Simba iliahirishiwa mechi, kwanini Kitayosce ilazimishwe kucheza pungufu?

Kichuchunge

JF-Expert Member
Dec 2, 2020
338
891
Desemba 28, mwaka 2021, Bodi ya Ligi Kuu Tanzania(TPLB) iliamua kuahirishwa kwa mchezo namba 69 wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Kagera Sugar FC na Simba SC uliokuwa uchezwe siku hiyo Saa 10:00 Alasiri katika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, kutokana na taarifa za kitabibu kuwa wachezaji 16 kati ya 22 wa Simba SC waliosafiri kwenda Bukoba kuonekana kuwa na dalili ya mafua na kukohoa hali inayochangiwa na mabadiliko ya hali ya hewa (Seasonal Influenza).

Simba ingeweza kulazimishwa kuchezesha wachezaji nane, iagize wachezaji wa Under 20, au la ipoteze pointi kwa mujibu wa Kanuni maana kuugua kwa wachezaji wao haikuwa kosa la Kagera kabisa ila Bodi ikatumia 'Busara' mechi ikaahirishwa.

Lakini jana Bodi hiyo ikashindwa kutumia 'Busara' hiyo hiyo kuahirisha mechi ya Azam na Kitayosce kutokana na baadhi ya wachezaji wa Kitayosce kutokidhi vigezo huku wengine, akiwemo golikipa wakiwa ni wagonjwa lakini wakalazimishwa wacheze hivyo hivyo wakiwa nane.

Je, hapa Bodi haikuona haja ya kutumia 'Busara' au inaonea timu ndogo?

Tujadili.
 
Desemba 28, mwaka 2021, Bodi ya Ligi Kuu Tanzania(TPLB) iliamua kuahirishwa kwa mchezo namba 69 wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Kagera Sugar FC na Simba SC uliokuwa uchezwe siku hiyo Saa10:00 Alasiri katika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, kutokana na taarifa za kitabibu kuwawachezaji 16 kati ya 22 wa Simba SC waliosafiri kwenda Bukoba kuonekana kuwa na dalili yamafua na kukohoa hali inayochangiwa na mabadiliko ya hali ya hewa (Seasonal Influenza).

Simba ingeweza kulazimishwa kuchezesha wachezaji nane, iagize wachezaji wa Under 20, au la ipoteze pointi kwa mujibu wa Kanuni maana kuugua kwa wachezaji wao haikuwa kosa la Kagera kabisaa ila Bodi ikatumia 'Busara' mechi ikaahirishwa.

Lakini jana Bodi hiyo ikashindwa kutumia 'Busara' hiyo hiyo kuahirisha mechi ya Azam na Kitayose kutokana na baadhi ya wachezaji wa Kitayose kutokidhi vigezo huku wengine, akiwemo golikipa wakiwa ni wagonjwa lakini wakalazimishwa wacheze hivyo hivyo wakiwa nane. Je hapa Bodi haikuona haja ya kutumia 'Busara' au inaonea timu ndogo? Tujadili.
Kiongozi, mbona hapa unaelezea kesi mbili tofauti? (Magonjwa vs Kuchelewa kuwasilisha majina FIFA kwa uzembe)

1. Kuahirishwa kwa mpira wa Kagera ilikuwa muhimu kwa pande zote mbili kuepusha kuenea zaidi kwa ugonjwa huo.

2. 2021 Covid 19 ilikuwa bado inaendelea kutafuna, hivyo hatua za kuahirisha mechi ile zilikuwa muhimu kuepuka madhara zaidi.

3. Mpaka jana asubuhi Kitayose (Tabora FC) walithibitisha kuingia uwanjani, na wako kamili, rejea maongezi ya Wasaf FM Sport Arena na Alhaji Rage.

4. Wajibu wa viongozi wa Kitayose ni upi, kama hawakutoa taarifa kwa TFF juu ya kukosekana kwa wachezaji wao, Je ulitaka TFF waote kuahirisha mechi??

Tafuta mechi nyingine ya kulinganisha, ila sio ya Simba vs Kagera, kwakuwa maudhui ya kuahirisha mechi hizo hayafanani.
 
Kiongozi, mbona hapa unaelezea kesi mbili tofauti? (Magonjwa vs Kuchelewa kuwasilisha majina FIFA kwa uzembe)

1. Kuahirishwa kwa mpira wa Kagera ilikuwa muhimu kwa pande zote mbili kuepusha kuenea zaidi kwa ugonjwa huo.

2. 2021 Covid 19 ilikuwa bado inaendelea kutafuna, hivyo hatua za kuahirisha mechi ile zilikuwa muhimu kuepuka madhara zaidi.

3. Mpaka jana asubuhi Kitayose (Tabora FC) walithibitisha kuingia uwanjani, na wako kamili, rejea maongezi ya Wasaf FM Sport Arena na Alhaji Rage.

4. Wajibu wa viongozi wa Kitayose ni upi, kama hawakutoa taarifa kwa TFF juu ya kukosekana kwa wachezaji wao, Je ulitaka TFF waote kuahirisha mechi??

Tafuta mechi nyingine ya kulinganisha, ila sio ya Simba vs Kagera, kwakuwa maudhui ya kuahirisha mechi hizo hayafanani.
Hii imeendaa
 
Hiyo timu isipokuwa makini itakuwa kibonde kwa timu kuifunga magoli inayotaka. Ilipandaje daraja? Ikiendelea hivyo itarudi daraja la chini na kucheza msimu mmoja tu. Cheki Singida fg imepanda na kuwa kitisho na kuwa big four ligi kuu mpaka kucheza kimataifa. Ina maana wafadhili hawaioni timu hiyo wakaifadhili ili ifanye vizuri, why Singida fg timu changa ifanye vizuri mara tu baada ya kupanda na kitayose iishie kwenye aibu kucheza msimu mmoja?
 
Ile nafasi ya Kitayose ilikuwa ya PAMBA waache wavune walichopanda

Hujuma dhidi ya PAMBA zilikuwa za wazi na Karia akaziba masikio Sasa aibebe na huku tuone
 
Kiongozi, mbona hapa unaelezea kesi mbili tofauti? (Magonjwa vs Kuchelewa kuwasilisha majina FIFA kwa uzembe)

1. Kuahirishwa kwa mpira wa Kagera ilikuwa muhimu kwa pande zote mbili kuepusha kuenea zaidi kwa ugonjwa huo.
Timu za Ligi Kuu zinaruhusiwa kuongeza na kuwatumia wachezaji wa timu za vijana hadi watano, hivyo kama kulikuwa wagonjwa wangeenguliwa wakawekwa vijana.
2. 2021 Covid 19 ilikuwa bado inaendelea kutafuna, hivyo hatua za kuahirisha mechi ile zilikuwa muhimu kuepuka madhara zaidi.
Rejea andiko la TFF, haukutajwa ni ugonjwa gani sasa wewe unalazimisha iwe ni Covid 19!
3. Mpaka jana asubuhi Kitayose (Tabora FC) walithibitisha kuingia uwanjani, na wako kamili, rejea maongezi ya Wasaf FM Sport Arena na Alhaji Rage.

4. Wajibu wa viongozi wa Kitayose ni upi, kama hawakutoa taarifa kwa TFF juu ya kukosekana kwa wachezaji wao, Je ulitaka TFF waote kuahirisha mechi??
Simba walilalamika tu wachezaji wetu wagonjwa mida ya saa 8, masaa mawili kabla ya mchezo, ingawa katika pre match walihudhuria vizuri. Kitayose walisema wamekuja na wachezaji wao wote, walipoambiwa wengine hawatocheza, wale wengine pia wakawa hawako vizuri kiafya (wagonjwa kama Simba), mechi haikuahirishwa na wakalazimishwa kucheza hivyo hivyo tena pungufu. Yanga waliwahi kuugua kule Mbeya, mechi haikuahirishwa, kulikoni kwa Simba tu?
Tafuta mechi nyingine ya kulinganisha, ila sio ya Simba vs Kagera, kwakuwa maudhui ya kuahirisha mechi hizo hayafanani.
 
Kwenye ishu ya kitayosce TFF hawana makosa. Mnyonge mpeni haki yaki yake huo ni uzembe wao wenyewe. TFF kila mara ilikuwa ikitoa update kuzikumbusha timu kufanya usajili kwenye mfumo wa FIFA Connect mpaka baadhi ya watu walikuwa wanacomnent kuwa hao TFF hawana kazi ya kufanya kisa tu kuzikumbusha timu lkn matokeo yake ndo haya.

Mpaka tarehe 14/8/23 Kitayosce na Mtibwa zilikuwa ndo timu pekee za NBCPL ambazo hazijaingiza jina hata moja. Hawa Kitayosce ukiangalia vizuri hawako serious hata jina lenyewe mpaka ligi inaanza hawajabadili huko TFF ila wao tayari washaanza kujiita Tabora united
 
Kwenye ishu ya kitayosce TFF hawana makosa. Mnyonge mpeni haki yaki yake huo ni uzembe wao wenyewe. TFF kila mara ilikuwa ikitoa update kuzikumbusha timu kufanya usajili kwenye mfumo wa FIFA Connect mpaka baadhi ya watu walikuwa wanacomnent kuwa hao TFF hawana kazi ya kufanya kisa tu kuzikumbusha timu lkn matokeo yake ndo haya. Mpaka tarehe 14/8/23 kitayosce na mtibwa zilikuwa ndo timu pekee za NBCPL ambazo hazijaingiza jina hata moja. Hawa kitayosce ukiangalia vizuri hawako serious hata jina lenyewe mpaka ligi inaanza hawajabadili huko TFF ila wao tayari washaanza kujiita Tabora united
Kanuni ya 17 ya Ligi Kuu, kifungu cha 22 kinasema:
"Wachezaji wote watatambulika kwa kutumia Leseni zao zitakazotolewa na kuidhinishwa na TFF. Mchezaji yeyote ambaye hatakuwa na leseni hatoruhusiwa kucheza katika mchezo husika."
Lakini kifungu cha 23 kinatoa unafuu kwa kusema:
"Katika mazingira maalum ya kukosekana Leseni ya mchezaji, TFF inaweza kutoa utambulisho wa dharura/muda ili kukidhi mahitaji ya kikanuni kwa mchezaji kucheza mchezo husika."
TFF ingetumia busara kwa kifungu cha 23 ili mchezo uchezeke kwa haki.
 
Kanuni ya 17 ya Ligi Kuu, kifungu cha 22 kinasema:
"Wachezaji wote watatambulika kwa kutumia Leseni zao zitakazotolewa na kuidhinishwa na TFF. Mchezaji yeyote ambaye hatakuwa na leseni hatoruhusiwa kucheza katika mchezo husika."
Lakini kifungu cha 23 kinatoa unafuu kwa kusema:
"Katika mazingira maalum ya kukosekana Leseni ya mchezaji, TFF inaweza kutoa utambulisho wa dharura/muda ili kukidhi mahitaji ya kikanuni kwa mchezaji kucheza mchezo husika."
TFF ingetumia busara kwa kifungu cha 23 ili mchezo uchezeke kwa haki.
Waliomba wakakataliwa?
 
Desemba 28, mwaka 2021, Bodi ya Ligi Kuu Tanzania(TPLB) iliamua kuahirishwa kwa mchezo namba 69 wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Kagera Sugar FC na Simba SC uliokuwa uchezwe siku hiyo Saa10:00 Alasiri katika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, kutokana na taarifa za kitabibu kuwawachezaji 16 kati ya 22 wa Simba SC waliosafiri kwenda Bukoba kuonekana kuwa na dalili yamafua na kukohoa hali inayochangiwa na mabadiliko ya hali ya hewa (Seasonal Influenza).

Simba ingeweza kulazimishwa kuchezesha wachezaji nane, iagize wachezaji wa Under 20, au la ipoteze pointi kwa mujibu wa Kanuni maana kuugua kwa wachezaji wao haikuwa kosa la Kagera kabisaa ila Bodi ikatumia 'Busara' mechi ikaahirishwa.

Lakini jana Bodi hiyo ikashindwa kutumia 'Busara' hiyo hiyo kuahirisha mechi ya Azam na Kitayose kutokana na baadhi ya wachezaji wa Kitayose kutokidhi vigezo huku wengine, akiwemo golikipa wakiwa ni wagonjwa lakini wakalazimishwa wacheze hivyo hivyo wakiwa nane. Je hapa Bodi haikuona haja ya kutumia 'Busara' au inaonea timu ndogo? Tujadili.

1: 22-16=?
A:6
B: 8

2:Then, msingi wa tatizo lako?

3: Toa taarifa na ombi rasmi
 
Kila kitu Cha mpira mnapenda kulinganisha na Simba, umesema mwenyewe kati ya wachezaji 22, 16 walikutwa na changamoto za afya Kwa hiyo walibaki 6. Kama ungekuwa ni mfatiliaji mpira ungejua ni idadi gani inayotakiwa Ili timu iweze kuingia uwanjani.
Umetoa kichekesho eti wangelazimishwa kuchezesha wachezaji wa U20, Yale hivi unajua ni hivi kwenye ligi Kwa timu inayotaka kushindanis ubingwa unaweza kuilazimisha ipange kikosi dhaifu, inawezekana ulikuwa unawaza zama za TFF ikiwa chini ya uongozi wa Malinzi.
 
Back
Top Bottom