FaizaFoxy
Well said
faiza foxy, so does
lara 1.
mie swla la wanawake naliona kwa namna tofauti zaid. leo sijaweza kupitia kauli mbiu ya siku ya wanawake na kuifahamu lkn nimejikuta naiikumbuka kauli mbiu isemayo
"tukiwezeshwa tunaweza"
binafsi kauli hii ni ya unyanyasaji hasa wa kijinsia manake ni wazi kwamba kama amekuwezesha basi ndiye aliyeweza na sio wewe uliyewezeshwa uliyeweza.
nikiongelea wanawake naongelea wale ambao wana hustle kusaka maji safi kwa matumizi ya ndani ambao hutumia muda zaid ya nusu siku kusaka ndoo moja ya maji, na akirudi nyumban baba anamtizama kama amepika ama laa na bado usiku anahitaj huduma.
nawafikiria zaid wanwake ambao hawana namna ya kujitetea kwasababu ya elimu, jukwaa la kuongelea, na uwezo wa kusikika ambao wao kwanafasi yao hutumia muda wao kujishughulisha na kazi za kuongeza kipato na wanapovuna baba ndiye humiliki mapato ya familia na ndiye muamuzi wa mwisho.
mwanamke huyu anashindw akuwa na maamuzi juu ya kipato chake, ailisheje familia yake awavesheje mwisho wa siku baba hupanga bajeti kubwa kwajili ya kilabuni na bajeti finyu kwaajili ya mahitaji ya familia.
na imagine mwanamke huyu ndiye ambaye watoto wake wanaugua kiseyeye, mwanamke huyu ndiye ambaye hana uwezo wa kuuguza ndg zake kisa kipato kidogo nk.
hivi mwanamke huyu wanawake wengine wanamsaidiaje? hivi hata tukipanga kwenye ofc zetu huduma zetu za kijamii huwa tunawafikiria hawa kwenye hiyo mipango? je kama wanawake wenye ushawishi twawezaje kuwafanya wenzetu wanufaike zaid na huduma zetu?
natamani kuona, wanawake walioko kwenye ngazi za maamuzi wakiwa na malengo madhubuti juu ya mahitaj ya wanawake wengine wasiokuwa na nafasi hiyo. natamani kuona mwanamke aliyeko na maamuzi kwenye upatikanaji wa maji anatoa priority kwa mwanamke mwenzie kupata maji na anakuwa na mipango ya kuhakikisha mwanamke huyu anayapata, kadhalika aliyeko kwenye afya, elimu, ustawi wa jamii, nk
siku kama hii iwe ni changamoto ya kuwakumbusha wanawake watoa maamuzi jinsi ya kupanga mipango ya kazi zao ikilenga kuwa na matunda mazuri zaid kwa wanawake wasiokuwa na uwezo kama wao.
zamani niliwah kudhani kwamba watu wote wana access na kila wanachokitaka kumbe nilikuwa sijui. kiukweli kuna wanawake wanaishi maisha magumu sana ambayo hata kuyawaza unashindwa. wapo ambao hata raha ya haya maisha unaweza kusema hawana ama hawaijui. ni changamoto sana.