Siku ya saba (Sabato) ni Jumamosi

Siku ya saba (Sabato) ni Jumamosi

KWANZA SIKU INAANZA JIONI
.... Ikawa jioni ikawa asubuhi siku moja... Mwanzo 1:5..Ikawa jioni ikawa asubuhi... Mwanzo 1: 8, 13, 19, 23, 31.

SIKU YA SABA MUNGU HAKUFANYA KAZI

.. Mungu akaibariki siku ya saba akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya Mwanzo 2:3

SIKU YA SABA NI LINI?

-Yesu alikufa saa tisa siku ya maandalio ya Sabato.... Marko 15:33 & 42 na alifufuka siku ya KWANZA ya juma baada ya Sabato... Marko 16: 1-6

-Siku ya maandalio ya Sabato ni ijumaa
USHAHIDI: Katoliki na waprotestanti wote wanaadhimisha "IJUMAA KUU" kwa dhana ya kwamba Yesu aliuwawa IJUMAA


-Sabato ni Jumamosi
USHAHIDI: Wayahudi hawajawahi kuacha kutunza Sabato "SIKU YAO YA SABATO NI JUMAMOSI"
Nani kakataa?

Wakristo wote na wasabato wakiwemo, wanatambua jumamosi ndiyo siku ya sabato.

Kitu pekee wasichokubaliana ni isue ya kufanya kazi.

Wakati wakristo hufanya kazi 24/7, wasabato wanajitahidi kufanya 24/6, lkn siku zote wanashindwa.

Wakati wakristo hukutana siku ya kwanza, wasabato hukutana siku ya saba tofauti kabisa na maagizo. Agizo ni kupumzika, wao hulazimika kusafiri kwenda ibadani.

Yesu aliye kiongozi wetu, hakuwahi kupumzika, siku ya sabato pamoja na kuingia hekaluni kufundisha, lkn alipiga na kazi pia

Yesu alikufa ijumaa, tangu sabato inaingia alikuwa amepumzika hadi alipofufuka jumapili. Hakuna kazi aliyoifanya. Hivyo alipumzika kwelikweli. Ndivyo ilivyo hata kwa Mungu, sabato alipumzika akifurahia kazi ya mikono yake, hakufanya lolote.

Kumbuka, kuabudu nako ni kazi, zaidi ya hayo, huambatana na shughuli mbalimbali kama safari ambazo kwa baadhi ya watu ni ajira.

Pia watumishi ktk kanisa, nao huwa kazini.
 
Kwani kuna mtu kakuzuia kuwa myahudi, usitulazimishe wote tuwe wayahudi. Sabato ni siku ya saba inategemea umemua kuhesabu kuanzia wapi
Ki biblia yuko sawa. Tatizo ni so what? Kuna msabato anapumzika? Tunaoabudu jumapili si kwa sababu ni siku ya saba, hapana, ni desturi tuliyochukua kwa mitume au wanafunzi wa Yesu ambao walikutana jumapili kufanya ibada.

Jumapili ni siku ya ushindi=Yesu alifufuka
Lkn pia ni siku aliyoshuka roho mtakatifu, hivyo kwetu ni ishara kubwa sana, ni siku ambayo shetani alitikiswa kwelikweli
 
Isaya 66:23 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema BWANA.

Kwa nini sabato kwako ni mhimu kuliko mwezi mpya?

Je, una hakika mbinguni siku ya ibada ni jumamosi?

Niambie kazi alizofanya Mungu siku ya sabato.

Niambie kazi unazoziacha siku ya jumamosi na unazoendelea kuzifanya.

Mbinguni ni starehe, siku zote ni kumtukuza Mungu pekee, wala hapatakuwa na kazi ya kumpinga shetani.

Hapa duniani mnajidanganya kupumzika na hamjawahi kupumzika. Ukifa aidha utapumzika au utakuwa kwenye ziwa liwakalo moto, mateso ya milele
Ni jambo lisilo na shaka kuwa sabato ni siku ya jumamosi ila chenye shaka ktk ulimwengu wa leo wa kiimani ni kwamba waitii amri hii ya Mungu ama wasiitii,,,

Dunia ya leo hamna wa kupinga kuwa sabato ni jumamosi ila watu wanachomiss ni kutambua kuwa sabato ni amri na utaratibu wa Mungu uliowekwa toka bustani eden na baadae kukumbushiwa pale mlimani Sinai kutoka 20:8 na baadae utaratibu huu ukaendelea kudumishwa na Yesu hata na mitume na kanisa la awali baada ya Yesu kupaa pia ni biblia hiyo hiyo inatuarifu kupitia kwa nabii Isaya 66:23 kuwa hadi kule mbinguni ibada itakuwa siku ya sabato

Watu hawafanyi ibada kwa kutii maagizo ya Mungu ila wanatii taratibu za wanadamu ambazo si salama kwao kufanya ibada isiyo na utii maana kabla ya ujio wa Yesu kutakuwa na makundi mawili moja linalofanya kwa utii kwa Mungu na jingine kwa kuongeza uchakachuzi na hapo kutakuwa na kundi lenye chapa ya mnyama yaani lisilo na utii kwa Mungu na jingine lenye muhuri wa Mungu kama tu ilivyokuwa kwa kaini na Abel, wote walitoa sadaka ila utii na unyenyekevu ukaleta tofauti
 
Hilo hata wao wanajua ni vile tu wanashupaza shingo maana hata jumapili wanayoabudu wanasema ndiyo siku Yesu aliyofufuka na maandiko yanasema siku aliyofufuka ilikuwa siku ya kwanza sasa ukihesabu toka hiyo jumapili siku ya kwanza jumamosi itakuwa ya saba

Lakini watakataa watasema hiyo ilikuwa ya wayahudi lakini ni uongo maana pale Edeni ilipoanzishwa hapakuwa na wayahudi wowote Lakini kwa maneno ya Yesu mwenyewe anasema

MK. :2:27
Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato.

Sabato ni kwa ajili ya mwanadamu na sote tu wanadamu kwa hiyo ni ya kila mmoja mtanzania, mkenya, muarabu, mhindi, na wote duniani hapa na siyo wayahudi pekee

Kwa hiyo ukiikataa uikatae kwa sababu zako binafsi lakini biblia maandiko ya haki yanasema sabato ni kwa ajili ya wanadamu
Swali ni wakati gani tunalumzika? Unajua maana ya kivuli? Maana sabato ilikuwa kivuli tu cha yajayo.
 
Isaya 66:23 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema BWANA.

Kwa nini sabato kwako ni mhimu kuliko mwezi mpya?

Je, una hakika mbinguni siku ya ibada ni jumamosi?

Niambie kazi alizofanya Mungu siku ya sabato.

Niambie kazi unazoziacha siku ya jumamosi na unazoendelea kuzifanya.

Mbinguni ni starehe, siku zote ni kumtukuza Mungu pekee, wala hapatakuwa na kazi ya kumpinga shetani.

Hapa duniani mnajidanganya kupumzika na hamjawahi kupumzika. Ukifa aidha utapumzika au utakuwa kwenye ziwa liwakalo moto, mateso ya milele
Endelea, maana unaelekea pazuri..
 
Hii ni KALENDA uliyotunga wewe? au ya sayari ipi? Unaishije bila hata kujua kusoma KALENDA? Soma hii hapa chiniView attachment 927436
Huu ni ushahidi dhaifu sana, hebu angalia hizi picha ambazo nimechukua screenshot kwenye simu halafu uniambie, je kwenye simu huwezi kuamua siku gani ianze kwenye juma!?
586B1335-94C1-4F2E-ACB4-C179C1E1BD8D.png
5C8F0A3F-BE58-41ED-AB51-90D3531D7DD3.png
77611817-616F-4761-A759-BB973494786E.png
 
Nani kakataa?

Wakristo wote na wasabato wakiwemo, wanatambua jumamosi ndiyo siku ya sabato.

Kitu pekee wasichokubaliana ni isue ya kufanya kazi.

Wakati wakristo hufanya kazi 24/7, wasabato wanajitahidi kufanya 24/6, lkn siku zote wanashindwa.

Wakati wakristo hukutana siku ya kwanza, wasabato hukutana siku ya saba tofauti kabisa na maagizo. Agizo ni kupumzika, wao hulazimika kusafiri kwenda ibadani.

Yesu aliye kiongozi wetu, hakuwahi kupumzika, siku ya sabato pamoja na kuingia hekaluni kufundisha, lkn alipiga na kazi pia

Yesu alikufa ijumaa, tangu sabato inaingia alikuwa amepumzika hadi alipofufuka jumapili. Hakuna kazi aliyoifanya. Hivyo alipumzika kwelikweli. Ndivyo ilivyo hata kwa Mungu, sabato alipumzika akifurahia kazi ya mikono yake, hakufanya lolote.

Kumbuka, kuabudu nako ni kazi, zaidi ya hayo, huambatana na shughuli mbalimbali kama safari ambazo kwa baadhi ya watu ni ajira.

Pia watumishi ktk kanisa, nao huwa kazini.
1. Kwa hiyo wayahudi ambao walipewa agizo la kuitunza Sabato na walioenda ktk masinagogi siku ya Sabato je walifanya kosa?

2. Je kwanini Yesu iwe desturi yake kwenda ktk masinagogi siku hiyo tu na siyo nyingine yoyote (Luka 4:16)?

3. Sawa kama ni siku ya kupumzika na ni AMRI ya 4 (Kutoka 20: 8-11), je kwanini hampumziki?

4. Je Amri ya SABATO ilifutwa Yesu alipokuja?

5. Na je ni nani alianzisha ibada ya jumapili (tafadhali weka ushahidi wa maandiko ya Biblia hata fungu moja?..

6. Je "kufufuka kwa Yesu au Pentecost" kutokea ktk siku ya kwanza ya juma kuna maliza umilele wa Sabato iliyosemwa katika kitabu cha Isaya?

7.Je siyo Mfalme Constantine wa Kirumi aliyeanzisha ibada ya jumapili miaka zaidi ya 300 baada ya kristo?

8.Je kulikuwa na mtume aliyekuwa hai wakati huo?

9. Je unaijua historia ya mamlaka na matendo ya Ruma ya kidinini ikiwa ni pamoja na vuguvugu la wana matengenezo?

10. Je unajua kuwa badiliko la siku ya ibada yaani kutoka Sabato ya Biblia kwenda jumapili ya Roma ya kidini ni moja ya "mamlaka" ambazo kanisa katoliki linajivunia?


UKITAKA TUTAWEKA HAPA USHAHIDI KUWA IBADA YA SIKU YA KWANZA HAINA CHIMBUKO LA BIBLIA
 
Huu ni ushahidi dhaifu sana, hebu angalia hizi picha ambazo nimechukua screenshot kwenye simu halafu uniambie, je kwenye simu huwezi kuamua siku gani ianze kwenye juma!?
View attachment 928687View attachment 928688View attachment 928689
Hizo ni picha zako siyo KALENDA inayotumika duniani labda ktk sayari nyingine.

Hatubishani hapa kama wapumbavu. Lazima facts zijengwe ktk maandiko na maisha halisi

Hata hivyo mpaka sasa hilo somo limeeleweka. WATU WAMEELEWA KUWA SIKU YA SABA NI JUMAMOSI.

Fuatilia mjadala, soma kwanza post zilizopita kisha twende pamoja
 
Hizo ni picha zako siyo KALENDA inayotumika duniani labda ktk sayari nyingine.

Hatubishani hapa kama wapumbavu. Lazima facts zijengwe ktk maandiko na maisha halisi

Hata hivyo mpaka sasa hilo somo limeeleweka. WATU WAMEELEWA KUWA SIKU YA SABA NI JUMAMOSI.

Fuatilia mjadala, soma kwanza post zilizopita kisha twende pamoja
Nimesoma post zote zilizotangulia, mi nataka kujua hizo siku za jumatatu hadi jumamosi zimetajwa wapi kwenye biblia!?
 
Haujasoma post zote
Nimesoma lakini sijaona ushahidi ilio wazi unaotaja hizo siku kwa majina yake zaidi ya watu kuunga unga bila kutaja vifungu husika ambapo Biblia inazitaja hizi siku
 
Hii ni Biblia gani mkuu,check Luka 24:1 kwenye Biblia zote nilizosoma inasomeka “Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari” Sasa hiyo Biblia inayoanza na neno “Jumapili “ imetoka wapi!?
 
Mungu alimaliza kazi ya uumbaji kwa mda wa siku sita na siku ya mungu sio siku ya kibinadamu muelewe hilo
 
Hii ni Biblia gani mkuu,check Luka 24:1 kwenye Biblia zote nilizosoma inasomeka “Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari” Sasa hiyo Biblia inayoanza na neno “Jumapili “ imetoka wapi!?
Ni sawa hiyo uliyo nukuru ni Biblia takatifu tafsiri ya kiswahili cha zamani.... Hiyo iliyoandikwa majina ya siku ni Biblia takatifu tafsiri ya kiswahili cha kisasa
 
Ni sawa hiyo uliyo nukuru ni Biblia takatifu tafsiri ya kiswahili cha zamani.... Hiyo iliyoandikwa majina ya siku ni Biblia takatifu tafsiri ya kiswahili cha kisasa
a. k. a HABARI NJEMA
 
Kama mungu angeihesabu sabato ni ya kupumzika tungeshaakufa wote maana we jiulize akipumzika mungu kuna atakaye baki kweli
 
Back
Top Bottom