barafuyamoto
JF-Expert Member
- Jul 26, 2014
- 32,405
- 29,811
Kuna watu wanamuita huyu bashe eti mzalendo, mzalendo bashe???
Yaani nawe unajiita mzalendo????Kuna watu wanamuita huyu bashe eti mzalendo, mzalendo bashe???
This is Stupid....Ukweli ni jambo zuri sana kulisema, lakini uzalendo ni kitu bora zaidi kuliko kitu chochote kile.
Hussein Bashe wewe uko ndani ya CCM na ajabu wewe unaongoza kwa kuiponda CCM kuliko hata ambavyo unaviponda vyama vya upinzani. Katika siasa tabia kama hii haikubaliki hata kidogo.
Wana CCM tumekuwa tukikufuatilia kwa karibu sana, na matamko yako, yanaonesha wazi kabisa wewe siyo mzalendo kwa chama chako kilichokulea mpaka kukufikisha hapo ulipofika.
Inawezekana madai yako yakawa na ukweli ama la; lakini namna unavyoyawasilisha na mahali unapoyawasilisha siyo sahihi hata kidogo. Sidhani kama Mwenyekiti ataendelea kukuvumilia. Mimi nikiwa kama mwanachama wa CCM nimekerwa sana na matamshi yako unayoyatoa bungeni. Acha kutafuta cheap publicity!
Bashe wewe ni msaliti, tena inaonekana unatumiwa na CHADEMA sababu ulikuwa swahiba wa Lowassa. You are a traitor! You are a mole and you have to be removed!
Nakushauri Mwenyekiti wangu mpendwa na Rais wetu, ndugu John Pombe Magufuli, muondoe haraka sana huyu kijana ndani ya chama chetu sababu sasa ameshaota MAPEMBE. Bashe ni hatari sana kwa mustakabali wa chama chetu (CCM).
Hakuna chama chochote kile cha siasa hapa Tanzania ambacho kingemvumilia mwanachama kama BASHE! Mifano ipo mingi sana.
Mbaya zaidi anayoyaongea Bashe bungeni hayana faida yoyote ile kwa wananchi wa jimbo lake! Kazi yako Bashe ni kuwawakilisha wapiga kura wa NZEGA na siyo kupigana na CCM na serikali yake!
Mheshimiwa Rais; naomba uunde kamati maalumu ndani ya CCM kwa ajili ya kumchunguza huyu bwana mdogo. Anakoelekea siko kabisa na hatufai tena ndani ya chama chetu.
Mimi nina uhakika wa 90% hata kama tukimfukuza uanachama huyu msaliti BASHE, jimbo la NZEGA bado tutalichukua. Wakati ni sasa!
By Son of Gamba.
hio ccm itabaki na wasukuma tu msipoangalia....na bashite...Nyerere alitabiri upinzani wa kweli utatoka ndani ya ccm yenyewe hivyo wakati umefika wa utabiri ccm inakatika vipande vipande .....na upinzani kuanza rasmiShida yangu ni Bashe anajipendekeza kwa wapinzani na kukidhoofisha chama chetu. Bashe ni msaliti wa chama.
Sijamwona mtu hapo. Hapo kila mmoja anatetea maslahi yake binafsi.hio ccm itabaki na wasukuma tu msipoangalia....na bashite...Nyerere alitabiri upinzani wa kweli utatoka ndani ya ccm yenyewe hivyo wakati umefika wa utabiri ccm inakatika vipande vipande .....na upinzani kuanza rasmi
Kama "BABA MUNGU" ni mjomba wako, basi itakuwa hivyo.
Lakini kama BABA MUNGU ni wetu sote, basi nasema, "USHINDWE KWA JINA LA YESU KRISTO!
Duh, hivi wazalendo wamekwisha hapa nchini hadi kumuorodhesha Bashe! Waulize akina Kubenea, Ndimara na Absolom Kibanda, hata ndugu wa marehemu Dan Mwakiteleko (Apumzike kwa Amani) watakwambia Bashe ni nani kwao na kwa Rostam Aziz.Huenda ukawa unamuona si mfia chama, lkn sie tunamuona ni mzalendo kwa nchi yake.
Hivi kila anayetamka maneno yake kutokana na hisia zake binafsi tayari anakuwa mshauri, tena wa kiwango cha kumshauri Mkuu wa Nchi na Serikali (dola)? haya ni mkubwa. Ukishauri ukaona umekuwa ignored basi tambua kuwa hujafikia hadhi hiyo.washauri