Simba vs Tiger

Nilishaona battle ya simba vs tiger wakuu sio poa, ilikua hivi wote walikua shimoni sijui waliingia vipi so hakuna aliekua anaweza kutoka yani ulipigwa mkono sio poa ilifikia point tiger alikua hawezi kuamka alikua anapigana kalala chali simba ndo alikua bado yupo active alikua anapigana akiwa bado kasimama ila kajeruhiwa balaa dam zimamwagika. Mwisho wakawa wote wanatazamana. Nilichogundua simba anapumzi kuliko tiger so naweza kusema simba ni habari nyingine anapigana mpaka kufa.
 

Huyo Come27 hawajui siberian tiger, tatizo wabongo wanapenda kukariri
 
na katika woote hao ma big cat ,jaguar ndio anaongoza kwa kuwa na strongest biteforce even kuliko simba na tiger ....


Mkuu, nilazima useme; bite force
relative to its body weight/size hapo Jagusr anawadi Cats wote.

Vinginevyo sio sawa hata kidogo kwamba Jaguar anamzidi Simba au Tiger kwa bite force.
 


Unawajua Siberian tiger wewe? Alafu Unaamini vipi hiyo video ni yakweli? Alafu tiger mwenyewe anaonekana hapo mdogo wakati tiger ni mkubwa more than jamii yoyote ya paka
 
duu mkuu hili battle linaonekana nila century sema tuu kma usemavyo halikuweza kuwekwa kwenye mkandaa ...soo boss wote waliaga maisha bila bingwa ??
 
Simba Dume hawezi poteza Nguvu na Pumzi zake kuwinda Swala au Nyumbu, hizo ni kazi za Jike. Dume ana winda Big Game Nyati, Twiga nk
Big game?

Halafu watoto amuachie nani?

Kazi za uwindaji zinasimamiwa na jike halafu kwenye hiyo big game haifanywi na simba mmoja labda kama akikutana na kinda la nyati
 
Hakuna mnyama porini mwenye tabu kama SIMBA DUME, simba dume akizembea anaweza kuzeeka bila kuoa
Maana ili awe na familia anatakiwa kuvamia pride na kugawa kipondo kwa Mzee wa kaya aliyeko
Na akikuta hiyo kaya majike wana watoto, majike pia husaidiana na Mzee wa kaya kufukuza huyu mgeni,
Kanuni Ya huko porini

Yale madume madogo madogo yanayotafuta familia Ya kujiweka, huwa yanatengeneza timu, yanawinda pamoja huku kila mmoja akifanya mishe ya kutafuta familia Ya kujiweka, na wakati Mwingine hili kundi la simba vijana huwa linatafuta mentor Mzee aliyepigwa huko kwenye familia yake kwa ajili ya kutoa mwongozo, maisha ya simba Dume ni magumu saana Sana na wana mwisho Mchungu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tafuta documentary Win ya hii battle ni 50/50 documentary niliyoangalia Tiger alikufa, simba alipata majeraha makubwa naamini Hata yeye hakuishi siku nyingi baada ya battle
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Si zani kama upo sawa kuna clip week iliyopita niliona chui ametoka na mamba ndani ya maji amembana kama chura
 
Kweli kabisa mkuuu. Nakuongezea kwamba Tiger vs African Leopards. Nakuhakikishia huyo tiger anakimbia pambano

Sent using Jamii Forums mobile app

We unaota! Chui apigane na tiger tangu lini!? Anaanzia Wapi?

Tiger ni mnyama mkubwa na mwenye nguvu nyingi sana anaweza kuua mnyama yoyote yule.

Ni simba pekee anayeweza kupambana na tiger! Tena awe simba dume!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chui apambane na simba?? Huu mzaa sasa
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mi niliona Nat Geo, very huge and tough nyati vs Simba dume, wee usiombe!

Kwa mara ya kwanza nilimpigia salute Simba!

Yaan ni alichangiwa na nyati kama 200, hivi, wale mademu zake Simba wakala kona wote, kidume akadili na nyati 200,

Mpaka wanamdedisha, aliwapiga makofi, na finger za kufa mtu kama 50 hivi!

Yaan hadi anakata roho alihakikisha kaondokoka na roho zao manina!

Salute king of the jungle!


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…