t blj
JF-Expert Member
- Dec 2, 2011
- 7,120
- 16,963
Trium yenye kipepeo!!
Haha umenichekesha sana , ilikuwa simu yangu ya pili hiyo!
Trium yenye kipepeo!!
Kama ulikua TZ lazima itakua ya mezani hiyo!
angalia vizuri ipo!!nokia 3310Sioni Nokia "Jeneza"
Trium yenye kipepeo!!
Haha umenichekesha sana , ilikuwa simu yangu ya pili hiyo!
Kulikuwa na Nokia fulani hivi, ina antena ya kupandisha na kushusha kama redio mkulima halafu inameza ile SIM CARD yote kama ilivyo pasipo kubandua ile Micro Chip.
Kabla hujaanza kuongea inabidi ukifunue kifuniko fulani hivi ambacho kilikuwa kinafunika keypad...
Enzi hizo ili ujulikane una simu basi unaiweka kwenye mfuko wa ghorofani "mfuko wa shati", bonge la simu kama kilo 2 hivi yaani ni kuchana mifuko ya shati mwanzo mwisho.
Simu yangu ya pili.... Siemen c25 ya kwanza ilikuwa sonnyerickson ya kufunguaya kianalogia hakuna sms wala nini tetetete
Simu yangu ya kwanza ilikua ni 3310 niliinunua Carphone Warehouse Clapham Junction SE London mwaka 2001.
simu yangu ya kwanza ilikuwa motorola ya kufunua na aria ya kuchomoa,hivyo ilikuwa 1998 mwanzoni,niliinunua kwa mtu kwa sh 50.000,ilikuwa na battery nene kama jiwe