GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,591
- 108,962
1. Henock Inonga
Nakiri ni Beki mzuri sana na nimekuja Kugundua pia kuwa kumbe ni Versatile na kwamba anaweza hata kucheza vyema tu Namba 6, Namba 8 na hata Namba 2.
Mchezaji huyu tokea aicheze vyema ile Kariakoo Derby na kupata Sifa nyingi nae ameshajaa Upepo kiasi kwamba sasa anajiona ndiyo Mchezaji mzuri Kikosini Simba SC kuliko wengine waliopo au aliowakuta.
Inonga amekuwa akipenda Kulaumu mno Wenzake Uwanjani huku muda mwingi akitaka Kuonekana kama Yeye ndiyo anacheza kwa Bidii kuliko Wenzake na hupenda sana Kucheza na Akili ya Kocha Pablo ili apendwe na aaminike zaidi Kwake.
Inonga aambiwe ukweli kuwa katika ile 'Kariakoo Derby' Kazi ya Kumkaba Mshambuliaji hatari na ninayemuogopa wa Yanga SC Fiston Mayele hakuifanya peke yake kama adhaniavyo bali alikabwa Collectively and Strategically na Mabeki Wenzake Wote na tena kama kuna Mtu ambaye Mimi GENTAMYCINE niliona ndiyo alimkaba vilivyo Mayele ni Beki Joash Onyango na siyo Yeye Henock Inonga.
2. Bernard Morrison
Huyu nadhani GENTAMYCINE nilishamsoma mno hapa JamiiForums na mpaka Kuutaka Uongozi wa Simba SC Kumkanya na Kumrekebisha ila naona Jana katika Mechi na Mlandege FC yamejirudia tena yale yale.
Uongozi wa Simba SC leo ngoja sasa niwapasulieni Ukweli wangu kwa Kuwaambia kuwa hakuna Mchezaji nisiyempenda Kikosini Simba SC na asiye na Faida Kwetu ( japo baadhi yenu hasa CEO Barbara Gonzalez ) mnamlea na Kumdekeza kama huyu Bernard Morrison.
Na nimepata Taarifa za Jikoni kabisa kutoka kwa Mmoja wa Kiongozi wa Simba SC na Mchezaji Mwandamizi Kikosini kuwa kumbe hata Kocha Mkuu Pablo Franco Martin nae si tu hamtaki bali hampendi kama ilivyo Kwangu ila anakingiwa Kifua.
Morrison ana Kiburi, Morrison Mjeuri, Morrison ana Hasira za Kipumbavu ( Kipopoma ), Morisson analazimisha Ufalme asioustahili kwa sasa ndani ya Simba SC, Morrison anapenda Kucheza sana na Jukwaa na ni mpenda Matukio yasiyo na Faida ama Kwake au hata kwa Klabu yetu pia, Morrison ana Dharau iliyopotiliza na isiyovumilika na mwisho kabisa nahisi Morrison ni Psychopath Case ila huenda Uongozi wa Simba SC bado haujaligundua hilo.
Akina Barbara Gonzalez ( CEO ), Mwenyekiti wa Bodi ya Simba SC Salim Abdallah Mhene 'Try Again', Mwenyekiti wa Simba SC ( Wanachama ) Murtaza Mangungu na Wewe 'Poti' wangu kabisa kutoka Mkoani Mara ( Musoma ) Kwetu Crescetius Magori ( Mshauri Mkuu wa Mwekezaji Mo Dewji ) na pia Mshauri wa CEO na Benchi la Ufundi la Simba SC endeleeni tu Kumlea na Kumdekeza huyu Mchezaji Bernard Morrison ila GENTAMYCINE nawaambia hapa hapa JamiiForums kuwa kuna Siku atatugharimu na ataigharimu pakubwa mno Simba SC yetu.
3. Pape Ousmane Sakho
Ni Mchezaji mzuri sana na mwenye Kipaji cha Kipekee kiasi kwamba kwa anavyocheza natabiri mapema kuwa huenda huko mbeleni Simba SC ikatajirika zaidi kwa Kumuuza Nje kwa Gharama za hata Kuwazidi akina Chama na Miquissone.
Hata hivyo pamoja na hizi Kongole ( Pongezi ) zangu Kwake Sakho nae ana Mapungufu yanayotakiwa Kurekebisha haraka kwani akiachwa namuona nae ana 'Elements' za akina Inonga na Morisson.
Sakho anapenda Kukurupuka, Sakho anapenda Sifa ( hasa Kucheza na Majukwaa ), Sakho ameshaanza Kuota Majipu Kwapani ( namaanisha Kuringa na kujiona ni kila Kitu sasa Kikosini ), Sakho anataka Kuulazimisha Ufalme wake sasa Simba SC wakati muda wake wa kuwa Mfalme nauona upo ndani ya miaka Miwili ijayo.
Sakho anataka kila Kitu cha Uwanjani awe anakifanya Yeye tu hata kama Kiufundi kwa Mazingira yaliyopo hapaswi kuyafanya Yeye, Sakho anapenda sana Kukaa na Mpira na Kupiga Chenga nyingi ( Over Dribbling ) kitu ambacho ni Hatari mno Kwake Kiafya kwani uwezekano wa Kuumizwa vibaya na kupata Majeraha makubwa mfano akikutana na Mabeki 'Wahuni' na 'Masela' akina Kelvin Yondan na Juma Nyosso ( ambao Wote sasa wako Geita Gold FC ) kwa Kocha Fred Felix Kataraiya Majeshi Minziro ni mkubwa.
Tafadhali waambiwe na wajitathmini!!!!
Nakiri ni Beki mzuri sana na nimekuja Kugundua pia kuwa kumbe ni Versatile na kwamba anaweza hata kucheza vyema tu Namba 6, Namba 8 na hata Namba 2.
Mchezaji huyu tokea aicheze vyema ile Kariakoo Derby na kupata Sifa nyingi nae ameshajaa Upepo kiasi kwamba sasa anajiona ndiyo Mchezaji mzuri Kikosini Simba SC kuliko wengine waliopo au aliowakuta.
Inonga amekuwa akipenda Kulaumu mno Wenzake Uwanjani huku muda mwingi akitaka Kuonekana kama Yeye ndiyo anacheza kwa Bidii kuliko Wenzake na hupenda sana Kucheza na Akili ya Kocha Pablo ili apendwe na aaminike zaidi Kwake.
Inonga aambiwe ukweli kuwa katika ile 'Kariakoo Derby' Kazi ya Kumkaba Mshambuliaji hatari na ninayemuogopa wa Yanga SC Fiston Mayele hakuifanya peke yake kama adhaniavyo bali alikabwa Collectively and Strategically na Mabeki Wenzake Wote na tena kama kuna Mtu ambaye Mimi GENTAMYCINE niliona ndiyo alimkaba vilivyo Mayele ni Beki Joash Onyango na siyo Yeye Henock Inonga.
2. Bernard Morrison
Huyu nadhani GENTAMYCINE nilishamsoma mno hapa JamiiForums na mpaka Kuutaka Uongozi wa Simba SC Kumkanya na Kumrekebisha ila naona Jana katika Mechi na Mlandege FC yamejirudia tena yale yale.
Uongozi wa Simba SC leo ngoja sasa niwapasulieni Ukweli wangu kwa Kuwaambia kuwa hakuna Mchezaji nisiyempenda Kikosini Simba SC na asiye na Faida Kwetu ( japo baadhi yenu hasa CEO Barbara Gonzalez ) mnamlea na Kumdekeza kama huyu Bernard Morrison.
Na nimepata Taarifa za Jikoni kabisa kutoka kwa Mmoja wa Kiongozi wa Simba SC na Mchezaji Mwandamizi Kikosini kuwa kumbe hata Kocha Mkuu Pablo Franco Martin nae si tu hamtaki bali hampendi kama ilivyo Kwangu ila anakingiwa Kifua.
Morrison ana Kiburi, Morrison Mjeuri, Morrison ana Hasira za Kipumbavu ( Kipopoma ), Morisson analazimisha Ufalme asioustahili kwa sasa ndani ya Simba SC, Morrison anapenda Kucheza sana na Jukwaa na ni mpenda Matukio yasiyo na Faida ama Kwake au hata kwa Klabu yetu pia, Morrison ana Dharau iliyopotiliza na isiyovumilika na mwisho kabisa nahisi Morrison ni Psychopath Case ila huenda Uongozi wa Simba SC bado haujaligundua hilo.
Akina Barbara Gonzalez ( CEO ), Mwenyekiti wa Bodi ya Simba SC Salim Abdallah Mhene 'Try Again', Mwenyekiti wa Simba SC ( Wanachama ) Murtaza Mangungu na Wewe 'Poti' wangu kabisa kutoka Mkoani Mara ( Musoma ) Kwetu Crescetius Magori ( Mshauri Mkuu wa Mwekezaji Mo Dewji ) na pia Mshauri wa CEO na Benchi la Ufundi la Simba SC endeleeni tu Kumlea na Kumdekeza huyu Mchezaji Bernard Morrison ila GENTAMYCINE nawaambia hapa hapa JamiiForums kuwa kuna Siku atatugharimu na ataigharimu pakubwa mno Simba SC yetu.
3. Pape Ousmane Sakho
Ni Mchezaji mzuri sana na mwenye Kipaji cha Kipekee kiasi kwamba kwa anavyocheza natabiri mapema kuwa huenda huko mbeleni Simba SC ikatajirika zaidi kwa Kumuuza Nje kwa Gharama za hata Kuwazidi akina Chama na Miquissone.
Hata hivyo pamoja na hizi Kongole ( Pongezi ) zangu Kwake Sakho nae ana Mapungufu yanayotakiwa Kurekebisha haraka kwani akiachwa namuona nae ana 'Elements' za akina Inonga na Morisson.
Sakho anapenda Kukurupuka, Sakho anapenda Sifa ( hasa Kucheza na Majukwaa ), Sakho ameshaanza Kuota Majipu Kwapani ( namaanisha Kuringa na kujiona ni kila Kitu sasa Kikosini ), Sakho anataka Kuulazimisha Ufalme wake sasa Simba SC wakati muda wake wa kuwa Mfalme nauona upo ndani ya miaka Miwili ijayo.
Sakho anataka kila Kitu cha Uwanjani awe anakifanya Yeye tu hata kama Kiufundi kwa Mazingira yaliyopo hapaswi kuyafanya Yeye, Sakho anapenda sana Kukaa na Mpira na Kupiga Chenga nyingi ( Over Dribbling ) kitu ambacho ni Hatari mno Kwake Kiafya kwani uwezekano wa Kuumizwa vibaya na kupata Majeraha makubwa mfano akikutana na Mabeki 'Wahuni' na 'Masela' akina Kelvin Yondan na Juma Nyosso ( ambao Wote sasa wako Geita Gold FC ) kwa Kocha Fred Felix Kataraiya Majeshi Minziro ni mkubwa.
Tafadhali waambiwe na wajitathmini!!!!