Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

BWANAHARUSI ALIYEJERUHIWA

SEHEMU YA MWISHO

ILIPOISHIA...

“Anahisi nikiwa mbali naye nitakuwa na mwanaume mwingine.”
“Whaat!!”nilimaka kwa hasira.
Nilimsihi sana nikimtaka aje nyumbani, lakini ndugu yangu aligoma, niliwasiliana na mumewe ambaye kwangu ni shemeji yangu, ili amruhusu mkewe aje kunisaidia kumuuguza mama, jamaa yule naye alinikatalia bila aibu. Dada yangu naye alimtii!

ENDELEA NAYO...


WATU huwa wanasema mtoto wa kike kwa mama, wa kiume kwa baba. Katika familia yetu ilikuwa kinyume chake. Ndugu zangu wa kike ambao ndio walitakiwa kuwa mstari wa mbele katika kumuuguza mama yetu wote walimpa kisogo.

Nadhani ni sahihi kusema dada zangu hawakuwa na uchungu na mama yao. Ukichilia mbali yule dada yangu wa Geita, kuna huyu aliyekuwa akiishi Tanga.

Yeye aliniambia hawezi kuja kumuuguza mama kwa kuwa mumewe alikuwa amekwenda nga’mbo kimasomo hivyo asingeweza kutoka kuja kijijini bila ruksa ya mumewe, akaongeza kuwa sheria ya dini ilikuwa hairuhusu yeye kutoka bila ruksa ya mumewe.

Kwa kweli nilikuwa napitia majaribu makubwa mno maishani. Kitendo cha dada zangu kushindwa kuja kumuguza mama yao kwa kuheshimu maslahi ya waume zao kiliniuma. Hata hivyo, kuna kitu nilijifunza kwenye jambo hilo, japokuwa niliumizwa na fikra zao.


Nilibakia na mama nikimuuguza. Mipango ya kilimo niliisimamisha. Niliendelea na kazi zangu za ufundishaji huku kila wiki nikiwa na kazi ya kumpeleka mama kwenye kliniki ya mazoezi.

Alikuwepo shangazi yangu mmoja ambaye mara nyingi alikuwa akija kunisaidia kumpa huduma muhimu kama kumwogesha, kumbadili nguo na kadhalika.

Kama ungepata bahati ya kumwona mama yangu, usingemtofautisha na mtu mwenye ugonjwa wa kiharusi. Mwanamke mnene mwenye mashavu makubwa, hakuwa yeye tena.

Alikuwa amekonda mashavu yamemnyauka na macho yenye makunyanzi yametumbukia kwa ndani.
Kila nilipokuwa nikimwangalia nilihisi uchungu.

Sikujua mipango ya Mungu ilikuwa ni nini, siri hiyo alibaki nayo yeye aliye juu. Mama ndiye faraja yangu iliyokuwa imesalia duniani.

Mama aliishi na maradhi yake kwa muda mrefu sana. Nadhani miezi karibu saba ama nane alikuwa akipambania uhai wake kitandani.

Kila baada ya ya wiki mbili nilikuwa nikimfanyia dua maalumu ili mwenyezi Mungu aweze kumfanyia wepesi katika maisha yake.

Katika kipindi fulani ilifika, yule shangazi aliyekuwa akinisaidia kumuuguza mama, naye aliugua, akawa haji tena nyumbani.

Ikabidi kazi alizokuwa akikifanya nimtafute mwanamke wa kuwa anamsaidia mama kwa malipo ya fedha.
Wakati ambao sikuwa na fedha, nilikuwa nikimuhudumia mwenyewe.

Nililazimika kungojea hadi giza liingie ndio nimwogeshe mama yangu.
Siku moja mwishoni mwa wiki, nilikuwa nimempeleka mama hospitali ni katika kliniki ya mazoezi. Wakati napita getini, nikasikia sauti ya mwanamke ikiniita nyuma yangu.

“Faraji!!”
Nikageuka kutizima. Lahaulaa!! Sikuamini kumwona Nasra Mfaume, mke wangu wa zamani.

Alikuwa amevaa sketi ndefu ya rangi ya zambarau ambayo iliburuza hadi chini. Juu alivaa blauzi nyeupe ya mikono mirefu, kichwani alijifunga ushungi wa rangi ya zambarau. Moyo wangu ulipiga kite baada ya kumwona mwanamke huyo.
“Ni wewe!!”

“Ni mimi...”alijibu uso wake ukiwa wenye tabasamu. Akaendelea kunichangamkia:
“Babari za siku?”

“Salama tu.” Nilimjibu nikiwa sina tashuishi yoyote usoni.
“Vipi kulikoni tena na mama?” alihoji huku akimwangalia mama aliye kuwa katika baskeli ya magurudumu.
“Anaumwa.”

“Ni nini na Tangu lini?”
“Mwaka sasa.”
“Nini tatizo?”
“Kiuno.”

“Poleni sana Faraji.” Alisema.
Nilimpa tabasamu jepesi lililosema: Ahsante.
“Mimi nimekuja jana.” Nasra aliendelea kusema.

Kimoyomoyo nikajisemea: Nani amekuuliza swali hilo?
“Kila la kheri Nasra.” Nilimwambia. Nikaondoka nikimwacha akinisinidkiza kwa macho.

****
Baada ya chakula cha usiku, nilikuwa nikifanya matayarisho kwa kwenda kumwogesha mama gizani. Maji ya moto nilikuwa nikiyapoza kidogo katika ndoo kubwa.

Wakati napeleka maji katika banda la uwani, nikaona kivuli cha mtu nyuma ya banda la kuku akiwa amejibanza. Kwa kuwa ilikuwa giza, nikahisi labda mwizi. Nikapaza sauti kuuliza:

“We nani?” niliuliza.
Nasra akatokeza kwa mwendo wa kunyata!!.
“Ni wewe tena umefuata nini!!” nilimaka.
“Nimekuja kukusaidia kumwogesha mama.”

“Hebu niondoke bwana.”
“Siendi popote.”
“Wewe si mke wa mtu!”
“Hata kama.” Alijibu, akanisogelea zaidi, uso wake mng’avu uling’aa gizani.

Alikuwa ananukia manukato ya mazuri.
“Kuwa mke wa mtu hainizuu kutoa msaada.” alisema.

“Sitaki matatizo hebu ishia zako.”
“Lau kama nisingekuwa chanzo cha mateso mengi maishani mwako, nisingekuwa hapa muda huu.”
“Kwa hiyo?”

“Nipo kulipa fadhila za mabaya niliyofanya kwako?”
“Kwa kumwosha mama yangu?”
Hakujibu. Nikaendelea kumzodoa.

“Kunisaliti, kumtelekeza mwanao na kuharibu maisha yangu. Inalipwa kwa kumwogesha mama yangu! Eti Nasra?” nilihoji huku nikimwangalia Nasra usoni.
Hakujibu alibakia ameghafirika, maneno yangu ni kama yalimgusa.

“Sikiliza Nasra,” nilisema tena.
“Hakuna jambo lolote la wema utakalofanya litakaloweza kunisahaulisha mabaya uliyonitendea, labda moyo wangu uamue tu kukusamehe. Weka akilini hilo.”

Nasra alishusha pumzi ndefu, akachutama na kuangua kilio cha chini chini.
“Huondoki?” nikamuuliza tena.

Alisimama, akataka kama kusema kitu, lakini akaghairi, akatembea kuelekea getini. Nikamfuata nyuma ili akitoka tu nifunge geti.

“Nimepewa talaka na mume wangu!” alisema huku akitembea.
“Kwa nini?”

“Ni kwa sababu sina kizazi!”
“Eeh!!! Kilikwenda wapi?”
Alisimama na kunigeukia kisha akaniuliza swali ambalo nililiona ni la kipumbavu. Akauliza:
“Unataka nikwambie?”


“Ulitegemea sintahoji kizazi chako kimekwenda wapi?”
Alitabasamu, sikujua kama tabasamu lake lilitokana na kufurahishwa na kauli yangu ama vipi.

Ninachokumbuka Nasra Mfaume alianza kunipa maelezo yaliyonikata maini. Alinisimulia:

“Wakati nakusaliti wewe dhidi ya yule sharobaro mwanamuziki, nilipata ujauzito....” alisema. Akasita kisha akaniangalia usoni, uso wangu ulisawijika kwa sentesi ile.

Nikawa kama nimewekwa kwenye theruji. Mwili wote ulipoa. Kumbe mke wangu aliwahi kupewa mimba na hawara wake. Loh!!.

Japokuwa nilikuwa nimekwisha achana na mwanamke yule lakini jambo lile liliniuma, maumivu yake utadhani tukio lilitokea jana tu.

“Eeh ikawaje?” nikamuuliza. Donge kavu lilinikaba kooni.
“Kwa kutotaka wewe kujua kama nina mwanaume mwingine, nilikwenda kuitoa mimba. Ilikuwa ni siri kati yangu na yule bwana.

Sikujua kama kwa kutoa ile mimba kulikuwa na athari, baada ya kuolewa na huyu bwana mwingine athari zake ndio nimeziona, sina kizazi.

Mume wangu huyo ameshindwa kabisa kuwa na simile na jambo hili, amenitaliki kwa kushindwa kumzalia mtoto. Nina siku nne tangu nitoke mikononi mwake.” Alimaliza.

Uso wa Nasra ulijawa machozi, nilishindwa kutathimini kilio chake kilitokana na nini hasa. Je ni kushindwa kupata mtoto?

Ama kupewa talaka? Aidha ni juu ya upumbavu wake wote kwa ujumla.
“Nimejifunza mengi maishani, nataka nisahihishe makosa yangu Faraji” alisema.

“Usiku mwema Nasra.”
Ndio kitu pekee nilichomwambia usiku ule.
Kauli hiyo ilifanya Nasra aangue kilio kama mtoto mdogo, sijui aliwaza kitu gani binti yule.

Labda alidhani naweza kuwa na huruma dhidi yake. Kwa kweli alikuwa mwanamke aliyevuruga maisha yake kwa ujuha wake mwenyewe.

Nilifunga geti na kurudi ndani kwa ajili ya kumwogesha mama yangu kipenzi.
Usiku ule nilipopanda kitandani, nilifikiria mambo yote aliyonieleza Nasra.

Pamoja na kwamba nafsi yangu ilikiri Nasra alikuwa mkosaji, lakini sauti moja ilinisihi kutomchukia daima mtu yule.
“Hakuna binadamu mkamilifu.

Wakati mwingine tunakosea ili tujifunze.” Sauti moja mawazoni iliniambia.
“Kwa makosa aliyoyafanya Nasra, kwa sasa atakuwa mwanamke bora pengine kuliko yeyote yule, maana amekwishakosea na kajifunza.

Mpe nafasi, ” sauti ile iliendelea kunishawishi.
Kwa kweli hadi kunapambazuka, lile donge kavu sijui hata lilipotelea wapi, nilikuwa na fikra tofauti kuhusu Nasra. Nilitaka niishi naye tena, ikiwezekana nimwoe upya!!!!!

*****
Ilikuwa ni siku mpya. Jumapili tulivu. Nilikuwa nimeamka tangu alfajiri nikifanya usafi wa hapa na pale.
Nilimwandalia mama stafutahi ya chapati za kumimina na mayai.

Akiwa anakunywa chai nikwamweleza kila kitu kilichotokea kwa Nasra. Pia nikamwambia nadhiri ya kurudiana na mwanamke huyo.

Masikini ya mungu mama yangu hakuwa na makuu, alikuwa radhi kwa kila kitu nitakacho.

Wakati tunaendelea na maongezi mara mlango wa geti uligongwa, nikamini kivyovyote vile mgongaji ni Nasra. Niliona itakuwa fursa nzuri kama nitazungumza na mrembo yule ili tuingie kwenye makubaliano ya kuanza maisha mapya pale kijijini.

Nilisimama na kwenda kufungua geti. Mara nilikutana na watu ambao sikuwategemea. Walikuwa ni askari polisi wawili waliovalia kijeshi.

“Wewe ndiye Faraji?”
“Kuna tatizo?” nilihoji. Ilikuwa ajabu, sikuwahi kufuatwa na polisi kwa miaka mingi sasa. Leo vipi tena. Kulikoni.

“Wewe ndiye Faraji!!” jamaa walirudia kuniuliza tena kwa amri.
“Ndio ni mimi, kuna nini?”
“Unahitajika kituoni.”
“Kuna tatizo gani?”

Jamaa hawakunipa jibu. Walinishika na kunipeleka kituoni. Hadi tunafika sikuwa nimejua kwa nini nikamatwe, ingawa kuna wakati nilihisi huenda kuonana kwangu na Nasra kuna uhusino fulani wa mimi kushikwa na polisi.

“Wewe ndiye Faraji Mpangalala?”mkuu wa kituo aliniuliza baada ya kuingizwa ofisini kwakwe.
“Ndio mimi. Kuna nini Afande?”
“Kwani hujaambiwa?”
“Sijaambiwa chochote!”

“Askari waliokuja kukukamata Ilibidi wakwambie wanakukamatia nini.”
“Hawakunieleza!” nilisema.
“Unahusishwa na kifo cha Nasra Mfaume” kamaanda alipasua jipu.

Lilikuwa ni bomu lililonifanya nilihisi ni ndoto inanipitia nikiwa nimelala usingizi.
“Nasra....Nasra ame....Nasra amekufa lini?”
“Jana usiku.”
“Jana usiku!!!!
“Ndiyo.”

“Nilikuwa naye!!!!”nilisema kwa wahaka huku nikimwangalia usoni yule kamanda.
“Tunajua ulikuwa naye, lakini baada ya kuachana naye ndipo alipokutwa na mauti?”

“Kivipi? Ilikuwaje? Kwa nini na wapi?”
“Hayo maswali nikuulize wewe!!”
“Whaat!!” nilimaka.
“Nisikilize bwana mdogo.” alisema kamanda akiwa ananiangalia kwa makini.

“Uchunguzi wa awali unanaonesha Nasra amejiua mwenyewe kwa kisu ndani ya chumba chake.”kamanda yule alisema huku akikuna ndevu zake zilizokuwa zimepunguzwa kwa mtindo wa mustachi.

“Hata hivyo Nasra kaacha ujumbe wenye maelezo yasiyojitosheleza sababu ya kujiua kwake, ujumbe huo unakutaja wewe kuwa moja ya sababu ya yeye kujiua, ndio maana uko hapa kusaidia polisi.”

“Uko wapi huo ujumbe?”
Alinipa kipande cha karatasi kilichoandikwa na Nasra. Nilisoma maneno yaliyoandikwa kwenye ujumbe ule yalinikata maini. Aliandika hivi:
“Faraji mpenzi...

Sioni, sababu ya kuendelea kuishi katika dunia kwa mateso makali ya nafsi. Dunia imenielemea na imenishinda. Hiki ndicho ninanistahili. Nisamehe kwa yote niliyokutendea maishani, angalau nakufa ili nikaungane na mwanetu Mwanda huko akhera.”

“Nooooo!” nilipiga kelele nikalia kama mtoto.
***
Siku mbili badaye niliachiwa huru baada ya uchunguzi wa kipolisi kuonesha sikuwa na kesi ya kujibu, niliwaomba polisi nikapaone mahali Nasra alipojiulia. Nikapelekwa kwao, mtaa wa Bweru.

Chumba cha Nasra kilikuwa kimefungwa kwa amri ya polisi, nilisukuma mlango nuru ya mwanga hafifu ikaangaza chumbani. Kitandani kulikuwa na mashuka yaliyotapakaa damu iliyokaukiana.

Damu ya Nasra Mfaume, damu ya Mwanamwali.
Nilimlilia Nasra hadi macho yakavimba, kifo chake kiliniuma mno, kwa kweli moyo wangu ulikuwa na majeraha makali sana.
Wiki moja badaye, Nasra alizikwa katika makaburi ya Lugongoni.

Mimi bado naishi kijiji cha Nguruka mkoani Kigoma, naendelea kumlea mama yangu ambaye bado hajaweza kusimama.
Mwisho kabisa nakushukuru kwa kusoma simulizi hii ya kweli ya maisha yangu. Naamini kuna funzo umepata maishani.

MWISHO.

Usikose kufutilia simulizi mpya
 
Daaaah wanawake bhana wanatupa tabu sana ,bora kuwa mpiga nyeto tu kuliko kuwa na mademu dizaini ya Nasra na Debora utapata tabu sana mwanaume
 
Daaaah wanawake bhana wanatupa tabu sana ,bora kuwa mpiga nyeto tu kuliko kuwa na mademu dizaini ya Nasra na Debora utapata tabu sana mwanaume
Acha tu mkuu,,masuala ya mademu yanapasua sana kichwa.ni bora ukawekeza kwenye issue zingine sio mapenzi..nme experience mengi
 
Acha tu mkuu,,masuala ya mademu yanapasua sana kichwa.ni bora ukawekeza kwenye issue zingine sio mapenzi..nme experience mengi
Yaap si unaona Faraji Maisha yake yalivyoyumba ghafla baada ya kuoa ,lakini wakati anawala na kuwapotezea aliishi vizuri kabisa,hawa viumbe hatari sana
 
SEHEMU YA 20

MWANZO nilidhani labda swali lake lilikuwa na maana nyingine zaidi ya vile linavyoweza kueleweka.

Lakini nilipoona uso wa daktari yule ukiwa katika hali ya kungoja jibu la swali lile nikatambua hakuwa na maana nyingine zaidi ya vilevile alivyohoji.

“Unamaana gani kusema hivyo?” “Sina maana yoyote zaidi ya kukuonya tabia ya kumwingilia mkeo kinyume na maumbile,” dokta akaniambia, tena alisema huku akiwa amenikazia macho.

Niliendelea kuchanganyikiwa. Mambo niliyokuwa naelezwa na daktari yule yalikuwa yakiniikoroga akili yangu. Kila kitu kilikuwa ni michoro isiyoeleweka.

Sikuwahi kuwa na michezo ya kishenzi kwa mke wangu, kitendo cha kutuhumiwa kumwingilia mke wangu kinyume na maumbile, ilikuwa ni fedheha mbaya sana.

“Sijawahi kufanya huo mchezo mchafu…” nilimwambia kwa ukali kidogo. “Una uhakika?” “Kabisa dokta, sijawahi kujihusisha na tabia za namna hiyo.” “Basi inawezekana kabla ya kukutana kwenu mkeo alipitia hii michezo,” dokta alinileza.

“Kujihususha na mapenzi kinyume na maumbile?” “Ndiyo,” alitikia kwa kwa upole.

Mate mepesi yakanijaa kinywani. Jambo lile lingewezekanaje wakati mimi ndiyo nilikuwa mwanaume wake wa kwanza?

Nilimkuta akiwa mwanamwali, tena bikira, mshamba kwenye ulimwengu wa mapenzi. “Lakini inawezekanaje hilo dokta? Mimi ndiyo nilikuwa mwanaume wa kwanza.

Nilimkuta akiwa mshamba kabisa kitandani.” nikauliza kwa fadhaa nikitaka ufafanuzi na uthibio juu ya alichonieleza.

“Kweli?” “Ndiyo.” niliitikia huku nikimwangalia usoni.

Alifikiria kitu kisha akasema: “Nimekuwa daktari wa wanawake huu mwaka wa 17, mwanamke anapojifungua, hutokea mara kwa mara kutokwa na haja kubwa, lakini kwa mkeo ilikuwa too much, uzoefu unaonesha mtu wa aina hii amekubuhu kwenye tabia za kuingiliwa kinyume na maumbile,” dokta alinipasha.

Nilijisikia vibaya sana, maneno ya Dk. Charles yalinisuta, yakanifanya nijione bwege. Tafsiri rahisi ni kwamba, maisha ya nyuma ya mke wangu yalikuwa na siri kubwa iliyojificha. “lakini usijali Faraji, siyo kesi sana, haya ni mambo ya kawaida tu maishani, ” daktari aliendelea kunitia moyo, kimuonekano ni kama yeye pia alibaini kwamba jambo lile lilikuwa ‘surprise’ kwangu, na alivyoona
Amber ruty.
 
BWANAHARUSI ALIYEJERUHIWA

SEHEMU YA MWISHO

ILIPOISHIA...

“Anahisi nikiwa mbali naye nitakuwa na mwanaume mwingine.”
“Whaat!!”nilimaka kwa hasira.
Nilimsihi sana nikimtaka aje nyumbani, lakini ndugu yangu aligoma, niliwasiliana na mumewe ambaye kwangu ni shemeji yangu, ili amruhusu mkewe aje kunisaidia kumuuguza mama, jamaa yule naye alinikatalia bila aibu. Dada yangu naye alimtii!

ENDELEA NAYO...


WATU huwa wanasema mtoto wa kike kwa mama, wa kiume kwa baba. Katika familia yetu ilikuwa kinyume chake. Ndugu zangu wa kike ambao ndio walitakiwa kuwa mstari wa mbele katika kumuuguza mama yetu wote walimpa kisogo.

Nadhani ni sahihi kusema dada zangu hawakuwa na uchungu na mama yao. Ukichilia mbali yule dada yangu wa Geita, kuna huyu aliyekuwa akiishi Tanga.

Yeye aliniambia hawezi kuja kumuuguza mama kwa kuwa mumewe alikuwa amekwenda nga’mbo kimasomo hivyo asingeweza kutoka kuja kijijini bila ruksa ya mumewe, akaongeza kuwa sheria ya dini ilikuwa hairuhusu yeye kutoka bila ruksa ya mumewe.

Kwa kweli nilikuwa napitia majaribu makubwa mno maishani. Kitendo cha dada zangu kushindwa kuja kumuguza mama yao kwa kuheshimu maslahi ya waume zao kiliniuma. Hata hivyo, kuna kitu nilijifunza kwenye jambo hilo, japokuwa niliumizwa na fikra zao.


Nilibakia na mama nikimuuguza. Mipango ya kilimo niliisimamisha. Niliendelea na kazi zangu za ufundishaji huku kila wiki nikiwa na kazi ya kumpeleka mama kwenye kliniki ya mazoezi.

Alikuwepo shangazi yangu mmoja ambaye mara nyingi alikuwa akija kunisaidia kumpa huduma muhimu kama kumwogesha, kumbadili nguo na kadhalika.

Kama ungepata bahati ya kumwona mama yangu, usingemtofautisha na mtu mwenye ugonjwa wa kiharusi. Mwanamke mnene mwenye mashavu makubwa, hakuwa yeye tena.

Alikuwa amekonda mashavu yamemnyauka na macho yenye makunyanzi yametumbukia kwa ndani.
Kila nilipokuwa nikimwangalia nilihisi uchungu.

Sikujua mipango ya Mungu ilikuwa ni nini, siri hiyo alibaki nayo yeye aliye juu. Mama ndiye faraja yangu iliyokuwa imesalia duniani.

Mama aliishi na maradhi yake kwa muda mrefu sana. Nadhani miezi karibu saba ama nane alikuwa akipambania uhai wake kitandani.

Kila baada ya ya wiki mbili nilikuwa nikimfanyia dua maalumu ili mwenyezi Mungu aweze kumfanyia wepesi katika maisha yake.

Katika kipindi fulani ilifika, yule shangazi aliyekuwa akinisaidia kumuuguza mama, naye aliugua, akawa haji tena nyumbani.

Ikabidi kazi alizokuwa akikifanya nimtafute mwanamke wa kuwa anamsaidia mama kwa malipo ya fedha.
Wakati ambao sikuwa na fedha, nilikuwa nikimuhudumia mwenyewe.

Nililazimika kungojea hadi giza liingie ndio nimwogeshe mama yangu.
Siku moja mwishoni mwa wiki, nilikuwa nimempeleka mama hospitali ni katika kliniki ya mazoezi. Wakati napita getini, nikasikia sauti ya mwanamke ikiniita nyuma yangu.

“Faraji!!”
Nikageuka kutizima. Lahaulaa!! Sikuamini kumwona Nasra Mfaume, mke wangu wa zamani.

Alikuwa amevaa sketi ndefu ya rangi ya zambarau ambayo iliburuza hadi chini. Juu alivaa blauzi nyeupe ya mikono mirefu, kichwani alijifunga ushungi wa rangi ya zambarau. Moyo wangu ulipiga kite baada ya kumwona mwanamke huyo.
“Ni wewe!!”

“Ni mimi...”alijibu uso wake ukiwa wenye tabasamu. Akaendelea kunichangamkia:
“Babari za siku?”

“Salama tu.” Nilimjibu nikiwa sina tashuishi yoyote usoni.
“Vipi kulikoni tena na mama?” alihoji huku akimwangalia mama aliye kuwa katika baskeli ya magurudumu.
“Anaumwa.”

“Ni nini na Tangu lini?”
“Mwaka sasa.”
“Nini tatizo?”
“Kiuno.”

“Poleni sana Faraji.” Alisema.
Nilimpa tabasamu jepesi lililosema: Ahsante.
“Mimi nimekuja jana.” Nasra aliendelea kusema.

Kimoyomoyo nikajisemea: Nani amekuuliza swali hilo?
“Kila la kheri Nasra.” Nilimwambia. Nikaondoka nikimwacha akinisinidkiza kwa macho.

****
Baada ya chakula cha usiku, nilikuwa nikifanya matayarisho kwa kwenda kumwogesha mama gizani. Maji ya moto nilikuwa nikiyapoza kidogo katika ndoo kubwa.

Wakati napeleka maji katika banda la uwani, nikaona kivuli cha mtu nyuma ya banda la kuku akiwa amejibanza. Kwa kuwa ilikuwa giza, nikahisi labda mwizi. Nikapaza sauti kuuliza:

“We nani?” niliuliza.
Nasra akatokeza kwa mwendo wa kunyata!!.
“Ni wewe tena umefuata nini!!” nilimaka.
“Nimekuja kukusaidia kumwogesha mama.”

“Hebu niondoke bwana.”
“Siendi popote.”
“Wewe si mke wa mtu!”
“Hata kama.” Alijibu, akanisogelea zaidi, uso wake mng’avu uling’aa gizani.

Alikuwa ananukia manukato ya mazuri.
“Kuwa mke wa mtu hainizuu kutoa msaada.” alisema.

“Sitaki matatizo hebu ishia zako.”
“Lau kama nisingekuwa chanzo cha mateso mengi maishani mwako, nisingekuwa hapa muda huu.”
“Kwa hiyo?”

“Nipo kulipa fadhila za mabaya niliyofanya kwako?”
“Kwa kumwosha mama yangu?”
Hakujibu. Nikaendelea kumzodoa.

“Kunisaliti, kumtelekeza mwanao na kuharibu maisha yangu. Inalipwa kwa kumwogesha mama yangu! Eti Nasra?” nilihoji huku nikimwangalia Nasra usoni.
Hakujibu alibakia ameghafirika, maneno yangu ni kama yalimgusa.

“Sikiliza Nasra,” nilisema tena.
“Hakuna jambo lolote la wema utakalofanya litakaloweza kunisahaulisha mabaya uliyonitendea, labda moyo wangu uamue tu kukusamehe. Weka akilini hilo.”

Nasra alishusha pumzi ndefu, akachutama na kuangua kilio cha chini chini.
“Huondoki?” nikamuuliza tena.

Alisimama, akataka kama kusema kitu, lakini akaghairi, akatembea kuelekea getini. Nikamfuata nyuma ili akitoka tu nifunge geti.

“Nimepewa talaka na mume wangu!” alisema huku akitembea.
“Kwa nini?”

“Ni kwa sababu sina kizazi!”
“Eeh!!! Kilikwenda wapi?”
Alisimama na kunigeukia kisha akaniuliza swali ambalo nililiona ni la kipumbavu. Akauliza:
“Unataka nikwambie?”


“Ulitegemea sintahoji kizazi chako kimekwenda wapi?”
Alitabasamu, sikujua kama tabasamu lake lilitokana na kufurahishwa na kauli yangu ama vipi.

Ninachokumbuka Nasra Mfaume alianza kunipa maelezo yaliyonikata maini. Alinisimulia:

“Wakati nakusaliti wewe dhidi ya yule sharobaro mwanamuziki, nilipata ujauzito....” alisema. Akasita kisha akaniangalia usoni, uso wangu ulisawijika kwa sentesi ile.

Nikawa kama nimewekwa kwenye theruji. Mwili wote ulipoa. Kumbe mke wangu aliwahi kupewa mimba na hawara wake. Loh!!.

Japokuwa nilikuwa nimekwisha achana na mwanamke yule lakini jambo lile liliniuma, maumivu yake utadhani tukio lilitokea jana tu.

“Eeh ikawaje?” nikamuuliza. Donge kavu lilinikaba kooni.
“Kwa kutotaka wewe kujua kama nina mwanaume mwingine, nilikwenda kuitoa mimba. Ilikuwa ni siri kati yangu na yule bwana.

Sikujua kama kwa kutoa ile mimba kulikuwa na athari, baada ya kuolewa na huyu bwana mwingine athari zake ndio nimeziona, sina kizazi.

Mume wangu huyo ameshindwa kabisa kuwa na simile na jambo hili, amenitaliki kwa kushindwa kumzalia mtoto. Nina siku nne tangu nitoke mikononi mwake.” Alimaliza.

Uso wa Nasra ulijawa machozi, nilishindwa kutathimini kilio chake kilitokana na nini hasa. Je ni kushindwa kupata mtoto?

Ama kupewa talaka? Aidha ni juu ya upumbavu wake wote kwa ujumla.
“Nimejifunza mengi maishani, nataka nisahihishe makosa yangu Faraji” alisema.

“Usiku mwema Nasra.”
Ndio kitu pekee nilichomwambia usiku ule.
Kauli hiyo ilifanya Nasra aangue kilio kama mtoto mdogo, sijui aliwaza kitu gani binti yule.

Labda alidhani naweza kuwa na huruma dhidi yake. Kwa kweli alikuwa mwanamke aliyevuruga maisha yake kwa ujuha wake mwenyewe.

Nilifunga geti na kurudi ndani kwa ajili ya kumwogesha mama yangu kipenzi.
Usiku ule nilipopanda kitandani, nilifikiria mambo yote aliyonieleza Nasra.

Pamoja na kwamba nafsi yangu ilikiri Nasra alikuwa mkosaji, lakini sauti moja ilinisihi kutomchukia daima mtu yule.
“Hakuna binadamu mkamilifu.

Wakati mwingine tunakosea ili tujifunze.” Sauti moja mawazoni iliniambia.
“Kwa makosa aliyoyafanya Nasra, kwa sasa atakuwa mwanamke bora pengine kuliko yeyote yule, maana amekwishakosea na kajifunza.

Mpe nafasi, ” sauti ile iliendelea kunishawishi.
Kwa kweli hadi kunapambazuka, lile donge kavu sijui hata lilipotelea wapi, nilikuwa na fikra tofauti kuhusu Nasra. Nilitaka niishi naye tena, ikiwezekana nimwoe upya!!!!!

*****
Ilikuwa ni siku mpya. Jumapili tulivu. Nilikuwa nimeamka tangu alfajiri nikifanya usafi wa hapa na pale.
Nilimwandalia mama stafutahi ya chapati za kumimina na mayai.

Akiwa anakunywa chai nikwamweleza kila kitu kilichotokea kwa Nasra. Pia nikamwambia nadhiri ya kurudiana na mwanamke huyo.

Masikini ya mungu mama yangu hakuwa na makuu, alikuwa radhi kwa kila kitu nitakacho.

Wakati tunaendelea na maongezi mara mlango wa geti uligongwa, nikamini kivyovyote vile mgongaji ni Nasra. Niliona itakuwa fursa nzuri kama nitazungumza na mrembo yule ili tuingie kwenye makubaliano ya kuanza maisha mapya pale kijijini.

Nilisimama na kwenda kufungua geti. Mara nilikutana na watu ambao sikuwategemea. Walikuwa ni askari polisi wawili waliovalia kijeshi.

“Wewe ndiye Faraji?”
“Kuna tatizo?” nilihoji. Ilikuwa ajabu, sikuwahi kufuatwa na polisi kwa miaka mingi sasa. Leo vipi tena. Kulikoni.

“Wewe ndiye Faraji!!” jamaa walirudia kuniuliza tena kwa amri.
“Ndio ni mimi, kuna nini?”
“Unahitajika kituoni.”
“Kuna tatizo gani?”

Jamaa hawakunipa jibu. Walinishika na kunipeleka kituoni. Hadi tunafika sikuwa nimejua kwa nini nikamatwe, ingawa kuna wakati nilihisi huenda kuonana kwangu na Nasra kuna uhusino fulani wa mimi kushikwa na polisi.

“Wewe ndiye Faraji Mpangalala?”mkuu wa kituo aliniuliza baada ya kuingizwa ofisini kwakwe.
“Ndio mimi. Kuna nini Afande?”
“Kwani hujaambiwa?”
“Sijaambiwa chochote!”

“Askari waliokuja kukukamata Ilibidi wakwambie wanakukamatia nini.”
“Hawakunieleza!” nilisema.
“Unahusishwa na kifo cha Nasra Mfaume” kamaanda alipasua jipu.

Lilikuwa ni bomu lililonifanya nilihisi ni ndoto inanipitia nikiwa nimelala usingizi.
“Nasra....Nasra ame....Nasra amekufa lini?”
“Jana usiku.”
“Jana usiku!!!!
“Ndiyo.”

“Nilikuwa naye!!!!”nilisema kwa wahaka huku nikimwangalia usoni yule kamanda.
“Tunajua ulikuwa naye, lakini baada ya kuachana naye ndipo alipokutwa na mauti?”

“Kivipi? Ilikuwaje? Kwa nini na wapi?”
“Hayo maswali nikuulize wewe!!”
“Whaat!!” nilimaka.
“Nisikilize bwana mdogo.” alisema kamanda akiwa ananiangalia kwa makini.

“Uchunguzi wa awali unanaonesha Nasra amejiua mwenyewe kwa kisu ndani ya chumba chake.”kamanda yule alisema huku akikuna ndevu zake zilizokuwa zimepunguzwa kwa mtindo wa mustachi.

“Hata hivyo Nasra kaacha ujumbe wenye maelezo yasiyojitosheleza sababu ya kujiua kwake, ujumbe huo unakutaja wewe kuwa moja ya sababu ya yeye kujiua, ndio maana uko hapa kusaidia polisi.”

“Uko wapi huo ujumbe?”
Alinipa kipande cha karatasi kilichoandikwa na Nasra. Nilisoma maneno yaliyoandikwa kwenye ujumbe ule yalinikata maini. Aliandika hivi:
“Faraji mpenzi...

Sioni, sababu ya kuendelea kuishi katika dunia kwa mateso makali ya nafsi. Dunia imenielemea na imenishinda. Hiki ndicho ninanistahili. Nisamehe kwa yote niliyokutendea maishani, angalau nakufa ili nikaungane na mwanetu Mwanda huko akhera.”

“Nooooo!” nilipiga kelele nikalia kama mtoto.
***
Siku mbili badaye niliachiwa huru baada ya uchunguzi wa kipolisi kuonesha sikuwa na kesi ya kujibu, niliwaomba polisi nikapaone mahali Nasra alipojiulia. Nikapelekwa kwao, mtaa wa Bweru.

Chumba cha Nasra kilikuwa kimefungwa kwa amri ya polisi, nilisukuma mlango nuru ya mwanga hafifu ikaangaza chumbani. Kitandani kulikuwa na mashuka yaliyotapakaa damu iliyokaukiana.

Damu ya Nasra Mfaume, damu ya Mwanamwali.
Nilimlilia Nasra hadi macho yakavimba, kifo chake kiliniuma mno, kwa kweli moyo wangu ulikuwa na majeraha makali sana.
Wiki moja badaye, Nasra alizikwa katika makaburi ya Lugongoni.

Mimi bado naishi kijiji cha Nguruka mkoani Kigoma, naendelea kumlea mama yangu ambaye bado hajaweza kusimama.
Mwisho kabisa nakushukuru kwa kusoma simulizi hii ya kweli ya maisha yangu. Naamini kuna funzo umepata maishani.

MWISHO.

Usikose kufutilia simulizi mpya
Ahsante sana Shunie mpnz kwa kujitolea kutulea hadithi. Mungu akubariki sana
 
Shunie asante sana dada, kwa story nzuri yenye huzuni ya kila aina na mafundisho lukuki. Kiukweli nimejifunza mengi sana hapa.....mengine yamenifurahisha na mengine yameniliza pia.

All in all, jua tupo pamoja....God bless you.
 
Shunie asante sana dada, kwa story nzuri yenye huzuni ya kila aina na mafundisho lukuki. Kiukweli nimejifunza mengi sana hapa.....mengine yamenifurahisha na mengine yameniliza pia.

All in all, jua tupo pamoja....God bless you.
Ahsante sana Shunie mpnz kwa kujitolea kutulea hadithi. Mungu akubariki sana
Asante sana shunie.hadithi ina mafundisho mno
Asante dear
Duh story inafunzo kubwa Sana asante Sana Shunie kwa kutuletea hii story pongezi nyingi ziende kwa mwandishi Mungu azidi kumbariki
mbarikiwe mnooooo
 
Sehemu ya 44

Sikuamini macho yangu. Nasra Mfaume, mke wangu wa ndoa, alikuwa amekunjwa na mwanaume mrefu mwenye misuli, wakiwa kama walivyozaliwa, waliikuwa wakifanya mapenzi, jamaa alikuwa amemkunja mke wangu kwa mtindo ambao mimi sikuwa kumfanyia mwanamke yule.

Nilijikuta nalia kama mtoto mdogo aliyetelekezwa na mzazi wake, mke wangu mrembo, niliyempenda kwa dhati, alikuwa amenipa pigo takatifu.

Baada ya kuona wameingiliwa, walishituka mno, hakuwategemnea kabisa tukio lile, wakiwa kwenye hali ya kuzubaa na taharuki kubwa, Issa na wenzake walikazana kufotoa picha.

Yule mwanaume alikuwa wa kwanza kugutuka na kuona alitakiwa afanye kitu kijificha na aibu ile, haraka alivuta shuka na kujifunika, hata hivyo alikwisha chelewa sana, picha nyingi zilikwisha ingia kwenye kamera za waandishi.

Mke wangu naye, baada ya kugundua alitakiwa ajistiri akavuta shuka jingine na kujifunika. “Tusameheni jaman,” hatimaye jamaa akasema, kauli ile ilikuwa ni mthili ya petrol katika moto, iliniudhi sana, hasira zilinipanda, nikiwa bado kwenye kilio cha uchungu, nilimsogelea na kutandika ngumi mbili za uso.

Kufumba na kufumbua uso wake ukajaa damu, tukio hilo likamliza mke wangu kwa hofu. Naye akaanza kuomba msamaha, tendo hilo likachochea chuki, nilimvaa na kutandika teke la tumbo akatapika chipsi kuku alizolishwa na yule bwana.

Mambo yote hayo yalikuwa yakirekodiwa na wale waandishi wa habari chakaramu.

Ndugu msomaji, nakusihi sana, kama unatabia za kutembea na wake za watu acha kabisa mchezo huo, nasema hivyo kwa sababu najua hali utakayokutana nayo siku ukifumaniwa.Na nakuhakikishia ndugu yangu, kama umezoea kula vya watu, ipo siku utakamatwa, usiombe kabisa ukutwe na tukio la kufamaniwa.

Haijalishi unazo nguvu nyingi, pesa, ama mamlaka katika serikali, ukifumaniwa na mke wa mtu, ndugu yangu, utapata tabu sana, hutowezi kabisa kupambana na mwenye mali wasaa huo.

Na sio siri, pamoja na sifa zote hizo ulizonazo, lakini mbele ya mume aliyekufuma na mkewe, huna la kufanya, unaweza jikuta unauawa na mwanaume dhariri, ambaye hajai kiganjani mwako, ikiwa tu, atakufumania na mkewe. Waswahili wanasema mke wa mtu ni sumu
Kwa teke la Mr Faraji nadhani bibie Naa alitapika manyoya
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom