Chagu wa Malunde
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 8,708
- 5,711
Naandika hivi ni kwa sababu Mh Rais unapokuwa katika ziara zako hapo ndipo kero za wananchi huibuliwa na kutatuliwa.
Maana wengi wa wasaidizi wako ni kama hawana msaada kwa wananchi. Misafara yako inaposimama kila mahali hapo ndipo akina mama na wazee walioonewa na kudhulumiwa huwa unawasaidia.
Mfano yule mama kule Kahama aliwatoa machozi watu mume wake aligongwa na trafiki lakini hakuna msaada aliokuwa ameupata mpaka msafara wako uliposimama.
Pia ulipofanya ziara Butimba prison ulimsaidia Kulwa aliyebambikiwa kesi ya mauaji. Sasa tunakuomba umalize likizo maana sikukuu zimeisha ili wananchi waje waibue kero zao kila utapopita.
Pia hata Mh Kassim naye amekuwa kimya kiasi cha wateule ambao wamejisahau kujisahau zaidi.
Hivyo tunakuomba urudi uwanjani ili usaidie wanyonge. Kwa ujumla watu wanaona ma-DC na ma-RC hawatatui kero za wananchi mpaka waone kuna ziara yako au ya Waziri Mkuu.
Maana wengi wa wasaidizi wako ni kama hawana msaada kwa wananchi. Misafara yako inaposimama kila mahali hapo ndipo akina mama na wazee walioonewa na kudhulumiwa huwa unawasaidia.
Mfano yule mama kule Kahama aliwatoa machozi watu mume wake aligongwa na trafiki lakini hakuna msaada aliokuwa ameupata mpaka msafara wako uliposimama.
Pia ulipofanya ziara Butimba prison ulimsaidia Kulwa aliyebambikiwa kesi ya mauaji. Sasa tunakuomba umalize likizo maana sikukuu zimeisha ili wananchi waje waibue kero zao kila utapopita.
Pia hata Mh Kassim naye amekuwa kimya kiasi cha wateule ambao wamejisahau kujisahau zaidi.
Hivyo tunakuomba urudi uwanjani ili usaidie wanyonge. Kwa ujumla watu wanaona ma-DC na ma-RC hawatatui kero za wananchi mpaka waone kuna ziara yako au ya Waziri Mkuu.