Nasoma lkn sielewi,mtu anakuwa na courage ya kusema sitaki mwili wangu as if ni kitu cha maana sana,ninachoamini mimi ni kuwa there is life after death,hii miili tunayoita ya kwetu na kuipangia masharti itabaki hapa duniani na itaoza,roho zetu ndio zitabaki hai,hii ni either peponi au motoni...
Boss , kuna ujumbe wangu DM kwako kiongoziMimi nikifa sitaki mambo mengi nichomwe moto tu, ila Kama haiwezekani Basi nifukiwe tu futi sita bila mambao Wala manguo... Raw and unsugarcoated!
Kama ulikuwa hujui mtu akifa funza na minyoo wanaingia ndani ya mwili(Mzoga) na kuchukua nutrients zote na kuzirudisha Tena ardhini ambapo udongo unautumia tena Kama rutuba... Ni proper system ya recycle ndio sababu nikiona mtu anajengewe na masimenti nachukizwa saana sababu naona Kama watu wanajaribu kuidhibiti nature isifanye kazi yake.
Death is inevitable!
Sawa mkuu nimekueleza hayo sababu nakumbuka hata mzee wangu aliagiza akifa akazikwe kijijini alikozikwa mama yake mzazi, lakini baada ya kifo chake kamati ya mazishi iliamua tofauti na akazikwa palepale mkoa alipofiwa na hayo yalikuwa maombi ya mkewe kuwa awe jirani na kaburi la mumewe.
Pia mzee aliacha wosia na mgawanyo wa mali, lakini suala la mirathi lilipofikishwa mahakamani, mahakama iliukataa wosia wake na kuagiza kitu tofauti na maagizo yake japo mahakama yenyewe inakiri kuwa wosia wa marehemu unawakilisha kauli yake halisi!
Mimi binafsi ningependa nikifa nizikwe tu kwa taratibu za kawaida kama walivyozikwa marehemu wengine walionitangulia, Lakini zaidi ningependa kila anayenifahamu popote alipo akinikumbuka aseme neno lolote kuniombea pumziko la amani huko nitakakokuwa sababu mimi pia nina utamaduni wa kuwaombea marehemu wote popote kila ninapohudhuria misiba au ibada makanisani!
Sure. Hata mimi mambo ya kubaba na kunukiana sitapenda kabisa. Nizikwe Kijijini kwetu kwenye shamba langu.Nikifa sitaki Kuzikwa kwenye makaburi ya Jumla nataka wanizikie nyumbani kwangu.
mkuu kwani kifo kipo safarini tu.....???ikitokea ndege imefeli angani ikaangukia kwenye nyumba yenu saa nane za usiku ikaua familia nzima je,kifo hakina honi mkuu.Haha
Mkuu, jiulize kabla wazazi wako ambao ndio waliokuleta hapa duniani hawajazaliwa, ulikuwa wapi..?!Wanichome kama Wahindi nione siku ya mwisho nitaludije
Sasa ukifa halafu shemeji akaolewa na mwanaume mwingine, na mauti yakamkuta huko... Unadhani mumewe atakubali mkewe azikwe kwenye 'kitanda' chako..?!Ndugu zangu wote na marafiki zangu wote wanajua kuwa siku yakufa kwangu nizikwe kwa kutumia kitanda ninacho lalia na mke wangu. Fedha yajeneza mnunulieni kitanda kipya na godoro. Wekeni pilo ya pili kando yangu ili akifa mfungue kaburi mmlaze tu hapo kando mrudishie mfuniko.
Kaburi natarajia kulichimba na kulijengea mwenyewe tiyari kwa maziko yangu
Wakuchome na majivu wakayatupe baharini ALIYEKUUMBA KUTOKA SPERM HADI KUWA WEWE FOR SURE ATAKURUDISHA.Wanichome kama Wahindi nione siku ya mwisho nitaludije
Looh, pole sana!Kwenye mali za baba yao? Hawakuambulia hata soks hata kijiko. Yuko mtoto wa nje ya ndoa ndo alijimilikisha vyote.
Hawa watoto wa nje ya ndoa ni hatari.
Nazidi kumngojea Mungu aje aamue mwenyewe.
Yani mtu afate maagizo ya marehemu?ukifa huna lako na huwezi kupangia watu kitu cha kufanya
Mimi kifo najua kipo na kitakuja tu...hakina siku saa.
Hivyo Basi...najiandaa na maisha baada ya kifo ambayo naamini yapo.
Nachoomba nife Hali ya kuwa Mola want yu radhi nami.
Kuzikwa nizikwe kwa taratibu za Dini yangu..ya uisilamu.
Hivyo yaani
Watu walivyo waoga wanaogopa hata kukomenti.
Kufa utakufa tu ndugu whether you like it or not!
Siku mzee wangu alipofariki. Wakati wa kwenda kuchukua mwili niliingia monchwari kwenda kusaini. Pembeni kulikua na meza mbili juu wamelazwa maiti nadhan walikua wanataka kuwasafisha. Niliwaangalia kwa kweri nilinyong'onyea sana. Kifo kinatisha hata kukiongelea