Sikulaumu wewe, bali namwombea apumzike salama

Sikulaumu wewe, bali namwombea apumzike salama

Raelish

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2013
Posts
489
Reaction score
162
Hakuna kitu ambacho kinaweza kukuachia shida na dhiki duniani kama kifo. Nyota yangu ilianza kung'aa nikawa darasa la nne baada ya kupata wastani wa A katika mtihani wangu, nikiwa sina hata ndala miguuni, kaptura ya shule iliyochanika, shati kubwa chafu, dunia ikiwa inanicheka huku nikipata faraja kutoka kwa baba yangu na mama yangu.

Ni wazazi wangu waliokua wamezaa watoto wanne wakiwa wanategemea kilimo cha jembe la mkono ili kuendesha maisha, silaha yao kubwa ikiwa ni upendo kwa watoto wao na kuwapa matumaini kuwa Mungu lazima atukumbuke siku moja.

Mwaka 2001, kaka yangu wa pili, baada ya kumaliza elimu ya msingi na kufanikiwa kuchaguliwa kidato cha Kwanza , alishindwa kwenda kwa sababu alikosa ada, ndipo alipoamua kuaga rasmi nyumbani na kuelekea mjini.

Nilikuwa mdogo kipindi kile lakini niliweza kuhisi maumivu makali ndani ya moyo wake, "mdogo wangu Mungu amekujalia akili lakini amekunyima uwezo, sijui kama utafika mbali katika elimu yako ila usiache shule wala usikate tamaa, maana hatujui kesho itakuwaje".

Mbele ya wazazi wapendwa, mimi nikiwepo, aliaga rasmi asubuhi yake akawa ameondoka huku akiniaminisha kuwa yupo tayari akafanye anavyoweza kuhakiksha nasoma ili nikomboe familia. Nakumbuka nilimsindikiza hadi stendi nikamwacha pale huku akinipa tsh mia. Maisha yaliendelea; baada ya miaka mitatu nilikuwa darasa la saba.

Kaka yangu akiwa mjini, alipata kazi ya kuuza mbao kwa tajiri mmoja pale mjini, alikuwa anapata chochote ambacho kilisaidia kuendesha maisha yake. Kumbe alikuwa anakumbuka ahadi yake kwangu akawa anatunza kiasi cha pesa.

Mwaka 2004 nikawa darasa la saba nikafanikiwa kufahulu katika shule ya sekondari Kibaha. Kaka yangu aliposikia alifurahi sana, akawa amenitumia Tsh 120,000 na wazazi wakaongeza Tsh 40,000 nikawa nimefanikiwa kwenda kuanza kidato cha kwanza, kipindi kile headmaster ni S. M Kayenga.

Shule ilinipokea na kila mtu aliweza kuona wazi hali yangu duni, kutokana na umri wangu mdogo nikawa nashindwa kuhimili ile hali, mara nyingi machozi ndio yalikuwa faraja yangu. Nilisoma kwa miaka minne bila kurudi nyumbani na nilikuwa nabaki shuleni.

Shule ilikuwa na utaratibu wa kuwalipa wale waliokuwa wanabaki kwa makubaliano ya kufanya usafi katika mazingira ya shule wakati wote wa likizo hivyo kupitia hilo nikaweza kulipa ada ambayo ilikuwa Tsh 70,000 kwa mwaka.

Nilihitimu kidato cha nne na kufanikiwa kufaulu vizuri combination ya CBG, nikaenda kujiunga kidato cha tano katika shule moja ya mission chini ya msaada wa kaka yangu ambaye sasa angalau alikuwa na maisha mazuri kwa sababu aliamua kwenda Msumbiji kwenye mgodi na huko alifanikiwa sana.

Sijui nini kilitokea nikiwa form six mawasiliano na kaka yakawa yamekata kabisa, kwa kuwa nilikuwa mkubwa niliweza kumudu maisha. Kidato cha sita nilimaliza na sikufanya vizuri sana,

Pale nilikuwa nadaiwa ada hivyo sikuweza kutoka na cheti. Ndipo nilipoingia rasmi mtaani kupambana na maisha, baada ya miaka kama miwili nikawa nafundisha shule moja private kama form six leaver. Nikapata simu kutoka Msumbiji, ilikuwa ni sauti ya dada iliniambia kuwa kaka ni mgonjwa sana hivyo niwahi mpakani Newala nikampokee maana amewekwa kwenye lori moja la mizigo.

Sikujiuliza sana, nikawa nimeenda kwa boss wangu, akanipa pesa nikaanza safari kuelekea Newala, nilipofika Newala nikapokea simu nyingine iliyoniambia kuwa ndugu yako alishushwa hapa mpakani ila tumemuwahisha hospitali hivyo njoo hospitalini.

Nilipofika pale sikuamini nilichokiona; alikuwa ni braza wangu mpenzi, macho ameyafunika, mwili wote umeisha, nilishindwa kujizuia kulia kwa sauti ya uchungu sana. Ndiyo, ni uchungu uliokuwa unatoka ndani kabisa ya moyo wangu.

Baada ya siku chache alifariki, nililia sana nikaona kabisa mimi nimezaliwa kwa bahati mbaya, umri wangu mdogo yanayonikuta makubwa.

Basi tulizika. Muda wa wiki nzima nikawa nashinda kwenye kaburi nikiamini huenda anaweza akatoka ili niwahi kumshika mkono nimrudishe nyumbani, nikirudi kwenye kibarua changu.

Bosi nilimwomba anisaidie kunisomesha elimu ya chuo akakubali, mwaka jana kupitia NACTE nikaomba nikapata diploma ya medicine, yaani clinical officer. Nikajiunga na chuo mwaka jana mwezi wa kumi. Juzi nimepigiwa simu na yule mfadhili wangu kuwa anatakiwa kurudi kwao Ulaya.

Nimechanganyikiwa sana, nawaza labda angekuwepo kaka yangu angenisaidia. Machozi yamerudi tena, moyo wangu unazimia ndio maana nasema "sikulaumu wewe kifo ila namwombea kaka yangu apumzike salama". Mapenzi yake ya dhati yamebaki kuwa kwangu, namiss uwepo wake.

Kwanini dunia, nani alikulazimisha unspoken?? Mbona unanitesa hivi? Kweli walimwengu watalia na mimi?? Nani atanifuta machozi yangu? Nani atashiriki Nami kikombe hiki?

Naomba msaada kwa yeyote ambaye anaweza kunisaidia kwa namna yoyote.

Natanguliza shukrani za dhati.

=============

Mkuu Raelish,
Pole sana na matatizo, Mwenyezi Mungu akuwekee wepesi na upate nafuu haraka na kwa amani.

Naomba nichukue nafasi hii kwa kuomba radhi kwa kuchelewa kujibu, hasa kwa wale ambao walikuwa wamenishtua nihusike kwa namna moja ama nyingine. Nimeshawasiliana na Raelish kwa kutuma PM, ili atimize baadhi ya vielelezo ili iwe rahisi kujua ni msaada aina gani anahitaji na wa kiasi gani itusaidie sisi kama wanajamvi kukusanya kwa nguvu hiyo.

Nawashukuru na wale wote walio onyesha nia ya kutaka sana kusaidia. Mara baada ya kumaliza mawasiliano na Raelish nitatoa mrejesho mara moja ili tuendelee na nia ya kuwa msaada kwa kiasi fulani katika maisha yake. Maelezo zaidi yatakuja baada ya kujibiwa na Raelish. Asanteni.

Pamoja Sana!

=======

TAARIFA:

Uongozi wa JamiiForums umejiridhisha na kuafiki kwamba matatizo ya Raelish ni genuine. Hivyo basi, utaratibu wa kuchangia utafanyika kama ifuatavyo;

Kwa wale walioahidi msaada wa kifedha, na hata wasioahidi ila wameguswa na wangependa kushiriki kwenye hili, wanaweza kufanya hivyo kwa kutuma kiasi cha pesa kupitia M-PESA, Namba ya Simu: 0757 525 366 (Jina litakalotokea ni OBEDI MNZAVA).

Tunatanguliza shukrani za dhati kwa nyote mlioshiriki na mnaoendelea kushiriki katika zoezi hili.

- Majina ya walioahidi kuchangia mpaka sasa ni;
Julius Malema Jr Nyalotsi Mokoyo miss chagga Idimulwa Alinda Kipilipili Billie CLEMENCY Kitulo Rugaijamu dagii MTUSIASA rosebud Freeland Deogratius n niester


Wengine pia mnakaribishwa.

Uongozi wa JF unalisimamia jambo hili kwa karibu na kwa umakini sana mpaka mwisho wake. Na litakapofikia, basi mrejesho utaletwa hapa.

Asante.
 
Pole sana lakini usikate tamaa,

Tulia tafakari ni kwa namna gani kwa mazingira uliyopo waweza kufanya shughuli (hata kufulia wanzako nguo wakakulipa) ili uweze kupata pesa za kujikimu kama ulivyofanya kwa Kaselenge.

Je shirika alipo huyo mfadhili wako hawezi kushawishi ukaendelea kupata huo ufadhili?
 
Kachingwe kaselenge, sec master huyu alikuwa kipindi kile, yey alikuwa ananisaidia kama yeye. Nimejaribu kuwasiliana naye aniunganishe na shirika, aminijbu akijaribu kufanya hivyo hata kabla hajaanza kunisaidia lakini walisema hawana nafasi, ndipo akaamua kuanza kunisaidia akiamin baadae watakubali kunisaidia lakini ndo hivyo wamekataa.
 
daaaaah,..so sad,kuna kitu kimenigusa sana hapa,.....
 
Pole. Wewe ni wa imani gani? Pita kwenye nyumba za ibada za imani yako, watakusaidia.
 
Pole sana na mambo ya dunia. Sasa hebu eleza unahitaji msaada gani. Kuna wakati wa kuhuzunika na wakati wa maisha kuendelea. Huwa haisaidii kulalamika bila kuwa na action plan. Weka mchanganuo hapa ili tujue tunasaidia vipi.

ONYO: Tutapitia rekodi zote kabla ya kusaidia maana wajanja mjini wamekuwa wengi sana. Na tutaanika kila kitu hapa hapa JF. Karibu tafadhali.
 
Kitulo Inabidi aweke mchanganuo wa nini anahitaji.
 
Last edited by a moderator:
pole ila atakama anaondoka anaweza akaendelea kukutumia ada
na kakwa perfomance yako serkln ukiomba ata degree ya elim utaenda
piga moyo konde mshukuru Mungu ushapata elimu na una afya njema kuna watu wanateseka zaid
 
Pole sana na mambo ya dunia. Sasa hebu eleza unahitaji msaada gani. Kuna wakati wa kuhuzunika na wakati wa maisha kuendelea. Huwa haisaidii kulalamika bila kuwa na action plan. Weka mchanganuo hapa ili tujue tunasaidia vipi.

ONYO: Tutapitia rekodi zote kabla ya kusaidia maana wajanja mjini wamekuwa wengi sana. Na tutaanika kila kitu hapa hapa JF. Karibu tafadhali.

Umenena vema sana mkuu.
Nausubiri huo utaratibu, naahidi kusaidia pindi kila kitu kuhusu huyu bwana kitakapowekwa wazi.
 
Story yako imenitonesha madonda yaliyoanza kukauka.
Nakuombea kwa MUNGU MUUMBAJI, akupatie jawabu lakini kile alichokitaka kaka yako (may his soul rest in eternal peace) kifikie na kidumu kwako, familia yako na wote walokutana na changamoto kama zako.
 
Ahsanten sana, kwa kweli mmeonesha kuguswa na huzun yangu, msaada ninaohitaji sana ni ada ya chuo, ndo Kwanza nipo mwaka wa Kwanza ila ada yote ya mwaka wa Kwanza tayari amenilipia,.. kama kuna detail zozote muhim ambazo natakiwa niweke basi mseme tu niweke nini ili kuthibitisha ninachoongea kuwa ni kweli.

Naomben msaada wenu binadamu wenzangu, najua hakuna ambaye ametosheka ila naomba kile kidogo ulichonacho unikumbuke namim ambaye sikupenda kuwa omba omba, ni majaliwa tu ya Mungu,.

"SIKULAUMU WEWE BALI NAMWOMBEA APUMZIKE SALAMA" kaka angu huko ulipo mdogo wako umeniachia giza, ni giza kinene kaka yangu.... Siwez kukufuru kwamb bora nkufuate........ Nakumbuka maneno yako kaka............. Zidi kuniombea nyota yangu ing'ae, nakupenda sana,,, RIP
 
Pole sana na mambo ya dunia. Sasa hebu eleza unahitaji msaada gani. Kuna wakati wa kuhuzunika na wakati wa maisha kuendelea. Huwa haisaidii kulalamika bila kuwa na action plan. Weka mchanganuo hapa ili tujue tunasaidia vipi.

ONYO: Tutapitia rekodi zote kabla ya kusaidia maana wajanja mjini wamekuwa wengi sana. Na tutaanika kila kitu hapa hapa JF. Karibu tafadhali.

Ndiyo, niweke zipi zingine ndugu yang, naomba mwongozo wako. Samahan na ahsante sana kwa kuonesha unaguswa na matatizo yangu. Ni kweli kuhuzunika tu haisaidii ila ndo hivyo udhaifu wa moyo.
 
Ahsanten sana, kwa kweli mmeonesha kuguswa na huzun yangu, msaada ninaohitaji sana ni ada ya chuo ambayo ni Tsh 2,595,400 kwa mwaka, ndo Kwanza nipo mwaka wa Kwanza ila ada yote ya mwaka wa Kwanza tayari amenilipia, chuo kinaitwa St bakhita,... Namba yangu ya simu ni 0763223724.... kama kuna detail zozote muhim ambazo natakiwa niweke basi mseme tu niweke nini ili kuthibitisha ninachoongea kuwa ni kweli. Naomben msaada wenu binadamu wenzangu, najua hakuna ambaye ametosheka ila naomba kile kidogo ulichonacho unikumbuke namim ambaye sikupenda kuwa omba omba, ni majaliwa tu ya Mungu,. "SIKULAUMU WEWE BALI NAMWOMBEA APUMZIKE SALAMA" kaka angu huko ulipo mdogo wako umeniachia giza, ni giza kinene kaka yangu.... Siwez kukufuru kwamb bora nkufuate........ Nakumbuka maneno yako kaka............. Zidi kuniombea nyota yangu ing'ae, nakupenda sana,,, RIP
Toa jina full la chuo ...majina yako full unayotumia chuoni. .namba za mawasiliano za chuo na akaunti namba ya chuo na majina yote ya mkuu wa chuo...usituelewe vbaya matapeli ni wengi mjini wadau apa ni wengi tutachanga usome kutoa ni moyo si utajiri ata Mungu anasema tumjaribu kwa matoleo wadau tumsaidie mwenzetu baada ya kujiridhsha
 
Sure,guys kwatulio guswa tumchangie jamaa jamani
 
Back
Top Bottom