SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,803
- 25,444
- Thread starter
- #101
SURA YA KUMI NA TATU
Baada ya dakika kadhaa, Raheem alifika hospitalini. Alishuka akaweka silaha yake nyuma ya kiuno akaifunika na koti. Akatoa simu.
“Mko wapi? ... Nakuja.”
Alisonga asichukue hata dakika tatu akawa ameshafika. Alikuta wenzake pamoja na inspekta Vitalis wakiwa wameketi kwenye mabenchi ya hospitali kama watu wangojeao taarifa na maelekezo toka kwa daktari.
“Karibu!” Mtemvu alimpokea.
“Ahsante. Vipi anaendeleaje?”
“Daktari kasema anaendela vizuri, japo kavunjika mikono na uso umeharibika vibaya mno.”
“Kilichosababisha ajali ni nini?”
“Kwa mujibu wa mashuhuda, Bwana Filbert aliacha barabara yake akaparamia upande wa pili.”
“… Ila mimi siamini hilo.” Pius alidakia. “Yani aache barabara yake afuate barabara ya upande wa pili! Kutakuwa kuna jambo tu.”
Raheem akatikisa kichwa chake kwa masikitiko.
“Na hicho ndo’ kinakutesa. Filbert amepata ajali sababu ya stress zake. Anyway, mwambie huyo mtu wenu anayewatisha tisha aache kunifuatilia. Nitampoteza katika huu uso wa dunia!”
K square, Mtemvu na Pius wakatizamana kwa kuduwaa.
“Naondoka, nitakuja baadae nikipata muda. Kwa sasa sipo vizuri. Mtanifikishia pole zangu kwa huyo majeruhi wa kujitakia.”
Aliaga hivyo akanyanyua mguu wake kuondoka. Alifika kwenye uwanja wa kutunzia magari lakini hakuona gari lake popote. Alitizama huku na huko pasipo kuona kitu. Akibung’aa hapo, akamuona bwana Pius akishuka. Haraka akamkimbilia.
“Unaenda wapi?”
“Kwangu, si unajua nina msiba.” Alisema Pius akitembea kana kwamba hana muda wa kupoteza.
“Mbona hujaondoka. Kuna mtu unamngoja?”
“Hapana. sioni gari langu!”
“Uliliweka wapi?”
“Pale! Nyuma ya ile Escudo nyekundu!”
“Una uhakika?”
“Asilimia zote! Lilikuwa pale kabisa!”
Waliongozana kumfuata mlinzi getini kumuuliza, mlinzi akasema hajaona gari la aina hiyo likipita getini isipokuwa tu kwenye kuingia kwake.
Raheem alichanganyikiwa. Pius alimshika bega akamwambia:
“Nadhani na wewe utakuwa mepata matatizo ya kisaikolojia.”
Akatabasamu kwa mbali.
“Nenda kalitafute vema.”
Pius alisema akiondoka zake.
Kwa mara ya kwanza Raheem alianza kuhisi wanayoyaongea wenzake yanaweza yakawa na chembe za ukweli ndani yake. Kuna mauzauza. Kuna mtu anawatafuta. Kuna mtu anawadai roho zao.
***
Muendelezo soma hapa
Baada ya dakika kadhaa, Raheem alifika hospitalini. Alishuka akaweka silaha yake nyuma ya kiuno akaifunika na koti. Akatoa simu.
“Mko wapi? ... Nakuja.”
Alisonga asichukue hata dakika tatu akawa ameshafika. Alikuta wenzake pamoja na inspekta Vitalis wakiwa wameketi kwenye mabenchi ya hospitali kama watu wangojeao taarifa na maelekezo toka kwa daktari.
“Karibu!” Mtemvu alimpokea.
“Ahsante. Vipi anaendeleaje?”
“Daktari kasema anaendela vizuri, japo kavunjika mikono na uso umeharibika vibaya mno.”
“Kilichosababisha ajali ni nini?”
“Kwa mujibu wa mashuhuda, Bwana Filbert aliacha barabara yake akaparamia upande wa pili.”
“… Ila mimi siamini hilo.” Pius alidakia. “Yani aache barabara yake afuate barabara ya upande wa pili! Kutakuwa kuna jambo tu.”
Raheem akatikisa kichwa chake kwa masikitiko.
“Na hicho ndo’ kinakutesa. Filbert amepata ajali sababu ya stress zake. Anyway, mwambie huyo mtu wenu anayewatisha tisha aache kunifuatilia. Nitampoteza katika huu uso wa dunia!”
K square, Mtemvu na Pius wakatizamana kwa kuduwaa.
“Naondoka, nitakuja baadae nikipata muda. Kwa sasa sipo vizuri. Mtanifikishia pole zangu kwa huyo majeruhi wa kujitakia.”
Aliaga hivyo akanyanyua mguu wake kuondoka. Alifika kwenye uwanja wa kutunzia magari lakini hakuona gari lake popote. Alitizama huku na huko pasipo kuona kitu. Akibung’aa hapo, akamuona bwana Pius akishuka. Haraka akamkimbilia.
“Unaenda wapi?”
“Kwangu, si unajua nina msiba.” Alisema Pius akitembea kana kwamba hana muda wa kupoteza.
“Mbona hujaondoka. Kuna mtu unamngoja?”
“Hapana. sioni gari langu!”
“Uliliweka wapi?”
“Pale! Nyuma ya ile Escudo nyekundu!”
“Una uhakika?”
“Asilimia zote! Lilikuwa pale kabisa!”
Waliongozana kumfuata mlinzi getini kumuuliza, mlinzi akasema hajaona gari la aina hiyo likipita getini isipokuwa tu kwenye kuingia kwake.
Raheem alichanganyikiwa. Pius alimshika bega akamwambia:
“Nadhani na wewe utakuwa mepata matatizo ya kisaikolojia.”
Akatabasamu kwa mbali.
“Nenda kalitafute vema.”
Pius alisema akiondoka zake.
Kwa mara ya kwanza Raheem alianza kuhisi wanayoyaongea wenzake yanaweza yakawa na chembe za ukweli ndani yake. Kuna mauzauza. Kuna mtu anawatafuta. Kuna mtu anawadai roho zao.
***
Muendelezo soma hapa