Sijui tumemkosea nini jirani yetu

Sijui tumemkosea nini jirani yetu

Nimeipenda iyo ila usisahau kuwa linaweza kuwa fupa lililomshinda fisi, paka wa mama ataliweza?
Huyo dawa yake ndogo sana, Nitakachokifanya kuna mawili anayoweza kuyafanya: aidha atafungasha virago na kuhama yeye na familia yake usiku kwa usiku na kuiacha nyumba tupu au atahamia kituo chochote cha polisi kilicho karibu akihofia maisha yake na kwake hataishi. Mark my words!
 
Wana JF habar zenu.

Naishi na familia yangu,miaka minne iliyopita tulihamia kwenye nyumba yetu hapa Dar.

Jirani yetu alitupokea kwa furaha na kutuambia habar za mtaa mzima,alituambia pia watu ambao yeye hawapend hatak tuongee nao.

Siku zinavyozidi kwenda tunatokea kuwazoea majirani wengine zaidi yake, kitendo hicho kimemuudhi na amegeuka adui yetu balaa, amewekea sumu mifugo yetu kuku na paka tuliye kuwa tunafuga wamekufa.

Kuna siku alikuja na mganga kwake tukashangaa kuku wetu mweusi haonekani na manyoya yapo shimon pake, bata wetu wakipita uwanjani kwake anawakata miguu.

Yaani tunaimbiwa taarab kila siku,alishawah kumvuta mdogo wangu kwake na kumng'ata begani mpaka tukampeleka hospital.

Akifagia kwake uchafu anatupa upande wetu coz sisi tupo chin yake kidogo,tumemripot police na kwa balozi mara kadhaa ila hatuoni hatua zozote zikichukuliwa,na hii inatuogopesha sababu anatumia had watoto wake kuwaumiza wadogo zangu na kutuibia mifugo yetu maskin tumepaki na vifaranga tu.

Naombeni ushauri.

Pole sana hili tatizo ata mimi nimewahi kulipata na kabla nilihofia kuwa nalo ingawa mimi bado sijahamia nyumba yangu lakini niliwasoma majirani zangu kabla, baada ya kuwasoma majirani zangu mimi niliona bora nigaramike lakini nipige ukuta nimefanya hivyo kabla hayajatokea kama hayo ya kwako.

Wakati napiga fence niliwahisi kuumia sana lakini hawakuwa na namna sasa wewe unachoendelea kukosea ni uvivu wako wa kujenga fence baina yenu tena pandisha ukuta hadi juu kama nyumba ni ya kwenu lakin kama ni ya kupanga na huwezi kumshikia kisu au panga basi endelea kupelekeshwa au uhame huo mtaa.
 
mtoa mada we ni boya na mkatili sana. mmdogo wako ameng'atwa na aliyemng'ata umemuacha mtaani? ukishindwa kuanzisha timbwili nenda polisi mje na difenda uzoe hadi watoto wake wanaobaka wadogo zako. huwatendei haki wadogo zako.
 
mtoa mada we ni boya na mkatili sana. mmdogo wako ameng'atwa na aliyemng'ata umemuacha mtaani? ukishindwa kuanzisha timbwili nenda polisi mje na difenda uzoe hadi watoto wake wanaobaka wadogo zako. huwatendei haki wadogo zako.
Sikusoma vizur mkuu kumbe na wadogo zake wamebakwa. Sasa anangoja nn hajui kosa la ubakaji ni kosa la jinai
 
lazima kuna ulichomzidi omba mungu maana kama ni Mshirikina madhara ya naweza kuwa makubwa jars kuwa nae mbali... .ni me ama ke!?
 
Mkuu wewe ni Dini gani? Kama sijakosea wewe umeokoka na unafuata sana maandiko

Unakuwa kama hujaishi nyumba za kupanga bhna

Kulikuwa kuna haja gani ya kwenda hadi polisi afu wewe ni mwanaumee

Kuna mmoja humu alileta uzi kuwataka wanaume kujiamini kuto kata tamaa ungesoma ungekusaidia

Kwa kifupi wewe komaa wewe ndo kichwa cha Familia dawa ya moto ni moto huyo unamuendea na NYENGO (sijui kwa lugha yenu mnaitaje) unaondoka na mguu mmoja au nyama ya kisigino

Hadi mtu anang'atwa bega ww ukiwa wapi mkuu huyo ilitakiwa upande nae afu unashuka na sikio kama sio jicho Heshima itakuja

Ukimpeleka polisi heshima haitakuwepo kikubwa ni unamuibukia vuuuuuuuuu home kwake unampiga huo mkwara hadi kesho aje kukufagilia uwanja wako huyo sio wa kulemba nae yeye ni mtu wa shari mtayamaliza kwa shari
 
Jirani wa namna hio ni kumptupia jini mahaba tu.
Andaa mikwanja nikurushi kwa simu..
Hata kuwa na muda na wewe tena.
Manake ndombolo ya solo 24/7.

Unamuacha akuimbie na taarabu?

Teh teh teh.
Au huyo Matola nini?
Manake hizo ndio tabia zake huyo mtoto.
Hahahahahahah!! Mbavu zangu
 
Acha kuwa muoga kaka mfuate moja kwa moja mwambie aache ujinga wake anaoufanya na ukiwezekana mpige bakora live....jifanye huna akili atakuogopa kama ukoma. Dawa ya moto ni moto..utalialia had lini...vitu vingine maliza kiume.
 
Back
Top Bottom