Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,190
- 34,526
- Thread starter
- #21
RIWAYA: SIKUJUA UNGENISALITI MPENZI (17)
MTUNZI: JOSEPH SHALUWA
SIMU: 0762 458590
EMAIL: joeshaluwa@gmail.com
FACEBOOK: Joseph Shaluwa
INSTAGRAM: josephshaluwa
Dulla akatoka nje haraka, kisha akampigia mbinja Bruno, ambaye alisimama, akiwa hatua chache kabisa kabla ya kulifikia geti la akina Bryson. Akamfinyia mkono akiashiria kwamba anamwita, Bruno akamfuata.
“Vipi?” Bruno akauliza.
“Wewe si una usafiri?”
“Ndiyo!”
“Nakuomba sana, hebu tuondoke kwanza maeneo haya, halafu nizungumze na wewe kuhusu huyo Bryson unayemtafuta!”
“Kwani vipi?”
“Nisikilize mimi!”
Bruno hakubisha zaidi, akaongozana naye hadi kwenye gari, wakaingia na kurudi hadi mjini kabisa. Wakaachana na dereva taxi, wakaingia kwenye baa moja na kuagiza vinywaji.
“Wewe ni ndugu yangu kaka, huyo Bryson unayemtafuta ni tapeli, sasa nimeona ni vyema nikueleze mapema ili kama ni mambo ya pesa uachane naye kabisa!”
“Ni tapeli?”
“Tena mkubwa!”
“Mungu wangu!”
“Kwani vipi, kuna pesa yoyote uliyompa?”
“Ndiyo...”
“Shilingi ngapi?”
“Milioni tano na hapa nilikuwa nampelekea nyingine moja!”
“Za nini sasa?”
“Alinifumania na mkewe!”
“Mungu wangu, hana mke yule, mke mwenyewe ni nani?”
“Ni...”
Bruno akaanza kusimulia kisa kizima, jinsi alivyokutana na Tunu kwa mara ya kwanza na jinsi alivyofumaniwa na Bryson akiwa na wenzake na kusema kwamba ni mkewe!
“Kaka umeibiwa...kwanza kama ni mkewe, kwanini haishi naye? Na hata pale siyo kwake ila huwa anakwenda mara nyingi, huyo Tunu mwenyewe unayemsema ni tapeli sugu, yaani umeibiwa ndugu yangu, lakini bora hiyo moja imebaki!”
“Sasa utanisaidiaje ndugu yangu?”
“Nenda Polisi, chukua askari uende nao pale, unaweza kumkamata maana alikuwa pale!”
“Sawa, nisaidie basi kaka!”
“Twende Chumbageni.”
“Poa.”
Wakatoka na kuachana na kila kitu pale baa, wakaenda zao katika Kituo Kikuu cha Polisi Chumbageni.
***
“Oyaaa wazee dili limebuma!” Bryson alikuwa akiwaambia wenzake.
“Kivipi?”
“Yule boya, atakuja na Polisi muda si mrefu, kuna mjinga-mjinga ameshaunguza picha!”
“Sasa?”
“Sasa nini? Kila mtu si ameshapata mgawo wake, hapa ni kujichenga tu, mimi hapa ni buti hadi Dar, Tanga si mahali salama tena kwangu!”
“Poa, mimi natambaa zangu Korogwe,” mwingine akadakia.
“Mie Moshi.”
Ndani ya nusu saa, kila mmoja alikuwa kwenye basi kwa safari ya kwenda sehemu aliyoona inafaa kujificha.
***
Gari lililojaa maaskari liliingia maeneo ya Sahare kwa kasi sana asubuhi hiyo, wakatafuta kwenye ile nyumba lakini hawakuwepo. Bruno akatoa wazo, kwamba waende Mabawa anapoishi Tunu, huko ndipo kulikuwa na vichekesho!
Tunu alikuwa amehama tangu usiku wa kuamkia siku ile.
“Amehamia wapi?” Mmoja wa askari wale akauliza.
“Alisema anahama mkoa kabisa.”
“Anakwenda wapi?”
“Arusha!”
“Arusha?!” Bruno akauliza bila kutarajia.
Akaketi chini na kuanza kulia kwa uchungu! Si fedha zote kati ya zile alizowapa akina Bryson zilikuwa zake, pale alikuwa na milioni moja na laki mbili tu! Zingine zilikuwa za kampuni. Tayari alishaona amepata hasara kubwa tena bila sababu.
“Usilie nyamaza, kulia hakutakusaidia kitu kama hatutabuni mbinu za kuwatia mikononi mwa dola kwanza!”
Maneno yale hayakuwa tiba yoyote kwa Bruno, tena ndiyo yalizidi kumwongezea simazi moyoni mwake. Hapakuwa na msaada zaidi kutoka kwa maaskari wale, hivyo akaachana nao, yeye na Dulla wakarudi kijiweni. Wakapata taarifa kwamba Bryson amekimbilia Dar.
“Sehemu gani?” Bruno akamwuliza kijana aliyemwambia.
“Usinitaje lakini!”
“Usijali, itakuwa siri.”
“Kwao ni Ilala-Bungoni, ni maarufu sana, kuna duka moja la spea za pikipiki linaitwa G8, kwenye kituo cha daladala, pale ndiyo kijiweni kwake, akishaharibu huku anakimbilia kule, anatulia mpaka soo likipungu anarudi!”
“Ahsante sana mzee, lazima niende Dar leo leo!” Bruno akamwambia Dulla.
“Dar?”
“Ndiyo!”
“Unadhani utampata?”
“Naamini hivyo!”
Jioni ile ile, Bruno alipanda basi la Raha Leo na kwenda Dar es Salaam, hakumuaga mtu yeyote zaidi ya Dulla. Wafanyakazi wenzake aliotoka nao Mwanza hakutaka kuwaeleza juu ya kilichotokea. Alifika Dar usiku wa saa tatu na dakika zake.
Hakuwa mgeni wa jiji, kwahiyo aliamua kuchukua daladala za Kariakoo, akashuka Magomeni – Usalama. Akatembea kwa miguu hadi kwenye mataa na kwenda kwenye kituo cha Magomeni - Kanisani.
Hazikupita dakika tatu, daladala iliyotoka Kawe kuelekea Buguruni ilipita. Bruno akaingia na kutulia kwenye siti. Akashuka kituo cha Bungoni akiwa amechoka sana. Zoezi la kwanza kufanya ni kuangalia lile duka la spea za pikipiki la G8 alilokuwa ameelekezwa.
Hakuchukua muda mrefu sana alifanikiwa kuliona, maana lilikuwa barabari kabisa. Hata hivyo lilikuwa limefungwa!
“Ok! Sasa nimeshajua pa kuanzia, ninachotakiwa kufanya hapa kwanza ni kutafuta mahali pa kulala, halafu mambo mengine yatafuata baadaye,” aliwaza Bruno akiondoka pale Bungoni.
Akachepuka kwenye mitaa miwili mitatu, kisha akaona gesti moja nzuri iliyomvutia. Akaingia na kulipa, akaenda chumbani kwake. Kwanza alioga, kisha akatoka nje kutafuta chakula, baadaye akarudi na kulala. Kitu kimoja kikiutawala ubongo wake; kumpata Bryson!
***
Saa mbili kamili za asubuhi Bruno alikuwa yupo kwenye soko la Mchikichini, Ilala – Boma, kazi kubwa iliyompeleka pale ilikuwa ni kutafuta jaketi na kofia. Aliponunua vitu hivyo, akavaa pale pale. Akaona bado kuna upungufu kidogo, akanunua miwani ya jua na kuvaa.
“Yes, hapa hawezi kunitambua,” akawaza akianza kutembea kwa miguu taratibu kuelekea kwenye mataa ya Boma.
Alitembea taratibu hadi Bungoni, akakaa kwenye Grocery moja iliyokuwa upande wa pili, akaanza kunywa bia zake taratibu huku macho yake yakiwa yanaangalia pale kwenye duka la spea.
Hadi kufikia saa saba mchana, bado hakumuona Bryson akitokea. Hilo likazidi kumuumiza sana kichwa chake. Muda wa kula ukafika, akala lakini bado hakufanikiwa kumuona. Alijua wazi kwamba hakutakiwa kumuulizia, kwani kwa kufanya hivyo asingeweza kumpata!
Saa tisa za alasiri akaamua kurudi zake chumbani kwake. Akaoga na kulala kidogo, saa kumi na mbili akatoka na kwenda moja kwa moja hadi kwenye duka la spea. Akajongea taratibu hadi dirishani.
“Habari yako brother?” Bruno akamsalimia.
“Poa, shwari?”
“Nipo poa.”
“Niambie kaka, unahitaji nini?”
“Samahani nina ndugu yangu namuulizia!”
“Nani?”
“Anaitwa Bryson, ni mjomba wangu!”
“Huna simu yake?”
“Nimepoteza!”
“Kwani wewe unatokea wapi?”
“Morogoro.”
“Hebu eleza ukweli kidogo bwana, ni ndugu yako au una ishu naye?”
“Hapana ni ndugu yangu, kama nilivyokuambia ni Anko wangu!”
“Kwanini umekuja kuulizia hapa?”
“Yeye mwenyewe aliniambia kwamba hapa ndiyo kijiweni kwake.”
Bruno alikuwa makini sana kujibu maswali ya yule mhudumu kwa umakini mkubwa ili aweze kumweleza ukweli. Yule kaka akamwangalia kwa muda akiwa kimya kabisa. Ni kama alikuwa akijifunza vitu fulani kupitia macho yake.
“Sikia...wewe ni mwenyeji sana hapa Dar?”
“Siyo sana, lakini kidogo naijua mitaa.”
“Unajua Club ya Wazee.”
“Hapana, iko wapi?”
“Utavuka barabara hapo, halafu pandisha nayo moja kwa moja, utaona miti mingi ya mijohoro kushoto kwako, hapo ndiyo Club ya Wazee!”
“Enhee!”
“Tangu jana Bryson amekuwa akishinda pale akinywa na marafiki zake.”
“Ok! Kaka nashukuru sana, ngoja niende,” Bruno akasema akiondoka taratibu akifuata maelekezo aliyopewa.
MTUNZI: JOSEPH SHALUWA
SIMU: 0762 458590
EMAIL: joeshaluwa@gmail.com
FACEBOOK: Joseph Shaluwa
INSTAGRAM: josephshaluwa
Dulla akatoka nje haraka, kisha akampigia mbinja Bruno, ambaye alisimama, akiwa hatua chache kabisa kabla ya kulifikia geti la akina Bryson. Akamfinyia mkono akiashiria kwamba anamwita, Bruno akamfuata.
“Vipi?” Bruno akauliza.
“Wewe si una usafiri?”
“Ndiyo!”
“Nakuomba sana, hebu tuondoke kwanza maeneo haya, halafu nizungumze na wewe kuhusu huyo Bryson unayemtafuta!”
“Kwani vipi?”
“Nisikilize mimi!”
Bruno hakubisha zaidi, akaongozana naye hadi kwenye gari, wakaingia na kurudi hadi mjini kabisa. Wakaachana na dereva taxi, wakaingia kwenye baa moja na kuagiza vinywaji.
“Wewe ni ndugu yangu kaka, huyo Bryson unayemtafuta ni tapeli, sasa nimeona ni vyema nikueleze mapema ili kama ni mambo ya pesa uachane naye kabisa!”
“Ni tapeli?”
“Tena mkubwa!”
“Mungu wangu!”
“Kwani vipi, kuna pesa yoyote uliyompa?”
“Ndiyo...”
“Shilingi ngapi?”
“Milioni tano na hapa nilikuwa nampelekea nyingine moja!”
“Za nini sasa?”
“Alinifumania na mkewe!”
“Mungu wangu, hana mke yule, mke mwenyewe ni nani?”
“Ni...”
Bruno akaanza kusimulia kisa kizima, jinsi alivyokutana na Tunu kwa mara ya kwanza na jinsi alivyofumaniwa na Bryson akiwa na wenzake na kusema kwamba ni mkewe!
“Kaka umeibiwa...kwanza kama ni mkewe, kwanini haishi naye? Na hata pale siyo kwake ila huwa anakwenda mara nyingi, huyo Tunu mwenyewe unayemsema ni tapeli sugu, yaani umeibiwa ndugu yangu, lakini bora hiyo moja imebaki!”
“Sasa utanisaidiaje ndugu yangu?”
“Nenda Polisi, chukua askari uende nao pale, unaweza kumkamata maana alikuwa pale!”
“Sawa, nisaidie basi kaka!”
“Twende Chumbageni.”
“Poa.”
Wakatoka na kuachana na kila kitu pale baa, wakaenda zao katika Kituo Kikuu cha Polisi Chumbageni.
***
“Oyaaa wazee dili limebuma!” Bryson alikuwa akiwaambia wenzake.
“Kivipi?”
“Yule boya, atakuja na Polisi muda si mrefu, kuna mjinga-mjinga ameshaunguza picha!”
“Sasa?”
“Sasa nini? Kila mtu si ameshapata mgawo wake, hapa ni kujichenga tu, mimi hapa ni buti hadi Dar, Tanga si mahali salama tena kwangu!”
“Poa, mimi natambaa zangu Korogwe,” mwingine akadakia.
“Mie Moshi.”
Ndani ya nusu saa, kila mmoja alikuwa kwenye basi kwa safari ya kwenda sehemu aliyoona inafaa kujificha.
***
Gari lililojaa maaskari liliingia maeneo ya Sahare kwa kasi sana asubuhi hiyo, wakatafuta kwenye ile nyumba lakini hawakuwepo. Bruno akatoa wazo, kwamba waende Mabawa anapoishi Tunu, huko ndipo kulikuwa na vichekesho!
Tunu alikuwa amehama tangu usiku wa kuamkia siku ile.
“Amehamia wapi?” Mmoja wa askari wale akauliza.
“Alisema anahama mkoa kabisa.”
“Anakwenda wapi?”
“Arusha!”
“Arusha?!” Bruno akauliza bila kutarajia.
Akaketi chini na kuanza kulia kwa uchungu! Si fedha zote kati ya zile alizowapa akina Bryson zilikuwa zake, pale alikuwa na milioni moja na laki mbili tu! Zingine zilikuwa za kampuni. Tayari alishaona amepata hasara kubwa tena bila sababu.
“Usilie nyamaza, kulia hakutakusaidia kitu kama hatutabuni mbinu za kuwatia mikononi mwa dola kwanza!”
Maneno yale hayakuwa tiba yoyote kwa Bruno, tena ndiyo yalizidi kumwongezea simazi moyoni mwake. Hapakuwa na msaada zaidi kutoka kwa maaskari wale, hivyo akaachana nao, yeye na Dulla wakarudi kijiweni. Wakapata taarifa kwamba Bryson amekimbilia Dar.
“Sehemu gani?” Bruno akamwuliza kijana aliyemwambia.
“Usinitaje lakini!”
“Usijali, itakuwa siri.”
“Kwao ni Ilala-Bungoni, ni maarufu sana, kuna duka moja la spea za pikipiki linaitwa G8, kwenye kituo cha daladala, pale ndiyo kijiweni kwake, akishaharibu huku anakimbilia kule, anatulia mpaka soo likipungu anarudi!”
“Ahsante sana mzee, lazima niende Dar leo leo!” Bruno akamwambia Dulla.
“Dar?”
“Ndiyo!”
“Unadhani utampata?”
“Naamini hivyo!”
Jioni ile ile, Bruno alipanda basi la Raha Leo na kwenda Dar es Salaam, hakumuaga mtu yeyote zaidi ya Dulla. Wafanyakazi wenzake aliotoka nao Mwanza hakutaka kuwaeleza juu ya kilichotokea. Alifika Dar usiku wa saa tatu na dakika zake.
Hakuwa mgeni wa jiji, kwahiyo aliamua kuchukua daladala za Kariakoo, akashuka Magomeni – Usalama. Akatembea kwa miguu hadi kwenye mataa na kwenda kwenye kituo cha Magomeni - Kanisani.
Hazikupita dakika tatu, daladala iliyotoka Kawe kuelekea Buguruni ilipita. Bruno akaingia na kutulia kwenye siti. Akashuka kituo cha Bungoni akiwa amechoka sana. Zoezi la kwanza kufanya ni kuangalia lile duka la spea za pikipiki la G8 alilokuwa ameelekezwa.
Hakuchukua muda mrefu sana alifanikiwa kuliona, maana lilikuwa barabari kabisa. Hata hivyo lilikuwa limefungwa!
“Ok! Sasa nimeshajua pa kuanzia, ninachotakiwa kufanya hapa kwanza ni kutafuta mahali pa kulala, halafu mambo mengine yatafuata baadaye,” aliwaza Bruno akiondoka pale Bungoni.
Akachepuka kwenye mitaa miwili mitatu, kisha akaona gesti moja nzuri iliyomvutia. Akaingia na kulipa, akaenda chumbani kwake. Kwanza alioga, kisha akatoka nje kutafuta chakula, baadaye akarudi na kulala. Kitu kimoja kikiutawala ubongo wake; kumpata Bryson!
***
Saa mbili kamili za asubuhi Bruno alikuwa yupo kwenye soko la Mchikichini, Ilala – Boma, kazi kubwa iliyompeleka pale ilikuwa ni kutafuta jaketi na kofia. Aliponunua vitu hivyo, akavaa pale pale. Akaona bado kuna upungufu kidogo, akanunua miwani ya jua na kuvaa.
“Yes, hapa hawezi kunitambua,” akawaza akianza kutembea kwa miguu taratibu kuelekea kwenye mataa ya Boma.
Alitembea taratibu hadi Bungoni, akakaa kwenye Grocery moja iliyokuwa upande wa pili, akaanza kunywa bia zake taratibu huku macho yake yakiwa yanaangalia pale kwenye duka la spea.
Hadi kufikia saa saba mchana, bado hakumuona Bryson akitokea. Hilo likazidi kumuumiza sana kichwa chake. Muda wa kula ukafika, akala lakini bado hakufanikiwa kumuona. Alijua wazi kwamba hakutakiwa kumuulizia, kwani kwa kufanya hivyo asingeweza kumpata!
Saa tisa za alasiri akaamua kurudi zake chumbani kwake. Akaoga na kulala kidogo, saa kumi na mbili akatoka na kwenda moja kwa moja hadi kwenye duka la spea. Akajongea taratibu hadi dirishani.
“Habari yako brother?” Bruno akamsalimia.
“Poa, shwari?”
“Nipo poa.”
“Niambie kaka, unahitaji nini?”
“Samahani nina ndugu yangu namuulizia!”
“Nani?”
“Anaitwa Bryson, ni mjomba wangu!”
“Huna simu yake?”
“Nimepoteza!”
“Kwani wewe unatokea wapi?”
“Morogoro.”
“Hebu eleza ukweli kidogo bwana, ni ndugu yako au una ishu naye?”
“Hapana ni ndugu yangu, kama nilivyokuambia ni Anko wangu!”
“Kwanini umekuja kuulizia hapa?”
“Yeye mwenyewe aliniambia kwamba hapa ndiyo kijiweni kwake.”
Bruno alikuwa makini sana kujibu maswali ya yule mhudumu kwa umakini mkubwa ili aweze kumweleza ukweli. Yule kaka akamwangalia kwa muda akiwa kimya kabisa. Ni kama alikuwa akijifunza vitu fulani kupitia macho yake.
“Sikia...wewe ni mwenyeji sana hapa Dar?”
“Siyo sana, lakini kidogo naijua mitaa.”
“Unajua Club ya Wazee.”
“Hapana, iko wapi?”
“Utavuka barabara hapo, halafu pandisha nayo moja kwa moja, utaona miti mingi ya mijohoro kushoto kwako, hapo ndiyo Club ya Wazee!”
“Enhee!”
“Tangu jana Bryson amekuwa akishinda pale akinywa na marafiki zake.”
“Ok! Kaka nashukuru sana, ngoja niende,” Bruno akasema akiondoka taratibu akifuata maelekezo aliyopewa.