nikaelekea maeneo ya jikoni.
Chumba hiko cha jiko kulikuwa na kila aina ya
chakula vyakula vingi vilikuwa vimehifadhiwa
kwenye Mafriji.
Niliwasha taa kisha nikaanza kufunua sufuria moja
baada ya jingine. Ghafla pua zangu zilianza
kuchezacheza, zikitanuka na kupata harufu ya nyama
iliko, nilijilazimisha kutoitaka hiyo harufu lakini wapi
ilizidi kunipanda kwenye akili yangu. Hatimae
nilisonga kule ambako iliko moja kwa moja hadi
kwenye Friji moja nilifungua nikakutana na nyama
ambayo iliwekwa ili isioze ilikuwa bichi. Akili yangu
ilibadilika kabisa na nikajihisi mtu tofauti maana
mpaka mate yalianza kunitoka. Nilijifosi kutochukua
lakini acha tu nilipata tabu sana, nikachukua kipande
kimoja nikakitafuna na kingine na kingine mpaka
kingine.
Hapo ndipo hali ilirejea kabisa. Lakini nilijiona mtu
mwenye nguvu nyingi sana alafu hisia za mwili
zilianza kunitawala. Kila kiungo changu kilikuwa na
hamu ya kufanya kazi, mikono yangu ilitamani hata
kuvurugavuruga vitu vilivyomo mule ndani, miguu
yangu iliwasha ilitamani hata kukimbiakimbia. Pia
sehemu zangu za siri nazo ndio usiseme nilijichafua
kama mara mbili hivi.
Nguvu ya Uume wangu ulikuwa mara dufu na
kawaida. Nilijilazimisha kutoka na kurudi kule
chumbani lakini huku jikoni sikuweka sawa kama
nilivyokuta mwanzo.
Nilichojua ni kujifuta tu ile harufu mdomoni. Kama
nilivyokuambia kila kiungo kilihitaji kufanya kazi
yake vile ipasavyo, nilimkuta bado Salha akiwa
kalala huku kajifunika shuka akiacha kichwa tu.
Salha nadhani alikuja lala kule kutokana na hali
yangu kuwa mbaya wakati ule wa usiku. Mimi tayari
akili yangu inanituma niweze kumuingilia kimwili
Daktari huyu aliyejitolea kunipa msaada.
Niliweza kumfunua ile shuka na kumkuta akiwa
kama alivyozaliwa na wakati huo taa ilishawashwa.
Akiwa anajizungusha kama kujinyoosha ndipo na
mimi akanifanya niwe chizi zaidi. Hapo nafahamu
sikuwa na akili yangu mwenyewr ila kama nilikuwa
naendeshwa tu. Nilivua nguo zote nikabaki kama
nilivyozaliwa haki ya nani sehemu zangu nyeti
zilisimama kama mchongoma.
Nilimshika mguu ndipo Salha akashtuka alipoamka
anakutana na mimi niko kwenye hali ile.....
Jamani Inauma sana sifurahishi ila yasikukute...
 
SEHMU YA KUMI NA SABA 17
ENDELEA……..
Baada ya Salha kuamka alinikuta mimi nikiwa
kwenye utupu wangu nikimkodolea macho kama
panya aliyebanwa na mlango. Sikuwa mtu wa
kawaida kabisa kama inavyotakiwa kwa wengine
kwani nilijihisi kama mnyama kabisa. ‘Mnali
unatakla nini naa! Mbona uko hivyo sasa’ alikuwa
anaongea lakini sikuwa namsikiliza kabisa
nilichofanya ni kuendelea kuushikilia ule mguu wake
na mimi nikiwa kwenye hali mbaya ya kutaka
kumuingilia kimwili dada wa watu.
Mpaka dakika kadhaa zilizopita hakika nilifanikiwa
kumvamia na kumsaula kila kitu, lakini kwa upande
wake hakuonyesha pingamizi yeyote kwangu Zaidi
ya kugugumia kama mtu ambae anaonea hali kuwa
anajua nini kinataka kuendelea na yeye ndie mhanga
mkuu. Mpaka muda wa dakika kama kumi tayari
nilishaweza kuingia langoni mwa dada Salha na
kumfanya yeye akihemea juu juu. Kutokana na mwili
wangu kuchemka damu kwa kasi sana misuli yangu
ya kila eneo hasa ile ya kiumeni iliweza kusimama
barabara mpaka Salha alilalama Zaidi.
Nakumbuka nilitumia muda wa masaa kama mawili
kamili bado sijatoka kwenye mwili wa Salha hadi
pale alipofanikiwa kuniondoa nay eye kukimbia
kabisa kupitia mlangoni. Binafsi nilikuwa bado
kabisa na ndio kama mchezo ulikuwa unaanza vile.
Kama dakika kadhaa hali yangu ilinitowerka na
mimi nikawa nimeishiwa nguvu kabisa ya kufanya
jambo lolote hata ile ya kusimama sikuwa nayo
kabisa. Hadi kufikia hapo nilipatwa na usingizi na
nikalala kabisa fofofo!.
Nikiwa usingizini Napata kuota ndoto mbaya sana
ambayo iliweza kunikumbusha baadhi ya mambo
Fulani ambayo yalipita kipindi cha nyuma. Niliweza
hata kumkumbuka mke wangu Mama Asante hata
yale yote ambayo yaliweza kupita, niliweza
kukumbuka pia bwana Paul na wale vijana wake
ambao walifanya njama zote za kuniondoa duniani
lakini iliweza kushindikana. Nilikumbuka pia hadi
kule kisiwani ambako wale vibwengo vilinidhuru na
kunifanya niwe kwenye hali kama hii ambayo hata
sasa Napata nayo tabu sana.
Niliamshwa na dada mfanya kazi wa mule ndani na
baada ya kuamka niliweza kushtuka sana na kuanza
kuvuta taswira ya mambo mengi sana lakini kati ya
hayo yote nilikumbuka tu jambo moja kuhusiana na
ile ndoto ya usiku wa manane. ‘kaka, samahani
kuna tatizo dada anakuita chumbani kwake’.
Nilipatwa mshangao sana kuitwa na Salha ‘kunas
tatizo gani ambalo limejitokeza huko?’ nilimuuliza
kama mtu ambae sikuhitaji usumbufu wowote ule
kwa muda ule.
‘hapana sijafahamu nini ambacho anakuitia ila
kaniambia fanya haraka nenda’ Basin na mimi
niliweza kuinuka na kuanza kuvuta mguu mmoja
hadi mwingine, japo nguvu sikuwa nazo lakini
nilijitahidi sana kutembea hivyohivyo lakini hofu
kubwa ambayo niliyokuwa nayo ni ile ya mimi
kuitwa chumbani kwake. Nilipofika mlangoni
nilisimama kisha nikawa nasikiliza kwa makini sana
kuna jambo gani ambalo linaendelea, Salha ni
mwanamke ambae anafanya kazi hospitalini lakini
yeye ni kama daktari tangu anichukue kutoka
hospitalini kwenye mikono ya polisi sikuweza
kumhoji Zaidi kuhusiana yeye na ile nyumba pamoja
na maisha yake kiujumla.
Nilipokuwa pale mlangoni niliweza kusikia sauti za
mwanamke zikiugulia kama mtu ambae anaumwa
malaria yaliyopanda Zaidi, niliogopa kiukweli nilizidi
kusikiliza kama labda kunaweza kuwa na
mwanaume ndani humo wakiwa wanafanya yao
lakini hapana, nilivuta pumzi na kuingia ndani humo
na kumkuta akiwa anatetemeka sana. ‘Salha vipi
lakini kuna tatizo gani’. Nilimuuliza swali ‘khaaa! Ina
maana hujui ulichonifanyia au’. Hapo nilishtuka sana
kuwa sikumbuki niliyomfanyia jana usiku? ‘Hapana
kabisa Salha kiukweli sikumbuki nini ambacho
kimetokea lakini?’ Salha nilimuona akitokwa na
chozi pasi na kujua nini ambacho nimemfanyia
kutoka ana madai yake.
‘Salha kiukweli8 unanichanganya kabisa kwa sababu
sifahamu chochote kile hadi sasa’. Ghafla anakuja
yule binti mfanya kazi baada ya kusikia mlango
ukigongwa nay eye kuruhusiwa kuingia ndani ‘Dada
samahani jikoni hakuna nyama’ nilishtuka kidogo
‘Wee hakuna nyama kivipi wakati nimeleta jana tu
hapa kwenyeb lile friji hakuna lile jeupe?’ ‘hakuna
ilaaaa…!’ ‘Niniiii’ Nimeona tu kama kuna nyama
zilizodondoka pale chini sijui ni panya au nini’.
Mpaka pale nikaishiwa pozi, niliamua kukaa kimya
tu bila hata kusema chochote kile.
Nilimuona Salha akinitumbulia macho kisha
akamgeukia tena yule binti na kumuuliza ‘Ina maana
humu ndani wameingia panya au lakini toka kwanza
nakuja nina mazungumzo hapa’ Aliondoka kama
alivyoelekezwa na akatuacha wawili mule chumbani.
‘Eheee! Hivi Mnali kaka angu wewe ni mtu wa aina
gani’ swali lake nilishindwa kumuelewa kwa nini
aulize mimi ni mtu wa aina gani na wakati ananiona
kuwa ni wakawaida sana ‘sijaelewa kwa nini
unauliza ilo swali’. ‘Kwa sababu jana usiku jambo
ulilonifanyia kiukweli sikuwa kulipata tangu nizaliwe
na nimjue mwanaume hakika mpaka hapa sasa
siwezi hata kusimama vizuri hata kama nikisimama
nadondoka nimeshiwa na nguvu kabisa ndio maana
nikamuomba huyu binti anichemshie hata supu
kidogo.
‘Akuandalie supu..jana nilichokufanyia hakuna hata
mwanaume ambae alishawahi kufanya jambo hilo
mh! Inawezekana vipi kwa mimi kufanya hivyo
sijakuelewa hata’. ‘ok! Ebu yaache kwanza hayo nina
jambo lingine nataka kukuuliza, ulisema kuwa
kwenye kazi zake za uvuvi ulishawahi kukutana na
matatizo mengi sana likiwemo kuingia kwenye
Kisiwa ambacho kilikufanya upate matatizo mengi
sana likiwemo….’
Nilimziba mdomo asiendelee kuongea ‘Ebu kuhusu
hayo mambo ebu niache kwanza maana kiukweli
mambo ni magumu na sitamani tena kusikia kule
ilaa nahitaji kuona familia yangu iliko je? Unaweza
kunirejesha kule ambako nilikuwa naishi’. Nilimuona
akiinuka kwa tabu sana huku akiwa kashikilia kanga
kwenye ukingo wa kifua chake. Nilijihisi niko tofauti
sana kutokana vile ambavyo alikuwa kavaa. ‘dada
samahani kama unataka kuamka tafadhali naomba
nitoke kwanzatutakuja kuongea baadae ukiamka’.
Nilimuona akizidi kuinuka kwa shida na alivyokaa
tayari ndipo akaniambia ‘khaa! Wee mnali mbona
unanichekesha na jana usiku ulivyoniingilia
hukuniona mwili wangu? Eeeh! Au ndio
kujishebedua tu hapa’.
kila jambo ambalo alikuwa analiongea pale nilikuwa
naona kama ananitania tu, sikuwa namuelewa, ‘haya!
Nakuomba kuanzia sasa uachane na kazi zote za
Uvuvi nataka nikupe biashara na ikiwezekana mimi
na wewe tuoane na tuzae watoto’. Nilijihisi
nahamaki baada ya kusikia swala la mtoto ndipo
nikaja kukumbuka kuwa nina kamtoto kangu
kanaitwa Asante jamanii akili yangu ilibadilika
palepale na kuanza kutaka kuondoka pale ndani na
kwenda kumtafuta mwanangu Asante. ‘Salha hapana
nimemkumbuka mtoto wangu Asante hapana
naomba nikamtafute mwanangu ile ni damu yangu’,
khaaa! Mnali ina maana una mtoto wewe? Aliuliza
ndio nina mtoto na tangu nipate matatizo sikuwahi
kumuona tena mpaka leo hii nakuja hapa hivyo
nahitaji kumuona mwanangu. Ajabu Zaidi kama
unavyowajua wanawake baadhi yao kama huyu
Salha akaanza kununa. Salha nakuomba haraka sana
unipeleke nyumbani kwangu nikamtafute mwanangu,
nilivyomuona kuwa hanijibu ndipo nikasimama kwa
hasira na kutoka mule chumbani Mnaliiii unaenda
wapi bwana ebu njoo hapa, sikutaka hata
kumsikiliza niliingia kule chumbani kutafuta nguo
zangu lakini sikuzipata, niliamua kurudi tena kule
chumbani huku nikiwa nimefura kwa hasira kama
mbogo aliyekoswa na mshale.
Salha nguo zangu umeziweka wapi?, Nguo za nini?,
nataka kuondoka, nilimuambia bila hata kumuogopa
kwa kuwa nimeshaanza kukumbuka tayari familia
yangu. ‘Ebu kaa kwanza hapa mimi nitakupeleka
huko kote ambako unahitaji kwenda lakini kaa
tuelewane, hakuna mkate mgumu mbele ya chai.
Nilitulia kabisa na kukaa chini kabisa huku nikiwa
nimekunja sura. ‘Mbona unakaa chini sasa njoo
hapa kitandani tuongee vizuri, aliendelea kunihimiza
mpaka pale niliposimama na kwenda pale kitandani
huku nikiangalia pembeni.
‘Nakuomba kwanza unieleze vizuri kuhusiana na
huyo mtoto wako’. Sikutaka hata kusubiri nilianza
kumhadithia mwanzo mwisho mpaka pale ambako
niliweza kuishia, kutokana na matatizo ambayo
nilipitia nilijikuta naanza kulia pale nikikumbuka mke
wangu ananidai talaka na kunimwagia maji ya
ukoko wa ugali hapo nilianza kutoa chozi mpaka
Salha akanifuta huku akinibembeleza na
kunikumbatia, nilikumbuka kuwa huyu ni mwanamke
ambae kanisaidia lakini simfahamu vyema hivyo
nilimuomba akae mbali kidogo na mimi ili nipate
kumhoji kwa undani Zaidi. Salha najua kuwa
umenisaidia sana tangu pale nilipokamatwa na
polisi hadi kufika kule hospitali na kukutana na
wewe hadi leo hii tupo pmoja kama hivi ila
nakuomba unieleze kwanza wewe ni nani hasa na
unaishi na nani hapa kwako, Salha nilimuoana akiwa
kaka kimya kwa muda kidogo kisha akaanza
kucheka pale.
Najua kuwa una shaka na mimi, ni kweli kama
bahati kwani hata mimi sikuwahi kuwaza kukusaidia
ila kutokana na matatizo yako ambayo ulinihadithia
nikajiona kuwa natamani na nahitaji kukusaidia
ndipo nikaweza kuongea na wale polisi na kukutoa
kinyemela kama vile, ila kuhusuu mimi maisha
yangu hapa bado mapema sana kujua ila ipo siku
utakuja kujua tu’.
Salha hapana hapa siwezi kukubali basi niache
niende kwangu mimi nashukuru kwa msaaada wako
nikiw na shida tena nitakuja kukufuata ili unisaidie,
nilijiona mtu mwenye hasira pale niliposimama na
kuanza kubwata mule chumbani, nilikuwa nimevaa
bukta tu iliyoishia kwenye ,magoti yangu nikaona
isiwe kesi nilitoka na kuingia chumbani kule
nikatafuta na kubahatisha kukuta shati na surali aian
ya jinz na wakati nilishazoea suruali za mtepweto
ambazo sikujua zilikuwa za nani nilichojua ni kuvaa
na kutoka kwa hasira, nafika mlango wa kutokea nje
umefungwa kila nikifungua haufunguki. Nikajua hapa
sasa nimekamatwa leo nilipiga hatua kwenda hadi
kwa Salha kumuomba tena ruhusa niondoke. ‘Salha
nakuomba labda unanidai shingapi nikupe?’
nilimuuliza kwa ujasiri nikiamini kuwa hatoweza
kutaja gharama kubwa, Nilimuona akichezesha
vidole huku akisimama na nguo yake ile palepale
aliiachia na kubaki kama alivyoletwa duniani asiee
nilijiziba uso nisione kwa kuwa nilikuwa
namheshimu japo sikukumbuka usiku nilimfanyia
nini. ‘Sikiliza ukitaka uondoke humu sharti ulifanye
hili ambalo nataka ulifanye, Lipi hilo nifanye sasa
hivi maana unajua nampenda sana mwanangu ebu
kama nimekukosea naomba unisamehe sana
nitaenda baharini nikivua na samaki ambao
nitawauza nitakuja kukupa wewe hiyo ela. Mnali
usijidangwanye ela nilizotumia kukuhudumia wewe
na kukutoa mbele za mapolisi mpaka sasa huwezi
kuzilipa kamwe labda kama unafanya kazi kwenye
mgodi wa madini. Khaaa! Ngoja kwanza Salha
nilipofika hapa nilikuwa na boksi langu kama
sanduku dogo liko wapi? Khaaa! Lile kuukuu
haliwezi kukaa ndani humu tumeshalitupa tayari nje
kwenye taka na sijajua kama gari la taka
halijachukua litakuwa huko, Mamaaa yanguuu
Salhaaa unaniua hivihivi kwa umasikini mwenzako
unajua wapi mimi nimelitoa lile Sanduku jamani
eeeeh!.
Sanduku lina nini lile na wewe eeeh!, basi ushaanza
kuwa chizi sasa Ebuu Naaaaa njooo mfungulie huyu
aondoke zake hapa anatuletea mambo ya ajabu eti
kisa anataka kuondoka haya nenda zako huko lione
kwanza na usirudi hapa, Nilimpuuzia lakini bora
mimi niondoke pale nikaanze maisha yangu binafsi,
Mlango ulifunguliwa ndipo nikaanza kuingia chooni
kwanza kisha nikawa narudi, nilipitia pale jikoni
kidogo kwa kuwa njia nihiyo moja ya kwenda
chooni. Nilipofika pale jikoni niliona friji likiwa tupu
ndipo kumbukumbu ikanijia kama nilishawahi kufika
pale muda Fulani, kichwa kilianza kunigonga kwa
nguvu sana huku nikitetemeka na mdomo kuanza
kuwa mchachu nikitamani nyama tena, aisee ndipo
nikaupata mkanda mzima kuwa niliyafanya mimi
yale na yule binti wa watu nilimuingilia mimi bila
hata kujijua kwa kile ambacho nakifanya.
Nilijikongoja kwa kulazimisha hivyohivyo na
sikutaka hata Salha au yule mwingine afahamu
kama mimi nimepatwa na nini. Mnalii wewe
unaenda wakati uko kwenye hali hiyoo rudi kwanza
haraka jamanii usiondoke dada! Anatapikaaa huku’
yule binti aliongea wakati huo mimi nakaribia geti
ukweli nilianza kutapika zile nyama mbichi za jana
nikafungua geti hata kabla mlinzi hajafungua, mlinzi
alinijia akiwa anafahamu kuwa mimi nimefanya
uhalifu hivyo akataka kunizuia kwanza lakini huwezi
amini hata nilichomfanya sifahamu huko nyuma
yangu maana alipokea ngumi takatifu hata yeye
mwenyewe alikoma kwa nini alinisogelea.
Safarai yangu nilitembea lengo niwe mbali na ile
harufu ya nyama kwani ile hali ikinianzia tu. Harufu
ya nyama naipata umbali mrefu sana. Mpaka pale
nilipofika na ile harufu ikakata ndipo hali yangu
ikakata kabisa. Nilianza kukosa nguvu sana maana
hali yangu ilizidi kuwa mbaya nikatafuta sehemu ili
niweze kutulia kwa muda kisha nitafute wapi niende.
Katika pitapita yangu kwa bahati nzuri nikakutana na
Musa akiwa kwenye gari yake ndipo akasimama na
kufungua mlango na kunijia pale. Mnalii vipi uko
hapa bwana unafanya nini?, nilimueleza shida yangu
japo najua kuwa yeye na rafiki yake wote ni
wanafiki na ndio ambao walifanya jitihada kutaka
kuniua kabisa kule baharini. Alinisogelea hadi pale
nilipo kwa mara nyingine kisha akaanza kucheka
kwa dharau sana hakika iliniuma kiukweli maana
sikupenda kitu ambacho kanifanyia, kwa hiyo
unanicheka baada ya kukuhadithia yaliyonipata
ulikuwa una maana gani sasa kuniuliza swali kama
hilo?, lakini Musa alizidi kunicheka sana. Tatizo
mnali unajifanya kujua sana ona sasa wenzako
bwana Paul aliturudisha tena na katununulia gari kila
mmoja twende basi maana sasa hivi mwenzetu ni
muathirika wa gonjwa la UKIMWI unahitaji msaada
wa mawzo pia si kukaa mpweke kama hivyo usije
kufa hapa.
Nilimuangalia tu basi kisha nikampungia mkono
aondoke zake nilichoamua ni kusimama pale
taratiibu kisha nikaongoza njia kubwa na kuanza
kuchapa rapa mdogomdogon pale. Mnaliii! Hakika
wewe ni Mzimu ila bwana Paulo akikusikia kama
upo mpaka sasa na umemkatalia kumfanyia kazi
zake hakika atakumaliza kabisa ni bora ukamuombe
msamaha mapema tu kabla’. Nilimpotezea kwa ule
upuuzi ambao alikuwa anauongea , sikuupenda hata
kidogo kuusikiliza. Mawazo yangu yalizidi kupaa na
kujiona tayari mimi si binaadamu kabisa, lakini
mawazo mengine yaliyonijia ni kuhuusiana na kile
sanduku langu dogo ambalo Salha anadai kuwa
kalitupa kwenye taka sikuwa naamini kama kweli
kalitupa maana nilimtilia shaka sana yule dada.
Kidogokidogo nilitembea hadi eneo moja ambalo
kidogo kuna polipoli na watu ni mara chache sana
kuweza kupita hivyo niuliamua kujiegesha
pembezoni mwa barabara na kutaka kutoa haja
ndogo, lakini ilinishangaza sana maana ilishindwa
kutoka kama kawaida yake Zaidi ilikuwa inatoka
huku nikiwa na maumivu makali sana nilijiuliza kwa
nini iwe hivi hata pale nilipoipata haja ndogo
mwishoni nilitokwa na damu jambo ambalo lilizidi
kunishangaza sana. Nilitembea Zaidi hadi pale
nilipoona kuwa naipata ile hospitali ambayo
mwanzo nilipelekwa kule. Kuanzia pale ndipo
nikapakumbuka nyumbani, safari hii ilikuwa majira
ya jioni baada ya mwendo mrefu sana nilitembea
mpaka miguu yangu ikawa inauma kwa kweli lakini
shida siku zote humfundisha mtu namna ya kufanya.
Mpaka majira ya saa moja jioni nafika kwenye
kibanda changu lakini ndani hakuna ambacho
nakikuta, mlango wangu umeondolewa na kila kitu
cha thamani mule ndani kimeondolewa na watu
ambao sikuweza kuwafahamu kwa kuwa sikuwa
hapo kabla. Nakumbuka siku ambayo natolewa pale
watu walikuwa kwenye harakati za sherehe nyumba
ya karibu pale hivyo nadhani ndio walitumia njia
hiyo sasa mimi kunimalizia kila kitu. Nilijipa moyo
kuwa mwenyezimungu yupo na atanisaidia kila
ninalotaka kuomba na nitafanikiwa sitokata tamaa
kabisa. Maamuzi ambayo niliona kuwa ni ya busara
kwa haraka hiyo ni kwenda kwa mjumbe wa pale
nyumbani kumpa ile taarifa. Nilipofika kwa kiongozi
kwanza alishtuka kisha akaonyesha wasiwasi na
mimi. ‘Mzee nimekuja kwako kuomba msaada
nyumba yangu tangu niondoke tayari imeharibiwa na
vitu vyangu vyote vimeibiwa sijui naishi vipi,
Nilimuambia kiongozi huyo. Sasa kijana kwanza
taarifa zako hapa zilizotufikia kuwa wewe umekufa
tangu miezi kadhaa nyuma iliyopita lakini juzijuzi
nikapata taarifa kuwa umerudi lakini sikupata bahati
ya kukuona kwani tayari ulishapelekwa kituoni kwa
uchunguzi Zaidi sasa nashindwa kukuelwa nah ii
taarifa. Nilishtuka kuambiwa kuwa mimi
nimetangaziwa kuwa nimekufa, lakini ni nani ambae
katangaza kuwa mimi nimekufa na kwa nini iwe
hivyo?’ kuna tajiri mmoja ambae alidai kuwa
ulikuwa unamfanyia kazi ya kumvulia samaki lakini
mwisho wa siku ulivyokwenda baharini hukurudi
kabisa hivyo akatangaza tauyari kuwa wewe
umekufa dunia.
Nilipatwa na uchungu sana kumbe hii ndio sababu
ambayo imewafanya hata kuiba kila kitu hapa
nyumbani kwangu. ‘ndio kwa kuwa hapakuwa na
msimamizi wa hizo mali zako kijana’. Nilisimama
na nikawa na maamuzi yungu mimi mwenyewe
kichwani mwangu.
Mjumbe nakuambia hivi kuanzia sasa lolote
nitakalofanya msije kunilaumu, khaaah! Toka hapa
kijana mfamaji haishi kutapatapa, jeuri hiyo ndio
ambayo ilimponza ndugu yako Kibona’…….
 
SEHEMU YA KUMI NA NANE 18
ENDELEA.........
.......Kwa kuwa bwana Mjumbe nilimuona akiwa
mbishi kama pilipili yenye kuwasha mdomoni pindi
inapoliwa. Niliondoka na kumuacha akiwa
ananiangalia huku akinisindikiaza kwa kauli ileile ya
awali ambayo nilipata kuisikia kwa umakini zaidi ya
awali."Wewe kijana huu mtaa utakushinda kabisaa
kwa hali hiyoo na kiburi hiko ndicho kilimfanya
Kibona aweze kufa". Nilitamani kusimama lakini
nikabakia kusikitika kwa nafsi yangu pamoja na
mwili wangu kuusongesha mbele kwa kutohitaji
swala lolote baya.
Nimeshafika hadi nyumbani nafanya nini hali ya
kuwa hakuna chochote kilichomo ndani, nabaki
kuduwaa na wakati nazidi kuduwaa ndipo nashtuka
kushikwa na mtu akiwa nyuma yangu hakuwa
mwingine bali ni yule mzee ambae aliniunganishia
dili kwa bwana Paul, "khaaa! Mnali, achaa weeee
haya mbona maajabu". Nilimuangalia sana huku
nikimshangaa "maajabu kivipi?" Nilimuuliza swali.
"Wewe huoni kama unazidi kuishangaza dunia haya
umeponapona vipi huko baharini!" Swali la huyu
mzee lilinipa picha kidogo kuwa dili la mimi kufa
kule lilipangwa na huyu akiwemo sasa atanitambua.
Nilipepesa macho kisha nikabadilisha sura ya
mshangao na kuweka sura ya huzuni niliyoichangany
a na busara za uongo kumbe nikiwa na lengo langu.
"Babu yangu huwezi kuamini kuwa walimwengu ni
wabaya sana na mwenyezimungu ni mkubwa sana
na hamtupi mja wake". Wakati huo nilikuwa
namshika bega nahisi huu muda ningekuwa na ile
ashki ya kuhitaji nyama mbichi na ukichanganya
hasira nilizonazo hakika ningemtafuna hata bega
nyambafu kama huyu. "Mh! Unasema kweli kijana
haya ilikuwaje maana sisi kusikia tu kuwa umekufa
huko baharini eti ulikuwa unafuata mwili wa rafiki
yako kibona ni kweli?".
Nilicheka kidogo, "babu hapa kuongelea mada hizo
hapana ebu tuingie ndani kisha nikuhadithie vyema".
Basi tuliingia ndani hali ya kuwa hajui kuwa nina nia
gani mimi kwake. Nilipohakikisha tumekaa mahali
ambapo hawezi kupita mtu yeyote na kutuona ndipo
niliposimama "hapa panatosha mzee" nilimuambia,
"haya nihadithie". Nilijipanga kumvaa vyema mzee
huyu kwa kumkaba shingo mpaka pale
atakaposema kile ambacho nakihitaji.
"Babuu! Unawafahamu watu ambao walitumwa kuja
kuniua kule baharini?". Nilibadilika kidogo kutokana
swali ambalo nilimuuliza na sauti ambayo niliitoa.
"Aaah ah ah! Kijana hapana ndio nataka kujua akina
nani hao". Nilimshika shingo barabara kisha
nikamuangusha chini hakika alikosa hata nafasi ya
kuongea vyema pamoja na kujitetea, niliyafanya
hayo huku nikikumbuka yale mabaya yote ambayo
niliyapata kule kisiwani.
"Babu nakuomba unieleze naamini dili la mimi kuja
kuvamiwa unalifahamu, kwa sababu wewe ndio
muhusika wa kila kitu ambacho kinafanywa kule
baharini naomba uniambie haraka kabla hata
sijabadilika nikakutafuna". Alipupapupa pale nikaona
jicho linamvimba na kuja rangi nyekundu nilimuacha
kidogo "Mnali unafanya nini unataka kuniua mimi
hapana ihusiki na jambo lolote lile kabisa".
Nilimbadilikia kwelikweli "mzee nakuomba sema
ukweli wako nitakunyonya nyama sasa hivi" wakati
huo tayari alishapokea kichapo mpaka suti zake
zote zikachafuka vumbi, kilichonipa uhakika ni zile
nguo kwani mtu wa pwani kama yule mzee ni nadra
kuvaa suti za ela.
Suti zile sikuziona kwa huyu mzee peke yake bali
hata kwa Musa pindi aliponikuta kule njiani akiwa
na gari niliamini kabisa hata Manyota na yeye
atakuwa nazo hizi na wamezipata wapi, itakuwa
kulekule kwa Paul ina maana kuwa anafanya nao
kazi hawa na ndio maana wamefikia hatua hii.
"Sawa siku hizi unafanya kazi gani?" Nilimuuliza
baada ya kuona kuwa zile nguo zinanitatiza.
"Hapana sifanyi kazi yeyote hata uvuvi nimeacha
kabisa". Nikaona hapohapo "sawa unafanya kazi na
bwana Paulo?" Hapo alisita kidogo. Mimi sikujali
kama ni mzee wa umri gani nilimfyatua vya kutosha
maana ni muuni na mzee asie na huruma anafanya
kazi ya kuuza madili kwa vijana.
Kazi ilikuwa pevu mpaka pale alipoamua kusema
ukweli kabisa kuwa Paulo ndie ambae katuma
kikundi cha watu ili waje kuniua mimi. Hakika
hasira nyingi zilinikamata na nilitamani hata kumuua
mzee yule, lakini punde si punde mdomo wangu
ulianza kuwa mchachu akili yangu kabisa niliiona
kuwa inaniruka mbali na kufanya mambo ya ajabu,
sasa ya leo ikawa kali zaidi ya zote wakati nazidi
kuangaika mzee huyu alibaki kuduwaa akishangaa
ile hali.
Mwili ulianza kutetemeka nguvu za miguu ilikuwa
mara dufu hamu ya nyama mdomoni ikihitajika,
"Babu nakuomba kaa mbali na mimi tafadhali kaa
mbali na mimi tafadhaliiiiiiiii". Mzee huyo alishuku
sana ile kauli alinijia karibu huku akisema "Kijana
hata kama umeniadhibu kiasi nashindwa kufanya
jambo ila siwezi kukuacha ukiwa peke yako
umepatwa na nini?". Alihoji.
"Hapana nakuomba ondoka haraka
nimeshakusamehe nendaaaaaa". Nilipiga ukelele
ambao sauti nilihisi kabisa sio ya kibinadamu "Sawa
ngoja nikaite gari ikupeleke hospitali haraka".
Nilitamani kumuambia kuwa hapana ila nguvu ya
maumbile tofauti yalinizidi ndipo niliachama mdomo
na kutoa ulimi wangu aisee nikiwa bado kwa mbali
najielewa niliona natoa ulimi usio wa kawaida
wenye rangi nyeusiiii yule mzee alipoona vile
alistaajabu na kujibamiza kwenye ukuta huku
akitafuta nafasi ya kukimbia.
Hasira zangu zilipelekea kufika kwenye hali ambayo
siwezi kuiongoza mwenyewe.
Ilichukua kama dakika kumi hivi kabla yeyote
kugundua nini kilinitokea zaidi ya yule mzee.
Nilimuona kwa mbali yule Mzee akija pamoja na
mtu mwingine kwa haraka sikumfahamu. Mimi hali
yangu ilirudi kama umeme unavyoshtua kwa yule
ambae kakamatwa na umeme. Palepale nilizimia ila
neno la mwisho nililosikia ni kuhusu mimi kunitoa
na kunipandisha kwenye gari. Sikujua ananipeleka
wapi huyu mzee.
 
SEHEMU YA KUMI NA TISA 19
ENDELEA...........
.......Safari ile sikuwa nafahamu napelekwa wapi,
kwa kuwa nilikuwa sijifahamu kabisa, hii ilitokana
na mwili wangu kukosa nguvu baada ya lile tukio
kunitokea kwa wakati mfupi kama ule na kupotea
ghafla. Ilinichukua muda sana mpaka hali yangu
kurudi kutoka kwenye usingizi mzito wa nusu kifo,
Nilishtuka baada ya kuhisi ubaridi mkali mwilini
mwangu, ndipo nilipoangalia macho yangu baada ya
kugundua kuwa sipo sehemu salama. Kilichonijulish
a kuwa sipo sehemu salama ni baada ya kuzisikia
kelele za watu wakicheka kwa kebehi ya aina yake.
"Niko wapi hapa mimi"
Nilijiuliza mwenyewe bila hata ya kupata jibu.
Niligeuza shingo yangu sehemu mbalimbali za ile
nyumba ndipo nikakutana uso kwa uso na bwana
Paul. Nilishtuka sana, kwani sikutegemea kama
yule mzee atanileta sehemu kama hii.
"Mnali?"
Paul alniita
Nilimuangalia tu bila kuitikia
"Unajisikiaje kuwa maeneo haya?"
Paul aliniuliza.
Pia hata hilo sikuweza kumjibu.
Sehemu hiyo walikuwepo pamoja na Manyota akiwa
na Musa. Mzee yule aliyenileta alikuja huku akiwa
kafungwa P.O.P Lile dude ambalo wanafungwa
shingoni kama mtu yule ambae amevunjika shingo,
nilipata picha kuwa yule mzee kaumia na kutokana
na kile kipigo nilichompa muda uliopita kwa kuwa
sikufahamu ni saa ngapi wakati huo.
"Ehee! Ameamka huyu mpuuzi?"
Aliongea huyo mzee,
"Ndio kaamka sasa ni muda wako"
Niliduwaa ndipo nilijinyoosha kidogo, viungo vyangu
havikuwa na ushirikiano kwani vilitoa sauti ya
kujivunjavunja pah! Pah! Pah!. Hii ilitokana na
uchovu mkubwa sana ambao niliupata.
"Kijana unanishangaza sana unajifanya mwerevu
kumbe umetumwa toka kuzimu huko, sasa leo
tutakumaliza na kukutia Asidi kali"
"Mzee ngoja kwanza, huyu hatupaswi kumuumiza
sana bado nina majukumu nae"
Aliongea paul.
"Sawa bosi tunakusikiliza"
"Sasa, Manyota na Musa nawaombeni mkachukue
lile begi pale kitandani kwangu"
Manyota na Musa walinyanyuka na kwenda
kuchukua lile begi ambalo Bwana Paul alilihitaji kwa
muda ule, huku nyuma tulibaki watatu mimi, Mzee
pamoja na bwana Paul.
"Bosi sikufichi huyu si binaadamu"
Aliongea yule mzee
"Kwa nini asiwe binaadamu?"
"Kwa sababu nimemshuhudia mimi mwenyewe
anabadilika na kuwa mtu tofauti, ulimi wake ulikuwa
mrefuuu alafu una rangi nyeusi kama nyoka hivi,
mimi sikufichi huyu tumuulie mbali"
"Sawa lakini si unajua Hoteli yangu ile mpya
inahitaji Mboga kutoka baharini!, pia hakuna mtu
mwenye ujuzi wa kuleta samaki wa kila aina tofauti
na huyu mpuuzi".
"Sawa lakini kule baharini, mimi nafahamika,
tukimuacha huyu atanitia dosari maana, maji
tumeyavulia nguo sharti tuyaoge, tumekosa kumuua
kule baharini na sijui alitoka vipi, yupo mzima
inatakiwa tumuue kabisa kama watu wa kukufanyia
kazi hiyo basi mimi namfahamu kijana mmoja
atafanya hiyo kazi"
Wakiwa wanaongea mimi nilibaki kuwasikiliza,
mawazo na akili yangu bado havikuweza
kuchambua kwa kina nini nifanye.
Hapo ndipo Manyota alikuja akiwa na lile begi
kama Sanduku, kwa mbali akili ilirudi kulikumbuka
Sanduku langu ambalo Salha aliniambia Mzoa taka
kabeba na kuondoka nayo, nilikumbuka pia kule
kisiwani yule jamaa kaniagiza safari ndefu ya
kuvuka Bahari kwenda upande mwingine ambako
kuna familia yake na akaniomba nikalipe kisasi
chake, hiyo ndio kazi aliyonipa na akanipatia zawadi
ya lile sanduku akiniambia litanisaidia mahali
popote hasa kiuchumi wangu.
Leo hii nipo mikononi mwa huyu Mshenzi,
anaelazimisha uwezekano ambao kwangu ni
mgumu. Basi Manyota alinipiga miguu yangu huku
akiwa anaelekea kwa Paul.
"Sasa, nataka mumpeleke kwenye kile chumba
haraka, baada ya hapo hakikisheni mnamlazimisha
kukubaliana na kazi yangu, ila mfungeni Nyororo
nzito sawa?"
Aliongea Paul
"Sawa bosi"
Leo rafiki ambao nilijua kuwa watanisaidia ndio
haohao wanashirikiana na mbaya kuniumiza, sikuwa
na uwezo wa kukataa, waliniburuza mule sakafuni,
hakika mwili wangu ulipatwa na maumivu kutokana
na vidonda vilivyotokana na mikwaruzo ya pale
chini.
"Mnali, unashindwa nini kukubali kufanya kazi na
huyu jamaa mambo yako yaende safi?"
Alisema Musa.
"Basi fikiria ukikubali utatuambia, hatukufungi
chochote kama anavyotaka Paul, ukipata majawabu
tuambie sawa"
Walitoka na ndipo wakaniacha peke yangu.
Nilijikaguakagua yale maeneo ambayo niliumia,
lakini kile chumba ni kizuri mbele yangu kulikuwa
na kabati ambalo lina Kioo, nilinyanyuka, kisha
nikajikagua huku nikisema
"Inawezekana vipi nimeathirika namna hii, maana sio
binadamu kamili?, je kwa nini nisikubali kabisa
kufanya kazi yake si Kuvua samaki tu! Nitakaopata
haohao basi, kwanza nina hamu ya kumtafuta
mwanangu Asante pamoja na lile Sanduku kwa
Salha anipe".
Nilikata shauri kuwa bora hata nikubali ili haya
mateso yasije kunifikishia umauti, baada ya kuona
kuwa hakuna njia ya kukimbia ndipo nikagonga
mlango ili wafungue na niwaeleze nini nimefikilia
kuhusu swala hilo.
Walifungua kisha nikawa nawaitikia tu.
"Oy umekubali?"
Manyota aliuliza
Mimi niliitikia kwa kichwa.
"Sasa ulikuwa unazingua nini, sasa Musa nenda
kamuite Bosi"
Musa akiwa katoka tulibaki wawili huku nyuma.
"Manyota nakuomba unieleze wapi naweza kumpata
mwanangu Asante"
Nilimuuliza
"Mpumbavu!, hapa sipo kushughulikia shida zako za
watoto fanya kazi kwanza"
"Lakini Manyota..."
"Manyota niniiiii!...nimekuambia kimya usiniuzi sasa
hivi bwanaa"
"Sawa..lakini wewe ni rafiki yangu naomb..."
"Paaaaaaah!..."
Kabla hata sijamaliza nilipokea kofi la shavuni,
nilipepesuka mpaka nikadondoka chini, nilihamaki
kutaka kumvamia.
"Eheeee! Unataka kupigana si ndio haya twende
sasa tuzipange...fala mkubwa wewe, unadhani nipo
kama zamani"
Nilitulia tu baada ya kuhisi naweza kuzidiwa hapa,
maana Manyota alikuwa amejazia mikono yake na
mwili sikujua alikuwa anakula nini maana kawa
bausa pamoja na musa.
Paul alikuja na kutukuta tukiwa tunaangaliana kwa
macho makavu.
"Ehee! Amekubali kweli?"
"Ndio bosi amekubali"
"Mnali..kweli umekubali?"
"Ndio nimekubali...kuvua samaki"
"Haaa!..haahahaaa!..haaahaaa...teh!..teh!".
Walinicheka sana kwa kweli sijui nilikosea kusema
au kwa sababu ya kule kukubali kuona
wamenikamata vyema.
"Manyota! kachukue mzigo haraka, sawaa!"
Manyota alifanya haraka na kurudi,
"Sasa kazi inaanza hapa! Unapeleka hili begi,
barabara ya saba kule mjini, kuna hotel moja
inaitwa # Zanzini_hotel . Manyota mpeleke alafu
hakikisha unampa maelekezo sawa".
Nilishangaa kazi gani hiyo ambayo naenda kuifanya
na sijajua kama nitafanikiwa hiyo kazi.
Je? Ni kazi gani hiyo
 
SEHEMU YA ISHIRINI 20
ENDELEA............
.......Paul alikuwa ananitazama huku akiwa
ananikazia uso, kiukweli mwili wangu ulikosa nguvu
kwa kuwa sikupata hata tone la maji wala chakula,
ilinipelekea kuwa mvivu sana hata katika uelekeaji
wangu wa mambo.
"Oy! Mnali vipi mbona unademadema.."
Manyota aliniuliza kwa kunikaripia, ila nilibaki tu
kumtazama huku nikimpa ishara ya kushika tumbo
langu kuwa nina hisi njaa kali.
"Haaa! Haahaaa! Eeeehee!"
Manyota, Musa pamoja na bwana Paul walinicheka
sana kwa dharau.
"Bosi, haka kajamaa kana njaa!"
"Oooh! Ni kweli asije akashikwa huko alafu
akatuchoma na sisi, kwa hiyo sasa"
"Bosi mpatie zile nyama za jana amalizie".
Mapngezi yao baina ya Paul na Manyota yalifika
hatua ya kujua kuwa mimi nahitaji kula, lakini kitu
ambacho wao wanataka kunipatia hakika sitaki hata
kukisikia masikioni mwangu.
"Vipi, unatikisa kichwa si una njaa"
Manyota alisema
"Ndio nina njaa ila sitaki hizo nyama, ikiwezekana
nipatieni ugali tupu bila mboga".
Wengi walinishanga
"Kha!"
"Huyu vipi anashangaza"
"Au anataka akufie huko mbele si ndio"
"Ndio inaonekana, ila mwache ale hiko atakacho".
Manyota aliondoka pamoja na bwana Paul kisha
wakatuacha sisi wawili.
Mimi nikiwa na begi lile ambalo ndani yake
sifahamu kuna mzigo gani, ikimaanisha kuwa ndio
mwanzo wangu wa kazi ni pale.
Nilipata kumuuliza Musa baadhi ya maswali kadhaa
ambayo nilihisi ni muhimu sana kwa upande wangu.
Kwa kuwa Musa kidogo alionekana kuwa na huruma
kushinda Manyota.
"Musa!..Musaa!"
Nilimuita kama mara mbili hivi
"Eheee!" Aliitikia
"Samahani...hivi ni kazi gani ambayo naelekea
kuifanya huko hotel ya # Zanzini ?."
Musa alichungulia kidogo kwenye ule mlango kisha
akanigeukia na kuniambia kitu ambacho kilinishtua
sana.
"Mnali.."
"Naam..Musa Nakusikiliza"
"Unaenda kufanyishwa kazi haramu...ya kuuza
madawa".
Ghafla palepale ananigeukia Musa na kuanza
kunitisha kwa maneno ya ajabu.
"Weeh! Kuwa kama wa kiume wewe utakufa kijinga
hapa..ona mwili umezoea kukesha kwenye maji tu
mpuuzi mkubwa wewe".
Kumbe ile hali ilikuja baada ya kuwaona Manyota na
jamaa mmoja wanakuja mule chumbani. Na mimi
nilizidi kujiweka chini kwa kupiga magoti kabisa na
kumuomba msamaha.
Zilipita dakika kadhaa nilikwisha kula na tumbo
langu likawa limeridhika barabara. Hapo sasa
Manyota aliniomba tutoke kwa ajili ya kazi ambayo
tunatakiwa kuifanya huko.
Geti lilifunguliwa, lakini binafsi nilikuwa napelekwa
tu kama mfugo usio na mchungaji.
"Panda kwenye gari haraka sana".
Nilipanda kwenye hilo gari kisha na yeye akapanda
kule nyuma niliko, Tukiwa tunamsubiri Dereva
aliyeko ndani na bwana Paul, ndipo walipotoka na
kuungana wote kwa pamoja ndani ya BMW. Bwana
paul alinigeukia.
"Kijana huu ndio mwanzo wako wa kupata Utajiri
sawa, ukileta uchizi wako utapaka upepo rangi".
"Sijakuelewa"
"Nina maanisha kuwa, Maisha yako yapo kwenye
hilo begi ukilifikisha salama basi utapata faida
kubwa ambayo hukutarajia, ila ukizingua utakiona
cha mtema kuni".
Nilibaki kuduwaa pale huku nikiwasikiliza kabla hata
hatujatoka.
"Maelezo mengi utayapata kwa Manyota".
Yeye alishuka na sisi tukaanza safari ya kuelekea
huko ZANZINI HOTEL. Kichwani mwangu niliwaza
kuwa Juma kaniambia huku naenda kuuza Unga, je?
Ni unga gani ina maana humu ndani ya begi kuna
unga..maswali yangu yalifika hatua mpaka nikawa
sielewi huku gari likikata upepo.
Au itakuwa huyu jamaa ana kazi za kuuza unga
mahotelini.
Ghafla Manyota alimsimamisha Dereva na
kumuambia kuwa aegeshe lile gari pembeni.
Gari liliegeshwa pembeni kama Manyota alivyohitaji,
kisha baada ya hapo akanijia na kuniambia utaratibu
na mustakabari wa kazi nzima ambayo tumekwenda
nayo pale.
"Mnali"
Nilimgeukia Manyota baada ya kuniita.
"Sikia"
"Unaona ile hotel paleee"
Niliangalia kwa makini ndipo nilipoliona lile jengo
ambalo alikuwa ananionyesha.
"Nenda pale!, upeleke hili begi, kwanza kuwa
makini sana na watu ambao wapo hapo, usikubali
mtu akunyang'anye hili begi sawa?"
"Ndio nimekuelewa"
"Pia ukifika utamkuta mtu kavaa suti nyeusi na
kofia, utamuulizia anaitwa bwana MOKU, yeye
atakukabidhi Brifcase ambalo unahitajika kuja nalo
hapa tunakusubiri".
"Nitawezaje kumjua huyo mtu?"
Nilipata kuuliza
"Nenda utamuona tu alafu kuwa makini na
nimekuambia kuwa yeyote ambae atakusumbua
kutaka kuchukua mzigo huu bila kuupata ule ambao
tumekuagiza pambana nae, baada ya hapo
tunakuacha huru pia utanunuliwa na vifaa vyote vya
uvuvi na utakuwa mvuvi hodari hapa na dunia nzima
kwa ujumla".
Niliposikia kuwa wataniachia huru na kupewa hivyo
vifaa nilitoka kwenye lile gari zuri, nilitembea kwa
harakaharaka sana ili nipate kuwahi kule ambako
niliambiwa kuwa nitakutana na bwana Moku.
Baada ya kufika hadi kwenye mlango wa ile floo ya
kwanza.
Kulikuwa na ukumbi mkubwa ambao watu wengi
walikuwa wanakunywa chai na vinywaji vingine,
nikiwa pale mlangoni naangalia nani muhusika
mbele yake nilishuhudia kuona televisheni
ikionyesha matangazo ya Uvuaji Samaki pamoja na
Kuogelea, nilishangaa kwa dakika kadhaa, ghafla
nilishtuka kuvamiana na dada mmoja hivi mweupe
mzuri mwenye rangi ya kuvutia.
Punde akaja mhudumu akiwa na sahani ya kinywaji
pamoja na vijipande vya nyama. Yule dada
alisimama baada ya kunigonga.
"Samahani sana kaka eti"
"Usijali dada angu".
Kile kitendo cha kugongana nilimwagiwa bia
ambayo mtu wangu wa jirani alikuwa anakunywa
huku anacheza. Yule dada alishika begi langu
khaaa! Nilishtuka nikajua ndio wale ambao
wanahitaji kunichukulia begi.
Ghafla yule dada akachomoka haraka, nilitoka pale
ili nifike mbele kwenye vyumba vingine ndipo
nikamuona yule mtu ambae alikuwa amevaa zile
nguo ambazo niliambiwa kuwa atavaa.
"Samahani ni nani Mr Moku?"
Niliuliza kwa ujasiri.
"Kijana umefika tayari sema"
Niliangalia pande zote nikaona kazungukwa na
baadhi ya vijana wenye kunenepeana miili yao.
Nikaona hapa pabaya sana.
"Nimepewa mzigo kukupatia ila.."
"Kijana umeeleweka....haya toa tuone ladha yake".
Mh! Nilishtuka sikupata maelezo zaidi kuhusiana na
ya kuonja na kuonja nini.
"Hapanahuruhusiwi".
Ndipo waliponigundua kuwa ni muoga alafu sijui ile
biashara vizuri.
"Pumbavu au umetumwa hapa eeeeh!! Kamata huyo
peleka kwenye gari haraka".
Kabla hajamaliza tayari nilishakabwa roba shingoni
na kusindikizwa na pigo takatifu lililonipeleka hadi
chini. Begi langu walilichukua nikiwa naona, baada
ya hapo sikujua nini kiliendelea..
Majira ya usiku najikuta nipo kwenye chumba
kimoja kidogo alafu nimefungwa kamba.
Ndipo ghafla mlango unafunguliwa......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom