Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Sehemu ya 44

Sikuamini macho yangu. Nasra Mfaume, mke wangu wa ndoa, alikuwa amekunjwa na mwanaume mrefu mwenye misuli, wakiwa kama walivyozaliwa, waliikuwa wakifanya mapenzi, jamaa alikuwa amemkunja mke wangu kwa mtindo ambao mimi sikuwa kumfanyia mwanamke yule.

Nilijikuta nalia kama mtoto mdogo aliyetelekezwa na mzazi wake, mke wangu mrembo, niliyempenda kwa dhati, alikuwa amenipa pigo takatifu.

Baada ya kuona wameingiliwa, walishituka mno, hakuwategemnea kabisa tukio lile, wakiwa kwenye hali ya kuzubaa na taharuki kubwa, Issa na wenzake walikazana kufotoa picha.

Yule mwanaume alikuwa wa kwanza kugutuka na kuona alitakiwa afanye kitu kijificha na aibu ile, haraka alivuta shuka na kujifunika, hata hivyo alikwisha chelewa sana, picha nyingi zilikwisha ingia kwenye kamera za waandishi.

Mke wangu naye, baada ya kugundua alitakiwa ajistiri akavuta shuka jingine na kujifunika. “Tusameheni jaman,” hatimaye jamaa akasema, kauli ile ilikuwa ni mthili ya petrol katika moto, iliniudhi sana, hasira zilinipanda, nikiwa bado kwenye kilio cha uchungu, nilimsogelea na kutandika ngumi mbili za uso.

Kufumba na kufumbua uso wake ukajaa damu, tukio hilo likamliza mke wangu kwa hofu. Naye akaanza kuomba msamaha, tendo hilo likachochea chuki, nilimvaa na kutandika teke la tumbo akatapika chipsi kuku alizolishwa na yule bwana.

Mambo yote hayo yalikuwa yakirekodiwa na wale waandishi wa habari chakaramu.

Ndugu msomaji, nakusihi sana, kama unatabia za kutembea na wake za watu acha kabisa mchezo huo, nasema hivyo kwa sababu najua hali utakayokutana nayo siku ukifumaniwa.Na nakuhakikishia ndugu yangu, kama umezoea kula vya watu, ipo siku utakamatwa, usiombe kabisa ukutwe na tukio la kufamaniwa.

Haijalishi unazo nguvu nyingi, pesa, ama mamlaka katika serikali, ukifumaniwa na mke wa mtu, ndugu yangu, utapata tabu sana, hutowezi kabisa kupambana na mwenye mali wasaa huo.

Na sio siri, pamoja na sifa zote hizo ulizonazo, lakini mbele ya mume aliyekufuma na mkewe, huna la kufanya, unaweza jikuta unauawa na mwanaume dhariri, ambaye hajai kiganjani mwako, ikiwa tu, atakufumania na mkewe. Waswahili wanasema mke wa mtu ni sumu
 
Sehemu ya 46

Jamaa pamoja na mwonekano wa mwili wa mazoezi, umarufu, uliotokana na kazi zake za muziki, sanjari na fedha zilizompa kiburi hapa mjini, wasaa ule alikuwa zoba mtozeni.

Kwani, baada ya lile teke la tumbo nililomtandika Nasra na kumfanya ajitapikie matapishi, nilimgeukia huyo njemba mwenye misuli thabiti, nikaendelea kumshushia kipigo cha mbwa koko.

Wandishi wa habari wakazidi kurekodi, kufumba na kufumbua utitiri wa watu wakajaa kwenye gesti ile.

Hazikupita dakika nyingi askari polisi waliwasiri, walinituliza kisha wakawataka watu wale wavae nguo, gumzo kubwa kuzunguka gesti ile, ilikuwa ni juu ya fumanizi.

Baada ya mke wangu na mtu wake kuvaa nguo, walitolewa nje na kupakiwa ndani ya defender la polisi, wakati mambo yote yanafanyika picha ziliendelea kufotolewa, mimi, mwenyekiti wa mtaa, pamoja na mhudumu wa gesti, tukatakiwa kuongozana na polisi wale.

Kwa pamoja tuliingia ndani ya gari la polisi na safari ya kuelekea kituo cha Oystabay ikaanza.

Baada ya kuwasiri, mke wangu na yule bwana waliingizwa kwenye ofisi za wapelelezi.

Mimi nikabakia nje,walichukuliwa maelezo mule ndani, muda mfupi badaye wakatolewa, ikawa zamu yangu kuhojiwa na kutoa maelezo.

Nilitoa maelezo mbele ya askari mpelelezi, nikamweleza kila kitu juu ya usaliti wa mke wangu hadi kumfumania.

“Huyo mwanamke ni mkeo au alikuwa mkeo?” askari kanzu akauliza, baada ya kumpa maelezo.

“Ni mke wangu” “Mbona yeye anasema wewe siyo mume wake ila ulikuwa mume wake kwakuwa mlishapeana talaka kitambo sana?”

“Anasema mimi siyo mume wake!” niliuliza kwa mshangao “Ndio, kwa mujibu wa maelezo yake anasema mlikwisha achana muda mrefu tu, ila wewe ndio unamng’ang’ania” askari yule alinipasha, nilishusha pumzi ndefu nikaumia sana moyoni.

Je itakuaje?

No isiwatishe kuruka moja mtiririko upo sawa alisahau kuedit
 
Sehemu ya 47

“Huyo mwanamke ni mkeo au alikuwa mkeo?” askari kanzu akauliza, baada ya kumpa maelezo. “Ni mke wangu” “Mbona yeye anasema, wewe siyo mume wake ila ulikuwa mume wake zamani, mlishapeana talaka kitambo sana?”

“Anasema mimi siyo mume wake!” niliuliza kwa mshangao “Ndio, kwa mujibu wa maelezo yake, anasema mlikwisha achana muda mrefu tu, ila wewe ndio unamng’ang’ania,” mpelelezi yule alinipasha, nilishusha pumzi ndefu nikaumia sana moyoni.

“Sasa nisikilize kwa makini,” yule mpelelezi aliongea huku akiwa amenikazia macho ya kipolisi. “Kisheria hakuna kesi ya fumanizi, kwa sababu tendo hilo limefanywa kwa makubaliano ya watu wazima.

Neno makubaliano ndio linatofautisha na kesi ya jinai iitwayo ubakaji.”aliweka kituo kisha akaendelea kunieleza. “Kimsingi kama mke wa mtu amefumaniwa linakuwa ni shauri la madai lenye lengo la kudai fidia au kuvunja ndoa na kutoa talaka.”

“Unaweza kufungua shauri mahakamani kwa kudai fidia kwa kudhalilishwa au ukataka kuvunja ndoa yenu kwa kuiomba mahakama isimamie utoaji wa talaka.”

Alihitimisha. “Nini mantiki ya kunieleza yote hayo?” “Swali zuri,” alisema kisha akaendelea.

“Nataka utambue, katika tukio la wewe kumfumania mkeo, watuhumiwa hawana kesi ya kujibu, hivyo jeshi la polisi, litawaachia huru.” “Sawa, mimi pia sina muda wa kupoteza kuwashitaki wapuuzi.” Nilisema nikiwa nimeghafirika.

Baada ya mazungumzo hayo, niliondoka kituoni nikarudi nyumbani, Nasra na hawara wake, sikuonana nao.

Nyumbani nilimkuta dada wa kazi aitwaye Doreen akimnywesha mwanangu uji. Mwanangu alikuwa bado mdogo sana, ndio kwanza alikuwa na miaka miwili na nusu.

Roho iliniuma sana. mwanangu alitakiwa awe na mama yake muda ule, bahati mbaya mwanamke alikuwa kiruka njia, nikaendelea kubaini muda si mrefu mtoto wangu angeyaanza maisha bila mzazi mmoja.

Kwa umri mdogo wa mtoto yule, nilitambua sheria inampa fursa Nasra kumlea ama kuishi naye.

Hilo lilizidi kuniumiza kichwa, sikutaka kabisa mtoto wangu akalelewe na mwanamke yule muhuni. niliingia bafuni nikaoga, nikabadili nguo kisha nikarudi sebeuleni ambako Doreen alikuwa bado akimpa uji.
 
Sehemu ya 48

Mtoto wangu Faraji aliponiona nimerejea sebuleni, alinifuata na kumuulizia mama yake. Jambo hilo lilinichoma sana moyoni, nilimkumbatia kifuani nikamdanganya mama yake angerudi muda si mrefu.

“Mama yake alivyotoka alimlilia hadi macho yakamwiva,” Doreen aliniambia. “Kwa hiyo mama yake aliondoka na kumwacha analia?”

“Ndio, alimlilia sana. aliniambia anakwenda kukutana na mtu muhimu, ila asingekawia kurudi.”

“Mtu muhimu ama hawara wake….” nilijikuta nimelopoka mbele ya Doreen, kitendo cha mke wangu.

Kumwacha mtoto analia na kwenda kufanya starehe na hawara wake. Niliudhika sana. “Pole baba,”Doreen aliniambia huku akiniangalia kwa huruma.

muda huohuo simu yangu iliita, kucheki alikuwa ni mama. “Hellow” “Hujambo baba?”sauti ya mama ilinilaki. “Sijambo mama.”

“Sasa mbona ulinikatia simu asubuhi?” nikakumbuka asubuhi wakati nazungumza naye, simu ya Issa ikawa inaingia ambapo niliisubirisha kabla ya kuikata baada ya kuelezwa mke wangu alikuwa gesti na mwanaume mwingine.

“Samahani mama, kuliktokea tukio baya ndio maana nikakata simu yako” nilimwambia. “Tukio gani?” Nikamuhadithia kila kitu, hadi naweka kituo, mama alishusha pumzi ndefu.

Akaniuliza swali moja tu. “Mtoto yuko wapi?” “Mtoto ninaye hapa.” “Unaweza kunikatia tiketi ya ndege ya kesho asubuhi nije?”

“Ndio naweza” “Basi hakikisha huyo mtoto haondoki mikononi mwako, hadi nitakapofika Dar es salam,” mama alinambia.

Kimwonekano naye hakuwa tayari kuona mtoto wangu anabakia mikononi mwa Nasra. “Vipi jambo ulilotaka kunieleza asubuhi?” nilimuuliza amama aliyekuwa bado yupo hewani.

“Mambo yote tutazungumza kesho nikifika.” Alinijibu tukaagana.

Baada ya kuagana, nilichofanya ni kumpigia Frank Majige, rafiki yangu afanyae kazi kwenye kampuni ya Fast Jet nikamwomba anifanyie mpango wa tiketi ya ndege ya kesho asubuhi.

Mara moja Frank akanihakikishia kunisaidaia jambo hilo. “Nipigie baada ya nusu saa nitakuwa tayari nimekamilisha jambo hilo,”aliniambia simuni Wakati Frank Mjige akinifanyie machakato wa tiketi, niliendelea kuwaza na kuwazua.

Katika mengi yaliyokuwa yakipita kichwani mwangu ni taswira ya mke wangu akiwa anafanya mapenzi na hawara wake.
 
Sehemu ya 49

Jambo hilo lilivyojitengeneza akilini mwangu, machozi yalinibubujika. nilimpenda sana Nasra Mfaume. Urembo wake uliochangizwa na uchotara wa kiarabu na kibantu, ulinivuta. Bikira niliyoikuta kwakwe, nikamwamini.

Kadhalika, siha na tabia njema ikawa kichocheo kilichonifanya niubwage moyo wangu kwa msichana huyo.

Hatiamye aliegeuka nyoka, tena nyoka mwenye sumu kali, aliniadhibu bila huruma. Maisha yangu yaliingia kwenye hali ngumu mno.

Upendo wote ukageuka chuki mbaya. donge zito lilinikaba kooni. nikiwa na mwanangu, nimeketi sebuleni. Hadi saa kumi jioni. Nasra hakurudi nyumbani.

“Eti hivi ndio nimwachie mwanangu! mwendawazimu peke yake anayeweza kukubaliana na ujinga huu.

Mwanamke gani hana uchungu na mtoto aliyemzaa mwenyewe, hadi sasa hajarudi na hajali maisha ya mwanaye yapo katika usalama gani,” nilinong’ona.

Ilipotimu saa kumi na mbili jioni, mdogo wake na mke wangu, Aisha. ambaye tangu nilifika nyumbani hakuwepo akaingia, aliniamkia kwa adabu kisha akaelekea chumbani kwake.

Muda mfupi badaye, akarudi sebuleni akiwa na begi lake la nguo. “Shemeji samahani,” alisema. “Dada kaniagiza hapa nyumbani.” “Kakuagiza nini?” nikaunguruma

“Ameniambia nije nimchukue mtoto, nimpeleke kwake.” “Ummepeleke wapi?” “Mahali alipo.” “Wapi?” nikauliza kwa ukali. “Tabata.”

“Mwanaizaya kweli huyu mwanamke, kwa nini akutume wewe asije mwenyewe? Kamwambie hapa hakuna mtoto wake, amwambia hawara wake amzalishe kama anataka sana mtoto,” nilibwatuka maneno ya hovyo hadi cheche za mate zikaruka.

Aisha ambaye alifanana sana na nduguye kuanzia rangi hadi zungumza yao, hakutia neno, aliishia kunieleza alikuwa amedhamilia kurudi kijijini siku inayofuatia, kwa kuwa pale nyumbani, hapakuwa na amani tena.

“Sawa, ukiondoka utawasalimia ndugu na jamaa na uwaeleza ukweli kuhusu vituko vya ndugu yako,”nilimwambia. “Sawa shemeji nimekuelewa.”

“Kwa hiyo unakwenda kwa ndugu yako Tabata kisha kesho ndio uondoke.” “Ndio. Itabidi nipeleke ujumbe ulionieleza Kuhusu mtoto.”

“Kwani huko Tabata yupo kwa nani?” nikamuuliza. “Yupo kwa mtu wake.” “Mtu wake kwa maana ya bwana wake?” “Ndio”

Jibu la Aisha lilinifanya nitamani kupaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom