Siku Dr. Slaa akiongea

Siku Dr. Slaa akiongea

Mzee wa Rula

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2010
Posts
8,169
Reaction score
3,358
Wadau ni muda sasa toka sintofahamu ya Dr. Slaa ilipozungumzwa na mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Freeman A. Mbowe.
Na leo japokuwa hajaliongelea moja kwa moja lakini ameliongelea kinyume nyume. Ni rai yangu sasa tuache kuliongelea hilo jambo kwa mbwembwe au muhemuko.

Ni wazi siku Dr. Slaa akiongea anaweza akabadili upepo wa kisiasa ambao tayari wanaCHADEMA wanaamini wameshavuka.

Tumuache Dr. Slaa sasa ufanye maamuzi yake binafsi kama ni ya kurudi au kuachana na siasa bila kejeli au dhihaka. Hapa pana vita isiyoonekana kwa macho na kauli ya Dr. Slaa inaweza kuwa na athari endapo ataendelea kutukanwa kisha akaamua tukose wote kama yule mama na nabii Suleman.

Nawasilisha.
 
Yule ni Mchungaji mwacheni atunze uchungaji wake Tena kumbuka kuwa yule ni msomi wa falsafa haendeshwi na mihemko ya kisiasa za maji taka. Na hawezi badilishwa na mitandao
 
Mbowe kasema watatumia jitihada zote wasimwache nje pamoja na sintofahamu ilotokea...
 
Mbowe kasema watatumia jitihada zote wasimwache nje pamoja na sintofahamu ilotokea...

Kauli hizi ni za maana sana na zinaweza kuleta kheri kuliko majigambo kuwa Dr. Slaa si Kitu. CCM wamewekeza hapo ili kusiwe na maelewano kisha tuanze kwanza hapo kujisafisha kisha kumsafisha Lowasa then ndiyo uje useme Sera zako.
 
Nikikumbuka mshikamano wa Mbowe na Slaa sielewi inawezekana vipi haya yafike huku.....
 
Huyo mzee ni mtaji. Kubwa kwa chama hawezi kutuacha jangwani
 
Mbowe anajua sana nguvu ya dr Slaa unamuona kabisa anaumia na sintofahamu ukweli anaheshimu kazi ya dr Slaa ndio maana amesema anapumzika ataungana nao baadaye Dr Slaa raisi wa mioyoni mwa watanzania unajua kuna nyakati za majaribu tunajuwa anapenda wananchi wake hawezi kutuache nyikani atatufikisha kwenye nchi ya ahadi
 
Nikikumbuka mshikamano wa Mbowe na Slaa sielewi inawezekana vipi haya yafike huku.....
usifikiri hii ishu imeanza leo. mbona ipo kitambo, sema ilikuwa chini ya kapeti. ni ukweli ulidhahiri kuwa slaa alikuwa anaburuzwa na mbowe. wakati huohuo mshauri mkuu wa mbowe akiwa mkwe wake mtei. kilichoamliwa na mtei-mbowe hakukuwa na wakukipinga. tatizo lenu nyie ni misukule. tuliwambia sana humu lakini ndo hivyo hamuambiliki. binafsi hata sishangai haya ninayoyaona.
mimi siko chadema lakini ninawashikaji wengi tu ndani ya chadema wanaonipa michapo kila kukicha. ajabu wewe upo chadema unaishia humu mitandaoni. aibu.
 
Sitakaa nimuamini tena binadamu anaitwa Freeman Aikaeli Mbowe.
 
Kumbe wewe ni kweli nilivyosikia kuwa ni BOY nyumbani kwa Mtei.

Ndiyo maana unajua yote yanaoendelea, BOY. Wahi kamfulie Chupi zake maana patachimbika.

Endelea kuiba SIRI za ndani za Mtei na kutuletea kwani utasaidia sana kulikomboa Taifa hili kutoka mikono ya CCM.

usifikiri hii ishu imeanza leo. mbona ipo kitambo, sema ilikuwa chini ya kapeti. ni ukweli ulidhahiri kuwa slaa alikuwa anaburuzwa na mbowe. wakati huohuo mshauri mkuu wa mbowe akiwa mkwe wake mtei. kilichoamliwa na mtei-mbowe hakukuwa na wakukipinga. tatizo lenu nyie ni misukule. tuliwambia sana humu lakini ndo hivyo hamuambiliki. binafsi hata sishangai haya ninayoyaona.
mimi siko chadema lakini ninawashikaji wengi tu ndani ya chadema wanaonipa michapo kila kukicha. ajabu wewe upo chadema unaishia humu mitandaoni. aibu.
 
Tatizo linalomsibu Dr Slaa lipo ndani ya familia yake mwenyewe, na siyo tatizo la Chadema, hata hivyo ninamtakia mapumziko mema akiwa nchini Australia na familia yake baada ya maandalizi ya safari ya kuondoka na familia yake nchini kukamilishwa na TISS kwa msaada wa mke wake.
 
Hizi akili za kujadili watu sijui tuweke lundi gani. Dr katulia kwake na familia yake,Ukawa mnamchokonoa.CCM wametulia,wanafanya yao. Baadaye mtadai mmeibiwa.
 
wasije kumfanya kama amina chifupa. wakamficha ana jambo la kutwambia ila kwa kua walimficha kajifia na siri yake



sasa isije tokea kwa slaa. tutawalaumu chadema
 
Ikimbidi Dr Slaa aongee...atasema mstari mmoja tu...
"Freeman Mbowe anapaswa kuongezwa kuwekwa namba 12 kwenye List of shame"
Wazee Wa mtakiona chamtema kuni magamba wanaweweseka mpaka na kamanda wao Wa vita ccm bye bye
 
Kwa mapenzi tuliyo nayo kwa Dr slaa naamini hawezi kutuangusha, muacheni katibu mkuu apumzike ata join mbele ya safari hatuwezi kwenda mbele bila Dr slaa.
 
Hizi akili za kujadili watu sijui tuweke lundi gani. Dr katulia kwake na familia yake,Ukawa mnamchokonoa.CCM wametulia,wanafanya yao. Baadaye mtadai mmeibiwa.


Wana JF tusizungumzie watu. Vyama vya siasa vinavyowapa nafasi za uongozi mafisadi hakika hata vingekuwa na 'sera' na 'mifumo' ya maendeleo, 'Safari za Matumaini/ Uhahika/ Mabadiliko/ Mageuzi/ nk) ni ndoto za alinacha. Watanzania makini waviweka pembeni vyama hivyo. Mchumia tumbo ni adui wa maendeleo.
 
Back
Top Bottom