Simama uhesabiwe (New episode)

Simama uhesabiwe (New episode)

Malisa Godlisten

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2010
Posts
202
Reaction score
1,588
Sinema yetu inaitwa SAFARI YA MATUMAINI. Episode maarufu ni hii inayoendelea sasa, inaitwa SIMAMA UHESABIWE. Ktk Episode hii watu kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wanasafiri kwenda kuhesabiwa nyumbani kwa stelling wa movie hii.

Tayari masheikh wameshahesabiwa, wachungaji wa pentecoste wameshahesabiwa, wanafunzi wa UDOM nao wameshahesabiwa, na leo madereva bodaboda wameenda kuhesabiwa. Cha ajabu wote wanaoenda kuhesabiwa wanadai hawajuani wala hawana mawasiliano yoyote na stelling wa movie hii.

Yani wakati bodaboda wa Mbarali wanajiandaa kwenda kuhesabiwa leo, hawakujua kama wachungaji walihesabiwa jana. Na Masheikh wa Bagamoyo walipoenda kuhesabiwa hawakujua kama kesho yake wanafunzi wa UDOM wangehesabiwa. Yani kila kinachotokea kwenye movie hi ni incidence.!

Cha ajabu hata stelling wa movie hii hajui nani anakuja kuhesabiwa kesho yake. Jana alipomaliza kuwahesabu wachungaji hakujua kama leo wangeenda bodaboda. Ameshangaa tu hao.! Na kesho pia atashangaa wengine hao. Yani wanakuja tu. Hajawaandaa.. Hajaorganize ujio wao.. Yeye anashangaa tu haoo.! Hahahaah.. hii Episode tamu sana.

Unataka kujua kesho nani wataenda kuhesabiwa? Usikose kuungana nasi hapo kesho kwa sehemu nyingine ya movie hii ya kusisimua, "SIMAMA UHESABIWE". !

Wasalaam,
Malisa GJ.!
 
Haiingilii akilini hata kidogo hata eti wachungaji watoke huko walikotoka kwa wilaya tofauti moja akitokea Kiasarawe na mwingine akitokea Kiteto mwingine akitoke Muleba na sehemu nyingine wakaenda na wakakutana Dodoma kwa wakati mmoja kufika mbele wakamkuta Hamisi Mgeja yule Mwenyekiti wa CCM shinyanga na wote wakastaajabu eti wamefika kwa Lowassa na mabango na eti wote wamekuja kumsihi Lowasa kugombea Uraisi na Walimkuta mwenyeji wao tayari anawasuburi siku hiyo hakwenda kokote alijistukia amendaa pilau ya wageni ameweka na maturubai bila ya kuwa na taarifa za ujio huo, na akawa tayari kuwasikiliza bila hata ya kuwa na appointment. KWELI HUU NI MUUJIZA
 
Kesho anakwenda Ridhwani Kikwete, Makonda, Membe, Sitta, January Makamba ... Kila mmoja atapita kuhesabiwa ... Lazima wajue kuwa Edo alianza kujipanga mapema sana! hawa wenye kuvuta shuka asubuhi kwa nguvu za ESCROW wajue kuwa wameumia tu ...

Sinema yetu inaitwa SAFARI YA MATUMAINI. Episode maarufu ni hii inayoendelea sasa, inaitwa SIMAMA UHESABIWE. Ktk Episode hii watu kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wanasafiri kwenda kuhesabiwa nyumbani kwa stelling wa movie hii.

Tayari masheikh wameshahesabiwa, wachungaji wa pentecoste wameshahesabiwa, wanafunzi wa UDOM nao wameshahesabiwa, na leo madereva bodaboda wameenda kuhesabiwa. Cha ajabu wote wanaoenda kuhesabiwa wanadai hawajuani wala hawana mawasiliano yoyote na stelling wa movie hii.

Yani wakati bodaboda wa Mbarali wanajiandaa kwenda kuhesabiwa leo, hawakujua kama wachungaji walihesabiwa jana. Na Masheikh wa Bagamoyo walipoenda kuhesabiwa hawakujua kama kesho yake wanafunzi wa UDOM wangehesabiwa. Yani kila kinachotokea kwenye movie hi ni incidence.!

Cha ajabu hata stelling wa movie hii hajui nani anakuja kuhesabiwa kesho yake. Jana alipomaliza kuwahesabu wachungaji hakujua kama leo wangeenda bodaboda. Ameshangaa tu hao.! Na kesho pia atashangaa wengine hao. Yani wanakuja tu. Hajawaandaa.. Hajaorganize ujio wao.. Yeye anashangaa tu haoo.! Hahahaah.. hii Episode tamu sana.

Unataka kujua kesho nani wataenda kuhesabiwa? Usikose kuungana nasi hapo kesho kwa sehemu nyingine ya movie hii ya kusisimua, "SIMAMA UHESABIWE". !

Wasalaam,
Malisa GJ.!
 
Na wote wanajua kwamba kwasasa yupo nyumba yake ya Dodoma na si ya Dar wala Monduli pasipo mawasiliano kati yao.
 
Tushasema hizi riwaya za lowassa zikome humu ndani
 
Natabiri kesho Polisi nao wataebda kumtembelea...maana nao wana hali ngumu...mambo ya kuishi kwenye mabati tena!
 
Mimi niliona shida sana, wachungaji wetu wanapotakiwa kufika jimboni huwa sahani ya sadaka huwekwa kwa ajili ya kumchangia nauli mchungaji ili aweze kufanikisha safari, leo tunaambiwa amefika Dodoma bila sisi kujitolea kumchangia wala hakuanga kama atakuwa na safari, nimeamini lile kundi la wasabato masalia waliokaa airport DAR wakisema wanasubiri ndege itakayowapeleka ughaibuni kuhubiri walikuwa sahihi. Iweje wachungaji wetu leo wamesafiri bila kutuchangisha nauli?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom