Simpendi mama yangu mzazi

Simpendi mama yangu mzazi

Pole sana Mkuu ila kwa uandishi huo bila shaka nyie ni Wazaramo wa Mwaneromango!
 
Kwa watu wasiokua na matatizo na mama zao hawawezi kukuelewa, mimi wangu hua akianza habari zake basi nafanya kukaa kimya yani simjibu chochote hata aseme nina jeuri sijui simheshimu yani simjibu kabisaaà na naondoka mbali nae.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwanamke ni kiumbe hatari sana kwa kweli nilikuwa naumia sana kuona mwanamke akinyanyaswa au kufanyiwa ukatili wowote ila nimekuja kugundua walikuwa sahihi kabisa kwa kweli niliwaamini wanawake alichonifanya huyu mwanamke simpendi mwanamke yoyote katika maisha aya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
'Mama yangu kajawa Na chuki .roho ya kisasi .uchonganishi Na mambo ya kujifanya mcha mungu.

Hapa kwenye kujifanya mcha mungu anajikuta kujua nani mchawi nani mwema.

Mama kamchonga Nisha kaka yangu wa kwanza Na baba. Kaka Ali mnunia baba kwa miaka saba .ata ivi wanaongea ila bound yao sio nzuri'.


Kwa maelezo yako inaonyesha wewe, na kaka mna matatizo ndio maana mnaendekeza chuki.

Duniani hakuna mbadala wa wazazi, huyo, mama ndiye aliyekubeba mimba akakulea kwa kidogo alichokuwa nacho hadi umekuwa mkubwa na akili sasa za kuweza kuona hayo unayoyaita mapungufu yake. Baba hapo unamtumia tu kuhalalisha chuki yako dhidi ya mama. Hakuna haja ya kuyaweka moyoni mapungufu ya wazazi wewe ili mradi umekua ishi mbali ukijitegemea na pia uwe unawasiliana na wazazi baada ya vipindi na kama kuna jambo la kifamilia unawashirikisha endelea kuwa nao wote wawili, wasaidie kiuchumi kulingana na uwezo wako hata kama wao kwa wao hawaelewani na uwapende mpaka hapo utakapowazika.

Usiwe fundi wa kuchambua kasoro za wazazi nakuambia kama unataka kuwafurahia watoto wako mwenyewe hapo baadae.

Huyo kaka yako anadai eti baba yenu anamjia ndotoni ila kwa kuwa yeye ameokoka basi anapambana naye ndotoni (ubatili, kiburi na majivuno yalioje !) Hizi vidhehebu vyenu vilivyoanzishwa na njaa za sadaka au uasherati vitanawapotosha.

Hakuna mahali chini ya mbingu ambapo hakuna matatizo/changamoto. Kila mwanadamu anao msalaba wa kuubeba hadi mwisho wa maisha yake; tofauti kati ya mtu na mtu ni je anauchukuaje huo msalaba?
 
Sio mungu.. andika Mungu.... Halafu wazazi ndio Mungu wa duniani...acha bange

Sent using Jamii Forums mobile app
Usiwape cheo au hadhi ya uungu wanadamu.
Hakuna Mungu wa duniani labda ni miungu au mungu wa duniani. Kuna Mungu tu ambae ni wa mahali pote sio duniani tu.

Hao wazazi umeagizwa uwaheshimu tu ili upate maisha marefu, heri na baraka hapa duniani.
 
...Aisee usiombe yakukute... Ee Mungu tukomboe waja wako... Pole kaka
 
mama ni mama tuu.......kuna mambo huwa hayatafakariki......pole sana dogo.duh
 
Usiwape cheo au hadhi ya uungu wanadamu.
Hakuna Mungu wa duniani labda ni miungu au mungu wa duniani. Kuna Mungu tu ambae ni wa mahali pote sio duniani tu.

Hao wazazi umeagizwa uwaheshimu tu ili upate maisha marefu, heri na baraka hapa duniani.
Uwa najiuliza ivi ni nani ambaye akukaa tumboni kwa mwanamke napata jibu ni Adam Na mkewe.kumbe utalatibu ni mwadamu itabidi akae tomboni kwa mwanamke .sasa kwanini tuwaone kama Mungu wa duniani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom