Dr leader
JF-Expert Member
- Jun 28, 2016
- 1,080
- 1,449
Siku ya msiba wangu
Haoni navyoumia, sichoki kubembeleza
Kila siku ninalia, huku nikimueleza
Karibu nitajifia, Moyo ushajimaliza
Siku ya msiba wangu, kwake iwe ni sherehe
Aalike na vigoma, na wapiga vuvuzela
Kwake nimetia koma, ila anipa madhila
Aniona ja ukoma, haoni zangu fadhila
Siku ya msiba wangu, kwake iwe ni sherehe
Na anywe pombe alewe, nafsini asuuzike
Vipi asinielewe, anafanya niudhike
Mpaka napiga yowe, ndani kunao mvuke
Siku ya msiba wangu, kwake iwe ni sherehe
Bwana wa muda apate, kama hakuwa anaye
Mimi nipo petepete, yote sababu ni yeye
Nimeshamvisha pete, na bado siko mwenyewe
Siku ya msiba wangu, kwake iwe ni sherehe
Yananiua mahaba, kosa ni wangu upendo
Shingoni linimekaba, kama vile ni magendo
Atajakuwa kahaba, Hatapata wa mhendo
Siku ya msiba wangu, kwake iwe ni sherehe
Abuuabdillah ✍️
Haoni navyoumia, sichoki kubembeleza
Kila siku ninalia, huku nikimueleza
Karibu nitajifia, Moyo ushajimaliza
Siku ya msiba wangu, kwake iwe ni sherehe
Aalike na vigoma, na wapiga vuvuzela
Kwake nimetia koma, ila anipa madhila
Aniona ja ukoma, haoni zangu fadhila
Siku ya msiba wangu, kwake iwe ni sherehe
Na anywe pombe alewe, nafsini asuuzike
Vipi asinielewe, anafanya niudhike
Mpaka napiga yowe, ndani kunao mvuke
Siku ya msiba wangu, kwake iwe ni sherehe
Bwana wa muda apate, kama hakuwa anaye
Mimi nipo petepete, yote sababu ni yeye
Nimeshamvisha pete, na bado siko mwenyewe
Siku ya msiba wangu, kwake iwe ni sherehe
Yananiua mahaba, kosa ni wangu upendo
Shingoni linimekaba, kama vile ni magendo
Atajakuwa kahaba, Hatapata wa mhendo
Siku ya msiba wangu, kwake iwe ni sherehe
Abuuabdillah ✍️