Nina Bible hapa nilipo naomba unitajie mstari unasema SABATO NI SIKU YA JUMAMOSI, ninyi watu ni wapotoshaji wakubwa. Na mlio wengi ni WANAFIKI mlioshindikana. Soma Bible vizuri uijue kweli nayo kweli itakuweka huru, acheni kufungwa fikra na mtu mmoja.
Nasubiri huo mstari mkuu.
UNAIKUBALI PASAKA ,IJUMAA KUU, ALHAMIS KUU, NA DOMINICA
ILA UNAJIFANYA HUJUI SABATO NI LINI
UNAFUNDISHWA NA PADRI YESU ALIFUFUKA JUMAPILI SIKU YA KWANZA YA JUMA ,ILA UNAJIFANYA HUJUI SIKU YA 7 NI LINI
WANAFIKI WAKUBWA NYIE
Katekisimo ya kanisa Katoliki la Roma inasomeka hivi:
"Swali: Ipi ndiyo siku ya Sabato?
"Jibu: Jumamosi ndiyo siku ya Sabato.
"Swali: Kwa nini sisi tunaitunza Jumapili badala ya Jumamosi?
"Jibu: Tunaitunza Jumapili badala ya Jumamosi kwa sababu kanisa Katoliki …. Liliihamisha ibada toka Jumamosi kwenda Jumapili".
- Peter Geirmannn, The Convert's Catechism of Catholic Doctrine (toleo la 1957). Uk. 50.
Kwa majivuno kanisa Katoliki linatangaza kwamba viongozi wa kanisa ambao ni wanadamu tu ndio waliofanya badiliko hilo.
"Siku ile takatifu, yaani, Sabato, ilibadilishwa kutoka Jumamosi kwenda Jumapili... si kutokana na maagizo yo yote yaliyoonekana katika Maandiko bali kutokana na hisia ya kanisa kwamba linao uwezo wake lenyewe… watu wale wanaofikiri kwamba Maandiko ndiyo yangekuwa mamlaka peke yake, kwa mantiki hiyo, ingewapasa kuwa Waadventista Wasabato , nao wangeitakasa Jumamosi." - Cardinal Maida, Askofu Mkuu wa Detroit, Saint Catherine Catholic Church Sentine, Algonac, Michigan, Mei 21, 1995.