Simba SC itoke hadharani ijitenge na imkemee huyu mwanasiasa

Simba SC itoke hadharani ijitenge na imkemee huyu mwanasiasa

DELETED ACCOUNT

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
9,805
Reaction score
15,475
Kuna video clip nimeiona jana ya mtu ambaye inasemekana ni Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Geita, anayejulikana kama Manjale akiitumia timu ya Simba na mafanikio yake kukinadi chama chake. Hii video inatia kichefuchefu maana huyu bwana anaongea kama vile yeye ni kiongozi pale Simba.


View: https://youtu.be/MYeHejL5V1c

Ni juzi tu nilitoa tahadhari kwa uongozi wa Simba wawe makini sana kutumika kwa klabu hii katika harakati za kisiasa. Hii video clip inatupa mwelekeo wa kule tunapokwenda na inaonyesha hatari iliyo mbele yetu.

Kama hawa wanasiasa wanataka wajimilikishe mafanikio ya Simba, wawe tayari pia kujimilikisha kushindwa kwa Yanga, Azam na Singida katika mashindano ya kimataifa msimu huu. Huyu bwana ameenda mbali hadi akaongelea sakata la derby na kwamba Simba ni ya chama chake na Yanga ni upande mwingine. Hili jambo halikubaliki katika ulimwengu wa football.

Bila kujali itikadi za kisiasa za mashabiki wa Simba, hili jambo halina afya njema kwa Simba SC hasa siku za mbeleni.

Viongozi wa Simba watoke hadharani na wakemee kutumiwa kwa klabu ya Simba katika majukwaa ya kisiasa. Kukaa kwao kimya kutaleta ishara kwamba wanabariki matamko haya na kwamba watakuwa tayari kubeba msalaba wa kile kitakachotokea mbeleni.
 
Naunga mkono hoja, Simba ikatae wazi wazi hizi propaganda za jumuia za CCM.

wanachama hatutaki kabisa kusikia.
Mtake mstake Simba na Yanga zitatumika kisiasa na viongozi hawawezi abadani kujitenga na siasa
 
Hizo timu ni Timu za Chama cha Mapinduzi mtake Msitake.

Muundo wa Kiuongozi wa Simba na Yanga kabla ya Mabadiliko ni C&p ya CCM.

1. Mwenyekiti.
2. Makamu Mwenyekiti.
3. Katibu Mkuu.
4. Katibu Mwenezi na propaganda nk.

MSISHANGAE SANA
 
Mtake mstake Simba na Yanga zitatumika kisiasa na viongozi hawawezi abadani kujitenga na siasa
Hatuwezi kuzichezea na kuziweka rehani hisia na furaha za watanzania kwa watu kama hawa ambao leo anaisifia Simba na kuichamba Yanga, kesho ikiwa kinyume naye anabadilika kama kinyonga.

Ni sawa uwe club una enjoy zako kinywaji na mziki mnene halafu mshamba mmoja akuletee mambo ya kiwaki.
 
Anzisha timu Yako ndio uitenganishe na siasa jinga kabisa wewe simba na yanga ni Mali ya ccm na wewe huna mamlaka yeyote ya kuziongelea hizo klabu sababu ni Mali ya ccm sio yako
 
Anzisha timu Yako ndio uitenganishe na siasa jinga kabisa wewe simba na yanga ni Mali ya ccm na wewe huna mamlaka yeyote ya kuziongele1 hizo klabu sababu ni Mali ya ccm sio yako
Ni kweli hizi timu zilianzishwa kwa malengo ya kisiasa na bado ipo hivyo, hata hawa viongozi ambao tupo nao wapo kwa idhini ya serikali iliyopo madarakani, ukiwa kinyume na serikani hauwezi kuwa kiongozi simba wala yangu, na nchi hii hatujaweza kutenganisha kati chama na serikali ndo maana mpaka leo ccm wanaweza kuchukua mali ya umma wakaifanya kuwa ya chama.
 
Ni kweli hizi timu zilianzishwa kwa malengo ya kisiasa na bado ipo hivyo, hata hawa viongozi ambao tupo nao wapo kwa idhini ya serikali iliyopo madarakani, ukiwa kinyume na serikani hauwezi kuwa kiongozi simba wala yangu, na nchi hii hatujaweza kutenganisha kati chama na serikali ndo maana mpaka leo ccm wanaweza kuchukua mali ya umma wakaifanya kuwa ya chama.
Watu wajinga kama hawa hawaelewi
 
Naunga mkono hoja, Simba ikatae wazi wazi hizi propaganda za jumuia za CCM.

wanachama hatutaki kabisa kusikia.
Mkuu, itawezekana kukemea hili kutoka kwa viongozi? Tutakosa ndege ya kwenda Morocco. Hata uto kipindi kile siasa ziliingizwa sana baada ya kufika fainali. Hii nchi kila kitu siasa na hili wanalitumia pia. Kikubwa ni kukomaa kiwanjani. Baaaas
 
Mkuu, itawezekana kukemea hili kutoka kwa viongozi? Tutakosa ndege ya kwenda Morocco. Hata uto kipindi kile siasa ziliingizwa sana baada ya kufika fainali. Hii nchi kila kitu siasa na hili wanalitumia pia. Kikubwa ni kukomaa kiwanjani. Baaaas
Kwani sisi wenyewe hatuwezi kodi ndege itupeleke Berkane? Lol
Uwezo tunao bhana, hatutaki siasa ktk jambo letu.
 
Back
Top Bottom