Siku ya kwanza kuingia shule ya bweni ya Serikali

Nilifika shule usiku sana bweni lina harufu kali sijapata kuisikia vile kuna mwalimu alinipokea akaniambia asubuhi tu niende ofisini kufanya usajili.

Asubuhi mapema nikawahi ofisin kwenda kufanya usahili bwenini nikawaacha madogo kadhaa wa o level wanajiandaa kwenda madarasani.

Ofisini ile kulipa ada zao na kukamilisha usahili wakague vyeti na kukutana na wagen wengine wapya hapa na pale nikamaliza kila kitu saa nne.

Kurudi bwenini washavunja kufuli saa nyingi Dawa kubwa zile za mswaki, makatoni ya sabuni za kuogea na za unga, mafuta ya kupaka, kalamu na mazaga yote wale washamba wameiba wameniacha na counter book, nguo taulo na vitabu vichache

Roho iliniuma sana vile uzoefu wa maisha ya boarding nayajua nikahisi ni uzembe wangu jambo moja wahuni walikosa hela sikuweka kwenye sanduku la chuma.

Baada ya tukio sikureport popote nilienda kununua dawa ndogo ya mswaki, mswaki mmoja na sabuni ndogo ya kuoegea

vitu vingine vyote nikaanza kuiba kimya kimya niliiba bila huruma nilikua naiba ile mbaya mwaka mzima wezi wanatajwa hakuna anayenihisi vunja vunja makufuli wako darasani naiba vingine hata sina shida navyo natupa chooni iba iba mbaya sana.

Uchaguzi TYCS nachaguliwa kua katibu mkuu hakuna anayewaza mwizi ni mimi bwenini nakemea uwizi asubuhi jion na vunja.

Baadaye nikaamua kuacha mwenyewe. Nilisimulia marafiki kadhaa baada ya kumaliza shule miaka mingi ilivyopita. Mama alisema niwaombe msamaha. Sikuwahi kufanya hivyo.
Hahahahahahhaahaah nimecheka Sana

Yaan wewe unawaita washamba na wameshakuibia
 
Tarime Secondary 2004.

Ilikuwa j3 ya wiki ya kufungua, hapo nimehama kutoka Mkolani Secondary kwa Mazula nikataka kwenda boardin nikapelekwa Tarime, picha linaanza nafika shule na Mama, nikapelekwa mpaka ofisini kwa second na bag langu kubwa na ndoo, sikununua fyekeo wala jembe. Ticha namshangaa anauliza mbona begi kubwa! Nikamwambia ni nguo za kubadili hizo nikaambiwa hizo za nyumbani hazihitajiki, zinahitajika mbili tu za kuvaa siku tukifunga, bi mkubwa akarudi nazo, mchana nikawa nimeshakula, ishu ikawa jioni, kwenda dining nakutana na wajomba wa form 5 na 4 na 6 na wengine hapo mimi niko form 3. Harage gumuuu, kuna jamaa alienipokea akanambia nisiogope, pale pako sawa, nikamwambia haina tabu. Harage likaungwa na mafuta mezani likatiwa pili pili ya kutosha watu tukaanza kupiga ugali. Badae prep huku baridi inanipiga hatari, baada ya siku ka 3 nikaona haya maisha hapa nitakufa, nikajitungia ugonjwa ili nirudi hom na ilikuwa nikirud ndio nitolee hapo, hamad! Baada kama siku mbili hivi mshua akaja shule akitokea Kenya akaja na mazaga kibao akaanza kuniusia hapo nisome, nikatulia. Maisha yakawa fresh tu, dining nikawa sikosi na pesa nilikuwa nayo nyingi tu ingawa sijuagi mpaka leo nilikuwa naitumia kwenye nini
 
Nakumbuka shule yetu ilikuwa na wanafunzi wengi walikuwa ni kutoka Kigoma,Tabora na Mwanza...washamba balaa...umeme ukikatika tunawapa ndoo wakachote umeme...yaani hata watu wazima walikuwa wanabeba ndoo kwenda kuchota umeme.....na tulikuwa tunawaambia wasiporudi na umeme wabaki huko huko....walipata taabu sana
Wakauchote wapi
 
Alirudi kesho yake akafikia ofsini kwa walimu ndio wakamleta mabwenini... Shule za wavulana zina vituko sana..
Yani ilikua ukiingia chooni lazma uingie na chupi au uchi na ukitoka unakaa chini ya mti kama dakika tano la sivyo ukiingia na nguo harufu ya choo utaibeba nusu saa....
Umenikumbusha kitu wallah ,unaenda zako na kanga na toilet paper,ukishatoka ndio unaenda kuvaa nguo la sivyo unanuka choo nguo zote,, hivi kwanini jamani vyoo vile vilikuwa na nini
 
Ile Kilamanjato Boys noma sana wenyewe tuliita "Kiliboys" hapa nakumbuka:-
1. Dogo mmoja form one ilikuwa siku ya ijumaa mchana ni makande hapa kunakuwa na vurugu sana bwaloni, yule dogo kawahi kajaza sahani akala kiasi kilichobaki akafungia kwenye mzinga(sanduku la chuma) ili jioni aendelee na makande yake asipange foleni ya ugali, wahuni wakamtaim ametoa wakageuza sanduku lile chini juu na kulitikisa sana kisha wakalirudisha kama lilivyokuwa. Pata picha alivyokuja kufungua sanduku baadae, ikumbukwe sanduku hili ndio lina kila kitu kuanzia uniform na vitu vingine.

2. Uzuri wa hii shule hakuna kukacha prepo ukajificha bwenini, mabweni yalikuwa na vibwengo sana hasa hasa bweni la horombo.

3. Shule ilikuwa mbali sana na wilayani, haina fensi huwezi hata kutoroka ni pori tupu na kuna tembo porini kutokea Kenya.

SIKU HIZI NASIKIA IMEPOA IMEKUWA SHULE YA WANAWAKE.
Wewe Martial hater kumbe umesoma kiliboys mkuu pale...
 
Mimi nimesoma bagamoyo secondary, shule pekee ukiwa ufukwen au baharin unaogelea unakua bado upo eneo la shule, kama advance hukusoma serikalin bas ww ni kilaza
Asantee

Haya wewe uliyesoma serikalini advance vp uko wizara gani sasa hv mkuu

 
Write your reply...nakumbuka kuvamia shamba LA shule kuchuma mkungu wa ndizi na kuuchoma bahat mbaya tukachoma shamba tulitoka nduki huku tukikimbizwa na mlinzi akijua waizi .bila kusahau nipo shule mwezi lakin sionekani darasani dining wala wapi route zangu ni Dom chaka na kitaa
 
I was luck, wakat naenda kuripot form five mzee alinisindikiza na gari ya ofisin kwake (STK) ile kufika tu shule sa 11 jion nikakuta wajomba wako parade basi nikasushwa pale kila mtu akaniona, ile STK ikamchanganya jamaa m1 akanipokea akanipeleka bweni moja la'kisure sana tulikua tunaliita UN (umoja wa mataifa), kiongoz wa chakula alikua anakaa UN ko tulikua tunakula na kusaza chakula daraja la kwanza. The following morning naamka nakuta wajomba wanaoga nje vimat*ko nje nje akat bafu zipo, with time na mim nikajikuta bingwa wa kuoga nje mixa kukatiza bweni to bweni na boxer tu ! Nilijifunza mengi those days
 
Ilikuwa form V, baada ya orientation, tunes za kujuana. Wengi tulishapewa majina ya rafiki wa rafiki ambae anakuja shule ile.

Dining siku ya kwanza mdada mmoja alimwaga magarage kisa alimkuta mende ndani ya bakuli. Kwakuwa bado tulikuwa na makula kula kuna waliomtengenezea orange squash na marie biscuits.

Baada ya miezi miwili pale shule, mdada alikuwa hodari wa kutoa mende kwa kijiko na kuendelea na menu.
Khe khe khe khe khe khe khe khe
 
Form 5 nilipangiwa na shosti angu tena comb moja..... Tukaenda wote tumevuuta hatari tumefika shule tunajikuta masista duu wajanja ndo sis asubuhi tunashangaa kuamka saa kumi na moja asubuhi hapo unapangiwa kufagia uwanja mkubwaa,afu umwagilie garden mpaka iwe tifu tifu baada ya hapo ukadeki choo afu saa moja sharp uwe parade ....aisee ikabid niulize hiz Kazi mpaka lini nikajibiwa ndo maisha ya kila siku niliangua kilio kisicho na mfano siku ya kwanza nikasema haya maisha siwez ,
Mda wa parade nipo na shati la tomato kidogo dogo na sketi ya kisista duu ya kiunoni nilikua nmeshashona home mwee mweee mwalimu kupita akatutoa mbele kwamba m shoga angu tumevaa kihuni tukapelekwa kwa Fundi wa shule tukashonewa mpaka shati kubwa kama la baba paroko kitamba kama cha shuka daa huku sket ya tumboni ndefu hatari
Nilienda na kikombe cha udongo kidogo dogo cheupe kama cha kahawa vile na kisahani changu kidogo kama kisosi maana o'level shule niliotoka full ubishoo ,doooh kufika SAA nne uji madai hatunywi tumbo litakua kubwa afu nashangaa watu wana majagi hahahaha..... Mwezi mrefu nikatafuta jagi langu na bakuli kubwa tu tena la plastic uji nikaunywa vizuri tuuuu na foleni ya ugali nikapanga
Shule ilikuwa kanda ya ziwa washamba washamba wengi tukaanza kuwacheka wahaya kwamba mjini wanajishauaga saana ila kumbe wana lafudhi mbovu inshort ni wakuja tuu tuliwacheka saana....

Nakumbuka siku ya kwanza tu nilipiga simu nyumban maisha magum siwez mzee akanimbia vumilia mpaka muhula uishe ndo utahama ,sasa muhula daah Kazi nying afu viongoz walikua wanaishi kwa raha saana hawafanyi kazi yeyote nikaona bora nikimbilie uongoz bahati mbaya viongoz wote form6 na uchaguz mpaka muhula wa pili ,siku ya kufunga niliondoka na kila kitu changu kufika nyumban shule nilizotaka kuhamia background ya result zao kwa comb yangu sio nzur tena wasichana ndo kabisa div3 , div4 na 0 maana nilikua pcm nikasema hapana bora nilipotoka comb yangu wanafaulu nikarudi baada ya miez miwili na tranka langu hahahaha nikakuta mwalimu wa zamu mnoko hatari akanipa adhabu ya kuvuta akanikatia shamba la kulima na kuchimba na kuzisombelea molam ndoo 25 ,shamba nikaajiri wanakijiji kimbembe molam anasimami nikabeba kufika ndoo ya 10 viungo vya mwili vikagoma havina ushirikiano kabisa naumwa kila sehemu nalia hatari nikarud Dom nikampigia mzee nikamwambia akasema nipe namba za mwalimu wako nikampa sijui waliongea nin baadae nashangaa naitwa sikwenda mwl akaja nipo kama nakaribia kufa akaniambia adhabu umesamehewa

Muhula wa pili baada ya mda ikafika kipind cha uchaguz nikasema hapa lazima niwe kiongoz kwa mikaz ya shule naweza kufeli bure nikachukua fomu bahati nzur kichwani nilikua vizuri nikachaguliwa academic
Baada ya kuwa kiongoz ndo maisha yakaanza sasa kwanza nikachagua room nayotaka ,ambazo nitofaut na wanafunz wa kawaida ndani mnakaa wawil tu chumba mapazia ,carpet hapo ndo nikaish kama nipo chuo mpaka namaliza .....

Nashukuru tu Mungu nilifaulu vzuri
 
Siku ya kwanza nilianza kula menu ya jioni ilikuwa ugali

Ugali ulikuwa wa unga uliokaa kwa muda mrefu hadi ukavundika ukawa na harufu fulani amaizing.

Nilikula matonge hayazidi matano nikaacha nikaenda kuumwaga, kesho yake njaa ililikamata maana sikula vizuri jana yake.

Ilipofika lunch ile harufi sikuiona tena(sikuijali) niliparamia menu bila kubakisha hata punje ya tonge. Kuanzia hapo nikazoea ugali moja kwa moja
Pole sana mkuu

Mi mzee wangu alikua ananipenda sana ... !!!

Shida nilizopitia ni yale ma quantum phyz
 
Form 5 nilipangiwa na shosti angu tena comb moja..... Tukaenda wote tumevuuta hatari tumefika shule tunajikuta masista duu wajanja ndo sis asubuhi tunashangaa kuamka saa kumi na moja asubuhi hapo unapangiwa kufagia uwanja mkubwaa,afu umwagilie garden mpaka iwe tifu tifu baada ya hapo ukadeki choo afu saa moja sharp uwe parade ....aisee ikabid niulize hiz Kazi mpaka lini nikajibiwa ndo maisha ya kila siku niliangua kilio kisicho na mfano siku ya kwanza nikasema haya maisha siwez ,
Mda wa parade nipo na shati la tomato kidogo dogo na sketi ya kisista duu ya kiunoni nilikua nmeshashona home mwee mweee mwalimu kupita akatutoa mbele kwamba m shoga angu tumevaa kihuni tukapelekwa kwa Fundi wa shule tukashonewa mpaka shati kubwa kama la baba paroko kitamba kama cha shuka daa huku sket ya tumboni ndefu hatari
Nilienda na kikombe cha udongo kidogo dogo cheupe kama cha kahawa vile na kisahani changu kidogo kama kisosi maana o'level shule niliotoka full ubishoo ,doooh kufika SAA nne uji madai hatunywi tumbo litakua kubwa afu nashangaa watu wana majagi hahahaha..... Mwezi mrefu nikatafuta jagi langu na bakuli kubwa tu tena la plastic uji nikaunywa vizuri tuuuu na foleni ya ugali nikapanga
Shule ilikuwa kanda ya ziwa washamba washamba wengi tukaanza kuwacheka wahaya kwamba mjini wanajishauaga saana ila kumbe wana lafudhi mbovu inshort ni wakuja tuu tuliwacheka saana....

Nakumbuka siku ya kwanza tu nilipiga simu nyumban maisha magum siwez mzee akanimbia vumilia mpaka muhula uishe ndo utahama ,sasa muhula daah Kazi nying afu viongoz walikua wanaishi kwa raha saana hawafanyi kazi yeyote nikaona bora nikimbilie uongoz bahati mbaya viongoz wote form6 na uchaguz mpaka muhula wa pili ,siku ya kufunga niliondoka na kila kitu changu kufika nyumban shule nilizotaka kuhamia background ya result zao kwa comb yangu sio nzur tena wasichana ndo kabisa div3 , div4 na 0 maana nilikua pcm nikasema hapana bora nilipotoka comb yangu wanafaulu nikarudi baada ya miez miwili na tranka langu hahahaha nikakuta mwalimu wa zamu mnoko hatari akanipa adhabu ya kuvuta akanikatia shamba la kulima na kuchimba na kuzisombelea molam ndoo 25 ,shamba nikaajiri wanakijiji kimbembe molam anasimami nikabeba kufika ndoo ya 10 viungo vya mwili vikagoma havina ushirikiano kabisa naumwa kila sehemu nalia hatari nikarud Dom nikampigia mzee nikamwambia akasema nipe namba za mwalimu wako nikampa sijui waliongea nin baadae nashangaa naitwa sikwenda mwl akaja nipo kama nakaribia kufa akaniambia adhabu umesamehewa

Muhula wa pili baada ya mda ikafika kipind cha uchaguz nikasema hapa lazima niwe kiongoz kwa mikaz ya shule naweza kufeli bure nikachukua fomu bahati nzur kichwani nilikua vizuri nikachaguliwa academic
Baada ya kuwa kiongoz ndo maisha yakaanza sasa kwanza nikachagua room nayotaka ,ambazo nitofaut na wanafunz wa kawaida ndani mnakaa wawil tu chumba mapazia ,carpet hapo ndo nikaish kama nipo chuo mpaka namaliza .....

Nashukuru tu Mungu nilifaulu vzuri
Aisee pole sana
 
Back
Top Bottom