Ndugu yangu joe5, kipi bora kati ya kujikopesha na KUIBA/KUFISADI? Mimi nadhani kama amejikpesha hilo ni jambo jema kwani atarudisha kuliko angeiba au kufisadi.
Pia ili kusiwe na double standard CDM waanzishe SACCOS kwa ajili ya staff wake tu ili kukabiliana na ukata wa maisha.
Hilo litapunguza rushwa au vitamaa vya hapa na pale kwani kila mtu anataka kiwanja au nyumba, gari na watoto wasome vizuri. Kukiwa na mikopo yenye riba nafuu ya nyumba, magari, elimu n.k itapunguza rushwa ya njaa.
Queen Esther[/QU
asante sana Queen Esther, walao ww umeelewa na umejibu kwa hoja,hv ndiyo JF ilivyotakiwa iwe.
tukirudi ktk post kinachogomba madai kwamba mkopo wake haukufata utaratibu na mazingira hayakuruhusu kwakuwa bado cdm haipati ruzuku ya kutosha kuendesha chana hata kufikisha mikoan na wilayani ushahidi ni harambee wanazofanya ktk M4C.sasa hapo ndo tunapohoji uadilifu wa babu hata km amekopa.
Joe5, heshima ni kitu cha bure, sio kwa waliokuzaa tuu hata wanaokuzunguka. Mtu mzima akiongea maneno magumu juu yako na kama kweli ulimkosea yanakupata hakika. Dr. Slaa ni mtu mzima, kutumia muda mwingi kumchafua kwa kitu ulichokuja nacho ni kutafuta laana, tena laana hiyo itafuata na watoto wako kizazi cha tatu na cha nne hakika.
Mimi sio CDM lakini naamini ktk heshima, utu na imani ktk dini ninayoiamini. Turudi kwenye misingi tuliyolelewa nayo tunapowajadili viongozi. Hata wale wanaomchafua mwl. Nyerere waache kama kweli wanaamini heshima ni kitu cha bure.
Watoto wetu wanaposoma some of the posts wanaanzaa nao kutoheshimu historia ya nchi yetu na viongozi pia. Ushauri wangu, tupime maneno tunayotoa humu jukwaani. Hata kama ni propaganda basi ziwe na mipaka. Anayekutuma yeye anakaa pembeni wewe unaogelea ktk dimbwi la laana na mikosi.
Huu ni ushauri tuu wapendwa na Mungu awabariki ktk kulitazama na kulifanyia kazi.
Queen Esther