Simba vs Tiger

Simba vs Tiger

We jamaa ndo umepata kazi? Mbona tanapa imekuwa tanapa kila post? We unahisi wote wanaosema tiger ni zaidi ya simba hamna anaefanya kazi tanapa au kazi za mbugani? Kwanini unaamini kila asie share uelewa sawa na wewe taarifa kazipatia YouTube? Na after all kwani video zinazokua uploaded YouTube source yake ni wapi, sio huko huko maporini na kwenye zoo wanyama waliko? Au kila anaejua taarifa za wanyama lazima awe alienda porini?
Si watalii, wafanyakazi na watengeneza film na makala za wanyama si ndo wanaweka hizi video mitandaoni na dunia nzima inaona! Punguza matangazo maana hata Kijazi sidhani kama anajitangaza hivi.

Kwa taarifa tu ni kwamba India wanaweza kuwa na taarifa zaidi juu ya hili maana ndo nchi pekee yenya hawa wanyama wote maporini wakiwa na Asiatic lion na Bengal tiger. Sio wewe unashupaza shingo kuwaongelea tiger wakati hamna pori la tanapa lenye tiger hata mmoja
Wewe sio mambo yote yanayotokea uko maporini yanaweza kurekodiwa.Video zinazowekwa mitandaoni ni sehemu kidogo sana. ila kwa kiasi kikubwa watu wanaofanya kazi uko maporini wanaona mambo mengi zaidi kuliko wewe unayesubiri matukio machache yanayorekodiwa nakuwekwa kwenye mtandao.
 
Mimi nipo mbugani, msala wa wanyama wa African usikie tuuuu, tatizo la watu wengi wabishaji wanaishia kwy Mbuga ya YouTube. Sasa huyo mtu unamuacha kama alivyo na uwezi kujua nguvu ya simba kwy cage akipigana simba akiwa msituni anapambana ndio utajua nguvu yake kama ni kwy yale majani yanalala yote na miti inaanguka. Dume la simba akiwa anamuangusha nyati yaani sio mchezo. Huyo Africa Leopards balaaa lake sio mchezo fisi wanamuogopa kama nn?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndivyo wabongo tulivyo ndugu. ujuaji mwingi kumbe hewa tu.
 
We jamaa ndo umepata kazi? Mbona tanapa imekuwa tanapa kila post? We unahisi wote wanaosema tiger ni zaidi ya simba hamna anaefanya kazi tanapa au kazi za mbugani? Kwanini unaamini kila asie share uelewa sawa na wewe taarifa kazipatia YouTube? Na after all kwani video zinazokua uploaded YouTube source yake ni wapi, sio huko huko maporini na kwenye zoo wanyama waliko? Au kila anaejua taarifa za wanyama lazima awe alienda porini?
Si watalii, wafanyakazi na watengeneza film na makala za wanyama si ndo wanaweka hizi video mitandaoni na dunia nzima inaona! Punguza matangazo maana hata Kijazi sidhani kama anajitangaza hivi.

Kwa taarifa tu ni kwamba India wanaweza kuwa na taarifa zaidi juu ya hili maana ndo nchi pekee yenya hawa wanyama wote maporini wakiwa na Asiatic lion na Bengal tiger. Sio wewe unashupaza shingo kuwaongelea tiger wakati hamna pori la tanapa lenye tiger hata mmoja
Aise tena acha kabisa kumfananisha Simba wa Afrika na hivyo vipaka vingine vya uko asia vinavyowinda sungura.
 
Kuna kipindi niliwahi kwenda loliondo na dingi sasa,tukiwa njiani kama mita 30 au 50 basi tukaona mti una anguka aise,gari ikasimamishwa.....mkono ulikuwa unaendelea kati ya nyati na simba dume wa wawili

Haikuwa kipolepole ulipigwa mkono wa haja nyati kumbe ni balaa akikasirika kama machozi ya damu yana mtiririka hivi mwisho wa pambano simba wote walikufa pale pale mbavu zao zilisagwa sagwa kabisa ila nyati aalivunjika miguubya nyuma yote na juu ya nundu hapo alikuwa ana bonge la shimo!!ila bado maafisa wanyapori walitutaadharisha kuwa huyo bado ni hatari mpaka walipo muua!

N:b kwa mara ya kwanza na kula nyama ya porini ila nyati siyo mtamu kama pofu nilikula pofu nikasema hakika kuku ni jina hata kitimoto haingi ndani

Sent using Jamii Forums mobile app
Mziki wa nyati usikie tu.Simba mwenyewe kuna wakati akijichanganya vibaya inabidi arudi nyuma kujipanga upya..Sasa ukitaka ufurahi ukute tifu la simba dume bachela na nyati dume aliyejeruhiwa.Hivyo vipaka vingine vyauko ulaya na asia vingekua afrika vingekua vinawinda swala wadogo tu ila sio Nyati.
 
Aise tena acha kabisa kumfananisha Simba wa Afrika na hivyo vipaka vingine vya uko asia vinavyowinda sungura.
Bora uwaambie vijana wa YouTube. Wao wakimuona African Lions wanamlinganisha na Simba wa kwy PlayStation. Baraaa la Simba wa apa African sio mchezo. wanyama wote wa Africa ni hatari tupu, anaua mnyama mkubwa na kumvuta umbali mrefu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mimi naona tiger is better

Huyu tiger anauwezo wa kuingia kwenye mto na kumchukua mamba akiwa mle mle kwenye maji jambo ambalo sio rahisi ukizingatia na kwamba nguvu ya mamba ni maji lakini si kwa chui

Halafu hata skills za uwindaji chui yuko vizuri zaidi, kama silaha basi naweza kumfananisha na AK47 wakati simba namfananisha na gobole

Action za chui ni noma hadi ndege anawinda, yani anajiviringa juu huko huko aliko ndege kisha anamdaka kwa mikono kama mtu

Simba dume ndo kabisa hata kuwinda halijui lenyewe kula kulala tu kazi zote limemuachia shemu
Nani alikwambia simba dume hawindi?.Simba dume ataacha kuwinda akishapambana akapata himaya yake, hapo sasa anakua mfalme kazi yake kubwa nikulinda himaya yake yamajike na watoto isijekuvamiwa na madume wengine.Ila anapokua bachela anawinda kama kawaida na hao ndo wanakuaga wakorofi kuliko dume mwenye majike.
 
Mjadala umekuwa mkali sana ishara ya kwamba wengi tunafuatilia na tunawapenda wanyama. Ni dalili nzuri na ishara kwamba kwa hili ustawi wao utawezekana maana kama kitu unakipenda ni dhahiri kwamba utakilinda.
Tuendelee kuwapenda wanyama hasa wa porini maana ustawi wao unategemea sana upendo wetu kwao na juhudi za kuwalinda. Tuache matumizi ya bidhaa zao kama nyama, kucha, ngozi na pembe zao, tisiingilie na tusitishe shughuli za kibinadamu katika maeneo yao ya asili ila pia tuendelee kuzitembelea mbuga na mapori wanamo hifadhiwa kwani kwa kufanya hivyo sio tu itapatikana pesa ya kuendelea kuwalinda kwa waliopewa mamlaka ila pia tutaendelea kupata elimu na kuwajua zaidi na hivyo kuwa na ari ya kuguswa na kuzidi kuwapenda.
Ni viumbe muhimu sana kwenye eco system kwahiyo uwepo wao unastablize uwepo wa uhai endelevu katika ulimwengu huu.

Pamoja na hayo yote simba aka baunsa wa gym za uswazi maana kutokuwa na vifaa mahsusi vya mazoezi vinamfanya avimbe kifua tu huku chini anaisha hawezi kuchukua round kwenye fight na Tiger wakiwa one on one. Hua nikiangalia umbo la simba dume namfananisha na tonge la ugali limechomekwa kwenye kijiti cha meno😀😆😀
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom