Akili Kichwani
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 1,508
- 216
Kila tarehe 10 march huadhimisha siku ya watoto wa mitaani kwani miaka kadhaa iliyopita tarehe na mwezi kama huo aliingia rasmi mitaani kama mtoto aishiye kwenye mazingira magumu hadi miujiza ilipotokea akakombolewa baada ya kusota huko mitaani zaidi ya miaka miwili. Baadhi ta shida alizopata akiwa huko mitaa ni ni pamija na
1. Kunusurika kuuwawa na watu wenye hasira akidhaniwa mwizi, baada ya kukurupushwa usiku kwenye vilabu vya pombe za kienyeji alikokuwa amelala, aliokolewa na msamaria mwema aliyekuwa akimfahamu
2. Kulala kwenye vilabu vya pombe za kienyeji, stand za mabasi na madarajani hata wakati wa masika
3. Kulimishwa mashambani, madukani na migodini kwa ujira wa ugali, nk.
Anasema katika maisha yake amewahi kujaribu kujinyonga mara mbili ……anaongeza kuwa hajawahi kuona mtu akimpenda kwa dhati maishani mwake………….. hata wanawake alianza kuwapata baada ya kupata kazi na hivyo kuwa na pesa za kuwahonga.
Ilitokea miujza, akatokea mtu akamuingiza shule na kumtunza kwa miezi sita tu kabla hajasema mzigo wa kulea umemuelemea na kumfukuza nyumbani……..lakini kamwe hamsahau mtu huyo, kwani kwake ana hadhi ya malaika wa Mungu kwani milango ya elimu aliyomfungulia, hakuna shida wala dhiki wala mtu yoyote aliyeweza kuifunga hadi leo!!!!!!…………….. kuna maelezo marefu hapo yanafuatia lakini sasa tuko naye chuo kimoja huku nje ya nchi, yeye akichukua PhD,………….
Amenisimulia haya baada ya kumkuta amepamba chumba chake kwa maua na akisikiliza nyimbo za gospel kwa wiki nzima mfululizo (kumbuka tarehe 10 march ni jumatano ijayo), ndivyo anavyoadhimisha siku hii kwa mwaka huu,………… kweli story yake inasikitisha sana……… machozi yamenitoka leo…………
je, tumfariji namna gani huyu ndugu?...............
1. Kunusurika kuuwawa na watu wenye hasira akidhaniwa mwizi, baada ya kukurupushwa usiku kwenye vilabu vya pombe za kienyeji alikokuwa amelala, aliokolewa na msamaria mwema aliyekuwa akimfahamu
2. Kulala kwenye vilabu vya pombe za kienyeji, stand za mabasi na madarajani hata wakati wa masika
3. Kulimishwa mashambani, madukani na migodini kwa ujira wa ugali, nk.
Anasema katika maisha yake amewahi kujaribu kujinyonga mara mbili ……anaongeza kuwa hajawahi kuona mtu akimpenda kwa dhati maishani mwake………….. hata wanawake alianza kuwapata baada ya kupata kazi na hivyo kuwa na pesa za kuwahonga.
Ilitokea miujza, akatokea mtu akamuingiza shule na kumtunza kwa miezi sita tu kabla hajasema mzigo wa kulea umemuelemea na kumfukuza nyumbani……..lakini kamwe hamsahau mtu huyo, kwani kwake ana hadhi ya malaika wa Mungu kwani milango ya elimu aliyomfungulia, hakuna shida wala dhiki wala mtu yoyote aliyeweza kuifunga hadi leo!!!!!!…………….. kuna maelezo marefu hapo yanafuatia lakini sasa tuko naye chuo kimoja huku nje ya nchi, yeye akichukua PhD,………….
Amenisimulia haya baada ya kumkuta amepamba chumba chake kwa maua na akisikiliza nyimbo za gospel kwa wiki nzima mfululizo (kumbuka tarehe 10 march ni jumatano ijayo), ndivyo anavyoadhimisha siku hii kwa mwaka huu,………… kweli story yake inasikitisha sana……… machozi yamenitoka leo…………
je, tumfariji namna gani huyu ndugu?...............