Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

SEHEMU YA 108


ILIPOISHIA

“Mungu wangu!!” nilimaka baada ya kutupa macho kwenye ile karatasi ya makubaliano, ambayo ilikuwa na maelezo ya lini natakiwa kuwa nimekwisha lipa deni lao.
“Vipi?”
“Umeona nini?”
“Ni lini?”


Nilitupiwa maswali.

“Kesho saa sita mchana ndiyo siku ya mwisho. vinginevyo nyumba yangu itapigwa mnada,” niliwaambia macho nimeyatoa pima.


ENDELEA NAYO...



Watu wote wakapigwa na taharuki, ni wazi kwa muda uliokuwa umesalia isingewezekana kuzuia nyumba ile kuuzwa.

Dalili ya Nyumba ya milioni 80 kupigwa mnada kwa deni la milioni 15 ikawa waziwazi.
“Mimi nina wazo?”
Mdogo wangu mmoja alisema, kila mtu akamsikiliza.

“Kwa muda uliosalia njia sahihi ni kukopa mahali pengine ili tulipe deni hili ambalo muda wake umekwisha.”
“Nani atatukopesha fedha yote hiyo kwa masaa yaliyosalia?”
Jibu halikupatikana.

Kwa kweli hapakuwa na namna ya kuzuia nyumba yangu kupigwa mnada, hadi kikao kinavunjika hapakuwa imepatikana suluhu ya kuzuia nyumba yangu kuuzwa.
Jambo pekee lililokuwa limepitishwa na ndugu zangu ni mimi kurudi kijijini kwetu.

Huko ningeishi na mama yangu huku nikitafuta kazi nyingine ya kufanya.
Kadhalika usiku ule tulilala tukiwa na mipango ya kuondoka ndani ya nyumba hiyo asubuhi ya siku inayofuatia. Hatukupenda kukutana na fedheha ya kufukuzwa na watu wa benki wakati mchakato wa kuipiga mnada nyumba ile utakapoanza.

Nakumbuka usiku huo sikupata japo lepe la usingizi, hadi kunakucha asubuhi sikuwa nimepata usingizi, nikiwa bado kitandani, niligutushwa na sauti kali ya geti likigongwa.

Tumbo likakata, nikahisi ni mwanzo wa kuadhilika mbele ya familia yangu, niliamini wagongaji lazima wangekuwa ni watu wa benki wamekwisha wasili.
“Ngo ngo ngo ngo!” mlango uligongwa kwa nguvu zaidi.

Nilitoka na kwenda kufungua geti! Sikuamini baada ya kukutana na mtu ambaye sikumtegemea. Nasra Mfaume. Mke wangu wa zamani. Alikuwa amesimama wima amevaa hijabu iliyofunika mwili wake wote kasoro uso na mikono yake.

Aliniangalia kwa macho yaliyojaa woga, mimi nikamwangalia kwa mshangao, sikutegemea kumwona muda ule. Mikono yake ilikuwa imechora hina na hilo likanitambulisha mtu yule alikuwa amefunga ndoa siku chache zilizopita.
Tuliangaliana kwa dakika nzima, kisha akaongea.

“Mwanangu Mwanda amekufa!” alisema.
Nilishindwa kuelewa kama lilikuwa ni swali ama alikuwa akinieleza. Lakini ile tizima yake ikanijulisha kwamba alikuwa akiniuliza.

“Kwa nini uko hapa Nasra?”
“Nataka jibu, ni kweli mwanangu amekufa?” alisema tena
“Ulimkimbia...”

“Nijibuuu!” alibweka kwa nguvu machozi yakimchuruzika na kutengeneza mifereji mashavuni pake.
“Nimekwisha mzika!”
“Unasema?!”

Nasra aliangua kilio kikubwa, sauti kali ya kilio chake ikawamsha ndugu zangu ambao walikuwa bado wakimalizia usingizi wao. Walitoka na kukuta Nasra Mfaume analia na kuombeleza.
“Analia nini huyu?”

“Atuondolee uchuro mja laana huyu.”
“Mwanamke amekosa haya, wenzio wanalilia mume bora, wewe unampiga teke bahati hiyo.”
“Eti naye anajiliza kwa kuondokewa na mtoto aliyemuua mwenyewe.”

“Atakuwa mwanga huyu si bure”
Ndugu zangu walimzodoa Nasra mfaume kadiri walivyoweza, walinisihi nirudi ndani na kuachana na mwanamke huyo, walifunga geti tukamwacha nje peke yake akiendelea kumlilia mwanaye.

Sijui roho gani ilinipitia, kwa mara ya kwanza nikajikuta naguswa na kilio cha Nasra, pamoja na kwamba dada zangu walikuwa wamenisihi kutosikiliza kilio cha mwanamke huyo, hata hivyo sauti moja ikanisihi nirudi nje.

Nilitoka ndani na kurudi tena getini. Nikamkuta Nasra akiendelea kulia kwa hisia kali.

“Nataka kuliona kaburi la mwanangu, ooh! Mwanangu jamani,”
“Hakuzikwa Tanzania.” nilimwambia
“Unasema!!! Unataka kuniambia mwanangu alizikiwa huko huko?”

Nasra alipagawa, nilichofanya ni kumshika mkono na kumwondoa mbali na nyumbani. Sikupenda ndugu zangu wanikutwe naye pale.

Nasra Mfaume alikuwa ni mzazi mwenzangu, niliona inafaa nimweleze kila kitu kilichojili hadi mtoto wetu mauti ikamfika.

Mrembo yule alilia na kulia, hata hivyo kilio chake hakikubadili ukweli wa jambo lile. Mwananetu alikuwa ametutoka.


ITAENDELEA...
 
Sehemu ya 109

Mfaume alikuwa ni mzazi mwenzangu, niliona inafaa nimweleze kila kitu kilichojili hadi mtoto wetu mauti ikamfika.
Mrembo yule alilia na kulia, hata hivyo kilio chake hakikubadili ukweli wa jambo lile. Mwananetu alikuwa ametutoka.

*****

Niliyanza maisha mapya, bila mtoto, mchumba, wala mke. Ni wiki mbili na siku kadhaa zilikuwa zimepita tangu niondoke jijini Dar na kuja kuyaanza maisha mapya kijijini Nguruka.

Kama nilivyokwisha simulia mwanzo kabisa, kitaaluma nilikuwa nina shahada ya ualimu ya chuo kikuu cha Dar es salam, hivyo pale kijijini, nilikuwa nimefungua kituo maalumu cha kufundisha masomo ya ziada kwa wanafunzi wa sekondari(tution center)
Kwa kuwa kipindi hicho kulikuwa na upungufu mkubwa wa walimu hasa wa masomo ya Sayansi, kazi ile ilinipa kiasi fulani cha fedha ambacho kiliyaendesha maisha yangu na ya mama yangu bila tatizo lolote.

Kila wakati nafsi yangu ilikuwa ikinisuta na kujicheka mwenyewe, kitendo cha kuporomoka kutoka kwenye mafanikio makubwa hadi kuangukia kwenye ualimu, ilikuwa tusi baya maishani, ualimu ni kazi iliyodharaulika hata na mtoto mdogo.
Niliapa kutorudi tena Dar es salam, niliweka nadhiri ya kumalizia maisha yangu katika kijijini kile.

Mwaka ulikatika, kazi ya kufundisha, haikuleta matokeo yoyote, ndipo fikra za kujiingiza kwenye kilimo cha tumbaku zikaanza kutembea kichwani kwangu. Mwaka huohuo nikaanza kutengeneza mazingira ya kujiingiza kwenye kilimo kabla ya mvua za masika kuaanza.

Nilimshirikisha mama juu ya mawazo hayo, hakuwa na pingamizi, aliniunga mkono. Nakumbuka siku hiyohiyo, nilinyonga baiskeli hadi kijiji kimoja kinaitwa Nyangabo, wenyeji wa Nguruka watakuwa wanapafahamu sehemu hii.

Huko alikuwa akiishi babu yangu upande wa ubabani kwangu, anaitwa mzee Nswima Mpangalala, lengo la kwenda huko ilikuwa ni kumwomba sehemu ya shamba lake ambalo ningelitumia kwa kilimo cha tumbaku kwa mwaka huo kabla ya mvua za masika kuanza.

Bahati nzuri babu yangu yule nilikuwa nimeshibana naye sana, kipindi kile nikiwa Dar es salam, kila mwezi nilikuwa nikimwagizia suti za bei mbaya na viwalo vya hapa na pale. Hivyo kwa siku hiyo nilipo mwomba sehemu ya ardhi kwa kilimo hakuwa na pingamizi kabisa.

Nilirudi nyumbani nikiwa na furaha, lakini nilipofika na kuingia ndani, nikamkuta mama amelala huku akilalamika maumivu makali ya kiuno. Alikuwa akijinyonga nyonga huku akigumia maumivu makali.
Nilichofanya ni kumnunulia dawa za maumivu na kumpa.

Lakini wapi, mama alizidi kulalamika kiuno. Niliamua kumkimbiza hospitali ya Nguruka. Alipokelewa na kuingizwa chumba cha uchunguzi. Nilibakia nje katika benchi roho ikinidunda.Baada ya kama dakika 20 kupita mama alitolewa akiwa kwenye kitanda cha magurudumu, alipelekwa wodini.

“Ana tataizo gani dokta” nilihoji.
“Amepatwa na maumivu ya mfupa katika kiuno, ni hali inayotokea mara nyingi kwa wazee, misuli na mifupa ya upande wa chini wa mgongo huchoka kutokana na umri.”

“Mungu wangu! Kwa hiyo atapona?”
“Ndio atapona, ila atachukua muda mrefu hadi kusimama na kutembea kama ilivyokawaida.”

Ilikuwa ni habari iliyonivunja moyo wangu, hakika niliamini lile lilikuwa ni bomu jingine ambalo lingeweza kuupasua moyo wangu maishani kama siku moja lingelipuka.

Kitendo cha kuambiwa itamchukua muda mama yangu hadi kusimama ilinichanganya sana.

Wiki moja badaye, tuliruhusiwa kurudi nyumbani. Tulirudi mama akiwa kwenye kiti cha magurudumu matatu, hakuweza kusimama kabisa, dokta alinipatia maelekezo ya kumpeleka kwenye kliniki ya mazoezi iliyopo hospitalia pale kila mwisho wa wiki.

ilinibidi nimpigie simu dada yangu wa Geita ili aje anisaidie kumuguuza mama, hasa kwa kumpa huduma za msingi kama kumwongesha, hata kumpeleka chooni.
Hata hivyo majibu aliyonipa baada ya kumweleza jambo hilo yalinichoma mno, alisema:

“Mume wangu amekataa nisije huko, hivyo nasikitika kumwambia siwezi kuja kumuuguza mama.” Sikuamini kusikia maneno hayo kutoka kwa ndugu yangu huyo.

“Hutaki kumuuguza mama yako?”
“Sio sitaki, bali mume wangu ndio hataki!”
“Kwa nini?”
“Haniamini?”
“Kivipi?”

“Anahisi nikiwa mbali naye nitakuwa na mwanaume mwingine.”
“Whaat!!”nilimaka kwa hasira.

Nilimsihi sana nikimtaka aje nyumbani, lakini ndugu yangu aligoma, niliwasiliana na mumewe ambaye kwangu ni shemeji yangu, ili amruhusu mke wake aje kunisaidia kumuguza mama, lakini jamaa yule naye alinikatalia bila aibu. Dada yangu naye alimtii!



Usikose sehemu ya mwisho mwisho ya mkasa huu wa aina yake.
 
Shunie Tulikua pa1 japo ilikua kimya kimya Ucjal mrembo! Shukree
 
Money Talk...
Ila jamaa faraji ametandikwa mno na mapenz,,yaan hakuna utofauti na maisha halisi ya mahusiano hasa masuala ya uaminifu..ni mambo yanayo tokea daily.

Nimefanikiwa kuipitia hii story,ina mafundisho mengi mnoo
nikwel usemacho ila naye kuna wakati alikuwa anakosea sana hadi kufikia hatua yakutaka kuyakatisha maisha yake,me alikera sana akivyokuwa ananyenyekea nakushindwa kuwa kama mwanaume
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom