Sijui tumemkosea nini jirani yetu

Sijui tumemkosea nini jirani yetu

Kama mnafuga mbwa basi atakuwa ana hamu ya kutoa-mbwa bandani mruhusu.
 
Wewe ni kibonde kiasi hicho? Una moyo mkubwa kama wa tembo yote hayo umefanyiwa ukayavumilia? Grow up! be a man kabla hajakudhalilisha siku moja atakukata vibao mbele ya mkeo na watoto wako!
Mi mwanamke
 
Wewe kwa nn ulianza kuongea na maadui zake? Mtu akiwa rafiki wa adui yako inamaana na yeye ni adui yako pia , ndio principles zisemavyo..


Ila kwa ushauri tu ungeweka fence kubwa ya kutosha na kila mtu aendelee na maisha yake , mimi sijui watu mnaishije bila fence. Mm kwa maisha niliyokulia mpaka sasa , ni bora nikawa na fence ila nyumba ikawa ya namna yoyote , au nikawa sina nyumba ila nikawa na fence...

Huna nyumba ila una fence kwani umegeuka mfugo?
 
Ndio maana alikuwa anakuwekea mipaka usizoeane na Majirani zako, sababu anajua fika ukizoeana nao (hao majirani) watakuambia ukweli kuwa yeye ni Kigagula
 
Hakuna kazi ngumu kama kuridhisha mtu, endeleeni na maisha yenu.
 
Atakuwa ni mchawi huyo jirani hivyo amegundua kuwa wewe na familia yako kuwa ni wachawi. Anachojifanya saizi ni kutaka kujua nani zaidi kati ya wewe na yeye ndo mana ameanza na hao paka wako wa kuchawi. Anapowakata miguu anataka aone kama utawapachikia miguu ya bondia ya kichawi. Kwani wewe paka wote hao tena weusi ni wa nini?
 
Utawezaje kuishi unaongea na mtu mmoja mtaani, coz yeye amegombana na karibia majiran wote, na ss ndo tunapakana nae kabisa,pia sisi hatujui ugomvi wao umeanzia wap, utaanzaje kuacha kuongea na mtu kwa sababu ya ugomvi usikuhusu na wala hauujui??

Hapo sasa,na jirani atakupangiaje maisha yako? Kama una uwezo weka fence,hata ya mabanzi kama alivyoshauri mdau hapo juu. Vitimbwi vikizidi mtokee tu na panga maana hamna namna nyingine.
 
Unapata wapi muda wa kuongeaongea na wapuuzi..fanya hivi ukitoka kazini nenda bar kapige tungi hadi giza liingie rudi nyumbani au kama ni mlokole kaa kwako jisomee vitabu vitakatifu huku ukinywa mirinda nyeusi..waepuke wapuuzi kama hao
 
ndio maana mie simwelewi na ninamshangaa Obama na sera yake ya kudhiiti silaha kuna mijtu kama huu inahitaji kununuliwa
hii kitu


MatebaAutoRevolver6in.jpg
 
hadi mda huu huyo jirani yako bado yupo hai?
 
Anawachukulia kwamba nyie ni watu waoga na dhaifu sana! Mtafutie vijana wa nguvu wamcharaze bakora za kutosha kama onyo!
 
Huyo dawa yake ni sala

Na msali sana amejaa nguvu za giza anaowaohopa lazima wana nguvu za Mungu.

Na lazima anawatenda mengine hamyajui. Salini sana tena sana mtaona atakavyowakimbia na kuacha kuwasumbua.
 
Wana JF habar zenu.

Naishi na familia yangu,miaka minne iliyopita tulihamia kwenye nyumba yetu hapa Dar.

Jirani yetu alitupokea kwa furaha na kutuambia habar za mtaa mzima,alituambia pia watu ambao yeye hawapend hatak tuongee nao.

Siku zinavyozidi kwenda tunatokea kuwazoea majirani wengine zaidi yake, kitendo hicho kimemuudhi na amegeuka adui yetu balaa, amewekea sumu mifugo yetu kuku na paka tuliye kuwa tunafuga wamekufa.

Kuna siku alikuja na mganga kwake tukashangaa kuku wetu mweusi haonekani na manyoya yapo shimon pake, bata wetu wakipita uwanjani kwake anawakata miguu.

Yaani tunaimbiwa taarab kila siku,alishawah kumvuta mdogo wangu kwake na kumng'ata begani mpaka tukampeleka hospital.

Akifagia kwake uchafu anatupa upande wetu coz sisi tupo chin yake kidogo,tumemripot police na kwa balozi mara kadhaa ila hatuoni hatua zozote zikichukuliwa,na hii inatuogopesha sababu anatumia had watoto wake kuwaumiza wadogo zangu na kutuibia mifugo yetu maskin tumepaki na vifaranga tu.

Naombeni ushauri.
Jirani wa namna hio ni kumtupia jini mahaba tu.
Andaa mikwanja nikurushie kwa simu..
Hatakuwa na muda na wewe tena.
Manake ndombolo ya solo 24/7.

Bado Unamuacha akuimbie na taarabu?

Teh teh teh.

Au huyo Matola nini?
Manake hizo ndio tabia zake huyo mtoto.
 
Back
Top Bottom