Sijui laki moja yangu imeenda wapi?

flulanga

JF-Expert Member
Jul 1, 2016
4,861
6,343
Nina kawaida kila mshahara ukiingia sitoi pesa bank mpaka tarehe 01 ndio naenda kutoa pesa yoteee yaani haijalishi mshahara umeingia tarehe ngapi, hata ukiwahi tarehe 22 sitoi pesa bank mpaka ikifika tarehe 01 ndio natoa.

Sasa tarehe 01 mwezi huu nikaenda kutoa pesa yoteee nikafanya maemezi yangu ya nyumbani kwangu nikabakiwa na kama laki 3 na 80 hii ndio nikaweka kwenye pochi. Matumizi madogo madogo nikawa nanyogoa kwenye pochi katika hiyo laki 3 na 80 na kwa hesabu zangu labda tokea hiyo tarehe 01 mpaka jana labda ningekuwa nimetumia elfu 80 kwahiyo nikawa najua kwenye pochi nitakuwa na laki 3 au ikipungua sana basi laki 2 na 70.

Lahaula nilichokikuta aiseeee nimejikuta kwenye pochi kuna laki 2 na elfu 2 aiseeee nimeumia sanaaaa

Sasa hii laki imeenda wapi? Yaani tokea tarehe 01 mpaka jana niwe nimetumia laki 1 na elfu 80 kweli jamaaniii? Kwahiyo nahii laki 2 mpaka tarehe 31 siitakuwa nayenyewe imeisha jamani eti maana ndio kwanza tupo katikati yamwezi.

Nitajenga kweli kwa hali hiii au ndio nitaishi nyumba yakupanga mpaka watoto wangu wajue mwenye nyumba ndio bibi yao!!!

Ndugu zangu wenye take home yalaki 5 nakidogo kama yangu mnawezaje kuweka akiba? Hali yakuwa mnaishi nyumba yakupanga kodi haizidi elfu 50 namke namtoto mmoja!!!

Kwanza naishi kwakujibana, nyumba naishi local, nakula kawaida sana, hakuna ndugu anayenitegemea, siombwiombwi pesa nandugu maana wengi wanamaisha yakawaida kama yangu, navaa kawaida mimi namke wangu..... Yaani hatuna makuu wote wawili ila sasa kuweka akiba ndio mtihani mzito......

Nipeni mbinu ndugu zangu ningependa niwe naweza kuweka akiba yalaki 2 kila mwezi.
 
Kwenye mshahara wako inabidi utenge kiasi fulani usevu hiyo ni piga ua garagaza..kinachobaki ndio unachukua kufanya Matumizi yako na ya nyumbani.

Mfano wewe katika hiyo 380000 ndo iliyobaki baada ya matumizi una uwezo wa kusevu sana tu.

Ukibahatika kupata kimradi kidogo cha kukuingiza pesa za hapa na pale utasev vizuri tu..au wife kama nae anajishughulisha na kuingiza Pesa kidogo mtawezana kukaa na kupanga matumizi ya pesa zenu ili mpate kusev.
 
Kwenye mshahara wako inabidi utenge kiasi fulani usevu hiyo ni piga ua garagaza..kinachobaki ndio unachukua kufanya Matumizi yako na ya nyumbani.

Mfano wewe katika hiyo 380000 ndo iliyobaki baada ya matumizi una uwezo wa kusevu sana tu.

Ukibahatika kupata kimradi kidogo cha kukuingiza pesa za hapa na pale utasev vizuri tu..au wife kama nae anajishughulisha na kuingiza Pesa kidogo mtawezana kukaa na kupanga matumizi ya pesa zenu ili mpate kusev.
Mkuu hiyo 380,000, ilikuwa kwaajili yamatumizi madogo madogo sana sana mboga ila sasa sio kwamba niyote ila kiasi fulani ndio kazi yake hiyo
 
Mkuu hiyo 380,000, ilikuwa kwaajili yamatumizi madogo madogo sana sana mboga ila sasa sio kwamba niyote ila kiasi fulani ndio kazi yake hiyo
Vipi wife anajishughulisha kidogo?kama ndio fanya mzungumze nonagenarian maisha yenu.kama hana fanya umtafutie kitu cha kufanya apate kuingiza mia mbili mia tatu.

Wewe ndie unaejua unalipwa kiasi gani,kwenye mshahara wako toa kiwango cha fedha usevu mkuu hakuna namna
 
Vipi wife anajishughulisha kidogo?kama ndio fanya mzungumze nonagenarian maisha yenu.kama hana fanya umtafutie kitu cha kufanya apate kuingiza mia mbili mia tatu.

Wewe ndie unaejua unalipwa kiasi gani,kwenye mshahara wako toa kiwango cha fedha usevu mkuu hakuna namna
Wife wangu nimama wanyumbani mkuu ila ndio lengo nisave nipate mtaji nimfungulie biashara
 
Jichange fasta mkuu umfungulie kitu aiseh..wote mkiwa mnajishughulisha na mnaelewana mnakaa na kupanga maendeleo yenu inapendeza sana..

Mshahara ni kama herufi y ukiigeuza.usipokuwa makini huchomoki aiseh
Sawa mkuuuu nimekupata
 
Back
Top Bottom