Simba waliokula watu katika bonde la Rufiji

Simba waliokula watu katika bonde la Rufiji

Siku moja tuko porini Selous huko ni fisi alituokoa.
Tumekaa tunachoma nyama ya nyati na mastori kibao kumbe Simba kanyata yuko pale jirani tu anaskiliza story na kuvizia.
E bana ile harufu nyamachoma fisi hao na kimbelembele chao wanachekacheka wakaharibu target ya Simba.
Yaani ule mvurugano toka kichakani fisi akipigwa mpaka pale kilingeni wamevuruga moto nyama zote tupa kule,
Si hata hatupo tushakimbia kwenye mahema.
Yule fisi alilia siku hiyo "mama nakufaaa"
Kwa kipigo
nimecheka sana icho kilio cha fisi akilia mamaaaa nakufaaa
 
Siku nyingine porini humo Selous Simba aliwakorofisha nini sijui mbwa mwitu.
Hakuna kitu Simba anaogopa ka hao wanyama.
Aloo wametoka huko kibati wanamkimbiza kimya kimya.
Sisi kwenye tenti letu tuko watatu mle ndani mlango tumeacha wazi.
Vuup Simba kazama ndani anahema.
Wala hakutuangalia kageuka kakausha anapiga chabo nje.
Baada ya muda wale mbwa mwitu wamekatiza mbio wanamfwata huku wanahema balaa.
Fikiria Simba Dume liko ndani mla limetugeuzia matako yake nalo linahema.
Lilikaa km saa nzima alafu badae kulipotulia hilo likatoka taratibu likatambaa mdogo mdogo.
Mda huo mle ndani wa kukojoa,kuhara alifanya.
Yule Simba sidhani km hakutuona,alitudharau tu kapita zake baada ya kuepuka kipondo cha mbwa mwitu.
Kama angeongea labda angesema "asante sana washkaji zangu binadamu mmeniokoa siku ingine msiache mlango wazi😆"
 
Dah
Mkuu umenikumbusha mbali sana. Story yako ina ukweli. Mwishoni mwa 1990s kabla daraja halijakamilika nilivuka hapo Rufiji river nikitokea Dar nikiwa na lika chini ya 16. Lengo lililkuwa kwenda Nangurukuru.
Tulifika hapo jioni kivuko hakifanyi kazi na ilikuwa lazima asubuhi niwe Nangurukuru. Ilibidi tupande mtumbwi wa kienyeji. Ilikuwa hatari sana kuvuka, kwani mamba unawaona na kuogerea sijui. Halafu mto upo speed kwani ilikuwa masika. Chakushangaza captain alikuwa haogopi kitu ndio kwanza alikuwa ananipa moyo kuwa tutafika ngambo salama.
Tulipovuka tu, kulia kulikuwa na guest house na kulikuwa na watu wengi balaa. Ufuska uliokuwepo pale Mungu tu ndio anajua. Sasa uwani kwa ile Guest kulikuwa na Mabafu mawili ambapo ukiwa bafu moja aliyekuwa anaoga bafu lingine unamwona. Sasa akaingia mdada wa makamo kuoga nikaanza kumchungulia mara akaniona. Kilichotokea hapo ni siri, lakini mbeya mmoja akaenda kumtonya mume. ile natoka tu mume huyo kafika na kuanza kumshtumu mke kwamba alikuwa na mtu. cha ajabu akunishtukia kutokana na kimo na lika langu. Ila sikufanya zambi zaidi ya kuchungulia na kubalishana maoni.
Kesho yake asubuhi tukapanda baiskeli kwenda Nangurukuru, baada ya ya dk 10 tunakutana na simba ana vitoto. Mzee akanambia nisikimbie akitusogera nichune. bahati nzuri yule simba alituangalia baadaye akapotelea porini. Nikaanza kuhisi kuwa ile zambi ya jana usiku ndio imesababisha kukutana na Simba. Mzee akaniambia kukutana au kuliwa na simba eneo hilo siyo story. Hakika nilipata uwoga ambao hadi leo siwezi kusahau.

Kimsingi ni kweli Bondo la Rufiji hasa upende wa lindi ilikuwa hatari wengi wameliwa sana na simba.
Naomba Mungu wa mbinguni mwenye huruma anisamehe na kunifutia zambi ile.
Kuna watu wanazaliwa ni wachamungu wa asili, Allah akuongoze na akusamehe wewe na mimi ndugu yangu.
 
Back
Top Bottom