Simu yako ya kwanza iko wapi katika hizi??

Simu yako ya kwanza iko wapi katika hizi??

englibertm

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2009
Posts
9,252
Reaction score
6,209
[h=3][/h]

IMG-20130517-WA004.png


IMG-20130517-WA007.png


IMG-20130517-WA005.png

IMG-20130517-WA003.png
Siku hizi watu mna masmartphone
 
Nilianza na nokia ya tochi mwaka 2006 niliinunua 20000 kwa mtu tena hela yenyewe ilikua pocket money ya term ya kwanza form five
 
Siemen C25(Twanga Pepeta)
Tena ilikuwa Used.

Nakumbuka ilikuwa 2002 jamaa aliniuzia
30000/- lakini nililipa kwa awamu
vocha ya zilikuwa za 10000,5000,3000
mwezi ukiisha salio lako lina expaya
kama hujalitumia.

Salio mwanzo ilikuwa ni mfumo wa U$
sasa utakuta vocha imeandikwa U$5,10 n.k
 
Simu yangu ya kwanza ilikua ni 3310 niliinunua Carphone Warehouse Clapham Junction SE London mwaka 2001.
 
simu yangu ya kwanza ilikuwa motorola ya kufunua na aria ya kuchomoa,hivyo ilikuwa 1998 mwanzoni,niliinunua kwa mtu kwa sh 50.000,ilikuwa na battery nene kama jiwe
 
Nilianza na nokia ya tochi mwaka 2006 niliinunua 20000 kwa mtu tena hela yenyewe ilikua pocket money ya term ya kwanza form five

Kipindi nipo skuli ukiwa na simu basi unaitumia kupigisha...enzi za Tritel, Buzz hizo unalonga usiku kucha bureeee.
Hakukuwa na SIM CARD ambazo ni hivi vidogo, bali simu ilikuwa inameza ile kadi nzima kama ilivyo pasipo kukibandua kile ki-micro chip.
 
Kulikuwa na Nokia fulani hivi, ina antena ya kupandisha na kushusha kama redio mkulima halafu inameza ile SIM CARD yote kama ilivyo pasipo kubandua ile Micro Chip.
Kabla hujaanza kuongea inabidi ukifunue kifuniko fulani hivi ambacho kilikuwa kinafunika keypad...
Enzi hizo ili ujulikane una simu basi unaiweka kwenye mfuko wa ghorofani "mfuko wa shati", bonge la simu kama kilo 2 hivi yaani ni kuchana mifuko ya shati mwanzo mwisho.
 
Kulikuwa na Nokia fulani hivi, ina antena ya kupandisha na kushusha kama redio mkulima halafu inameza ile SIM CARD yote kama ilivyo pasipo kubandua ile Micro Chip.
Kabla hujaanza kuongea inabidi ukifunue kifuniko fulani hivi ambacho kilikuwa kinafunika keypad...
Enzi hizo ili ujulikane una simu basi unaiweka kwenye mfuko wa ghorofani "mfuko wa shati", bonge la simu kama kilo 2 hivi yaani ni kuchana mifuko ya shati mwanzo mwisho.

Kuna wengine walikuwa wanazifunga kwenye mkanda kiunoni just for pride
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom