SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,803
- 25,444
- Thread starter
- #61
SURA YA NANE
Baada ya hodi fupi wakati huu ambao ulikuwa unaelekea mchana, Mama Beatrice alimuita mfanyakazi wake mpya wa ndani, Rema, na kumuamuru akafungue geti.
Mwanaume mrefu mwenye mwili uliojaza misuli barabara akiwa kavalia suti nadhifu na tai akaingia ndani ya uzio wa nyumba ya Mtemvu. Mwendo wake ulikuwa mkakamavu akijiamini. Uso wake ulikuwa mrefu na wenye ndevu zilizochongwa vyema.
Macho yake yalikuwa tulivu na taratibu yalikuwa yanapekuwa mazingira aliyokuwepo. Kwa jina afahamika kama Vitalis – Vitalis Byabata. Inspekta wa polisi aliyerudishwa nyumbani baada ya kutumika kama ajenti wa polisi wa kimataifa ‘interpol’ kwa takribani miaka kumi na tano akiwa mwanaume aliyechangia vyema harakati za kudidimiza na kutokomeza ugaidi duniani.
Mwanaume aliyetia mkono wake kwenye mauaji ya viongozi wa kigaidi wa Al-Qaeda: Anwar Al Awlaki, Saleh al-Somali na Abu Ayyub al-Masri pamoja na wale wa kundi la kigaidi la Taliban Abdul Ghani Beradar na Baitullah Mahsud.
Pamoja na mchango wake wote huo, si dunia wala watanzania waliokuwa wanamjua kwa mapana na marefu. Ukiachana na usalama wa taifa, jeshi la polisi na Interpol hakuna mtu mwingine yeyote aliyekuwa anafahamu nondo za ngumi zake, akili yake pevu kwenye ugunduzi wa hatari na wepesi wake kwenye kufanya maamuzi yaliyokuwa yanawaacha hoi maadui zake ndani ya muda mfupi. Wenzake huko Interpol walikuwa wamembatiza jina la ‘the black angel’.
“Karibu sana, inspekta Vitalis.” Mama Beatrice alisema kwa tabasamu akisimama.
“Ahsante sana, mama. Habari ya saa hizi?” Vitalis aliuliza wakibadilishana mikono.
“Njema. Ni kitambo sana sijakuona, wanasemaje huko ulaya?”
“Hawana usemi. Sijui nyie huku nyumbani?”
“Mmh, ni majaribu tu huku kwakweli. Nimefurahi sana kukuona. Nimeanza kupata ahueni mapema.”
“Mkuu, amenieleza yanayowakumba. Tutasaidiana kutatua tatizo, naamini.”
Inspekta Vitalis aliketi kwenye kochi lililokuwa limekaa hapo nje pamoja na Mama Beatrice, baada ya muda mfupi bwana Mtemvu akatoka ndani akiwa amevalia vema na briefcase mkononi. Inspekta Vitalis alisimama akampatia salamu ya kijeshi Mtemvu alafu wakaongozana mpaka kwenye gari na kuondoka, inspekta Vitalis akikamatia usukani.
“Hapa unavyoona, nikitoka tu mke wangu naye anapanda gari lake kwenda kwa dada yake, anaogopa sana kukaa nyumbani. Inabidi uwe makini sana, Vitalis. Huyo mtu mtu anayenifuatilia si wa kawaida. Ni hatari mno. Mauaji yake ni ya kutisha na hayabakizi dalili zozote za mapigano wala purukushani.”
Mtemvu alisema kisha akatengenezea miwani yake ya macho.
“Usihofu mkuu. Nitajitahidi kwa nguvu na akili yangu yote kukuhakikishia usalama.”
Wakati gari lajongea na mwendokasi wake wa kawaida, haikuchukua muda mrefu Vitalis kugundua kuna gari lawafuata kwa nyuma. Alitizama vioo vya ubavu wa gari akalisoma gari hilo kwa makini lakini jitihada zake za kung’amua sura ya dereva ziligonga mwamba.
Aliongeza mwendokasi akijaribu kuyavuka magari yaliyokuwa mbele yake, baada ya muda alilipoteza gari lililokuwa linamfuatilia. Hakuliona tena kwenye vioo mpaka wanafika ofisini.
Inspekta Vitalis hakumwambia mkuu wake alichokiona, alimfungulia mlango wa gari akaongozana naye mpaka mlangoni mwa ofisi. Waliingia ndani ya ofisi wakakuta vitu shaghalabaghala. Makaratasi yalikuwa yametupwa na kuchanwa chanwa. Hakuna kitu kilichokuwepo kwenye hali yake ya kawaida – ofisi ilikuwa mithili ya eneo lililopigwa bomu. Jambo hilo likamshangaza Mtemvu pamoja na inspekta Vitalis.
“Mkuu, uliacha ofisi hivi?”
“Hapana! Nashangaa.”
“Ngoja basi kidogo papo hapo.”
Inspekta Vitalis alipekua ofisi na macho yake yaliyotembea kila eneo. Aligundua dirisha la ofisi ilikuwa wazi, alilisogelea akatizama mazingira ya hapo kabla hajatoa shingo yake nje na kutizama kama kuna kiashiria chochote cha mvamizi.
Hakuona kitu.
Aliendelea kupekua asipate kitu cha kumsaidia kwenye upelelezi. Mwishowe akamtaka mkuu wake ajaribu kuwaita na kuwauliza watu waliokuwepo doria ya ulinzi siku hiyo, ama watumie mrejesho wa kamera za cctv kama watapata jambo.
Kabla halijaamuliwa la kufanywa, simu ya Mtemvu iliita. Alikuwa ni bwana Pius akimtaarifu mwenzake yaliyojiri usiku wa kuamkia hiyo siku. Mtemvu alipopata hizo taarifa za Pius alishangazwa mno na kuzidi kuogopa. Hakukaa tena ofisini, aliongozana na inspekta Vitalis waende nyumbani kwa rafiki yake: Pius upesi.
Walijiweka kwenye gari chombo kikaondoka kwa mwendo wa wastani. Wasichukue hata muda mrefu barabarani, vioo vya kando vya gari vikamuonyesha inspekta Vitalis kwamba kuna gari linawafuata. Tena gari lile lile lililokuwa linawafuatilia mwanzoni!
Inspekta Vitalis alilitizama gari hilo kwa makini taratibu akikanyagia mafuta. Baada ya muda gari hilo lilipotea. Halikuonekana wapi limeelekea. Inspekta Vitalis aliwaza na kuwazua ila mwishowe akajaribu kupuuzia na kuendelea na safari. Usipite muda mwingi, inspekta Vitalis aliliona lile gari lililopotea kwa mbele.
Hapo moyo ukampasuka kwa hayo mazingaombwe. Aliongeza mwendokasi wa gari kulikaribia lile gari alilolitilia mashaka ili apate kumuona dereva. Lakini walipokata tu kona, lile gari halikuonekana tena. Lilitokomea kwa mara nyingine mbele ya macho ya inspekta Vitalis!
Inspekta alishusha pumzi ndefu akikaza macho ya mashaka. Kama alihesabu muda basi ilichukua dakika mbili tu, gari lililotokomea likaonekana tena mbele ya macho yake. Sasa lilikuwa nyuma yao kwa mujibu wa vioo vya pembeni. Na tena likiwa linakuja kwa kasi kuwafuata kama vile linadhamiria kuwagonga!
“Mkuu funga mkanda!” Inspekta Vitalis alipayuka akiliondoa gari kwa kasi kubwa. Alikwepa magari yaliyo mbele yao kwa pupa na kusababisha tafrani barabarani. Honi nyingi ziliita. Na magari mengine yaligongana yakijitahidi kumkwepa. Muda mchache baadae, inspekta Vitalis akiwa katika kasi yake kubwa, alitizama kwenye vioo asione tena lile gari.
Bwana Mtemvu aliyekuwa anahema kwa nguvu uso wake ukivuja jasho, alitizama nyuma kama ataona kitu. Akauliza:
“Inspekta kuna nini?”
Inspekta Vitalis akashusha pumzi.
“Mkuu, kuna mtu alikuwa anatufuatilia.” Mtemvu akageuka tena na kutizama nyuma.
“Nani?”
“Sijui! Kuna gari lilikuwa linatufuatilia tokea tumetoka nyumbani.”
“Umefanikiwa kumuona dereva?”
“Hapana! Nimejitahidi kutizama lakini sijaona mtu.”
“Na plate number?”
“Haikuwa na plate number, mkuu.”
Mtemvu alitikisa kichwa chake akakiegemeza kwenye kioo cha dirisha la gari. Uso wake ulizama kwenye dimbwi la mawazo. Nani anamfuatilia na anataka nini kwake? Hakupata jibu kabisa. Kuna muda alifikiri yupo kwenye ndoto ya kutisha na anatamani aamke lakini haikuwa hivyo.
Kunyamaza kwake kulisababisha ukimya ushike gari na hakuna mtu aliyefungua kinywa mpaka wanaingia kwenye kiwanja cha bwana Pius walipokuta watu kadhaa tayari wameshawasili wameketi chini ya maturubai.
***
Muendelezo soma hapa
Baada ya hodi fupi wakati huu ambao ulikuwa unaelekea mchana, Mama Beatrice alimuita mfanyakazi wake mpya wa ndani, Rema, na kumuamuru akafungue geti.
Mwanaume mrefu mwenye mwili uliojaza misuli barabara akiwa kavalia suti nadhifu na tai akaingia ndani ya uzio wa nyumba ya Mtemvu. Mwendo wake ulikuwa mkakamavu akijiamini. Uso wake ulikuwa mrefu na wenye ndevu zilizochongwa vyema.
Macho yake yalikuwa tulivu na taratibu yalikuwa yanapekuwa mazingira aliyokuwepo. Kwa jina afahamika kama Vitalis – Vitalis Byabata. Inspekta wa polisi aliyerudishwa nyumbani baada ya kutumika kama ajenti wa polisi wa kimataifa ‘interpol’ kwa takribani miaka kumi na tano akiwa mwanaume aliyechangia vyema harakati za kudidimiza na kutokomeza ugaidi duniani.
Mwanaume aliyetia mkono wake kwenye mauaji ya viongozi wa kigaidi wa Al-Qaeda: Anwar Al Awlaki, Saleh al-Somali na Abu Ayyub al-Masri pamoja na wale wa kundi la kigaidi la Taliban Abdul Ghani Beradar na Baitullah Mahsud.
Pamoja na mchango wake wote huo, si dunia wala watanzania waliokuwa wanamjua kwa mapana na marefu. Ukiachana na usalama wa taifa, jeshi la polisi na Interpol hakuna mtu mwingine yeyote aliyekuwa anafahamu nondo za ngumi zake, akili yake pevu kwenye ugunduzi wa hatari na wepesi wake kwenye kufanya maamuzi yaliyokuwa yanawaacha hoi maadui zake ndani ya muda mfupi. Wenzake huko Interpol walikuwa wamembatiza jina la ‘the black angel’.
“Karibu sana, inspekta Vitalis.” Mama Beatrice alisema kwa tabasamu akisimama.
“Ahsante sana, mama. Habari ya saa hizi?” Vitalis aliuliza wakibadilishana mikono.
“Njema. Ni kitambo sana sijakuona, wanasemaje huko ulaya?”
“Hawana usemi. Sijui nyie huku nyumbani?”
“Mmh, ni majaribu tu huku kwakweli. Nimefurahi sana kukuona. Nimeanza kupata ahueni mapema.”
“Mkuu, amenieleza yanayowakumba. Tutasaidiana kutatua tatizo, naamini.”
Inspekta Vitalis aliketi kwenye kochi lililokuwa limekaa hapo nje pamoja na Mama Beatrice, baada ya muda mfupi bwana Mtemvu akatoka ndani akiwa amevalia vema na briefcase mkononi. Inspekta Vitalis alisimama akampatia salamu ya kijeshi Mtemvu alafu wakaongozana mpaka kwenye gari na kuondoka, inspekta Vitalis akikamatia usukani.
“Hapa unavyoona, nikitoka tu mke wangu naye anapanda gari lake kwenda kwa dada yake, anaogopa sana kukaa nyumbani. Inabidi uwe makini sana, Vitalis. Huyo mtu mtu anayenifuatilia si wa kawaida. Ni hatari mno. Mauaji yake ni ya kutisha na hayabakizi dalili zozote za mapigano wala purukushani.”
Mtemvu alisema kisha akatengenezea miwani yake ya macho.
“Usihofu mkuu. Nitajitahidi kwa nguvu na akili yangu yote kukuhakikishia usalama.”
Wakati gari lajongea na mwendokasi wake wa kawaida, haikuchukua muda mrefu Vitalis kugundua kuna gari lawafuata kwa nyuma. Alitizama vioo vya ubavu wa gari akalisoma gari hilo kwa makini lakini jitihada zake za kung’amua sura ya dereva ziligonga mwamba.
Aliongeza mwendokasi akijaribu kuyavuka magari yaliyokuwa mbele yake, baada ya muda alilipoteza gari lililokuwa linamfuatilia. Hakuliona tena kwenye vioo mpaka wanafika ofisini.
Inspekta Vitalis hakumwambia mkuu wake alichokiona, alimfungulia mlango wa gari akaongozana naye mpaka mlangoni mwa ofisi. Waliingia ndani ya ofisi wakakuta vitu shaghalabaghala. Makaratasi yalikuwa yametupwa na kuchanwa chanwa. Hakuna kitu kilichokuwepo kwenye hali yake ya kawaida – ofisi ilikuwa mithili ya eneo lililopigwa bomu. Jambo hilo likamshangaza Mtemvu pamoja na inspekta Vitalis.
“Mkuu, uliacha ofisi hivi?”
“Hapana! Nashangaa.”
“Ngoja basi kidogo papo hapo.”
Inspekta Vitalis alipekua ofisi na macho yake yaliyotembea kila eneo. Aligundua dirisha la ofisi ilikuwa wazi, alilisogelea akatizama mazingira ya hapo kabla hajatoa shingo yake nje na kutizama kama kuna kiashiria chochote cha mvamizi.
Hakuona kitu.
Aliendelea kupekua asipate kitu cha kumsaidia kwenye upelelezi. Mwishowe akamtaka mkuu wake ajaribu kuwaita na kuwauliza watu waliokuwepo doria ya ulinzi siku hiyo, ama watumie mrejesho wa kamera za cctv kama watapata jambo.
Kabla halijaamuliwa la kufanywa, simu ya Mtemvu iliita. Alikuwa ni bwana Pius akimtaarifu mwenzake yaliyojiri usiku wa kuamkia hiyo siku. Mtemvu alipopata hizo taarifa za Pius alishangazwa mno na kuzidi kuogopa. Hakukaa tena ofisini, aliongozana na inspekta Vitalis waende nyumbani kwa rafiki yake: Pius upesi.
Walijiweka kwenye gari chombo kikaondoka kwa mwendo wa wastani. Wasichukue hata muda mrefu barabarani, vioo vya kando vya gari vikamuonyesha inspekta Vitalis kwamba kuna gari linawafuata. Tena gari lile lile lililokuwa linawafuatilia mwanzoni!
Inspekta Vitalis alilitizama gari hilo kwa makini taratibu akikanyagia mafuta. Baada ya muda gari hilo lilipotea. Halikuonekana wapi limeelekea. Inspekta Vitalis aliwaza na kuwazua ila mwishowe akajaribu kupuuzia na kuendelea na safari. Usipite muda mwingi, inspekta Vitalis aliliona lile gari lililopotea kwa mbele.
Hapo moyo ukampasuka kwa hayo mazingaombwe. Aliongeza mwendokasi wa gari kulikaribia lile gari alilolitilia mashaka ili apate kumuona dereva. Lakini walipokata tu kona, lile gari halikuonekana tena. Lilitokomea kwa mara nyingine mbele ya macho ya inspekta Vitalis!
Inspekta alishusha pumzi ndefu akikaza macho ya mashaka. Kama alihesabu muda basi ilichukua dakika mbili tu, gari lililotokomea likaonekana tena mbele ya macho yake. Sasa lilikuwa nyuma yao kwa mujibu wa vioo vya pembeni. Na tena likiwa linakuja kwa kasi kuwafuata kama vile linadhamiria kuwagonga!
“Mkuu funga mkanda!” Inspekta Vitalis alipayuka akiliondoa gari kwa kasi kubwa. Alikwepa magari yaliyo mbele yao kwa pupa na kusababisha tafrani barabarani. Honi nyingi ziliita. Na magari mengine yaligongana yakijitahidi kumkwepa. Muda mchache baadae, inspekta Vitalis akiwa katika kasi yake kubwa, alitizama kwenye vioo asione tena lile gari.
Bwana Mtemvu aliyekuwa anahema kwa nguvu uso wake ukivuja jasho, alitizama nyuma kama ataona kitu. Akauliza:
“Inspekta kuna nini?”
Inspekta Vitalis akashusha pumzi.
“Mkuu, kuna mtu alikuwa anatufuatilia.” Mtemvu akageuka tena na kutizama nyuma.
“Nani?”
“Sijui! Kuna gari lilikuwa linatufuatilia tokea tumetoka nyumbani.”
“Umefanikiwa kumuona dereva?”
“Hapana! Nimejitahidi kutizama lakini sijaona mtu.”
“Na plate number?”
“Haikuwa na plate number, mkuu.”
Mtemvu alitikisa kichwa chake akakiegemeza kwenye kioo cha dirisha la gari. Uso wake ulizama kwenye dimbwi la mawazo. Nani anamfuatilia na anataka nini kwake? Hakupata jibu kabisa. Kuna muda alifikiri yupo kwenye ndoto ya kutisha na anatamani aamke lakini haikuwa hivyo.
Kunyamaza kwake kulisababisha ukimya ushike gari na hakuna mtu aliyefungua kinywa mpaka wanaingia kwenye kiwanja cha bwana Pius walipokuta watu kadhaa tayari wameshawasili wameketi chini ya maturubai.
***
Muendelezo soma hapa
