Mrs Gudman
JF-Expert Member
- Jul 3, 2015
- 613
- 1,300
Ee bhana eeh hapa duniani huwaga kuna nyakati ngumu sana ambapo unaweza tamani kiama kitokee utoweke kuliko fedhedha au hali flani ya aibu na maumivu yanayokukuta .
Leo nimekumbuka tukio moja ambalo siwezi lisahau maisha yangu yote ,nilikuwa advance enzi hizo miaka kadhaa ilopita ticha wa kemia akasema kutakuwa na test(Physical chemistry) test enyewe ni swali moja tu la calculation na mfano wa hilo swali tushafanya na nimeelewa vizuri tu ,basi buana siku kaa mbili hivi kila mtu anajiandaa .
siku ya mtihani ikafika swali likaja lile lile hadi data hazijabadilika lina marks 25 na lipo moja tu,tukagawiwa karatasi tukapewa dakika tano tusome swali ,nilipoliona swali nikafurahi pia mana naona kabisa 25 yote nachukuwa ha ha
Nikachukua karatasi nikaandika jina ile nashika tu peni nianze kuandika data ,akili ikafuta kila kitu hata kucollect data siwezi yani sielewi ,nikawa najaribu nikumbuke basi hata fomula itanisaidia kucollect data nikashindwa pia kukumbuka fomula ,kumbuka hilo swali nalijua na nimelisoma vilivyo.
Dah nikawa naangalia pembeni je wenzangu wanafanya? kiukweli darasa nzima kila mtu alikuwa bize kukokotoa isipokuwa mimi tu.
Teacher anapita anaangalia jinsi watu wanafanya naona anapita kwangu mimi nimeandika tu jina huku zishatangazwa zimebaki dk 15 tu time iishe.
Nikainama juu ya dawati nikawa nasali Mungu anikumbushe kanuni ,kiukweli sikukumbuka ,nikakemea pepo la usahaulifu wapi mwisho wa siku nikabadili maombi ,nikawa natamani litokee janga lolote tetemeko au kiama woote tutoweke tu kuliko vile majibu yanavyoenda kuwa mimi nina 0/25 wenzangu wooote wana 25/25
Maombi hayo pia Mungu akuyajibu ,nikasikia pens down ,tukakusanya mimi nimeandika jina tu.
Kila mtu anafuraha vicheko na kumshukuru teacher kwa ile feva ,ilibidi niende tu bwenini kulala
Majibu yalitoka robo tatu ya darasa ilipata 25/25 mimi nikapata 2/25 hizo 2 niliwekewa tu kama zawadi ya kuandika jina na kuaribu karatasi ha ha.
Kitu gani kimewahi kukupata kama mimi???
#TIRIRIKA
#TUNATOKAMBALI
Sent using Jamii Forums mobile app
Leo nimekumbuka tukio moja ambalo siwezi lisahau maisha yangu yote ,nilikuwa advance enzi hizo miaka kadhaa ilopita ticha wa kemia akasema kutakuwa na test(Physical chemistry) test enyewe ni swali moja tu la calculation na mfano wa hilo swali tushafanya na nimeelewa vizuri tu ,basi buana siku kaa mbili hivi kila mtu anajiandaa .
siku ya mtihani ikafika swali likaja lile lile hadi data hazijabadilika lina marks 25 na lipo moja tu,tukagawiwa karatasi tukapewa dakika tano tusome swali ,nilipoliona swali nikafurahi pia mana naona kabisa 25 yote nachukuwa ha ha
Nikachukua karatasi nikaandika jina ile nashika tu peni nianze kuandika data ,akili ikafuta kila kitu hata kucollect data siwezi yani sielewi ,nikawa najaribu nikumbuke basi hata fomula itanisaidia kucollect data nikashindwa pia kukumbuka fomula ,kumbuka hilo swali nalijua na nimelisoma vilivyo.
Dah nikawa naangalia pembeni je wenzangu wanafanya? kiukweli darasa nzima kila mtu alikuwa bize kukokotoa isipokuwa mimi tu.
Teacher anapita anaangalia jinsi watu wanafanya naona anapita kwangu mimi nimeandika tu jina huku zishatangazwa zimebaki dk 15 tu time iishe.
Nikainama juu ya dawati nikawa nasali Mungu anikumbushe kanuni ,kiukweli sikukumbuka ,nikakemea pepo la usahaulifu wapi mwisho wa siku nikabadili maombi ,nikawa natamani litokee janga lolote tetemeko au kiama woote tutoweke tu kuliko vile majibu yanavyoenda kuwa mimi nina 0/25 wenzangu wooote wana 25/25
Maombi hayo pia Mungu akuyajibu ,nikasikia pens down ,tukakusanya mimi nimeandika jina tu.
Kila mtu anafuraha vicheko na kumshukuru teacher kwa ile feva ,ilibidi niende tu bwenini kulala
Majibu yalitoka robo tatu ya darasa ilipata 25/25 mimi nikapata 2/25 hizo 2 niliwekewa tu kama zawadi ya kuandika jina na kuaribu karatasi ha ha.
Kitu gani kimewahi kukupata kama mimi???
#TIRIRIKA
#TUNATOKAMBALI
Sent using Jamii Forums mobile app