Sijui nianzie wapi?

Watoto watatu ni wengi sana na ni vigumu kumpata mwanamke anayeweza kuwalea hao watoto wako watatu.
Hasa ukiangalia mioyo ya wanawake wetu hawa.

Kwani ni wanawake tu? Mwanaume anaweza kuoa mwanamke wa watoto watatu na kulea?
Hili sio la upande mmoja, wote linatuhusu
 
never never,
worse enough hajawahi hata siku moja kunieleza kua simridhishi haja zake, Kazi nilipiga vizuri hilo hata yeye alikiri.

What goes around comes around. Nahisi kuna siri au chimbuko la hili.

Pole sana
 
Fanya hivi...watt wakubwa peleka boarding Huyomdogo mpelekee mama ako kama yupo au kama ikishindikana mpmkeo amlee akfkifkia umr wa miaka minne chukua mtt wako....kuusu kurud yana nae ucthibut ata kuongezea mactrec Bure mwishoe akuue uache wtt wako kwan amekupunguzia aclmia za uaminf huwez kumu amin kama zaman tract me or not kwan nkwel Huyo mwanamke cmwaminf mwache na wakat watt hawapo utapata wakat mzur wa kutafuta mwanamke mwingine na kucpend nae...kuusu kuzaa nae ucogope unaweza kuzaa nae hata watt wawil ucogope watt nmubaraka kutoka kwamungu ivyo mungu mwenyewe atafungua njia mtalea2 na mkwapanga vizur mbona mtafurai wenyewe.....niiite Mrs engeneer...
 

achana na huyo mwanamke mwisho wa siku atakuuwa kwa presha au ukimwi. kaa lea watoto peke yako, mungu akikujaalia upate mwanamke mwenye mtoto/watoto ambaye anajielewa, usiogope mzigo wa kulea maana malezi sana ni chakula, nguo, matibabu na vitu vingine vidogovidogo, kama baba yao anawasilisha matumizi na mama yao anafanya kazi wala haitakusumbua. Lakini huyo mwanamke wako ingekuwa mimi nasonga mbele siangalii nyuma.
 
hili la DNA mnataka jamaa afe haraka aisee

Imagine akienda akikuta sio wake anaweza kukutana na muumba siku si zake na inaonekana anawapenda watoto sana. Anaweza pia akaendelea kuwalea kama wake lakini mama yao akigundua amejua sio wake n analea tu, akaanza kuleta fujo na kuchukua watoto ili tu kumuumiza zaidi.
 

Mmmh! Hilo jambo gumu lakini daktari wa mtu ni yeye mwenyewe.
 

Ameshasema mama amewahi kuwakimbia watoto wake mwenyewe kwa muda unazidi siku sits sasa jiulize je huyu mama anaupenda kwa watoto? Baba angeondoka amwachie nyumba nini kingetokea? Labda angekua huru kuleta hawara zake, na angewaharibu watoto kisaikolojia.
 
mkuu unahakika watoto wote ni wako??
mkuu lengo hapa sio kujua watoto ni wangu au lah, ninachoamini mimi nikua hawa watoto wamezaliwa ndani ya nyumba yangu, nimewalea kwa gharama zangu, and thanks god they are very happy. hata kama nilidanganywa nakuhakikishia hakuna baba mbadala wa hawa watoto. kwahiyo issue ya kwenda kucheki DNA kwangu haitanisaidia kwani kwa vyovyote vile mi ndio nitabaki mlezi wa hawa watoto.
 
Mtoto wa Miezi 9 unachepuka? Pole kaka swala la kuoa kwa sasa huna haja ya kulifikiria
 
Mkuu Kahema upo mkoa gani ? Labda niweze kukupa nasiha ( counsel )...
 
Last edited by a moderator:

Mkuu nilikuwa nasubiri majibu ya hili swali ili nijue kwa kiasi wewe ni mtu wa namna gani.Una moyo wa kipekee sana aisee sijui kwanini huyo mwanamke hakuliona hilo.

Jitahidi ulee watoto wako kwa moyo wote watakupatia baraka nyingi sana.Waweza mtafuta dada wa kazi ukamlipa vizuri akakusaidia majukumu hapo nyumbani.

Usifikirie kumrudisha mwanamke yule hapo nyumbani.Ni mzinzi, na wazinzi hawana jema la kuwapa watoto wako.MUNGU alikuwa na maana yake kukuonyesha tabia za huyo mwanamke ili uzijue ujiokoe na wanao.

Kwa umri wako bado Una uwezo wa kupata mke mzuri tu baadae lakini usiwe na haraka.Nenda taratibu ili kosa la kuoa kurubembe lisijirudie.

Kila la heri.
 
Pole sana mkuu.... maana hata Avatar yako inaonesha unapenda sana familia.
 

Achana nae atakuletea magonjwa huyo.
 

kahema!
pole sana! usibabaike hauko peke yako. kwanza tafita sababu kwa nini mkeo anaenda nje hill ndio swala la singi sababu inswezekana wewe ndio kidonda hivyo hata ikioa mwingine atafanya hiyo hiyo! pili, kuwapenda watoto wako kusikuzuie maisha yako ya baadae it all depends on how you plan it especially on choosing your next spouse but since you have three children already, I advice you to go for a woman who has one child and is also desperate with life like you, you can cope. But But I warn you this shouldn't be your fore most thought or idea, first scrutinize the innermost relationship with your wife if at you all find you find yourself weak somewhere don't dare attempting any act forward other than reconciling with your wife because it is said A DEVIL YOU KNOW IS BETTER THAN AN ANGEL YOU DONT KNOW.nitafute ritchelous@gmaii.com yaliishanipata hayo am 64 now mwisho kabisa nimeoa Guyana.
 
kwa ajili ya watoto msamehe si kwa ajili ya dhambi aliyokutendea bali kwa ajili malezi ya hao watoto.
mrudishe umfanye kama mlezi wa hao watoto kwa sababu hata ukiwapeleka boarding angali wakijua mama yao hampo pamoja hawatatulia kwenye masomo yao.
we mrudishe alafu kwa sababu hautakuwa na mapenzi naye kama zamani tafuta kipozeo ambaye ukitoka kwake ukifika nyumbani hautamchukia tena mkeo kwa kuwa ngoma itakuwa droo.
 
Kwanza nenda kapime huu ugonjwa wa Kisasa, then vuta pumzi za kutosha kulea wanao na mwisho usifikirie kumrudisha mkeo kwa sasa na pia usiwaze kuoa kwa kipindi kifupi kijacho kwani wapo na utawapata au pengine baada ya tafakari na tafakuri ukamrudia mkeo. Kama una uhakika kakucheat na vidume V3 ni wazo huyo mkeo haridhiki hata kama mngemuoa wanaume w2 na aina hii ya wanawake na hata wanaume ni pasua kichwa kwani hata ufanye juhudi kiasi gani starehe yake ni kukutana na wanaume tofauti tofauti na siyo kuridhishwa. Anza hatua sasa na hutoijutia safari yako ila ukigeuka kurudi nyuma nachelea kusema hata usalama wako na wanao uwapendae utakua shakani. Pole kwa masaibu na Happy New Year of 2015.
 
Kahema nimesoma tena thread yako pamoja na comments za watu na wewe ulivyojibu. Nimegundua kuna tatizo kubwa nyuma yenu ambalo hujafunguka. usipofunguka hata kwa kifupi, itakua ngumu kupata ushauri muafaka. na withdraw kwa sasa comments zangu za mwanzo za nini ufanye. Jaribu kufunguka kidogo ili tukupe ushauri unaostahili. Sipati picha mke kukimbia watoto wake for 6 days...!!! what went wrong, hebu funguka hapa na utuambie mlikutana wapi katika mazingira gani. Kingine usimlaumu sana, duniani hapa kuna mambo mengi, kuna mwanamke namfahamu alimkimbia mume wake na watoto watatu, mdogo akiwa na 9 months, akaenda kwa mwanamme mwingine, huko akazaa watoto wawili. hapa ninapoandika comments hizi, alishaachana na huyo mwanamme wa pili sasa hivi ni teja (mla unga na bangi) wa kupindukia. Ni mama mwenye degree yake huyu, above 40 lakini hapa ndipo alipoishia. watoto wake wote kaacha kwa baba zao. familia yake inadai aliondoka kimazingara kwa mume wa mwanzo. sina hakika na hili. hainingii akilini mwanamke kupotea na kuacha watoto watatu. mimi hata mmoja simuachi no matter what... Funguka kaka yangu, hapa ndio penyewe kwa ushauri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…