Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Sijui kwa nn nasra kafa jamani kuna nyingine imeanza nimekutag
Mawazo yalimzidi kimo .. kuachwa na yule msanii ..kukataliwa na faraji kufariki kwa mtoto wake na kukosa uzazi mpaka kupewa talaka ni matukio ambayo yaliyo pelekea kujihisi kuwa dunia haimuhitaji tena
 
Mawazo yalimzidi kimo .. kuachwa na yule msanii ..kukataliwa na faraji kufariki kwa mtoto wake na kukosa uzazi mpaka kupewa talaka ni matukio ambayo yaliyo pelekea kujihisi kuwa dunia haimuhitaji tena
Na kweli alijihisi dunia imemtenga
 
Sante sana@Shunie ake.
Kama ni kweli hii stori ni ya ukweli basi faraji ana mitihani sana na Mungu amfanyie wepesi kwakweli maana magumu anayopitia yahitaji imani na moyo wa subra kwakweli.
Hii story ina mafundisho mengi sana.
 
BWANAHARUSI ALIYEJERUHIWA

SEHEMU YA MWISHO

ILIPOISHIA...

“Anahisi nikiwa mbali naye nitakuwa na mwanaume mwingine.”
“Whaat!!”nilimaka kwa hasira.
Nilimsihi sana nikimtaka aje nyumbani, lakini ndugu yangu aligoma, niliwasiliana na mumewe ambaye kwangu ni shemeji yangu, ili amruhusu mkewe aje kunisaidia kumuuguza mama, jamaa yule naye alinikatalia bila aibu. Dada yangu naye alimtii!

ENDELEA NAYO...


WATU huwa wanasema mtoto wa kike kwa mama, wa kiume kwa baba. Katika familia yetu ilikuwa kinyume chake. Ndugu zangu wa kike ambao ndio walitakiwa kuwa mstari wa mbele katika kumuuguza mama yetu wote walimpa kisogo.

Nadhani ni sahihi kusema dada zangu hawakuwa na uchungu na mama yao. Ukichilia mbali yule dada yangu wa Geita, kuna huyu aliyekuwa akiishi Tanga.

Yeye aliniambia hawezi kuja kumuuguza mama kwa kuwa mumewe alikuwa amekwenda nga’mbo kimasomo hivyo asingeweza kutoka kuja kijijini bila ruksa ya mumewe, akaongeza kuwa sheria ya dini ilikuwa hairuhusu yeye kutoka bila ruksa ya mumewe.

Kwa kweli nilikuwa napitia majaribu makubwa mno maishani. Kitendo cha dada zangu kushindwa kuja kumuguza mama yao kwa kuheshimu maslahi ya waume zao kiliniuma. Hata hivyo, kuna kitu nilijifunza kwenye jambo hilo, japokuwa niliumizwa na fikra zao.


Nilibakia na mama nikimuuguza. Mipango ya kilimo niliisimamisha. Niliendelea na kazi zangu za ufundishaji huku kila wiki nikiwa na kazi ya kumpeleka mama kwenye kliniki ya mazoezi.

Alikuwepo shangazi yangu mmoja ambaye mara nyingi alikuwa akija kunisaidia kumpa huduma muhimu kama kumwogesha, kumbadili nguo na kadhalika.

Kama ungepata bahati ya kumwona mama yangu, usingemtofautisha na mtu mwenye ugonjwa wa kiharusi. Mwanamke mnene mwenye mashavu makubwa, hakuwa yeye tena.

Alikuwa amekonda mashavu yamemnyauka na macho yenye makunyanzi yametumbukia kwa ndani.
Kila nilipokuwa nikimwangalia nilihisi uchungu.

Sikujua mipango ya Mungu ilikuwa ni nini, siri hiyo alibaki nayo yeye aliye juu. Mama ndiye faraja yangu iliyokuwa imesalia duniani.

Mama aliishi na maradhi yake kwa muda mrefu sana. Nadhani miezi karibu saba ama nane alikuwa akipambania uhai wake kitandani.

Kila baada ya ya wiki mbili nilikuwa nikimfanyia dua maalumu ili mwenyezi Mungu aweze kumfanyia wepesi katika maisha yake.

Katika kipindi fulani ilifika, yule shangazi aliyekuwa akinisaidia kumuuguza mama, naye aliugua, akawa haji tena nyumbani.

Ikabidi kazi alizokuwa akikifanya nimtafute mwanamke wa kuwa anamsaidia mama kwa malipo ya fedha.
Wakati ambao sikuwa na fedha, nilikuwa nikimuhudumia mwenyewe.

Nililazimika kungojea hadi giza liingie ndio nimwogeshe mama yangu.
Siku moja mwishoni mwa wiki, nilikuwa nimempeleka mama hospitali ni katika kliniki ya mazoezi. Wakati napita getini, nikasikia sauti ya mwanamke ikiniita nyuma yangu.

“Faraji!!”
Nikageuka kutizima. Lahaulaa!! Sikuamini kumwona Nasra Mfaume, mke wangu wa zamani.

Alikuwa amevaa sketi ndefu ya rangi ya zambarau ambayo iliburuza hadi chini. Juu alivaa blauzi nyeupe ya mikono mirefu, kichwani alijifunga ushungi wa rangi ya zambarau. Moyo wangu ulipiga kite baada ya kumwona mwanamke huyo.
“Ni wewe!!”

“Ni mimi...”alijibu uso wake ukiwa wenye tabasamu. Akaendelea kunichangamkia:
“Babari za siku?”

“Salama tu.” Nilimjibu nikiwa sina tashuishi yoyote usoni.
“Vipi kulikoni tena na mama?” alihoji huku akimwangalia mama aliye kuwa katika baskeli ya magurudumu.
“Anaumwa.”

“Ni nini na Tangu lini?”
“Mwaka sasa.”
“Nini tatizo?”
“Kiuno.”

“Poleni sana Faraji.” Alisema.
Nilimpa tabasamu jepesi lililosema: Ahsante.
“Mimi nimekuja jana.” Nasra aliendelea kusema.

Kimoyomoyo nikajisemea: Nani amekuuliza swali hilo?
“Kila la kheri Nasra.” Nilimwambia. Nikaondoka nikimwacha akinisinidkiza kwa macho.

****
Baada ya chakula cha usiku, nilikuwa nikifanya matayarisho kwa kwenda kumwogesha mama gizani. Maji ya moto nilikuwa nikiyapoza kidogo katika ndoo kubwa.

Wakati napeleka maji katika banda la uwani, nikaona kivuli cha mtu nyuma ya banda la kuku akiwa amejibanza. Kwa kuwa ilikuwa giza, nikahisi labda mwizi. Nikapaza sauti kuuliza:

“We nani?” niliuliza.
Nasra akatokeza kwa mwendo wa kunyata!!.
“Ni wewe tena umefuata nini!!” nilimaka.
“Nimekuja kukusaidia kumwogesha mama.”

“Hebu niondoke bwana.”
“Siendi popote.”
“Wewe si mke wa mtu!”
“Hata kama.” Alijibu, akanisogelea zaidi, uso wake mng’avu uling’aa gizani.

Alikuwa ananukia manukato ya mazuri.
“Kuwa mke wa mtu hainizuu kutoa msaada.” alisema.

“Sitaki matatizo hebu ishia zako.”
“Lau kama nisingekuwa chanzo cha mateso mengi maishani mwako, nisingekuwa hapa muda huu.”
“Kwa hiyo?”

“Nipo kulipa fadhila za mabaya niliyofanya kwako?”
“Kwa kumwosha mama yangu?”
Hakujibu. Nikaendelea kumzodoa.

“Kunisaliti, kumtelekeza mwanao na kuharibu maisha yangu. Inalipwa kwa kumwogesha mama yangu! Eti Nasra?” nilihoji huku nikimwangalia Nasra usoni.
Hakujibu alibakia ameghafirika, maneno yangu ni kama yalimgusa.

“Sikiliza Nasra,” nilisema tena.
“Hakuna jambo lolote la wema utakalofanya litakaloweza kunisahaulisha mabaya uliyonitendea, labda moyo wangu uamue tu kukusamehe. Weka akilini hilo.”

Nasra alishusha pumzi ndefu, akachutama na kuangua kilio cha chini chini.
“Huondoki?” nikamuuliza tena.

Alisimama, akataka kama kusema kitu, lakini akaghairi, akatembea kuelekea getini. Nikamfuata nyuma ili akitoka tu nifunge geti.

“Nimepewa talaka na mume wangu!” alisema huku akitembea.
“Kwa nini?”

“Ni kwa sababu sina kizazi!”
“Eeh!!! Kilikwenda wapi?”
Alisimama na kunigeukia kisha akaniuliza swali ambalo nililiona ni la kipumbavu. Akauliza:
“Unataka nikwambie?”


“Ulitegemea sintahoji kizazi chako kimekwenda wapi?”
Alitabasamu, sikujua kama tabasamu lake lilitokana na kufurahishwa na kauli yangu ama vipi.

Ninachokumbuka Nasra Mfaume alianza kunipa maelezo yaliyonikata maini. Alinisimulia:

“Wakati nakusaliti wewe dhidi ya yule sharobaro mwanamuziki, nilipata ujauzito....” alisema. Akasita kisha akaniangalia usoni, uso wangu ulisawijika kwa sentesi ile.

Nikawa kama nimewekwa kwenye theruji. Mwili wote ulipoa. Kumbe mke wangu aliwahi kupewa mimba na hawara wake. Loh!!.

Japokuwa nilikuwa nimekwisha achana na mwanamke yule lakini jambo lile liliniuma, maumivu yake utadhani tukio lilitokea jana tu.

“Eeh ikawaje?” nikamuuliza. Donge kavu lilinikaba kooni.
“Kwa kutotaka wewe kujua kama nina mwanaume mwingine, nilikwenda kuitoa mimba. Ilikuwa ni siri kati yangu na yule bwana.

Sikujua kama kwa kutoa ile mimba kulikuwa na athari, baada ya kuolewa na huyu bwana mwingine athari zake ndio nimeziona, sina kizazi.

Mume wangu huyo ameshindwa kabisa kuwa na simile na jambo hili, amenitaliki kwa kushindwa kumzalia mtoto. Nina siku nne tangu nitoke mikononi mwake.” Alimaliza.

Uso wa Nasra ulijawa machozi, nilishindwa kutathimini kilio chake kilitokana na nini hasa. Je ni kushindwa kupata mtoto?

Ama kupewa talaka? Aidha ni juu ya upumbavu wake wote kwa ujumla.
“Nimejifunza mengi maishani, nataka nisahihishe makosa yangu Faraji” alisema.

“Usiku mwema Nasra.”
Ndio kitu pekee nilichomwambia usiku ule.
Kauli hiyo ilifanya Nasra aangue kilio kama mtoto mdogo, sijui aliwaza kitu gani binti yule.

Labda alidhani naweza kuwa na huruma dhidi yake. Kwa kweli alikuwa mwanamke aliyevuruga maisha yake kwa ujuha wake mwenyewe.

Nilifunga geti na kurudi ndani kwa ajili ya kumwogesha mama yangu kipenzi.
Usiku ule nilipopanda kitandani, nilifikiria mambo yote aliyonieleza Nasra.

Pamoja na kwamba nafsi yangu ilikiri Nasra alikuwa mkosaji, lakini sauti moja ilinisihi kutomchukia daima mtu yule.
“Hakuna binadamu mkamilifu.

Wakati mwingine tunakosea ili tujifunze.” Sauti moja mawazoni iliniambia.
“Kwa makosa aliyoyafanya Nasra, kwa sasa atakuwa mwanamke bora pengine kuliko yeyote yule, maana amekwishakosea na kajifunza.

Mpe nafasi, ” sauti ile iliendelea kunishawishi.
Kwa kweli hadi kunapambazuka, lile donge kavu sijui hata lilipotelea wapi, nilikuwa na fikra tofauti kuhusu Nasra. Nilitaka niishi naye tena, ikiwezekana nimwoe upya!!!!!

*****
Ilikuwa ni siku mpya. Jumapili tulivu. Nilikuwa nimeamka tangu alfajiri nikifanya usafi wa hapa na pale.
Nilimwandalia mama stafutahi ya chapati za kumimina na mayai.

Akiwa anakunywa chai nikwamweleza kila kitu kilichotokea kwa Nasra. Pia nikamwambia nadhiri ya kurudiana na mwanamke huyo.

Masikini ya mungu mama yangu hakuwa na makuu, alikuwa radhi kwa kila kitu nitakacho.

Wakati tunaendelea na maongezi mara mlango wa geti uligongwa, nikamini kivyovyote vile mgongaji ni Nasra. Niliona itakuwa fursa nzuri kama nitazungumza na mrembo yule ili tuingie kwenye makubaliano ya kuanza maisha mapya pale kijijini.

Nilisimama na kwenda kufungua geti. Mara nilikutana na watu ambao sikuwategemea. Walikuwa ni askari polisi wawili waliovalia kijeshi.

“Wewe ndiye Faraji?”
“Kuna tatizo?” nilihoji. Ilikuwa ajabu, sikuwahi kufuatwa na polisi kwa miaka mingi sasa. Leo vipi tena. Kulikoni.

“Wewe ndiye Faraji!!” jamaa walirudia kuniuliza tena kwa amri.
“Ndio ni mimi, kuna nini?”
“Unahitajika kituoni.”
“Kuna tatizo gani?”

Jamaa hawakunipa jibu. Walinishika na kunipeleka kituoni. Hadi tunafika sikuwa nimejua kwa nini nikamatwe, ingawa kuna wakati nilihisi huenda kuonana kwangu na Nasra kuna uhusino fulani wa mimi kushikwa na polisi.

“Wewe ndiye Faraji Mpangalala?”mkuu wa kituo aliniuliza baada ya kuingizwa ofisini kwakwe.
“Ndio mimi. Kuna nini Afande?”
“Kwani hujaambiwa?”
“Sijaambiwa chochote!”

“Askari waliokuja kukukamata Ilibidi wakwambie wanakukamatia nini.”
“Hawakunieleza!” nilisema.
“Unahusishwa na kifo cha Nasra Mfaume” kamaanda alipasua jipu.

Lilikuwa ni bomu lililonifanya nilihisi ni ndoto inanipitia nikiwa nimelala usingizi.
“Nasra....Nasra ame....Nasra amekufa lini?”
“Jana usiku.”
“Jana usiku!!!!
“Ndiyo.”

“Nilikuwa naye!!!!”nilisema kwa wahaka huku nikimwangalia usoni yule kamanda.
“Tunajua ulikuwa naye, lakini baada ya kuachana naye ndipo alipokutwa na mauti?”

“Kivipi? Ilikuwaje? Kwa nini na wapi?”
“Hayo maswali nikuulize wewe!!”
“Whaat!!” nilimaka.
“Nisikilize bwana mdogo.” alisema kamanda akiwa ananiangalia kwa makini.

“Uchunguzi wa awali unanaonesha Nasra amejiua mwenyewe kwa kisu ndani ya chumba chake.”kamanda yule alisema huku akikuna ndevu zake zilizokuwa zimepunguzwa kwa mtindo wa mustachi.

“Hata hivyo Nasra kaacha ujumbe wenye maelezo yasiyojitosheleza sababu ya kujiua kwake, ujumbe huo unakutaja wewe kuwa moja ya sababu ya yeye kujiua, ndio maana uko hapa kusaidia polisi.”

“Uko wapi huo ujumbe?”
Alinipa kipande cha karatasi kilichoandikwa na Nasra. Nilisoma maneno yaliyoandikwa kwenye ujumbe ule yalinikata maini. Aliandika hivi:
“Faraji mpenzi...

Sioni, sababu ya kuendelea kuishi katika dunia kwa mateso makali ya nafsi. Dunia imenielemea na imenishinda. Hiki ndicho ninanistahili. Nisamehe kwa yote niliyokutendea maishani, angalau nakufa ili nikaungane na mwanetu Mwanda huko akhera.”

“Nooooo!” nilipiga kelele nikalia kama mtoto.
***
Siku mbili badaye niliachiwa huru baada ya uchunguzi wa kipolisi kuonesha sikuwa na kesi ya kujibu, niliwaomba polisi nikapaone mahali Nasra alipojiulia. Nikapelekwa kwao, mtaa wa Bweru.

Chumba cha Nasra kilikuwa kimefungwa kwa amri ya polisi, nilisukuma mlango nuru ya mwanga hafifu ikaangaza chumbani. Kitandani kulikuwa na mashuka yaliyotapakaa damu iliyokaukiana.

Damu ya Nasra Mfaume, damu ya Mwanamwali.
Nilimlilia Nasra hadi macho yakavimba, kifo chake kiliniuma mno, kwa kweli moyo wangu ulikuwa na majeraha makali sana.
Wiki moja badaye, Nasra alizikwa katika makaburi ya Lugongoni.

Mimi bado naishi kijiji cha Nguruka mkoani Kigoma, naendelea kumlea mama yangu ambaye bado hajaweza kusimama.
Mwisho kabisa nakushukuru kwa kusoma simulizi hii ya kweli ya maisha yangu. Naamini kuna funzo umepata maishani.

MWISHO.

Usikose kufutilia simulizi mpya
Shangazi Shunie hureyyyy nimemaliza. Barikiwa sn mama
 
Sante sana@Shunie ake.
Kama ni kweli hii stori ni ya ukweli basi faraji ana mitihani sana na Mungu amfanyie wepesi kwakweli maana magumu anayopitia yahitaji imani na moyo wa subra kwakweli.
Hii story ina mafundisho mengi sana.
Zaidi ya mafundisho jamani inasikitisha sana
 
SEHEMU YA 19

Daktari alishauri tuondoke na turudi kesho yake kwa kuwa uzalishaji wa mke wangu ilikuwa na mizengwe mingi.

Kauli ya daktari ilinitisha, hata hivyo nilipiga moyo konde na kuondoka kuerejea nyumbani. Usiku ule sikulala, moyo ulikuwa ukinidunda, presha ilikuwa juu.

Siku iliyofuatia. Asubuhi na mapema, niliamka nikajiandaa, kisha nikamwaga shemeji yangu Aisha, nikimtaka yeye aje Hospitalini badaye mchana, baada ya kumaliza shughuli zake asubuhi ile.

Niliendesha gari hadi Posta, kwa kuwa magari yalikuwa machache, muda mfupi badaye nilikuwa Regency. Baada ya kufika manesi walinipokea kwa sura zisizokuwa na chembe ya ukarimu wowote.

Mapigo ya moyo yakaanza kunidunda, nikanza kuhisi heunda kuna jambo baya limetokea dhidi ya mke wangu na mtoto. “Vipi hali ya mke wangu?’ nilimuuliza nesi mmoja.

“Daktari Charles Meleka amesema ukifika tu ukamwone ofisini kwake,” badala ya kujibu swali, nesi yule aliniambia kitu kingine kabisa. “Mke wangu ni mzima?” niliuliza kwa wahaka mapigo ya moyo yakinIenda kasi “Kaka hebu kuwa mwelewa,” nesi alizidi kuwa mkali.

Nikaona nisiendelee kurumbana na yule mwanamke, nilichofanya ni kwenda kwenye ofisi ya dokta Charles Meleka.

Baada ya kuingia ndani ya ofisi ile dokta Cherles alikuwa ameketi katika kiti cha kuzunguka huku mezani kwake kukiwa na mafaili kadhaa.

“Hongera Mr Faraji Hussein…” Dr Charles alianza kunipasha baada ya kuingia. “Mkeo kajifungua mtoto wa kiume tena kajifungua salama kabisa….lakini”

Dr Charles Meleka alisema. “Lakini nini?” nikauliza kwa kiherehere. “Kwanini unafanya mapenzi na mkeo kinyume na maumibile?” Dr Charles Meleka aliniuliza kwa ukali. Nikabaki nimepigwa na bumbuwazi.

...!!! Hii kubwa kuliko..!!
 
SEHEMU YA 28

“Njoo chumbani,” nilimwambia bila kujibu swali lake.

Tuliongozana hadi chumbani mtoto tukimwacha mikononi kwa dada wa kazi. Doreen. “Mke wangu,” nilimwita tukiwa chumbani.

“Bee.” “Ungependa kuona maisha ya mwanao yakishia kulelewa na baba au mama wa kambo?” “Kivipi mume wangu?” “Sikutoshelezi kimapenzi?”

“Mbona sikualewi? “Tupo wanaume wangapi tunaokuvua nguo yako ya ndani?” “Heeee!!!” alihamaki baada ya swali hilo.

“Nakuuliza tena, tupo wanaume wangapi tunaokuvua nguo yako ya ndani?” “Faraji naomba unitake radhi,” akaniambia kwa ukali.

Nilinyamaza nikavuta pumzi, donge zito lilinikaba kooni, nilimsimulia mambo yote niliyoelezwa na daktari.

Habari ile ilimshitua sana mke wangu, lakini bado uso wake uliendelea kuonesha ni kuumbe asiyekuwa na hatia yoyote maishani.

“Faraji kama umenichoka niambie, lakini siyo kwa kunitafutia sababu namna hii” hatimaye akaniambia. “Kukutafutia sababu!!!.”

“Ndio, unanitafutia sababu” “Kwa taarifa yako, hili siyo jambo la kwanza kuelezwa juu ya uhuni ufanyao…” nikasema nikiwa nimemkazia macho.

“Wakati unajifungua ulijisaidia sana haja kubwa kitandani, na madaktari husema hali hiyo huwatokea wanawake wanaojihusisha na ngono kinyume na maumbile.”

Nilimpasualia. “Faraji shika adabu yako” aliniambia kwa ukali. “Sasa niambie ni lini nilikuingia kinyume na maumbile” “Unikome!!” alisema

Nikamchapa kibao. Akabweka kama jibwa koko. Bila kutegemea Akanivaa akiwa amechanua vidole vyake na kuniparua usoni kwa makucha.

Hasira zilinipanda nikamtandika kofi jingine usoni. Kilichofuata baada ya hapo ulikuwa ni ugomvi mkubwa sana.

Songombingo lile likawakusanya majirani ambao walikuja hadi chumbani kutuamulia, mke wangu alikuwa na hasira za mbogo akaanza kupasua vitu vya ndani hovyo.

Wakati huo mwanangu asiyejua lolote alikuwa akilia muda wote. Ghafla ndoa ikawa chungu kama shubiri.

JE NINI KILITOKEA?

Aisee Faraji pole sana..ngoja niendelee nitakupa pole vzr nikishamaliza...‍♀️
 
Sehemu ya 46

Jamaa pamoja na mwonekano wa mwili wa mazoezi, umarufu, uliotokana na kazi zake za muziki, sanjari na fedha zilizompa kiburi hapa mjini, wasaa ule alikuwa zoba mtozeni.

Kwani, baada ya lile teke la tumbo nililomtandika Nasra na kumfanya ajitapikie matapishi, nilimgeukia huyo njemba mwenye misuli thabiti, nikaendelea kumshushia kipigo cha mbwa koko.

Wandishi wa habari wakazidi kurekodi, kufumba na kufumbua utitiri wa watu wakajaa kwenye gesti ile.

Hazikupita dakika nyingi askari polisi waliwasiri, walinituliza kisha wakawataka watu wale wavae nguo, gumzo kubwa kuzunguka gesti ile, ilikuwa ni juu ya fumanizi.

Baada ya mke wangu na mtu wake kuvaa nguo, walitolewa nje na kupakiwa ndani ya defender la polisi, wakati mambo yote yanafanyika picha ziliendelea kufotolewa, mimi, mwenyekiti wa mtaa, pamoja na mhudumu wa gesti, tukatakiwa kuongozana na polisi wale.

Kwa pamoja tuliingia ndani ya gari la polisi na safari ya kuelekea kituo cha Oystabay ikaanza.

Baada ya kuwasiri, mke wangu na yule bwana waliingizwa kwenye ofisi za wapelelezi.

Mimi nikabakia nje,walichukuliwa maelezo mule ndani, muda mfupi badaye wakatolewa, ikawa zamu yangu kuhojiwa na kutoa maelezo.

Nilitoa maelezo mbele ya askari mpelelezi, nikamweleza kila kitu juu ya usaliti wa mke wangu hadi kumfumania.

“Huyo mwanamke ni mkeo au alikuwa mkeo?” askari kanzu akauliza, baada ya kumpa maelezo.

“Ni mke wangu” “Mbona yeye anasema wewe siyo mume wake ila ulikuwa mume wake kwakuwa mlishapeana talaka kitambo sana?”

“Anasema mimi siyo mume wake!” niliuliza kwa mshangao “Ndio, kwa mujibu wa maelezo yake anasema mlikwisha achana muda mrefu tu, ila wewe ndio unamng’ang’ania” askari yule alinipasha, nilishusha pumzi ndefu nikaumia sana moyoni.

Je itakuaje?

No isiwatishe kuruka moja mtiririko upo sawa alisahau kuedit

Duuh kweli Nasra ni noumaaah...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom