Siku yangu ya kwanza kujiunga JF nilidhani haya

Nilidhani kuwa google ndio JF maana kabla sijaijua JF, nilikuwa kila nikiuliza swali Google, majibu yake yalikuja kwa kumalizia na link ya JF(maana nilikuwa najibiwa na members waliowahi kuchangia kwa majibu yao nayona nikiwa huko huko google hata kama mimi siyo member). nilijua ili nipate jibu la uhakika nilikuwa kama nauliza mbinu za kuwa tajiri namalizia na JF mwishoni mwa swali langu... hali hii ilinifanya niipende JF kuanzia hapo!
 
Mimi wakati naingia JF mwaka 2009 niliambiwa kwamba kila kinachosemwa humu vingi ni ukweli, tena ukweli usiopatikana magazetini.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa ingawa hapa katikati kuliingia vihabari vya uongo kuvunja sifa hii lakini bado kuna ukweli mwingi wa mambo mengi yanayosemwa humu.

 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…