DodomaTZ
Member
- May 20, 2022
- 71
- 107
ATM maalum ya kutolea huduma za vipimo vya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi VVU ijulikanayo kwa jina la “Jipime”, ( HIV Self Testing) imezinduliwa Jijini Mbeya kwa lengo la kuhamasisha wananchi kupima na kutambua afya zao ili kujilinda dhidi ya maambukizi mapya ya virusi hivyo.
Huduma hiyo imezinduliwa na Mkurugenzi Mkazi wa Walter Reed Army Institute of Research (WRAIR) kutoka Ubalozi wa Marekani Mark Breda, akiwa na mabinti na wananchi wengine waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa mashine hiyo na kuwataka vijana kuendelea kuchukua tahadhari, kuepuka maambukizi mapya ya Ukimwi.
“Serikali ya Marekani kupitia WRAIR tumefanikiwa kufadhili upatikanaji wa mashine hizi zitakazo sambazwa hapa Mbeya na mikoa yote ya nyanda za juu kusini kupitia Shirika la HJFMRI ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za VVU katika jamii” alisema Mark Breda.
Awali akizungumza kuhusu lengo la kuweka “ATM” hizo kwenye maeneo ya kutolea huduma za kijamii Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la HJF Medical Research International (HJFMRI) inayosambaza upatikanaji wa vipimo vya kujipima VVU vya Jipime (HIV self-testing) Sally Chalamila, alisema shirika lake limelenga kuwafikishia wananchi huduma za VVU katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa vipimo vya Jipime na uhamasishaji wa matumizi kondomu.
“Mashine hizi zimeletwa kusaidia jitihada za serikali kufikia malengo ya kitaifa ya kufikia 95-95-95 ambapo katika 95 ya kwanza inataka kila mtanzania kutambua afya yake kwa kupima VVU. Vipimo hivi vitapatikana bure na kila mwananchi ataweza kujipima VVU kupitia maelezo yaliyopo kwenye mashine na kipimo husika na endapo kipimo kitaonyesha kuwa na maambukizi anatakiwa kufika kwenye kituo cha afya ili kufanya kipimo cha uhakikisho” alisema Sally Chalamila.
Shirika la HJFMRI ni shirika la Kimataifa lisilo la Kiserikali linalotekeleza afua za matunzo na matibabu ya VVU kwa ushirikiano wa karibu na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais - TAMISEMI kupitia Timu za Usimamizi wa Afya za Mikoa na Halmashauri katika mikoa ya Mbeya, Songwe Rukwa na Katavi. Aidha mkoa Ruvuma shirika linatekeleza afua moja tu ya Tohara kwa wanaume ili kujikinga na maambukizi.
Sally alisema hapo baadae mashine hizo zitawezeshwa kutoa huduma za dawa kinga maarufu kama PrEP na kwa mkoa wa Mbeya wanakusudia kweka mashine kwenye maeneo yote ya starehe, vyuo vikuu, na maeneo yenye mikusanyiko mingi ya watu.
“Katika utekelezaji wetu wa afua hizi za UKIMWI hapa nchini, tumegundua kuwa kuna changamoto ya maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi kwa vijana wenye umri kati ya miaka 15 mpaka 24, ambapo hali ya maambukizi mapya kwa vijana hao ni asilimia 40 huku vijana wa kike ikiwa ni asilimia 80 na wakiume ikiwa ni asilimia 20, uwepo wa mashine hizi zitasaidia sana kundi hili kunufaika na njia za kujikinga na maambukizi mapya ya VVU,” aliongeza Sally.
Huduma hiyo imezinduliwa na Mkurugenzi Mkazi wa Walter Reed Army Institute of Research (WRAIR) kutoka Ubalozi wa Marekani Mark Breda, akiwa na mabinti na wananchi wengine waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa mashine hiyo na kuwataka vijana kuendelea kuchukua tahadhari, kuepuka maambukizi mapya ya Ukimwi.
Awali akizungumza kuhusu lengo la kuweka “ATM” hizo kwenye maeneo ya kutolea huduma za kijamii Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la HJF Medical Research International (HJFMRI) inayosambaza upatikanaji wa vipimo vya kujipima VVU vya Jipime (HIV self-testing) Sally Chalamila, alisema shirika lake limelenga kuwafikishia wananchi huduma za VVU katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa vipimo vya Jipime na uhamasishaji wa matumizi kondomu.
“Mashine hizi zimeletwa kusaidia jitihada za serikali kufikia malengo ya kitaifa ya kufikia 95-95-95 ambapo katika 95 ya kwanza inataka kila mtanzania kutambua afya yake kwa kupima VVU. Vipimo hivi vitapatikana bure na kila mwananchi ataweza kujipima VVU kupitia maelezo yaliyopo kwenye mashine na kipimo husika na endapo kipimo kitaonyesha kuwa na maambukizi anatakiwa kufika kwenye kituo cha afya ili kufanya kipimo cha uhakikisho” alisema Sally Chalamila.
Shirika la HJFMRI ni shirika la Kimataifa lisilo la Kiserikali linalotekeleza afua za matunzo na matibabu ya VVU kwa ushirikiano wa karibu na Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais - TAMISEMI kupitia Timu za Usimamizi wa Afya za Mikoa na Halmashauri katika mikoa ya Mbeya, Songwe Rukwa na Katavi. Aidha mkoa Ruvuma shirika linatekeleza afua moja tu ya Tohara kwa wanaume ili kujikinga na maambukizi.
Sally alisema hapo baadae mashine hizo zitawezeshwa kutoa huduma za dawa kinga maarufu kama PrEP na kwa mkoa wa Mbeya wanakusudia kweka mashine kwenye maeneo yote ya starehe, vyuo vikuu, na maeneo yenye mikusanyiko mingi ya watu.
“Katika utekelezaji wetu wa afua hizi za UKIMWI hapa nchini, tumegundua kuwa kuna changamoto ya maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi kwa vijana wenye umri kati ya miaka 15 mpaka 24, ambapo hali ya maambukizi mapya kwa vijana hao ni asilimia 40 huku vijana wa kike ikiwa ni asilimia 80 na wakiume ikiwa ni asilimia 20, uwepo wa mashine hizi zitasaidia sana kundi hili kunufaika na njia za kujikinga na maambukizi mapya ya VVU,” aliongeza Sally.