Mr George Francis
Senior Member
- Jun 27, 2022
- 186
- 212
SIKU 470 NIKIWA NA HOFU YA KUAMBUKIZWA VIRUSI VYA UKIMWI.
[Sehemu Ya 1 ]
Tarehe 1 mwezi wa 12 ya kila huwa tunaadhimisha siku ya UKIMWI duniani.
Katika kutambua umuhimu wa siku hii kwa jamii na taifa letu kwa ujumla, naomba tupate funzo kupitia historia yangu na jinsi nilivyoishi siku 470 nikiwa na hofu ya kuwa na virusi vya UKIMWI.
Miaka kadhaa nyuma niliangukia katika huba la mapenzi na Binti mmoja wa Kizanzibari ambaye tulikutana chuoni.
Alikuwa ni Binti mzuri sana wa sura, shepu na hata tabia zake zilinivutia pia. Hivyo, haikuwa ngumu kwangu kumpenda na kumuamini.
Tulianza kama marafiki lakini mwisho wa siku tukajikuta katika mahusiano ya kweli na yasiyo na kificho.
Kabla ya dating yetu ya kwanza, nakumbuka aliwahi kuniambia kuwa yeye ni muathililika tangu kuzaliwa kwake.
Lakini kwa jinsi alivyo, uzuri na umbile lake, sikuweza kabisa kumuamini bali nilidhani ni mtu ambaye hataki tu kudate na mimi.
Nusrat alinishauri basi tukapime lakini niliona tu kama ananizingua.
Kwakuwa alikuwa ananipenda sana, hakutaka kunipoteza hatimae alikubali tudate bila kupima na kujua Afya zetu, japo alisisitiza sana juu ya matumizi ya condoms.
Baada ya kuzoeana tukajikuta wote hatukumbushani tena matumizi ya condoms.
Tukiwa mwaka wa mwisho chuoni Nusrat, alibeba ujauzito. Sikuwa na wasiwasi hatakidogo kwani tulipanga kuoana, baada ya kumaliza masomo.
Lakini ili kuanza kliniki ya uzazi ilitakiwa mama mjamzito na baba mtarajiwa wa mtoto ambaye ni mimi tukapime kwa usalama wetu na usalama wa mtoto aliye tumboni.
Kupima HIV haikuwa desturi yangu. Nilikataa katakata kupima. Nikamwambia "kapime mwenyewe bwana!"
Sijui alijitetea vipi hospitali lakini alikubaliwa kupima peke yake nakurudi na majibu.
Nilisoma kikaratasi cha majibu nikiwa natetemeka, jasho linanitoka. Majibu yalionesha kuwa Nusrat alikuwa ni HIV positive.
"Mungu wangu! Nimeshakufa mimi!!" Nilijisemea huku nabubujikwa na machozi. Lakini yeye wala hakuonesha wasiwasi wowote, nadhani kwakuwa alikuwa anaifahamu hali yake tangu zamani.
Nilibadilisha kabisa mtazamo wangu juu ya maisha. Tangu siku ile nilijua tu itakuwa nimeshaathirika mimi ni wa kufa leo ama kesho.
#No_Learning_No_Earning
So we have to Learn.
NAME : Mr George Francis
📩 mr.georgefrancis21@gmail.com
Inaendelea.....
[Sehemu Ya 1 ]
Tarehe 1 mwezi wa 12 ya kila huwa tunaadhimisha siku ya UKIMWI duniani.
Katika kutambua umuhimu wa siku hii kwa jamii na taifa letu kwa ujumla, naomba tupate funzo kupitia historia yangu na jinsi nilivyoishi siku 470 nikiwa na hofu ya kuwa na virusi vya UKIMWI.
Miaka kadhaa nyuma niliangukia katika huba la mapenzi na Binti mmoja wa Kizanzibari ambaye tulikutana chuoni.
Alikuwa ni Binti mzuri sana wa sura, shepu na hata tabia zake zilinivutia pia. Hivyo, haikuwa ngumu kwangu kumpenda na kumuamini.
Tulianza kama marafiki lakini mwisho wa siku tukajikuta katika mahusiano ya kweli na yasiyo na kificho.
Kabla ya dating yetu ya kwanza, nakumbuka aliwahi kuniambia kuwa yeye ni muathililika tangu kuzaliwa kwake.
Lakini kwa jinsi alivyo, uzuri na umbile lake, sikuweza kabisa kumuamini bali nilidhani ni mtu ambaye hataki tu kudate na mimi.
Nusrat alinishauri basi tukapime lakini niliona tu kama ananizingua.
Kwakuwa alikuwa ananipenda sana, hakutaka kunipoteza hatimae alikubali tudate bila kupima na kujua Afya zetu, japo alisisitiza sana juu ya matumizi ya condoms.
Baada ya kuzoeana tukajikuta wote hatukumbushani tena matumizi ya condoms.
Tukiwa mwaka wa mwisho chuoni Nusrat, alibeba ujauzito. Sikuwa na wasiwasi hatakidogo kwani tulipanga kuoana, baada ya kumaliza masomo.
Lakini ili kuanza kliniki ya uzazi ilitakiwa mama mjamzito na baba mtarajiwa wa mtoto ambaye ni mimi tukapime kwa usalama wetu na usalama wa mtoto aliye tumboni.
Kupima HIV haikuwa desturi yangu. Nilikataa katakata kupima. Nikamwambia "kapime mwenyewe bwana!"
Sijui alijitetea vipi hospitali lakini alikubaliwa kupima peke yake nakurudi na majibu.
Nilisoma kikaratasi cha majibu nikiwa natetemeka, jasho linanitoka. Majibu yalionesha kuwa Nusrat alikuwa ni HIV positive.
"Mungu wangu! Nimeshakufa mimi!!" Nilijisemea huku nabubujikwa na machozi. Lakini yeye wala hakuonesha wasiwasi wowote, nadhani kwakuwa alikuwa anaifahamu hali yake tangu zamani.
Nilibadilisha kabisa mtazamo wangu juu ya maisha. Tangu siku ile nilijua tu itakuwa nimeshaathirika mimi ni wa kufa leo ama kesho.
#No_Learning_No_Earning
So we have to Learn.
NAME : Mr George Francis
📩 mr.georgefrancis21@gmail.com
Inaendelea.....