Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
Dar es Salaam ya Tanganyika ilikuwa na fursa nyingi sana za kazi kwa vijana. Vijana wakitoka mikoani na walipata ajira na kuendesha maisha yao. Ajira nyingi zilikuwa Bandarini kazi ya ukuli, hii ilikuwa ni nguvu yako tu, wengi walikua ni vibarua wa siku. Kulikua na kazi za Reli, kung’oa majani relini hii nayo ni nguvu yako tu, kibarua cha siku.
Wale waliojua lugha ya mkoloni kidogo walifundishwa kupika na kuhudumia wateja. Hawa walipata kazi mahotelini. Ajira ya u house boy kwenye makazi ya wazungu ilipatikana. Hii ilihitaji sana reference, kama mjomba ndiye mpishi wa Bwana Smith, una chance kubwa ya kuwa gardener au yaya wa bwana Smith. Gardener, yaya, mpishi, dereva wote walipata mkataba wa kazi na waliweza kukopeshwa nyumba za National Housing kwani walikua na uhakika wa mshahara.
Makuli wengi walitokea Kigoma, Tabora, hasa ile njia iliyokuwa ya Watumwa kutoka Ujiji. Wengi walipata viwanja Kariakoo mpaka Magomeni na walijenga nyumba za udongo na makuti. Hawa ndiyo walikuwa kupangisha vyumba kwa wageni walioingia mjini.
Maisha kama mke wa kuli, inabidi uwe na mafuta ya karafuu, mume akitoka kazini wife, ale baada ya hapo umchue mgongo na miguu alake vizuri na kesho aende kibaruani.
Mazuri ya Dar ya Tanganyika yalikuwa mengi sana.
Wale waliojua lugha ya mkoloni kidogo walifundishwa kupika na kuhudumia wateja. Hawa walipata kazi mahotelini. Ajira ya u house boy kwenye makazi ya wazungu ilipatikana. Hii ilihitaji sana reference, kama mjomba ndiye mpishi wa Bwana Smith, una chance kubwa ya kuwa gardener au yaya wa bwana Smith. Gardener, yaya, mpishi, dereva wote walipata mkataba wa kazi na waliweza kukopeshwa nyumba za National Housing kwani walikua na uhakika wa mshahara.
Makuli wengi walitokea Kigoma, Tabora, hasa ile njia iliyokuwa ya Watumwa kutoka Ujiji. Wengi walipata viwanja Kariakoo mpaka Magomeni na walijenga nyumba za udongo na makuti. Hawa ndiyo walikuwa kupangisha vyumba kwa wageni walioingia mjini.
Maisha kama mke wa kuli, inabidi uwe na mafuta ya karafuu, mume akitoka kazini wife, ale baada ya hapo umchue mgongo na miguu alake vizuri na kesho aende kibaruani.
Mazuri ya Dar ya Tanganyika yalikuwa mengi sana.