KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,590
- 4,600
CCM ni tofauti sana na nyama vingine vya siasa nchini ambavyo vina usajili kamili na wa kudumu chini ya sheria ya vyama. Sifa pekee za CCM zinjidhihirisha wazi wazi katika masuala mazito ya kitaifa yafuatayo:-
- CCM ni chama pekee chenye azma ya kuhahakikisha kwamba Muungano wa Tanzania na mapinduzi ya Zanzibar vinaheshimiwa , vinalindwa na vinaendelezwa wakati wote.
- CCM ni chama pekee chenye azma ya kuhakikisha kwamba ardhi inaendelea kuwa rasilimali kuu ya Taifa na inayoendelezwa kwa maslahi ya wananchi wote.
- CCM ni chama pekee chenye azma ya kutaka kuona Tanzania ni Taifa lenye umoja, amani, utulivu na mshikamamo madhubuti wa kitaifa wakati wote.
- CCM ni chama pekee chenye amza ya kuhahakisha kwamba utawala wa sheria na utawala vinalindwa na kuendelezwa wakati wote.
- CCM ni chama pekee chenye azma ya kuhakikisha kwamba watanzania tunajenga maadili na demokrasia ya vyama vingi katika mazingira ya amani yanayokataa siasa za uchochezi, kashfa, uzandiki,ubaguzi wa rangi, ukabila, umajimbo na udini mambo ambayo ni kinyume na haki za binadamu.