Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

Simulizi: Bwana Harusi aliyejeruhiwa

SEHEMU 10

Joto lake likaongeza hisia za ajabu, wakati vidole vyangu vikihamia katikati ya mfereji wa uti wa mgongo na kutambaa kutokea juu hadi kwenye makalio ya chotara yule. Alishindwa kabisa kuizuia sauti isimtoke.

“Fa…Fa…Faraaahh…Jiiii!” Sikukoma. Vidole vyangu vikiwa vinafanya ziara pande zote za mwili wake, mdomo wangu niliusogeza kwenye matiti yake. Kisha nikawa nazimung’unya zile chuchu kama pipi.

Lilizuka balaa!. Nasra alikuwa akipiga kelele za ajabu sana. Ukubwa wa Kelele za mahaba, niliona zingeweza kumstua mjomba Majeed na shemeji Aisha.

Nilichofanya ni kufungulia redio sauti ya juu, ili sauti ya redio angalau imeza ukelele wa Nasra Mfaume.

“ Ngoja…ngoja kidogo,” Nasra alinisihi baada ya kuwa nimerudi kuendelea pale nilipoishia. “Kuna jambo ningependa nikueleze,”aliniambia “Jambo gani bibie?”
“Mwenzio sijawahi kufanya huu mchezo.”
“Acha masikhara.”

“Haki ya…..” “Tangu uzaliwe?”
“Ndio”
“Kwahiyo wewe ni bikira?”
“Kabisa.”

“Kama ni kweli nitakupenda maradufu,” nilimwambia. Uso wake ulikuwa umesawijika. “Kwahiyo unasemaje?” nikamuuliza.

“Naogopa…Utaniumiza!!!” “Huwezi kuumia”
“Kivipi?’
“…kwani unamiaka mingapi?”
“ 22” “Huwezi kuumia. Ushakuwa mkubwa, siwezi kukumiza mpenzi”
“Na ukiniumiza Je?”
“Nitandike kibao.”

Alitabasamu na mimi nikatabasamu. Nikamsogeza karibu, nikampa kinywa change, kisha tukaanza kunyonyana ndimi.

Mchuano ukaanza upya. Nilimwandaa kiasi cha haja. Sikutaka kabisa kumuumiza hasa ukizingatia siku hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kufanya tendo la ndoa maishani mwake.

Kwa kweli ndugu msomaji, usiku huo ni siku ambayo siwezi kuisahau maishani mwangu..

Penzi nililolipata kwa mke wangu ambaye mimi nilikuwa ndiye mwanaume wake wa kwanza, lilikuwa ni tamu pengine kuliko penzi nililowahi kupewa na mwanamke yeyote maishani.
*****
Asubuhi kulipokucha, nilikuwa wa kwanza kuamka, mionzi hafifu ya jua la asubuhi ambayo huwa inapenya chumbani kwangu kupitia dirishani. Iliniangazia .

Pembeni, mke wangu alikuwa bado akikoroma, saa ya ukutani ilionyesha ni saa mbili asubuhi, nilipiga miayo ya kivivu, nikajiondoa kitandani.

ITAENDELEA.
Hold on Hold on " please ..ngoja nikapige CHAPUTA kwanza
 
SEHEMU YA 19

Daktari alishauri tuondoke na turudi kesho yake kwa kuwa uzalishaji wa mke wangu ilikuwa na mizengwe mingi.

Kauli ya daktari ilinitisha, hata hivyo nilipiga moyo konde na kuondoka kuerejea nyumbani. Usiku ule sikulala, moyo ulikuwa ukinidunda, presha ilikuwa juu.

Siku iliyofuatia. Asubuhi na mapema, niliamka nikajiandaa, kisha nikamwaga shemeji yangu Aisha, nikimtaka yeye aje Hospitalini badaye mchana, baada ya kumaliza shughuli zake asubuhi ile.

Niliendesha gari hadi Posta, kwa kuwa magari yalikuwa machache, muda mfupi badaye nilikuwa Regency. Baada ya kufika manesi walinipokea kwa sura zisizokuwa na chembe ya ukarimu wowote.

Mapigo ya moyo yakaanza kunidunda, nikanza kuhisi heunda kuna jambo baya limetokea dhidi ya mke wangu na mtoto. “Vipi hali ya mke wangu?’ nilimuuliza nesi mmoja.

“Daktari Charles Meleka amesema ukifika tu ukamwone ofisini kwake,” badala ya kujibu swali, nesi yule aliniambia kitu kingine kabisa. “Mke wangu ni mzima?” niliuliza kwa wahaka mapigo ya moyo yakinIenda kasi “Kaka hebu kuwa mwelewa,” nesi alizidi kuwa mkali.

Nikaona nisiendelee kurumbana na yule mwanamke, nilichofanya ni kwenda kwenye ofisi ya dokta Charles Meleka.

Baada ya kuingia ndani ya ofisi ile dokta Cherles alikuwa ameketi katika kiti cha kuzunguka huku mezani kwake kukiwa na mafaili kadhaa.

“Hongera Mr Faraji Hussein…” Dr Charles alianza kunipasha baada ya kuingia. “Mkeo kajifungua mtoto wa kiume tena kajifungua salama kabisa….lakini”

Dr Charles Meleka alisema. “Lakini nini?” nikauliza kwa kiherehere. “Kwanini unafanya mapenzi na mkeo kinyume na maumibile?” Dr Charles Meleka aliniuliza kwa ukali. Nikabaki nimepigwa na bumbuwazi.
lmfao " Mambo ya Zanzibar hayo'.. binti anatunza bikira ya papuchi lakini ya 0712 marinda kwishnehi mpaka uyapige pasi
 
SEHEMU YA 20

MWANZO nilidhani labda swali lake lilikuwa na maana nyingine zaidi ya vile linavyoweza kueleweka.

Lakini nilipoona uso wa daktari yule ukiwa katika hali ya kungoja jibu la swali lile nikatambua hakuwa na maana nyingine zaidi ya vilevile alivyohoji.

“Unamaana gani kusema hivyo?” “Sina maana yoyote zaidi ya kukuonya tabia ya kumwingilia mkeo kinyume na maumbile,” dokta akaniambia, tena alisema huku akiwa amenikazia macho.

Niliendelea kuchanganyikiwa. Mambo niliyokuwa naelezwa na daktari yule yalikuwa yakiniikoroga akili yangu. Kila kitu kilikuwa ni michoro isiyoeleweka.

Sikuwahi kuwa na michezo ya kishenzi kwa mke wangu, kitendo cha kutuhumiwa kumwingilia mke wangu kinyume na maumbile, ilikuwa ni fedheha mbaya sana.

“Sijawahi kufanya huo mchezo mchafu…” nilimwambia kwa ukali kidogo. “Una uhakika?” “Kabisa dokta, sijawahi kujihusisha na tabia za namna hiyo.” “Basi inawezekana kabla ya kukutana kwenu mkeo alipitia hii michezo,” dokta alinileza.

“Kujihususha na mapenzi kinyume na maumbile?” “Ndiyo,” alitikia kwa kwa upole.

Mate mepesi yakanijaa kinywani. Jambo lile lingewezekanaje wakati mimi ndiyo nilikuwa mwanaume wake wa kwanza?

Nilimkuta akiwa mwanamwali, tena bikira, mshamba kwenye ulimwengu wa mapenzi. “Lakini inawezekanaje hilo dokta? Mimi ndiyo nilikuwa mwanaume wa kwanza.

Nilimkuta akiwa mshamba kabisa kitandani.” nikauliza kwa fadhaa nikitaka ufafanuzi na uthibio juu ya alichonieleza.

“Kweli?” “Ndiyo.” niliitikia huku nikimwangalia usoni.

Alifikiria kitu kisha akasema: “Nimekuwa daktari wa wanawake huu mwaka wa 17, mwanamke anapojifungua, hutokea mara kwa mara kutokwa na haja kubwa, lakini kwa mkeo ilikuwa too much, uzoefu unaonesha mtu wa aina hii amekubuhu kwenye tabia za kuingiliwa kinyume na maumbile,” dokta alinipasha.

Nilijisikia vibaya sana, maneno ya Dk. Charles yalinisuta, yakanifanya nijione bwege. Tafsiri rahisi ni kwamba, maisha ya nyuma ya mke wangu yalikuwa na siri kubwa iliyojificha. “lakini usijali Faraji, siyo kesi sana, haya ni mambo ya kawaida tu maishani, ” daktari aliendelea kunitia moyo, kimuonekano ni kama yeye pia alibaini kwamba jambo lile lilikuwa ‘surprise’ kwangu, na alivyoona
 
Sehemu ya 21

“Ndiyo maana nilipoingia hapa manesi hawakunichangamki, kumbe kulikuwa na kasheshe wakati mke wangu anajifungua!”

“Faraji nikwambie mara ngapi hayo ni mambo madogo, hebu achana nayo na jaribu kusahau.

“Siri kubwa ya kuwa na furaha maishani ni kutokukumbuka mambo mabaya ya nyuma…”alisema, kisha akabadili mada.

“Mkeo amejifungua mtoto wa kiume,” aliniambia akifunua funua makablasha yaliyokuwa mezani.

“Kweli?” “Kwa nini nikudanganye?” “Ahsante dokta, ahsante kwa kumsaidia mke wangu.” “Karibu tena Faraji,” alisema huku akinipa mkono wa pongezi.

Alinipeleka kwenye kitanda alicholala mke wangu na mtoto

Nilipofika nilimkumbatia mke wangu na kumpa pole na pongezi ya kunizalia dume la mbegu.

“Ahsante mume wangu, hongera na wewe pia kwa kunipa mimba,” mke wangu naye alinipa pongezi zilizonifanya nijione kidume.

Wakati wote nilimwonesha uso wa tabasamu, sikupenda kabisa malumbano na mke wangu katika kipindi kile cha uzazi.

Hata Dk. Charles aliendelea kunisihi niachane kabisa na mambo yale ambayo kama ningeyaibua pengine yangepelekea ndoa yangu kuwa matatani.

Nilimuitikia na kumuhakikishia amani ya kudumu kati yangu na Nasra, mwanamke mrembo mwenye asili ya Kipemba, ambaye nilichaguliwa na wazazi wangu kama mke.

Tuliruhusiwa kurudi nyumbani, tukiwa na mtoto mzuri wa kiume, niliwataarifu ndugu na jamaa juu ya kupata mtoto, ilikuwa ni furaha kubwa.

Kwa kuwa mke wangu alikuwa akitakiwa kupata huduma za hapa na pale kama kukandwa maji na kuelekezwa mambo mengine juu ya malezi ya mtoto mchanga, ilibidi mama yangu afunge safari kutoka Nguruka aje Dar es salam kwa ajili ya kufanya kazi hiyo.

Baada ya ujio wa mama, nyumba yangu ikazidi kuwa na furaha, mama alimsadia mke wangu katika kila kitu alichohitaji.

Mtoto naye alizidi kukua, na miezi michache badaye tulimpa jina. Tukamwita Mwanda.

Siku zilikwenda, miezi ikayoyoma. Sakata la mke wangu kuingiliwa kinyume na maumbile niliendelea kuliweka kiporo.
 
SEHEMU YA 22

Kama nilivyosema awali sikupenda kuleta ukizani wowote kati yangu na mke wangu hasa katika nyakati zile.

Furaha, vicheko na tabasamu viliendelea kushamiri katika familia yangu, kwa kweli nilikuwa ni moja ya vijana wachache wanaofaidi matunda ya elimu yangu.

Wazungu wana msemo mmoja unaosema: “It is always the very good times of one’s life that normally turns into one’s very bad times in no time…”

Hii ina maana kwamba kama mtu akiwa katika maisha mabovu hakuna kibovu zaidi kitakachomkuta zaidi ya hicho, lakini akiwa kwenye maisha mazuri ndiyo ataona mabadiliko pale hali hiyo itakapotoweka.

Na kwa kawaida maisha mazuri huwa hayadumu. Wakati nasoma chuo kikuu cha Dar es Salaam msemo huu nilikuwa nauelewa sana.

Ajabu katika nyakati zile nilisahau kabisa juu ya ukweli huu. Wakati nikiwa nimesahau kabisa juu ya falsafa hii ghafla amani ndani ya nyumba yangu ikaanza kutoweka.

Mambo yalianza kama masikhara. Kukawa na mikwaruzano ya hapa na pale kati ya mke wangu na mama yangu mzazi, mama yangu alikuwa akimtuhumu mke wangu kwa tabia ya kupenda sana kuchati na simu kuliko mambo muhimu, wakati mke wangu naye alikuwa akimtuhumu mama kwa tabia ya kupenda kulalamika kwa mambo madogo madogo.

Madai yote hayo, yalipoletwa mbele yangu, niliyapuuza, kwakuwa sikuona kama yanamashiko. Sikujua kama nakosea. Na sikujua kama kwa kupuuza migogoro ile ilikuwa ni mwanzo wa kuingia kwenye historia mbaya sana maishani.

Je nini kilitoke?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom