SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,803
- 25,444
- Thread starter
- #41
* SURA YA SITA *
Upepo mwanana wa bahari na kinywaji laini kilichokuwa kinakanda koo lake kavu, vilimbembeleza akasinzia kwenye kiti. Baada tu ya muda mfupi akili yake ilianza kumrejeshea yale yaliyopita.
Miezi kadhaa tu nyuma akiwa kwenye kikao cha siri pamoja na wenzake wanne: Bwana Pius Mbwambo, Raheem Victor, Filbert Waziri na Katende Katende, almaarufu kama K square.
“Mzigo umeshafika Rome, sasa tunafanyeje?” Sauti nyepesi ya bwana Katende iliuliza jopo. “Inabidi mmoja aende huko.” Mtemvu akashauri na kuongezea, “Mimi nimeshamaliza kazi yangu ya kuhakikisha usalama, tumteue mmoja akasimamie zoezi hilo.”
Bwana Pius akagonga meza.
“Nani akubali kwenda huko?” Aliuliza akitoa macho. “Kusema ukweli mimi sipo tayari! Hili jambo ni hatari sana!”
Raheem akatabasamu. “Sasa mnadhani ni nani atakayeamua kujitoa sadaka?” Alidhihaki. “K square upo tayari? ... Filbert upo tayari? ... Pius upo tayari? ... Mtemvu je? ... Si unaona? Hakuna anayekubali.
Tulifanya ujinga sana kuanza kufanya hii kazi kabla ya kupanga nani atakayesimamia hilo swala kwa uaminifu mkubwa. Unaona sasa inavyotugharimu? Tumepewa taarifa mzigo umewasili, then what is next? Tutawaachia wale wazungu?”
Kimya kikatwaa umati kwa dakika kadhaa kabla ya bwana Filbert Waziri kutia neno: “Kwani hatumuamini Amerigo? Tumuache asimamie tu!”
“Hapana!” Mtemvu akapayuka. “Unadhani hii ni biashara ya nyanya? ... What if akatudhulumu? Unaenda kushtakia wapi? Unampatia wapi? Hatujafikia kiasi cha kumuamini kina hiko.” Mtemvu alitema cheche, bwana Pius na wengineo wakamuunga mkono.
“Ni kweli!” Alisema K square. “Hatuwezi kumuamini kirahisi rahisi hivyo, haswa kwenye biashara kama hii. Tunamuhitaji mtu mwingine mbali na sisi kwasababu ya usalama. Mtu tutakayemuamini, mtu ambaye tunajua anatokea wapi na tutampatia wapi akileta ushenzi. Au nyie mnaonaje?”
“Ila tutampatia wapi huyo mtu wa kumuamini kiasi hiko?” Filbert Waziri aliuliza. Baada ya mafikirio kidogo, Mtemvu alipendekeza:
“Bwana Malale!”
Wenzake wakamtizama na macho yaliyotaka kufahamu zaidi.
Bwana Malale … Bwana Malale … Bwana Malale … Sauti ya kunong’oneza ilisikika ikififia masikioni mwa Mtemvu. Alikurupuka toka usingizini. Alitizama pande zake zote nne kisha kashusha pumzi ndefu akitikisa kichwa chake kwa masikitiko. Alichoropoa simu yake mfukoni akapiga.
“Haloo! Yes Pius, unaweza ukaja Palace hotel mara moja? Ni muhimu sana.” Alipokata simu akamuita pia Katende na Filbert pamoja na Raheem ambaye yeye alitoa udhuru. Baada ya dakika chache tu, wakawa tayari wamewasili kuitikia wito.
“Niambie Pius! Vipi huko mbugani wanyama wanasemaje?”
“Aaah safi tu!” Alijibu Pius kisha haraka akaeleza hofu yake: “Vipi, mbona ghafula? Kuna chochote au una dili jipya?”
Muhudumu alikuja akawahudumia. Mvinyo na nyama choma ziliteka meza na kufanya iwe ndogo kuliko uhalisia. Ilikuwa ni Pius, Filbert na K square tu ndio waliokuwa wanakula, Mtemvu alitumia maji pekee baada ya kumaliza glasi yake ya sharubati.
“Samahani sana kwa kuwaharakisha na wito wangu wa ghafula. Nina tatizo linanikabili. Can you imagine ndani ya usiku mmoja wamekufa watu watatu nyumbani kwangu katika mazingira ya kutatanisha?”
Swali hilo likateka nyuso za wenzake walioguswa kwa namna moja ama nyingine. Waliacha kula wakamtizama Mtemvu.
“Bro, are you serious?” Filbert aliuliza. Mtemvu aliminya mdomo wake alafu akanena kuonyesha ametingwa.
“Ndani ya usiku mmoja.” Mtemvu alianza kufafanua, “Dereva wangu amekufa na wafanyakazi wawili wa ndani. Vifo vyao mpaka sasa hivi sielewi nini kimesababisha. Nimewakuta wakiwa wanamwaga tu madamu huku anayetenda hayo asionekane kabisa! Sielewi kuna nini! Mbali na hapo nimekuwa nikiona mauzauza! Nahisi kuna mtu ananifuatilia! Si bure kanisa!”
Kabla ya kutia neno Filbert Waziri alitazamana na wenzake kwa bumbuwazi kisha akaguna akimtizama Mtemvu.
“Mtemvu, are you serious or unatutania? Mbona leo sio sikukuu ya wajinga brother?” Mtemvu akatizama chini akikuna kiwaraza chake. Alikunywa kwanza fundo moja la maji ndipo akaendeleza soga yake ya kutisha.
“Sio kwamba nawatania ndugu zangu. Nawaeleza ukweli, ukweli ulio uchi kabisa! Hamjapata kusikia lolote juu ya hayo kwasababu tu ya cheo changu huko usalama, la sivyo sijui!” Akaweka kituo anywe maji.
“Ila kama nilivyowaeleza, dereva wangu: Mustafa, pamoja na wafanyakazi wangu wa ndani wameuwawa. Simjui muuaji ni nani na sijui anataka nini. Sijui ametumwa na nani?”
Zaidi tu ya kushtukiza, kila mtu akatandwa na hofu. Chakula hakikulika tena wala vinywaji havikugusa koo. Nyuso zenye taharuki na ukakasi wa mawazo zilitungwa wakiwa wanajaribu kufumbua fumbo lililoonekana ni gumu sana kung’amuliwa. Kabla lisaa halijamegeka, daktari wa Mtemvu alifika hotelini.
“Bwana Mtemvu, wakati unanipigia ndio nilikuwa namalizia ile shughuli. Kusema ukweli nimeshangazwa na hivyo vifo vingine. Kwa mujibu wa chunguzi, Mustafa amekufa kutokana na kupasuka kwa mishipa ndani ya mwili wake hivyo kupelekea damu kuvujilia ndani kwa ndani mpaka kifo.
Na kuhusu wafanyakazi wako wa ndani, vifo vyao ni vya kufananana – kutobolewa na kitu kirefu chenye ncha kali shingoni mwao. Lakini ajabu sijaona michubuko wala chochote kuashiria kama walipitia purukushani zozote kabla ya vifo vyao. Inaonyesha muuaji ni mtu mwenye utaalamu wa hali ya juu. Bado sijajua alitumia mbinu gani!”
“Si unaona!” Mtemvu alishadadia. “Niliwaambia mimi, kuna tatizo jamani!”
“Sasa tunafanyaje?” Filbert akauliza kwa hofu. Macho yalikuwa yamemtoka ndita za woga zikijichora kwenye paji la uso. Hakuna kingine walichokiamua zaidi ya kuimarisha ulinzi maradufu, wawe macho zaidi na lolote litakalotokea wajulishane.
Kikao kilifungwa wakatawanyika. Mtemvu alielekea kuichukua miili ya marehemu na hatua za mazishi zikafanyika zikichukua siku mbili tu baada ya miili ya marehemu kurudishwa kwenye makazi yao huko vijijini. Habari hazikusambaa hata kidogo. Hakuna aliyejua nini kilijiri ndani ya uzio wa nyumba ya bwana Mtemvu isipokuwa daktari, marafikize na polisi.
Kwa siri alipeleka miili hiyo huko vijijini akitoa pesa taslimu kufanikisha na kumaliza zoezi. Siku ya tatu aligeuka kurudi nyumbani kwake. Kwakuwa Mama Beatrice alikuwa bado yupo nyumbani kwa dada yake ilimlazimu siku hiyo akae peke yake nyumba nzima, hakuwa na jinsi.
Alipiga moyo konde akijiaminisha ya kuwa yeye ni mwanaume na yupo radhi kupambana na adui yake. Mkononi akiwa ameshikilia bunduki yake ndogo alijipumzisha kwenye kochi atizame televisheni.
Kwakuwa alikuwa amechoka mno na purukushani za msiba na hakupata muda wa kupumzika huko vijijini, usingizi haukupata vizingiti kumtwaa haraka; macho yalifumba mdomo ukaachama akilegea na kuacha bunduki yake ikae mbali. Muda mfupi tu baada kuanza kukoroma, akapata mgeni.
Hakuwa mgeni wa kawaida! Kilikuwa ni kivuli kilichopita kwenye mwanya wa mlango kisha kikajisogeza mbele kabisa ya Mtemvu na kusimama papo. Baada ya muda si mwingi, Mtemvu alijikuta akiwa amelala bafuni. Hakuwa na nguo yoyote, na kwenye kioo cha bafu aliachiwa ujumbe uliosomeka:
‘Mpaka pale wasaa utakapowadia’
*****
Muendelezo soma hapa
Upepo mwanana wa bahari na kinywaji laini kilichokuwa kinakanda koo lake kavu, vilimbembeleza akasinzia kwenye kiti. Baada tu ya muda mfupi akili yake ilianza kumrejeshea yale yaliyopita.
Miezi kadhaa tu nyuma akiwa kwenye kikao cha siri pamoja na wenzake wanne: Bwana Pius Mbwambo, Raheem Victor, Filbert Waziri na Katende Katende, almaarufu kama K square.
“Mzigo umeshafika Rome, sasa tunafanyeje?” Sauti nyepesi ya bwana Katende iliuliza jopo. “Inabidi mmoja aende huko.” Mtemvu akashauri na kuongezea, “Mimi nimeshamaliza kazi yangu ya kuhakikisha usalama, tumteue mmoja akasimamie zoezi hilo.”
Bwana Pius akagonga meza.
“Nani akubali kwenda huko?” Aliuliza akitoa macho. “Kusema ukweli mimi sipo tayari! Hili jambo ni hatari sana!”
Raheem akatabasamu. “Sasa mnadhani ni nani atakayeamua kujitoa sadaka?” Alidhihaki. “K square upo tayari? ... Filbert upo tayari? ... Pius upo tayari? ... Mtemvu je? ... Si unaona? Hakuna anayekubali.
Tulifanya ujinga sana kuanza kufanya hii kazi kabla ya kupanga nani atakayesimamia hilo swala kwa uaminifu mkubwa. Unaona sasa inavyotugharimu? Tumepewa taarifa mzigo umewasili, then what is next? Tutawaachia wale wazungu?”
Kimya kikatwaa umati kwa dakika kadhaa kabla ya bwana Filbert Waziri kutia neno: “Kwani hatumuamini Amerigo? Tumuache asimamie tu!”
“Hapana!” Mtemvu akapayuka. “Unadhani hii ni biashara ya nyanya? ... What if akatudhulumu? Unaenda kushtakia wapi? Unampatia wapi? Hatujafikia kiasi cha kumuamini kina hiko.” Mtemvu alitema cheche, bwana Pius na wengineo wakamuunga mkono.
“Ni kweli!” Alisema K square. “Hatuwezi kumuamini kirahisi rahisi hivyo, haswa kwenye biashara kama hii. Tunamuhitaji mtu mwingine mbali na sisi kwasababu ya usalama. Mtu tutakayemuamini, mtu ambaye tunajua anatokea wapi na tutampatia wapi akileta ushenzi. Au nyie mnaonaje?”
“Ila tutampatia wapi huyo mtu wa kumuamini kiasi hiko?” Filbert Waziri aliuliza. Baada ya mafikirio kidogo, Mtemvu alipendekeza:
“Bwana Malale!”
Wenzake wakamtizama na macho yaliyotaka kufahamu zaidi.
Bwana Malale … Bwana Malale … Bwana Malale … Sauti ya kunong’oneza ilisikika ikififia masikioni mwa Mtemvu. Alikurupuka toka usingizini. Alitizama pande zake zote nne kisha kashusha pumzi ndefu akitikisa kichwa chake kwa masikitiko. Alichoropoa simu yake mfukoni akapiga.
“Haloo! Yes Pius, unaweza ukaja Palace hotel mara moja? Ni muhimu sana.” Alipokata simu akamuita pia Katende na Filbert pamoja na Raheem ambaye yeye alitoa udhuru. Baada ya dakika chache tu, wakawa tayari wamewasili kuitikia wito.
“Niambie Pius! Vipi huko mbugani wanyama wanasemaje?”
“Aaah safi tu!” Alijibu Pius kisha haraka akaeleza hofu yake: “Vipi, mbona ghafula? Kuna chochote au una dili jipya?”
Muhudumu alikuja akawahudumia. Mvinyo na nyama choma ziliteka meza na kufanya iwe ndogo kuliko uhalisia. Ilikuwa ni Pius, Filbert na K square tu ndio waliokuwa wanakula, Mtemvu alitumia maji pekee baada ya kumaliza glasi yake ya sharubati.
“Samahani sana kwa kuwaharakisha na wito wangu wa ghafula. Nina tatizo linanikabili. Can you imagine ndani ya usiku mmoja wamekufa watu watatu nyumbani kwangu katika mazingira ya kutatanisha?”
Swali hilo likateka nyuso za wenzake walioguswa kwa namna moja ama nyingine. Waliacha kula wakamtizama Mtemvu.
“Bro, are you serious?” Filbert aliuliza. Mtemvu aliminya mdomo wake alafu akanena kuonyesha ametingwa.
“Ndani ya usiku mmoja.” Mtemvu alianza kufafanua, “Dereva wangu amekufa na wafanyakazi wawili wa ndani. Vifo vyao mpaka sasa hivi sielewi nini kimesababisha. Nimewakuta wakiwa wanamwaga tu madamu huku anayetenda hayo asionekane kabisa! Sielewi kuna nini! Mbali na hapo nimekuwa nikiona mauzauza! Nahisi kuna mtu ananifuatilia! Si bure kanisa!”
Kabla ya kutia neno Filbert Waziri alitazamana na wenzake kwa bumbuwazi kisha akaguna akimtizama Mtemvu.
“Mtemvu, are you serious or unatutania? Mbona leo sio sikukuu ya wajinga brother?” Mtemvu akatizama chini akikuna kiwaraza chake. Alikunywa kwanza fundo moja la maji ndipo akaendeleza soga yake ya kutisha.
“Sio kwamba nawatania ndugu zangu. Nawaeleza ukweli, ukweli ulio uchi kabisa! Hamjapata kusikia lolote juu ya hayo kwasababu tu ya cheo changu huko usalama, la sivyo sijui!” Akaweka kituo anywe maji.
“Ila kama nilivyowaeleza, dereva wangu: Mustafa, pamoja na wafanyakazi wangu wa ndani wameuwawa. Simjui muuaji ni nani na sijui anataka nini. Sijui ametumwa na nani?”
Zaidi tu ya kushtukiza, kila mtu akatandwa na hofu. Chakula hakikulika tena wala vinywaji havikugusa koo. Nyuso zenye taharuki na ukakasi wa mawazo zilitungwa wakiwa wanajaribu kufumbua fumbo lililoonekana ni gumu sana kung’amuliwa. Kabla lisaa halijamegeka, daktari wa Mtemvu alifika hotelini.
“Bwana Mtemvu, wakati unanipigia ndio nilikuwa namalizia ile shughuli. Kusema ukweli nimeshangazwa na hivyo vifo vingine. Kwa mujibu wa chunguzi, Mustafa amekufa kutokana na kupasuka kwa mishipa ndani ya mwili wake hivyo kupelekea damu kuvujilia ndani kwa ndani mpaka kifo.
Na kuhusu wafanyakazi wako wa ndani, vifo vyao ni vya kufananana – kutobolewa na kitu kirefu chenye ncha kali shingoni mwao. Lakini ajabu sijaona michubuko wala chochote kuashiria kama walipitia purukushani zozote kabla ya vifo vyao. Inaonyesha muuaji ni mtu mwenye utaalamu wa hali ya juu. Bado sijajua alitumia mbinu gani!”
“Si unaona!” Mtemvu alishadadia. “Niliwaambia mimi, kuna tatizo jamani!”
“Sasa tunafanyaje?” Filbert akauliza kwa hofu. Macho yalikuwa yamemtoka ndita za woga zikijichora kwenye paji la uso. Hakuna kingine walichokiamua zaidi ya kuimarisha ulinzi maradufu, wawe macho zaidi na lolote litakalotokea wajulishane.
Kikao kilifungwa wakatawanyika. Mtemvu alielekea kuichukua miili ya marehemu na hatua za mazishi zikafanyika zikichukua siku mbili tu baada ya miili ya marehemu kurudishwa kwenye makazi yao huko vijijini. Habari hazikusambaa hata kidogo. Hakuna aliyejua nini kilijiri ndani ya uzio wa nyumba ya bwana Mtemvu isipokuwa daktari, marafikize na polisi.
Kwa siri alipeleka miili hiyo huko vijijini akitoa pesa taslimu kufanikisha na kumaliza zoezi. Siku ya tatu aligeuka kurudi nyumbani kwake. Kwakuwa Mama Beatrice alikuwa bado yupo nyumbani kwa dada yake ilimlazimu siku hiyo akae peke yake nyumba nzima, hakuwa na jinsi.
Alipiga moyo konde akijiaminisha ya kuwa yeye ni mwanaume na yupo radhi kupambana na adui yake. Mkononi akiwa ameshikilia bunduki yake ndogo alijipumzisha kwenye kochi atizame televisheni.
Kwakuwa alikuwa amechoka mno na purukushani za msiba na hakupata muda wa kupumzika huko vijijini, usingizi haukupata vizingiti kumtwaa haraka; macho yalifumba mdomo ukaachama akilegea na kuacha bunduki yake ikae mbali. Muda mfupi tu baada kuanza kukoroma, akapata mgeni.
Hakuwa mgeni wa kawaida! Kilikuwa ni kivuli kilichopita kwenye mwanya wa mlango kisha kikajisogeza mbele kabisa ya Mtemvu na kusimama papo. Baada ya muda si mwingi, Mtemvu alijikuta akiwa amelala bafuni. Hakuwa na nguo yoyote, na kwenye kioo cha bafu aliachiwa ujumbe uliosomeka:
‘Mpaka pale wasaa utakapowadia’
*****
Muendelezo soma hapa
