Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 2,563
- 7,321
Baada ya Yanga kutoa tamko lao la hawatacheza mechi mpaka matakwa yao yatakapofanyiwa kazi, Simba nao ni kama wanasubiri Yanga isilete Timu tarehe 15, ili adai point 3 za mezani... na hasipopewa point 3 za mezani nae anagoma mpaka haki itendeke. Ikumbukwe tayari mamlaka za mpira Nchini zimeshatangaza tarehe ya Derby kuwa ni June 15. Simba anamuwimda Yanga hajichanganye kutokuleta Timu uwanjani tu ajibebee point. Hapo ndipo msemo wa vita ya panzi furaha kwa kunguru maana yake inatimia.
Wakati Yanga wanarumbana na TFF na Bodi ya Ligi... Simba nao wamevaa darubini wakisubiri kanuni zivunjwe hili nao wagomee au wadai point tatu mezani....
Mechi hii ya tarehe 15 ikihairishwa inakuwa mechi ya 2 ya derby iliyoharishwa kwa Timu hizo hizo ndani ya msimu mmoja.
Ujumbe kutoka Simba baada ya masaa machache ya mimi kupost habari hiyo hapo juu
Wakati Yanga wanarumbana na TFF na Bodi ya Ligi... Simba nao wamevaa darubini wakisubiri kanuni zivunjwe hili nao wagomee au wadai point tatu mezani....
Mechi hii ya tarehe 15 ikihairishwa inakuwa mechi ya 2 ya derby iliyoharishwa kwa Timu hizo hizo ndani ya msimu mmoja.
Ujumbe kutoka Simba baada ya masaa machache ya mimi kupost habari hiyo hapo juu